“Labda alinipenda zamani kwa kuwa
alijua mimi ndiye ningekuwa mrithi. Lakini sasa upepo umebadilika na yeye
kabadilika, anampenda tu mwanamke mrithi wa familia tajiri ya Masawe.
Kwake, haijalishi yeye ni nani cha muhimu ni urithi tu alionao.”
Lisa aliongea kwa uchungu sana..
“Habari nilizozisoma asubuhi ya leo ziliripoti kwamba Mzee Kamote na bodi
inayosimamia Kituo cha Utamaduni na Teknolojia cha Taifa walihusika mara
kwa mara katika kupokea hongo, kwa hivyo anasimamishwa kazi na kuchunguzwa. Tukio la zabuni la jana pia limebatilishwa. Kulingana na maoni
yaliyotolewa mtandaoni, wengi
wanadhani kuwa Kibo Group ilimpa
Mzee Kamote rushwa ambayo
ilichangia Kibo Group kupata matokeo ya zabuni hiyo hapo jana.
Lisa alipigwa na butwaa. “Hii inawezekanaje?”
“Kwa nini nikudanganye? Ngoja nikuonyeshe habari hiyo.”
Pamela aliwasha simu yake haraka na kutafuta tovuti ya habari hiyo ili kumuonyesha Lisa. Lisa alishangaa kabisa. Alihisi kuwa kuna jambo geni kuhusu sadfa hiyo.
"Yajayo yanafurahisha!"
Pamela alisema kwa furaha kubwa, "Unaona, makampuni mengi makubwa ya tasnia ya ujenzi yalishiriki katika zabuni jana, na walitumia muda mrefu na rasilimali nyingi za wafanyakazi na nyenzo katika maandalizi ya tukio hilo. Juhudi zao zote
zimeishia bure sasa. Nadhani kituo
kimemchukiza kila mtu.”
Lisa aliamini hivyo baada ya kuwaza. Hata hivyo, ilikuja kama habari njema
kwake kwamba juhudi za Lina
hazikufaulu.
•••
Ndani ya ofisi za Kibo Building Design Group, Jones Masawe, mkurugenzi
mkuu, alikuwa amekasirika sana hivi
kwamba kifua chake kilikuwa hatarini
kupasuka muda wowote. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Lina kumuona
baba yake akivimba kwa hasira. Akiwa
ameinama upande mmoja, hakuthubutu
kusogea hata kidogo.
Siku moja tu nyuma, wasimamizi wakuu wa kampuni walikuwa wamesherehekea
mafanikio ya zabuni ya Kituo Cha
Teknolojia Na Utamaduni Cha Taifa, lakini kesho yake furaha hiyo ilianza
kuyeyuka taratibu baada ya kusikia
kuwa Mzee Kamote alikuwa
amekamatwa na TAKUKURU. Je, angefanya nini ikiwa kuhusika kwa
Mzee Kamote katika hongo
kungefichuliwa?
“Mama…” Lina alimwangalia mama yake, kwa wasiwasi. Mama Masawe
alimpiga bega na kumfariji. “Usijali. Kwa kuzingatia hali ya baba yako kwa miaka
mingi, ataweza kusuluhisha hili tatizo.”
"Hata kama naweza kusuluhisha, sifa ya Kibo Group itaathiriwa kwa kiasi
kikubwa," Jones Masawe alijibu kwa hasira.
Mama Masawe alimkodolea macho
mumewe. "Hii sio kazi ya Lina.
Amefanya kwa kadri yake. Yeyote
kutoka kwa kampuni ambaye
angejihusisha nayo angekumbana na hali kama hii. Kwa kweli, kuna mtu
alipanga kumdanganya Mzee Kamote.
hata Jones Masawe hajamaliza
sentensi yake, meneja mkuu ghafla
akaingia ndani na kusema, “Bw.
“Sina maana ya kumlaumu…” Kabla
Masawe, kuhusu mpango wa ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa klabu ya Simba, mratibu alitupigia simu hivi punde na kutufahamisha kwamba hawatafanya kazi na sisi tena. Pia, Hoteli ya
Kimataifa ya Holmes ilisema kwamba hawatafikiria kufanya kazi nasi.”
Jones Mwasawe alihisi kizunguzungu
huku akiwa amefura kwa hasira. Hii ndiyo miradi miwili mikubwa ambayo
Kibo Group ilikuwa ikilenga kwa muda wa miaka miwili iliyopita na ilikuwa
karibu kuipata.
Meneja mkuu kisha akaongeza, “Mbali na hayo, kampuni yetu ilituma maombi ya kutembelea maonyesho ya dunia
katika nchini ya India mapema, lakini
sasa wametukataa moja kwa moja. Bw.
Masawe, je kampuni yetu imemkosea
nani? Ni wazi kuna mtu anayeichafua
Kibo Group nyuma ya mgongo wetu.”
Jones alianza kutetemeka. Yeye ndiye
alikuwa ameongoza Kibo Group kwa
juhudi na kwa miaka mingi na hakuwahi
kugombana na mtu. "Siku zote
nimekuwa nikifanya kwa uangalifu
katika tasnia hii kwa miongo kadhaa.
Sijawahi kumuudhi mtu yeyote.”
“Inaweza kuwa… Lisa ?” Lina aliongea
kwa kusitasita. “Usinielewe vibaya.
Sijaribu kumsema vibaya. Haikuwa
suala kubwa wakati Lisa aliponikokota
nje ya Mgahawa wa Grapefruit wakati
huo. Lakini, Janet na Cindy walikuwa
wamekasirika sana wakati huo.
Walisema kwamba wangefanya jambo
kuhusu hilo. Wote hawa wanatoka
kwenye familia za matajiri wenye
ushawishi mkubwa. Huoni kwamba
tatizo linaweza kuwa lilianzia hapo?”
"Hakika inahusiana na Lisa!” Mama
Masawe alinguruma.
“Mwambie arudi.” Usemi wa Jones
uligeuka kuwa wa kusikitisha.
"Bw. Masawe, kuna jambo moja ambalo huenda hulijui…” Meneja mkuu alisita
kabla ya kusema, “Video ya moja kwa moja kwenye chaneli moja ya yotube
ilionyesha matukio machache ya aibu jana usiku, na Lisa akatokea kuwa
mhusika wa kike. Hata hivyo, video hiyo ilizimwa wakati polisi walipoingia na kuwakamata watu hao. Baada ya tukio hilo, polisi waliondoa video zote
zilizosambazwa mtandaoni na kutangaza kwamba Lisa alikuwa wakala wa siri wa polisi!”
Lina alishangaa kwa kufoka, “Hiyo ilikuwa hatari! Yeye hata hajapitia
mafunzo ya upolisi, sasa amekuwaje wakala wa siri?”
Mama Masawe aliuma meno. “Ni
wakala gani wa siri? Kuna uwezekano
mkubwa alijifanya kuwa wakala wa polisi baada ya kupata matatizo. Ni lazima polisi ndio waliomuokoa. Ni aibu iliyoje.”
Meneja mkuu akasema, “Ndiyo. Hicho ndicho kimekuwa kikienea katika
mtandao. Inajadiliwa sana kuwa maisha ya Lisa ni ya fedheha. Sifa yake
imeharibiwa sana.”
“Ni kiumbe mbaya sana. Kwa sababu yake, sifa ya familia ya Masawe imeharibiwa.” Akiwa amekasirika kwa hasira, Jones Masawe alichukua
chombo kwenye meza na kukitupa. “Tafuteni njia ya kumrudisha. Sitaki abaki nje na kuendelea kuwa fedheha kwa familia.”
SURA YA 27
Lisa aliruhusiwa kutoka hospitali baada ya siku mbili. Alvin binafsi aliendesha
gari hadi hospitali kumchukua.
Akikumbuka jinsi alivyotendewa kwa ukarimu isivyo kawaida, Lisa alijisikia
faraja sana. Akiwa anaendesha gari kurejea nyumbani, Alvin alipitia kwenye
maduka kufanya shopping kwanza.
"Charlie amekuwa mbaguzi sana wa chakula wakati haukuwa karibu naye
kumpikia siku chache zilizopita. Nunua viungo zaidi na umtayarishie kitu kizuri.”
Alvin alimwambia Lisa.
Akiwa anautazama uso wake wa kifahari, Lisa alijiuliza sana ikiwa ni Charlie au ni Alvin ambaye alikuwa mbaguzi wa chakula.
"Unasubiri nini? Harakisha." Alvin alimkurupua. Alikuwa amechoshwa na
vyakula visivyopendeza ambavyo Hans
alimletea kwa siku mbili zilizopita.
“Oh.” Lisa alifungua mkanda na kushuka kwenye gari. Kwa kuwa
alikuwa amemfanyia wema na hisani
kubwa wakati huo, alipanga
kumwandalia chakula kizuri ili
kuonyesha kuwa anajali fadhila zake.
Alipokuwa akiingia kwenye jengo la maduka, zaidi ya aina kumi ya mapishi ya Charlie yalimwangazia akilini mwake.
Kulikuwa na viungo vingi sana alihitaji
kununua. Pia alikusudia kupata mtindi, maziwa mabichi, matunda, na vyakula
vingine.
Baada ya duru moja ya ununuzi, aligundua kuwa mkokoteni ulikuwa
tayari umejaa. Hakika ilikuwa ni shida
kwake kubeba vitu vyote peke yake.
Baada ya kufikiria kidogo, alimtumia
Alvin ujumbe kwenye WhatsApp.
[Alvlisa, nimenunua vitu vingi, na sidhani kama naweza kubeba kila kitu.
Unaweza kunisaidia kubeba mifuko michache?] Baada ya kutuma ujumbe huo, hakusikia kutoka kwake kwa muda wa dakika tano. Alipumua na kuacha kuwa na matarajio makubwa kwake na kufikiria kubeba mwenyewe mizigo ile. Akiwa katikati ya mawazo yake, ghafla aliona kivuli kikubwa cha mtu kikiibuka. Alipoinua kichwa chake, umbo refu na wima la Alvin likatokea mbele yake.
"Nilitaka tu ununue viungo vya Charlie, lakini umekuja kununua duka zima."
Alvin alimkejeli Lisa baada ya kuona lundo la vitu alivyokuwa amenunua.
Lisa alieleza haraka, “Nilikuwa nikifikiri
kwamba wewe na Charlie hamjaweza
kula chakula chochote kinachofaa siku
chache zilizopita, kwa hivyo nimenunua zaidi…”
Alvin aliinua mkono wake na kumkatisha kwa kukunja uso, “Nilikula vizuri. Alikuwa Charlie ambaye hakula vizuri, usijumuishe na mimi. Mimi si mbaguzi wa chakula.”
“Una uhakika?”
"Ndio, Charlie hakula vizuri." Alvin alihakiki usemi wake.
Ili kumwokoa asipoteze heshima yake, Lisa aliitikia kwa kichwa na kueleza
kwa fikira, “Vitu ninavyonunua vyote ni vya lazima. Unahitaji kula mtindi, maziwa freshi, na matunda kila siku ili mwili wako upate lishe ya kutosha.
Huenda ukaonekana mzima sasa, lakini unafanya kazi kwa bidii kila siku na hata kunywa pombe kwa nyakati fulani. Kwa
hiyo, ni lazima utunze mwili wako na kula mlo kamili unapokuwa nyumbani.”
Alvin aliposikia hivyo alipigwa na butwaa. Macho yake yalifichua hisia zinazokinzana.
Kabla ya hii, hakuna mtu aliyejali kuhusu lishe yake. Watu wengine
walichojali zaidi ni uwezo wake wa kuleta manufaa kwa familia ya Kimaro na kama alikuwa ametimiza mahitaji ya familia ya Kimaro.
Lisa kisha akaongeza, “Ninahitaji
viungo hivi katika upishi wangu. Pia
nilinunua hizi tambi ili nikupikie
ukichelewa kutoka kazini. Tunahitaji
toilet papers na sabuni za maji kwa ajiliya usafi pia.”
Wakati huo, Alvin alikuwa chini ya hisia
kwamba mwanamke huyu alipaswa
kuwa mke wake, kutokana na kwamba
alikuwa anajali sana kila kitu ndani ya nyumba.
Akionyesha kisanduku cha karatasi, Lisa aliendelea, “…hii tishu itawekwa kwenye gari lako. Kwa hiyo si mara zote utalazimika kutumia karatasi ya tishu iliyotolewa kwenye kituo cha mafuta. Aina hii ya tishu ni nafuu sana…”
"Tangu lini ninatumia karatasi ya tishu iliyotolewa bure kwenye kituo cha mafuta?"
“Ipo kwenye gari lako. Bado ipo.” Kwa kuogopa kwamba alikuwa na wasiwasi juu ya kuokoa heshima yake, Lisa alijifanya kuwa alipenda vitu alivyotumia Alvin. “Haijalishi. Ninapenda kwa kuwa unatumia vitu visivyo na bei sana. Nimefurahi kukutana na mwanamume ambaye anaishi maisha ya kujali matumizi mazuri ya pesa.
Wewe ni mfano wa mwanaume kamili
ninayependa kuishi naye."
Akiwa amezidiwa na pongezi hizo za
ghafla, Alvin aliinamisha kichwa chini. Jinsi alivyotazama juu na kumwangalia
kwa macho angavu ilimkumbusha mara ya kwanza walipokutana. Ikilinganishwa na mwonekano wake mbaya siku mbili zilizopita, sura yake isiyo na aibu sasa
hivi ilimfanya ajisikie vizuri.
"Haupaswi kufanya kazi kama mbunifu. Unapaswa kuwa mama wa nyumbani."
Alvin alimtania.
Lisa alicheka. "Nataka tu kuwa mama wa nyumbani na chumbani pia."
"Nenda ulipe bili sasa." Alvin alimwambia kwa kupotezea.
Muuzaji mwenye shauku ambaye
alikuwa akitangaza bidhaa fulani
aliharakisha hadi kwenye kaunta ya
kulipia na kuwazuia wawili hao. “Halo
bwana na bibie. Je! ninyi mnataka
kununua Durex? Tuna promosheni
ianyoendelea ambapo unanunua moja na kupata moja bila malipo. Ni kweli inaokoa pesa.”
Lisa aliona haya kuona kisanduku kidogo cha kondomu mkononi mwa muuzaji. “Hapana… Hakuna haja. Hatuhitaji.”
“Ohhh. Nyote wawili ni watu waliooana
hivi karibuni, kwa hiyo mnapanga kupata mtoto?” Muuzaji aliuliza bila
kujua lolote.
“Ndiyo.” Akiogopa kwamba muuzaji angeendelea kuwasumbua
Lisa alinong'ona kitu na kisha akamvuta
Alvin mbele.
"Nani kasema anataka kupata mtoto?"
Alvin alimtazama Lisa kwa jicho kali.
“Nilikuwa namdanganya tu aende zake, au unataka kuzinunua?" Lisa aliuliza kwa kawaida.
“Acha kuota. Hata kama ningenunua, sitaitumia na wewe.” Licha ya maneno yake ya kikatili, sura ya Lisa ilitabasamu kwa furaha.
Baada ya wao kuondoka kwenye maduka, Alvin aliendesha gari kurudi
nyumbani Walipofika nyumbani, Lisa
aliingia moja kwa moja jikoni kuandaa
chakula. Mwanzoni Lisa alifikiri
kwamba alikuwa ameandaa chakula
kingi sana. Mara tu Alvin alipoanza kula, alifikiri chakula kisingetosha. Alionekana
kuwa na njaa ya siku mbili. Chakula
kiliisha kwa muda mfupi. Baada ya
chakula cha mchana, Alvin na Charlie
walilala kwenye kochi kwa uvivu, akijipumzisha kidogo ili chakula kishuke
taratibu.
“Unapanga kufanya nini baadaye?
Utaendelea kutafuta kazi?” Alvin alimuuliza Lisa
“Tulizungumzie hilo baadaye. Nitaenda kusajili laini ya simu kwanza.” Lisa ajibu.
“Usijali kuhusu hilo. Ikiwa huwezi kupata kazi, kaa tu nyumbani unipikie. Kama
una shida ya pesa nitakupatia kiasi chochote muda wowote unaotaka.”
Alvin alimwambia huku akitoka.
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda.
“Unakwenda kazini sasa hivi?”
"Ndio, bado nina kazi nyingi ya kushughulikia." Mara baada ya kuondoka, Lisa alitupia macho muda
huo ambao ulionyesha ni saa saba
mchana. Kwa kweli alimuonea huruma
kwani kuwa bosi haikuwa rahisi.
Hakuwa na hata mapumziko baada ya
chakula cha mchana. Pengine alikuwa
ameiba tu muda nje ya ratiba yake
yenye shughuli nyingi ili kumchukua hospitali.
SURA YA28
Baada ya Lisa kusajili laini ya simu
mchana huo, simu yake ilionyesha zaidi ya simu kumi ambazo hazikupokelewa.
Alikuwa amerudisha namba yake ileile ya zamani. Simu hizo zilipigwa na
Pamela Masanja, Jones Masawe, na
Mama Masawe, na watu wengine
wengi. Je, inawezekana kwamba walikuwa na wasiwasi juu yake baada ya kujua kilichomtokea? Bila kujali
sababu, alimpigia simu mama yake.
“Mama…”
“Hatimaye umenipigia simu tena.” Sauti ya hasira ya Mama Masawe ilisikika.
“Unakusudia kukaa nje hadi lini? Njoo
nyumbani sasa hivi.”
Ule msemo 'njoo nyumbani' ulimfanya Lisa ahisi uchungu ndani kabisa, akauliza kwa hasira. “Hapo bado ni nyumbani kwangu?”
“Lisa, ikiwa hautarudi sasa, usirudi
milele. Huhitaji tena kumtambua baba yako na mimi pia.” Mama Masawe
alikata simu mara baada ya kumaliza kuongea.
Baada ya kusitasita, hatimaye
Lisa aliamua kurudi nyumbani. Kwani, Jones na Mama Masawe ndio
waliomzaa na kumlea. Pia alitaka
kuwapelekea rekodi iliyo na maneno ya Juma Masudi nyumbani na waisikie ili
wajue rangi halisi za Lina.
Saa moja baadaye, aliendesha gari hadi
kwenye jumba la kifahari la familia ya Masawe. Ingawa ilikuwa imepita zaidi ya mwezi mmoja tu tangu aondoke
nyumbani hapo, alihisi kwamba watu
wanaoishi hapo walikuwa wageni kabisa kwake. Baada ya kuegesha gari lake aliingia ndani. Jones, Mama Masawe, na Lina wote walikuwa sebuleni. Mara tu Lisa alipoona sura ya Lina, chuki iliwaka ndani yake. “Baba, Mama, unajua kwamba Lina aliiba mpango wangu, na yeye—”
“Lisa, sijali kunishtaki nje, lakini
unawezaje kuthubutu kunirushia matope hapa?” Tabasamu la uchungu lilienea
kwenye uso wa Lina. "Tayari nimesema sijafanya."
Mama Masawe alivuta uso mrefu pia.
“Kwa nini unamwakia tu dada yako kwa
maneno makali kila unapomwona?”
“Nina ushahidi.” Lisa mara moja akatoa
simu yake na kucheza rekodi ya Juma
Masudi. Mara tu Lina aliposikia sauti ya Juma, sura yake ilibadilika kidogo. Hata hivyo, upesi alipata utulivu na kusema
kwa huzuni, “Ulimpata wapi mtu huyu wa kumlaghai kurekodi haya? Juma ni nani? Hata simfahamu.”
Lisa aligeuka na kumtazama baba yake kwa macho mekundu kidogo. “Baba, Lina alihamisha mamilioni ya pesa kwenye akaunti ya Juma ambayo
unaweza kuangalia mwenyewe. Alikulia kijijini na alijifunza kubuni tu baada ya wewe kumkubali. Kwa kuzingatia kwamba alijifunza kwa muda mfupi tu, angewezaje kutokeza na muundo mzuri kama huo?”
"Baba na mama, sikufanya hivyo."
Machozi yalitiririka usoni mwa Lina.
Mama Masawe alikunja uso na kunyoosha mkono wake. "Lisa , nionyeshe hiyo rekodi." Akiwa na moyo
mpole kidogo, Lisa akamkabidhi simu
kwa utiifu. Mama Masawe alifungua faili ya kurekodi na kulifuta mara moja.
"Mama, wewe ... kwanini?"
Lisa alishangaa kwa kitendo cha hicho cha mama yake, lakini alivyotaka
kumpokonya simu yake, alikuwa ameshachelewa.
Mtazamo wa Mama Masawe
ulidhihirisha ukatili wake kwa mara nyingine tena. “Siwezi kukuacha uharibu
sifa na mustakabali wa dada yako kwa rekodi hii ambayo inaweza kuwa ya uwongo. Afadhali kuifutilia mbali.”
Lisa alichanganyikiwa sana hivi
kwamba alitetemeka. Mara moja, alitoa kicheko kisicho na maana. “Sasa
naona. Ninyi nyote hata hamjali ikiwa
rekodi ni ya kweli au la. Mnachojali ni kumkingia kifua Lina tu. Unawezaje
kuwa mkatili hivyo? Mimi pia ni binti yako.”
Jones alipiga meza na kusimama.
“Kama ningejua mapema kwamba
ungekuwa mtu hatari sana, ningalikuacha wakati huo. Angalia
mambo ya ajabu ambayo umefanya. Umepoteza sifa yako kwa kufanya
jambo la aibu tena hadhahari na kurekodwa kwenye video. Je, mtu
yeyote mwenye heshima angependa kukuoa katika siku zijazo? Pili, ni nani
aliyekukosea hadi ukatufanya kupoteza miradi mikubwa michache?”
"Sijui unazungumza nini." Lisa akatikisa kichwa huku akilia. “Kama wazazi
wangu, hamna wasiwasi nami tangu
mlipoona nimekutana na matatizo kama
hayo?”
“Hicho ndicho unachostahili,” Mama
Masawe alizungumza kwa njia ya
dharau, “Si ajabu Ethan alikutupa kwa
sababu haujitambui kabisa.”
Lisa alishindwa kabisa kusema. Hata wazo dogo la matarajio ndani yake
lilikatishwa tamaa. Alijiona mjinga sana. Hakupaswa kurudi. Ukweli haukuwajali baba yake wala mama yake hata kidogo. Muhimu zaidi alikuwa ni Lina.
Akiwa amehuzunika, Lisa alinyoosha
mkono wake kwa mama yake.
“Nirudishie simu yangu mama, nitaondoka. Mtu mwenye aibu kama mimi hastahili kurudi. Sistahili kuwa na uhusiano na ninyi nyote pia.”
"Unapanga kuendelea kuzurura mitaani na kuleta aibu kwa familia yetu sivyo?"
Jones alicheka. “Afadhali ukae
nyumbani na kutafakari matendo yako.
Ukiamua kusema ukweli, nitafikiria
kukurudisha kwenye kampuni.”
Mara Jones alipomaliza kuzungumza, alipiga makofi. Walinzi wachache
walitoka kwenye mlango na kumkamata
Lisa mara moja.
“Nyie mnajaribu kufanya nini?
Mnaniteka nyara, huh?” Lisa alikasirika.
Kamwe katika ndoto zake kali hakuwahi
kufikiria kuwa familia yake ingewahi
kumfanyia kitendo kama hicho.
“Ninamfundisha tu binti yangu somo. Mleteni juu na kumfungia chumbani.”
Jones Masawe alisema.
Lina akashauri haraka, “Usifanye hivi baba. Baada ya yote, Lisa bado ni mdogo na hajakomaa. Zaidi ya hayo, daima kuna wageni wanaokuja
kututembelea hapa. Haitakuwa nzuri
ikiwa atapiga mayowe kutoka juu.
Jones alishtuka. “Uko sahihi. Kwanini…
Hebu tumpeleke mbali kabisa
tukamfungie katika nyumba ya Old
Moshi.”
Lisa alianza kuingiwa na hofu. Katika
miaka michache iliyopita, alikuwa
amerudi huko kijijini kwao Mbokomu, Moshi vijijini mara moja tu kwa ajili ya
shughuli za matambiko. Nyumba hiyo
ilikuwa imejengwa na ukoo wa Masawe
miaka mingi sana iliyopita. Ingawa sehemu ya nyuma ya nyumba ilikuwa
imerekebishwa kidogo, eneo jirani
lilikuwa ukiwa na la kutisha. Hatimaye
Lisa alielewa ni kwanini Lina
alimuombea apelekwe huko. “Lina, wewe ni mtu mbaya sana—”
Mama Masawe alimpiga Lisa kofi
usoni. "Nyamaza! Dada yako anajaribu
kukuombea, kumbe unamtukana.
Hakika wewe ni mbaya sana!”
mkono wake. Akiwa amechanganyikiwa
"Mpelekeni sasa hivi." Jones alipunga
na mabadiliko ya tabia ya Lisa , alijiuliza
ni kitu gani kilimfanya awe mbaya kiasi kile. Akiwa amepitiwa na usingizi, Lisa hakujua safari ya gari iliendelea kwa muda gani. Aliachwa moja kwa
moja kwenye nyumba ya zamani ya kijijini baada ya hapo.
Walinzi wachache wakafunga mlango
mkuu mara moja. Hata madirisha
yalifungwa kwa misumari. Mbaya zaidi
hakukuwa na umeme wala maji. Hata
blanketi hakupewa, na ukizingatia baridi
la milima ya old Moshi kipindi hicho, Lisa alihisi kuganda. Kwa vile simu yake
ilikuwa kwa Mama Masawe, hakujua
muda huo ulikuwa ni saa ngapi.
Nyumba hiyo kubwa ya zamani ilikuwa
imejengwa kwenye eneo kubwa, ikiwa
imezungushiwa na ukuta mkubwa
yapata mzunguko wa kiwanja cha
mpira. Ndani yake kulijaa pori la
migomba na miti ya miparachichi na mifenesi hivyo kuifanya nyumba ile kubwa kuwa ya kutisha sana ndani
yake. Upepo ulivuma na hivyo kugonga mlango na madirisha, sauti ya kutisha ya popo waliokimbizana pia ilisikika. Lisa karibu awe mwendawazimu.
Akajikunja juu ya kitanda kwa uwoga mkubwa, hakuthubutu kusogea hata
kidogo. Aliogopa giza. Aliogopa sana. Mara tu alipogundua kuwa dirisha limefunguliwa, alikimbilia huko. Bibi mzee aliweka bakuli la wali kupitia
dirishani. Mara Lisa alimshika mkono na kumsihi, “Bibi naomba uniache niende. Ikiwa hilo haliwezekani, angalau washa taa na unipe kitanda na blanketi, tafadhali.”
"Hapana. Hili ni agizo kutoka kwa bwana na bibi Masawe" Bibi kizee
alijitenga na mikono yake kikatili. Kisha, kulikuwa na kishindo kwenye dirisha likifungwa.
Akiwa amesimama gizani, Lisa alikuwa anaumia sana hivi kwamba alishindwa
kupumua. Alikuwa amefanya nini hasa? Kwanini kila mtu alimtenda hivi? Alikuwa amevuliwa utu wake. Hata uhuru na maisha yake ulichukuliwa pia.
Alimchukia Lina, Bw. Masawe, Bi. Masawe, na Ethan kabisa. Hata hivyo, hakuweza kukata tamaa. Alitaka kubaki hai na kulipiza kisasi. Alijaza wali mdomoni. Hakukuwa na kitu kingine zaidi ya wali. Mbaya zaidi mchele ulikuwa umevunda. Machozi yalimwagika usoni mwake. Ikiwa hakuna mtu angekuja kumwokoa, labda asingeweza kutoka nje ya nyumba hiyo akiwa hai.
Bibi kizee alitoa simu kwa mbali kidogo na mlango mkuu. "Lina, nimefanya kila kitu kulingana na maagizo yako."
“Usijali. Kwa mwonekano wa mambo, hakika hataweza kuishi kwa zaidi ya siku nne.”
SURA YA 29 Baada ya Alvin kutoka kazini, alienda moja kwa moja kwenye mkutano kuhusu kesi ya kimataifa ya kifedha usiku. Akiwa amekunywa pombe wakati wa mkutano, alihisi kizunguzungu kidogo. Mara baada mkutano
kumalizika, alirejea nyumbani. Hali ya nyumba ilikuwa tulivu na kimya. Baada
kuingia ndani ya nyumba hiyo na kuwasha taa, Charlie alimkimbilia.
Aliendelea kulia ‘mieww…mieww..’ huku
akikumbatia mguu wake.
"Charlie, unataka
huh?" Alvin akatikisa kichwa chake taratibu. Baada
“Sawa. Anza kupunguza halijoto kesho.
Natumai ... atafia nyumbani."
nini,
ya muda kidogo, aliona kitu kibaya kwa
Charlie ambacho hakuweza kufahamu hadi alipoisugua pua yake kwenye
bakuli tupu. Charlie alikuwa na njaa. Je, Lisa hakumlisha? Mara moja
akammiminia chakula cha paka Charlie ambaye alionekana kuwa na njaa kali.
Alvin alikwenda chumbani kumtafuta
Lisa, na kugundua kuwa alikuwa
hajarudi. Uso wake ukajawa simanzi ghafla.
Mwanamke huyu amekuwa
akisababisha matatizo yasiyoisha. Hapo awali alilazwa hospitalini, na sasa kwa
kuwa hatimaye alikuwa amerudi
nyumbani kwake, alimwacha Charlie
katika hali kama hiyo. Bado alikuwa
hajarudi ingawa tayari ilikuwa ni usiku
sana. Akatoa simu yake ili ampigie, lakini simu yake ilikuwa imezimwa. Je, kuna jambo jingine lililomtokea?
Baada ya kuitoa simu yake, Alvin
alifuatilia mahali alipo Lisa. Kwa bahati nzuri, alipomkabidhi simu siku hiyo,
alikuwa amewasha ufuatiliaji wa eneo (gps) kwa kuhofia matukio mabaya
yangeweza kumtokea tena. Baada ya kufuatilia eneo lake, Alvin alimtumia ujumbe Hans. [Niangalizie eneo hili.]
Dakika moja baadaye, Hans alipiga simu, “Hii ni nyumba ya familia ya Masawe ambapo wazazi wa Lisa wanaishi.”
"Nimeelewa." Alvin alikata simu kwa hasira. Alvin alishindwa kabisa kumtafakari
Lisa. Alikuwa tu akionyesha ladha ya fadhila baada ya yeye kumtendea
wema. Sasa alikuwa ameenda
nyumbani kwao bila kumpigia hata simu kwanza. Mbaya zaidi alikuwa amezima
simu yake. Alikuwa na maana gani?
Je, hakuwa na mpango wa kurudi nyumbani kwake baada ya kusamehewa na familia ya Masawe?
“Afadhali asirudi milele” Alvin alijiapiza moyoni. Asingemjali tena hata kama
angekuwa na matatizo. Kamwe asingetarajia kwamba Lisa angekuwa hana moyo kiasi hicho.
Hakukuwa na habari juu yake kwa siku
tatu zaidi. Hakujibu hata simu zake.
Kilichomshusha moyo zaidi Alvin ni kwamba hakula vizuri katika siku hizo
tatu. Hata alitembelea mgahawa ambao
ulitoa chakula kitamu zaidi kama
ilivyopendekezwa na Sam, lakini aliona chakula hicho hakikupendeza.
Wakati fulani, alishuku kwamba jambo
fulani linaweza kuwa limetokea kwa
Lisa. Hata hivyo, kila alipowasha simu
yake kuangalia mahali alipo, mara zote
ilimuonyesha yupo kwenye nyumba ya familia ya akina Masawe. Wazazi wake wa kumzaa wasingeweza kumdhuru, aliamini hivyo. Ni wazi kwamba alikuwa ameamua kumsahau na kumpuuza kwa makusudi.
Katika siku tatu mfululizo alikuwa amepooza sana ofisini. Muda wa kutoka
kazini ulipofika, mara moja alifungasha vitu vyake na kuondoka. Kisha
akagongana na Sam mlangoni.
“Unaenda nyumbani kumtunza Charlie?
Lisa bado hajarudi?"
"Usimtaje tena mwanamke huyu." Alvin aliendelea mbele akionekana kutokujali.
Sam alishtuka. “Sikuwa na jinsi zaidi ya
kukuuliza kwani Pamela aliniomba kujua
kuhusu Lisa. Alisema hajaweza
kuwasiliana naye, hivyo ana wasiwasi
kwamba kuna jambo limempata.”
"Siku zote hizi amekuwa katika nyumba ya familia ya Masawe, sivyo?" Alvin alisimama akiwa ameganda palepale.
Ilieleweka kuwa Lisa hakumpigia tena simu kwani wote wawili walikuwa
wamekutana tu muda si mrefu, lakini
Pamela alikuwa rafiki yake mkubwa.
“Ngoja nimpigie simu tena.” Sam
alijaribu kupiga simu.
Alvin alishuka kwa kutumia lifti bila kumsubiri. Akiwa njiani kuelekea
nyumbani, alihisi mambo yanazidi kuwa
mengi huku akiwaza. Hata hivyo,
aliogopa kwamba huenda akawa
anawaza kupita kiasi juu ya Lisa wakati
Lisa mwenyewe hata hamfikirii kabisa.
Bila kutarajia, Alvin alipokea simu
kutoka kwa Sam mara baada ya kufika nyumbani kwake.
“Hilo haliwezekani kabisa. Sasa hivi
Pamela aliniambia kwamba alitembelea
familia ya Masawe. Wakamwambia
Lisa ameenda nje ya nchi kupumzika, lakini hawakumpa namba yake ya mawasiliano. Damn, kuna kitu kinaweza kuwa kimemtokea?"
Alvin alikunja uso. “Sifikirii hivyo. Baada ya yote, yeye ni binti wa damu kabisa wa familia ya Masawe.
“Labda sivyo. Pamela alisema kuwa
familia ya Masawe ina upendeleo sana kwa Lina na inambagua Lisa.
“Sawa. Nitaifuatilia hiyo.” Alvin alisema.
Akiwa na hasira, Alvin kisha akampigia
Hans simu. "Tafuta ni wapi
Lisa alionekana mara ya mwisho."
Saa moja baadaye, Hans alimletea
habari fulani. “Lisa alienda kwenye
nyumba ya familia ya Masawe siku tatu
zilizopita. Muda mfupi baada ya kuingia
ndani ya nyumba hiyo, familia ya Masawe ilielekea kwenye nyumba ya zamani iliyoko Moshi kwa kutumia gari
lao. Pengine atakuwa yupo huko.”
“Unamaanisha kuwa anaweza kuwa kafungiwa?”
"Uwezekano mkubwa sana. Familia ya Masawe haingeenda huko isipokuwa kwa matambiko yao ya familia wakati wa mapumziko ya mwisho wa mwaka. Isitoshe, mahali hapo ni mbali sana.”
Alvin aliishika simu yake kwa nguvu.
“Fanya uchunguzi ujue mahali nyumba hiyo ilipo kisha unichukue. Nitatembelea nyumba hiyo mimi mwenyewe."
SURA YA 30
Kwa kuzingatia kwamba Moshi iko mbali
sana kutokea Dar es Salaam, Hans
aliendesha gari kwa saa sita kabla ya
kufika huko. Tayari ilikuwa ni saa sita
usiku walipofika. Nyumba ya ukoo wa Masawe ilikuwa katika kijiji cha
Mbokomu wilaya ya Mosh vijijini. Alvin aliposhuka tu ndani ya gari ndipo
alipogundua kuwa mahali hapo palikuwa na ukiwa wa kutisha.
Palizungukwa na ukuta mkubwa wenye eneo sawa na uwanja wa mpira.
Migomba mingi na miti mikubwa ya miparachichi pamoja na mifenesi
ilizunguka jumba hilo na kuliweka katikati. Hakuna mtu aliyeishi humo kwa
wakati wote. Jumba hilo lilitumika
sanasana kwa ajili ya wanaukoo wa Masawe kukutana mwisho wa mwaka.
Kutoka kwa mlango mkuu, ilionekana
kuwa nyumba hiyo ilikuwa ya miaka ya sabini au themanini hivi.
Alvin aligonga mlango, lakini hakukuwa na majibu. Kwa hivyo, mara moja
alipanda juu ya ukuta. Dakika
alipokanyaga chini, miale ya mwanga
ilimulika. "Wewe ni nani? Mbona unaingia ndani ya nyumba usiku wa manane?”
Alvin aligeuka nyuma na kumuona bibi kizee aliyekuwa ameshika tochi.
“Natafuta mtu. Niligonga mlango sasa hivi, lakini hukufunguliwa.”
“Mimi pekee ndiye ninayeishi hapa. Ondoka sasa hivi.” Bibi kizee
alimsukuma. Alvin alimsukuma tu yule bibi kizee akarudi nyuma. Alichukua
tochi na kuelekea kwenye ile nyumba ya ghorofa moja. Alipotazama huku na kule, akapata mshtuko. Aligundua kuwa madirisha yote yalikuwa yamefungwa
kwenye sakafu zote mbili huku mlango
nao ukiwa umefungwa.
"Fanya haraka uondoke sasa, au nitaita polisi." Kwa hofu, bibi kizee alimsukuma
Alvin kwa nguvu zaidi.
“Afadhali upige simu polisi waje
wakukamate kwa kosa la kumfunga mtu kinyume cha sheria.” Usemi wake
ulithibitisha zaidi dhana yake. Yule bibi kizee akaogopa mara moja.
Alvin akapiga hatua kubwa mbele, kisha
akaupiga teke mlango kwa nguvu. Hata baada ya kuupiga kwa muda mrefu, bado alishindwa kuuvunja ule mlango.
Alipoona shoka pembeni ya nyumba, alivunja dirisha moja kwa kutumia shoka hilo na kuruka ndani ya nyumba.
Harufu mbaya ikajaa puani mwake. Kwa
kuwa nyumba hiyo haikuwa na umeme, ilimbidi kumtafuta Lisa chumba kwa
chumba. Hatimaye, alimkuta amejikunja
kwenye kona ya kitanda cha mbao.
Bado alikuwa amevalia nguo ile ile
ambayo aliiona kabla ya kuondoka mchana ule. Kulikuwa na baridi kali
kwenye milima ile ya Old moshi. Hata
hivyo, hakukuwa na blanketi na mito
kwenye kitanda alichokuwa amelalia
Lisa. Hakukuwa na hata na tandiko la kitanda. Alipomkaribia, aliweza kuhisi harufu
iliyokuwa ikitoka mwilini mwake. Hata
hivyo, hakuweza kuwa na kinyaa juu ya harufu hiyo. Alimkimbilia na kumtikisa
kwa nguvu, lakini hakuonyesha kushtuka. Mwili wake ulikuwa wa baridi
kama barafu, huku uso wake ukiwa mweupe kama kipande cha muhogo.
Kwa bahati nzuri, aligundua kutoka
kwenye ncha ya pua yake kwamba
bado alikuwa akipumua kwa shida, au angefikiria kuwa amekufa. Alvin
akambeba na kukimbilia mlango mkuu.
Bibi kizee aliyekuwa amejificha nyuma ya mlango aliingiwa na hofu baada ya
kutambua hali ya Lisa . Kwa kuogopa
kukaa tena, mara moja alikimbia kwa
kutumia mlango wa nyuma. Alvin
hakuwa na muda wa kumkimbilia
kumshika. Ikiwa asingempeleka
Lisa hospitalini muda huo, bila shaka angeweza kufa.
Wakiwa njiani kuelekea hospitalini, Lisa
alibaki ametulia mikononi mwa Alvin.
Alvin aliinamisha kichwa chake huku
akimtazama usoni. Mashavu
yake yalikuwa yamekonda, huku
midomo yake kama jeli ilikuwa mikavu na yenye kupasuka. Alivin hakuamini
hakuamini kabisa baada ya kujionea tukio hilo. Lisa alikuwa binti wa damu wa familia ya Masawe lakini walimfanyia
unyama kama ule. Walikuwa wabaya
sana! Ndani kabisa, Lisa alielemewa na kufadhaika na mateso. Alvin alimuonea
huruma mwanamke huyo. Wakati huo
huo, alijilaumu tena kwa kutomtafuta
mapema.
Alvin alimpeleka Lisa katika hospitali ya Mawenzi. Alvin alikosa utulivu wakati
akisubiri nje ya chumba cha dharura. Karibu nusu saa baadaye, daktari
alitoka kwenye chumba cha dharura na kusema, "Ikiwa mngechelewa kufika
hapa kwa saa moja baadaye, tusingeweza kumwokoa.”
“Amezinduka?” Alvin alipumua kwa huzuni. Hatimaye uzito ulikuwa umeondolewa moyoni mwake.
"Ndio, lakini mwili wake umedhoofika
sana. Pia, ana homa ya nimonia.” Akiwa amemkazia uso Alvin, daktari aliongeza, “Hajapata maji ya kunywa kwa angalau
siku tatu, na pengine hakula chakula
cha kutosha pia ama chakula alichokula kilikuwa hakifai. Inawezekana
itamchukua nusu mwezi hivi kupona.”
Sio tu kwamba Alvin alishtuka, bali pia
Hans alipigwa na butwaa. "Je, akina Masawe wana chembe ya ubinadamu kweli?" Uso wa Alvin ukaanguka. "Itume habari yote kwenye mitandao, eleza kila kitu kilichotokea leo ili ulimwengu ujue rangi halisi za familia ya Jones Masawe."
“Sawa.” Hans akakubali.
Baada ya Lisa kupata huduma ya kwanza, kesho yake safari yakurejea Dar ikaanza. Lisa aliota ndoto ambapo
alikuwa karibu kufa. Hata hivyo, alipokea kumbatio la uchangamfu
kutoka kwa mtu aliyesitasita kumwacha aende zake. Ikaja akilini mwake
kwamba alikuwa kweli ... bado yuko hai!
Hili ndilo wazo lililompata Lisa mara ya kwanza alipofumbua macho yake.
Wakati huo, mwili wake ulikuwa
umefunikwa na blanketi ya joto. Kulikuwa na taa ndogo inayowasha
wodini, na kiyoyozi kilikuwa kimewashwa. Hakuwa katika nyumba ya zamani ya giza. Hii ilikuwa ni baada ya kufika Dar es Salaam ambapo Alvin alimpeleka kwenye hospital binafsi ya Premier Care clinic, Masaki.
"Lisa , hatimaye umeamka, mwanamke aliyelaaniwa!" Pamela alimrukia kwa macho mekundu na kusema kwa sauti ya kilio, "Unaendelea kulazwa hospitali baada ya hospitali, na kila wakati hali ni mbaya zaidi kuliko hapo awali. Umenitisha sana.”
“Ni wewe uliyeniokoa?” Lisa aliuliza kwa mshangao. Alikumbuka tu kwamba
alihisi kizunguzungu na alionekana
kuwaka. Tumbo pia lilikuwa likimuuma
sana. Kwa kweli alifikiri kwamba
angekufa kwa vile aliteswa sana na
njaa, baridi na kiu.
“Hapana, ni Alvin ndiye aliyekuokoa.”
Pamela alimwambia. “Nilikuwa
nimeenda nyumbani kwenu kukutafuta, lakini haukuwepo. Nilisikia ulipelekwa
Moshi na kufungiwa kwenye jumba lenu la ukoo. Mara moja niliwasiliana na
Alvin, na akaenda kukuokoa usiku huo.
Hapo awali, ulikuwa katika hospitali ya
Mawenzi kwa matibabu. Umekuwa
katika hali nzuri tangu jana, kwa hivyo
Alvin alikuhamisha hadi Hospitali hii.
Hajalala vizuri kaka wa watu kwa siku
chache zilizopita kwani alikuwa
akikutunza kila wakati. Nimemuomba
aende nyumbani akapumzike.”
"Ni yeye …?" Lisa alinong'ona kwa kutokuamini, macho yake yakiwa mekundu.
Kinyume na matarajio yake, alikuwa
amemwokoa kutoka kwenye matatizo
tena na tena. Kwa kweli, hakuwa
amemfanyia kitu kingine chochote kando na kumpikia yeye na Charlie mara chache. Alikuwa na deni kubwa kwake.
"Hapo zamani, ulidai kwamba yeye ni mtu asiyejali. Nadhani yeye ni mzuri sana, pamoja na kasoro zake ndogondogo." Pamela aliongeza, “Hata aliviambia vyombo vya habari habari
kuhusu wewe kufungwa na kunyanyaswa na familia ya Masawe.
Hisa za Kibo Group zimekuwa zikishuka
tangu jana, na wengi wanawakosoa
baba na mama yako mtandaoni.
Hutapingana na wazo lake, sivyo?
“Sitathubutu!” Kwa kutajwa kwa familia ya Masawe, macho ya Lisa yalionyesha
hisia kubwa ya chuki. “Kwa vile
walipanga kuniua, sitawaacha salama.
Nitalipiza kisasi kwao hivi karibuni au baadaye!
Pamela alipumua. “Usijali, Kibo group imeumizwa sana safari hii. Thamani
yake ya soko imeshuka kwa angalau dola milioni kadhaa.
Lisa alisema bila kujali, "Pamela, nitawafanya wale wote walionidhulumu walipe gharama siku moja."
Pamela alipigwa na butwaa alipohisi
mabadiliko ya mtazamo wa Lisa . “Kwa kweli, unaweza kumwomba Alvin akusaidie. Hufikirii… ameanguka kwa ajili yako?”
SURA YA31
Alvin na Sam walingia hospitalini pale
mida ya jioni. Sam aliweka kikapu cha matunda kwenye meza ya kahawa, kisha akamsalimia Lisa kwa tabasamu.
"Shemeji, unajisikia vizuri?"
"Vizuri zaidi." Lisa kwa siri alitazama
pembeni kwa Alvin aliyekuwa kasimama kimya. Lisa alipepesa macho yake kwa
utii. "Samahani kwa kukuletea shida tena." “Ni vyema kama umelitambua hilo.
Nilidhani wewe ni mjinga tu.” Alvin alikasirika bila sababu kumuona
Lisa akiwa amekonda mithili ya mfuko wa mifupa. Maneno makali yakamtoka
kinywani mwake. “Sijapata amani hata siku moja tangu nikuoe. Sitaki kuhojiwa
na polisi ukiwa umekufa siku moja.
Unaelewa?" "Haitatokea tena wakati ujao." Lisa
aliuma mdomo wake uliopauka kuzuia
machozi yasiendelee kuchuruzika
mashavuni mwake.
Upepo wa kufadhaika ulimpitia. Alvin
hakutaka kuendelea kumfundisha, lakini
alihitaji aache kufanya makosa ya
kipumbavu namna hii. “Simu
niliyokununulia iko wapi? Kwa nini
iliachwa nyumbani kwa akina Masawe?”
"Mama yangu alinidpokonya na kuikatalia."
"Kweli wewe ni nguruwe." Alvin alifoka.
“Uko sahihi. Tafadhali niite Nguruwe Masawe kuanzia sasa.”
Mapovu ya kicheko kilichoshindwa
kuzuilika yalitoka kwenye midomo ya Sam, na kulainisha hali ya wasiwasi katika wodi ya hospitali. “Sawa, Alvin, acha kumponda. Hakuna mtu ambaye
angetarajia ukatili kama huo kutoka kwa wazazi wake waliomzaa.”
Lisa alitetemeka. Baada ya kuona
hivyo, Alvin aligeuza macho yake kwa
Lisa na kumuonya. "Kaa mbali na familia hiyo ikiwa unataka kubaki hai."
"Hiyo ni sawa." Sam aliitikia kwa kichwa. “Zingatia tu kumwandalia rafiki yangu chakula. Tazama jinsi amekuwa na hasira baada ya kutoweza kufurahia milo yako iliyopikwa nyumbani katika siku chache zilizopita.”
“Sam Harrison.” Alvin akatupa jicho la hatari upande wake.
Sam aliacha kusema mara moja. Lisa hakuweza kupinga tabasamu usoni mwake. “Nitapona hivi karibuni na nianze kukupikia tena.”
"Kaa kimya na uzingatie kupona." Sauti ya Alvin ilikuwa ya ukali kama kawaida, lakini maneno yake yalileta uchangamfu moyoni mwake.
“Alvin, asante, kweli.” Lisa alishukuru kwa dhati.
•••
Siku mbili baadaye, Ethan akiwa
kwenye ofisi za kampuni yao, ‘Lowe Enterprises’, alikutana na habari ya Lisa
mtandaoni iliyosambazwa pamoja na cheti cha matibabu kilichotolewa na Dk Johnson. Ethan alishtushwa sana. Mara moja, aliingia kwenye gari na kukimbilia
kwenye makazi ya akina Masawe.
Alipofika, aliwahoji wanandoa hao wazee huku akijaribu sana kuzuia
hasira yake. “Mjomba Jones na Shangazi Masawe, ni kweli mlimfungia
Lisa kwenye makazi ya zamani
ambapo mlikataa kumpa maji na kumlisha chakula kibovu?”
“Upuuzi gani huu Ethan. Ulikua na sisi muda wote. Unafikiri tunaweza kufanya
hivyo?" Johes Masawe alikasirika na kufadhaika kwa wakati mmoja. “Kwa
kweli, nilimweka kwenye makazi ya
zamani lakini alitunzwa vizuri na
watumishi kwa chakula kitamu kila siku.
Yeye ni binti yangu wa kuzaliwa, hata hivyo. Ningewezaje kuwa mkatili hivyo?”
"Lakini inaenea mtandaoni kwamba ..."
Lina alimkatisha kwa huzuni, "Zote ni habari za uwongo. Sielewi kwa nini
Lisa angeidharau familia yake kama hivi baada ya kuondoka kwenye makazi ya zamani na marafiki zake. Mama na Baba wana wasiwasi sana juu yake.
Walimweka tu katika makao ya zamani ili asichangamane na watu wabaya na kuharibu sifa yake huko mitaani tena.”
Hilo lilimshangaza Ethan. Maneno magumu yalienea usoni mwake baada ya kukumbuka uvumi aliosikia muda si mrefu uliopita. Sasa, alielewa uamuzi wa familia ya Masawe. “Samahani, sikuwaelewa nyote.”
Mama Masawe aliweka mkono juu ya kifua chake kwa huzuni. "Sijali maoni ya
watu juu yetu mtandaoni kwani
tumeshindwa kama wazazi. Lakini Kibo Group ambayo tumetumia muda mwingi na juhudi kuijenga iliharibiwa mara moja. Hisa za kampuni ziko chini kabisa kwa siku kadhaa zilizopita na thamani yake ya soko ilipungua kwa zaidi ya dola milioni. Kinachotia wasiwasi zaidi ni kwamba kila mtu mtandaoni anaisusia
Kibo Group sasa. Mambo yatakuwa mabaya sana ikiwa hii itaendelea."
Ethan alikatishwa tamaa na
alichokisikia. Kufaulu au kutofaulu kwa kampuni ya Kibo Group kulimuathiri sana yeye mwenyewe. "Tunahitaji
kudhibitisha kwa umma kuwa familia ya
Masawe iko kwenye uhusiano mzuri na
Lisa. Kisha, tunaweza kuajiri kundi la
watu kutangaza hili mtandaoni ili kufuta uvumi huo.”
“Ni wazo zuri.” Johes alikubali kwa
kichwa. "Tarehe ya sherehe yako ya
uchumba inakaribia. Vyombo vya habari
pia vitakuwepo. Tunahitaji tu Lisa kujitokeza ili kubadilisha taswira ya kampuni.”
“Atajitokeza kweli?” Lina alimtazama Ethan kwa wasiwasi. “Ujue bado anakupenda. Sidhani kama anaweza akaja."
“Nitafikiria jambo fulani la kumshawishi
Lisa ahudhurie.” John Masawe alisema. •••
Lisa alilazwa hospitalini kwa siku tatu kabla ya kuruhusiwa kurudi nyumbani.
Aliporudi nyumbani alishangaa kuona
kwamba Charlie alikuwa ameongezeka unene. Alifikiri kwamba paka huyo
angekuwa dhaifu kwa kukosa mtu wa
kumtunza ipasavyo siku chache
zilizopita.
Alvin alipofika nyumbani baadaye usiku
huo, alimsikia Lisa akinung'unika wakati
akimlisha paka. “Charlie, inabidi uache
kula sana. Angalia ukubwa wa tumbo lako. Ni kana kwamba una mimba ya
kujifungua!”
Tumbo la mimba la Charlie lilikuwa likiongezeka kadiri siku zilivyopita. Alvin
asingeweza kuweka siri hiyo kwa muda mrefu zaidi. Hata hivyo, bado ilikuwa
bora kuwa na mtu wa kumhudumia nyumbani. Alvin alitokea tena akiwa
amevaa nguo za kawaida za mapumziko. Lisa alikuwa tayari
ameshaandaa meza ya chakula.
Lisa alimwandalia Alvin meza ya
shukrani iliyojumuisha aina zake zote za vyakula anavyopenda. Macho ya
Alvin yaliwaka kwa furaha baada ya
kuvitazama vyakula
vilivyotapakaa mezani. “Nimechoshwa na kula vyakula vilivyochomwa na kukaangwa. Tengeneza hata supu au
kitoweo wakati mwingine,” Alvin
alijivungisha kama kawaida yake huku
akivishambulia.
Baada ya chakula cha jioni, Alvin alirudi
kwenye chumba cha maktaba
kuendelea na kazi. Alvin aliendelea na kazi hadi karibu saa sita usiku.
Lisa alitayarisha kahawa na kumpelekea. Alvin alikuwa ameketi
kwenye dawati, akichanganua hati zilizo
chini ya mwanga mkali huku akirejelea
kompyuta ya mkononi kwa wakati
mmoja. Jozi ya miwani yenye fremu za
dhahabu ilikaa kimya kwenye daraja la pua yake.
"Utaendelea kutazama hadi lini?" Lisa
alimuuliza Alvin wakati akimkaribisha
kikombe cha uji wa ulezi.
Alvin akafunga laptop yake na kugeuka
kumwangalia kwa utulivu kisha
akapokea kikombe cha kahawa.
“Sijawahi kukuona umevaa miwani hapo
awali. Nilikaribia kuzimia kwa sababu ya haiba yako ya kuvutia,”Lisa alisema huku akitabasamu.
“Bado hujaacha maneno yako?”
Lisa akaguna. Hatimaye, muda mfupi baadaye, alizungumza tena, “Mwonekano wako mzuri hunivutia kwa njia tofauti kila siku. Kadiri
ninavyokutazama, ndivyo ninavyozidi kuvutiwa nawe. Haichoshi…”
Kabla Lisa hajamaliza sentensi yake, ghafla mkono mkubwa ulionekana kumziba mdomo. Mkono wa Alvin ulinuka kama msonobari mkavu. Harufu hafifu ilimtuliza kwa kushangaza.
Muhimu zaidi, mkono wake ulikuwa na
joto sana!
"Nyamaza." Macho ya Alvin yalipepesa chini ya lenzi za miwani yake.
Alihisi mashavu yake yakiungua pia.
Baada ya kuondoa mkono wake,
aliweka kikombe cha kahawa kwenye meza. "Ninahisi lazima uwe umechoka
kufanya kazi usiku kucha. Kikombe cha kahawa kitakuchangamsha kidogo."
Alvin aliitazama ile kahawa iliyochanganywa kwenye mazima.
Hakika ilionekana kumvutia.
"Lisa , unajaribu kunifanya nishindwe kulala, hujui kahawa kufukuza usingizi?"
"Hapana, kahawa haifukuzi usingizi."
Alimshawishi. “Itakuchangamsha tu na kukufanya ujisikie na nguvu mpya kimwili na kiakili."
Alvin aimtazama huku pembe za mdomo wake zikicheza kwa dharau.
"Sawa. nitakunywa. Ila nikikosa usingizi ujue tutakesha wote hapa.”
“Usijali. Hata ukisema tulale pamoja
hadi asubuhi, nitafanya.” aliahidi.
“Sithubutu kutegemea hilo. Ninaweza
kufa kabla hata halijatokea.” Alvin alijibu
huku akijinywea kahawa yake.
Lisa ambaye alikuwa ametoka tu kudhihakiwa, alitoka nje ya maktaba
akiwa ameudhika. Aliapa kumthibitishia kuwa ipo siku angemtaka tu!.
SURA YA32
Saa saba usiku Lisa alishtushwa na
ndoto zake mbaya, ndipo akagundua
kuwa alikuwa anatokwa na jasho
kwenye paji la uso wake. Mara moja
akawasha taa. Utulivu ulikuja juu ya
mwili wake taratibu huku mwanga
ukitawala giza.
Alikuwa ameota juu ya kufungiwa ndani ya nyumba ile yenye giza tena. Sehemu
hiyo ilijaa kila aina ya kelele za kutisha
usiku. Kwa hofu, alijikunja ndani ya shuka. Ilikuwa ni shida kwake kulala peke yake sasa. Baada ya muda wa kufikiria, alijifunika blanketi na kubisha hodi kwenye mlango wa chumba cha kulala cha Alvin.
“Nani huko?” Alvin, ambaye alikuwa amekereka kwa kuamshwa usiku wa
manane, aliuliza kwa sauti iliyojaa hasira. “Ni mimi.” Lisa aliitikia kwa hofu. Nusu
dakika ikapita kimya kabisa. Alipotaka kukata tamaa, mlango ulifunguliwa
ghafla kutoka ndani. Alvin akatokea upande wa pili wa mlango. Nywele zake
zilikuwa zimevurugika na macho yake
meusi yalionekana kuogopesha.
"Afadhali uwe na sababu nzuri ya kunisumbua."
“Naogopa kulala peke yangu…” Lisa alitetemeka. Alivin aliinua macho yake taratibu.
Jasho lilikuwa likimvuja Lisa usoni kwa sababu ya hofu. Hata hivyo, alishangazwa na blanketi alilokuwa ameshikilia mikononi mwake.
"Hii ni mbinu yako nyingine ya kunitongoza?" Alvin alikiri moyoni mwake kuwa karibuni uzalendo ungemshinda. Hata hivyo, alikuwa amechoka sana na kazi za kutwa nzima
na bado alihitajika kuamka mapema
kwa ajili ya kesi mahakamani kesho
yake. “Ni usiku sana. Nahitaji kulala
hata kama wewe huna haja ya kulala.”
"Sio hivyo." Lisa hakutaka kubaki peke
yake chumbani kwake. Aliongeza nguvu
na kuvuta kona ya mkono wake. “Tangu
nifungiwe kwenye nyumba ya giza kijijini
naogopa kulala peke yangu usiku.
Ninasumbuliwa na jinamizi la kutisha. Tafadhali niruhusu nilale japo kwenye
sakafu ya chumba chako. Niko serious.”
“Si ulikuwa umelala vizuri hospitalini?”
"Nilikuwa na mlezi wakati huo." Lisa alijitetea huku akitetemeka.
Ni Alvin ambaye alikuwa amemuokoa
kutoka kwenye nyumba hiyo ya zamani. Mahali hapo palikuwa kimya sana na giza muda wote kama usiku. Hata
mwanaume angepatwa na kiwewe
baada ya kufungiwa mle ndani kwa siku tatu. Lisa aliona kusita kwake kama kukubali, na akatoa ahadi haraka. "Naapa sitakusumbua."
“Kumbuka ahadi yako.” Alvin alirudi
kitandani kwake bila wasiwasi.
Baada ya kupata kibali chake, Lisa haraka akaweka blanketi kwenye
sakafu karibu na kitanda chake. Alvin alikaa makini kwa muda mfupi lakini
punde akapitiwa na usingizi. Hata hivyo muda fulani baadaye, kilio cha Lisa kilimwamsha tena.
“Fungua mlango… Tafadhali… ni baridi… giza sana… ninaogopa.”
Alvin akajiinua kutoka kitandani.
Mwangaza wa mbalamwezi
uliomiminika kupitia dirishani ulimulika
kivuli chini. Lisa aliyekuwa amejikunja
ndani ya blanketi alikuwa ameziba
masikio yake kwa nguvu. Mwili wake
wote ulikuwa ukitetemeka kwa hofu.
“Lisa amka. Ni ndoto tu.” Alvin alitoka
kitandani ili kumvuta mikono. Lakini, Lisa alikuwa kazama kabisa katika
ndoto hiyo mbaya. Uso wake wa hofu
ulikuwa umepauka kama kauzu. Akiwa
hana njia nyingine, akamvutia kifuani
kwake na kumpigapiga mgongoni
taratibu. "Ni sawa. Uko salama sasa…” Sauti ya Alvin ilikuwa na athari ya kutuliza
ambayo polepole ililegeza mkazo
mwilini mwake.
Uso wake mdogo ulisukumwa kifuani
mwake. Nywele zake za giza
zinazong'aa zilikuwa zimening'inia
mabegani mwake huku nyuzi kadhaa
zikiwa zimepigwa plasta kwenye ukingo
wa uso wake wa kusikitisha lakini mzuri.
Pia alitoa harufu hafifu ya kutuliza. Hii
haikuwa harufu ya manukato, badala yake, ilikuwa harufu ya shampoo yake.
Hakuwahi kutambua jinsi shampoo yake
ilinukia vizuri hadi wakati huu. Harufu
hiyo ilimfunika taratibu hadi akafumba
macho hatimaye. Aliwaza kumwachia
mara baada ya kutulia kabisa. Hata
hivyo, ilikuwa tayari asubuhi iliyofuata
alipofungua tena macho yake.
Wawili hao walijikuta wakitumia kitanda kimoja, shuka moja na mto mmoja.
Mkono wake wa kushoto na mguu wa kushoto ulikuwa umewekwa juu ya mwili
mwake. Kulikuwa na tabasamu la
kudumu kwenye pembe za midomo
yake. Ilionekana alikuwa na usingizi mzuri. Alvin pia hakujisikia raha. Alihisi hata
kwa sekunde ya haraka kwamba
walikuwa kama wanandoa wapya. Alvin
aliwaza bila kufikiria kwa sekunde
chache kabla ya kunyanyua blanketi
kwa uangalifu ili asimame. Bila
kutarajia, mtazamo chini ya blanketi
ulimshangaza. Karibu vifungo vyote vya
pajama za Lisa vilitenguliwa. Wakati
huo Lisa naye alifungua macho yake
polepole. Macho yao yalikutana na
mboni zake zlipanuka polepole.
Alipiga kelele kwa mshtuko sekunde tu alipogundua kuwa alikuwa amelala
mikononi mwa Alvin. Lisa alinyanyuka kwa haraka na kujiweka mbali na mwanaume huyo. "Kwa nini ... kwa nini umenileta kitandani kwako?"
Alvin alidhihaki kwa kutoamini.
“Ulinizunguka huku ukilia wakati ukiota ndoto mbaya jana usiku. Nilikuwa nikikufariji na kukutuliza…”
“Umenifariji?” Aliona jambo hili kuwa gumu kuamini. Uso wa Alvin ukajaa hasira. “Unajaribu kusema nini? Lisa, sema kweli sasa
hivi. Je, jana usiku kilikuwa ni kitendo cha makusudi? Ulikuja chumbani
kwangu ili kunitega, huh?"
“Sijui unazungumza nini. Nililala vizuri sana.” Alikumbuka bila kufafanua kuwa
alipata ndoto mbaya mwanzoni, lakini
alihisi amani wakati sauti ya upole ilinong'ona masikioni mwake. Subiri, sauti hiyo ya upole ilikuwa ya Alvin?
Alvin alimtazama kwa macho makali wakati anainuka na kusimama. "Kabla hujaendelea kuongea, angalia hali ya nguo zako za kulalia."
Akiwa amechanganyikiwa, Lisa
alishusha macho yake. Sura ya mshtuko na aibu ilimwangazia usoni mwake alipojiona alivyokuwa kifuani.
Mikono yake iliruka kukifunika kifua
chake mara moja.
Alvin akafoka. “Uigizaji mzuri. Nina hakika ulifungua vifungo hivyo kwa siri ili kunitega.”
“Sina haja ya kufanya hivyo.” Lisa
alijisikia kulia wakati huu. “Vifungo
vilifunguka vyenyewe. Si kosa langu
kuwa na matiti makubwa.”
"Kwa hivyo kama una matiti makubwa ndiyo uyaache waziwazi? Sema tu
ukweli kuwa unajaribu kunitega." Alvin
alisema huku akimtazama Lisa kwa
dharau. “Ndiyo! Um… Ninaweza kueleza hili. Ni kwa sababu mimi…nakupenda kupita
kiasi,” Lisa alisema kwa sauti iliyotiwa chumvi. Akiwa amechanganyikiwa, alisonga mbele na kuishika shingo ya Alvin. Kwa kweli, Alvin alishtushwa na kitendo chake cha ghafla na ambacho hakuwa amekitarajia.
‘Je, mwanamke huyu alikuwa akijaribu
kumlazimisha busu?’ Alvin alijiuliza
huku picha ya midomo yake nyororo
ikaingia akilini mwake. Alisita kwa
sekunde kadhaa kabla ya kusikia
maumivu makali mashavuni mwake.
Lisa alikuwa amempiga Lovebite!. Alvin alimsukuma Lisa kwa nguvu huku
mkono wake ukiruka kufunika sehemu aliyong’atwa.
“Lisa, unathubutu vipi? Usifikiri sitakuadhibu kwa hili.” Macho ya Alvin yalikuwa kama miali ya moto.
Lisa akacheka tu kwa mzaha huo na kumwambia. “Kwani hujawahi kuiona kwenye sinema za kihindi? Waigizaji wakuu huwa wanamng’ata mtu wanayempenda sana. Nilikuwa najaribu tu kuacha alama kwako.”
Alvin akapiga hatua kadhaa mbele, huku akiwa ameuma meno kwa hasira.
"Unanichukulia kama mjinga sivyo?"
"Sawa, unaweza kuning’ata na wewe kulipiza kisasi." Lisa alijikaza na kuinamisha uso wake karibu na Alvin.
"Ning’ate kwa nguvu kadri uwezavyo.
Ukining’ata kwa nguvu zaidi nitajua unanipenda zaidi.”
Bila hata kujiuliza, Alvin alikiweka
kichwa cha Lisa katikati ya viganja vyake na kumng'ata kwa nguvu kwenye shavu. Shavu nene la Lisa lilikuwa nyororo na laini kama jeli. Hakutaka kusogeza midomo yake mbali.
“Loo!” Lisa alipiga kelele kwa uchungu.
Hatimaye, Alvin baada ya kuona meno yakiwa yameganda kwenye mashavu yake yaliyonenepa, alimwachia.
"Kumbuka adhabu hii."
Lisa alijifanya mwenye haya licha ya maumivu. "Hapana, hii siyo adhabu, huu ni uthibitisho wa upendo wako."
"Endelea kuota." Alvin alicheka kwa
kejeli kabla ya kuingia bafuni na
kufunga mlango kwa nguvu. Taswira
kwenye kioo ilionyesha alama za meno kwenye shavu lake mwenyewe. Alihisi
kukimbilia mlangoni ili kumchana mwanamke huyo vipande vipande.
Ilimbidi awe mahakamani siku hiyo kwa
hiyo ilimbidi aende akiwa amevalia barakoa. Akiwa amekasirika, Alvin
alipata tu kifungua kinywa kidogo kabla ya kuondoka nyumbani.
Saa tatu asubuhi Alvin aliwasili ofisini
kwao. Sam alimpokea kwa swali, “kwa nini umevaa barakoa? Unaumwa?"
Alvin alikataa kujibu. "Eh, ni vizuri kuwa unajali na kuvaa barakoa ili kuzuia
kueneza korona. ” Sam alimpongeza
baada ya kumuona yupo kimya.
Baada ya kukamilisha taratibu kadhaa
za kiofisi, walielekea katika mahakama ya Kisutu kwa ajili ya kusimamia kesi.
Dakika kumi baada ya kuwasili kwao,
kesi ilikuwa karibu kuanza. Sam nusura
aangue kicheko hadharani wakati Alvin alipotoa barakoa yake na kufichua
alama za meno kwenye shavu lake.
"Ni nini …?"
"Nimeng’atwa na mbwa." Sauti kali ya Alvin ilisikika kwa vitisho. Aliingia ndani ya chumba cha mahakama kwa hatua kubwa.
Sam hakuweza kujizuia tena kuangua
kicheko. Alvin alifikiri angeweza kumpumbaza? Mwanamume huyo
alikuwa ameng’atwa na mwanamke.
Hakuwahi kumuona Alvin akiona aibu
vile. Kwa hiyo alimpiga picha kwa siri na kuituma kwenye group lao la whatsapp.
SURA YA 33
Lisa alipumzika nyumbani kwa siku
kadhaa, akisubiri alama za meno
shavuni kwake kutoweka kabla ya kwenda kutafuta kazi mpya. Lakini, kila alikotuma maombi ya kazi, alipokea maoni hasi tu.
"Bi Jones, samahani lakini hatuajiri waizi wa kazi za wangine."
"Bi Jones, kashfa yako imekuwa habari ya kawaida katika sekta ya ujenzi.
Hakuna mtu anayethubutu kukuajiri tena.”
"Bi Jones, familia ya Jones Masawe imetangaza kwenye mtandao wa sekta nzima kwa siri kwamba mtu yeyote ambaye atathubutu kukuajiri atakuwa anawadharau waziwazi."
Lisa alikutana na majibu kama hayo
kwenye mahojiano ya kazi na makampuni kadhaa aliyotuma maombi.
Alikatishwa tamaa kabisa na kupandwa
hasira kwani alikuwa ametumia muda
mwingi na bidii katika elimu yake lakini
bado hakuweza kupata kazi.
“Pipiii…” Mara akagutushwa na sauti ya honi. Gari lililokuwa karibu naye lilipiga
honi mara kadhaa. Hakutambua kama mtu huyo alimkusudia yeye hadi alipomwita jina lake. "Lisa !"
Lisa alitazama kwenye gari hilo na kuona uso mzuri ukichungulia nyuma ya dirisha la Range Rover. “Joseph? Unafanya nini hapa?" Lisa alipatwa na mshangao wa furaha baada kumuona mwandamizi wake kutoka Chuo Kikuu
cha New South Wales alikokuwa ameenda kusoma.
“Nina ofisi katika jengo hili. Nilikuona ukitoka nje nikashangaa unafanya nini hapa." Joseph aliegesha gari lake
pembeni na kumpa ishara aingie ndani.
Lisa alipoingia ndani ya gari alijibu kwa
kinyonge, “Nimekuja kwa mahojiano ya kazi, lakini sijafanikiwa.”
“Hata wewe hukuweza kufanikiwa na sifa zako?” Joseph aliona jambo hilo
kuwa gumu kuamini.
“Nimekosana na familia yangu na wananichafua kwenye mtandao mzima wa sekta ya ujenzi. Sifa yangu yote
inazidi kuporomoka!” Lisa alimwambia
Joseph kwa huzuni na kumweleza kila kitu kwa undani wake.
“Siamini kwamba unaweza kuiba kazi
za wengine. Inapaswa kuwa kinyume chake." Tabasamu likatanda usoni mwa
Joseph. "Sawa, nimeanzisha kampuni mpya hapa Dar es Salaam na bado sina
wafanyikazi wa kutosha. Njoo ujiunge na timu yangu."
Lisa alishtuka na kuguswa wakati huo
huo. “Huna shaka nami hata kidogo?”
"Najua wewe ni mtu mzuri wa tabia na ninafahamu vyema vipaji vyako.
Nilikuwa nimekupendekezea hapo awali kwamba tuanzishe biashara pamoja
huko Uganda baada ya kuhitimu, lakini ulisisitiza kusaidia biashara ya familia na kukaa karibu na mpenzi wako. Vipi umeolewa sasa hivi?" Joseph aliuliza.
Lisa akainamisha kichwa kwa aibu na kujibu. "Tuliachana."
Joseph alionekana kushangaa lakini haraka akamfariji kwa upole. "Ni sawa.
Bado wewe ni kijana na mrembo. Nina hakika unaweza kupata mtu bora zaidi.”
"Inatosha kuzungumza juu yangu.” Lisa akahamisha mada. “Unafanya vizuri
sana kwenye kazi. Nilisikia umekuwa
mbunifu watatu bora zaidi huko Uganda
na hata kuchapisha vitabu kadhaa.” Lisa alitania huku
akitabasamu. "Na sasa unajaribu
kushindana hapa Bongo pia?"
"Jiunge na kampuni yangu ikiwa unadhani nina uwezo. Ninahitaji watu
wenye talanta kama wewe,” Joseph alimshawishi kwa bidii, “naweza kukupa mshahara mkubwa. Unaweza pia kuwa mwanahisa biashara itakapoingia sokoni.”
"Sawa, nitakuandalia chakula cha jioni leo ili kusherehekea kuwa bosi wangu."
Lisa hakika hakutarajia mshangao huu wa kupendeza. Alimpigia simu Alvin na kumwambia. “Sitakuwa nyumbani kuandaa chakula cha jioni. Panga mwenyewe."
Alvin alikasirika sana siku hiyo kwa
sababu wengine walikuwa wakimdhihaki
kwa siri kutokana na alama za meno
kwenye shavu lake. “Nini tena muda
huu? Usifanye ujinga wako ukidhani
nitakuokoa tena. Sina muda.” Alvin
alimjibu kwa hasira.
Lisa alimwambia kwa upole. "Ninaenda tu kula chakula cha jioni na rafiki yangu
niliyekutana naye nikiwa nasoma nje ya nchi."
Alvin alicheka kwa kejeli. "Loo, kwa hivyo ni rafiki kutoka chuo kikuu wakati huu. Usisahau jinsi ulivyotekwa hotelini na rafiki yako wa shule ya sekondari mara ya mwisho.”
"Nilikuwa nakupa taarifa tu. Kwaheri.”
Lisa alikata simu kwa papara.
Hali ya kukatishwa tamaa iliangaza machoni pa Joseph alipouona uso wake wenye hasira. “Mpenzi mpya? Au mume?”
Alitoa macho kwa mshtuko. "Hapana. Ni
mwenzangu tu… Housemate.” Lisa
hakuwa amekosea hata hivyo kwa
kujibu vile. Ingawa Alvin alikuwa mume wake halali wa ndoa, mwanamume
huyo alikataa kukiri hilo. Kwa hivyo, uhusiano wao ulikuwa wa maonyesho tu. Joseph alitoa tabasamu hafifu.
"Ilionekana kama unazungumza na mpenzi wako."
“Um… Kweli?” Lisa alihisi mapigo ya moyo yakirukaruka. Hivi ndivyo
alivyokuwa akitangamana na Alvin. Labda ilisikika tu kwa sababu walikuwa
wakiishi katika nyumba moja.
Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu
alipokutana na Joseph huko Marekani.
Wawili hao walifurahia jioni pamoja na
chakula cha jioni kilidumu hadi saa tatu
usiku. Alimpa lifti na kumpeleka hadi
nyumbani kwani siku hiyo Lisa hakuwa
anatumia gari lake.
“Kumbuka kuripoti kwangu kesho asubuhi. Nimechukua mradi wa jengo la kifahari katika eneo la Mbezi Beach.
Utaenda kuchukua vipimo kesho."
“Hakika.” Lisa alimpungia mkono wa kwaheri. Macho yake yaliikodolea gari hiyo aina ya Range Rover kwa mbali
kabla hajageuka kuelekea nyumbani.
Kwa bahati mbaya, alimgundua Alvin, akiwa amevaa nguo za kawaida za
mapumziko akimtazama chini kwa
hasira kutoka kwenye ngazi. Charlie
alikuwa ametulia mikononi mwake, akionekana kama alikuwa karibu kulala.
“Rafiki yako ni mwanaume?” Alvin
aliuliza kwa hasira, ndita zilizokuwa
zimekunjwa katikati ya macho yake
zingeweza kumfinya inzi hadi kufa.
Alipofikiria jinsi ambavyo alilazimika
kuvumilia chakula kilichotengenezwa
mgahawani vibaya wakati Lisa alifurahia
jioni hiyo kula na kucheka na mwanaume mwingine, hasira ilimpanda kama mawimbi ya bahari.
“Ndiyo, yeye ni mwandamizi wangu kutoka chuo kikuu…”
Alvin alimkatisha. “Lisa, ngoja nikukumbushe kuwa umeamua kuolewa na mimi. Afadhali uangalie matendo yako hata kama tuko kwenye ndoa ya mkataba. Sitaki kusalitiwa.”
Tabasamu usoni mwa Lisa likaganda.
“Unasemaje? Nilitoka tu kwenda kula
chakula cha jioni na rafiki. Je, unanifikiria miye ni mhuni sana?”
"Nani anajua? Nimekufahamu kwa muda mfupi tu.” Alvin aliongea kwa
tabasamu la kejeli. "Mbali na hilo, huwezi kwenda tu kwa chakula cha jioni na kusahau kuhusu jukumu lako kama
mhudumu wa Charlie. Unawajibika kwa
ajili yake kwani wewe ndiwe uliyemsababishia ugonjwa.”
“Charlie yuko sawa sasa. Nadhani hata
aliongezeka kilo chache,” Lisa alijibu kwa upole. Bila shaka angebishana naye ikiwa asingekuwa kaokoa maisha yake mara mbili.
Alvin alicheka. “Sawa, kwa nini
ameongezeka uzito? Unapaswa kujitafakari. Nataka umtunze paka, sio kumnenepesha.”
Lisa alishindwa cha kusema.
Kuongezeka kwa hamu ya kula kwa
Charlie lilikuwa kosa lake pia.
Alikaribia kushindwa kuzuia hasira
iliyokuwa ikifuruma kifuani mwake.
"Sawa, nitampa paka chakula kidogo
kuanzia sasa."
"Hilo halitasaidi pia." Alvin bado
alimkalia vibaya. “Je, ikiwa paka ndani yake atakuwa na utapiamlo?”
“Sawa, unataka nini basi? Samahani, lakini mimi si mfugaji wa paka kitaaluma.” hatimaye Lisa alisema kwa hasira.
“Hata mimi sijui.” Alvin naye akajibu kwa ukali. “ Ifanyie utafiti na umfikirie zaidi
Charlie. Mpeleke matembezini ukiwa huru. Usimpe chakula tu kisha umruhusu alale siku nzima.” Kisha
kusema hayo, Alvin alitembea kuelekea
kwenye bustani ya jirani na Charlie mikononi mwake.
Lisa aliishia kumshangaa tu mwanamume yule mwenye gubu.
Alitaka kushiriki naye furaha ya kupata
kazi mpya, lakini hakuweza kujisumbua
kuzungumza naye kwa sekunde
nyingine zaidi. Alipokuwa akiingia ndani
kuelekea chumbani kubadilisha nguo, sauti kali ilisikika nyuma ya mgongo wake. "Nina njaa."
Alitazama nje na kumwona mtu
aliyeketi kwenye bustani, akionekana kama mnyama mwenye njaa kali anayesubiri kulishwa.
Lisa alikataa, kwani bado alikuwa amekasirika kutokana na kejeli zake hapo awali. "Samahani, mimi ni mhudumu wa paka wako, sio mhudumu wako." Alisisitiza maneno matatu ya mwisho. Alvin alionekana kutopenda. Alichia tabasamu la kejeli na kuongea kwa sauti ya kutetema. "Huu ndio upendo unaotangaza kuwa wewe ni mke wangu?"
'Ninachotaka ni nafasi ya kuwa
shangazi wa Ethan! Umeipata hiyo!'
Lisa alijiwazia, lakini hakuthubutu
kuyasema maneno hayo kwa sauti.
Akiwa amekasirika kidogo, aliingia jikoni na kuanza kuandaa chakula.
Alvin alikuwa akisubiri chakula kwa hamu akiwa anazunguka bustanini na paka wake. Hakuna chochote zaidi ya chakula alichotayarisha Lisa kilichomtia hamu tena. Labda alikuwa amemtilia
dawa kwenye chakula alichokuwa anakula muda wote huo.
Baada ya kifungua kinywa asubuhi
iliyofuata Alvin alikuwa amevaa kiofisi
tayari kuelekea kazini alipogundua Lisa
naye alikuwa amebadilika na kuvaa
kimtoko-mtoko hivi. Lisa alikuwa
amevaa shati la waridi iliyokolea na
suruali ya jeans iliyombana kidogo.
Alionekana kama mfanyabiashara
hodari, lakini mavazi hayo pia
••••••
yaliangazia umbo lake mwanana.
Isitoshe, alikuwa amejipodoa kidogo na hereni za lulu zilining'inia chini ya masikio yake. Aliona ni vigumu kumvua macho mrembo huyo.
Alvin aligundua kuwa Lisa alikuwa akitoka. “Unatoka kwenye miadi yako tena?” Sauti yake ilikuwa ya chini
ikionyesha kutofurahishwa kwake.
“Hapana, naenda kazini. Nilipata kazi mpya jana. Nitakuwa nyumbani
kuandaa chakula cha jioni na pia kumtembeza Charlie baada ya hapo.”
Alvin hakupata maneno ya kubishana na hilo. Pamoja na hayo, hakuwa na wasiwasi kuhusu kazi yake.
Akamuuliza. "Unagawa vipeperushi tena?"
"Hapana. Mimi ndiye mbunifu mkuu
wakati huu." Alicheka kabla ya
kuchukua mkoba wake na kuondoka
mlangoni. Alvin alimfuata nyuma yake na kutoka naye pamoja. Koo lake lilihisi kukauka
huku akiibia jicho lingine la umbo lililopinda la yule mwanadada. “Unataka lifti?”
“Hapana, asante.” alikataa bila kusita. “Nitaendesha gari.” Alvin hakuwa na la kusema.
Saa mbili na nusu asubuhi Lisa aliingia
katika eneo lake jipya la kazi kwa wakati
ufaao. Ilikuwa ni mshangao kujua
kwamba wafanyakazi wengine wote
walikuwa vijana na wenye shauku.
Mbali na hilo, wote walikuwa wahitimu
tofauti ambao walikuwa wamesoma nje ya nchi.
Joseph alimtambulisha Lisa kwa
wafanyakazi wenzake kabla ya kuingia
naye ofisini. Kisha alitoa ramani. "Hii ni nyumba ya Bw. Kelvin Mushi yenye
ukubwa wa mita za mraba 3,000 katika
eneo maarufu la Mbezi Beach. Huyu mtu aliwahi kuwekeza ng'ambo biashara
zake na ndivyo nilivyokutana naye. Tumefahamiana kwa muda mrefu sasa.”
Joseph alitikisa kichwa kwa umakini. "Anapanga kutulia nyumbani hapa Dar
es Salaam kwa hiyo anataka
kutengeneza jumba hili kwa ajili ya
makazi. Fanya bidii kwenye mradi huu.
Hakuna kikomo cha gharama kwenye
ukarabati, lakini kila kitu lazima kiwe
kamili. Ana mradi mwingine unaosubiri kuzinduliwa mwishoni mwa mwaka.
Natumai kujenga naye ushirikiano wa muda mrefu.”
Tabasamu likatanda tena usoni mwa
Joseph. “Kwa kweli, rafiki wa kike wa
mpwa wa Bw. Mushi anatoka katika
historia ya ubunifu majengo na mambo
ya ndani, lakini Bw. Mushi hakutaka
kutumia kampuni hiyo kwa sababu
hapendi sana ubunifu wao hivyo
anakarabati jumba lake kwa siri bila
kumwambia mtu mwingine yeyote wa familia yao, kwa hivyo na wewe huna
budi kuficha hili. Usifanye mambo kuwa magumu kwa Bw. Mushi.”
Bila kukawia, Lisa alitoka ofisini na
kuendesha gari hadi Mbezi Beach. Hiki ni miongoni mwa viitongoji vya kifahari
zaidi hapa Dar es Salaam. Ni matajiri tu ndio wanaweza kumudu kujenga mali
hapo.
Gari lake lilisimamishwa na mlinzi
kwenye mlango wa geti, hivyo ikabidi
atembee hadi ndani. Mwanamume
aliyeonekana kuwa na umri wa miaka
30 hivi alikuwa amesimama kando ya kidimbwi cha kuogelea. Mtu huyo mrefu
alionekana kuwa na sura ya upole. Suti
nyeusi ya biashara iliyotengenezwa kwa
ufundi ilimpendeza sana.
Kwa mshangao, Lisa aliuliza kwa utulivu, “Bw. Mushi?”
“Ndiyo. Je, wewe ni mbunifu kutoka
kampuni ya Joseph? Wewe ni mdogo kuliko nilivyotarajia." Mshangao wa kweli uliangaza machoni pa Kelvin Mushi.
“Joseph alinitangulia mwaka mmoja
katika chuo kikuu. Bw. Mushi, unakaribishwa kunibadilisha ikiwa
haujaridhika baada ya kuona kazi yangu.” Maelezo ya Lisa yalikuwa
shwari na ya kujiamini. "Mbali na hilo, sidhani umri una uhusiano wowote na uwezo. Wewe mwenyewe ni kijana sana, Bw. Mushi.”
Kelvin alitabasamu. "Siwezi kubishana na hilo."
Lisa alimpatia Kelvin business card
yake. Kelvin akaitazama. "Lisa Jones Masawe. Jina maarufu sana hili."
“Ni jina la kawaida kabisa.” Lisa alihisi
moyo wake ukirukaruka. Kwa kuhofia kwamba huenda amesikia kuhusu
uvumi mbaya unaoenezwa na familia ya Masawe. “Ikiwa haujali, Bw. Mushi, unaweza kuniambia mawazo yako tunapozunguka jumba hili la kifahari.”
Kelvin aliongoza njia na kumuonyesha
kila sehemu ya jumba hilo. Mbali na hilo, alitaja matakwa yake ya kuwa na ukumbi wa mazoezi, ukumbi wa michezo, uwanja wa mpira wa kikapu, na bwawa la kuogelea la ndani.
Lisa alikuwa na wazo la jumla la liliendana na matamanio yake. Katika
chini ya nusu saa, alimpatia mchoro
mzuri mikononi mwake.
Kelvin aliutazama mchoro ule, hakuweza kupata kitu cha kubaini makosa. Mpango huo wa kubuni ndio hasa alikuwa ameufikiria. "Bi jones, wewe ni mzuri kama wabunifu wakubwa ambao nimewaona kutoka nje ya nchi. Sio mbaya. Wazo la bwawa hili la kuogelea la ndani ni la kibunifu kweli.”
"Itaonekana bora zaidi baada ya kuisanifu." Lisa aliongezea.
“Hakika, una muda wa wiki moja.
Ningependa kuanza ukarabati haraka iwezekanavyo.” Kelvi akampa Lisa business card yake. “Unakaribishwa kunitafuta ofisini kwangu michoro itakapokamilika. Hii ni kadi ya jina langu."
Kadi ile ilionyesha Kelvin Mushi alikuwa ni mkurugenzi wa kampuni ya
Usafirishaji, Golden Corporation.
Baada ya kuondoka kwenye jumba lile, Lisa alipanga kuangalia miundo ya majengo mengine ya kifahari katika
kitongoji hicho. Alipotoka tu nje ya geti, aliona Harrier nyeusi ikiingia kwenye
moja ya majengo makubwa ya kifahari. Hilo lilikuwa gari la Alvin.
‘Ina maana amenunua nyumba huku
pia?’ Lisa alijiuliza bila majibu kabla ya kushtuliwa na sauti ya kiume. “Kwa nini uko hapa?” sauti aliyoifahamu vizuri ilisikika nyuma yake ghafla. Ethan
alikuwa kasimamisha gari pembeni kidogo mwa barabara akitazamana naye. Lisa alitazama na kumwona
Ethan akitoka kwenye Lamborghini yake. Wakati huo alikuwa akigeuka ili
kuondoka, lakini alishtuka kidogo
kugongana naye hapo.
“Mimi ndiye ninayepaswa kuuliza. Wewe na Lina mnapanga kununua
jumba la kifahari hapa, au unatafuta nini huku?" Lisa alirudisha swali.
“Hapana. Niko hapa kuangalia nyumba ya mjomba wangu. Jumba lake linahitaji kukarabatiwa na ninapanga kumshawishi kukabidhi mradi huo kwa
Lina.” Ethan alimwambia Lisa huku akimkazia macho usoni. “Unaona Lisa, ningeweza kumshawishi mjomba akupatie huo mradi wa kukarabati jengo lake la kifahari kama mimi na wewe tungekuwa bado tunaelewana vizuri.”
Ethan alimwambia kwa kujidai.
Hapo awali Lisa aliliona gari la Alvin na punde akamwona Ethan mitaa hiyohiyo, je hii ilikuwa ni bahati tu? Kwa kuwa
wawili hao walikuwa wamefuatana na aliamini walikuwa na uhusiano wa mjomba na mpwa, Lisa alihisi kuwa
Alvin alikuwa amenunua jumba la kifahari huko Mbezi Beach na Ethan
alitaka amshawishi ili ampatie Lina kwa
ajili ya kulikarabati. Hilo lilimuuma sana
Lisa. Ethan alitabasamu kwa dharau alipoona hali ya mawazo imeifunika sura ya Lisa.
" Unajutia maamuzi yako sasa? Na bado, utajuta sana!”
Lisa alikasirishwa na maneno ya Ethan nusu ya kutema damu. Lisa alimshangaa Ethan kwa kufikiri alikuwa
akimuwazia yeye. Ni mawazo ya Alvin ambayo yalimfanya akose raha muda
huo. Alijiuliza kwanini Alvin anunue jumba huko kisirisiri kisha amkabidhi
Lina mradi wa kukarabati jumba hilo?
Hicho ndicho hasa kilikuwa kikimuuma
Lisa. hata kama hakuridhika na ubunifu
wa Lisa, ulikuwa ni uamuzi wake
kuchagua kampuni nyingine yoyote ya kubuni muundo wa ukarabati wa jumba
lake, lakini siyo kukabidhi mradi wa ukarabati kwa Lina!
"Sawa, mjomba wako ndiye mwenye
uamuzi wa mwisho juu ya nani atampa kazi ya ukarabati, sio wewe. Labda
atashawishiwa kwa urahisi na mke wake. Maneno yako ni kama kinyesi tu kwangu." Lisa alimjibu Ethan kwa hasira. Ethan alikunja uso baada ya kusikia hivyo. “ Mjomba wangu bado hajaoa. Isitoshe mimi na yeye zinaiva sana, na kwa kawaida huwa anakubali chochote ninachomwambia.”
Lisa alitabasamu kwa dharau. “Hakika
muombe akufanye mrithi wa mali zake na uone kama atakubali.”
“Umerukwa na akili.” Uso Ethan ulibadilika kwa hasira. “Si ajabu
kwamba Mjomba Jones na Shangazi
masawe walikufungia kwenye jumba lao
huko Moshi. Hakika unastahili.”
Maneno yake yalichochea chuki
iliyozikwa ndani ya moyo wa Lina. "Ethan, unafahamu lakini unachokiongea?"
“Kwani nimekosea? Uliwaambia waandishi wa habari kwamba familia ya Masawe ilikufungia na kukutesa. Lakini unaonekana mwenye nguvu na mwenye
afya kwangu, kana kwamba umekuwa ukiishi vizuri. Uwepo wako ni bahati
mbaya sana kwa familia ya Masawe. Unajua kwamba kwa sababu ya
shutuma zako, sifa ya Kibo Group
zimeharibiwa na bei yao ya hisa
imeshuka sana? Thamani ya soko ya kampuni ilipoteza dola milioni mbili kwa usiku mmoja.”
Lisa alihisi hamu kubwa ya kummeza
Ethan mzima mzima. "Kitu pekee
kinachonifanya nisikitike ni kwamba, mwanzoni nilipoteza muda wangu
kukupenda sana bila kujua kuwa huna
akili hata kidogo. Akili ulizonazo
zinakutosha kujua chakula tu na njia ya kwenda chooni, basi!"
Ili kuepuka asije akapandisha hasira
mbaya nakufanya mambo
yasiyotarajiwa, Lisa aliwasha gari, akakanyaga mwendo na kuanza kuondoka.
SURA YA34
"Subiri." Ethan
alimzuia na kumwambia. “Sherehe
yetu ya uchumba na Lina imepangwa
mwishoni mwa mwezi huu. Lazima
uhudhurie sherehe hiyo. Ni wewe
uliyeharibu sifa ya Kibo Group hivyo
unawajibika kuiokoa.”
“Bullsh*t! Niondokee hapa ,wenda
wazimu wewe. Siwezi kusubiri kuona
Kibo Group ikifilisika kabisa. Ulisaliti
uhusiano wetu na bado una jeuri ya
kunidai nijitokeze kwenye sherehe yako
ya uchumba. Una wazimu nini! Huna hata aibu?!" Lisa alilaani.
Ethan hakuonesha hata wasiwasi.
Alizidi kumzuia Lina na kumwambia tena.“Sherehe yetu itaambatana na kumbukumbu ya kuadhimisha miaka 80 ya kuzaliwa kwa bibi yako. Alikupenda
sana tangu ukiwa mdogo, unajua! Na afya yake inazidi kuzorota kila siku, na nani anajua amebakisha muda gani?
Bado hutaki kuhudhuria?”
Mwili wote wa Lisa ulimsisimka huku
akimtazama Ethan kwa hasira kali.
“Yaani sherehe ya kuzaliwa bibi yangu
mnaijumuisha na mambo yenu ya kijinga?”
"Na ukiacha kuja bibi yako atasema
unamdharau, kumbuka bibi yako ndiye
mtu pekee aliyebaki anakupenda!"
Maneno ya Ethan yalijaa dharau.
“Usijali. Nitakuja." Lisa alikubali kwa hasira na kuondoka. 'Nitakuwepo na mjomba wako Alvin. Nataka kukuangamiza wewe na mchumba
wako asiye na maana kabisa!’ Lisa alijisemea kimoyomoyo wakati anaondoka. 'Nataka kumfanya mjomba wako kuwa mtiifu kwangu 100%. Lina
hataweza kujiunga na familia yenu mradi tu sitakubali!' Lisa alijiwazia kwa hasira.
Ethan alitikisa kichwa kwa dharau
wakati akimwangalia Lisa akitokomea
kwa mbali. Baada ya Lisa kupotea machoni mwake, Ethan alitembea
kuelekea kwenye jumba la kifahari la mjomba wake, Kelvin Mushi.
Kelvin alikuwa akikagua mchoro
alioachiwa na Lisa kwenye kiti cha
mapumziko chini ya mti. Alikunja uso na
kuuficha mchoro ule kwa siri baada ya kugundua kuwasili kwa mpwa wake.
"Mjomba, lini utaanza kukarabati jumba lako?" Ethan alikuwa ameona mchoro
kabla haujafichwa.
"Ulisikia kutoka kwa bibi yako sivyo?"
“Ndiyo,” Ethan alijibu huku akitabasamu.
“Umelidhamiria kweli jambo hili? Acha
Kibo Group ishughulikie suala hilo. Lina mwenyewe ni mbunifu mzuri. Mpe
nafasi.”
Kelvin alizuia hamaki yake alipoinuka
na kusimama. "Ethan, najua mambo
kadhaa kuhusu wabunifu katika
kampuni ya Kibo Group. Mtindo wao wa ubunifu ni wa kifahari lakini ni wa
kizamani sana na unatofautiana sana
na malengo yangu. Nimeishi nje ya nchi
kwa muda mrefu sana na ninapendelea mitindo fulani ya kigeni.”
"Sawa, unaweza kuwasilisha mawazo yako kwa Kibo Group. Sifa ya kampuni yao imeathiriwa sana hivi karibuni. Mjomba, tafadhali unaweza kuwasaidia?”
"Hapana." Kelvin alipunga mkono wake hewani bila kusita. "Naweza
kukubaliana na chochote mbali na hili.
Nina viwango vya juu vya makazi
yangu. Nimekutana na Lina hapo awali. Kusema kweli, hana uzoefu na hajui
chochote kuhusu vifaa vya kisasa vilivyo
kwenye fasheni. Ataharibu tu nyumba yangu.”
Ethan aliona aibu kidogo. Ni mchumba wake walikuwa wakijadiliana, hata hivyo, hivyo alizidi kumpigania. "Lakini
alifanya vyema katika mradi wa Kituo
cha Utamaduni na Teknolojia..."
"Usisahau kuwa alishinda zabuni kwa
sababu tu nilimpambania! Ukaribu wangu na Mzee Kamote ndiyo ulimpa
nafasi hiyo." Sura ya kutofurahishwa ilijiosha usoni mwa Kelvin alipokuwa
akiongea kuhusu hili. "Mbali na hilo, unapaswa kushukuru kwamba Mzee
Kamote hakutufichua au tungekuwa katika matatizo makubwa."
Ethan alihisi moyo wake kuzama.
"Sawa, sio jambo kubwa ikiwa hukubaliani. Kwa hiyo unaenda kwa
mbunifu gani? Nauliza kwa udadisi tu na si kingine.” Ethan aliuliza huku macho
yake yakiwa yamelenga kwenye mchoro.
"Joseph Ruta, ni rafiki yangu kutoka
Uganda. Alifungua tawi hapa Dar es
Salaam.” Kelvin alikabidhi mchoro huo
kwa mpwa wake. "Hii imeundwa na
mmoja wa wabunifu wake. Alitoa
mchoro wa jumba zima la mita za
mraba 3,000 kwa chini ya nusu saa, bila
kusahau kutoa maelezo ya undani kikamilifu kulingana na mapendekezo yangu. Nimeridhika sana.”
“Lisa?” Ethan aliganda kwa sekunde kadhaa alipoona saini ya Lisa chini
kulia mwa mchoro. Alikumbuka kugongana naye getini hapo awali.
Ilivyoonekana, alikuwa hapo kubuni muundo wa jumba la mjomba wake.
"Ndio, huyo ndiye." Kelvin alijibu kwa
dhati. "Mjomba, huwezi kumwajiri Lisa," Ethan alisema kwa uchungu, "Yeye ni binti mdogo wa familia ya Jones Masawe niliyekuambia hapo awali. Aliwahi kuwa
mpenzi wangu lakini amekuwa na sifa
mbaya sana. Sio tu kwamba aliiba kazi
ya mtu mwingine, lakini pia aliharibu sifa ya wazazi wake mwenyewe.”
Hili lilimshangaza Kelvin. Haishangazi
alidhani jina hilo halikuwa geni akilini mwake. Lakini alipokumbuka tabia ya fadhili na adabu ya Lisa, alikunja uso.
"Sidhani kama anahitaji kuiga wengine, kutokana na talanta zake. Nimepata uzoefu mzuri wa kushughulika na watu wa aina zote katika ulimwengu wa biashara. Yeye ni kipaji adimu, na sidhani kama yeye ni mtu asiyeheshimika. Kinyume chake kabisa, Ethan, nadhani una chuki dhidi yake!”
“Kweli humjui vizuri Lisa mjomba!”
“Mbona unanishangaza?
Tulipozungumza kwa simu siku za nyuma, hukuweza kuacha kumpongeza lakini sasa umechukizwa naye ghafla.
Je, alikukosea kwa namna fulani? Ni
wewe uliyemsaliti kwanza nikikumbuka vizuri.”
Ethan hakuwa na neno la kukanusha
jibu ambalo hakulitarajia. Kelvin akaendelea kumhutubia. "Vile vile,
unaendelea kujivunia vipaji vya Lina, lakini sioni uwezo wake. Kama si kweli
kwamba yeye ndiye mrithi wa familia ya Masawe, nisingemtazama kwa mara ya pili mwanamke kama yeye.”
Kelvin alichukua mchoro kutoka
kwenye mikono ya mpwa wake na moja
kwa moja akaelekea mlangoni.
Kelvin alikuwa tayari ameondoka muda
mrefu wakati Ethan alipotulia tena
kiakili. SURA YA35
Lisa alitumia karibu siku nzima akifikiria
kuhusu sherehe ya uchumba wa Ethan
na Lina.Hatimaye, ilikuwa wakati wa
kurudi nyumbani. Aliharakisha kurudi
nyumbani mara moja, lakini Alvin
hakurudi mapema hadi ilipokuwa usiku
sana.
"Nadhani nilikuona Mbezi Beach leo."
Lisa alimwambia Alvin kwa uso mkavu.
“Ulikuwepo huko leo?” Alvin alikodoa
macho kwa mshangao.
“Ndiyo, ulikuwa unafanya nini pale?”
Tabasamu likatanda usoni mwake.
"Labda umenunua nyumba katika eneo hilo?"
"Hapana." Alvin alikanusha huku
akichukua ‘chopsticks’ kutoka mezani.
“Sam alikuwa amenisumbua
kumsindikiza huko kutazama eneo lake. Siyo kwamba siwezi kununua
nyumba kubwa ila ninahofia woga wako.
Majumba ya kifahari huwa ni makubwa sana, yatakutisha na majinamizi yako.”
Lisa alimsikia maelezo yake lakini
angemwamini ikiwa Ethan asingesema
wazi kwamba mjomba wake alinunua
jumba la kifahari huko Mbezi Beach.
Kwa akili ya Lisa, Alvin ndiye alikuwa
mjomba wa Ethan, kwa hiyo hakuelewa
nia yake ya kuficha jambo hilo kwake.
Alikuwa hapendi afahamu kuhusu mali
zake, au alikuwa akipanga kumpatia Lina kukarabati jumba hilo ndiyo maana
aliamua kumficha? Lisa angeweza kukubali uwezekano wa wazo la kwanza
lakini wazo la pili lilimchefua nyongo.
Aliichukia sana familia ya Masawe kwa
kujaribu kuchukua maisha yake, pamoja na kinyongo chake kisicho na mwisho
dhidi ya Lina.
"Ni sawa ikiwa ulifanya hivyo. Sitakulazimisha kuniajiri kama mbunifu wako,” alisema kwa mzaha nusunusu.
"Tayari nimesema sijanunua, unanilizamisha ili iweje?" Jibu lake lilikuwa la moja kwa moja.
Lina aliizungusha vidole vyake kwenye
meza na kubadilisha mada ya mazungumzo. “Sawa, basi, labda pengine kuna hafla utakayohudhuria hivi karibuni? Labda utahitaji mwenzi wa kike wa kuambatana naye?”
“Hapana.” Alvin alijibu kifupi.
“Um… Sawa.” Lisa alishangaa. Alitaka kuuliza, ‘vipi kuhusu sherehe ya uchumba ya mpwa wako?’ lakini alisita. Alijishaua tu kwa kusema, “lakini mimi
ninahitaji mwenza.”
Alvin akaziweka chopsticks juu ya meza na kumtazama moja kwa moja machoni.
"Unajaribu kusema nini?"
“Bibi yangu atafikisha miaka 80 mwisho wa mwezi. Kumbukumbu ya kuzaliwa
kwake inaadhimishwa pamoja na sherehe ya uchumba ya Ethan na Lina.
Sina chaguo ila kujitokeza. Bibi yangu
amekuwa mkarimu sana kwangu tangu
nilipokuwa mdogo. Je, ungependa kwenda pamoja nami?” Lisa alijipa
ujasiri kusema hivyo. Alimtazama kwa macho ya kutarajia.
Ilimchukua Alvin sekunde kadhaa kutoa jibu lake. “Nakumbuka nilikuambia kabla hatujafunga ndoa kwamba sitakutana na watu wa familia yako.”
"Kwa hiyo hata kwenye sherehe ya uchumba hutaenda?" Lisa aliuliza kwa kufoka.
“Kwa nini niende, Ethan au Lina wanahusiana nini na mimi?” Alvin
aliuliza Haikuwa na maana yoyote kwake kwani hakuijua familia hiyo hata
kidogo.
'Kwa hiyo wewe si mjomba wa Ethan?'
Lisa alitaka kuuliza hivyo, akasita. Hata hivyo, ikiwa angeuliza hivyo, huenda
angekisia kwamba alimjia kwa nia
isiyofaa. Hivyo akasema, “kwa sababu watu wengine wengi mashuhuri jijini
watahudhuria sherehe hiyo pia, kwa hivyo nilifikiri…”
“Samahani, lakini sina mpango wa kuhudhuria hafla za viwango vya chini kama hivyo.” Alvin alizima mada kwa
kauli ya kejeli.
Lisa alikosa la kusema. Kiwango cha chini? Alikataa kuhudhuria sherehe ya
uchumba wa mpwa wake kwa sababu
hiyo? Alikuwa bora kiasi gani wakati
huo? Je, huu ulikuwa ni mtazamo wa kiburi wa kila mtu aliyerudi nyumbani baada ya kukaa miaka mingi nje ya nchi? Maswali magumu yalitawala uso wake.
“Mbali na hilo, nitakushauri usiende pia.
Siwezi kuhangaika kwenda kukuokoa
tena pindi familia ya Masawe
itakapokufanyia ushenzi.” Alvin
alimuonya kwa ukali huku akimkodolea macho. Lisa alipoteza hamu ya kula ghafla.
Alichukua simu yake na kuanza kuchati na Pamela kupitia WhatsApp.
Lisa: [ Na ulisema Alvin anaweza kuwa na hamu kidogo nami? Samahani, lakini sijisikii hata kidogo. Kila sekunde ninayotumia naye hufanya damu yangu ichemke.]
Pamela: [Hey, endelea kujaribu. Je, tunaweza kutoka kula chakula cha jioni? Imekuwa siku nyingi sana.]
Lisa : [Hapana. Alvin atachukia nikiondoka nyumbani.]
Pamela: [Haya, wewe si mlinzi wake wa nyumbani. Unamdekeza sana.]
Akiwa hana chaguo lingine, Lisa alipanga vyombo na kutokea tena baadaye akiwa kabadilisha mavazi. “Nitatoka kwa muda kidogo baadaye.”
"Wapi?" Macho ya Alvin yalijawa na kero. "Unaenda kunywa pombe tena au kwa familia ya Masawe? Au unaenda kwenye miadi na mwandamizi wako?
Usisahau bado unapaswa kumpeleka
Charlie matembezini baada ya kula."
Lisa alipoteza ujasiri wa kusema ukweli. "Ninaenda kufanya shopping na Pamela. Hali ya hewa inazidi kuwa joto na ninahitaji nguo mpya."
Alvin alimtazama juu na chini kabla ya kutoa maamuzi. "Sawa, nahitaji nguo mpya pia, kwa hivyo ninulie chache pia.
Tumia tu kadi ya benki niliyokupa mara ya mwisho,” Alvin alisema kwa uvivu.
Lisa alikosa la kusema. Kwa kweli
hakuwa na nia ya kwenda shopping ila alitaka tu kufurahia chakula cha jioni na Pamela. “Sawa, sawa, nitakwenda kukunulia. Unavaa saizi gani?"
"Hata hujui ninavaa saizi gani bado una
ndoto ya kunikaribia kitandani kwangu?"
Alvin aliongea akiwa seroius, ilibidi
kwanza Lisa acheke.
"Sawa, unatafuta nguo za bei gani?"
Lisa alimuuliza tena.
“Yoyote, mradi utaipenda.” Alvin pia
hakuwa na uhakika. Baada ya yote, siku zote alikuwa na wabunifu binafsi wa
kutengeneza nguo zake.
Dakika kumi baadaye, Pamela alifika
akiwa kwenye gari lake. Lisa aliingia
ndani ya gari huku akionekana kukata
tamaa. “Twende dukani. Alvin anataka
nikamnunulie nguo.”
“Lakini vipi kuhusu chakula? Bado sijapata chakula tangu mchana nilikuwa busy kweli.” Pamela alisema kwa kuchanganyikiwa. Lisa hakuwa na jinsi zaidi ya kumwambia ukweli. Pamela alimtazama tena kwa dharau. “Heshima yako imeenda wapi? Umekuwa mnyonge sana kwa Alvin tofauti na zamani. Mbona kwa Ethan hukuwa hivi?”
“Huelewi. Alvin hutumia kisingizio cha jinsi nilivyosababisha Charlie awe mgonjwa dhidi yangu,” alijibu Lisa.
"Mbali na hilo, aliokoa maisha yangu mara mbili na ninataka kulipa fadhila."
"Hakuna mtu mwingine anayemdhibiti mkewe namna hii," Pamela alidhihaki.
“Sawa, achana naye. Najua mimi ni mlinzi wake wa nyumbani.”
Lisa aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha
abiria alionekana kukata tamaa.
“Unadhani nisipojishusha naweza kusimama mbele ya kina Ethan kama
shangazi yao? Sherehe ya uchumba wao inakaribia.”
Pamela alitikisa kichwa kufikiria hili.
“Labda Alvin anakuchukulia wewe kama mfanyakazi wa nyumbani ambaye unapika vizuri. Lazima ubadili mawazo yake kidogo, na njia bora ya kufanya hivyo ni kumwonjesha mapenzi yako.”
Lisa alibaki kimya. "Jaribu kuwa mke mpaka kitandani kwake, usiishie jikoni tu." Pamela akamtupia jicho la kustaajabisha. “Unajua ninachomaanisha.”
Lisa alipigwa na butwaa. Uso wake ukajawa na aibu. "Anaweza kunitoa kitandani mara moja."
“Unaweza kumlewesha hoi. Wanaume
hupoteza kujizuia mara wanapokuwa walevi. Mambo yatakuwa mazuri zaidi
ikiwa utapata mimba ya mtoto wake. Nafasi yako kama malkia wa familia
itaimarishwa bila wewe kuendelea kupigana. Sawa, ni lazima upange hili vizuri. Tegeshea karibu na siku baada ya hedhi yako kwani utakuwa na uwezo wa kunasa mimba zaidi wakati huo.”
Akili ya Lisa ilikuwa imechanganyikiwa na mawazo mengi tofauti. Hakuwa na
mpango wa kubeba mimba ndani ya uhusiano wao usioeleweka? “Lakini hanipendi. Familia kama hiyo sio mazingira bora kwa mtoto…”
“Lazima uwe umejitayarisha kwa hili
ulipoamua kuoana naye bila kusita,”
Pamela alimkatalia, “Mbali na hilo, si
unataka kulipiza kisasi wewe? Hii ndiyo
njia bora ya kujumuika katika familia ya
Lowe na kuwaletea matatizo kwa
kutumia nafasi yako kama mke wa Alvin
Kimaro. Fikiria kuhusu hili! Na hawawezi
kukutukana kwa sababu utapewa nafasi ya juu kuliko wao katika uongozi wa familia.” "Wazo zuri." Lisa alionekana kuafiki.
"Lakini kwa nini wewe hujafanya hivyo na Patrick?” Pamela akakosa majibu.
SURA YA 36
Nusu saa baadaye, wote wawili walifika
katika moja ya maduka makubwa ya kifahari ya Oyster Bay. Lisa hakuacha
kunung'unika tangu dakika ile alipoingia
dukani. “Kwa nini umenileta hapa?
Nguo zao ni ghali. Alvin ni mtu wa
kawaida na mchumi sana kwenye hela.
Pamoja na pesa zote alizonazo yeye
anaendesha Harrier tu. Ndiyo, avavaa
vizuri na anapendeza lakini nguo zake
hutengenezewa na wabunifu wake
binafsi, hakika amenituma kwa hili kama mtego tu. Atanifokea sana kwa
kumnunulia nguo za gharama kama hizi” "Lakini mfanyabiashara aliyefanikiwa kama yeye anapaswa kuvaa kitu cha gharama zaidi. Wewe unatakiwa umbadilishe. Angalia, vipi kuhusu mtindo huu?" Pamela alimkokota hadi kwenye duka la kifahari la nguo za kiume na kumuelekezea suti moja kali.
Lisa aliitazama kwa haraka. "Suti ni nzuri, lakini umbo lake haliendani na la Alvin."
"Sawa, basi mchukulie ile pale, ni nyembamba kama yeye, itamfaa sana au vipi," Pamela alishauri lakini Lisa
alikuwa bado na wasiwasi. Hata hakuwa na uhakika alitaka kumnunulia nini Alvin.
"Twende zetu. Ni ghali sana hapa.” Kwa aibu, Lisa alianza kumkokota rafiki yake
kuelekea mlangoni. Muuzaji akawasogelea na ghafla wakasimama kumsikiliza. "Suti hii ni mtindo mpya kabisa, imetengenezwa na mbunifu maarufu Sheria Ngowi. Kuna suti mbili tu kama hizi katika nchi nzima.”
"Hah, unaweza kuokoa muda na nguvu yako. Watu hohehahe kama yeye hawataweza kumudu.” Maneno ya
dhihaka yalivuma hewani. Kisha, Janet Kileo na Cindy Tambwe wakaingia machoni mwao.
“Miss Kileo, Bibi Tambwe…” Macho ya muuzaji yaling’aa huku mara moja
akikimbia kwenda kuwasalimia.
Janet alimtupia jicho la pembeni Lisa
huku akijigamba. “Kwa hiyo umejipatia bwana mpya? Lakini yeye ni mtu mdogo
tu hana lolote. Mtu wako ni mwanasheria uchwara tu. Hata
angekuwa na mafanikio kiasi gani katika kazi yake, bado anategemea matajiri tu kama sisi ili kupata pesa.”
Pamela alicheka kwa hasira. “Mwanasheria? Je! unajua kuwa mpenzi wake…”
Kabla Pamela hajamaliza usemi wake, Lisa alimshika mkono wake na kutikisa
kichwa. Ndoa yake na Alvin ilikuwa siri.
Alijiuliza ni mwanaume gani Janet
alikuwa amekosea na kudhani kuwa mi mpenzi wake.
Tabasamu la furaha likaangaza usoni
mwa Cindy. Alikumbuka jinsi alivyokuwa
akiambatana sana na Lisa hapo zamani
kwa sababu familia yao ilikuwa bora
zaidi. "Lisa, labda unapaswa kununua
mahali pengine. Nijuavyo mimi kuna
pesa chache tu kwenye kadi yako sasa.”
“Cindy, usivuke mipaka.” Pamela alikasirika. Kabla hawajakosana urafiki, Pamela alikuwa amemueleza Cindy juu ya hali ngumu ya Lisa, bila kutarajia Cindy angewageuka na kuwasaliti bila wasiwasi.
Kama ilivyotarajiwa, muuzaji alionyesha kutokuwa na subira aliposikia kwamba
kina Lisa walikuwa hawana pesa za kutosha. “Tafadhali muondoke ikiwa
hamna uwezo wa kumudu hili. Tuna upungufu wa wafanyakazi na hatuwezi kuhudumia kila mtu.”
"Nani kasema hatuwezi kumdu?"
Pamela akatoa kadi yake ya benki.
Janet alidhihaki, “Cindy, ni bora
ulivyoamua kuachana nao. Marafiki kama hawa watakuchoresha tu.”
Cindy naye akazidisha machungu ya
Lisa. "Kwa kweli, lazima apige vizinga kwa marafiki ili anunue nguo."
Lisa , ambaye kwa kawaida alikuwa mvumilivu sana, hakuweza tena kuvumilia dhihaka hizo.
“Hakuna shida hivi ni vitu vidogo sana kwangu nikitaka nanunua tu pesa ipo.”
Lisa aliwarusha roho. “Hili ni toleo la pekee, hakuna hata mmoja wenu anayeweza kugusa hapa.” Alichomoa kadi ya benki aliyopewa na Alvin na kumkabidhi muuzaji. “Si ulisema una seti mbili tu za hii suti? Nazitaka zote.
Sitaruhusu mtu mwingine yeyote kuvaa
nguo zinazofanana na za mpenzi wangu.”
Hii ilimshangaza muuzaji, lakini ni nani angekataa pesa? "Kwa seti zote mbili zitafikia jumla ya shilingi milioni tano."
Lisa alihisi miguu yake ikiishiwa nguvu.
Hakuwa na hakika kama Alvin angemvumilia kwa kumnunulia nguo za gharama ya shilingi milioni tano. Lakini, vipi ikiwa ingezidi kikomo cha kadi?
Alijiuliza huku akihisi angeibeba vipi aibu yake mbele ya wale wambea
waliokuwa wakimkodolea macho.
Alipoibia sura za Janet na Cindy
waliokuwa wakingoja kwa hamu aaibike ili wamcheke, alijilazimisha kutoa kadi.
'Naomba tu iwe na pesa za kutosha,' alijiwazia mara kwa mara.
"Lakini, ni lazima nikukumbushe kwamba hatukubali kurudishiwa bidhaa za toleo maalum, ukinunua umenunua,"
muuzaji alimpa angalizo mapema.
Lisa alihisi ubongo wake ukiganda, lakini akajisemea kimoyomoyo, ‘potelea mbali’.’ Cindy aliziba mdomo kwa mshangao wa madaha. "Lisa, natumai haukuwa umepanga kurudisha nguo baadaye."
Lisa alicheka kana kwamba alikuwa anasikia utani wa kuchekesha.
"Sitafanya kitu cha kimasikini kama hicho. Pia, acha kuniita Lisa . Kusikia ukisema unaita jina langu masikio yangu yanauma.” Aligeuka
kumwangalia muuzaji. “Fanya haraka uniandalie. Sitaki kuendelea kuwasikia mbwa vichaa wakinibwekea.”
“Wewe…” Donge la hasira lilitawala usoni mwa Cindy lakini hakuwa na cha
kufanya. Janet alimshika mgongo Cindy na
kumwambia kwa kujishaua. “Achana
naye. Ngoja tuangalie duka la gharama
zaidi. Kiukweli, nadhani nguo za hapa bado ni nafuu sana. Labda sweety
wangu hatazipenda.”
“Kweli.” Cindy alielewa maana yake
mara moja. Aliridhika hasa alipowazia sura ya Lisa yenye aibu baadaye
wakati kadi itapokataliwa.
Lisa akawakazia macho na kuwafanyia kiburi kana kwamba yeye ndiye tajiri
mkubwa duniani. Kadi ilikubaliwa bila shida yoyote. Muuzaji alimkabidhi begi
la shopping. "Hizi hapa ni nguo na risiti, Bibiye." Lisa alihisi kuguswa ghafla
wakati huu. Hakutarajia Alvin angempa kadi ya benki yenye zaidi ya shilingi
milioni moja.
“Inatosha. Twende!” Janet ambaye alisubiri pembeni kumuona
Lisa akidhalilishwa, aliunganisha
mikono yake na Cindy na kuondoka
huku akiwa amefadhaika moyoni.
Pamela alimpiga Lisa kwa kiwiko. "Sio mbaya. Alvin ni mkarimu sana, ila basi tu."
Lisa hakuweza kuachia tabasamu licha ya kujilazimisha. Alihisi mzigo mzito
ukimlemea kifuani. Miguu yake iligeuka kuwa mrenda alipokuwa akitoka nje ya duka na nguo za thamani ya shilingi milioni tano.
“Hapana, lazima atafikiri ninamfanyia ubadhirifu makusudi. Hivi unamjua Alvin wewe, hapa amefanya kunitega tena apate sababu ya kunisema baadaye.”
Lisa alihofia
“Acha kujiogopesha. Alvin ana thamani ya mamia ya mamilioni ya pesa. Kiasi
hiki kwake ni cha kununulia karanga tu.”
Pamela alimtuliza.
“Huelewi. Yeye ni mchumi. Akiwa na utajiri wote huo mfukoni mwake, anaishi katika nyumba ya vyumba vitatu tu, anaendesha gari la milioni 30, na anatumia tishu za bure tu zinazotolewa na kituo cha mafuta. Simu anatumia ya kichina, Saa kwenye mkono wake pia ni chapa ndogo isiyo na umaarufu. Hata sabuni anazoogea na losheni
anazopaka ni bei ya kawaida tu. Nyumbani kwake hataki kuajiri hata
mtumishi mmoja. Unafikiri ataacha
kunisema kwa kumnunulia nguo za milioni tano, tena kwa pesa yake?”
"Vema, yeye ... Yeye ni mzuri sana na pesa zake, basi." Pamela hakujua
matajiri wengine ambao waliishi
kichumi kama yeye. "Naweza
kukukopesha hiyo pesa, kama atakuzingua utamrudishia."
“Sawa. Nitaona jinsi atakavyojibu
kwanza. kama atanisema vibaya
nitamrudishia milioni tano yake. Wewe nitakulipa pole pole.” Lisa aliafiki.
Lisa alipoteza hamu ya kuendelea kununua baada ya hapo. Hakutaka
kukutana tena na wasichana wale wawili wasio na maana.
Lisa alikula chakula cha usiku na Pamela hadi saa nne usiku. Kisha, alielekea nyumbani huku akiwa na hofu.
Kwa kuogopa kwamba angemsumbua
Alvin aliyekuwa ndani ya nyumba, hakuthubutu kuwasha taa.
SURA YA37
"Umerudi
alitokea
ghafla kwenye mlango wa chumba cha
kulala, na kulikuwa na makali ya uhakika katika sauti yake.
Lisa alipata mshtuko na kujiona
mwenye hatia sana. Alijiuliza ikiwa
mapema sana!" Alvin
alitumia muda mrefu kumngojea arudi
nyumbani ili kuuliza ni pesa ngapi alizotumia. "Linapokuja suala la shopping, wanawake huwa wanasahau wakati."
Alvin akawasha taa pale sebuleni, kisha
akamtazama Lisa kwa sekunde mbili. Akamsogelea na kunyoosha mkono wake.
"Unataka nini?" Lisa hakusogea hata kidogo. Hata hivyo, baada ya kidole
chake cha shahada kugusa midomo yake, hali alianza kupata hisia ngeni
kwenye mwili wake. Lisa alitazama ncha ya kidole kile cha Alvin kwa butwaa.
Ukucha wake ulionekana nadhifu na mzuri, lakini alikuwa akijaribu kufanya nini? Akiwa amechanganyikiwa, alimng'ata kidole kwa upole kwa kutumia meno yake.
Mwili wa Alvin uliganda. Alihisi kana
kwamba mguso wa shoti ya umeme ulikuwa ukisafiri katika mwili wake mara
moja. Alimkazia macho kwa macho meusi ambayo yalionyesha kutokuamini. "Unafanya nini?"
'Hivi si ndivyo unavyotaka? Lisa aliachia kidole chake na kusema kwa sauti ya chini, "Uligusa midomo yangu na kuingiza kidole chako baada ya hapo, sasa mimi ningefanyaje ..?"
"Lisa, una akili chafu sana."
Alimpotezea kabisa. "Nilitaka tu kukuonyesha mabaki ya chakula kwa kidole changu kwa sababu haukufuta mdomo wako vizuri baada ya chakula."
Lisa aliaibika sana hivi kwamba
akainamisha chini uso wake. Alitamani
hata kuchimba shimo na kujifukia humo.
Hata hivyo, kilichofanyika kilifanyika.
Hakuwa na la kufanya ila kusema kwa
kusita, “Huwezi kunilaumu kwa hili. Una
kidole kizuri sana. Nilishindwa kuzuia hisia zangu nilipokiona.”
Alvin alitoa kidole chake kilichokuwa kinawaka kwa msisimko. Alicheka alipotamka maneno hayo yasiyo na aibu huku uso uso ukiwa mkavu kama kauzu. “Umeshika nini?”
Lisa alitetemeka, kisha akanong'ona, "Suti yako. Samahani, nilikununulia suti zenye thamani ya shilingi milioni tano
kwa bahati mbaya.”
Alvin alikunja uso kwani hakuwahi kuvaa suti ya bei nafuu namna hiyo.
Suti zake ziligharimu bei kama ya gari.
Moyo wa Lisa ulimshtuka alipomuoa
Alvin yupo kimya. "Ni nzuri na za
kipekee pia"
"Kwanini zote mbili zinafanana?" Alvin
alimkatisha maneno yake. “Huu?” Lisa alipigwa na butwaa. “Kwa sababu… Ni toleo maalumu. Kuna suti
mbili tu za aina hii katika nchi nzima. Sikutaka kuona mtu mwingine akivaa suti sawa na wewe maana itakuwa ni fedheha. Machoni mwangu, wewe ni mtu wa kipekee sana, mzuri, na mtanashati. Nadhani rangi hii inafaa zaidi kwako. Huwa nakuona umevaa
suti kama hizi na hata sijachoka nazo.
Tafadhali nisamehe kwa kuwa mbinafsi kidogo.”
Alipomaliza kuongea, alitazama sura yake kwa siri. Aligundua kuwa Alvin
alikuwa akimtazama na kukunja
midomo yake.
"Kazi nzuri. Nimependa ustadi wako wa kuchagua rangi” Alvin akanyoosha
mkono wake na kuyabana mashavu ya
Lisa. "Utakapostaafu kuwa mbunifu wa
majengo katika siku zijazo, unaweza kuwa katibu wangu. Utakuwa
ukinipangia nguo za kuvaa kila siku.”
“Umezipenda?” Lisa aliuliza huku akiyakodoa macho yake.
“Kwa nini nisizipende?”
“Nilikuwa na wasiwasi kwamba
utalalamika ni za gharama kubwa kwa sababu… niligundua kuwa nguo
unazovaa kwa kawaida hazionekani kuwa za gharama…” Lisa alilazimisha
tabasamu kwa aibu kwa kuogopa kuwa maneno yake yangeumiza jeuri ya
Alvin. “Hehee. Kwa kweli, hakuna ubaya
wowote. Ninaelewa kuwa wewe ni mtulivu na mtu usiyependa kujionyesha, na hilo ndilo linalonivutia sana kwako.”
Alvin alipigwa na butwaa. Hapo ndipo
akagundua kuwa nguo alizokuwa akivaa
kawaida zilionekana za bei rahisi kwa
Lisa. Alimshangaa sana Lisa kwa jinsi alivyomchukulia juu juu. hakujua kuwa
nguo zote alizokuwa anavaa Alvin Kimaro zilikuwa ni 'customized brand',
ama nguo zilizotengenezwa mahususi kwa wateja maalunu. Nguo zake zote
zilikuwa za kipekee za hazikufanana na wengine. Si zile za kuchagua chagua tu kwenye maduka.
“Ni sawa. Utaelewa baadaye.” Alvin akagusa kichwa chake kwa huruma, kisha akaingia chumbani.
Siku iliyofuata, Alvin alivaa suti ya kahawia aliyonunuliwa na Lisa.
Alipotoka nje ya chumba kile, Lisa alimtazama na kupigwa na butwaa
kwa muda. Ingawa alimuona akiwa
amevalia kila aina ya suti, hisia za ajabu
zilimjaa kichwani kwa sababu tu hiyo
ndiyo suti aliyomnunulia. Alihisi
mchanganyiko wa furaha na
kuchanganyikiwa. Ilionekana kana
kwamba alikuwa mume wake halisi wakati huo. Alvin akampiga jicho.
Alipogundua kuwa alikuwa akimtazama kwa butwaa, kwa namna fulani alikuwa katika hali ya uchangamfu.
Alipokuwa akitoka nje ya nyumba hiyo, kuna jambo lilimjia kichwani. “Sikuona
umenunua nguo yoyote jana usiku, kwanini” Alimuuliza
"Hapana, nilikuwa na kazi ya kukununulia wewe nguo." Alipokumbuka furaha ya kumnunulia mpenzi wake
nguo tabasamu lilisambaa usoni mwake.
"Nadhani ulikuwa na shida ya kwenda kula chakula cha jioni na si kununua nguo, ungesema ukweli tu." Alvin
alimdhihaki, akimuonyesha waziwazi.
"Ah, kwa nini unanifikiria hivi?" Ili
kuficha aibu yake, Lisa alisema kwa sauti nzito ya kutaniana, ”nilikosa tu nguo zinazonifaa, nitaenda siku nyingine.”
Alvin alihisi koo lake linamuuma.
Alifungua vifungo viwili kwenye shingo ya shati lake na kusema, “Kama una muda, nenda ukanunue nguo leo kwa kutumia kadi yangu. Nguo hizo zitakuwa malipo kwa kunipikia na kumhudumia Charlie kama mhudumu wangu.”
Alielekea ofisini kwake mara baada ya kumaliza kuongea.
Hans alipoingia tu kwenye kampuni ya mawakili, alipigwa na butwaa kuona suti ya Alvin. Kwa haraka akasema, “Bw.
Kimaro, sijawahi kukuona ukivaa suti za aina hii…”
“Lisa aliinunua madukani jana.” Alvin aliongea huku akifungua faili la kesi.
Sam, ambaye alikuwa amefika tu mlangoni, alisikia maneno hayo. "Wow, unavaa suti zinazouzwa madukani siku?” Sam aliuliza huku akitazama suti
ya Alvin kwa shauku na kuichunguza. "Ni toleo maalum la Sheria Ngowi…. Nimezoea kukuona ukivaa nguo zilizotengenezwa mahususi kwa ajili yako pekee, tena na wabunifu wa nje ya nchi, au ni kwa sababu Lisa alikununulia hii…?”
Kwa hali ya huzuni, Alvin alimtupia jicho la kijeuri. “Mwanamume mzima unakuja kuchunguza nimevaa nini leo, huna kazi za kufanya, eeh?”
“Sikuja kwa ajili hiyo.” Sam alisema.
Alvin alimtupia faili usoni mwake, na maneno “toka ofisini kwangu”
yakachomoka mdomoni mwake.
"Sawa sawa. Usiwe na wazimu. Niko
hapa kukuambia kitu.” Sam akamwambia. “Babu yangu
atasherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 80 kesho usiku. Amesikia
kwamba upo Dar hivyo ameniomba nikwambie kuhudhuria sherehe hiyo.”
Sam alichukua kadi ya mwaliko na kuiweka juu ya meza.
Alvin aliitazama kadi hiyo na kukumbuka kitu. Lisa pia alimwalika kwenye sherehe ya kuzaliwa ya miaka
80 ya bibi yake.
"Pia ni bora ukaja na mpenzi wako,"
Sam alikumbusha. “Kama unavyojua, dada yangu amekuwa akipendezwa nawe kwa miaka mingi. Pia, babu yangu
amekuwa akitaka sana kukuoza dada
yangu. Hataacha kukusumbua kwa hilo”
Alvin alijipapasa paji la uso huku
akiwaza ni nani aende naye kama mpenzi wake.
Lisa? SURA YA38
Siku mbili zile Lisa alikuwa busy sana na kazi huku pia akilifikiria ushauri
aliopewa na Pamela wa kuweka mambo sawa na Alvin. Siku hiyo jioni akiwa anawaza hayo, Alvin alimpigia simu.
“Uko wapi?”
"Ofisini." “Nitumie anwani yako. Nitakuchukua hapo chini ndani ya dakika 20. Nataka unisindikize kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa.”
Hapa ndipo Lisa alipoona fursa. Macho ya Lisa yaling'aa, lakini baadaye alijawa na kinyongo. “Tufanye dili, kama
utakubali kunipa kampani kwenye
sherehe ya kuzaliwa ya bibi yangu, na mimi nitakubali kukupa kampani leo.”
“Kama hutaki niitatafuta mtu mwingine.”
Alvin hakumbembeleza.
Alvin alipotaka kukata simu, Lisa alitupilia mbali kiburi chake na kukubali haraka. “Njoo unichukue. Katika uwanja wa mapenzi, yule anayependa sana ndiye anayepoteza. Nimejikuta nikipoteza kabisa moyo wangu kwako.
Alvin una nini?” Lisa alichombeza
kijanja. Alichukua chupa ya thermos na kuendelea kunywa kahawa yake. Hata
yeye alivutiwa na ustadi wake wa kumtania Alvin kimapenzi.
Sekunde chache baadaye, sauti ya
Alvin ilisikika upande wa pili. "Simu
yangu imeunganishwa kwenye gari
kupitia Bluetooth, na Sam ameketi
kando yangu anakusikia ukiongea upuuzi wako.”
Lisa alitema kahawa mdomoni mwake
ikamwagikia kwenye skrini ya kompyuta
bila kujijua. Sauti ya Sam baadaye ilisikika, “Si vibaya shemeji. Sikuwahi
kufikiri kama na wewe unajua maneno matamu ya mapenzi kiasi hiki.
Haishangazi Alvin--"
"Nakuja kukuchukua." Alvin alimwambia
Lisa na simu ilikatwa moja kwa moja
kabla Sam hajamalizia usemi wake.
Lisa alilala juu ya meza, akiona aibu hadi kufa. Alinyanyuka baadaye kidogo na kupakia vitu vyake na kushuka chini.
Wakati huo alipokea simu kutoka kwa
Pamela. “Mambo yalikuwaje? Ulifanikiwa
kufanya chochote na mume wako jana usiku?”
“Hapana,” Lisa alimjibu haraka, “lakini aliniomba nimsindikize kwenye hafla ya siku ya kuzaliwa usiku wa leo. Nadhani hii ndiyo nafasi. Lakini nina wasiwasi kama atakunywa pombe. Anapotoka kwa shughuli za kijamii usiku, sijawahi
kumuona akinywa pombe!”
Lisa alihema huku akijua kuwa Alvin
alikuwa ni mtu mwenye kujitambua.
"Hafla ya kuzaliwa?" Pamela alipigwa na butwaa kwa muda. “Ni siku ya
kuzaliwa ya babu ya Sam ya miaka 80?
Mimi pia nitakuwepo.”
“Nafikiri hivyo. Alvin hana rafiki
mwingine zaidi ya Sam.” Lisa alisema.
“Hiyo itakuwa poa sana, tutakutana.
Nitawapanga watu kunywa na Alvin na
kujaribu kumlewesha. Hilo
lisipofanikiwa, nitaleta dawa…” Pamela
alimhakikishia. “Hakika Alvin atakutaka
mwenyewe bila kupenda.”
Lisa akashusha pumzi ndefu. Hakuwa na uhakika kama alikuwa amejipanga
kiakili kwa hilo licha ya Pamela kuwa
ameanza kumsaidia kuandaa kila kitu
kwa haraka. Alisubiri kwa hamu kando ya barabara. Lakini Alvin alipofika Lisa
alionekana kuzama kwenye mawazo
mazito kiasi kwamba hakusikia mlio wa
honi.
Beep! Beep!
Alvin alimkazia macho Lisa aliyekuwa
kazama kwenye mawazo fulani
yaliyomfanya atabasamu kwa aibu.
Alikuwa amejifunika uso huku
kasimama kando ya barabara.
Alishindwa kabisa kumwelewa. Hakuwa
na uhakika ni nini kilikuwa akilini mwake
pia. Je, alikuwa kiziwi?
Sam alikodoa macho na kutabasamu.
"Alvin, kwa njia fulani ninahisi kuwa mke wako anafikiria juu ya kitu kichafu, na labda uko kwenye mawazo yake ..."
"Yeye si wewe, sawa?" Alvin alimtazama kwa ukali, ingawa alikuwa na mashaka pia juu ya hilo.
“Kusema kweli, kadiri ninavyomwangalia Shemeji, ndivyo namuona kuwa mzuri. Kwa kweli, nashangaa uliwezaje kumpata kabla yangu hali wewe ni mgeni na mimi
ninaishi naye kitongoji kimoja.. "
Kabla Sam hajamalizia sentensi yake, sauti kali ikamkatisha. Alvin alimwonya bila huruma, “usijaribu kuwa na mawazo machafu juu yake. Yeye si mtu ambaye
unaweza kumpata kirahisirahisi tu.”
Baada ya hapo, alifungua mlango na kutoka nje ya gari. Alitembea moja kwa
moja kuelekea kwa Lisa.
Lisa alipomwona Alvin ghafla alishtuka
kutoka kwenye mawazo kiasi kwamba
alipiga hatua mbili nyuma na kutaka
kudondoka kutokana na viatu vyake
virefu. Alvin alipomuona Lisa anakaribia kuanguka, alinyoosha mkono wake
kumshika kiuno na kumweka kwenye mikono yake ili aweze kujiweka sawa.
Ikiwa hii ingetokea siku nyingine yoyote, Lisa angekuwa na wasiwasi kidogo.
Hata hivyo, alikuwa akimuwaza Alvin
ambaye hana nguo muda mfupi uliopita.
Sasa kwa vile ncha ya pua yake ilikuwa
karibu na kifua chake, mwili wake
ulibadilika ghafla na kutetemeka kama
amepigwa shoti ya umeme.
“Ninatisha kiasi hicho, hata unataka
kuanguka baada ya kuniona?” Alvin
alinua kichwa chake na kumuuliza.
"Hapana, umenishtua tu." Haraka alirudi
nyuma na kujiweka sawa.
"Ingia kwenye gari." Alvin alifungua mlango na kukaa kwenye kiti cha dereva. Lisa aligundua kuwa kuna mtu alikuwa kwenye siti ya mbele, kwa hivyo bila
kupenda akaenda kwenye siti ya nyuma. Kwa aibu, hakuweza kukabiliana na Sam.
“Habari, Shemeji. Ulikuwa unafikiria nini sasa hivi, mbona hukusikia honi?” Sam
alionyesha tabasamu baya. "Kutokana na mwonekano wako, naweza kukisia kuwa ulikuwa ukimfikiria Alvin."
"Ndio, nilikuwa nikimfikiria," Lisa alisema bila kujali kwa sauti ya upole. Kisha, akatazama chini haraka.
Baada ya kuachia 'wow', Sam alijifunika
kifua chake na kusema kwa huzuni, “Sikupaswa kuuliza swali hilo. Kuona
haw lovey- dovey nyote wawili mlivyo, ninahisi kushikwa na wivu. Hata hivyo, Alvin hana utu wa kupendeza, na ana hasira mbaya. Pia ana tabia nyingi
chafu. Unapenda nini hasa kutoka
kwake?” Sam aliuliza kwa utani.
Moyoni mwake, Lisa alimpa Sam mia
kwa mia kwani alikuwa sahihi kabisa.
Hata hivyo, alimsifia tu Alvin ili kumlinda
kihisia, “Kwa kuwa sasa ninampenda, naona udhaifu wake wote kuwa ni sifa
zake nzuri. Kinyume chake, wanaume
wapole na waelewa hunifanya nihisi
kutokuwa salama. Napenda sifa zake
tu. Akinizingua na mimi namzingua basi, yanaisha!” Maneno ya Lisa
yalimvimbisha kichwa haswaa Alvin,
Akamgeuzia macho Sam na
kumwangalia kwa kejeli.
Sam alihisi kana kwamba alikuwa
amedhihakiwa na Lisa. "Sikupaswa kusema chochote kumbe?" Alvin
alimpuuza tu.
Lisa akasema, “Hapana, hapana. Wewe ni mcheshi, Sam Harrison. Uwepo wako unanifanya nihisi nimetulia zaidi.”
“Unamaanisha kwamba huna utulivu unapokuwa pamoja nami?” Alvin
aligeuka ghafla.
Lisa alisafisha haraka hali ya hewa.
“Hivi mtu aliyependa huwa ana utulivu kweli? Unapokuwa na mtu
unayempenda, unahisi kana kwamba
moyo wako unadunda kwa nguvu kila wakati na unashindwa kabisa kuutuliza."
Alvin aligonga usukani kwa kidole bila
kusema chochote. Pamoja na taaluma
yake ya uanasheria, alikuwa amekutana na mjuzi wa kubumba na kuchezea
maneno kama yeye.
Akiwa ameketi kando ya Alvin, Sam alishikwa na wivu. Hakuwahi kukutana na msichana yeyote ambaye aliendelea kukiri mapenzi yake kupitia hotuba
yake. Lisa akabaki kimya akicheza na simu yake katika siti ya nyuma. Ghafla, Pamela alimtumia video mbili. Pamela alikuwa na kawaida ya kumtumia video za vichekesho. Lisa alifikiria vivyo hivyo wakati huo, kwa hivyo alibofya video
hizo mara moja. Kabla hajajua niki
kitajiri, sauti kali ilijaza sehemu sehemu yote ya ndani ya gari. Tukio la ajabu
likaonekana kwenye kioo cha simu yake baadaye. Lisa aliingiwa na kiwewe cha ajabu na kuizima simu mara moja.
Hata hivyo, gari lilikuwa tayari
limesimama. Wanaume hao wawili
walimtazama kwa namna ya ajabu.
Mara moja, alitamani kukimbia kwa
kuruka nje ya dirisha.
“Aha… Acha nieleze. Nilikuwa nikisoma kitabu na mara kirusi kikaingia...” Lisa alibabaika.
Sam aligusa pua yake kwa sura ya aibu.
“Sawa shemeji. Ni kawaida tu, hata
mimi hutazama hizo vdeo kwa siri nyumbani. Sikujua kwamba na wewe
huwa utazama mpaka kwenye gari.”
Lisa alikosa la kusema.
Uso wa Alvin ulijawa na hali ya huzuni.
"Ninakuonya, usitazame tena mambo
machafu kama hayo hata kama ni kwa siri"
SURA YA39
Alvin alipandwa na hasira kila alipofikiria
kuwa Lisa alikuwa akimwangalia
mwanamume mwingine akiwa uchi
kwenye video. Hakuwa na haya kama nini! Sam alimtetea Lisa, "ili kuiweka kwa njia
nyingine, inaweza kuchukuliwa kama nyenzo ya kujifunza wakati mwingine.
Labda shemeji anajifunza kwa ajili yako."
Lisa aliitikia kwa kichwa chinichini,
akikubaliana na kauli ya Sam. Lakini
Alvin alizungumza kwa sauti ya huzuni,
“hakuna haja ya hilo. Hatahitajika
kufanya hivyo na mimi. Hata kama hilo
likitokea, mimii ndiye nitapanga tufanyeje, si yeye.”
Kauli ya Alvin ilikuwa tofauti kabisa na vile alivyoamini Lisa. Sasa alifahamu
kwamba Alvin hakuvutiwa naye hata
kidogo, aliinamisha kichwa chini kwa
kukata tamaa. Sam akamtazama kwa
huruma. Kisha akahema kwa masikitiko
baada ya kuona jinsi Alvin alivyokuwa
mkatili wa hisia zake na hana mapenzi naye. Baada ya nusu saa, gari lilisimama.
Lisa aliinua kichwa chake na kugundua kuwa walikuwa wamefika ‘Miracle studio’, saluni ambayo ilitoa huduma ya urembo na mitindo mbalimbali. Ingawa
hakuwahi kufika hapo awali, alisikia
kwamba ‘Miracle Studio’ ilikuwa saluni
ya kike inayojulikana zaidi kwenye huduma ya urembo na mitindo huko
Masaki.
Alvin akageuka na kusema, “Nenda wakakuhudumie kwanza, mimi kuna
jambo naenda kufanya. Nitakuchukua baada ya muda mfupi.”
Lisa alipigwa na butwaa. "Alvlisa, labda
hujui utaratibu wa saluni hii kuwa
haikubali mtu yeyote hata kama wewe
ni tajiri kiasi gani hadi uwe umeweka
appointment mwezi mmoja kabla.”
“Alvinani?” Sam akaangua kicheko. Muda mfupi baada ya kuanza kucheka, macho makali yakaelekezwa kwake. Uso wa Sam uliganda kidogo, kisha
akasema haraka, “Hatuhitaji kuweka nafasi. Nenda tu juu. Nimemjulisha mhusika mkuu kuhusu hilo.”
“Oh.” Lisa alipumua kwa siri kwa kuridhika. Kwa hakika, familia ya Harrison ilikuwa familia yenye nguvu sana, hawakuweza kupingwa kwa lolote. Mara tu alipopanda ghorofani, meneja wa saluni alimkaribisha na kumfanyia huduma binafsi ya urembo na mavazi yeye binafsi.
Saa moja baadaye, Alvin alikuwa
amerudi, lakini Lisa hakuwa amemaliza
kuhudumiwa. Alvin alikaa kwenye kochi
na kumsubiri kwa muda. Upesi mlango wa chumba cha watu mashuhuri
ulifunguliwa na Lisa akatoka nje akiwa
tofauti na alivyoingia. Alivalia vazi refu
lililopambwa kwa almasi mwili mzima. Sio tu kwamba vazi hilo lilikuwa la kung'aa, lakini pia lilifafanua sura ya umbo lake la kuvutia na kupendeza
kikamilifu. Nywele zake, ambazo zilionekana kuwa nyeusi kama mwani, zilijipinda kwa mawimbi na kuanguka juu ya mabega yake. Alionekana
mrembo na mwenye kuvutia kuliko siku zote.
Macho ya Alvin yalimtoka kwa hisia
inayowaka. Kwa muda mrefu alikuwa amejua uzuri wake. Tofauti na wanawake wengine wengi siku hizi, hakuwa amepitia upasuaji wa plastiki ama kuongeza makabrasha mengine
mwilini ili kuwa na uzuri kama huo.
Hakutarajia kuwa angeonekana kuvutia
sana hata akiwa amejipodoa kidogo tu.
"Alvlisa,
Mara tu Lisa alipoona macho yake, midomo
ninaonekana mzuri?"
yake iliangaza tabasamu la furaha.
Alitembea kuelekea kwake, akitumaini kwamba angeelekeza macho yake kwake.
Alvin alikaa kimya huku akikazia macho
yake kifuani mwake. Lisa aliona haya baada ya kuona hivyo. Alihisi macho ya
Alvin kama yanamchoma kifua. "Hey, unatazama nini?"
Alvin aliongea kwa mkazo, kinyume na matarajio ya Lisa. "Nenda ukabadilishe."
“Kwanini, kwani kuna shida gani?”
Lisa alichanganyikiwa.
"Nguo hii inakufichua sana, siipendi.”
Aligeuka na kushuka chini mara baada ya hapo.
Kwa hasira, Lisa alihisi bomu la atomiki
likilipuka kichwani mwake. Kutokana na
mtazamo wake mapema, ilikuwa
imempa hisia kwamba alikuwa
amevutiwa naye, lakini alivyobadilika
kwa kauli yake akashindwa kumwelewa kabisa. Msimamizi wa duka kando yake alisema
kwa tabasamu, "Bi Jones, Bw. Kimaro anakujali sana." Lisa alitoa macho na
kumtazama meneja wa duka. Macho yake yalionyesha hali ya kutokuamini.
“Kwa kawaida, mwanamume anapomjali sana mwanamke, anakuwa na wivu
naye. Asingetaka mwanamke wake avae mavazi ya kuvutia wanaume
wengine, na ni yeye pekee anayeruhusiwa kukuona hivyo.”
Kwa tabasamu meneja wa saluni
aliongeza, “Baada ya kufanya kazi hapa
kwa miaka mingi, nimekutana na
wanaume wengi lakini wachache wa aina ya Kimaro. Mimi ni mjuzi mzuri wa tabia za wanaume.”
Aliposikia maneno yake, Lisa alijawa na moto wa matumaini. Je, Alvin hakutaka watu wengine wamwone akiwa amevaa
nguo za kufichua umbo lake? Hiyo liliwezekana. Lisa alibadilisha na kuvaa nguo ndefu nyeupe ambayo haimkumbana sana. Ilimpendeza lakini haikuyafichua
maumbile yake. Baada ya hapo akashuka chini na bila kutarajia, alimuona Alvin akivuta sigara. Alvin alivuta sigara mara chache sana. Siku
hiyo labda ilikuwa mara yake ya kwanza kumuona akifanya hivyo hadharani.
Hata hivyo, alionekana kuvutia tu alipovuta sigara. Kwa kuwa alikuwa akimpenda Alvin, chochote
atakachofanya hakika kingeonekana
kuwa kizuri tu kwake.
Lisa alimwendea na kumvuta mkono.
"Alvlisa, nguo hii ni sawa?"
Alvin alimtupia jicho la kuridhika. Wakati
huu, alikuwa amevaa kizamani, kistara na kujisikia kifahari. Lakini bado Alvin
alikuwa na uhakika kuwa Lisa angevutia macho ya watu usiku huo. Ghafla, alijuta kuchagua kumtoa nje. Alipaswa kumficha.
“Twende zetu.” Alvin aliiweka sigara kwenye sinia ya majivu na kuongoza kutoka nje.
Akiwa ameshika gauni lake, Lisa alitembea taratibu kiasi. Wakati
Alvin alipogeuza kichwa chake, uso wake ulikuwa umekunjamana.
Akamsogelea na kumuinua kiunoni moja kwa moja. Kwa ushirikiano, Lisa
aliweka mikono yake shingoni mwake, kisha akatazama kidevu chake kizuri.
Alichukuliwa na mshangao wa sura yake ya kuvutia.
Lisa akamuuliza kwa upole, “Hukuniruhusu nivae lile gauni kwa sababu ulihisi linaufichua sana mwili
wangu? Je, ni kwa sababu unanipenda au?” Pamoja na hayo, kulikuwa na hali ya ukimya. Baada ya kushuka chini, Alvin alimweka Lisa moja kwa moja
kwenye siti ya nyuma ya gari lake. Kwa sauti ya kejeli, alisema, "Kitaalam, wewe ni mke wangu, hata hivyo. Sitaki uvae kwa njia isiyofaa na kujidhalilisha.” Uso wa Lisa ulimtoka. Hakujisikia
kuzungumza naye katika safari yao yote. Gari liliingia ndani ya nyumba ya familia ya Harrison iliyojaa wageni. Msururu wa magari ya kifahari ulionekana kwenye
eneo la maegesho nje ya jumba hilo la kifahari. Lisa alikasirika kidogo kwani
hakuyaona magari ya akina Masawe na Mushi. Ethan angetokea pale, bila
shaka angeshangaa kumuona akiwa
amemshika mkono mjomba wake.
Waliingia ndani huku mikono ya Lisa ikiwa imeizunguka mikono ya Alvin.
Alvin aligeuza kichwa chake na kumpa ukumbusho, “Usiku wa leo, unaweza kujidai hadharani kwamba wewe ni mpenzi wangu.”
Macho ya Lisa yalimtoka. Dakika
iliyofuata, hata hivyo, Alvin akabadilika tena. “Usiwe na furaha kupita kiasi. Hii ni kwa sababu sitaki tu Mzee Harrison anitambulishe kwa msichana mwingine.”
Katika usemi huo, Lisa alijihisi kutumiwa kama ngao tu, na uwepo wake ukakosa maana ghafla! Lisa alikosa la kusema.
“Sawa. Niko tayari kukulinda kutokana na kila aina ya majanga na kukusaidia bila kujali!”
Kabla hajamaliza maneno yake, msichana mmoja aliyevalia gauni la rangi ya shampeni alitembea kuelekea kwa Alvin kwa umaridadi. "Alvin, ni muda mrefu umepita tangu tulipokutana mara ya mwisho."
Lisa alishindwa kuendelea na kitendo chake. Msichana huyo alikuwa binti mdogo wa familia ya Harrison, Angela Harrison, ambaye pia alikuwa dada mdogo wa Sam. Lisa alikuwa amemwona mara moja kwa mbali alipohudhuria hafla furani ya chakula cha jioni kipindi cha nyuma. Kutokana na usemi wake uliojaa sauti nyororo, Lisa alifikiri kwamba Angela angeweza kuwa mshindani wake.
“Alvin, vipi mbona mkeo hujaja naye
leo? Ni muda mrefu umepita tangu
nilipomwona mara ya mwisho. Nimem’miss sana.”
"Hajambo," Alvin alijibu kwa unyonge.
Angela kisha akapiga kelele. “Alvin, mbona umekuwa Dar kwa muda mrefu, lakini hukuja kuniona. Bado
unakumbuka kuwa uliahidi kutazama jinsi ninavyoimba na kucheza violin?
Hujatimiza ahadi.” Kwa hayo alimkazia macho Alvin kwa husuda.
Lisa alishikwa na wivu. Alikuwa
amesimama pale pale, lakini Angela alionekana kumchukulia kama hamuoni
vile. Lisa akajikoholesha na kusema.
“Alvlisa, unaweza kumtambulisha
kwangu? Yeye ni…?” Lisa alimshika mkono Alvin huku akionyesha sura ya kimahaba. SURA YA 40
Alvin alitabasamu alipoona jinsi
Lisa alivyopata wivu haraka. “Dada yake Sam.”
“Yeye ni nani? Kwa nini yupo karibu yako” Sura ya uchungu ikapita usoni
mwa Angela.
Akikunja midomo yake myekundu, Lisa alisema, “Halo, Bi. Harrison. Mimi ni mpenzi wake. Huenda hujaniona
hapo awali, lakini ulipaswa kusikia
kuhusu jina langu. Mimi ni Lisa Jones, msichana mrembo zaidi niliyetokea
kuuteka moyo wa Alvin.” Mdomo wa Alvin ulimsisimka kwa maneno yake ya aibu. Angela alitoa macho huku akiwa
haamini jinsi msichana huyo alivyokosa
aibu. Kisha akadhihaki, “Hehe.
Samahani, sijasikia kuhusu wewe kuwa
msichana mrembo zaidi. Hata hivyo, nimesikia kuhusu tabia ya kipumbavu ya
Lisa kutoka kwa familia ya Jones
Masawe hivi majuzi. Ulipoteza urithi
wako kwa dada yako, ambaye alitoka
mashambani, akapewa haki ya urithi wa familia ya Masawe, na baadaye ukafukuzwa kutoka kwa familia hiyo. Siamini kuwa Alvin angetaka kuwa na mtu kama wewe usiye na future yoyote...”
Lisa alihisi kana kwamba kuna kitu kimepenya moyoni mwake. Alikosa la kusema.
“Angie.” Macho ya Alvin yalimwelekea Angela. “Jiangalie. Lisa ni mpenzi wangu kweli.”
“Inawezekanaje?” Angela aligeuka rangi. "Hata halingani na hadhi yako nzuri."
Lisa hakuridhika, akajibu mapigo ya Angela, “kwanini nisiendane naye? Mimi ni beatuful na yeye ni handsome. Tunaposimama pamoja, tunaendana
vizuri kwa sura. Mtoto wetu wa baadaye
bila shaka ataonekana kuvutia.”
Mdomo wa Angela ukasisimka kwa hasira. Alisema kwa kejeli, “Unajidanganya. Utapunguza IQ ya kizazi cha Alvin."
Kuwatazama wanawake hao wawili
wakirumbana kulimfanya Alvin apate maumivu ya kichwa. Kisha akapiga paji
la uso wake na kusema. “Sawa, Angie.
Nitapeleka salamu zangu kwa babu
yako sasa. Tutaonana baadaye.”
Alipomaliza kuongea, alipiga hatua
kuelekea kwenye jengo kuu akiwa na
Lisa bila kumsubiri Angela ajibu.
Lisa akafunga mdomo wake, hakusema
neno lolote katika safari hiyo. Kwa vile
alikuwa akila vizuri na kulala vizuri kwa
siku za karibuni, mashavu yake
yalikuwa yamenenepa tena. Alionekana
mrembo sana.
Alvin alinyoosha mikono yake ili kuyabana mashavu ya Lisa huku
akimwambia. “Angie bado ni mtoto, na amekuwa akidekezwa tangu akiwa
mdogo. Usijishushe kwa madhaifu yake.”
Lisa akacheka. "Usijali, sitajishusha kufikia kiwango cha Angie. Kwa kuwa upo naye karibu sana, kwanini hukufikiria kumfanya ajifanye mpenzi wako? Baada ya yote, unalibebisha hadi jina lake, unamwita Angie. Mimi ni mtu wa kukaa tu kama picha, mtu ambaye hata jina langu linakukera.”
Alvin akajibu, “…Kwa hiyo ni kwa sababu nilimuita Angie na sikuiti Lisa?”
"Bila shaka hapana. Je, mimi ni mtoto mdogo kuweza kuona hisia za mtu?"
Lisa alidlazimisha tabasamu.
Alvin alijihisi mnyonge ghafla. "Angela
alikuwa akicheza na Sam na mimi nyuma ya nyumba tulipokuwa wadogo.
Ninamchukulia kama dada mdogo."
Hapo hapo wakafika kwenye jengo kuu. Akiwa amevalia suti yake safi, Mzee
Harrison alimpungia mkono Alvin kwa nguvu. “Alvin, yaani leo ndo unakuja
kuniona ingawa umekuwa Dar es
Salaam kwa muda mrefu sasa. Kwanini
kunisusa hivi? Unanidharau kwa sababu mimi ni mzee?” Aliongea huku akikenua
tabasamu la kizee, Mzee Harrison.
“Hapana kabisa. Unaonekana mdogo kuliko hapo awali, Mzee Harrison.” Alvin alimkabidhi mzee yule zawadi yake ya siku ya kuzaliwa.
Mzee Harrison alielekeza macho yake
kwa Lisa na Alvin akamtambulisha.
“Huyu ni mpenzi wangu.”
“Ah, hatimaye umepata mwenzi. Hiyo inasikitisha. Hapo awali nilipanga kukupatia mtu. Kuna wanawake wengi wa ajabu hapa." Mzee Harrison alimkabidhi zawadi Lisa . “Hii hapa ni zawadi kwa ajili yako tunapokutana kwa mara ya kwanza, mke wa mjukuu wangu. Alvin ameteseka sana katika maisha yake. Tafadhali mtunze.”
Lisa alifurahishwa. Hakuwa na uhakika
kama aikubali au laa. Isingeonekana vizuri kama angeikataa.
"Ikubali tu kwani ni ishara ya upendo ya Mzee Harrison kwako." Alvin alitikisa kichwa.
Lisa alipopokea zawadi hiyo, Alvin akampigapiga mgongoni. "Nisubiri
kwenye ukumbi wa wageni." Pengine
alikuwa amekwisha maliza kucheza
kipande chake, hivyo akamwona hana
umuhimu tena kuwa karibu yake. Lisa
akajiondokea zake.
Aliposhuka tu aligongana tena na Angela. "Ulikuwa unanisubiri hapa kwa makusudi, Bi.Harrison?"
Bila kustaajabisha, tabasamu lilitanda usoni mwa Angela. Angela alinyanyua kidevu chake kwa maneno ya jeuri.
“Afadhali ukae mbali na Alvin. Yeye si mtu unayeweza kumudu kuwa naye.”
“Itakuwaje kama sitakaa naye mbali, eeh?” Lisa aliuliza kwa shauku ya
kutaka kujua. “Unampenda sawa, lakini yeye anakuchukulia tu kama dada mdogo.”
Angela alibaki akihema. "Kwa hiyo?
Kwa familia ya kifahari kama Kimaro, wanajali kuhusu ndoa iliyolingana vizuri
katika suala la hadhi ya kijamii. Kusema
ukweli hata humjui vizuri Alvin.
Wanafamilia yake hawatakukubali kwa
sababu hulingani naye. Kwa sasa, anaburudika tu na wewe. Familia yake
itakutimulia mbali na hautakanyaga hata msingi tu wa geti.” Alidhihaki kwa kejeli na baadaye akaondoka kwa njia ya kiburi.Lisa alikasirishwa kwa namna
fulani na maneno yake lakini hakufikiria kabisa. Hata hivyo cheti cha ndoa
kingekuwa tegemeo lake kubwa kwa wakati wote.
Baada ya Lisa kuondoka kwenye jengo
kuu, punde alikutana na Pamela.
“Angalia, hii ndiyo pombe
niliyotayarisha. Nitatafuta mtu wa kumlewesha Alvin baadaye. Ikiwa
hajalewa, lazima uchukue mbinu
yoyote kwa kumfanya ale hii kitu.
Kumbuka, hii itaanza kutumika saa mbili
baada ya kuila." Pamela aliweka vitu
vile mikononi mwa Lisa.
Lisa alijisikia vibaya sana. "Je, hii
itasababisha madhara yoyote?"
“Mbona bado una wasiwasi nami kwa jinsi ninavyokupambania? Haina shida na haitaathiri afya yake.”
"Ikiwa atashtukia, hakika ataniua."
Lisa aliogopa.
“Labda awe hanithi lakini kama ni rijali hatatoboa! Ikiwa ningekuwa mwanamume nikaamka na kumwona
mwanamke mrembo kama wewe akiwa amelala kando yangu asubuhi na mapema, bila shaka ningehisi raha.
Alvin pia ni mtu wa kawaida.” Pamela alimtoa wasiwasi.
Lisa alivutiwa na maneno yake. Muda mfupi baadaye, Alvin alirudi.
Alvin alipofika tu mlangoni, kuna mtu wa ajabu alienda kumsumbua. "Bw.
Kimaro, sifa yako inakutangulia. Kwa
kweli, kwa muda mrefu nilitaka
kukufahamu. Ngoja nikupe toast.”
“Kunywa tu mwenyewe. Sihitaji kinywaji.” Baada ya kukutana na watu
kama yeye mara nyingi sana tangu ujana, Alvin hakutaka kuwa karibu nao.
Kisha Alvin aligongana na watu
wachache kama hao ambao alibaki
kuwa jeuri kwao. Pamela alipumua, akitazama tukio hilo kwa siri. “Jamani, mumeo ni mtu wa kipekee ambaye
haonyeshi heshima kwa wengine hata
kidogo. Bado hajanywa hata glasi moja
hadi sasa, ana kiburi. Watu wasiomjua wangedhani kwamba anatoka katika
familia yenye nguvu zaidi nchini.”
“Ngoja nimfuate.” Lisa alimwambia
Pamela huku akijongea kwa Alvin.
Muda si muda Alvin akamtazama
Lisa ambaye alimsogelea kimya kimya.
Lisa alifikiri kwamba Alvin angekuwa
busy kujichanganya na wengine na kuzungumza mambo ya biashara kama
watu wengine walivyofanya. Hata hivyo, walikuwa wakihudhuria sherehe ya kuzaliwa iliyojaa watu wa tabaka la juu ambapo ilikuwa ni kawaida kwa watu kupanua mitandao yao. Lakini Alvin alijitenga nao na kumpeleka Lisa nyuma ya ukumbi ambapo waliketi na kunywa.
“Si unatoka kwenda kujumuika?
Ninaona matajiri wachache kutoka sekta ya fedha.” Alijaribu kumshawishi atoke nje. Aliingiwa na hofu kwani asingeweza kufanya lolote ikiwa angeendelea kubaki naye.
"Sipendezwi." Alvin alipiga kinywaji
chake kama hataki hivi.
Lisa akapepesa macho. “Unataka nikumiminie mvinyo kidogo? Kuna
mvinyo hapa wa kiitaliano unaonekana
kuwa na ladha nzuri."
"Ikiwa unataka kuinywa, endelea. Lakini utafute kabisa pa kwenda endapo
utailewa na kufanya vituko.” Alvin alijibu na kumpa tahadhari.
Baada ya kukaa kimya, mara Lisa alisimama tena. “Ngoja nikuletee chakula, sawa? Hujapata chochote usiku wa leo.”
"Hakuna haja." Hakupendezwa na chakula kingine chochote zaidi ya chakula alichopika Lisa.
"Hapana. Chakula ni nishati kwa
wanadamu. Lazima ule kitu hata kama
hujisikii, jilazimishe kiasi.” Kwa hayo, Lisa alitoka kwenda kuchukua matunda na vyakula vingine.
Kwa siri, Lisa alitia kile kitu alichopewa na Pamela kwenye chakula. Aliporudi, aliweka chakula mbele ya Alvin. Kisha, akaweka kipande cha nyama ya mbuzi iliyochomwa karibu na mdomo wake.
Kwa kuwa ilikuwa mara yake ya kwanza kufanya kitendo hicho kiovu, alihisi
kukosa amani. Mikono yake ilitetemeka hasa pale macho makavu ya Alvin
yalipomkazia usoni. Aliapa kwamba angekata tamaa ikiwa Alvin angekataa kula. SURA YA 41
Muda mfupi baadaye, Alvin aliinamisha kichwa chake na kula kipande cha nyama alichokuwa ameshika Lisa.
"Endelea kunilisha." Alvin alinogewa. Lisa alikosa la kusema. Hata hivyo,
aliendelea kumlisha chakula chote
kwenye sahani huku akihisi woga na
hatia. Alvin aliinuka mara baada ya kumaliza kula. “Twende nyumbani.”
Lisa alishtuka. "Tunaenda nyumbani saa hii?" Haikuwa imefika hata saa mbili bado. Ikiwa wangeondoka mara tu baada ya kula, bila shaka Lisa angekuwa mtu wa kwanza kushukiwa baadaye.
“Wewe usiondoke. Unaweza kukaa
hapa usiku kucha.” Alvin aliweka msimamo. Alvin aliona ni kupoteza muda kujichanganya na watu wengine, hakuwa pale kwa ajili ya kujionyesha.
Alijitokeza tu pale kwa ajili ya heshima yake kwa Mzee Harrison. Kwa
kuzingatia kwamba alikuwa akisisitiza
kuondoka, Lisa hakuwa na jinsi zaidi ya kuondoka pamoja naye.
Baada ya kuingia kwenye gari, alimkabidhi zawadi ambayo alipokea
kutoka kwa Mzee Harrison.
"Ishike," Alvin alisema kwa upole.
“Lakini ni ghali. Sidhani kama ni lazima nichukue…”
“Hii ni ghali kwako tu." Alvin alitabasamu
kwa dharau hafifu. Inavyoonekana, alikuwa akidhihakiwa kama maskini.
Lisa alitazama chini akaingiwa na hofu akijua kwamba kuna dhoruba ingetokea muda si mrefu.
Walipofika nyumbani, alimtazama kwa
siri Alvin kwa nyuma huku akiwa na
woga na wasiwasi, akijisemea
kimoyomoyo. 'Samahani, Alvin. Hakika
nitakutendea vyema siku zijazo. Nitii tu usiku wa leo.’
Baada ya kuingia ndani, Alvin alienda
kuoga. Kisha akaelekea kwenye
chumba chake cha maktaba ili ili
kufanya mkutano kwa njia ya video.
Katikati ya mkutano huo, ghafla alihisi
mwili wake unawaka moto. Hakujisikia vizuri hata baada ya kuvua koti lake.
“Uko sawa, bosi? Uso wako
umekunjamana.” Msaidizi wake upande wa pili wa video aliuliza kwa mshangao.
“Sijisikii vizuri. Tuendelee kesho.
Mfuatilie kwa uangalifu Jack Kimaro
huko.” Alvin alizima kompyuta yake na kurudi moja kwa moja bafuni kwa ajili ya kujimwagia maji baridi. Haijalishi
alijimwagia maji kiasi gani, bado alihisi joto likpanda kwa kasi. Alijua kwamba
kuna jambo lilikuwa baya kwake. Hakula wala kunywa sana usiku ule, lakini
kwanini… Subiri! Alikuwa amekula
chakula alichochukua Lisa. Kwa wazo
hili, uso wake ulionyesha hasira kali.
Alithubutuje!
Mlango wa bafuni ulipigwa teke kwa
kishindo. Jambo hilo lilimshtua sana
Lisa aliyekuwa akitandika kitanda
chake. Alimwona Alvin akimfuata, matone ya maji yamefunika mwili wake.
Uso wake ulijaa ukali. “Dawa yake
ilianza kumchukua ama?” Lisa alijiwazia. “Kuna nini… Una shida gani?”
Lisa alikurupuka huku akirudi nyuma kwa hofu. Ghafla, aliogopa.
"Uliweka nini kwenye chakula ulichonilisha kwenye sherehe?"
Alvin alimshika mkono na kumburuta kutoka sakafuni. Macho ya
Lisa yalimtoka. Hakutarajia kwamba angefahamu mapema namna ile.
“Mimi… sijui unasema nini.”
"Bado unakataa, huh?" Alvin akaibana shingo yake, macho yake yakidhihirisha chuki. "Nani mwingine angepata nafasi ya kufanya huu ujinga kama si wewe?"
Lisa alikuwa karibu kukosa hewa. Hakuwahi kufikiria kwamba majibu ya
Alvin yangegeuka kuwa ya kutisha sana. Aliogopa sana. “Ilikuwa… mimi
ndiye niliyefanya… Samahani!” hatimaye Lisa alikiri.
Shingo ya Lisa iliuma sana hivi
kwamba machozi yalitiririka usoni mwake. Alihisi kwamba alikuwa
amekutana ana kwa ana na Ziraili!
Alijuta sana!
“Mwovu kiasi gani wewe! Nilikuamini sana!” Hasira zikamlipuka Alvin kifuani.
Kwa nini afanye jambo kama hilo?
Alichochukia zaidi maishani mwake ni kudanganywa! Alimchukia, lakini
taratibu alianza kuhisi anapoteza
fahamu. Baada ya kutoka nje ya
udhibiti, akamtupa Lisa kitandani. Nguo
za Lisa zilichanika kwa sababu ya
vurumai hiyo. Aliamka na kukimbilia
bafuni kuoga tena.
Kelele ya mshindo wa mlango ikasikika.
Mshindo huo ulimfanya Lisa ahisi kama
umepiga moyoni mwake.
Lisa alitetemeka kwa woga huku
akijizuia kulia. Alipojiuliza ni nini kingeendelea baada ya hapo alikosa
nguvu kabisa. Alikuwa amekosea!
Alikuwa amekosea sana. Hakupaswa
kushawishiwa kutumia mbinu ya aina
hiyo! Lisa aliacha macho yake yatoe
machozi, akijihisi mwenye hatia sana.
Maji katika bafu yalimwagika kwa dakika
45. Akiwa na wasiwasi kuwa kuna
jambo limemtokea Alvin, Lisa alijipa
moyo na kuusogelea mlango wa bafu
na kuugonga. "Uko salama? Samahani.
Je! unanihitaji—”
mwanamke kama wewe.” Mlango wa
"Nyamaza. Afadhali nife kuliko kumgusa
bafuni ulifunguliwa kwa nguvu. Akiwa
amelowa kichwani hadi miguuni, Alvin alimtazama Lisa kwa macho mekundu yaliyoiva hasira. Lisa aliduwaa kwa mshangao. "Uliweka kiasi gani kwenye chakula?"
Alvin alikuwa katika hali mbaya lakini alijikaza tu na kujifanya mgumu.
Hakutaka kabisa kujishusha na kukubali msaada wa Lisa. Kwa hasira, alimvuta
bafuni na kumlowesha kwa maji ya baridi. Kabla hata maji ya baridi
hayajamwagika kichwani mwake, Lisa alianza kutetemeka. Ni pale tu Alvin alipogundua kuwa anashindwa kupumua ndani ya maji ndipo alipomwachia. Alilaani kwa sauti nzito na kuupiga mlango kwa nguvu. Kisha, akavaa nguo zake na kukimbia nje
haraka. Lisa alitoka bafuni kwa aibu.
Alitaka kumfuata, lakini alikuwa amechelewa.
Saa sita usiku Sam alikimbia hospitali na kumkuta Alvin akipokea dawa kwa
njia ya dripu kitandani. Wakati huo, alipigwa na butwaa, asijue amcheke au amhurumie Alvin kwa jinsi alivyokuwa akihangaika kumtuliza askari wake
aliyeng’ang’ana kusimama wima muda wote. Sam alijikuta akimuonea wivu
Alvin, alitamani tukio hilo lingemkuta yeye, asingelaza damu. Uso wa alvin
ulikuwa bado haujatulia kwa wakati huo.
“Kwa nini umekuja kutesekea hospitalini? Ulipaswa kumtii Lisa mara moja na kumaliza matatizo yako
nyumbani. Suala hilo lingetatuliwa
chumbani kwako.” Sam alimwambia
Alvin huku akizuia kicheko chake.
nitakachokufanyia.” Alvin aliyakodoa
“Sema hivyo tena uone
Ilikuwa yapata saa
moja usiku muda
huo na Lisa bado hajarejea nyumbani.
Ilikuwa imepita saa moja tangu Alvin arudi nyumbani kutoka kazini na hapakuwa na dalili zozote za kuwepo Lisa. Hakumjali hata Charlie tena.
Ilionekana kweli alikuwa amefikia kikomo cha uvumilivu.
Charlie.
matunda.” Alvin akambeba paka mikononi mwake. Charlie alicharuka
mara kadhaa akigoma kubebwa. Paka yule mjamzito alikataa kutoka, lakini
Alvin alilazimisha kutoka pamoja naye.
Kulikuwa na maduka kadhaa yaliyokuwa kando ya barabara kuu ya mtaa huo. Alvin aliingia kwenye duka la matunda. Alitazama na kukagua
matunda kwa muda lakini hakuwa na uhakika wa kununua. Mawazo makuu
"Njoo,
Twende tukanunue
kichwani mwake yalikuwa juu ya Lisa!
Kwa nini Lisa hakuwa nyumbani bado?
Muuza duka la matunda akiwa
amesimama kando ya mlango alikuwa
akimtazama kwa siri kijana huyo mzuri wa kipekee. Nini kilikuwa kikiendelea
juu yake? Alikuwa akizunguka duka
mara nyingi zaidi kuliko alivyoweza
kuhesabu lakini hakuwa amenunua chochote. Pia alimuona akiendelea
kutupa macho kuelekea barabarani. Je, inawezekana kwamba alipendezwa
naye lakini alikuwa na haya kumuanza?
Sura ya aibu ilitanda usoni mwake.
Hatimaye, akapata ujasiri wa kumkaribia.
Bila kutarajia, Alvin akamkwepa muuza
duka yule huku akipiga hatua kubwa
kuelekea mlangoni. Akatoka nje akiwa
na ameghairi kununua chochote. Akiwa
amefika kwenye barabara inayoelekea
nyumbani kwake, hapo ndipo
alipogundua gari la BMW likiwa
limeegeshwa kando ya barabara ile upande wa pili. Mwanadada mrembo
alitoka kwenye gari.
Wow, Alvin alishuhudia mwanamume
mwingine alishuka kwenye gari
na kuajribu kumshika mpenzi wake.
Alikuwa amesalitiwa licha ya kubarikiwa na sura nzuri kuliko yeye. Iliuma sana
sana!
Upande wa pili wa barabara.
Lisa alimshukuru Kelvin kwa dhati
tena. Alipogeuka tu, alimuona Alvin
akimsogelea kwa hatua kubwa huku
akiwa amemkumbatia Charlie.
Mwangaza hafifu wa mbalamwezi
kutoka juu ulimulika uso wake wenye
huzuni. Alikosa la kusema!
Ilikuwa ni mara ya pili tu kwake kurudi
nyumbani usiku namna ile akiwa
amesindikizwa na wanaume tofauti.
Kwanini siku zote alikutana na Alvin?
Na mara zote mbili alikuwa na mwanaume mwingine aliyempa lifti
kumleta nyumbani? Alijua kwa vyovyote vile Alvin angemdhalilisha milele kwa
tukio hilo. Kwa hiyo, alijitetea kabla Alvin hajapata nafasi, “Sijisikii vizuri sana leo.
Kama kuna chochote unataka kuniuliza, tafadhali subiri kesho ili uniulize chochote.”
“Sidhani hivyo. Nahisi lazima utakuwa umechoka kwa kutumia siku nzima na jamaa yako. Vizuri? Ulipewa lifti ya kurudi nyumbani kwa Range Rover
mara ya mwisho na sasa imebadilika kuwa BMW, huh? Si mbaya, Lisa.
Unapanda matawi siku hizi. Jambo la muhimu ni kwamba, wanajua wewe ni aina ya mwanamke wa hali ya chini
ambaye unaweza kufanya lolote ili tu
kuingia kwenye kitanda cha mwanamume!”
Alikuwa ametoka tu hospitalini na hajaingia hata ndani. Kichwa chake kilikuwa kimeanza kujisikia vizuri lakini
homa yake ilianza kumpanda tena baada ya kusikia matusi ya Alvin. Hili lilimchosha sana kiakili. Alvin aliongea mara chache sana siku za nyuma lakini mbona amekuwa muongeaji ghafla?
"Sitaki kubishana na wewe." Ilikuwa
inachosha kurumbana kila walipokutana. Lisa aliinamisha kichwa chake na kuanza kuondoka.
Tabia yake ya kumpotezea ilimkasirisha zaidi Alvin. Akamshika mkono kwa nguvu. "Unamaanisha nini? Kwa hiyo huniongeleshi sasa kwa kuwa umepata mtu tajiri zaidi? Umetoka siku nzima na haujarudi nyumbani hadi usiku wa
manane. Je, ni makosa kwangu
kukuuliza kuhusu hilo?”
SURA YA 45
Kwa namna alivyomshika alikua
akimuumiza, lakini hakuwa na nguvu ya kuutoa mkono wake. Alichohisi ni kukata tamaa na uchovu. Aliinua macho yake kukutana na macho makali ya
Alvin. “Inakuathirije nikichelewa kurudi nyumbani? Ninakaa kwako, lakini
nimekuwa nikikupikia na kukusafishia. Isitoshe, ulinidanganya kuhusu mimi
kumpa Charlie chakula kilichomdhuru tumbo wakati kumbe paka wako ana
mimba. Paka anaendelea vizuri zaidi
kuliko hapo awali. Si lazima niwajibike
kwa ujauzito wake. Mimi si niliyempa mimba.”
“Unathubutu vipi kunijibu hivi?” Alvin
akamtupia macho ya jeuri na magumu. Uso wake ulikuwa umetanda hasira.
Mwanamke huyo alikuwa amefanya
jambo baya lakini alikuwa akibishana
kana kwamba alikuwa katika haki.
“Usisahau kuwa wewe ni…”
“Ninajua kuwa mimi ni mke wako kisheria, lakini je, umewahi kunitendea kama mke?” Lisa alicheka. "Kwa maoni yako, mimi si kitu zaidi ya mwanamke asiye na aibu, duni kuliko mtu yeyote unayemjua."
“Ikiwa ndivyo ilivyo, kwa nini ulitaka kuolewa na mimi? Alvin alikasirishwa na tabia yake ya kupindukia. “Ni vyema ukajua hilo…”
"Hiyo ni sawa. Sikujua hili hapo awali na niliendelea kufikiria ningeweza kupata nafasi. Niache tu kuanzia sasa! Tuko
kwenye ndoa ya mkataba tu hata hivyo, na ni mimi ndiye niliyekulazimisha.”
"Angalau unakumbuka kuwa ulilazimisha kuingia kwenye hii ndoa."
Sauti ya Alvin ilikuwa kali. “Sitaki kuwa
na uhusiano wowote na wewe.
Sitaki kuchafuliwa na ugonjwa mchafu utakaoleta nyumbani baada ya kuupata kutoka mahali pengine.”
Lisa alihisi damu ikikimbilia juu ya kichwa chake. Mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa hasira.
Alikuwa amepanga kukaa hadi Charlie ajifungue kwa kuwa paka huyo alikuwa amempenda kwa dhati. Lakini, aligundua kuwa asingeweza kukaa pale kwa dakika nyingine tena.
Lisa akafungulia tabasamu la kejeli.
"Hakika, ili nisichafue nyumba ya Bw.
Kimaro kwa uwepo wangu mchafu, nitahama wakati huu."
"Je, hii ni moja ya hila zako?"
Tabasamu la kujilazimisha lilienea usoni
mwa Alvin. Hakuamini angefanya hivyo.
Alikuwa ametumia bidii nyingi kujaribu
kulala naye, hata hivyo.
Bila kumjali, aliondoa mkono wake kutoka kwake na kukimbilia chumbani.
Alichukua begi lake na kuanza kufungasha vitu vyake kwa kasi ya radi.
Hakuwa na vitu vingi kwa hiyo haikuchukua muda.
Alvin alimtazama kando ya mlango.
Akiwa amechanganyikiwa, alifungua vifungo vya juu vya shati lake.
Mwanamke huyu alikuwa mzuri sana katika uigizaji. Hakutafakari makosa
yake mwenyewe hadi sasa. Je, asingemkaripia hata kama angekuja
nyumbani kwa gari la mwanamume mwingine?
Lisa alimaliza kupakia mizigo yake na kuiweka mezani ile kadi ya benki
aliyompa hapo awali. "Sikutumia senti ya ziada mbali na gharama za kila siku."
Hakufurahishwa na sauti ya hiyo.
“Nimefurahi kusema hivyo. Si mimi niliyekulipia gharama za chakula cha kila siku na ziara zile za hospitali?” Alisema kwa tabasamu la kejeli.
"Hakika, nitapata malipo ya kamisheni kutoka kazini kesho na nitakulipa."
Baada ya kumjibu hayo, Lisa hakuweza
kujizuia kukaa hapo kwa sekunde nyingine tena. Alichukua begi lake na kuelekea mlangoni. Kabla ya kuondoka, alimuona Charlie akimtazama kwa
huzuni. Machozi yalimtoka. Alishuka chini ili kumpigapiga paka kichwani.
'Samahani, siwezi kukutunza tena. Jitunze.'
kukasirishwa na tukio lililokuwa mbele yake. Uso wake ulikuwa umeharibika
kwa mikunjo ya hasira. Alifikiri
mwanamke huyo alikuwa anajifanya tu.
“Lisa usijutie uamuzi wako. Ukitoka
"Charlie, rudi hapa!" Alvin alihisi
kwenye mlango huu, sitakuruhusu
urudi hata ukipiga magoti kuomba.”
“Usijali kwa sababu sitafanya hivyo!”
Lisa aliinuka na kupiga hatua bila
kuangalia nyuma.
Kelele za kitu kikivunjika vipande vipande zilisikika nyuma yake wakati
akifunga mlango. Hata hivyo, haikujalisha tena.
Hatimaye Lisa aliondoka. Dakika 40
baadaye, alionekana nyumbani kwa
Pamela. Akiwa kazidiwa na usingizi wa kufa mtu, Pamela alipiga miayo ya
usingizi kwa mgeni ambaye
hakumtarajia. “Mmegombana tena?
Unapanga kukaa hapa kwa siku ngapi
wakati huu?" Pamela alimpokea kwa maswali.
“Ni mbaya zaidi wakati huu, sitarudi
huko tena.” Lisa alibadilisha slippers za nyumbani kabla ya kuingia.
"Unatania. Ulimtaka mwenyewe akuoe na sasa umebadilisha mawazo yako?"
Lisa alilazimisha tabasamu la uchungu. "Sio kila mpango utakupatia faida.
Nitaufikiria kama uwekezaji ulioshindwa."
"Una uhakika?"
"Ndio." Lisa alijilaza kwenye kochi.
Bado alionekana kutokuwa sawa.
"Nimechoka. Kweli, nimechoka sana."
Pamela alikunja uso. "Una homa?"
"Ndio." Lisa alipambana na machozi
yaliyokuwa yakimtoka. “Kila mtu aliliona
hilo isipokuwa Alvin. Natamani pia
kujaliwa na kutunzwa. Hata kama yeye
ni mjomba wa Ethan, siwezi kupata
heshima ya Lina ikiwa Alvin hatanipenda na kuniheshimu.”
Pamela alimtazama kwa makini na akagundua kuwa kweli amekata tamaa. Walikuwa marafiki bora kwa miaka mingi. “Hamna shida. Ninaheshimu uamuzi wako. Kwanini usikae hapa na mimi? Hata hivyo ninaishi peke yangu.”
”Sio wazo bora. Wewe na Patrick je…?”
Kwa aibu, Pamela alimkodolea macho rafiki yake. “Achana naye, anaishi kwao na huwa tunaonana kwa miadi.
"Lakini mmekuwa pamoja kwa mwaka mmojana bado hamtaki kuoana."
Lisa alipepesa macho na kujibu baada ya muda. "Amekuwa na shughuli nyingi
hivi karibuni tangu achukue uongozi wa kampuni ya familia yao. Tunaonana
mara moja au mbili tu kwa wiki, kwa
hivyo unaweza kuwa na uhakika. Nilipendekeza utafute mahali hapo awali kwa sababu Ethan alikuwa anakuja
kukutafuta hapa. Lakini sasa ameacha.”
Tabasamu usoni mwa Lisa likabadilika na kuwa dhihaka kwa kutajwa kwa mtu huyo. "Nadhani anachoweza kufikiria kwa sasa ni Lina."
“Basi, ni mtu mjinga sana. Sherehe ya uchumba wake inafanyika katika siku chache. Una uhakika unataka kuhudhuria hafla hiyo?" Pamela alimtazama kwa wasiwasi.
"Ndio, lakini nitaenda kwa sababu ya sherehe ya bibi yangu kwenye siku yake ya kuzaliwa."
"Naogopa akina Masawe watajaribu
kukuhadaa tena. Nasikitka sitaweza
kukusindikiza kwa sababu nina mtihani
chuoni siku hiyo. Lakini Patrick
anahudhuria tukio hilo pia. Nitahakikisha
yupo kukusaidia.”
Lisa alihisi utulivu usio wa kawaida. Hata ingekuweje, mpango wa kumtumia
Alvin kama njia ya kulipiza kisasi
ulikuwa umekwama! Alikuwa amepata
amani na hilo hatimaye. Alikuwa karibu
kupoteza maisha hapo awali na
heshima yake ilikuwa imekanyagwa. Hakuna kitu ambacho kingeweza
kumtisha tena.
Pamoja na hayo, ilimbidi atafute njia ya
kumlipa Alvin haraka.
SURA YA 46
Siku iliyofuata, bosi wake, Joseph Ruta, alirudi kutoka katika safari yake ya
kikazi nje ya nchi. Lisa alimfuata ofisini
akiwa na ombi maalum. “Je,
inawezekana kuomba malipo ya awali ya mshahara wa mwezi huu? Ninadaiwa
pesa na watu…” alisema kwa sauti ya chini, kwa aibu.
“Hakuna jambo kubwa. Unadaiwa kiasi gani? Niambie kiasi hicho na nitakutumia pesa mara moja.” Joseph alimwambia Lisa. “ Bw. Mushi
anaendelea kupongeza uwezo wako. Ninaweza pia kukulipa mapema juu ya mradi wa Mbezi Beach." Akatoa simu yake. "Je, Shilingi milioni ishirini zinatosha?"
Hilo lilimshangaza sana Lisa. "Hapana, hapana, milioni tano zinatosha."
Bado alikuwa na bahasha nzito
aliyopokea kutoka kwa mzee Harrison, pamoja na ile aliyopewa na Kelvin jana yake mchana. Alipanga kumlipa Alvin
ziada kidogo endapo angetaka kupiga
hesabu. “Usionekane umezidiwa sana. Mradi wa
Mbezi Beach wa Bw. Mushi unagharimu
zaidi ya shilingi milioni mia tano.
Kamisheni yako juu ya hili ni zaidi ya milioni hamsini kwa haraka haraka."
Joseph alihamisha milioni ishirini
kwenye akaunti ya Lisa mara moja.
“Endelea kufanya kazi hiyo nzuri,”
Joseph alisema ili kumtia moyo.
Lisa aliguswa sana. Aliamua kwamba
aangeendelea kuzingatia kazi yake kwa
moyo wake wote na kuachana na mawazo ya Alvin.
Tangu Lisa aondoke nyumbani kwa
Alvin, Alvin alikuwa amebadilika sana.
Hakuwa na raha na alikuwa mkali muda
wote. Sam alikuwa akimwonea huruma
na wasiwasi sana kwani hata kula
hakula vizuri.
"Lisa bado hajarudi?" Sam alimuuliza.
•••
"Sitaki kusikia jina la huyo mwanamke likitajwa masikioni mwangu." Alvin alijibu kwa dharau. Ilikuwa ni mida ya chakula
na mara tu aliposikia jina la Lisa likitajwa tumbo lake lilianza kunung'unika ghafla.
Sam alikuna ncha ya pua yake. "Najua umezoea chakula chake, lakini huwezi
kujiua kwa njaa kwa kuwa ameondoka."
"Sivyo," Alvin alijibu, akionekana kukasirika. "Hatimaye naweza kujiweka
sawa sasa kwa kuwa ameondoka."
Jasho lilitokeza kwenye paji la uso la Sam. Hakuwa amegundua upande huu wa rafiki yake hapo awali. Ghafla
alimshangaa Lisa kwa kuweza kuishi
na mwanaume huyo kwa muda mrefu.
Angekuwa ni yeye
angepandwa wazimu baada ya siku chache.
“Kesho ni sherehe ya uchumba ya Lina na Ethan. Lisa labda atakuwa huko pia. Familia ya Masawe ilinitumia mwaliko pia. Je! niende na… nimshawishi?”
Alvin alimgeuzia macho Sam na kumuuliza. "Nilidhani ni sherehe ya kuzaliwa kwa Bibi Masawe wa miaka 80?"
"Sijawahi kusikia hivyo." Sam akatikisa kichwa.
Uso wa Alvin ulionekana mzito.
Ilionekana kuwa familia ya Masawe
haikupanga kusherehekea siku ya kuzaliwa ya bibi kizee huyo hata kidogo,
sasa Lisa alipanga kwenda huko
kufanya nini? Mwanamke mjinga huyo.
Je, hakuogopa kuonewa tena na watu
hao? Alvin alijiwazia hayo na punde
akaona bora aachane nayo.
"Hakuna maana kufanya hivyo. Huu ni ujanja wake mwingine tu. Ngoja uone. Nina hakika atakuja na kuniomba
msamaha kabla ya uchumba.” Alvin alimhakikishia Sam.
Baada ya sekunde chache, alipokea ujumbe mfupi kwenye WhatsApp kutoka kwa Lisa .
"Angalia, inakuja." Akabonyeza ujumbe huo kuona Lisa amefanya uhamisho
mara tatu na kuweka shilingi milioni sita kwenye akaunti yake. Uso wa Alvin uliganda. Sam alisogea mbele kidogo ili kuibia.
Akiwa amechanganyikiwa, alisema, “Anatumia pesa nyingi kukuvuta tena.”
"Ndio." Uchangamfu wa Alvin ulirejea kidogo. “Ni lazima itakuwa moja ya mbinu zake nyingine.”
Status ilionyesha bado Lisa anaandika.
Alisubiri kuona angesema nini. Sekunde 20 baadaye, Alvin alipokea ujumbe mwingine wa maandishi. [Milioni sita zinajumuisha gharama za hospitali hapo awali. Nina hakika ni zaidi ya inavyotakiwa lakini ninahisi fadhili leo.]
Tabasamu la fumbo lilienea kwenye uso wa Alvin. “Naam, vizuri. Mwanamke huyu ana ujasiri wa simba.” Alijiwazia
Alvin.
Sam, ambaye alikuwa ameibia mtazamo wa ujumbe huo, alisema. “Hii lazima iwe mbinu ya kuvutia umakini wako. Sio tu kwamba anajaribu
kukuhonga pesa bali angalia jina lake la mtumiaji-Alvlisa,."
Alvin alijisikia vizuri zaidi aliposikia hivyo na akafunua tabasamu la kejeli. "Kwa hiyo? Haijalishi tena. Hata kama atapiga magoti mbele yangu na kuomba kwa
usiku tatu…” Hata hivyo, kabla
hajamaliza sentensi hiyo, Lisa alibadilisha jina lake la mtumiaji la WhatsApp na kuwa 'Mwanzo Mpya'.
Alibadilisha hata status yake kuwa: [Nataka tu kujali mambo yangu kuanzia sasa na kuendelea.]
Macho mazito na meusi ya Alvin
yalichuruzika kwa jazba. Aliiweka simu yake pembeni, na punde si punde, uso wake ukabadirika. "Usimtaje mtu huyu mbele yangu tena." Kisha, akaondoka kwa hasira. Sam alishindwa kabisa
kusema chochote. •••
Lisa aliingiwa na wasiwasi baada ya kutuma ujumbe huo wa kejeli. Hata
hivyo, pamoja na kumsaidia, Alvin
alikuwa amemdhalilisha sana kwa siku
za karibuni na alihisi anahitaji
kujisimamia yeye mwenyewe.
Hata hivyo, baada ya kutopata jibu
lolote kutoka kwa Alvin, alihisi kana
kwamba mzigo huo mzito umeondolewa
kifuani mwake. Hatimaye, hakuna hata mmoja wao aliyekuwa na deni kwa
mwenzake tena.
Simu yake ilitetemeka ghafla. Kulikuwa na maandishi mapya ya WhatsApp.
Alinyanyua simu akidhani ni Alvin, kumbe ujumbe ulitoka kwa Kelvin. [Ni vizuri kuwa na mwanzo mpya.
Mwanamke anahitaji kujitendea vizuri zaidi. Ikiwa huna furaha na maisha, sio kwa sababu hautoshi. Baadhi ya watu au mambo fulani hayafai kuthaminiwa.]
Lisa alihisi kizunguzungu moyoni mwake. Alihisi matumaini zaidi kuhusu wakati ujao aliposoma ujumbe huo
wenye kutia moyo. Hata hivyo, aliona ni ajabu sana kwani ilionekana kana
kwamba Kelvin alijua alikuwa ameachwa.
Mbali na hilo, alikuwa amebadilisha
status yake sekunde chache tu zilizopita. Je, Kelvin alikuwa akimfuatilia
zaidi kwenye mitandao yake ya kijamii?
Baada ya kufikiria hili kwa ufupi, alijibu:
[Asante kwa kitia-moyo]
Hata kama Kelvin alikuwa
amependezwa naye kweli, Lisa hakuwa
na mpango tena wa kuwa na mpenzi.
Mahusiano yake yote ya awali yalikuwa
yamemuumiza sana. Isitoshe, hakuwa hata na talaka bado.
SURA YA 47
Zilkuwa zimebaki siku chache tu kufikia
siku ya kuzaliwa kwa bibi yake Lisa, Bibi
Masawe. Siku hiyo pia ndiyo ingekuwa
sherehe ya uchumba kati ya Lina Jones
na Ethan Lowe. Sherehe zote mbili
zilifanyika kwa pamoja katika hoteli ya
nyota saba ya ‘Heavens On Earth
Resort.’ Ni matajiri tu ndiyo wangeweza
kufanya sherehe katika hoteli hiyo.
Siku ya sherehe hiyo, familia ya Masawe na familia ya Lowe walikuwa
wametumia kiasi kikubwa sana cha pesa kukodisha ‘The Paradise Hall’, ukumbi wa kifahari zaidi wa sherehe unaopatikana katika hoteli hiyo.
Lisa alikuwa amesimama kwenye
mlango wa ukumbi huo akiwa na kadi ya mwaliko mikononi mwake. Hakuweza
kujizuia kuachia machozi ya huzuni machoni mwake. Wakati fulani huko
nyuma kabla Lina hajarudi, Jones
Masawe aliahidi kupanga harusi yake na Ethan katika hoteli hiyo hiyo na kwenye ukumbi huo huo. Kweli, sherehe ya uchumba ilikuwa ikifanyika na Ethan bado alikuwa bwana harusi. Lakini, aliyebadilika ni chumba wa kike, baala ya Lisa, alikuwa ni dada yake, Lina!
Lisa aliingia kwenye ukumbi wa
sherehe, akiwa amevalia nguo ile nyeupe aliyovaa kwenye sherehe ya siku ya kuzaliwa ya Mzee Harrison mara ya mwisho. Kundi la waandishi wa
habari lilikuwa likingoja mlangoni kwa ajili ya kuripoti matukio ya sherehe hiyo ya familia hizo mbili maarufu. Waandishi walimvizia Lisa na kumrushia maswali mfululizo.
“Bi Lisa, si ulidai familia ya akina Masawe ilikufungia na kukutesa? Kwa
nini bado uko hapa kuhudhuria sherehe ya uchumba ya Lina na Ethan?”
'Je, ni kwa sababu akina Masawe
hawakukutendea vibaya hata kidogo?
Je! kila kitu kilikuwa ni uzushi wa mawazo yako mwenyewe?"
Lisa hakuwa mjinga. Alijua mara moja
kwamba waandishi walikuwa
wamepangwa na familia ya Masawe.
Bila shaka walikuwa wamehongwa na kuelekezwa cha kusema. Alitarajia jambo hili litokee, hivyo akaitikia kwa
utulivu. "Leo ni siku ya kuzaliwa ya bibi yangu, anatimiza miaka 80. Nipo hapa kusherehekea pamoja naye.”
“Kweli? Hatukusikia chochote kuhusu hilo. Tunajua tu kuwa sherehe ya leo ni ya uchumba kati ya familia ya Masawe na familia ya Lowe.”
“Lisa, mavazi uliyovaa ni ya kuvutia.
Ikiwa sijakosea, ni mavazi ya toleo la kipekee kutoka kwa mkusanyiko wa msimu wa joto wa brand ya kifahari. Si ulisema akina Masawe walikutendea vibaya sana, sasa umewezaje kumudu vazi la gharama kiasi hiki?”
Tabasamu la kejeli lilienea usoni mwa
Lina kabla hajauliza. "Sawa, familia ya Masawe imekulipa kiasi gani ili
kuniaibisha leo?"
“Haya siyo majibu mazuri. Wewe ni tofauti sana na Lina ingawa nyote wawili
mnatoka katika familia moja.”
“Hakika! Lina hata alituletea juisi na soda mapema. Umelelewa na wanandoa wa Masawe tangu kuzaliwa lakini adabu yako haiendani na familia
hiyo.” Waandishi walizidi kumshambulia
Lisa.
Lisa alikodoa macho. Kijana mtanashati
aliyevalia suti ya kijivu alikuja
kumuokoa. Vitisho vikali vilionekana
katika sauti yake. "Leo ni siku muhimu
kwa familia ya Masawe na Lowe.
Wageni wengi wa heshima watajitokeza
kwenye tukio hili, akiwemo Cindy
Tambwe. Hata hivyo kundi hili la
mapaparazi limemvizia msichana dhaifu
ili kumwaibisha. Je, yeye ni msanii au mtu maarufu mtandaoni? Kwa kuwa
mnapenda sana kumhoji, kwa nini
msimhoji kwa mazuri?”
Waandishi wa habari walitawanyika polepole, na kicheko cha kicheko
kikatoka kwenye midomo ya Lisa .
"Asante sana, Bw. Patrick Jackson. Umekuwa tofauti baada ya kuchukua
nafasi ya ukurugenzi katika kampuni yenu. Si ajabu rafiki yangu Pamela
anaanguka kichwa chini kwa ajili yako.”
Lisa alimpa sifa za shukrani mtu huyo, mpenzi wa Pamela, Patrick Jackson aliyemwokoa kutoka kwa mapaparazi.
"Acha wewe. Pamela amekuwa
akinipigia simu tangu jana usiku ili
kuhakikisha nakulinda kwa lolote.
Twende,” alisema huku akitabasamu.
Lisa alikuwa karibu kuitikia kwa kichwa
wakati mwanamke mrembo aliyevalia
mavazi ya manjano angavu alisonga
mbele ya mwanamume huyo kwa miguu
yenye viatu vya visigino virefu ili
kumshika mkono. “Patrick unatembea
haraka sana na siwezi kukupata. Karibu nianguke sasa hivi.”
Lisa alimtazama mwanamke
huyo. "Huyu ni Linda Sheba kutoka kwa familia ya Sheba. Pia amealikwa
kwenye sherehe ya uchumba usiku
huu,” Patrick alimtambulisha Linda kwa
Lisa.
"Loo," Lisa akadakia, akielekeza macho yake kwa mwanamke huyo na kumpa
mkono wa salamu. Alicheka na kuongea ki-nusu-utani. “Nilishtuka sana kumuona
akijibebisha kwako. Nilidhani ndiye
mpinzani wa Pamela."
Patrick akashtuka akamtazama Linda
aliyekuwa kamuegemea kichwa chake
kwenye bega lake, akamtoa taratibu na
kumwambia Linda kwa uchungu, “Linny,
nilikuambia hivyo mara nyingi hatuwezi
kuishi kama tulipokuwa wadogo tena. Watu wengine wanaweza kutufikiria vingine.”
“Nimezoea. Isitoshe, baada ya kuja hapa, kwa kawaida ninakuona kama
mwenza wangu kwa usiku huu.” Linda
alitoa ulimi kwa kucheza kabla ya
kumwambia Lisa , “Haya, mimi ni rafiki wa Pamela pia na huwa tunabarizi kila
wakati. Nitasikitika ikiwa utaathiri
uhusiano wao kwa kumpelekea maneno yasiyo sahihi.”
"Ni sawa, Lisa hajasema chochote kibaya." Patrick akampigapiga Linda
kichwani. “Twendeni tukaketi.”
Wote watatu walianza kutembea
kuelekea kwenye ukumbi wa sherehe
kwa pamoja. Lisa alimtazama kwa
haraka Linda kwa pembe ya macho
yake. Kwa sababu fulani, alimtilia
mashaka yule binti. Msichana huyo
hakika alikuwa na nia ya siri.
Tangu Lina alipomwibia Ethan, Lisa alihisi kana kwamba alikuwa
amesitawisha uwezo wa pekee ambao
ungeweza kuchanganua kwa usahihi
utu wa mwanamke. Isitoshe, mwanaume anawezaje kuwa na urafiki wa karibu hivyo na mwanamke
mwingine mbali na mpenzi wake? Hii
bila shaka haikuwa ishara nzuri.
Wakati huohuo, Jones Masawe na mkewe walimwona Lisa kwa mbali na
kumpa ishara kwa tabasamu. Lisa
hakutaka kuona sura zao bali alitembea
kuelekea kwao hata hivyo kwa sababu ya bibi yake.
Bila kutarajia, ghafla Mama Masawe
alimkumbatia karibu na kuzungumza kwa upendo. “Bw. Chande, huyu ni binti
yangu mwingine kipenzi, Lisa. Yeye sio
jasiri tu, bali pia mkarimu na mwadilifu.
Si muda mrefu uliopita, hata alishirikiana na polisi kama wakala wa siri ili kuangusha kikundi kinachotengeneza video haramu. Dada yake ataolewa hivi karibuni lakini yeye bado hajapata mchumba. Je, huna mtoto wa kiume mdogo…”
Msururu wa hisia ulipita usoni mwa huyo mzee Chande. Kwa kiasi fulani
video iliyomwonyesha Lisa akiwa karibu
kubakwa na Zakayo kabla hajaokolewa na Alvin ilikuwa imesambaa kwa watu wengi na kuathiri sana sifa yake.
Hakuna familia ambayo ingethubutu kumchukua tena.
"Oh, sawa, anaonekana kama msichana
mzuri. Nasikitika mwanangu mdogo
tayari yuko kwenye uhusiano. Huyo, si
Mwenyekiti wa Bodi ya Sukari?
Imekuwa muda mrefu…ngoja nionane
naye mara moja.” Mzee Chande alitoa
udhuru na kuondoka haraka.
Jones Masawe alisema kwa kukata
tamaa, “Usijali, Lisa . Nitakutafutia
mume mwema leo.” Lisa alichukia sana kwa maigizo aliyoyaona yakifanywa na wazazi wake. Tayari alikuwa amekata tamaa kwa wanandoa hawa.
“Mnaweza kuacha kujifanya sasa. Ninyi ndio mliopanga waandishi wa habari mlango kwa ajili yangu, na sasa,
maneno yanawatoka kana kwamba sisi ni familia yenye furaha. Hakuna haja ya kuendelea kuigiza. Niko hapa tu leo kusherehekea siku ya kuzaliwa ya Bibi. Sipendezwi na kitu kingine chochote.”
Mama Masawe alipunguza hasira yake na kusema taratibuo, “Lisa mwanangu, ni nini kilikupata hata ukakosa moyo
kiasi hicho? Haijalishi ni nini, tumekulea
tangu kuzaliwa kwako na tulitumia muda
mwingi na bidii kukuelimisha. Ni jambo
moja kwamba hutambui makosa yako
lakini hata unatudharirisha hadharani?
Je, dhamiri yako imekuacha? Mbali na matatizo yako na Lina, je kuna kitu
kingine tulichokukosea? Tulikupeleka katika nyumba ya zamani pia kwa faida yako mwenyewe!”
“Umesema kweli, sina sababu ya kuwachukia. Nyinyi wawili mlinileta
katika ulimwengu huu, lakini hiyo
haimaanishi kuwa nanyi mnaweza
kuchukua uhai wangu pia!”
Lisa alicheka kwa hasira.
Jones alipiga kelele, “Tangu lini
tukataka kuchukua uhai wako?
Kulikuwa na kila kitu kwenye ile nyumba
ya Moshi, kila kitu cha msingi
kilikuwepo. Na ile nyumba haijawahi
kukatika maji wala umeme, sasa
nilishangaa kusikia kuwa nilikuwa
nimekukataza kula au kupata maji.”
Jambo hilo lilimshangaza sana Lisa. Ina maana bibi kizee alikuwa ni mpango wa nani? "Lakini yule bibi mzee… " Kabla hata hajauliza swali lake, sauti kali
ilimkatisha ghafla.
SURA YA 48
“Lisa , umeikuja kweli!" Sauti ya Lina ya mshangao ikajaa chumbani.
Kabla Lisa hajajibu, Lina alimshika kwa mkono wake wa kushoto na kuunganisha na mkono wake wa kulia na wa mama yao. “Vipi mkuu! Hatimaye familia yetu imekamilika.”
Lisa aliinua mkono wake aliokuwa
ameushika Lisa na kusema kwa ukali, “Tafadhali sogeza mkono wako mbali. Sitaki mazoea na wewe!”
“Lisa , unamaanisha nini?” Sura ya aibu
ilisambaa kwenye uso mzuri wa Lina.
Haraka haraka akamshika Ethan mkono na kumsihi kwa upole. “Ethan, zungumza na Lisa . Tumealika wageni wengi leo na ni muhimu familia yetu iwe na amani kati yetu.”
Ethan alifikiri Lisa alimaanisha kuzua
matatizo tena hivyo akamwangalia kwa makini. Lakini, katika sekunde iliyofuata
alishtushwa kabisa na mvuto wa Lisa.
Lisa alikuwa amevaa nguo ndefu
nyeupe. Nywele zake nzuri zilikuwa katika hali ya kawaida lakini maridadi.
Alionekana kuvutia sana.
Lina alionekana mrembo pia, lakini ilikuwa hasa kwa sababu ya mapambo na mapodozi yake. Hakuweza
kulinganishwa na uzuri wa asili wa
Lisa hata kwa tabaka nene za
mapambo. Ikiwa sio kwa kila kitu
kilichotokea huko nyuma,
Lisa angekuwa mtu ambaye alikuwa
akimchumbia siku hiyo.
Uchungu mwingi ulimkumba Lina baada ya kumuona Ethan akimtazama
Lisa kwa butwaa. Alisema tu kwa lengo la kumshtua Ethan. "Lisa unaonekana mrembo leo. Natumai ulitumia masaa mengi kujiandaa kwa usiku wa leo.
Tazama, kila mtu hawezi kuacha kukutazama.” Aibu ilitanda kwenye uso mzuri wa Ethan huku akirudisha macho yake mara moja.
Mama Masawe alichukizwa na hali hiyo.
"Lisa , nimekualika hapa leo ili kutoa baraka zako, sio kuwa kivutio cha
sherehe. Leo ni siku kuu kwa dada yako.”
Bila kukawia, Lisa alijibu kwa huzuni, “Samahani kwa hilo lakini halikuwa kosa
langu kupendeza, ilinichukua dakika
kumi tu kujiandaa. Yote inakuja kwa
sababu ya uzuri wangu wa asili. Sipaswi
kulaumiwa kwa kuzaliwa mrembo kuliko
yeye. Hata hivyo si mimi niliyemzaa.”
“Wewe…” Mama Masawe hakupata neno la kumfaa Lisa kutokana na maneno yake ya kejeli.
Lisa aligeuka kumwangalia Lina kabla ya kucheka tena. “Una wivu wa siri
kwamba mimi ni mrembo kuliko wewe, sivyo? Sema moja kwa moja badala ya kujaribu kutupa vidokezo vya hila kushoto na kulia wakati wote.”
“Lisa sivyo namaanisha.
Ninakupongeza kwa dhati." Machozi ya huzuni yalikuwa yakibubujika taratibu machoni mwa Lina.
Ethan hakuweza tena kuvumilia. “Lisa umetosha? Wewe pekee ndiye
uliyekuwa mkali kwa Lina tangu mwanzo.”
"Hapo sasa, kuna mtu anajitokeza kukulinda, raha iliyoje?" Lisa aliongea kwa tabasamu la kejeli. Ethan alitoa macho kwa hasira.
Hatimaye Johes Masawe alizungumza, “Sawa, bado tuna wageni wanaingia.
Lisa nenda kwenye chumba cha faragha ukamwangalie bibi yako.
Utarudi tena sherehe itakapoanza."
“Nitaondoka baada ya kumuona bibi, sina shida na sherehe hii.” Lisa alijibu kwa jeuri kama kawaida.
“Itabidi umlishe chakula baadaye.”
Jones akamkatisha kwa kukosa subira, “Bibi yako alipooza baada ya kuanguka muda mfupi uliopita. Hawezi hata
kujilisha mwenyewe sasa hivi.”
Habari hizi ziliulipua moyo wa Lisa kama bomu. Hakuamini
alichokisikia. Ilikuwa imepita mwezi
mmoja tu tangu amtembelee bibi yake
mara ya mwisho na alikuwa mzima. Hili lingewezaje kutokea? “Mbona
unaniambia vitu vya ajabu?!” Lisa aliuliza kwa mshangao.
“Nenda, hutufai hapa. Hakuna kingine
unaweza kufanya mbali na kutukasirisha tu”
Lisa aliondoka kwa haraka kuelekea
chumba cha faragha. Bibi kizee
mwenye mvi alikuwa ameketi kwenye
kiti cha magurudumu, akitazama dirishani bila mwelekeo. Mwanamke
mwingine karibu naye alikuwa akimnywesha maji.
Machozi yalitiririka mashavuni mwake.
"Samahani bibi, nimekuja kukuona sasa hivi." Hakuwa amemtembelea kwa siku
chache zilizopita ili kuepusha kumfanya
bibi yake kuwa na wasiwasi.
Mbali na babu yake ambaye alikuwa
ameaga dunia, bibi yake ndiye pekee
aliyesalia katika familia ya akina
Masawe ambaye alimtendea mema
tangu akiwa mdogo. Tangu alipokuwa
msichana mdogo, Jones Masawe na mkewe walikuwa wakimkalipia bila hata
sababu. Bibi yake ndiye pekee aliyempenda kwa dhati bila masharti.
Hata hivyo, alipoondoka kutafuta elimu zaidi nje ya nchi, bibi yake huyo alirudi
Moshi.
"Bibi Masawe kwa kiasi fulani ni kiziwi sasa, kwa hivyo hasikii vizuri,"
mwanamke aliyekuwa akimhudumia alisema.
“Na wewe ni…” Lisa hakumtambua
mwanamke huyu. Shangazi Manka
ndiye alikuwa daima mlezi wa bibi yake.
"Familia ya Masawe waliniajiri kumtunza
Bibi Masawe. Unaweza kuniita
Shangazi Helen.” Alijitambulisha yule
mwanamke.
“Lakini vipi kuhusu Shangazi Manka?”
"Inavyoonekana, aliona shida kumtunza Bibi Masawe baada ya kupooza na akajiuzulu." Alijibu Helen
Jambo hilo lilimshangaza Lisa. Manka
alikuwa amemtunza bibi yake kwa zaidi ya miaka 30 na wote wawili walikuwa wamejenga uhusiano mzuri. Bibi
Masawe alimhitaji zaidi kwa kipindi hicho, kwa hiyo ilionekana kuwa
haiwezekani kwamba angeondoka wakati huo. Labda Manka alikuwa
akizeeka naye na kazi hiyo ilikuwa imemchosha. Alisikitika sana kufikiria
hali ya bibi yake. Alipiga magoti mbele
ya yule mzee na kuushika mkono wake.
“Bibi, mimi ni Lisa, niko hapa kukuona.”
Bibi Masawe alimtazama kwa
mshangao kabla ya kufunua tabasamu alilolifahamu. “Ni wewe, Sheryl.
Umekuwa nje siku nzima tena? Haraka ubadilishwe nguo safi. Baba yako
anatupeleka out kwa chakula cha jioni.”
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda mfupi baada ya kusikia hivyo. Sheryl
alikuwa shangazi yake, lakini alikuwa ameaga dunia zaidi ya miaka 20
iliyopita.
“Bibi, umem’miss tena Shangazi Sheryl?” Bibi Masawe hakuonekana
kumuelewa na kuanza kunung'unika bila mpangilio. Lisa aliketi karibu na bibi
kizee huyo akihisi kukata tamaa.
Karibu saa 12 jioni, Jones alitokea tena
chumbani. "Mlete bibi yako nje kwa chakula."
"Naweza tu kumlisha humuhumu ndani kutokana na hali yake." Alihisi kuudhika kumtazama baba yake usoni.
"Sijakupa chaguo. Lazima utoke naye huko nje sasa hivi ili kula chakula cha amani na familia yetu. Vinginevyo, sitakuruhusu kuonana na bibi yako tena,” Jones aliagiza.
Lisa hakujua Jones alikuwa na maana gani. Alikuwa amesema maneno 'familia yetu'. Ilionekana kwamba alikuwa ameamua kumtenga kabisa na familia.
“Sawa, nitamleta.”
SURA YA 49
Lisa alimsukuma Bibi Masawe, aliyekuwa kwenye kiti cha magurudumu kutoka nje ya chumba hicho na kuelekea kwenye ukumbi wa sherehe.
Waliekezwa kuketi kwenye meza moja
na wanandoa waliokuwa
wakichumbiana, Lina na Ethan.
Baada ya kuketi, alimuona
Kelvin Mushi akiwa ameketi kwenye
meza kuu nyingine iliyotengwa kwa ajili ya jamaa wa karibu. Sura ya kuchanganyikiwa ilienea usoni mwa
Lisa. Hapo mwanzo Kelvin alimwambia
kuwa ni ndugu wa mbali kwa familia hizi
zote mbili lakini kwanini alikuwa amekaa
pamoja na Jones Masawe na Bibi
Masawe?
Kingine kilichomshangaza Lisa ni kuhusu Alvin. Kwanini hakuhudhuria
sherehe hiyo ingawa alikuwa mjomba
wa Ethan? Kinyume chake, Janet Kileo
na Cindy Tambwe, ambao walikuwa ni marafiki wa kudandia tu wa Lina, walijitokeza. Lisa alicheka kwa ndani.
Hakika Lina alikuwa amejitolea kujenga
uhusiano wa kinafiki na watu ambao
hakuwapenda.
Sherehe ya uchumba ilianza saa kumi na mbili na nusu jioni. Emcee wa shughuli alipanda jukwaani kumshukuru kila mtu kwa uwepo wake. Hatimaye, Ethan na Lina walialikwa kwenye jukwaa. Lina aliyekuwa amevalia nguo nyekundu alisimama karibu na Ethan aliyekuwa amevalia suti nyeusi. Wawili hao walionekana wakamilifu pamoja.
Wageni walianza kutoa maoni juu ya wanandoa. "Nilisikia kwamba binti wa
kwanza wa Masawe, Lina amekulia kijijini ilhali yeye ni mrembo na mwenye utulivu. Si ajabu kwamba Ethan amemwangukia.”
“Kulikuwa na uvumi mwaka jana
kwamba Ethan angechumbiana na Lisa.
Hakika ningemchagua Lina pia kama
ningekuwa katika viatu vyake. Utu mzuri
hushinda zaidi ya yote."
Kelele hizo zilipita masikioni mwa
Lisa kama dhoruba za upepo, lakini aliamua kuzipuuza na badala yake
akazingatia kumlisha bibi yake. Kilichomuumiza zaidi Lisa ni baada ya
Cindy, ambaye alikuwa ni rafiki yake wa zamani, kupanda jukwaani kukabidhi
pete za uchumba.
Cindy alisema kwa mzaha kwenye kipaza sauti, “Kwa kweli, nimemjua
Ethan kwa takriban miaka saba au minane sasa na ni kama kaka mkubwa
kwangu. Wasichana wengi walikuwa wakimfuata nyuma katika shule ya sekondari lakini hakuna hata mmoja wao aliyemvutia macho. Nilifikiri hakuna
mtu angewahi, hadi alipokutana na Lina na kumkubali mara ya kwanza.”
Akamtupia macho Lisa . “Lisa , utaungana nami na kuwapa salamu zako, sivyo?”
“Uko sawa.”
Lisa aliweza kuhisi kejeli katika kila neno lake. Cindy asingeweza kujuana
na Ethan kama Lisa asingalikuwa rafiki yake. Rafiki yake wa zamani sasa
alikuwa akimpongeza mpenzi wake wa zamani kwa ndoa yenye furaha. Je, hii
inaweza kuwa kejeli kiasi gani?
“Oh, hakika.” Lisa aliinua glasi yake
taratibu huku tabasamu la ajabu likienea usoni mwake. "Nimegundua hakuna mtu anayeweza kukosa aibu kuliko ninyi
watatu." Lisa alikohoa kidogo kama
anayejiweka sawa kwa jambo furani
kisha akasema. “Naomba kwanza
tushuhudie hadithi ya mapenzi ya hawa wachumba. Tafadhali elekezeni macho
yenu kwenye skrini, " Lisa alisema.
DJ aliweka wimbo mzuri wa kimahaba.
Lakini, onyesho la picha kwenye screen
lilikuwa linaonyesha picha za Lisa na
Ethan. Baadhi ya picha zilichukuliwa
walipokuwa watoto wadogo. Chache
kati ya picha hizo zilimwonyesha Ethan alipokuwa amesafiri maili nyingi kuvuka
anga na bahari ili kumtembelea Lisa alipokuwa akisoma nje ya nchi.
Walionekana wenye furaha sana kwenye picha.
Ni wazi kwamba wageni waalikwa katika
ukumbi wa sherehe walishtuka.
Familia za Lowe na Masawe hazikufurahishwa. Jones alipiga meza na kuinuka haraka. “Upuuzi gani huu?
Zima mara moja.”
Mara moja skrini ilifungwa, lakini sekunde chache za kuonekana picha zile zilitosha kusababisha ghasia kati ya wageni. “Nini kinaendelea? Je, Lisa na Ethan
walikuwa pamoja hapo awali?”
“Nani alifanya hivi? Inaweza kuwa
Lisa?" "Pengine. Nilifikiri alikuwa anafanya mambo ya ajabu tangu alipoingia ndani.”
Lisa alikunja uso kidogo kama alikuwa na machale kwamba kitu mbaya ilikuwa
karibu kutokea. Lisa hakuhusika na chochote juu ya jambo hilo lakini ni wazi, mtu fulani alikuwa akijaribu
kumseti. Mtu pekee ambaye angeweza
kufanya haya yote labda alikuwa Lina!
Mwanamke huyo kweli alitoa sadaka
sherehe yake ya uchumba kwa sababu ya kumdhalilisha Lisa? Ukatili ulioje!
"Ni nani aliyefanya hivi?!" Mama
Masawe alipiga kelele kwa hasira.
Fundi mitambo akasonga mbele haraka.
“Mama Masawe, samahani sana.