The Bournemouth Protocol on Mass Grave Protection and Investigation - Swahili translation

Page 11

Ulinzi pia unalinda mabaki ya binadamu dhidi ya uchafuzi, uchafuzi wa mazingira, wizi, watapeli na upelekaji/uhamishaji wa miili kwenda maeneo ya pili, ambapo mhalifu anataka kukwepa kugunduliwa. Kupitia bila ruhusa na kubadilisha kunaweza kuwa kosa la uhalifu katika mfumo wa ndani.31 Masharti ya kabla ya mfumo madhubuti wa ulinzi: • Uthibitishaji wa ripoti na ushahidi kupitia mbinu mbalimbali na vyanzo vingine. • Kuweka kwenye ramani na kuweka kumbukumbu za makaburi ya halaiki kulingana na kiwango chao na muktadha wa eneo yaliko. Hatua muhimu za ulinzi zinaweza kujumuisha: • Kulinda eneo na kudhibiti ufikiaji: ruhusa ya kisheria32 ya kufikia ardhi inapaswa kutafutwa na kupatikana. Hii inaweza pia kuhitaji ushirikiano wa jamii na idhini kwa utekelezaji. Ufikiaji unaweza kuathiriwa na uwepo wa maeneo muhimu ya kitamaduni, sababu za kijiografia na udhibiti. Hatari zinazopatikana kwenye eneo ni pamoja na vilipuzi ambavyo havijalipuka na uchafu. • Hatua za ulinzi zinaweza kujumuisha: uzio ili kulinda mzunguko wa nje; ufunikaji wa njia mlalo ili kulinda mabaki kwenye sehemu za juu na walinzi wa usalama na ufuatiliaji ndani ya eneo. Hatua kama hizo pia zinategemea urefu wa muda kati ya ugunduzi na uchunguzi, muktadha wa kieneo na hatari katika eneo (kwa mfano, kuwekwa katika hatari ya viasili na wanyama). Kulinda eneo kunaweza kuhitaji hatua za usalama kwa wale wanaotoa hatua za ulinzi, kwani maoni ya umma yanaweza kuwa dhidi yao. • Huenda ufikiaji halisi usiwezekane kila wakati kwa mfano ambapo wachunguzi hawawezi kuingia nchini. Ufuatiliaji ndani ya eneo kupitia picha za setilaiti inaweza kuwa njia pekee ya ulinzi inayopatikana. Ulinzi unapaswa kutolewa iwe eneo limebadilishwa au la.

C. Uchunguzi Kanuni za kimataifa Chini ya sheria za haki za binadamu ya jukumu la kufanya uchunguzi madhubuti inamaanisha kuwa uchunguzi unahitaji kuwa huru na wa kutosha (kwa mfano, Kifungu cha 12 cha CED), unaoweza kubaini ukweli na kutambua waliohusika.33 Hii ni pamoja na kupata ushahidi wa uchunguzi wa kisheria na uchunguzi wa maiti, kwa rekodi kamili na sahihi na uchambuzi huru wa majeraha na sababu ya kifo.34 Uchunguzi lazima uwe na mamlaka ya kutosha kupata maelezo na kuwawajibisha maafisa. Unapaswa kufanyika kwa haraka; kwa jumla, ni jukumu linaloendelea la kuchunguza35 lakini ni jukumu la njia na sio mwisho.36 Mahakama ya Marekani ya Haki za Binadamu inasisitiza hitaji la uchunguzi kuzingatia muktadha mpana na utata unaozunguka matukio37 ili kufikia ‘ukweli kamili zaidi wa kihistoria unaowezekana, ikiwa ni pamoja na ubainishaji wa mitindo ya hatua ya pamoja’38 kulingana na haki ya kujua ukweli (kwa mfano, Kifungu cha CED cha 24(2)). CED inabainisha zaidi katika kifungu cha 12(4) kwamba nchi wanachama zinapaswa ‘kuchukua hatua zinazohitajika za kuwekea vikwazo vitendo vinavyozuia kufanyika kwa uchunguzi. ‘Ambapo inafaa, hii inaweza kujumuisha ushirikiano wa kimataifa katika ya Mataifa na mashirika husika (Kanuni za Kuongoza za CED, Kanuni ya 3(4)). Uchunguzi unaofuatilia malengo ya kibinadamu tu huenda “kivyake usiweze kuwa wa kutosha kufikia kiwango cha uchunguzi madhubuti’ kama inavyotakiwa na Mkataba wa Ulaya Ibara ya 2.39 Kulingana na Kanuni za Orentlicher40; ‘[b]ila kujali kesi zozote za kisheria, waathiwa na familia zao wana haki isiyo na kikomo ya kujua ukweli kuhusu mazingira ambayo ukiukaji ulifanyika na, ikiwa kuna kifo au kutoweka, hatima ya waathiriwa’. Chini ya sheria ya kimataifa ya kibinadamu, familia zina haki ya kufahamishwa kuhusu hatima ya wanafamilia wao, na zinaweza kutumia Taifa ili kutoa maelezo (Kifungu cha 32 cha Itifaki ya Ziada ya I). Kanuni ya 117 ya Kanuni za CIHL inaashiria kwamba mgogoro vya vita vya silaha wa kimataifa na suio wa kimataifa wahusika kwenye mgogoro

Angalia, kwa mfano, Sheria ya Iraqi Namba 13 ya 2015, Sheria ya Maswala na Ulinzi na Makaburi ya Halaiki, kurekebisha Sheria Nambari 5 ya 2006, Ulinzi wa Makaburi ya Halaiki. 32 Kanuni ya 10(3) ya Kanuni za Kuongoza za 2019 kuhusiana na utafutaji wa watu waliopotea zinaamrisha ufikiaji bila kizuizi kwa mamlaka zinazofaa ikiwa ni pamoja na ‘mamlaka kamili ya kufanya ziara zisizotangazwa kwa kila mahali ambapo mtu aliyepotea anaweza kuwa, ikiwa ni pamoja na vituo vya kijeshi na polisi na majengo ya kibinafsi’. Pale inapohitajika, hii inapaswa kujumuisha ‘utunzaji wa eneo linalohusiana na utafutaji’ (ibid). 33 Kukhalashvili and others v Georgia, Hukumu, Maombi ya ECtHR Nambari 8938/07 na 41891/07 (2 Aprili 2020) aya ya 129. 34 Ibid, katika aya ya 129. 35 Aslakhanova and others v Russia, Hukumu, Maombi ya ECtHR Nambari 2944/06 na 8300/07, 50184/07, 332/08, 42509/10 (18 Disemba 2012) yaa ya 230. 36 Da Silva v United Kingdom, Hukumu ya Baraza Kuu, Maombi ya ECtHR Nambari 5878/08 (30 Machi 2016) vifungu vya 231-238, inatoa muhtasari kamili wa Baraza Kuu wa mahitaji ya uchunguzi madhubuti. 37 The Massacres of El Mozote and other Places v El Salvador, Hukumu kuhusu Ustahili, Malipo na Gharama, Mahakama ya Kimarekani ya Haki za Binadamu Mfululizo wa C Nambari 252 (25 Oktoba 2012) aya ya 299. 38 Valle Jaramillo et al. v Colombia, Hukumu ya Ustahili, Malipo na Gharama, Mahakama ya Kimarekani ya Haki za Binadamu Mfululizo wa C Nambari 192 (27 Novemba 2008) aya ya 102. 39 Cyprus v Turkey, Hukumu ya Baraza Kuu, Maombi ya ECtHR Nambari 25781/91 (10 Mei 2001) aya ya 135. 40 Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Binadamu, Ripoti ya mtaalam huru ili kusasisha Seti ya Kanuni za kupambana na ukiukwaji (18 Februari 2005) Hati ya UN ya E/CN.4/2005/102/Add.1 (kwa kifupi Kanuni za Orentlicher) Kanuni ya 4. 31

9


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.
The Bournemouth Protocol on Mass Grave Protection and Investigation - Swahili translation by Bournemouth University - Issuu