waandishi ebook 1686264728.12888

Page 1

KURASA.....126-150

Sura ya 126 “Usifanye, usifanye.” Kwa kufikiria onyo

la Alvin jana yake, Willie alimzuia Lisa mara moja. “Alikataa kuniruhusu

nikuambie kuhusu hilo. Kwa kuzingatia

kwamba nimeshiriki video zangu za

faragha na wewe, tafadhali unaweza

kujifanya kuwa hujui lolote, Bi Jones?”

Lisa alishangaa kusikia hivyo kutoka

kwa Willie. Alvin alikuwa kweli mtoto wa

familia tajiri ya Kimaro? Kwa kuwa Willie

alikuwa akimheshimu na kumuogopa

sana Alvin, inawezekana kwamba Alvin

alikuwa na nguvu kubwa kuliko Willie?

Inawezekana kuwa yeye ndiye mrithi wa familia ya Kmaro? Asingeweza kamwe

kufikiria kuichokoza familia ya Kimaro.

STORY............LISA

Familia ilikuwa ngumu sana kwa mtu wa kawaida kama yeye kufikiria.

“Sawa, nakuahidi, lakini naweza kujua Lina alikufahamu vipi?” Lisa aliuliza huku akijilazimisha kutulia.

"Ni Stephen ambaye alimtambulisha kwangu," Willie alidhihaki, "Msaidizi wangu anafahamiana na familia ya Kileo. Stephen alitaka kuanzisha

uhusiano nami, kwa hiyo akamtuma mpenzi wake kwangu.”

Lisa alishangaa “Unafurahia kulala na rafiki wa kike wa rafiki yako?”

Willie alitoa kikohozi kidogo. “Kweli, mke si mtamu kama mchepuko. Inavutia zaidi kulala na mpenzi wa mtu mwingine.”

Lisa alikosa la kusema. Alikuwa na shauku kubwa ya kumuuliza ikiwa yeye

ndiye pekee mwenye tabia mbovu

katika familia nzima ya Kimaro au ikiwa kuna wengine wote walikuwa hivyo, ikiwemo Alvin, lakini hakufanya hivyo.

Baada ya kurudi ofisini, Lisa alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa. Hapo awali aliolewa na Alvin kwa kudhani kuwa alikuwa mjomba wa Ethan.

Baadaye, aligundua kwamba alikosea na akafikiri kwamba Alvin alikuwa wakili tu. Nani alijua kuwa yeye alikuwa mtoto wa familia tajiri na maarufu zaidi nchini?

Naam, haikumshangaza. Badala yake, aliona kuwa ilikuwa na mantiki. Huenda

Alvin alikuwa akimpima. Ikiwa

angekutana na Alvin akajiweka wazi

utambulisho wake, angehisi kwamba

amempenda kwa ajili ya mali zake.

Vilevile Alvin angempeleka

kumtambulisha nyumbani kwao, familia yake labda isingemkubali.

Ghafla, alihisi kuchoka. Ili kujizuia

kuwaza kupita kiasi, alibofya kipande

kimojawapo cha video ambazo Willie

alimtumia. Mwanzoni, alikuwa akijaribu tu kuangalia juujuu. Kinyume na matarajio yake, video hiyo iligeuka kuwa ya kufurahisha sana hivi kwamba Lisa

ambaye alikuwa hajakomaa kama Lina aliguna.

Alipotambua kwamba alikuwa amezama

katika video hiyo, Shani alimkumbusha hivi kwa uchungu, “Bi Jones, ulisema

hutaitazama, sivyo? Zaidi ya hayo, Bwana Kimaro hatakuruhusu kutazama aina hii ya mambo.”

"Lo... Hatajua kama utatunza siri." Lisa

alitoa tabasamu la aibu. Kwa kuwa Alvin

asingemruhusu hata kutazama picha

zisizofaa za Willie, bila shaka

angemchuna akiwa hai iwapo angejua

kuhusu jambo hili. Shani alishindwa cha

kusema. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kulifumbia macho.

Lisa alipokuwa akiitazama video hiyo, wazo zuri lilimjia. Alimwita msaidizi

wake haraka. “Nakumbuka mjukuu wa Amiri alisema kwamba kuna mnada unakuja?”

“Ndiyo, ni usiku wa leo. Mratibu wa manada amekualika pia kwenye tukio.

Watu wengi matajiri wa hapa Dar na mikoa mingine watahudhuria.”

“Sawa. Hata mimi nitaenda.” Lisa alicheka. Leo itakuwa siku ya giza zaidi katika maisha ya Lina.

Hotelini Baada ya kutoka kwenye ofisi

za Mawenzi Investments, Willie alikuwa

tayari kufungasha vitu vyake na

kuondoka Dar. Kukaa katika jiji moja na

Alvin kulitisha maisha yake.

Alipousukuma tu mlango wa chumba,

•••

alimuona mtu mrefu akiwa ameketi

kwenye kochi la ngozi, akifanana na mfalme. Miguu yake iligeuka kuwa

milegevu kama mlenda, na midomo yake iliendelea kutetemeka. “Kaka

Alvin, umekuja kwa wakati ufaao. Nilikuwa karibu kukuambia kuwa

nilienda Mawenzi Investments na kusuluhisha suala hilo. Hakuna mtu

atakayethubutu kumsababishia Lisa matatizo tena.”

“Najua. Umefanya vizuri sana.” Alvin

alikaa pale bila wasiwasi huku hisia za heshima kubwa zikitoka kwenye uso wake mzuri. Willie alijawa na furaha moyoni kusikia hivyo. Kabla hajaongea, midomo myembamba ya Alvin ilianza

kusonga. "Lakini ... hakushuku chochote?"

Mara tu Alvin alipomaliza kuongea, hali ya wasiwasi na hofu ilitawala mazingira.

Moyo wa Willie ulionekana kuganda.

“Usinidanganye, Willie,” Alvin alionya kwa upole, “unakumbuka kilichotokea ulipokuwa na umri wa miaka 18 baada ya kunidanganya, sivyo?”

Willie akatetemeka. Mwaka aliofikisha

miaka 18 ulikuwa mwaka wake wa giza kuwahi kutokea.

kama jani linalopigwa na upepo, Willie aliogopa sana kumficha. "Sasa anajua

kwamba unatoka katika familia ya Kimaro, lakini sikumwambia makusudi

kuhusu hilo. Yeye ndiye aliyenitega, na nilifanya makosa. Zaidi ya hayo, majina yetu ya mwisho ... "

Alvin akasugua macho yake. Alijua

mapema kwamba Willie, mpuuzi yule

kijana, angeshindwa kufanya kulingana na maagizo yake na kuishia

kumuumbua zaidi.

"Yeye ... alishuku." Huku akitetemeka

Willie alisema kwa kigugumizi, “Kaka

Alvin, una wasiwasi kwamba

atajikombakomba kwako na kukusumbua baada ya kukujua wewe ni nani? Kwa kweli, hii ni kawaida sana kwetu. Haijalishi tunaenda wapi, wanawake wengi humiminika kwetu. Hata hivyo, hadhi yake ni ya chini sana

kuwa mpenzi wako.

"Nyamaza." Macho makali ya Alvin yalimkumba. "Ondoka Dar mara moja."

“Sawa, sawa. naondoka sasa hivi kaka.”

Willie pia hakujisikia kubaki mahali hapo

pabaya palipomchachia. Mara moja

akafungasha vitu vyake na kuondoka

kama anayefukuzwa.

Alvin aliinuka na kuelekea kwenye

dirisha lililokuwa ndani ya chumba

hicho. Akili yake sasa ilikuwa

imevurugika kabisa Alikuwa mtu

mwenye shaka. Alipokuwa akiishi katika

neema ya utajiri wa familia ya Kimaro

tangu alipokuwa mdogo, wanawake

wengi walikuwa wamemtumia kwa

kisingizio cha kumpenda kwa sababu ya utambulisho wake, jambo ambalo lilimjaza chuki. Kwa hiyo, hakuwahi

kumwambia Lisa kuhusu utambulisho wake halisi, akitumaini kwamba

angempenda yeye kama yeye na si kwa utajiri wake. Hata hivyo hakuna marefu

yasiyo na ncha. Hatimaye Lisa alikuwa

amejua kuhusu utambulisho wake.

Angemwonaje?

Hans alimwambia kwa upole, “Usijali, Bwana Kimaro. Lisa alikupenda tangu

alipokutana nawe kwa mara ya kwanza

kwenye baa. Wewe ndiye anakupenda, na haihusiani na utambulisho wako.”

"Hiyo ni

Alvin alijisikia raha.

Kweli, kwa nini alikuwa anafikiria kupita

kiasi? Alikuwa ameanguka kwa ajili

sawa."

yake bila matumaini, kama yeye

mwenye alivyosema.

•••

Saa kumi na moja jioni, gari jeusi

lililoonekana kuwa la gharama kwa

mwonekano wake lilikuwa limeegeshwa nje ya mlango wa jengo la Mawenzi

Investments. Muda mfupi baadaye, Lisa alishuka kwenye gari huku yule

aliyekuwa kwenye kiti cha dereva akivua koti lake. Alionekana akiwa

amevalia shati jeupe chini ya fulana, ambayo ilisisitiza umbo lake refu. Akiwa na sura nzuri ya kuvutia, alitoka kama

mhusika kutoka kwenye kitabu cha hadithi za kubuni.

Ingawa alimuona kila siku, sura yake ya kuvutia haikukosa kumshangaza.

Hakika asngechoshwa na sura ya mwanaume huyo.

Alipojua kuhusu utambulisho wake siku

hiyo, alikuwa akipingana na mawazo

yake kila mara. Hata hivyo, wakati huo,

alikuwa na hakika kwamba asingeweza

kuvumilia kumwacha mwanamume huyo.

Siku zote alikuwa mtu ambaye alikaa karibu naye katika nyakati ngumu zaidi.

Siku hiyo, alimsaidia kukabiliana na dhoruba tena. Haijalishi jinsi gani safari yao ya mbele ingekuwa ngumu, alisisitiza kuwa pamoja naye.

“Mbona unanitazama?” Alvin alibana

ncha ya pua yake, alikuwaakijshtukia.

Lisa aliitazama saa iliyokuwa kwenye

mkono wake, jambo ambalo

lilimkumbusha jinsi alivyokuwa akimshangaa kwa aina ya nguo zake.

Ikamjia akilini kwamba huenda nguo

hizo zilikuwa zikificha utambulisho wa

Alvin kwa makusudi.

“Ninautazama uso wako mzuri. Pia, niko

katika hali nzuri leo. Uliona jinsi Jones

na Lina walivyofedheheka? Lina siku

zote alijifanya kuwa safi na aliishi kwa

unafiki wakati huo. Sasa, kila mtu anamdharau.”

“Ndiyo.” Baada ya kumsikia akipiga

kelele, Alvin aliinua macho yake na kuuliza, "Kuna chochote unachotaka kuniuliza?"

Sura ya 127

Lisa alipigwa na butwaa. Alikuwa amepanga kumuuliza Alvin kuhusu

utambulisho wake halisi. Hata hivyo, uhakika wa kwamba alimwomba Willie

afiche utambulisho wake ulionyesha

kwamba hakutaka kumfunulia. Katika

hali hiyo, hakujisumbua kumuuliza.

"Hapana." Alvin taratibu akadondosha macho yake. Lisa alimtazama wakati

huo na kusema, “Nitahudhuria mnada

usiku wa leo, kwa hivyo sitakuwa

nyumbani kwa chakula cha jioni.

Unataka… kwenda pamoja nami?”

Aliuliza kwa tahadhari ingawa alihisi kwamba Alvin asingekubali kwenda pamoja naye. Kwa kuzingatia tabia yake ya kiburi na dharau, asingependezwa na tukio la aina hiyo.

“Sawa.” Alvin akakubali.

“Huu?” Lisa aliduwaa, akifikiri kwamba alimsikia vibaya.

“Nimesema sawa. Mbona unashangaa?” Alvin alitazama sura yake iliyopigwa na tabasamu.

"Lakini hupendi kushiriki katika hafla

zinazofanyika Dar se salaam, leo imekueje?"

"Ninakuja ili kuzuia wanaume wowote wasikucheze." Alvin alijibaraguza.

Aliendesha gari kwa umakini huku

macho yake yakiwa yametazama

barabara iliyo mbele. Lisa aligeuza

kichwa chake na kutazama wasifu wake

kamili kwa muda. Hakuweza kujizuia

kumpa busu la shavuni. Usukani

uliokuwa mikononi mwake ulitetemeka, kisha akamwambia kwa utani, “Usinichezee kimapenzi ninapoendesha gari.”

Sentensi hiyo ilionekana kuwa ya kawaida. Lisa alicheka na kujibu, “Najua. Itasababisha ajali mbaya sana, si ndiyo?" "Hapana." Akamtazama. "Itasababisha moyo wangu kuruka."

Mapigo ya moyo wa Lisa yakagongana na kifua. Hali isiyoeleweka ilionekana

kujaa kwenye mishipa ya mwili wake

mzima. Moyo ulimwenda mbio zaidi

baada ya kumbusu. Wakati huo, alikuwa na hamu kubwa ya kumbusu kwa

mapenzi. Hata hivyo, alitilia maanani

zaidi usalama barabarani.

Saa moja na nusu usiku, Mnada ulikuwa

karibu kuanza katika jumba la mikutano

la Karimjee. Watu mashuhuri kutoka

Dar es Salaam na mikoa jirani waliingia

ukumbini mmoja baada ya mwingine.

Kama mwenyekiti wa Mawenzi

Investments, Lisa alionekana kuwa

kivutio cha tukio hilo. Umati ulimsonga

mara tu alipoingia ndani.

Ethan naye alikuwepo. Alivyoona jinsi

Lisa anafuatwa sana na watu kwa

mbali, Ethan alijawa na uchungu.

Kamwe katika ndoto zake hakutarajia

kuwa mpenzi wake ambaye awali

alimwacha kwa ajili ya Lina angekuwa

mwenyekiti mpya wa Mawenzi

Investments ndani ya muda mfupi.

Wakati huo watu wengi walimwona

mpumbavu. Kwa kweli, Ethan alikuwa

mpumbavu. Alimkosea kipumbavu sana

Lisa na kwa hivyo akakosa nafasi ya kuwa naye. Akiwa na mwanamume bora kando yake sasa, aliona kwamba asingekuwa na nafasi yoyote kwake.

Mchumba wake mpya, Tracy Laizer, alikuwa ameketi kando yake na kuubana mkono wake. "Nilisikia kwamba yeye ni mpenzi wako wa zamani, ni kweli?"

'Yote ni ya zamani." Ethan alilazimisha tabasamu. Alijua kwamba angeweza tu kufanya kazi kwa bidii ili kuifurahisha familia ya Laizer kwa sasa.

“Ni vizuri kwamba unajua. Maadamu unanipenda sana, familia yangu itakutegemeza,” Tracy alisema kwa upole.

Upande mwingine, Lisa naye alimwona

Ethan pia kwa sababu ya suti yake

nyeupe iliyovutia. Mwanamke wa ajabu

kutoka familia mashuhuri alisimama

kando yake. Moyoni mwake, Lisa alihema huku akimfikiria mwanaume

ambaye aliyemuona kuwa mkamilifu wakati ule. Kinyume na matarajio yake yote, mwanamume huyo aligeuka kuwa mtu ambaye angemsaliti kwa ajili ya mamlaka na umaarufu.

“Unamtazama Ethan?” Ghafla sauti ya Alvin ya kuonya ilisikika.

"Nilikuwa nikifikiria juu ya jambo fulani."

“Ulikuwa unafikiria nini?” Alvin alikasirika.

"Yajayo yanafurahisha. Onyesho nzuri inakuja. Utajua baada ya muda mfupi.”

Lisa aliinua uso wake, macho yake angavu yaking'aa kwa ucheshi. Uso wa

Alvin ukalegea taratibu.

Wanawake kadhaa ambao waliolewa na wafanyabiashara matajiri walimzunguka Lisa na kumpongeza.

“Mwenyekiti Jones, hili gauni umenunua wapi? Ni nzuri!"

"Mkufu uliovaa umetoka kwa Tiffany na ndio muundo mpya zaidi, sivyo?"

"Habari za jioni, the bosy lady?"

Ghafla Janet alishika glasi ya mvinyo

mwekundu na kumsogelea Lisa kwa nia mbaya. “Ah, Mwenyekiti Jones, sikutarajia kwamba ungekuwa na jeuri ya kushiriki katika mnada. Subiri kidogo, sina uhakika kama bado nitakuita

Mwenyekiti Jones sasa hivi.”

"Unamaanisha nini, Bi Kileo?" mmoja

wa wanawake hao, Madam Clark, aliuliza huku akihema.

Janet akahema. “Pengine ninyi nyote

hamfahamu kilichotokea. Nilisikia

kwamba Mwenyekiti Jones alimpiga

Willie Kimaro aliyetoka Nairobi wakati wa sherehe ya kumbukumbu ya

Mawenzi Investments jana usiku.”

"Nini? Unamaanisha huyo Willie kutoka familia ya Kimaro?"

"Ndio, ni yeye." Janet akaitikia kwa

kichwa. “Rafiki yangu aliniambia

kwamba Mwenyekiti Jones alisababisha

uso wa Bwana Kimaro kuvimba, na

Bwana Kimaro alikasirika sana. Sijui

hata atafanya nini! Hiyo ilikuwa ni sawa na kujitakia matatizo makubwa sana

kwako, Mwenyekiti Jones. Hivi mtu

kama wewe unawezaje kuichokoza

familia ya Kimaro? Natumai utakuwa

uko salama na unaendelea vizuri

nitakapokuona tena.”

Wanawake wote walishtuka na kurudi

nyuma mmoja baada ya mwingine.

"Imekuwa muda tangu tulipokutana mara ya mwisho, Madam Ngololo."

Muda mfupi baadaye, kundi la wanawake lilitoa visingizio na kuondoka mahali hapo mara moja. Hawakuwa

tayari kukaribiana na mtu aliyeiudhi familia ya Kimaro. Tukio hilo halikuwa la mzaha. Walijua kuwa kwa kuwa Lisa

alikuwa ameichokoza familia ya Kimaro, alikuwa amejihukumu kifo. Ingekuwa haina maana kumsogelea.

Bila kujisumbua kuliweka wazi jambo

hilo, Lisa alimkazia macho Janet kana

kwamba ni mlemavu wa akili.

Ikizingatiwa kuwa alikuwa na uhusiano wa kirafiki na Lina, kwa nini Lina

hakumwambia ukweli?

"Halo, mume wangu ananiita."

"Lazima uwe na hofu, sawa? Pengine hukutarajia kwamba utapoteza nafasi ya mwenyekiti wakati ndio kwanza umeanza kuifurahia.” Janet alitabasamu kwa kuridhika kisha akageuka kumtazama Alvin. "Bwana. Kimaro, nakushauri ujiepushe naye ili usije ukaingizwa kwenye matatizo haya.”

Alvin alimwangalia tu bila kujali

alichosema. Janet alifikiri kwamba

maneno yake yalikuwa yameamsha

kupendezwa kwake, hivyo mara moja akasema, “Msaidizi mkuu wa Willie ni jamaa yangu. Ukija na kuniomba msaada, hakika nitakuunganisha naye.”

Kwa namna fulani, Lisa alihisi kucheka.

Hata Willie alimuogopa sana Alvin. Kwa

wazi, msaidizi maskini asingekuwa na maana yoyote kwake.

mbele huku akimshika mkono Alvin. Hakuwa

hata na muda wa kupoteza kumwambia Janet ukweli.

Akiwatazama wanaondoka, Janet alicheka nyuma yao. Aliweza kuwa ameridhika kwa muda huo, lakini kile

ambacho kingefuata kingemwacha akilia baadaye.

Mara baada ya kuketi, Alvin alimtazama

mwanamke aliyekuwa kando yake kwa namna ya kinyonge. “Kwanini

usingelifafanua sasa hivi hilo jambo lako? Au lina uhusiano wowote na madai yako kwamba yajayo yanafurahisha?”

"Unanielewa vizuri, Alvilisa." Lisa alitabasamu.

“Alvlisa, mpuuze tu huyu kichaa. Hebu tutafute nafasi tukae.” Alisonga

Alvin aligundua kuwa tangu Lisa awe

mwenyekiti, alikuwa na ujuzi zaidi wa kucheza na wengine. Baada ya kusema

hivyo, halikuwa jambo baya hata

kidogo. Ilibidi awe mwovu na mkatili

zaidi ili ahitimu kuwa mke wake katika siku za mbeleni.

Mnada ulianza muda mfupi baadaye.

Kwa kweli, mnada wa usiku huo ulikuwa tukio la kuchangisha harambee fulani.

Lisa aliinua kadi yake ya zabuni kwa picha mbili za uchoraji zenye thamani

ya shilingi milioni kadhaa. Bidhaa ya mwisho ilikuwa 'Mkufu wa Malkia'.

Ulikuwa ni mkufu unaometa na kishaufu

cha almasi ya rubi inayong'aa ukiwa

umeketi juu ya satin nyeusi. Mkufu huo

uliundwa kwa ustadi. Hata mnyororo

huo ulipambwa kwa almasi ndogo, ambayo ilifanana na safu ya nyota.

Wanawake wote walishangaa kuuona ule mkufu, na pia ulikuwa umemvutia Lisa. Alvin alimtazama Lisa kwa macho ya kina. Kwa wakati huo, mwendesha mnada alianzisha kwa shauku, "Sasa ni wakati wa kuvutia zaidi. Hapo awali, mfalme wa zamani wa nchi fulani alipata

mbunifu mzuri zaidi wa kuunda mkufu, na ilimchukua miaka miwili

kuukamilisha. Kito hiki kina karati 383.4 za almasi. Kuna uvumi kwamba ikiwa

mtu atampa mwanamke wake mpendwa Mkufu huu wa Malkia, watakuwa

pamoja milele. Huu ndio mkufu ambao kila mwanamke anauota. Zabuni ya

kuanzia kwa bidhaa hii usiku wa leo ni shilingi bilioni 1.6.”

Bei hiyo ya ajabu ilizua taharuki

ukumbini. Hata hivyo, upesi mtu fulani

akapaza sauti na kusema, “bilioni 1.7.”

Kwa udadisi, Lisa alitazama upande ule, na kugundua kuwa alikuwa ni Ethan.

Sura ya 128

Kila mtu alianza kumzungumzia Ethan.

“Ni Ethan kutoka Lowe Corporation. Ni mkarimu kiasi gani kwake.”

"Nilisikia kwamba yuko kwenye uhusiano na yule mwanadada kutoka katika familia tajiri ya Laizer, yule tajiri wa Tanzanite."

“Naona. Familia ya Laizer ni maarufu sana huko Mererani. Bwana Laizer ameopoa mawe ya thamani ya bilioni sana juzijuzi tu, atakuwa na pesa sana.”

“Hasa. Lakini mwenyekiti wa sasa wa Mawenzi Investments, Lisa Jones, alikuwa ni mpenzi wake wa zamani.”

“Mpenzi wa Lisa wa sasa hana kitu, yeye ni wakili tu. Nadhani hawezi kumudu kumnunulia mpenzi wake mkufu huu wa gharama.”

Wakiwa wameingia kwenye tmajibizano ya kidaku, ghafla umati wa watu

ukahamishia macho yao kwa Lisa. Lisa hakutarajia kwamba angehusika katika

mazungumzo hayo. Haraka alimshika

Alvin na kusema kwa sauti ya chini, “Usijisumbue kuhusu yale ambayo wengine wanasema. Maoni ni kama mapambo tu. Kimsingi, hayana faida yoyote isipokuwa kwa kuvutia pongezi kutoka kwa wengine. Ni kama vitu vya mitumba ambavyo havifai kuvitumia."

Alvin alimtazama Lisa kwa umakini.

Kwa kweli aliona kuvutiwa kwake na

Mkufu wa Malkia kupitia macho yake.

Alifikiri kwamba angemwomba

amnunulie, akizingatia kwamba alikuwa

amejua kuhusu utambulisho wake

kwamba alikuwa tajiri mkubwa kutoka

familia maarufu ya Kimaro. Kinyume na matarajio yake yote, itikio lake lilikuja

kama mshangao. Haishangazi kwamba

walisema mwanamke atasaidia kuokoa

pesa za mwanamume ikiwa kweli

alikuwa akimpenda. Alikunja mdomo

wake kuwa tabasamu la kupendeza, akainua kasia yake ya zabuni na kusema kwa sauti ya kiume na ya kiburi, "bilioni 2.5."

Akiwa ameduwaa, Lisa alihisi kana

kwamba kichwa chake kilikuwa

kinamlipuka. “Umerukwa na akili?

Nilikuambia usiweke dau lolote.”

"Bilioni 2.6." Janet, ambaye alikuwa

karibu, ghafla aliinua kasia yake ya zabuni.

Lisa alimshika mkono Alvin. “Acha

kuinua kasia yako. Hakika hawezi

kumudu. Anapandisha bei kwa

makusudi kujionyesha tu ili akuvute na wewe umpandie kwa juu.”

Alvin hakuweza kuwa na wasiwasi juu yake. Alitumia mkono mwingine kuinua kasia yake. "Bilioni tatu." Ukumbi mzima ulikumbwa na ghasia baada ya Alvin

kutaja bei hiyo iliyoonekana kufunga mnada.

Akiwa na shilingi bilioni 2.3 kuwa

kikomo chake, Ethan alimkodolea macho Alvin kwa uchungu. Alvin

alikuwa mkatili kiasi gani! Ethan alikunja ngumi kwa kutoridhishwa kwani si tu

kwamba alishindwa kumpiku Alvin

kumnyakua Lisa, bali pia alishindwa kumpiku kuunyakua ule mkufu.

Tracy aliyekuwa kando ya Ethan alipumua kwa husuda. “Sawa, inatosha.

Mkufu wa thamani ya bilioni tatu si wa mchezo hata kidogo."

“Ndiyo.” Ethan alitazama chini, akivumilia maumivu yake ndani kabisa.

Tena, Janet aliinua mkono wake ili kupandilia dau. Alvin alitoa macho yake ya ajabu ghafla. “Unaweza kuinua mkono wako na kuropoka bei unayotaka, lakini sitakupandilia tena.

Fikiri kwa makini ikiwa kuna pesa za kutosha mfukoni mwako kabla hujafanya hivyo.”

Mkono wa Janet ukaganda, akasita mara moja. Kwa kweli, alikuwa akijaribu tu kuongeza bei ili kumkomoa Alvin.

Stephen kwa haraka akaondoa kasia

yake na kumwonya kwa hasira, “Usiwe mpuuzi. Ikiwa kweli utatumia mabilioni ya pesa za familia yetu kwenye mkufu tu, niamini, nitakupiga kofi hadi kufa."

Akiwa amekasirika, Janet alinyamaza kimyaa! Lakini, kwa kweli alikuwa na

wivu wa ndani kwa ndani kwa wazo la utayari wa Alvin kutumia shilingi bilioni tatu kwenye mkufu kwa ajili ya Lisa.

“Kaka, mbona Alvin ni tajiri kiasi kwamba anaweza kutumia mabilioni ya shilingi kirahisi rahisi tu? Inawezekana kwamba anatoka kwa familia ya

Kimaro? Inawezekana kuwa ni ndugu yake na Willie Kimaro?”

"Nyamaza. Hiyo haiwezekani." Stephen hakukubaliana naye kabisa. “Sijawahi

kusikia hivyo. Tofauti na yeye, tunahitaji

kiasi kikubwa cha pesa kwa mtiririko wa biashara wa kampuni. Nadhani

anatumia mapato yake ya uanasheria kununua mkufu. Labda anafikiria kuwa

nafasi ya Lisa kama mwenyekiti wa

Mawenzi Investments ni ya kudumu na

kwamba thamani yake itakuwa ya

mamia ya mabilioni ya shilingi. Kwa

hivyo, anajaribu kugusa na kukamata

moyo wake kwa kutumia bilioni hizi tatu.

Kwa bahati mbaya, anashindwa

kutambua kwamba Lisa atapoteza

nafasi hiyo kwa muda mfupi tu.”

Hatimaye kulikucha kwa Janet, lakini alibaki na hasira. “Kaka, si alimkosea

Willie jana? Kwa nini hajamfundisha somo?” Stephen alipigwa na butwaa.

Alipokumbuka kutoweza kumpata msaidizi wa Willie siku hiyo, ghafla

alihisi kuzama. Punde si punde, alihisi kwamba alikuwa akiwaza kupita kiasi.

"Nilisikia Bwana Kimaro aliumia sana jana usiku, kwa hivyo huenda labda

hajapata nafuu."

“Kwa yote ambayo Lisa alimfanyia, hakika hatamwacha salama hadi ahakikishe kuwa amekufa." Janet alitoa tabasamu.

Sura ya 129

Hatimaye, Alvin alipata zabuni ya juu

zaidi ya mkufu huo kwa bei ya shilingi bilioni tatu. Msimamizi wa mnada kwa

tahadhari alimkabidhi Mkufu wa Malkia mbele ya macho ya kila mtu. Alvin

akautoa ule mkufu mwekundu uliokuwa unameremeta kwa umaridadi. Alipoutoa nje, alimwambia Lisa ambaye alikuwa ameduwaa kwa sauti nzito, “Simama.”

Lisa alisimama huku akionekana kuchanganyikiwa. Umbo lake la kuvutia lilionekana katika macho yake angavu na safi.

Midomo maridadi na myembamba ya Alvin ilijikunja na kuachia tabasamu la kupendeza. Akainama kidogo na kuuweka ule mkufu shingoni mwake.

Sauti yake ya kiume, tulivu ilisikika kwa mtetemo wa kupendeza. "Kuanzia leo na kuendelea, utakuwa malkia wangu."

“Wow!” Mwanamke mmoja kando yake alishtuka kwa mshangao.

Moyo wa Lisa ulikuwa unadunda.

Ijapokuwa bei ya mkufu huo iliufanya

moyo wake kumuuma sana kiasi cha

kuvuja damu, tukio hilo lilikuwa limegeuza mnada kuwa harusi yao.

Mwanaume huyo alikuwa ametimiza matakwa yake yote.

Kilichomshangaza zaidi Lisa ni tabia ya kimapenzi ya Alvin. Ule mkufu

mwekundu wa almasi uliokuwa umeketi

kwenye ngozi yake ya chokoleti ulikuwa unameremeta. Ulimfanya aonekane

kama malkia wa heshima. “Asante.

Nakupenda sana Alvilisa." Lisa

alisimama kwa vidole vyake na kumbusu mdomoni hadharani. Ilikuwa ni denda zito haswa la karibia dakika

nzima.

Baada ya busu, uso wake mzuri na wa

kuvutia ulianza kuona haya kwa sababu

aligundua kuwa watu wengi walikuwa

wakimtazama. Macho ya Alvin

yalimtoka kwa huzuni licha ya kuwa na

furaha kubwa moyoni. Hakika, mwanamke wake alikuwa akivutia zaidi

na zaidi. Alihisi hamu ya kuendelea kumbusu hadharani.

Ethan alitazama pembeni huku

akionyesha huzuni. Ilionekana kana

kwamba moyo wake ulikuwa

umepasuliwa kwa uchungu. Hapo awali

Lisa alipomwambia kuwa

amemwangukia Alvin, hakuamini

kabisa. Lakini hatimaye aliamini sasa.

Hakika, mwanamke aliyekuwa

akimchukulia kama mpenzi wake wa

pekee sasa alikuwa amempenda mtu

mwingine. Mtu huyo alikuwa bora zaidi

na mzuri kuliko yeye. Akiwa amejawa

na majuto, Ethan hakutaka kuendelea

kubaki mahali hapo hata kwa muda.

Aligeuka na kuwa karibu kuondoka.

Lakini kabla hajaondoka, skrini kubwa

ya video iliyokuwa jukwaani iliangaza

ghafla. Kila mtu alifikiri kwamba ilikuwa ni shughuli ambayo mratibu wa mnada alikuwa ametayarisha. Hata hivyo, wote walishangazwa na tukio hilo la ajabu kabisa. Sauti tofauti kabisa zilisikika upesi kutoka kwenye spika.

“Huogopi kwamba Stephen atajua kuhusu hili? Eeh?.”

"Tayari anajua, na hatajali. Yeye ndiye aliyenitaka nilale na wewe leo.”

“Haah! Unasema kweli?. Kama ni kweli basi nashukuru kwa heshima yake ya kunipatia mwanamke wake."

Mazungumzo ya kushtua yalisikika

katika ukumbi huo. Uso wa mwanamume ulikuwa umefichika, ilhali

uso wa mwanamke ulionekana wazi

kwa umma. Kwa kushangaza, alikuwa

Lina, msichana kutoka kwa familia ya

Jones Masawe, tajiri ambaye amekuwa

akinyemelea kiti cha Lisa kwa gharama

yoyote. Stephen hata alikuwa ameambatana naye na kujionyesha hadharani wakati

wa kuhudhuria hafla fulani na shughuli za kijamii siku za karibuni. Kwa hivyo, kila mtu tayari alijua kuwa Lina alikuwa mpenzi wa Stephen. Kilichoshtua kila

mtu zaidi ni kwamba Stephen

hakusalitiwa kuhusu jambo hili. Kweli

alipanga mpenzi wake alale na mwanaume mwingine.

Ilitisha sana! Mnada wa usiku huo

ulihudhuriwa na wanawake wengi

matajiri. Walimtazama Stephen kwa

dharau na karaha. Hali hiyo ilimfanya

Stephen aingiwe na hofu ya upofu.

Kamwe katika ndoto zake mbaya zaidi

hakufikiria kwamba kuna mtu

angethubutu kucheza video ya Willie na

Lina wakiwa wamelala pamoja. Nani

alifanya hivyo?! "Zima skrini! Zima

sasa!” Alinguruma kwa hasira. Lakini, hakuna mtu aliyemsikiliza. Kila mtu alikuwa akipiga porojo tu huku

wakitazama tamthilia hiyo ikiendelea.

“Mtu wa aina hii anatisha kweli. Kwa kweli alimtuma mpenzi wake kwa mwanamume mwingine kwa ajili ya kutimiza lengo lake.”

"Kwa bahati nzuri, sikukubali wakati familia ya Kileo ilipotaka kuwa na uchumba na binti yangu."

“Ndiyo. Haendani kabisa na mambo anayoyafanya. Ni bora nikae mbali na familia ya Kileo siku zijazo.”

"Huenda pia anamtumaga Janet kulala na wanaume, si ndiyo tabia yake?"

“Hilo linawezekana. Hapo awali nilikuwa

na hisia kwa Janet, lakini nitasahau tu juu yake. Sitaki kusalitiwa bure.”

Mbele ya shutuma za umma, Janet

alikasirika sana hivi kwamba alipiga kelele, “Nani alifanya hivi? Haina

uhusiano wowote na mimi!” Janet na Stephen, ambao mwanzoni walijisikia

fahari, walikuwa na aibu sana wakati huo.

Ethan alipokuwa anajiandaa kuondoka, uso wake mzuri ulibadilika rangi. Alifikiri

kwamba tayari alikuwa anajua rangi

halisi za Lina. Hakujua kuwa alikuwa anachukiza zaidi kuliko vile alivyofikiria kuwa. Hakujua hata Lina kweli alikuwa na wanaume wangapi. Mara tu

alipokumbuka kuwa alikuwa kwenye

uhusiano naye hapo awali, alihisi hamu

ya kutapika. Ethan alikuwa

amezungukwa na wageni waliokuwa

pembeni yake waliokuwa wakitazama

tamthilia hiyo. Wakaanza kumsema

waziwazi. "Nilisikia kwamba Ethan alimtosa Lisa kwa ajili ya Lina wakati huo."

"Pengine alivutwa na matumizi ya Lina ya mbinu za hila. Sikutarajia Bwana

Lowe kupendezwa na aina hii ya mwanamke.”

“Hasa. Lina ni mshenzi sana.

Ninashangaa kama Bwana Lowe pia

alikuwa akifanya uchafu wa aina hii na Lina wakati huo."

Akiwa mpenzi wake, Tracy hakuweza

kustahimili maoni hayo, kwa hiyo

aligeuka na kuondoka. Hakuweza

kueleza maumivu yake kwa kutumia

maneno, Ethan alimfuata haraka. Kabla

hajaondoka, alimuona Lisa akimtazama

kwa huruma na kejeli. Kwa wakati huo,

alionekana kuelewa kila kitu. Pengine hii

ndiyo ilikuwa adhabu na masaibu ya

mwisho ambayo alimletea. Alikuwa amefaulu. Kuanzia wakati huu na

kuendelea, angehisi kutapika kila alipomfikiria Lina.

Ni njia nzuri kabisa aliyotumia kuua ndege watatu kwa jiwe moja.

Lisa aliridhika kabisa na matokeo.

Tabia ya Lina isiyo na aibu iliwekwa wazi kwa watu wote wenye nguvu huko

Masaki. Ilikuwa nzuri kwake kwa vile

alifurahia ujasiri wa kutongoza

wanaume. Hakuna mwanamume mmoja ambaye angekuwa na ujasiri wa kutosha kumuoa katika siku zijazo.

“Umemaliza kuitazama?” Akiwa

amekunja sura yake sawasawa, Alvin

alizungumza kwenye sikio la Lisa.

Alifunika macho yake na kusema kwa

sauti ya hasira nzito, "Hivi ndivyo

ulivyomaanisha ulivyosema kuwa

yajayo yanafurahisha? Nilikuonya jana

usiku usiangalie miili ya wanaume

wengine isipokuwa wangu tu.”

Hali ya huzuni ilimfunika Lisa na kumfanya ashtuke. Kisha akapigwa na wazo. “Sikuikagua. Shani ndiye aliyefanya hivyo."

“Unadhani nitakubali uongo wako?

Unapima IQ yangu?" Alvin alicheka. Lisa alishindwa cha kusema.

"Nitashughulika na wewe tukirudi nyumbani," Alvin alimuonya vikali.

Muda mfupi baadaye, mratibu wa mnada alizima skrini mara tu alipopata fahamu zake. Hata hivyo, karibu video nzima ilikuwa imechezwa. Ilikuwa

imeharibu sifa za Lina na Stephen kabisa. Lisa akiwa ameridhika, akatembea hadi kwenye maegesho ya magari akiwa na Alvin.

nyuma yao

Sura ya 130

Stephen na Janet Kileo waliwakimbilia wakiwa wamefura. Uso wa Stephen

ulijawa na hasira kali. Hakutaka kitu zaidi ya kumnyonga Lisa akiwa hai.

Alvin alimvuta Lisa nyuma yake, umbo lake refu na kubwa likitoa ulinzi wa

nguvu kwa Lisa.

"Lisa Jones, wewe ndiye ulicheza ile video?" Stephen alifoka kwa hasira.

“Sawa, umenikera mno. Ikiwa sitakuua, basi jina langu si Stephen Kileo.”

Janet naye alisema kwa msisimko, “Unajua umemkosea nani? Huyo ndiye

Willie Kimaro! Hata kama umemficha uso, hatakuacha kwa kuwa

umesambaza video zake kama hizi.”

“Simama hapo!” Sauti ya ukali ikasikika

Lisa aliinua macho yake na kutabasamu

kwa dharau. “Umewahi kujiuliza hii video imetoka wapi na ni nani aliyenipa?

Au ulifikiri ningethubutu kurekodi kitu kwenye chumba cha Willie Kimaro?”

Stephen na Janet wote walikua hoi kwa wakati mmoja. Muda mfupi baadaye, Stephen akatikisa kichwa. "Hiyo haiwezekani. Video hii huwezi kuwa ulipewa na Wiliie Kimaro. Ulimkosea jana usiku, kwa hiyo tayari anakuchukia. Umepata mtu wa kudukua simu ya

Bwana Kimaro? Sawa, wewe ndiye uliyeanzisha hii. Nitampigia msaidizi wa Willie sasa hivi. Msaidizi wake ni rafiki yangu wa karibu sana.”

"Endelea kuota. Huenda hujui kuwa

Willie Kimaro aliondoka Dar asubuhi ya leo.” Lisa alitabasamu kwa uso

uliolegea. “Hivi mpenzi wako mzuri

hakukuambia? Asubuhi ya leo, Willie

alikuja Mawenzi Investments na kusema

kwamba hatafuatilia suala la jana usiku

tena. Willie pia alimdhalilisha sana Jones na binti yake. Sasa, kila mtu

katika kampuni anajua Lina Jones alipanda kitanda cha mwanamume mwingine kutafuta kufadhiliwa. Wale wawili baba na binti yake hawana hadhi tena ya kuja kwenye kampuni."

“Usijaribu kunidanganya. Hakuna kitu kama hicho." Stephen hakumwamini hata kidogo. Alipiga moja kwa moja nambari ya msaidizi wa Willie Kimaro.

Baada ya muda mrefu, simu

iliunganishwa na sauti iliyolaaniwa kutoka upande wa pili, “Stephen Kileo, unawezaje kuthubutu kuwasiliana nami?! Umeniharibia! Hata nilipoteza

kazi yangu.”

"Nini kimetokea?" Stephen aliuliza kwa sauti ya kuchanganyikiwa.

"Sijui. Vyovyote iwavyo, Lina Jones na wewe, nyinyi wawili ni mashetwain kabisa, mmemkasirisha sana Bwana

Kimaro. Tayari amerejea Nairobi bila kupenda.” Simu ilikatwa kwa haraka. Stephen aliganda kama sanamu ya mbao. Alimtazama Lisa ambaye alikuwa akitabasamu na ghafla akahisi damu

yake ikishindwa kutembea kwenye mishipa. "Ulifanya nini kwa Bwana

Kimaro?"

“Sina haja ya kujieleza kwa mtu kama wewe. Stephen Kileo, sikutaka

kushughulika nawe, lakini ni kosa lako

kumtambulisha Lina kwa Willie. Sasa, sifa yako imeharibika, na nadhani sio

watu wengi watathubutu kuwasiliana na

familia ya Kileo kwa ushirikiano katika

siku zijazo. Unaweza kuendelea na

ndoto ikiwa bado unataka kuoa mke

kutoka katika familia yenye hadhi sawa na yako.” Lisa akamaliza hotuba yake

na kuondoka zake kwa furaha huku

akimshika mkono Alvin aliyekuwa

kakasirika sana hadi kushindwa

kuongea. Janet aliyebaki nyuma alishika kichwa na kupiga kelele. "Stephen, haya

mambo yametokeaje?" 'Yote ni kwa sababu ya ujinga wa Lina. Yule mjinga hata hajitambui kabisa.”

Stephen aliitoa hasira yake. "Sitamsamehe Lina kamwe. Naelekea nyumbani.”

Gari lilikuwa kimya, hewa ya wasiwasi ilitanda kila kona. Alvin akaminya

midomo yake myembamba, umbo lake

maridadi lkionekana kutulia kama

sanamu. Lisa alimtazama kwa siri huku

akijaribu kumwongelesha bila mafanikio.

“Bado una hasira? Kwa kweli

nililazimika kukabiliana na Lina wakati

huu. Nilitamani kutapika kila

nilipoutazama mwili wa Willie Kimaro. Sasa, ninachotaka ni kwenda nyumbani na kuutazama mwili wako mzuri ili niweze kuosha macho yangu…”

“Sasa ndiyo unataka kunitazama?” Alvin ghafla alimkazia macho. Lisa akaguna na kukubali kwa kichwa.

"Sawa, nitakuruhusu uangalie usiku kucha." Alvin alikubali ghafla. Lisa alipigwa na butwaa na kukosa la kusema. Alvin alikunja uso na kumuonya tena. "Ikiwa hii itatokea tena ..." “Haitatokea tena,” Lisa aliapa, "Ikiwa itatokea, Mungu na aniadhibu nisiuone tena mwili mkamilifu wa Alvilisa

maishani mwangu."

"Nyamaza." Alvin alicheka. “Hiyo video bado ipo kwenye simu yako? Nitafuta

kila kitu kwenye simu yako tukifika

nyumbani. Willie Kimaro ni mchafu sana kijana yule, sijui tabia hiyo kaitoa wapi!"

"Nakubali. Ingawa nimeona kidogo tu, sijisikii vizuri hata kidogo.” Lisa alijifanya kuchukizwa. "Alvilisa, najua huna tabia mbovu kama hii, si ndiyo?"

“Utaijua tu tabia yangu, ikiwa ni nzuri ama mabaya.” Alvin alijibu akicheka.

Baada ya kurudi nyumbani, Lisa alivua

Mkufu wa Malkia wa almasi kwa

uangalifu baada ya kukaa chini ya taa ya mezani na kuuangalia kwa upendo.

“Ni mzuri sana. Hakuna dosari hata kidogo.”

"Nakumbuka ulisema haupendi vito vya mapambo." Alvin alitembea nyuma yake na kumtania, "Hata ulisema ni mtumba tu."

Lisa aliona haya na kusema kwa

kigugumizi, “Mimi… nadhani ni ghali sana. Ni shilingi bilioni tatu. Itachukua muda gani kupata kiasi hicho cha pesa?" "Ethan Lowe alikuwa tayari kutoa bilioni mbili kwa ajili ya mwanamke wake, kwa nini nijali kuhusu kiasi hiki?" Alvin alicheka kwa unyenyekevu. "Kwangu mimi, pesa haijalishi. Muhimu ni kwamba unaupenda."

Lisa akapepesa macho, mara akaelewa kuwa alikuwa akijaribu kushindana na Ethan. Hata hivyo, hiyo haikujalisha. Kadiri alivyokuwa akipambana na Ethan ndivyo ilivyokuwa ikionyesha kuwa anamjali.

“Alvilisa, Ethan kwa kweli hana

uhusiano wowote nami. Mimi pia

simpendi tena. Ninayempenda ni

wewe." Aligeuka na kumkumbatia shingo na kumbusu usoni.

Moyo wake uliuma. Hapo awali, ingawa alipata pesa nyingi, hata hivyo

ilionekana kama hazina faida yoyote. Sasa, ilionekana kana kwamba alikuwa

amepata maana ya kupata pesa.

Midomo yake myembamba ilijikunja

huku akimpa sura isiyoeleweka. "Ni hayo tu?"

Lisa alionekana kujua alichokuwa akiongea na kuinamisha kichwa chini.

Alvin alicheka na kumnyanyua. "Si ulisema unataka kunitazama?"

“Hapana…” Uso wa Lisa ukageuka kwa woga. Alikuwa ni hodari wa kusema

maneno makubwa, lakini ndani alikuwa ni mwoga kuyatekeleza.

"Kwa hiyo ulikuwa unanidanganya si ndiyo?" Alvin akakisugua kidevu chake

taratibu. Sauti yake ilisikika kana

kwamba ni sauti ya simba.

Mapigo ya moyo ya Lisa yalimuenda kasi, akazidi kuogopa. Alimsukuma kwa

haraka. “Si ulisema hukula chakula cha kutosha wakati wa chakula cha jioni?

Nitakwenda kukupikia.” Harakaharaka akamtoroka na kutoa tabasamu la hovyo chini ya macho ya Alvin.

Alvin alipotoka kuoga, Lisa alikuwa

amepika chakula chenye harufu nzuri na kumtengea. Hakuwa amekula

chakula cha jioni kilichopikwa na Lisa kwa muda mrefu na mara moja

akakichukua ili kukionja. Kilikuwa ni chakula cha kawaida tu, lakini hakujua

jinsi Lisa alivyokipika maana ladha

ilikuwa ya kipekee sana kila wakati. Lisa

alimsaidia kukausha nywele zake

zilizolowa maji huku akimwangalia akila

chakula kile kitamu.

“Upishi wangu bila shaka ni mtamu sana, lakini ulisema hukuupenda nilipokutengenezea mara ya kwanza. Wewe ni mnafiki sana, lakini wewe pia unajua kunipenda sana.”

Alvin aliona aibu. Ilikuwa ni kidogo sana

kwa mwanamume kuelezewa kama mnafiki. Alimvuta kwenye mapaja yake

na kuonyesha kutofurahishwa.

“Unamwita nani mnafiki mkubwa? Hebu

thubutu kusema tena?”

“Nakuzungumzia wewe. Bado unakataa kukiri… Mmh…”

Kabla Lisa hajamalizia, busu la kutawala la Alvin likaanguka kwenye midomo yake. Alimbusu bila kupumua, na hatimaye alipomwacha, alimwambia

akiwa amemshika mabegani

"Ukithubutu kusema tena nakuongeza zaidi ya hili..."

alirudia tena huku akicheka. Inaonekana

alikuwa amefanya kamchezo fulani ka makusudi.

Alvin akamkamata tena na kumpa busu. Wakati huu, alipigwa busu kali zaidi.

Mikono yake mikubwa ilimkumbatia kwa nguvu kumzuia asikwepe. Lisa alikuwa

na hasira na furaha kwa wakati mmoja.

Alvin alikuwa jabari kupita kiasi na

hakuruhusu mtu yeyote kuzungumza kwa utani juu yake.

Punde, Lisa alianza kulegea na

kuzidiwa na hisia, Alvin alimbeba hadi kitandani. Alvin alikuwa amevaa bukta

nyepesi tu alipotoka kuoga. Aliivua na

kumtazama Lisa na kusema kwa sauti

ya unyonge, “si ulisema unataka

kunikodolea macho ili kuosha macho yako? Unaweza kuanza sasa.”

“Wewe ni mnafiki, kwani uongo…” Lisa

Uso wa Lisa uliwaka moto. Hakuwahi

kufikiria kwamba Alvin angekumbuka jambo lile tena.

Umbo lake lilikuwa zuri sana. Hakuwa

na misuli kupita kiasi bali mtanashati na mwenye nguvu. Zaidi ya hayo, alikuwa

ametoka tu kuoga, hivyo harufu yake ya kiume na harufu ya gel ya kuogea

ilimfanya apate hisia nzuri za utamu.

Sur ya 131

Nywele za Alvin zilikuwa zimekaushwa tu na kuachwa zikiwa zimevurugika kwa fujo. Kwenye uso wake mzuri, kulikuwa na hisia zisizo na kikomo za kimapenzi zikitoka kwenye mwili wake wote.

Lisa alimtazama kwa shauku. Wakati

huo, alitaka sana kumshukuru Pamela.

Ni kosa alilofanya Pamela la

kumchanganya Alvin na Kelvin, mjomba

wake Ethan, ndilo lililompeleka Lisa

kwake. Alikuwa amemsaidia mara kwa

mara. Ni yeye pia aliyemfanya awe na ujasiri wa kuishi licha masaibu yote

aliyokutana nayo.

Usiku huo, alimpatia Mkufu wa Malkia, kwa gharama ambayo ilimfanya kuwa

mwanamke tajiri na aliyevutia kuliko wote Masaki nzima.

“Alvilisa…” Lisa alinyanyuka na kushika

shingo yake. Uso wake wa ajabu uliangaza kwa aibu. "Tunaweza ... tujaribu?"

Alikuwa ameamua. Bila kujali kama

familia ya Kimaro ingemkubali au la katika siku zijazo, alitaka kumpa Alvin

kitu cha thamani zaidi alichostahili.

Alvin aliganda! Yeye alikuwa sugu kwa

mambo hayo siku nyingi, na alikuwa

hajaenda mbali zaidi pia. Mbona Lisa

alikuwa ameamua ghafla…?! Au ni kwa

sababu alijua utambulisho wake halisi?

“Kwa nini?” Macho yake mazito yalimtazama kana kwamba alitaka kuona kupitia kwake.

Lisa alikuwa amefunikwa na aibu na hakuona sura yake ya kushangaza.

Alikuwa ameuzika uso wake mdogo katika kifua chake. “Kwa sababu

nakupenda. Sijawahi kuwa na uhakika wa hisia zangu kama nilivyo sasa.” Lisa

alijibu kwa aibu.

Alvin alisugua nywele zake laini na ndefu juu ya kichwa chake kwa udadisi.

Hakuridhika na jibu lile. Kulikuwa na wanawake wengi sana waliomzunguka ambao walitaka sana kumrukia kwa

sababu tu walijua utambulisho wake halisi, kwamba yeye ni mwanamume tajiri.

haongei wala hafanyi chochote na akaona aibu. “Usinielewe vibaya, ni moyo tu ndiyo umenituma, sina nia ya kukujaribu na wala sikulazimishi. Kama hutaki basi tuache…” Alimsukuma na kukaribia kuinuka, lakini mwili wa Alvin haukumruhusu kunyanyuka.

"Ikiwa utanishinikiza kwa njia hiyo, basi nitakubali kwa kusita," Alvin alisema kwa sauti.

Lisa alimtazama kwa hasira. “Si lazima ufanye kwa kusitasita. Sikulazimishi na sijali hata hivyo…” Kabla hajamaliza, Alvin akambusu. Wakati huo, alielewa.

Haijalishi alikuwa akifikiria nini, ni kweli alimtaka! Zaidi ya hayo, alikuwa amekiri

kwake muda mrefu uliopita. Hakukuwa na haja ya kutilia shaka kwamba alimpenda.

“Kwa nini? Je!… hutaki?” Lisa aliona

Dakika chache baadaye, aliufunga

mlango kwa nguvu na kwenda bafuni kuoga tena. Lisa alifoka kwa hasira ya kuachwa akiwa ‘ameiva’.

Dakika 20 baadaye, Alvin alitoka kuoga akiwa na sura tofauti. Hakumgusa tena Lisa wala kuwambia kitu chochote.

Moyo wa Lisa uliumia alipofikiria juu yake.

‘Sitathubutu kumwambia katika siku zijazo.’ Alijiapiza kimoyomoyo kwa unyonge. Alikumbatia shingo yake na kuuzika uso wake kifuani mwake.

Alikuwa na haya sana hivi kwamba hakuweza kuongea tenakwa muda mrefu. "Potezea tu kwa leo. Utakuwa

mwanamke wangu mapema au baadaye." Sauti ya Alvin

alipomkumbatia ilikuwa ya kutetemesha sana.

Wawili hao walipolala, hawakujua kwamba habari kuhusu tukio la hisani

usiku huo zilikuwa zimeenea mitandaoni. Kila mtu alijua kuhusu hilo.

Wakati huo, katika makazi ya Jones

Masawe, Jones kwa mara nyingine tena

alipokea simu kutoka kwa wadaku.

“Bwana Jones, umeona sura duni ya binti yako? Hehe, nipe basi binti yako

alale nami kwa usiku mmoja na nitafanya kazi nawe kwenye mradi."

"Nyamaza!" Mwili wa Jones ulitetemeka

kwa hasira huku akilaani, “Weka kinywa chako ksafi unapoongea na mimi!”

“Hehe, ningewezaje kuwa msafi kuliko

binti yako? Nani angethubutu kutaka

takataka kama hiyo?"

"F*ck off! Usinipigie tena.” Jones

aliivunja simu yake.

Alikuwa ameishi kwa miaka mingi na tayari alitumia nusu ya maisha yake, lakini hakuwahi kufedheheshwa kama ilivyokuwa siku hiyo. Hapo awali, alifikiria kwamba angeipata Mawenzi Investments kwa urahisi, lakini ilienda mbali zaidi na mikono yake. Si hivyo tu, hata alipoteza sifa na heshima yake ya mwisho. Alikasirika sana hivi kwamba alipoteza busara yake. Alichukua ufagio na kwenda juu ili kumpiga Lina.

“Wewe b*tch, yote ni makosa yako! Tangu uliporudi, tulipoteza Kibo Group na sifa yetu. Hata mimi pia nimefedheheshwa katika umri huu.

Mjinga sana wewe!”

"Hapana!" Lina alipiga kelele mara kwa mara na kuendelea kujificha. "Baba, nilifanya hivyo kwa ajili ya familia ya Jones. Ni wewe ulinishauri nimfurahishe Bwana Kimaro.”

"Nilitaka umfurahishe kwa zawadi, sio kulala naye, paka wewe!" Jones alipiga

kelele. Kadiri alivyokuwa akisema

ndivyo hasira zilivyozidi kuongezeka na ndivyo mikono yake ilivyozidi kuwa matata.

“Una kichaa? Ni binti yetu!” Mama

Masawe aliingia ndani na kumsukuma.

Alipoona sura ya Lina iliyochubuka na kupigwa, alilia kwa huzuni.

“Afadhali nisiwe na binti kama yeye!”

Jones alimnyooshea kidole na kumkaripia, “Ningejua kwamba haya yangetokea knisingekurudisha kabisa.

Ikiwa sio wewe kurudi, ningekuwa na ugomvi na Lisa? Ikiwa hukunitia moyo, ningemuua mama yangu kwa mikono

yangu mwenyewe? Isingekuwa wewe

hata Lisa angeingia Mawenzi

Investments angenisikiliza na kuniacha niwe mwenyekiti.”

Lina aligeuka rangi, na mwili wake ukatetemeka huku akijilaumu

mwenyewe.

Mama Masawe hakuweza kumsikiliza

tena. Alimkumbatia Lina kwa nguvu na kupiga kelele, “Inatosha! Ni wazi Lisa

ndiye aliyetulazimisha kufikia hatua hii, lakini bado unamlaumu na kumpiga

Lina. Unataka tu kumalizia hasira yako

kwa kumuonea mtu mwingine."

“Bado una ujasiri wa kusema hivyo?

Binti mzuri uliyemlea mwenyewe hana

haya wala aibu. Ninachojutia zaidi ni kwamba nilikuoa na kumzaa!”

"Sawa, kwa kuwa unajuta, tutaondoka!"

Mama Masawe alilia na kuushika

mkono wa Lina kabla ya kutoka nje.

Muda si muda, nyumba nzima ikawa

tupu na ya kutisha.

Sura ya 132

Jones alitetemeka upepo wa baridi

ulipovuma. Kwa mara ya kwanza, hisia ya majuto ilipanda moyoni mwake.

Ilikuwa wazi kuwa alikuwa na familia

nzuri. Ilivunjikaje kwa muda wa miezi mitatu tu?

Siku iliyofuata, Jones alipokea simu kwamba alikuwa amefukuzwa kutoka

kwenye bodi ya wakurugenzi wa Mawenzi Investments. Alikimbilia

kwenye kampuni hiyo kwa hasira, lakini mlinzi wa mlangoni hakumruhusu kabisa kuingia na kumfukuzia nje. Kwa

kuwa hakuwa na mahali pengine pa kwenda, Jones aliishia kulewa kwenye baa na alirudi tu nyumbani usiku wa

manane.

Usiku huo, kwa ulevi alisukuma mlango

wa nyumba yake kwa unyonge na

hakukuwa na taa ndani, na mwanga wa

mbalamwezi wa baridi ulipenya kupitia

madirishani. Kulikuwa na kiti cha magurudumu katikati ya sebule, na juu

yake aliketi mwanamke mzee mwenye

mgongo ulioinama na nywele

zilizotawanyika. Sura hiyo ilionekana ya kutisha haswa. Jones aliogopa sana hivi

kwamba miguu yake ilidhoofika.

Aligeuka na kujaribu kukimbia. Hata

hivyo, mlango ulifungwa nyuma yake, na sebule ikawa giza.

“Mama…” Jones alipiga magoti chini

kwa woga, akitetemeka kama jani

lililosukumwa na upepo.

“Mwanangu, mbona unaniogopa sana?”

Kiti cha magurudumu kiliteleza mbele

polepole, na sauti ya mwanamke mzee

ikasikika.

Jones alirudi nyuma kwa hofu. “Mama, mama, usije. Tafadhali, si mimi niliyekudhuru. Kuna mtu mbaya."

“Si wewe uliyenidhuru?” Kicheko cha kutisha cha yule kikongwe kilisikika pale

sebuleni. "Ulifanya hivyo kwa ajili ya hisa na pesa. Lakini kwa nini

umenidhuru? Si nilikutunza tangu ujana? Ulimwengu wa kuzimu hautaki

kunikubali kwa sababu mliniondoa kabla ya siku zangu, kwa hivyo imenibidi tu kurudi kukutafuta. Mwana…”

Kiti cha magurudumu kilikuwa kikikaribia zaidi na zaidi. Jones alipiga magoti chini

na kuinama kwa nguvu, machozi na vilio vikimtoka. “Mama, nilikosea. Nilikosea.

Nilianza kuhangaika, lakini sikutaka kukuumiza. Ilikuwa Mama Masawe.

Mama Masawe ndiye alikusogezea mto.

Nenda kwake badala yake.

“Kama hukukubali, angeniua?”

Mwanamke mzee alicheka na kulia

wakati huo huo.

“Mama, samahani.” Jones alibubujikwa na machozi, akijihisi mnyonge. “Nilitiwa moyo na wawili hao, mama na bintiye.

Sikutaka kukukuua, samahani. Tafadhali niache uende…”

"Kwa kuwa unajua kuwa ulikosea, nitakuondoa sasa." Mkono wa mwanamke mzee ulimshika, lakini

Jones aliogopa sana kusogea. Doa lenye unyevunyevu lilimtoka kwenye

‘gongo’ lake huku akijikojolea. Taa ziliwaka ghafla!

Maafisa kadhaa wa polisi walitoka jikoni, na mwanamke mzee kwenye kiti cha magurudumu akavua wigi lake kabla ya kusimama.

Jones alipigwa na butwaa na kutetemeka. “Shangazi Manka…”

"Bwana. Jones, kuna mtu aliripoti

kwamba unashukiwa kumuua Madam

Bibi Masawe. Na wewe mwenyewe

umekiri hapa. Polisi sasa

wanakukamata rasmi.” Afisa huyo akatoa pingu na kumfunga mikono.

“Hapana, hapana…” Jones alijitahidi sana kujificha. “Nilikunywa pombe kupita kiasi. Nilikuwa naongea ujinga tu.”

"Mjomba, nimerekodi kila neno ulilosema." Lisa alitoka na simu. Uso wake ulikuwa umejaa huzuni. “Ulikuwa mwana pekee wa kiume wa bibi. Alikuwa mzuri kwako na alikulea kwa uchungu, lakini mwishowe, ulipanga njama na wengine kumuua. Bado unakumbuka jinsi alivyokufa? Je, huoti ndoto mbaya? Je! dhamiri yako haikuumi?”

“Usiseme tena…” Jones alikuwa tayari

amekunywa pombe nyingi. Sambamba na jinsi alivyokuwa amepatwa na woga, akili yake ilikuwa karibu kuzimia.

Lisa alisema kwa ujeuri, “Tayari nimekusanya ushahidi mwingi. Ikiwa

hutaki kufa gerezani, bora utoe ukweli wako kwa uaminifu.

Vinginevyo, Mama Masawe bila shaka atajaribu kukwepa mashtaka

mahakamani baadaye.”

Jones hakumwamini. “Umekusanya ushahidi gani?”

"Bibi alitibiwa hospitalini, na hospitali ina rekodi zake za matibabu. Daktari

alisema kwamba ingawa bibi alikuwa

amepooza wakati huo, haikuwezekana afe ghafla hivyo. Pia kuna Aunty Helen

ambaye ulimwajiri badala ya Aunty

Manka kumtunza Bibi. Yuko tayari

kufika mahakamani sasa…”

Jones aligeuka rangi. Alijua kwamba

alikuwa katika matatizo.

Kama asingetoa ushahidi muda huo,

basi angeweza kuishia jela wakati

Mama Masawe angesukuma shutuma

hizo kwake. “Sawa, nitakiri. Ilikuwa

Mama Masawe. Alichukua fursa wakati

bibi yako alikuwa amelala na…” Labda

ilikuwa dhamiri yake ya mwisho, lakini

hatimaye Jones alianguka chini na kulia.

Lisa na Aunty Manka nao walilia. Hawakutarajia mwisho wa Madam Bibi

Masawe kuwa mbaya kiasi hicho.

Aunty Manka aliuliza, “Swali la mwisho.

Siku hiyo bibi madam Masawe

alipoanguka kutoka kwenye ngazi, ni Lina ndiye aliyemsukuma?"

Masawe alitikisa kichwa, lakini akifikiria

juu ya utu wa Lina, alihisi kwamba labda

alifanya hivyo. Hata hivyo, alikuwa na

binti mmoja tu na hakutaka aende jela.

"Kwa kweli sijui kuhusu hilo." Jones

Mwishowe, Jones alichukuliwa na polisi

kwa mahojiano. Lisa alitazama jumba la giza nyuma yake. Hapo awali palikuwa

nyumbani kwake, lakini sasa palikuwa mahali ambapo hakutaka tena kukanyaga. Alichukua funguo na kuzitupa kwenye nyasi kabla ya kugeuka na kutoka nje ya mlango.

Gari lao la kifahari lilikuwa limeegeshwa mlangoni. Alvin alikuwa amesimama

huku kaegemea gari. Kulikuwa na mvua kidogo usiku huo, na matone ya mvua

yalitua kwenye kichwa na mabega yake. Lisa alimtazama kwa mahaba, macho yake mazito na safi yalipendeza kama mwanga wa nyota pekee angani.

Wakati huo, Lisa, ambaye hakuwa na

nyumba, alionekana kuwa amepata

nyumba. Aliruka mikononi mwake, na

Alvin akafunua koti lake ili kumfunika

ndani yake.

"Alvlisa, hatimaye nimelipiza kisasi."

Lisa akasonga mikononi mwake. “Lakini sina furaha hata kidogo. Ninajuta

kwamba sikukaa zaidi na Bibi hapo awali. La sivyo, asingekufa vibaya hivyo.”

Machozi ya Lisa yalilowanisha shati kifuani mwa Alvin. Alvin hakujua jinsi ya

kuwafariji wengine. Alimsubiri amalize kulia na huku akimpigapiga tu kichwani.

“Umefanya vizuri usiku wa leo. Hakukuwa na ushahidi wowote bado

uliweza kumfanya Jones Masawe akiri yeye mwenyewe!"

“Nilicheza kamari, kupata ama kukosa.

Nilicheza kamari juu ya ubinadamu

wake. Nilicheza kamari kwenye kile

kilichosalia kwenye hatia na dhamiri ya

Jones. Nilicheza kamari kwamba

angekuwa mbinafsi kiasi cha

kumsingizia Mama Masawe.” Sauti ya

Lisa iliendelea kusikika. "Nilikuwa tayari

nadhani kwamba Jones asingefanya

hivyo mwenyewe. Ili kupunguza adhabu yake, bila shaka angesema kwamba ni Lina au Mama Masawe waliofanya hivyo. Kwa kweli sikutarajia Mama Masawe angekuwa mkatili kiasi hicho.”

“Mama Masawe ana uhakika wa kwenda jela. Twende, usiku umeenda sana.” Alvin alifungua mlango wa gari.

Lisa ghafla akashika mkono wake. Macho yake makubwa meusi

yalitazama ndani yake aliposema, “Alvlisa, nina wewe tu sasa. Utaniacha pia?”

“Sitafanya hivyo.” Alvin akainama na kumbusu kwenye paji la uso huku akiongea kwa upole.

Lisa alifumba macho. Kwa wakati huo, alifikiria kwamba asingemuacha kamwe

maishani mwake. Ni baadaye tu ndipo

alipogundua kwamba walikuwa bado

wachanga sana kwenye mapenzi, na kulikuwa na mambo ambayo

yangebadilika.

•••

Saa tisa usiku, Lina na Mama yake

walikuwa wamelala fofofo kwenye

chumba cha hoteli. Kengele ya mlango ililia ghafla.

"Ni nani huyo?" Mama Masawe

alifungua mlango kwa hasira. Alifikiri

kwamba ni Jones ndiye aliyewafuata kuwafanyia fujo.

Hata hivyo, mara mlango

ulipofunguliwa, kundi la polisi liliingia na kumfunga pingu. “Mama Masawe, unashukiwa kumuua Mzee Madam

Masawe. Upo chini ya ulinzi!”

"Nini?" Mama Masawe alipigwa na

butwaa na kuruka kwa haraka.

"Sikumuua mimi."

“Mumeo tayari ameshatoa maelezo

kamili kituoni. Ni wewe uliyemkaba mama mkwe wako kwa mikono yako

mwenyewe.” Macho ya polisi yalijaa dharau. Mwanamke huyo hata alimuua

mama mkwe wake mwenyewe! Mtu wa aina hii hakuwa na maadili kabisa. Polisi

hawakumpa nafasi ya kujitetea, wakamtoa nje.

“Mama, nini kinaendelea?” Lina

alikurupuka kutoka kitandani na kukimbilia kumshika, lakini polisi

hawakumruhusu kumgusa.

Sura ya 133

Mama Masawe akapaza sauti na kusema, “Baba yako ni mnyama!

Kaenda kunichongea polisi kuwa

nilimuua bibi yako. Lina, lazima ujilinde.”

Mama Masawe alichukuliwa upesi, na

Lina akaanguka chini. Alikuwa

ameteseka kijijini kwa zaidi ya miaka 20, na haikuwa rahisi kwake kuja mjini. Lakini, kabla hata mwaka haujaisha, familia yake ilisambaratika kabisa! Ikiwa kitu kingetokea kwa Jones Masawe na Mama Masawe, angekuwa na sifa gani za kuwa binti mkubwa wa familia ya Jones? Hapana, hapana. Hakutaka kurudi enzi hizo!

Alimpigia simu Stephen Kileo kwa

haraka. “Stephen, nakuomba. Tafadhali nisaidie. Mama na baba yangu

wamekamatwa na polisi. Maadamu utanisaidia, nakuahidi kuwa nitakuwa mkeo. Nitakupa nusu ya hisa za

Mawenzi Investments.”

“Lina Jones, nimeelewa sasa. Bahati

mbaya humwandama yule aliye pamoja

nawe. Kwanza, ilikuwa Ethan Lowe, na

sasa mama na baba yako wanaenda

jela. Sifa yangu pia iliharibiwa kabisa na

wewe. Potea na ukae mbali nami siku

zijazo. Kukuona tu kunanifanya nitamani

kutapika!” Stephen alikata simu moja

kwa moja. Lina alipigwa na butwaa kabisa.

Hakuweza kuelewa. Haikuwa kitambo

kirefu matajiri wote huko Masaki

walikuwa wamemshikilia. Ilikuwa

imechukua muda mfupi tu, na sasa, kila

kitu kilikuwa kimebadilika. Kila kitu

kilikuwa kosa la Lisa Jones! Aliamini ni Lisa aliyemharibia maisha na

kumdumbukiza katika hali hiyo mbaya.

Kwa nini Lisa alikuwa bado yupo hai?!

Moyo wa Lina ulikuwa umejaa wazimu.

Wakati huo alikumbuka kitu kama mtu

aliyeshukiwa na roho mtakatifu na

kufunuliwa jambo. Alikumbuka alikuwa

na picha za Lisa alizopigwa hotelini siku

ambayo Lina alimtengenezea njama za

kubakwa. Ni siku ile ambayo alilaghaiwa

kwenda kuwasilisha michoro yake

hotelini kwa ajili ya mradi wa Mawenzi

aliokuwa akiupigania kuupata, ambapo

kwa bahati nzuri aliokolewa na Kelvin.

Alikumbuka picha hizo zilikuwa kwenye

simu yake. Alipoziona, alishtuka kwanza kabla ya kusisimka mara moja.

Picha hizo zilikuwa za Lisa akiwa karibu

sana na Kelvin Mushi utasema ni wapenzi. Alijua kutoka eneo ambalo

picha zilipigwa kuwa ni wakati wa kumtia Lisa dawa ndani ya chumba cha

hoteli.

Hapo awali, Lina alitaka wanaume fulani

wambake Lisa, lakini Kelvin Mushi

alikuwa amefika kwa wakati. Lakini Lina

alifanikiwa kupata picha za video

zilizomwonyesha Kelvin akiwa kamnyanyua Lisa mikononi mwake.

Hakutarajia kamwe kwamba zingekuwa bado zimo kwenye simu yake.

kukaa na Alvin?” Lina aliwaza kwa

“Haha, kwa picha hizi, Lisa atawezaje

furaha. Sifa yake kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments pia ingeathiriwa. Lina alitafuta haraka nambari ya mwandishi wa udaku!

•••

Saa tatu asubuhi Lisa alipoamka, alikuwa peke yake kitandani. Mvua

ilikuwa imenyesha usiku kucha na alilala usingizi mnono sana. Sasa kwa kuwa

alikwisha lipiza kisasi kwa kifo cha bibi yake na Bibi na Bwana Masawe wote

walikuwa jela, alihisi utulivu na raha kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu.

Pia ilikuwa ni nadra kwake kuamka akiwa amechelewa sana.

Alikaa na kuangalia muda lakini

akagundua kuwa kuna missed call nyingi kwenye simu yake. Nyingine

zilikuwa kutoka ofisini, nyingine kutoka

kwa Kelvin, na hata kulikuwa na missed calls nyingi zaidi kutoka Pamela.

Pamela alikuwa amempigia simu mara

saba au nane.

Haraka alimpigia tena huku akicheka.

“Mbona umenipigia simu mara nyingi sana asubuhi? Kuna kitu kilitokea?"

“Kuna kitu kilikutokea? Inamaana bado hujui?” Sauti ya wasiwasi ya Pamela ilisikika. "Nenda uangalie habari zinazovuma sasa."

Lisa alipigwa na butwaa alipoingia

mtandaoni. Aliona video iliyokuwa inatrend ikiwa na jina lake na Kelvin na kubofya habari ile. Matokeo ya utafutaji yakasomeka, 'Mwenyekiti mrembo wa

Mawenzi Investments afumwa kwenye pozi tata na mpenzi wake' ghafla yalitokea.

Lisa alihisi kuogopa. Alipobofya kwenye

makala hiyo, alipigwa na butwaa kuona

video ya Kelvin Mushi akiwa kambeba

juujuu huku akiwa kamwinamia kama

anambusu shingoni. Chumba kilikuwa na baridi, lakini ghafla alihisi joto sana!

“Unafanyiwa njama?”

Pamela alisema

kwa wasiwasi, "Kwa utu wako, haiwezekani kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mtu mwingine zaidi ya Alvin. Ninakuamini, lakini wengine wanaweza wasikuamini.”

Pamela alikuwa hajamaliza kuongea wakati mlango wa chumba cha kulala

ulifunguliwa kwa nguvu. Alvin aliingia kwa nguvu huku uso wake mzuri ukiwa

umefunikwa na hasira kali. Machoni mwake kulikuwa na sura iliyoonyesha

hakutaka kitu zaidi ya kumrarua vipande vipande. Lisa alikuwa hajamwona akiwa na hasira hivi kwa muda mrefu. Haraka

akakata simu na kumueleza. “Umeona hizo picha? Usielewe vibaya—”

“Kwa hiyo unataka nikupongeze, sivyo?"

Alvin aliikamata simu iliyokuwa

mikononi mwake na kumrushia. Macho

yake ya giza yalifunikwa na tamaa, karaha, na chuki. “Angalia wewe

mwenyewe hizo picha za kuchukiza.

Unadai kuwa humpendi Kelvin Mushi, lakini ulimkumbatia kwa nguvu na hata

kumvua nguo. Lisa Jones, mbona huna haya?” Simu yake iligonga kifua chake kwa

nguvu. Ilimuuma, lakini sio kama moyo wake ulivyouma. Ni wanaume wangapi

wangeweza kutulia ikiwa wangeona picha kama zile? Alikuwa kavurugwa kabisa na hizo picha zake.

“Hapana, nilifanyiwa njama, sema tu sikukuambia ukweli! Usiku huo, Lina Jones alinilazimisha kunywa dawa, na Kelvin Mushi alitokea kwa bahati nzuri

akaniokoa. Hakuna kilichotokea kati yetu." Lisa alitikisa kichwa kwa

masikitiko huku akieleza, “Nilijiloweka kwenye maji baridi usiku kucha.”

"Unanichukulia kama mjinga?" Kicheko

cha kutisha cha kijeuri kilisikika kutoka

kwenye koo la Alvin. “Uliponilisha kwa

hila madawa kama hayo, hata

mwanamume kama mimi nilishindwa

kuvumilia. Ilinibidi niende hospitalini

kuwekewa dripu ili nipate nafuu, lakini

wewe unasema ulishinda kwa

kujiloweka kwenye maji baridi tu?”

“Ninasema ukweli.” Lisa alilazimisha

kujibu malalamiko yake na kujaribu kueleza, “Naweza kuapa—”

"Nyamaza! Lisa Jones, kwa kweli

sitakuelewa!” Alvin ghafla akashika

kidevu chake kwa nguvu. “Unajifanya

kuwa msafi na mtulivu mbele yangu, ukisema kwamba unaogopa… Kumbe ni janja janja yako tu kuendelea

kunifanya mjinga?! Ngoja nikuulize.

Picha hizi zilipigwa lini? Nakumbuka…

nilienda Nairobi kwa siku chache na

Shangazi Linda akasema hukurudi

usiku kucha…”

“Sikufanya hivyo! Hakuna kilichotokea kati yangu na Kelvin, simpendi…” Lisa akatikisa kichwa kwa nguvu.

"Kwa hivyo mawazo yangu yalikuwa

sawa." Alvin hakumsikiliza hata kidogo. Macho yake yalijaa dhihaka na kejeli.

“Nilikupigia simu usiku ule. Simu yako ilikuwa imezimwa usiku kucha. Hah, kumbe ulikuwa na Kelvin Mushi, sivyo?"

Kadri alivyozidi kuongea ndivyo hasira zilivyozidi kumpanda. Ilikuwa ni kama

kuna jeraha kwenye moyo wake, na chumvi iliendelea kupakwa juu yake.

Ilimuuma sana hata akashindwa kupumua. Pamoja na mashaka na shutuma zake, moyo wa Lisa ukazidi kuwa mzito na mzito. Kulikuwa na uaminifu mdogo

sana kati yao. Kwa kweli hakujua jinsi ya kumshawishi. “Kama… Kama

huniamini, unaweza kuangalia

mwenyewe,” Lisa alikunja ngumi na

kusema bila kujielewa.

Alvin alicheka kana kwamba amesikia mzaha. Sauti yake ilijaa dharau

alipozungumza, “Baada ya kutazama hizo picha, kukutazama tu kunanifanya nijisikie mchafu. Sitathubutu kushika mwili wako mchafu. Kumbe ndiyo

maana jana machale yalishika nikaacha.”

Lisa alijeruhiwa sana moyoni mwake.

Jana yake usiku, alijisikia kana kwamba

alikuwa mwanamke mwenye furaha

zaidi duniani, lakini mara tu kulipopambazuka, ilionekana kana

kwamba dunia nzima ilikuwa

imeporomoka. Picha hizo zilitoka wapi?

Alikumbuka kwamba wakati

wanaondoka, Kelvin alisema kwamba

aliivunja kamera. Haraka akapiga

namba ya Kelvin.

Simu ilipounganishwa, sauti ya Kelvin ya wasiwasi ilisikika. “Lisa, tayari nimeshaona kila kitu. Mimi sina neno ila nina wasiwasi na wewe. Alvin atakuelewa kweli? Naweza kumpigia simu ili nimweleweshe?”

Sura ya 134

Hapo awali, Lisa alihisi mashaka kidogo, lakini baada ya kusikia sauti ya

Kelvin, alihisi kwamba alikuwa na mawazo potofu. Kelvin alikuwa muungwana sana. Asingeweza kamwe kueneza picha kama hizo.

“Amekasirika sasa. Ukimpigia simu

utazidi kumkasirisha zaidi.” Lisa alitabasamu kwa uchungu. “Si ulisema siku ile uliharibu kamera? Kwa nini…”

"Niliiharibu. Hata niliiangalia wakati huo hakukuwana picha zozote." Sauti ya

Kelvin ilionyesha jinsi alivyokuwa na

huzuni. "Nadhani kamere zilikuwa

zinahamisha picha wakati zikirekodi. Nilikuwa mzembe. Niligundua kuwa

picha hizo mtandaoni zilisambazwa na ripota baada ya kupewa na Lina.”

Lisa alitabasamu kwa hasira. Alikuwa amemdharau Lina. Picha hizi zilikuwa za uchochezi sana.

“Samahani.” Kelvin aliomba msamaha

tena. “Sijali kwa vile mimi ni mwanaume, lakini itaathiri sana sifa

yako. Ikiwa kuna chochote ninachoweza kukufanyia, nijulishe tu na nitajaribu niwezavyo kukusaidia.”

"Asante. Nina simu kutoka ofisini ninayohitaji kuipokea. Tuongee baadaye.” Lisa haraka akakata simu kwa Kelvin na kupokea simu kutoka kwa msaidizi wake, Tunu.

“Mwenyekiti Jones, njoo ofisini haraka.

Uvumi kuhusu kashfa yako unavuma na laini ya simu ya kampuni inashikiliwa na

waandishi wa habari. Inabidi

ushughulikie jambo hili haraka

iwezekanavyo.”

“Sawa, nitakuja mara moja.” Lisa

hakujali tena na kubadilisha nguo zake haraka kabla ya kushuka.

Alipotoka nje, aligundua kwamba Shani

hakuwepo na hakumfuata tena ili kumlinda. Moyo wake ukaingia giza.

Alvin ndiye alikuwa amepanga Shani

amlinde. Sasa kwa kuwa alitaka

kumuacha, alimfukuza Shani pia.

Baada ya kufikia kwenye kampuni hiyo, waandishi wengi walikuwa

wamesimama mlangoni. Aliingia kutoka

kwenye viwanja vya maegesho.

Alipopanda ghorofani, watendaji kadhaa

walikuwa tayari wakimsubiri ofisini.

"Mwenyekiti Jones, kuna wanamtandao wengi kwenye mtandao wanaokukaripia kwa kuwa... 'wazi' sana…” Paji la uso la

Freddie Ngololo lilijawa na jasho baridi. Tayari alikuwa ametumia neno lenye

ukakasi sana. “Kwa kifupi, hali si nzuri sana na sifa yako kama mwenyekiti wa kampuni naogopa kusema kwamba inaathiri sana.

Uso wa Lisa ambao tayari ulikuwa

umekunjamana ulizidi kuwa mbaya.

Mara nyingi alisoma magazeti ya udaku

mtandaoni na alijua vyema uovu wa watumiaji wa mtandao dhidi ya wanawake katika kashfa kama hizi.

"Je, idara ya PR ina mawazo yoyote?"

Lisa aliuliza huku akikuna kichwa.

Meneja Mkuu Ngololo alisema, “Idara

ilifanya mkutano mapema asubuhi.

Tunafikiri njia bora ni kutangaza rasmi

kuwa wewe na Kelvin Mushi ni wapenzi

ili kushusha joto. Kwa kweli, hata

wafuatiliaji wa habari hii wanasema

Kelvin Mushi na wewe mnaendana sana

na mnalingana vyema katika hali ya kijamii. Hakika utapokea mwitikio

chanya kutoka kwa watu mitandaoni na kashfa hii itageuka kuwa baraka

kwako.”

"Ndiyo…Ndiyo!" Meneja wa idara ya PR alitabasamu haraka na kusema, “Wakati

huo, tunaweza pia kuipandisha hadhi

Mawenzi Investments, Kwa taswira

yako kama mwenyekiti wa bodi, na taswira ya Kelvin Mushi kama

mwenyekiti wa Golden Corporation, mnaweza kuwa mabalozi wazuri wa kampuni.” Watendaji walikubaliana na wazo hili.

Kadiri Lisa alivyozidi kusikiliza ndivyo

alivyozidi kukosa la kusema. "Hapana, tayari nina mpenzi."

Meneja Mkuu Ngololo alianguka kwa aibu. “Sawa… Lakini ulipigwa picha ukiwa na Bwana Mushi. Ukikataa, itakuwa mbaya kwa picha yako, na kila mtu atakudharau kwa kuwa na maisha ya faragha yasiyo na uaminifu. Ikiwa suala hili halitashughulikiwa vyema, sura ya Mawenzi Investments itaathirika pakubwa.”

"Niliwekewa madawa ya kulevya wakati huo. Unaweza kueleza moja kwa moja kwenye tovuti rasmi.” Lisa alisimama na kuwatazama watendaji hao kwa macho makavu. "Hii ni kampuni ya mali isiyohamishika. Maadamu mali zetu zimejengwa kwa ubora mzuri, bado tunaweza kupata nyota zilizo na picha nzuri za kututangaza. Ikiwa kweli

tumeathiriwa, basi haiwezi kusaidia.

Siwezi kumuumiza mpenzi wangu kwa

sababu ya kampuni, kama vile baadhi yenu hamtawaacha wake zenu kwa ajili ya faida. Kila mtu ana msingi wake."

Umati ukanyamaza. Baada ya nusu dakika ya kimya, Meneja Mkuu Ngololo

alitikisa kichwa. "Tutafanya kama Mwenyekiti Jones anavyosema."

Baadaye, ukurasa wa Facebook wa

Mawezni ulichapisha taarifa kwa umma.

[Picha zilipigwa zaidi ya mwezi mmoja

uliopita. Mwenyekiti Jones alifanyiwa njama na kulishwa madawa ya kulevya.

Kwa bahati nzuri, Kelvin Mushi

alionekana kwa wakati na kumuokoa

Mwenyekiti Jones, lakini hakuna

kilichotokea kati ya pande hizo mbili.

Wawili hao bado ni marafiki wa karibu

sasa. Tunatumai kila mtu ataelewa na ataacha kujadili suala hilo.]

Kisha, Kelvin binafsi ali’share chapisho hilo. [Wakati huo, Mwenyekiti Jones alikuwa

ameleweshwa dawa za kulevya, lakini

aliokolewa haraka na kulowekwa

kwenye bafu baridi. Ni mwanamke

mwenye heshima sana. Natumai kuwa

watu hawatamwelewa vibaya na kumtusi kwa sababu ya picha chache.]

Baada ya chapisho kupakiwa, athari

ilikuwa nzuri ya kushangaza.

Watu wengi walimsifu Kelvin kwa kuwa

mungwana na msikivu, na Lisa kwa

kuwa hodari na jasiri. Baadhi ya watu

hata waliwashauri na kuwaambia wawe

wapenzi badala ya marafiki. Walisema

walikuwa ni kapo zinazofaa zaidi katika ulimwengu wa biashara.

Katika kampuni ya sheria, Jennings

Sollicitors, Ofisi ilionekana kuwa na giza la ukiwa. Alvin alikuwa amekaa siku

nzima kwenye simu yake. Asubuhi, kila

mtu alimkemea Lisa, lakini upepo

ulibadilika ghafla mchana. Kila mtu

alipiga kelele kwa Lisa kuungana na Kelvin.

•••

Aliibomoa simu yake pale pale kwa hasira. "Hivi watu kwenye mtandao siku

hizi hawana kitu cha maana cha kufanya? Eti hawa wawili wanaendana vizuri? Hivi ni vipofu?”

Hans aliyekuwa amesimama pembeni aliitazama ile simu iliyosambaratika akiwa hoi. Angelazimika kununua simu mpya tena. Hakujua hata idadi ya simu

ambazo Alvin alikuwa amevunja tangu awe na Lisa.

“Bwana Kimaro, watu kwenye mtandao wote ni wavivu sana. Usiwajali.” Hans alimpoza kimawazo.

Alvin alikodoa macho. Hakutaka, lakini

alikuwa amesoma yale ambayo watu

walisema kuhusu Kelvin Mushi kuwa na mapenzi makubwa kwa Lisa, na Lisa

kuwa na hisia nzuri kwa Kelvin.

Kulikuwa na watu wanaotunga hadithi

ya mapenzi ya kipuuzi kuhusu

kupendana kwao kwa siri.

Tumbo la Alvin liliwaka kwa hasira.

Akaketi na kufungua laptop yake, vidole

vyake vikiruka kwenye keyboard.

Dakika chache baadaye, Hans

aligundua kuwa habari ya Kelvin na Lisa

ilikuwa imetoka kwenye habari

zanazovuma mtandaoni! Ilishangaza!

Bwana Kimaro kweli alikuwa amedukua

akaunti ya facebook ya Mawenzi moja kwa moja.

“Alvin...” Mlango wa ofisi ulifunguliwa

ghafla na Sam Harrison akaingia.

Alipomwona Alvin ambaye alionekana

kama mfalme wa pepo, alitetemeka.

“Nilifanya uchunguzi. Usiku huo, Lina

Jones aliingia na watu wachache na

alionekana kwenye jumba hilo la hoteli.

Wakati huo, pia alimwagiza meneja wa

hoteli hiyo kwamba hakuna mtu

anayeruhusiwa kuingia katika chumba alichopanga.”

Alvin alikodoa macho. Ilionekana kana kwamba tukio hilo la Lisa lilikuwa ni njama. Hata hivyo, jinsi alivyokuwa amembusu Kelvin kimahaba bado

ilimkasirisha. "Umegundua ni wakati gani Lisa na Kelvin waliondoka?" Aliuliza kwa huzuni.

"Asubuhi," Sam alikohoa kwa upole na kusema kwa sauti ya chini, "Walitoka asubuhi baada ya kubadilisha nguo."

Maneno hayo yaliposikika, Alvin aliivunja kompyuta moja kwa moja.

Mwanamume na mwanamke katika

chumba pamoja, na mwanamke hata

kulishwa madawa ya kulevya.

Inawezekanaje kuamini kwamba

hakuna kilichotokea kati yake na

Kelvin?

Sam alimtazama kwa huruma. Kusema kweli, pia hakuamini kabisa kwamba

Lisa hakuwa na hatia. “Sawa… Lisa pia ni mwathirika katika hili… Nilisikia

kwamba Lina Jones aliingia na walinzi wawili wakati huo. Kama Kelvin Mushi

asingetokea, matokeo yangekuwa mabaya zaidi.”

"Unamaanisha nini? Unasema

ninapaswa kumshukuru Kelvin Mushi?”

Macho jeuri ya Alvin yalimtoka.

"Mwishowe, yeye ndiye mjinga.

Anaendelea kuanguka kwa hila za

familia ya Jones mara kwa mara.

Baadaye, alijaribu hata kunihadaa na

kuwa marafiki na Kelvin. Ananichukulia

kama mjinga”

Sam alikuna ncha ya pua yake na

kusema. “Hata hivyo, tayari

nimekuchunguzia. Ni juu yako ikiwa

unataka kuachana naye au kuendelea naye.”

Alvin hakuwa na mahali pa kutoa

uchungu wake. Aliwasha sigara na kumwambia Sam. "Twende tukanywe

vinywaji vichache na mimi leo usiku."

Sura ya 135 Usiku huo, Alvin alikunywa glasi baada ya glasi ya pombe. Sam hakuweza

kumzuia. Uvumilivu wa pombe wa Alvin

ulikuwa mkubwa, lakini alikunywa sana

usiku huo na cha kushangaza alilewa kidogo. "Nimemkumbuka Sarah ghafla."

Alitazama usiku nje ya dirisha na

kunong’ona, “Kati ya wanawake wote

waliobahatika kuingia kwenye maisha

yangu, ndiye pekee aliyekuwa na moyo

wake wote kwangu. Hakukuwa na

udanganyifu na hakukuwa na usaliti.

Kwa nini alikufa?”

Sam alishika glasi yake, maumivu makali yakimtoka moyoni.

Kile ambacho wengine walikiona kwa

Alvin kilikuwa ni Kilima cha juujuu

kilichoonyesha ufahari wake, lakini Sam alijua kwamba Alvin alikua bila mapenzi ya wazazi wake. Ndani ya moyo wake

alikuwa ni mtu asiyejiamini sana katka

suala zima la mahusiano. Hata

alipokuwa akisoma shule, waliomwendea walikuwa na ajenda za siri na kumfanya aingiwe na mashaka makubwa. Wakati huo, Alvin aliumia

sana. Kama rafiki yake, Sam ghafla alijuta

kumwita Dar es Salaam. Hakutarajia

kwamba moyo wa Alvin, ambao siku

zote ulikuwa umeganda, ungehamaki

ghafla. Sam aliongozana naye kunywa

hadi Alvin akalewa sana. Ilikuwa ni mara ya pili Sam kumuona Alvin akiwa

amelewa kiasi hicho.

Kwenye meza ya vinywaji, simu mpya ilitetemeka kila mara. Lisa alikuwa

akimpigia simu Alvin mara kwa mara. Sam alichukua simu na kuitikia. Sauti ya Lisa ilisikika kutoka upande wa pili. “Uko wapi? Mbona umechelewa sana? Njoo nyumbani, tutayaongea tu yataisha sawa…"

"Alvin amelewa." Sam akamkatisha.

"Nakuja kumchukua mara moja," Lisa alisema kwa hofu.

"Hakuna haja. Hutaweza kumbeba hata hivyo. Nitamrudisha mimi mwenyewe.”

Baada ya simu kukatika, Lisa alisubiri mlangoni. Kulikuwa na mvua usiku huo

tena, na matone ya mvua yalidondoka

nje na kulowanisha kila kitu. Nusu saa

baadaye, Sam aliegesha gari lake.

Alipumua kwa huruma na upole baada

ya kumuona Lisa akiwa amesimama

kwenye upepo wa baridi.

Baada ya gari kuegeshwa, Lisa alifungua mlango wa siti ya nyuma.

Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Alvin akiwa amelewa sana.

Uso wake mzuri ulionyesha wazi kuwa alikuwa amelewa, na alionekana

kupoteza fahamu pale kwenye siti ya nyuma. Yeye na Sam walimsaidiana

kumwingiza Alvin hadi chumbani pamoja. Lisa alimtazama Sam huku

akihisi mnyonge. “Bwana Harrison, asante. Mimi…”

“Ni sawa, Alvin aliniambia niachunguze jambo hili. Najua hukukusudia.” Sam

alikuwa na maumivu ya kichwa. Pia

hakujua la kusema. “Nitaondoka sasa hivi.”

Lisa aliona kuwa Sam alikuwa

akimchukulia tofauti na hapo awali.

Hakucheka na kutabasamu kama

alivyomfanyia siku za nyuma. Alikua na huzuni kidogo kwa sababu yake. Alijua

kwamba hakutaka kuzungumza naye sana, lakini hakuweza kujizuia kuuliza, “Bwana Harrison, unajua Alvin anachofikiria kuhusu hili?”

"Lisa, mwanaume yeyote angechukizwa na hilo," Sam alisema bila kuficha, "Ungemwambia Alvin juu ya hili mapema. Sasa kwa kuwa imejulikana bila wewe kusema, kusema kweli inatia uchungu sana.”

Uso wa Lisa ulipauka. “Hakuna kilichotokea kati yangu na Kelvin. Ni kweli."

“Ni bure kuniambia hivyo. Unahitaji Alvin

akuamini.” Sam akatikisa kichwa na kuondoka.

Lisa alibaki ameduwaa kwa muda.

Alielewa nini Sam alimaanisha. Alvin hakumuamini. Afanye nini? Alikuwa

anampenda kweli sasa. Hakutaka kumuacha. Alimtazama sana yule mtu pale kitandani. Huenda ikawa ni kwa sababu alikuwa amekunywa pombe

kupita kiasi na hakujisikia vizuri, hivyo tumbo lake pia likawa na usumbufu.

Aliendelea kupapasa tumbo lake. Kiyoyozi cha kuongeza joto kiliwashwa mle chumbani na hakuwa amevua koti lake, kwa hiyo jasho likatoka upesi

kwenye paji la uso wake. Lisa alichota beseni la maji ya baridi. Alivua koti lake, akafungua kola ya shati lake, na kuufuta uso wake mzuri kwa taulo.

“Sarah…” Mwanaume huyo alimshika

mkono ghafla, na manung’uniko ya chinichini yakatoka kwenye midomo

yake myembamba. Lisa aliganda kana

kwamba ndoo ya maji baridi

imemwagwa juu yake.

Sarah? Huyo alikuwa nani? Je, alikuwa mpenzi wake wa zamani?

Lisa aliuvuta mkono wake kutoka kwenye mshiko wake kwa nguvu.

Mkono wa mtu huyo ulishika hewa, na akamwita tena, “Sara”.

Aligeuka na kukaa pembeni ya kitanda.

Macho yake yalikuwa mekundu, na moyo wake ulikuwa umechomwa kana

kwamba alikuwa akichomwa kisu.

Inauma! Asubuhi iliyofuata, Alvin aliamka na hangover. Kichwa chake kilimuuma, na tumbo lake lilihisi kukosa raha pia.

Alitazama mazingira na kugundua kuwa alikuwa katika chumba chake cha kulala

katika nyumba yake. Kwanini Sam

alimrudisha pale? Kwa kweli hakutaka

kukutana na Lisa kabisa. Hata hivyo, alikuwa amekunywa pombe kupita kiasi

jana yake usiku na alikuwa akijisikia

vibaya sana muda huo.

Alipotazama huku na kule, ghafla aliona kikombe cha maji ya uvuguvugu na

vidonge viwili vya tumbo vimekaa kando ya kitanda cha kulalia. Macho yake

meusi yalimtoka. Alihisi ni Aunty Linda ndiye aliyemwkea dawa hiyo. Alichukua

dawa huku moyo wake ukiwa umechanganyikiwa. Alishuka tu baada ya kunawa na wakati tumbo lake lilihisi vizuri kidogo.

Shangazi Linda alipokuwa akifanya

usafi alimuona Alvin akishuka.

Alitabasamu. "Bi Kimaro anakuandalia kifungua kinywa sasa hivi."

Alvin akaenda kwenye meza ya chakula. Kulikuwa na nyama na

nguruwe iliyochomwa, supu ya kuku wa kienyeji, maziwa fresh, maziwa, juisi ya limao...

Mlango wa kuteleza wa jikoni ukafunguliwa, na Lisa akatoka na chungu cha mtori. Alivaa gauni la rangi ya waridi na aproni iliyofungwa kiunoni

mwake. Nywele zake zilikuwa zimefungwa kama mkia wa farasi, na kufunua uso wake mdogo na safi. Ilimfanya aonekane mpole na mtulivu.

"Ulikunywa sana jana usiku, kwa hivyo ni bora ukaanza kwa kula kitu chepesi asubuhi. Mtori ni rahisi kusagwa na hautakuwa mzigo kwenye tumbo lako.”

Lisa alisema huku akivuta bakuli la mtori na kuliweka mbele yake.

Alvin aliutazama ule mtori kisha

akamtazama Lisa. Taswira ya yeye

kushika shingo ya Kelvin na kumbusu

kwa nguvu ghafla ilionekana akilini

mwake. Kamba ya uvumilivu moyoni

mwake ilionekana kukatika kwa nguvu.

Alinyanyuka na kuumwaga mtori moja

kwa moja kwenye pipa la takataka.

Kisha akamtazama kwa macho ya jeuri. "Vitu unavyopika ni vichafu."

Uso wa Lisa ulibadilika ghafla. Baada ya muda mrefu, alipepesa macho yake ambayo yalikuwa yakitoka kwa machozi. “Kwa kuwa unafikiri mimi ni mchafu, kwa nini nisiondoke?” Kwanza

likuwa ameita jina la mwanamke mwingine alipolala, hata hivyo. Kwa

kweli, labda hakumpenda sana.

Alvin aliganda alipomsikia hivyo. Macho yake yaliyokuwa na damu kwa mbali

yalimtazama ghafla. “Unataka kuondoka? Unataka kwenda kwa Kelvin

kukaa naye sasa? Kila mtu kwenye

mtandao anawaambia nyinyi wawili

mnafaa kuwa pamoja. Nyinyi ndio

wanandoa wanaofaa zaidi katika

ulimwengu wa biashara.”

"Hapana." Lisa hakuweza kulala usiku

kucha kwani alijiona hana nguvu. “Naondoka kwa sababu hutaki kuniona.”

"Hata kama unanichukiza, unatakiwa kukaa katika nyumba hii," Alvin alifoka kwa hasira, "Maadamu nipo karibu, unaweza tu kuota kuwa na Kelvin. Acha nikuambie, Lisa Jones, kwa kuwa umenichokoza, usifikirie hata kuniacha nikiwa mzima!”

Kisha, akaondoka.

Lisa alitabasamu kwa uchungu. Hivi, alikuwa bado mzima? Tayari alikuwa amepoteza moyo wake kabisa.

Sura ya 136

Alvin alikaa kwenye siti ya nyuma ya gari lake. Alikuwa ametawaliwa na maamuzi ya hasira mapema asubuhi, lakini sasa ghafla alihisi njaa sana.

Tumbo lilianza kumuuma tena. Aliwasha

sigara kwa hasira. Ikiwa angejua

kwamba hilo lingetokea, angemaliza kula kifungua kinywa chake kwanza

kabla ya kupandisha hasira zake za kijinga. "Bwana Kimaro, ngoja nikununulie chakula." Hans alimtazama kwa wasiwasi.

“Sina njaa. Nenda uniletee Lina Jones

hapa,” Alvin alisema kwa upole, “Sikuzote nilitaka Lisa ashughulike naye, lakini haina maana sana. Nitamalizana naye mwenyewe.”

Hans aliitikia kwa kichwa. Ilionekana

kana kwamba ingemlazimu kumuombea

Lina kwa kile ambacho alihisi kilikuwa

kinaenda kumkuta. •••

Katika kampuni ya Mawenzi

Investments. Lina alifukuzwa moja kwa

moja na walinzi. Hakutaka kuondoka na

kuishia kupiga kelele mlangoni, “Hata

kama baba yangu alikamatwa, bado ana hisa kwenye kampuni na mimi bado ni mtoto wake. Nina haki ya kurithi hisa zake na kufurahia gawio langu.”

“Potelea mbali!” Yule mlinzi alimtemea mate isivyostahili. “Kila mtu anajua

kuwa wazazi wako walimuua bibi mzee

ili wapate hisa za Mawenzi Investments. Walimuua Mzee Madam Masawe.

Hawana utu kabisa. Mwenyekiti Jones

tayari ameomba mawakili wengi

kurejesha hisa za Jones Masawe. Utarithi nini? Endelea kuota!"

"Subiri. Nitakaporudi Mawenzi, nitafanya maisha yako kuwa mabaya zaidi kuliko

kifo. Lina alitetemeka kwa hasira.

Hata mlinzi alithubutu kumdhalilisha

sasa. Kweli dunia haikuwa ya haki. Ni

wazi alikuwa ametuma picha zote za

uchafu za Lisa na Kelvin kwa waandishi

wa habari jana yake, lakini sio tu kwamba ilishindwa kuharibu sifa ya Lisa, bali watu walianza hata

kumuoanisha na Kelvin sasa. Ilikuwa inakasirisha sana na kukatisha tamaa.

Alitembea kando ya barabara wakati gari lisilo na nambari ya leseni lilisimama ghafla mbele yake. Kisha, watu wawili wakamsukuma moja kwa moja kwenye gari.

"Unafanya nini?" Kabla Lina hajajibu, alifunikwa kwenye gunia na kupoteza fahamu. Muda si muda, ndoo ya maji

baridi ilimwagiwa juu yake na akapiga kelele kutokana na baridi. Gunia lilipasuliwa.

"Baridi ilikuwa nzuri?" Hans alimtazama kutoka juu.

Lina alitazama juu na kufikiria kuwa

anaonekana kuwa mzoefu kidogo.

Baada ya muda, alimkumbuka. "Ni wewe. Wewe ni msaidizi wa Alvin Kimaro…”

"Ni vizuri kukumbuka." Hans aliachia

tabasamu hafifu. Akageuka pembeni, akamfunua mtu aliyekaa kwenye sofa

ambalo halikuwa mbali. Mwanaume huyo alivalia suti nyeusi na kushika sigara mkononi, moshi ukitanda hewani. Macho yake ya wino yaliangaza na mwanga mweusi uliokuwa mkali kama kisu. Mwanamume huyo alitoa sauti ya kutisha. Lina alimtambua. Hofu isiyoelezeka ikapanda kutoka ndani ya moyo wake.

"Bwana. Kimaro, unajishughulisha na kazi ya kisheria. Unataka

kunyang'anywa leseni yako kwa kuvunja

sheria? Ninakuonya, afadhali uniache mara moja, la sivyo sitakuacha kamwe.”

Hans alicheka kana kwamba amesikia

mzaha. “Unacheka nini? Huwezi kuelewa nilichosema?” Lina alicheka. “Hebu

niambie, haufahamu kuwa mimi ni mwanamke wa Willie Kimaro? Unajua

Bwana Kimaro ni nani? Unajua kuwa ananipenda sana? Ikiwa huniamini, unaweza kuchukua simu yangu na kuangalia picha zetu pamoja.”

Alvin alimaliza kuvuta sigara na kuitupa

kwenye sinia ya majivu kabla ya kuinuka. Mwili wake mrefu ulitembea

polepole kuelekea kwake. Lina alifikiri anaogopa na akacheka. “Alvin Kimaro, wewe ni mwanasheria tu. Willie Kimaro

si mtu ambaye mtu kama wewe

unaweza kudiriki kumuudhi—”

Kabla hajamaliza, Hans alimpiga kofi

kwenye shavu na kumng'oa jino

mdomoni. Lina alipiga mayowe, “Willie hatakusamehe—”

Smack! Kofi jingine likasikika. Baada ya makofi kadhaa, Lina alipoteza meno

machache na hakuthubutu kuongea tena. "Nyamaza." Hans alitabasamu.

“Unafikiri Willie Kimaro ni nani?

Hujaelewa kwa nini Willie alibadili

mtazamo wake kwako haraka hivyo?”

Lina aliganda. Alimtazama Alvin na ghafla akakumbuka kuwa jina lake la mwisho lilikuwa Kimaro pia. “Hilo

haliwezi kuwa. Sijawahi kusikia mtu

anaitwa Alvin katika familia ya Kimaro."

“Unawajua watu wangapi katika familia ya Kimaro?" Hans alidhihaki. “Acha

nikwambie, Alvin Kimaro ndiye kaka

mkubwa katika familia ya Kimaro.

Amekuwa akisimamia familia tangu

akiwa na umri wa miaka 20.”

Ubongo wa Lina ulivuma kana kwamba anaota. Kila mtu alijua kwamba kaka

mkubwa, wa ajabu wa familia ya Kimaro alikuwa mtoto wa Leah Kimaro. Mtu

huyo alikuwa mtu wa chinichini sana, lakini mbinu zake za ukatili zilijulikana

sana. Aliingia katika kampuni hiyo akiwa na umri wa miaka 20. Mjomba wake wa pili alipokaidi, alimvunja mguu wake mbele ya umati.

Baada ya kuchukua jukumu la

kuongoza KIM International, alipanua biashara yake hadi ng'ambo kwa kasi ya radi na hata akaingia katika nyanja za

mawasiliano, fedha, na teknolojia

kwenye masoko ya nje ya nchi kwa

haraka haraka. Kwa wakati huo, alikuwa

ameingia kwenye orodha ya watu

miamoja tajiri zaidi Afrika, akiachwa kwa

karibu sana na kina Dangote, Mo Dewji,

Bhakresa na wengineo. Kulingana na uvumi, alikuwa mtu wa tatu tajiri zaidi

nchini Tanzania na pia wa kushangaza

zaidi. "Hiyo haiwezekani. Unasema uwongo!”

Lina alikuwa akiingiwa na wivu. Lisa

alimkamataje mtu kama huyo?

“Kwa nini nikudanganye? Huyo mjinga

Willie Kimaro aliogopa sana hivi

kwamba alikojoa kwenye suruali yake

alipomwona Bwana Kimaro. Hans alifoka. “Lina Jones, Bwana Kimaro

hakutaka kushughulika na wewe mara ya kwanza, lakini hukupaswa kumpa

Lisa Jones dawa ya kulevya. Na kwa

kweli hukupaswa kutoa picha hizo

kwenye vyombo vya habari.”

Lina alishtuka. Alipiga magoti mbele ya

Alvin na kutetemeka. “Bwana Kimaro, mimi ni mjinga. Nilikuwa mjinga.

Tafadhali nisamehe sana.”

Alvin akampiga teke kwa kuchukia. Ujeuri wa macho yake ulidhihirisha

kwamba hakutaka chochote zaidi ya kumwangamiza kabisa. “Unadhani

nitakuacha ukipumua?”

"Hapana, hapana, hapana. Haikuwa mimi. Sikupiga picha.” Lina akatikisa kichwa kwa hofu. “Nilitumiwa na mtu nisiyemjua. Ni kweli nilimpa Lisa dawa

usiku huo, lakini Kelvin Mushi alipokuja, kamera ya video iliyokuwa chumbani iliharibiwa.”

“Hukuwa wewe?” Uso wa Alvin ulikaza

zaidi huku alama ya mshangao ikimulika

machoni mwake, akiamini hadaa ya

Lina. "Naapa." Lina alikuwa amepoteza meno

kadhaa na mdomo wake ulikuwa

umejaa damu. “Kama ningekuwa na

hizo picha ningezitumia kumtishia Lisa

zamani. Ningewezaje kumruhusu kukaa

katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda

mrefu hivyo na kuwaweka wazazi

wangu jela?”

“Kiapo chako hakina thamani.” Uso wa Alvin ulizidi kutisha, lakini aliamini

maneno ya Lina. Ikiwa hakuwa yeye, basi ni nani?

Alikuwa na wazo, na midomo yake

ikachanua katika tabasamu. Usiku huo, mbali na Lisa, ilionekana kana kwamba

kulikuwa na Kelvin pekee. Kwa Kelvin

Mushi haikuwa rahisi hata kidogo kwa

Lisa kumshuku. Lisa alijua kwamba

anampenda, lakini bado alikuwa tayari

kuendelea kuwa na urafiki naye. Kelvin

alikuwa ameenda ng’ambo kufungua

ofisi ya tawi alipokuwa kijana, kama

yeye tu. Anawajua watu wenye uthubutu

wa kuvuka mipaka na kwenda

kufanikiwa nje ya nchi huwa wajanja

wajanja sana. Alvin hakumwamini

Kelvin hata kidogo. Lina alijua kwamba alimwamini na akasema kwa haraka, “Bwana Kimaro, tafadhali niruhusu niende. Ninaahidi sitomsumbua Lisa tena. Nitaondoka Dar es Salaam.”

“Unadhani nitakuacha uondoke kwa amani?” Alvin alitabasamu kwa giza.

“Nimechunguza mambo yako. Ulikulia kijijini baada ya kuibiwa ukiwa mtoto mdogo, ukatolewa usichana wako na mwanakijiji ukiwa na umri wa miaka 15.

Baadaye katika shule ya sekondari, ulifumaniwa zaidi ya mara kumi na waume za watu. Uliwekwa kinyumba na tajiri mmoja na hata kutoa mimba zisizo na idadi. Ni aibu iliyoje. Hukuwa na maisha mazuri hata baada ya kurudi

kwenye familia ya akina Masawe.”

Uso wa Lina ulikuwa umepauka kwa

aibu. Hii ilikuwa historia yake ya giza. Alikuwa ameifunika kwa makini sana, lakini mtu huyu kwa kushangaza aliweza kujua juu yake. Alikuwa anatisha sana.

"Kwa kuwa unapenda wanaume sana, nitakuozesha mume wa kuishi naye."

Alvin alisema na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Punde, mzee mfupi na mbaya mwenye umri wa miaka 50 aliingia. Alipomwona Lina, alimeza mate ya uchu. "Bwana

Kimaro, unaniruhusu nimuoe?"

Lina alimtazama Hans kwa uso wa kutisha. “Usimruhusu anioe. Nitakwenda na wewe. Unaweza kufanya chochote unachotaka. Unaweza kunifanya vile

Willie alinifanya pia!”

Hans alikwepa nyuma kwa kuchukizwa.

“Usinishike, nachukia mambo machafu.

Usimwogope sana. Anaonekana kuwa

mzee, lakini ana umri wa miaka 40 tu na amekuwa peke yake kwa miaka kadhaa

kwa sababu hakuweza kupata mke. Utamfuata kijijini na kumpatia mtoto.”

Kisha, Hans akaondoka, akimuacha

Lina nyuma. Alilia kwa kukata tamaa, lakini hakuna mtu aliyemjali. Wakati

huo, alijuta sana. Hakupaswa

kumlazimisha Lisa Jones kuondoka

nyumbani wakati huo. Hakupaswa

kumsukuma Bibi Madam Masawe chini

ya ngazi.

Lakini, hakuna na dawa ya majuto

katika ulimwengu huu.

Sura ya 137

Katika mlango wa kituo cha polisi, Lisa

alikuwa amemaliza tu kurekodi ushahidi

wake mara ghafla akasikia mtu akiliita

jina lake.

“Lisa.” Aligeuka nyuma na kumuona

Kelvin akija kwake huku akiwa na tabasamu usoni mwake. Hali ya hewa ilikuwa ya baridi, na alikuwa amejifunika kitambaa shingoni.

"Ni bahati tu nimekuona. Kwa nini upo hapa?” Lisa alilazimisha tabasamu kumsalimia. Kila alipokuwa akimuona, alizikumbuka picha zile na mgogoro kati ya Alvin na yeye.

"Kuna jamaa wa nyumbani alifanya

tukio la ajabu, kwa hivyo nilikuja kumdhamini." Kelvin alionekana hoi.

"Nilisikia kwamba Jones Masawe na Mama Masawe walikamatwa hivi majuzi. Je wewe…”

“Ndio, polisi waliniita hapa kuchukua maelezo yangu. Kesi hiyo itafikishwa

mahakama wiki ijayo kisha watasomewa hukumu.”

"Hongera, hatimaye umelipiza kisasi kwa bibi yako." Kelvin alifurahi kusikia hivyo.

“Asante.” Tabasamu la Lisa halikumfikia machoni. Alionekana kuchoka kabisa.

Kelvin alitembea pamoja naye kuelekea sehemu ya maegesho, huku akimtazama njiani. “Unaonekana umechoka. Umekuwa ukipumzika vizuri kweli? Na Alvin bado hajakuelewa tu…?!”

"Hatuwezi kuzungumza juu ya hili?" Lisa alimkatisha.

"Ni kosa langu." Kelvin alionekana kuwa na hatia. “Kosa lako kivipi? Ulinisaidia usiku ule.

Kama si wewe, ningefanyiwa ukatili

mbaya na pengine ningeweza kujiua

muda mrefu uliopita. Jana, hata

ulishirikiana nami kufafanua hali

ilivyokuwa na kuokoa sifa yangu.

Ninapaswa kukushukuru,” Lisa alitikisa

kichwa na kusema kweli.

Wawili hao walizungumza huku

wakitembea. Lakini kijana mmoja

aliibuka kando yao ghafla na

hawakumjali, wakidhani ni mpita njia tu.

Hata hivyo, ghafla mwanamume huyo

alitoa kisu cha matunda kutoka kwenye

mfuko wake wa suruali na kukichoma

kuelekea kifuani kwa Lisa.

“Lisaaa!” Kelvin aliona Lisa amechelewa

sana. Alipoona kile kisu kinataka

kumchoma, alinyoosha mkono haraka

kukizuia, na kisu hicho kikapenya

kwenye mkono wake.

Wakati Lisa anajibu, mtu huyo alikuwa

amechomoa kisu haraka ili kumchoma

Lisa tena. Kelvin angeweza tu kutumia

mwili wake kumkinga, na kisu kikapenya

sehemu ndogo ya mgongo wake.

“Msaada!” Lisa alilia. Kwa msukumo aliushika mkono wa mwanaume huyo.

"Wewe ni nani?!”

“Hutakiwi kunifahamu. Ni kosa lako kuwa mwanamke wa Alvin Kimaro.

Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda

mrefu sasa.” Mwanaume huyo alifichua uso wake wa kutisha huku akiendelea

kudunga kisu kwenye mwili wa Kelvin

kana kwamba alikuwa na wazimu.

Kwa bahati nzuri, walikuwa karibu na kituo cha polisi. Polisi mmoja alisikia

kilio cha kuomba msaada na haraka

akakimbia ili kumshika mhalifu.

Punde, ambulensi ilifika na upesi

ikampeleka Kelvin hospitalini. Hata

hivyo, tayari alikuwa amepoteza damu

nyingi njiani na kupoteza fahamu. Lisa

alipiga simu kwa haraka kwa Ethan, ambaye alikimbia mara baada ya Ambulance kufika hospitali.

Mlango wa Emeregence Room

ulisukumwa, na daktari akatoka na fomu mkononi. “Kisu kilichomwa kwenye figo ya kushoto ya mgonjwa na inabidi itolewe mara moja ili kuokoa maisha yake. Familia ya mgonjwa iko wapi? Tafadhali saini mara moja.”

Lisa alipigwa na butwaa. Ethan pia aliona ni vigumu kukubali. "Daktari, lazima ni lazima figo iondolewe? Kwani hakuna namna nyingine?"

"Necrosis tayari imeingia kwenye figo ya kushoto, kwa hivyo haina maana sasa," daktari alisema bila msaada, "Kama

tungeweza kuiokoa, bila shaka tungeiokoa."

Ethan hakuwa na la kufanya zaidi ya

kuvumilia maumivu na kusaini zile karatasi. Lisa alitoa machozi ya uchungu. “Yote ni makosa yangu. Mtu huyo alitaka kuniua. Mjomba wako

ndiye aliyetumia mwili wake kunisaidia kuzuia kisu."

Ethan alikuwa na hisia tofauti.

Hakutarajia Kelvin angekuwa na hisia za kina namna hiyo kwake. Sasa, pia alikuwa na wasiwasi sana kuhusu usalama wa Kelvin. Angeweza tu kusema, “Usifikirie juu yake. Daktari alisema kuwa kuondoa figo yake

kutaokoa maisha yake. Mwili wa mwanadamu bado unaweza kufanya

kazi na figo moja tu. Anapaswa kuwa

mwangalifu zaidi katika siku zijazo."

Lisa alitabasamu kwa uchungu. Kelvin

alikuwa anaenda kupoteza figo.

Angewezaje kuwa mzima kama hapo

awali? "Umewajulisha babu yako?"

“Hapana, babu na bibi wamezeeka na sitaki kuwapandisha presha. Tusubiri hadi upasuaji wa Mjomba umalizike.”

Ethan alimtazama na kuhema moyoni

mwake. Aliogopa hasa kwamba babu na bibi yake wangezimia ikiwa wangejua ukweli.

Kwa bahati nzuri, saa tatu baadaye, Kelvin aliokolewa. Operesheni ilikuwa

imekwisha, lakini bado hakuweza kufumbua macho.

Muda si muda, polisi walifika hospitalini.

Walipomwona Lisa walimwambia. “Bi.

Jones, tumemhoji mhalifu. Mtu aliyetaka kukuua anaitwa Zigi Kabwe. Yeye si mwenyeji wa hapa Dar.”

Lisa alikasirika. “Hata simfahamu mtu huyu.”

Afisa huyo alitikisa kichwa. “Kulingana na maelezo yake, alikuwa na dada yake pacha anayeitwa Lily Kabwe. Miaka

mitano iliyopita, Lily Kabwe alikuwa na umri wa miaka 17 tu, lakini alivutia

macho ya Thomas Njau kutoka kwa familia ya Njau huko Nairobi. Thomas

alimbaka Lily kwa nguvu baada ya kukataa kulala naye na akaamua

kujirusha hadi kufa kutoka kwenye

jengo kutokana na fedheha. Familia ya

Kabwe ilimshtaki Thomas. Wakati huo, kulikuwa na karibu ushahidi kamili, lakini

familia ya Njau ilimwajiri Alvin Kimaro

kutetea kesi yao. Alvin Kimaro alidai

kuwa Lily alimtongoza Thomas lakini

Thomas alimdharau, hivyo akaamua

kujiua kwa sababu ya unyonge wake.

Mahakama haikushindwa tu

kumwadhibu Thomas, lakini hata

ilimfanya Lily aonekane kama mtu duni

asiye na maana. Mama yake hakuweza

kuvumilia na na akapata presha.

Amefariki hivi karibuni…”

Lisa alishtuka. Alijua tu kwamba Alvin hawezi kushindwa mahakamani, lakini hakujua kwamba alikuwa amechukua kesi nyingi zisizo na moyo wa utu. "Kwa hivyo, alitaka kuniua ili kulipiza kisasi kwa Alvin Kimaro?"

“Ndiyo. Alitoweka miaka mitano iliyopita baada ya kesi hiyo, na tuligundua tu kwamba alirudi Dar es salaam mwaka huu. Alitaka Alvin Kimaro ajue uchungu wa kufiwa na mpendwa wake, lakini…

Alvin Kimaro amezungukwa na walinzi na ni mwangalifu sana, kwa hivyo Zigi

Kabwe ameshindwa kutimiza lengo lake licha ya kujaribu kwa miaka kadhaa.”

Afisa huyo alimwambia, “Amekuwa akikufuata kwa muda, lakini umekuwa ukilindwa na mlinzi siku hizi za karibuni.

Ni leo tu ndipo alipata nafasi hiyo kwa sababu hukuwa na mlinzi.”

Ghafla, Lisa alionekana kugundua kitu.

Siku chache zilizopita, Alvin alikuwa

amepanga ghafla Shani afuatane naye

kama mlinzi wake. Haikuwa kumlinda

dhidi ya Jones na binti yake bali

kumtazama Zigi Kabwe. Hata hivyo, hakumwambia chochote.

Haukuwa ulinzi wake hata kidogo.

Kama Kelvin asingetokea siku hiyo, angekufa. Hofu isiyo na kipimo

ikaufunika moyo wake. Lisa ghafla

alifikiri kwamba hakumfahamu kabisa

Alvin kama alivyodhani.

"Kwa nini kulipiza kisasi kwako kwa kile

Alvin Kimaro alichofanya kwa mtu

mwingine?" Ethan alikasirika. “Lisa, nakushauri ukae mbali na Alvin Kimaro.

Nani anajua ni maadui wangapi

amewachokoza kwa miaka mingi?

Nilisikia huwa anaenda mahakamani

kuwatetea matajiri tu, madhalimu na

mafisadi, je ni haki za wangapi

amedhulumu? Lazima atakuwa

amepata pesa nyingi kwa njia isiyo halali."

Lisa alinyamaza, akiinamisha kichwa

chini na uso wa huzuni. Moyo wa Ethan uliumia. Ikiwa asingefanya chaguo baya

hapo kwanza, Lisa asingeangukia kwa

Alvin Sura ya 138

Saa nne usiku, Alvin aliingia kutoka nje

akiwa na uso jeuri na mkali. Alipanda

juu ndani ya dakika mbili kabla ya kushuka tena kwa haraka. "Lisa bado hajarudi?" "Hapana." Shangazi Linda aliogopa

kidogo sura yake.

“Mbona bado hajarudi?”

"Sijui. Yeye hapokei simu pia.” Aunty

Linda alipomaliza kuongea, hali ya joto ndani ya jumba hilo ilionekana kushuka na kumfanya ashtuke.

Alvin akatabasamu kwa ujeuri. Vizuri. Hata baada ya kumsaliti na Kelvin, bado hakujua jinsi ya kuishi. Ilikuwa tayari saa nne usiku lakini hakuwa amefika

nyumbani bado. Hata hakupiga simu nyumbani. Mwanamke huyo hakubadilika kamwe.

“Bwana Kimaro,” wakati huo, Hans alikimbia kutoka nje. “Nimepata habari.

Zigi Kabwe alimvamia Miss Jones nje ya kituo cha polisi leo, lakini Kelvin

Mushi alimzuia na kuchomwa visu vingi mwilini. Lisa yuko salama, lakini Kelvin amejeruhiwa vibaya na sasa anatibiwa hospitalini.”

Mwili wa Alvin uliganda pale pale huku

macho yake meusi yakiwa yamemtoka

ghafla. “Shani yuko wapi? Amechoka

kazi? Si nilimwambia amlinde Lisa?”

Hans alipumua na kukumbusha kwa upole, “Bwana Kimaro, ulisahau?

Ulipoona picha za Lisa na Kelvin kwenye vyombo vya habari siku moja

kabla ya jana, ulishindwa na kumwambia Shani aache kumlinda Miss

Jones. Ulimwambia Shani amwache Bibi Jones kwa hiari yake mwenyewe.”

'Nilimwambia asimlinde Lisa na kweli

aliacha kumlinda Lisa? Ana akili timamu?" Alvin alishindwa kujizuia tena.

Hans alikuwa kimya. Shani alifuata tu maneno ya Alvin kwa utii.

“Twende hospitali.” Alvin akatoka nje.

Baada ya kufika hospitalini, alivamia

moja kwa moja hadi kwenye wodi ya watu mashuhuri. Kelvin bado alikuwa

katika hali ya kukosa fahamu. Mrija wa

oksijeni ulikuwa umefungwa kwenye

pua yake, na Lisa alikuwa akifuta uso wake kwa kitambaa.

Tukio hilo lilimchoma macho Alvin bila

huruma. Hapo zamani alipokuwa

amelazwa hospitali, alikuwa amemtunza

vile vile. Sasa, alikuwa akimtunza mwanamume mwingine.

"Njoo hapa," alimtazama na kusema

polepole, "Tuondoke haraka."

Lisa aliacha harakati zake na kutikisa

kichwa. “Bado hajaamka. siwezi kuondoka.”

"Lisa Jones, huelewi nilichosema?"

Mwali wa hasira kweny moyo wa Alvin

ukawashwa papo hapo. Sauti yake

ilikuwa ya kikatili sana. "Ninakupa nafasi ya mwisho."

Sauti yake iliufanya moyo wa Lisa

kusinzia. Alikaribia kuchomwa kisu hadi

afe siku hiyo. Hakuona kuwa alikuwa

ametapakaa damu? Je, aliwahi kumjali?

"Alvin Kimaro, kuwa mwenye busara.

Kama si Kelvin, ningekuwa maiti kufikia sasa. Alimlinda mpenzi wako. Ni sawa

ikiwa huna shukrani yoyote, lakini mtazamo wako unawafanya watu wahisi

kwamba wewe ni mnyama mwenye damu baridi.”

“Mimi ni mnyama mwenye damu

baridi?” Alvin akapiga hatua kuelekea kwake. Alikuwa amemfanyia mengi,

akimlinda mara kwa mara, hata kumpenda. Hata hivyo, alikuwa

akimshutumu kwa kuwa na damu baridi? Maneno hayo mawili yaliupiga moyo wake kama kisu, na kusababisha maumivu yasiyovumilika.

"Unapaswa kuwa tayari umejua kwa nini

Zigi Kabwe alitaka kuniua," Lisa

alidhihaki, "Hivi kweli familia maarufu ya

Kimaro ina ukata wa pesa kiasi kwamba

unalazimika kupigania kesi isiyo ya haki

kwa pesa hizo kidogo? Au ilikuwa kwa ajili ya umaarufu? Ulifika kileleni na kupata sifa uliyonayo sasa katika ulimwengu wa wanasheria kwa

kuwakanyaga watu wengine?”

Alvin alikunja ngumi. Mishipa ya nyuma ya mkono wake ilitoka nje. "Lisa Jones, elewa hili. Mimi ni mwanasheria.

Wanasheria hushinda au kushindwa tu.

Mimi si mjumbe fulani wa haki.”

"Lakini mtu hawezi kuishi bila dhamiri."

Lisa akatikisa kichwa. Ghafla aligundua

kuwa yeye na Alvin walionekana kutoka dunia mbili tofauti kabisa.

“Nimekufanyia mambo mengi, lakini leo hii unasema sina dhamiri?”

Alvin alimtazama kwa hasira. Hajawahi

kumtendea mwanamke kinyume sana

hapo awali, lakini alipinga kila kitu katika

sentensi moja. “Kwa sababu Kelvin

alitoa maisha yake ili kukuokoa, kwa

hiyo unataka kuwa pamoja naye? Ni kweli, siku zote amekuwa akikufuata.”

"Acha kuongea ujinga." Lisa alikasirika.

"Amepoteza figo kwa sababu yangu. Siwezi hata kukaa na kumtunza? Hiki

ndicho kitu kidogo zaidi ninachoweza kumfanyia baada ya kuokoa maisha yangu.”

“Sijali. Njoo tuondoke mara moja. Kelvin Mushi sio mtu mzuri kama unavyofikiria

wewe. Kelvin ndiye aliyetuma picha hizo kwa siri kwa Lina. Alijifanya kama mtu

mzuri juu ya uso lakini alicheza hila za siri gizani. Alikuwa ni mnafiki tu.” Alvin

hakujali hata kidogo kuhusu hali ya Kelvin. "Nadhani wewe ndiye ambaye sio mzuri." Lisa alikasirika.

Muda huo Ethan aliingia kutoka nje

akiwa na nguo. “Lisa, nimekuletea nguo. Unapaswa kubadilisha haraka…” Kabla

hajamaliza, akamuona Alvin na uso wake ukiwa mweusi mara moja. “Nani

alikuruhusu kuingia humu? Ondoka haraka..."

Alvin alimtazama kisha akamtazama

Lisa kabla ya kucheka ghafla. “Si ajabu hutaki kuondoka. Mpenzi wako wa

zamani yuko pamoja nawe, na mpenzi wako mpya amelala kitandani. Una jozi

hii ya mjomba na mpwa wake

iliyozunguka moyoni mwako. Lazima uwe na furaha tele.”

"Nimekuozea, siku zote nimekuwa mtu kama huyo moyoni mwako." Macho ya

Lisa yalikuwa mekundu huku mwili

ukimtetemeka bila kuvumilika.

“Alvin Kimaro, umeenda mbali sana. Je, hilo ni jambo ambalo mwanadamu

anaweza kusema?” Ethan hakuweza kuvumilia. Akatupa zile nguo pembeni na kumpiga ngumi Alvin. Alvin aliinua mkono wake kwa urahisi ili kuizuia, na Ethan akanguruma kwa hasira.

“Hapana, wewe si binadamu hata kidogo. Lisa na mjomba wangu wamebeba tu matokeo ya matendo yako maovu. Walikaribia kupoteza maisha kwa sababu yako, lakini huna ubinadamu. Ondoka mbele yangu!”

"Nitaondoka, lakini sitaondoka peke yangu, lazima nimchukue mwanamke wangu." Alvin alinyoosha mkono kumnyanyua Lisa begani. Ethan alikimbia kumzuia, lakini Hans alimzuia haraka.

“Alvin Kimaro, niache! Usifanye hivi! nitakuchukia.” Lisa alianza kumpiga mgongoni, lakini Alvin alipuuza.

“Huchukii kuwa mimi ni mchafu? Je, huogopi kwamba nitakuchafua?” Lisa alipiga kelele.

Alvin akamshusha na kumtupa kwenye

gari. Hans akawasha gari na kufunga milango. Lisa alijua kwamba

asingeweza kushinda dhidi yake na akachagua kukaa mbali naye

iwezekanavyo, bila kumwangalia hata kidogo.

Moyo wa Alvin uliudhika sana, akawasha sigara ili avute katika safari nzima. Lisa alikohoa mfululizo. Alijua

kuwa hapendi kuvuta sigara hata kidogo

kabla ya hii, lakini sasa, alikuwa akivuta sigara mara kwa mara. Hakupenda

wanaume wanaovuta sigara, na hakupenda wanaume wasio na akili

kama yeye hata kidogo.

Baada ya kufika nyumbani, Alvin alimbeba tena na kumtupa kitandani.

Lisa alipanda na kusema kwa ujeuri,

“Utanifunga tena? Alvin Kimaro, mimi ni mwenyekiti wa kampuni sasa. Kuna

watu wengi nyuma yangu

wananitegemea. Siamini kwamba

utaweza kunifunga maisha yangu yote.”

“Kila saa ni ampuni, kampunii! kampuni, ni upuuzi tu kwangu.” Alvin alimuigiza kwa kubana pua. “Je, utaniamini

nikisema nitaifunga kesho?” Alvin alifoka na kumpa jicho la pembeni. "Si

tayari kabisa unajua utambulisho wa jina langu?"

Macho meusi ya Lisa yalitetemeka.

Ilibadilika kuwa tayari alijua. Je, Willie Kimaro alimwambia? Yule mwongo

aliyelaaniwa. Yeye ndiye alisema

atamficha Alvin. Ingawa hakuwa wazi

kuhusu utambulisho halisi wa Alvin

katika familia ya Kimaro, pamoja na

ujuzi wake, angeweza kweli kufanya

hivyo. Familia ya Kimaro ilimiliki 25% ya

hisa za kampuni hiyo, ukichanganya na

ujuzi wake wa sheria, kufumba na kufumbua tu alikuwa anaukosa uenyekiti wake!

"Alvin Kimaro, ungekuwa na furaha zaidi

ikiwa ningeuawa na Zigi Kabwe leo?"

Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku

machozi yakimtoka. "Ninamtunza Kelvin si kwa sababu ninampenda, lakini kwa sababu ninamshukuru."

“Sitakuruhusu umkaribie tena.” Macho ya Alvin yalikuwa yamepoa sana.

Alikuwa na hisia kwamba ikiwa

angemruhusu Lisa abaki na Kelvin kwa

muda mrefu, angempoteza milele. Japo

alikuwa amepoa kwake, bado hakutaka

kutengana naye baada ya kujua kuwa

alikuwa amenyweshwa dawa na Lina.

Hata hivyo, hakuweza kuondoa fundo

lililokuwa moyoni mwake. Bado alihitaji

muda. Sura ya 139

“Lisa Jones, kama kweli unanipenda, usiende kwa Kelvin Mushi tena. Hii ni nafasi ya mwisho ninayokupa.” Alvin alimtazama kwa kina, sauti yake

ikisikika kwa ukali na kishindo.

Lisa alipigwa na butwaa. Ingawa alimchukia na kumkasirikia, bado moyo wake ulimpenda. "Na wewe je? Unanipenda?" Ikiwa alimpenda, kwa nini

aliita jina la mwanamke mwingine wakati alikuwa amelewa?

"Naweza kukupenda, na ninaweza kuacha kukupenda wakati wowote."

Alvin alisema bila kujali kabla ya kugeuka kuondoka.

Lisa alikaa kitandani huku akishangaa

kidogo. Alvinaliweka wazi kuwa upendo

wake unaweza kubadilika wakati

wowote. Je, ni kwa sababu

hakumpenda vya kutosha?

Katika chumba chake cha maktaba, Alvin alisimama mbele ya dirisha akiwa

na glasi ya divai nyekundu, akitazama nje ya dirisha matone ya mvua

yakishuka chini taratibu. Alitumaini kwamba Lisa alimuelewa. Ndio, ingawa

alimpenda, ikiwa angetaka kuendelea kujihusisha na Kelvin Mushi, basi

angeweza tu kuachana na upendo huo. Ingawa Kelvin alikuwa ameokoa maisha

yake, Alvin alikuwa ameokoa maisha yake mara nyingi zaidi. Asingeweza

kuvumilia kumuona mwanamke wake

akimlipa fadhila kwa kumhudumia

hospitali. Alvin alikunywa divai nyekundu kwa machungu.

Hans alisimama nyuma yake kimya.

“Bwana Kimaro, kwa nini hukumwambia

Bi Jones kuhusu picha hizo?”

“Kuna faida gani kumwambia? Je, angeniamini? Kelvin Mushi ndiye

mwokozi wake sasa. Atafikiri kwamba

ninamsingizia kwa makusudi kwa sababu simpendi,” Alvin alidhihaki. Hans alikuwa kimya. Ilibidi akubali

kwamba Kelvin Mushi alikuwa amedhamiria sana. Ili kumlinda Lisa, hata alitoa sadaka maisha yake. Ikiwa hata yeye angelikuwa mwanamke, angeliguswa pia.

Usiku sana, Lisa alioga na kukaa kitandani huku akiwa ameduwaa.

Mwishowe, alichukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Pamela, akimwomba aende hospitali kumuona Kelvin kwa niaba yake.

Pamela : [ Usiniambie! Kelvin Mushi

alipoteza figo kwa ajili yako?

Nini unadhani; unafikiria nini?

Usichanganyikiwe tu, sawa?]

Lisa: [ Sikuwahi kufikiria kwamba angefanya hivyo. Nina deni kubwa kwake. Sitaweza kumlipa maisha yangu yote.]

Pamela : [ Hapana, usifikirie sana juu yake. Chukulia tu ni ajali ya kawaida. Ninapanga kumleta Patrick nyumbani kwa Krismasi. Kisha nitaandamana naye hadi kwa familia ya Jackson katika Mkesha wa Mwaka Mpya.]

Lisa: [ Nyinyi watu mmesuluhisha matatizo yenu?]

Pamela : [Nilimchunia kwa nusu mwezi, na aliniahidi kukutana na Linda haraka

iwezekanavyo katika siku zijazo. Nitamtambulisha mpenzi kwa Linda pia.

Nataka kumpa Patrick nafasi moja zaidi.

Ninampenda kupita kiasi. ]

Lisa: [ Hongera kwa kumpata tena Bwana wako.]

Alipotuma tu ujumbe huo, mlango wa chumba cha kulala ulifunguliwa. Mkono wake ulitetemeka, na akazima skrini bila fahamu kabla ya kuweka simu chini.

“Unachat na nani?” Alvin alitoa harufu ya mvinyo mwekundu, na uso wake wote uliwaka kwa hasira. “Nionyeshe simu yako.”

Lisa hakuamini. Alvin hakuwahi kuangalia simu yake hapo awali, lakini alikataa kumpa kabisa. "Alvin, usiende mbali sana."

unawasiliana na Ethan Lowe au Kelvin Mushi nyuma yangu?” Alvin hakuwahi

kuwapenda wanaume ambao

walisisitiza kuangalia simu za wanamke

wao, lakini alipoona tabasamu kwenye midomo ya Lisa mapema, moyo wake

ulikosa raha ghafla. Alipaswa kuwa na uhakika Lisa alikuwa anachat na nani!

Lisa hakuwahi kufikiria kwamba

uaminifu kati yao ulikuwa umeshuka sana. Hata hivyo, huenda

asingemuelewa tena ikiwa angeona

yaliyomo kwenye simu yake, kwa hiyo

alisema tu waziwazi, “Nilikuwa niachat na Pamela . Alikuwa akizungumza

kuhusu mpenzi wake. Pia… ataenda

hospitali kumwona Kelvin. Siwezi

kwenda mwenyewe, lakini marafiki

zangu wanaweza kwenda kwa niaba

yangu.” Alitazama kinyonge jinsi sura

nzuri ya Alvin ikibadilika na kuwa mbaya

kwa hasira iliyoonekana waziwazi kwa

"Mbali sana? Nitajuaje kama

macho. Moyo wake ulihisi kuchoka ghafla. “Lisa Jones, wewe ndiye uliyekuwa unachat na Kelvin Mushi? Ni kitanda changu unacholala sasa ujue.” Alvin alichukua simu yake na kuivunjavunja ukutani. Kelele kubwa ilimfanya Lisa kuziba masikio yake kwa hofu.

Alvin aliinua mikono yake na kumkandamiza kitandani, akimbusu kwa nguvu kwenye mdomo. "Niambie, busu langu linakupendeza zaidi, au busu la Kelvin Mushi ndilo tamu zaidi?"

Akambusu kana kwamba ana wazimu.

Lisa alikuwa akiumia tu kutokana na busu hilo na kumsukumia mbali, lakini hakuweza kumzuia hata kidogo.

Alvin alikuwa amekunywa nusu chupa ya divai nyekundu katika chumba chake

cha maktaba. Ubabe wake ulionekana

kuongezeka mara moja. Alipokumbuka

busu lake na Kelvin, macho yake

yakawa mekundu huku akimbusu zaidi.

"Alvin unaniumiza bwana." Lisa alikwepa kwa maumivu.

“Kwanini unakwepa busu langu?

Unatamani ningekuwa Kelvin badala yake?” Alvin alikuwa tayari amezidiwa na moto wa wivu. Akararua nguo yake ya kulalia kwa nguvu. "Au aliufanya

usiku huo kuwa usiosahaulika sana, ndio maana umeenda naye kituo cha polisi leo? Huwezi kumwacha kabisa?”

Lisa aliogopa sana. Haraka haraka

akamshika mkono na kutikisa kichwa bila msaada. “Hapana, nimechoka.

Ninaogopa leo sitaki…”

“Hutaki kwa sababu ni mimi, sivyo?”

Alvin alicheka ghafla. “Akili yako imejaa

Kelvin Mushi sasa. Ungekuwa tayari

kama angekuwa yeye, si ndiyo?"

“Mbona unaendelea mbali sana Alvin, hutaki kunielewa kwanini?” Lisa alijisikia

kuchoka sana na kukata tamaa.

Alikaribia kufa siku hiyo, lakini hakumjali hata kidogo. Alijua tu jinsi ya kumtilia shaka.

Alitabasamu kwa huzuni na hakuhangaika tena, akamwacha afanye anavyotaka. “Sawa, fanya tu kama unataka. Fanya chochote unachotaka.”

Machozi yake yalimtoka kwenye pembe za macho yake na kutiririka kwenye nywele zake. Macho yake yalikuwa hafifu.

Siku zote alikuwa akitiliwa shaka, kukanyagwa, na kudhalilishwa naye, lakini bado alikuwa binadamu.

Mwili wa Alvin ukakakamaa kana

kwamba alipigwa ghafla kichwani.

Kwanini amekuwa hivi? Ilikuwa ni kama

amekuwa pepo. Hakuweza kujizuia kwa

mwanamke? Kweli alipoteza busara

kwa sababu ya mwanamke? Aligeuka na kukimbilia bafuni. Maji baridi

yakamwagika juu ya mwili wake, na ghafla akajichukia. Alipotoka kuoga, Lisa alikuwa amelala chali pembeni ya kitanda, mtupu kabisa hana chochote baada ya nguo zake kularuliwa na Alvin. Kama kware mdogo, alijikunyata, hana

msaada wowote, tayari kukwakupaliwa na mwenye mwenye njaa kali!

Alvin hakufanya chochote tena, alilala

upande wa pili wa kitanda kimya! Wawili

hao walitenganishwa kwa umbali, lakini

hakuna aliyemkaribia mwenzake.

Hakujua kuwa Lisa ambaye alikuwa

amemrudisha nyuma kimawazo

machozi yalikuwa yakimtoka. Hakupata

usingizi mpaka ilipofika usiku sana.

Kulipopambazuka, Alvin aliamka, lakini

Lisa hakuwapo tena kitandani. Haraka

akainuka na kushuka chini. Lisa alikuwa

amekaa kwenye meza ya chakula

akinywa uji wake wa ulezi. Macho ya Alvin yalilegea kidogo, na akashuka

haraka. Aliketi kando yake na kuuliza

kwa ukali, "Kiamsha kinywa changu kiko wapi?"

Sura ya 140

“Bwana Kimaro, kifungua kinywa chako kimefika.” Shangazi Linda alitoka na kifungua kinywa alichotengeneza.

Alvin akakitazama, na uso wake ukachukizwa mara moja. "Lisa Jones, kwanini hukuniandalia kiamsha kinywa?"

"Wewe ndio ulisema chakula changu ni kichafu kama mimi." Lisa alimtazama

kwa utulivu. Siku zote alikuwa hivi.

Alipomuelewa vibaya, alimdhalilisha

kwa kumwambia chakula chake ni

kichafu na asimpikie tena, lakini sasa

alitaka apike tena. Je, hakuchoka kumnyanyasa? "Nitengenezee sasa hivi." Uso wa Alvin ulikuwa mbaya kwa hasira.

"Hapana. Mimi siyo yaya wako.” Lisa alisimama baada ya kumaliza uji wake. "Naenda kazini."

Alvin aligeuka na kuongea na Shani aliyekuwa amesimama mlangoni.

“Mfuate kwa karibu. Akithubutu kwenda hospitali, mpige na umrudishe hapa.”

"Mimi sio mtumwa wako." Macho ya Lisa yalikua mekundu kwa hasira.

Tayari alikuwa ameamua kutokwenda hospitali, lakini bado alisisitiza kumlazimisha kumwekea mlinzi wa kumchunga. "Alvin Kimaro, usiende mbali sana."

“Kwa kuwa ulinichanganya, unapaswa

kuwa tayari kuwa mtumwa wangu.

Hakuna anayeweza kwenda kinyume na mimi.” Alvin hakujieleza sana, lakini maneno yake yalitosha kudhihirisha

hasira zake.

Lisa alichukua mkoba wake na kuondoka huku Shani akimfuata.

Njiani kuelekea ofisini kwake, haijalishi

Lisa aliendesha gari kwa haraka vipi, Shani alikuwa makini naye muda wote.

Kwenye maegesho, Lisa alishuka

kwenye gari na Shani akamfuata kwa

nyuma kwa kasi.

“Shani, unaweza kuacha kunifuata?

Sitaenda hospitalini.” Lisa alitmwambia

Shani kwa upole. Kwa kweli, hakuwa na

shida yoyote na mlinzi yule.

"Samahani, hili ni agizo la Bwana
Kimaro, bosi wangu."

“Agizo ni la Alvin, lakini usalama ni wa

kwangu. Najua namna ya kujilinda mwenyewe!” Lisa mwishowe alikasirika.

“ Sawa, Alvin alikuajiri? Anakulipa kiasi gani? Mimi nitakupa mara mbili." Lisa

akatoa kadi kwenye begi lake.

Shani hakujali. “Bi Jones, haijalishi

unanipa kiasi gani. Nilifunzwa na familia

ya Kimaro. Ninafanya kazi kwa ajili yao

tu.” Lisa alipigwa na butwaa. Je, familia

ya Kimaro ilikuwa na watu wengi kama

Shani? Familia ya Kimaro ilionekana

kuwa na mambo mengi zaidi kuliko vile alivyofikiria. “Kwa hiyo lazima umekuwa na Alvin kwa muda mrefu. Kwa maana

hiyo unamjua mtu anayeitwa Sarah?”

Hali ya wasiwasi ikaangaza kwenye

macho tulivu ya Shani. Ingawa lilitoweka

hapo hapo, Lisa bado aliliona vizuri.

“Nilimsikia Alvin akimzungumzia siku

moja akiwa amelewa. Lazima awe

mpenzi wake wa zamani. Walikuwa wanapendana sana?"

“Bi Jones, hayo yote ni ya zamani. Bwana Kimaro ana wewe tu moyoni mwake sasa,” Shani alisema haraka.

"Ndio hivyo?" Lisa alitabasamu kwa kujidharau. Alikuwa akimpima tu Shani, lakini jibu la Shani lilimhakikishia kwamba kweli Alvin alikuwa na mpenzi wa zamani anayeitwa Sarah. Alimwita jina lake wakati alikuwa amelewa. Je, iliwezekanaje kuwa Lisa ndiye pekee moyoni mwake sasa?

“Shani, asante kwa kuniambia hivi.”

Aligeuka na kwenda juu ofisini.

Shani alimfuata kinyonge. •••

Siku iliyofuata, saa kumi na nusu jioni, Pamela alitoka hospitali baada ya

kumtembelea Kelvin, akihisi huruma

moyoni mwake.

Kama asingekuwa amekosea na

kumchanganya Alvin na Kelvin hapo

mwanzo, huenda Lisa na Kelvin

wangekuwa tayari wameoana. Hapo

Kelvin asingepoteza figo pia. Hata

hivyo, haikufaa kujutia juu ya maziwa yaliyokwishamwagika sasa.

Akatoa simu yake na kumpigia Patrick.

“Patrick, unakwenda kuwachukua

wazazi wangu, au unaenda moja kwa

moja kwenye Mgahawa tuliokubaliana kukutana?”

“Niko na mkutano ofisini ambao

unaweza kuendelea hadi saa kumi na moja na nusu. Nitaenda huko moja kwa

moja baadaye. Nisaidie kuomba radhi

kwa wazazi wako kwa ajili yangu,”

Patrick alisema kwa sauti ya upole.

“Ni sawa, lakini usichelewe. Baba yangu

anachukia watu ambao hawatimizi

ahadi zao.” Pamela alimuonya kwa

upole. “Usijali, ni suala la maisha yangu. Hakika sitachelewa. Tayari

nimekuandalia zawadi ambayo wazazi

wako watapenda. Tutafunga ndoa

mapema, nami nitakuwa mumeo.”

Patrick akatabasamu kwa dhati. Moyo

wa Pamela ulikuwa mtamu alipokuwa akimsikiliza.

Baada ya kukata simu, Pamela

aliendesha gari kuwachukua wazazi

wake kisha akaenda Mambo Garden

Restaurant. Ilikuwa saakumi na moja

kamili jioni alipofika. Baada ya kuagiza

chakula, kaka yake Forrest alifika. Saa

kumi na mbili jioni bado Patrick alikuwa

hajafika. Babake Pamela alikosa subira, akasema, “Kwa nini bado hajafika? Si

sawa kutufanya wazee tungojee.”

Pamela alisema, “Baba, ni saa za jioni sasa. Pengine kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani.”

Mama yake aliitikia kwa kichwa na kukubali. “Wafanyabiashara wana mambo mengi ya kushughulikiwa mwishoni mwa mwaka, hiyo inaeleweka. Kuwa na subira zaidi.”

Pamela alimpigia simu Patrick, lakini hakupokea, akajifariji. "Lazima asipokee kwa sababu yuko barabarani, atakuwa karibu tu hapa."

Baada ya nusu saa nyingine, Patrick hakutokea tu. Baba yake alikasirika. “Ni mara yake ya kwanza kukutana nasi lakini anatuletea dharau namna hii. Hata ukimpigia simu ni bure. Sidhani kama yeye ni mkweli hata kidogo. Sitakubali kukuruhusu uolewe naye.”

Wakati huu, mama yake hakusema

chochote, na Forrest pia alikuwa na uso wa kukata tamaa. “Achana naye. Sio

kama hakuna wanaume wengine ulimwenguni."

Pamela alihudhunika. Mbele ya

shutuma za familia yake, alijilazimisha kutotoa machozi. Yeye tu alijisikia

kukata tamaa sana kwa aibu. Zamani, alimuahidi mara nyingi, lakini sasa, hata

alikosa mkutano wa kwanza pamoja na wazazi wake. Je, alimpenda kweli?

Mama yake akasema. “Pamela, jambo

la muhimu zaidi katika maisha ya mwanamke ni kupata mwanaume

ambaye ni mzuri kwako kwa moyo wote.

Bado wewe ni mdogo, kwa hivyo

usikimbilie kuolewa. Sasa, tule. Chakula

kinakuwa baridi.” Wakati wote wa

chakula, ilikuwa kama anatafuna nta.

Mpaka mwisho, Patrick hakutokea, wala

hakupiga simu hata mara moja

kuelezea shida ni nini.

Baada ya kuachana na familia yake, Pamela aliendesha gari hadi ofisini kwa

Patrick. Ofisi yake ilikuwa tayari

imefungwa. Alianza kuhisi wasiwasi

kidogo. Alikuwa na wasiwasi kwamba

huenda Patrick alikuwa amepata ajali ya

gari au kitu kibaya. Hata hivyo, hakujua

namba za wazazi wa Patrick. Baada ya

kusita kwa muda, alimpigia simu Linda.

Hakutarajia kuwa mtu aliyemjibu

angekuwa ni mwanamume ambaye

sauti yake aliifahamu vizuri. “Habari, Pamela…”

Pamela alitazama sura yake iliyokuwa na ukungu kwenye dirisha la kioo mbele

yake na ghafla akacheka peke yake. Je,

alionekana kama mjinga? “Kwa nini

hukupokea nilipokupigia simu? Na

mbona unapokea simu ya Linda?”

“Pamela, samahani. Linda alipata ajali

ya gari jioni. Niko hospitalini sasa. Nilisahau kabisa hata kuchukua simu yangu ofisini,” Patrick alisema kwa hatia, “Oh, nimechelewa sana?

Mmemaliza kula? Tafadhali mwambie baba na mama smahani kwa kushindwa kuja.

Nitawaalika kwenye chakula cha jioni wakati mwingine.”

"Hakuna haja tena," Pamela alisema kwa sauti isiyo na maana.

"Pamela, ilikuwa ni dharura wakati huu ..." “Ndiyo, kila kitu kuhusu Linda ni dharura. Kwani amekufa? Kilema?

Kwani hana wazazi tena, ana wewe tu?"

Moyo wa Patrick ukasisimka. "Pamela, unawezaje kusema maneno kama haya? Kwani Linda alitaka kupata ajali?

Hata kama humpendi, unapaswa angalau umuonee huruma.”

Pamela alidhihaki. “Sawa, nimekuuliza swali. Kwani amekufa? Amepooza?

Mlemavu?”

Sura ya 141

“Umemaliza?” Patrick alikasirika.

"Yuko sawa kabisa, sivyo?" Pamela alielewa kila kitu sasa. “Patrick, niko serious. Usirudi kwangu tena baadaye. Tunaachana.”

"Inatosha. Unapaswa kujua ni mistari gani hupaswi kupita.”

“Imekwisha. Utakuwa na Linda tu machoni pako. Ndio, unaweza kwenda upande wa Linda ikiwa amepata ajali, lakini huwezi kuonana kabisa na familia yangu. Hukunipigia hata simu. Leo

ilikuwa siku muhimu kwetu, lakini haujali

hata kidogo. Katika siku zijazo, sitakuwa na matarajio zaidi kwako, na sitatumaini

chochote pia. Natumai hatutakutana tena.” Pamela akakata simu na kuuzika

uso wake mikononi huku akilia kwa uchungu.

Baada ya kulia alifuta kabisa

mawasiliano ya Patrick na Linda.

Alikuwa amechoka sana kuteswa na

watu hao wawili. Ilikuwa ni bora

asingekuwa na matarajio, matumaini, na

asingekuwa na maumivu. Wakati huo, alitaka kutafuta mtu wa kunywa na kuzungumza naye. Alitaka kumpigia simu Lisa, lakini akakumbuka kuwa Lisa

hakuwa huru sasa. Kwa hivyo, aliendesha gari hadi baa mwenyewe.

Baa zote za Masaki zilikuwa katika

barabara moja. Kulikuwa na baa chache tu ambazo watoto matajiri wangetembelea.

•••

Saa

tano usiku, Sam na Alvin walishuka

kutoka kwenye chumba cha juu cha

jumba lake. Baada ya kula chakula cha

jioni usiku huo, Alvin hakutaka kurudi

nyumbani kwake, kwa hivyo Sam

aliongozana naye kwenye baa tena.

Lakini, Alvin hakunywa sana siku hiyo, labda kwa sababu alikuwa amechoka kwa kulewa jana yake.

"Alvin, unarudi Nairobi kwa ajili ya mwaka mpya? Kama utakuwepo, babu yangu alikuomba uje kwetu,” Sam

alisema huku akitembea. Alipotazama pembeni, mara akamuona mwanamke

ameketi kando ya baa hiyo. Alivaa koti la pamba la rangi ya manjano lililofifia

lililosaidiana na ngozi yake nzuri, na

nywele zake ndefu za mawimbi

zilining'inia kwenye mabega yake. Hata hivyo, alionekana kulewa kabisa.

Wanaume wawili waliokuwa kando yake

waliendelea kumvutavuta na kumsumbua.

“Siyo Pamela Masanja yule? Mbona anakunywa peke yake hapa?” Sam na

Pamela walikuwa wamekutana mara

kadhaa hapo awali, na alikuwa na

mtazamo mzuri juu yake. Alikuwa msichana mchangamfu na

anayejitambua na hakuharibiwa na mambo ya kupita. Alvin alimtazama na

kumtambua kuwa ni rafiki mkubwa wa

Lisa. Akasugua macho yake. Ikiwa kitu

kingetokea kwa rafiki yake, bila shaka

Lisa angekuwa na wasiwasi. "Nenda

ukawaondoe hao watu wawili."

Sam mara moja akasogea na kuwashika wale watu waliokuwa

wakipepea mgongoni mwa Pamela.

“Wewe sh*t... Bwana Harrison…”

Mwanaume huyo aliuona uso wa Sam

waziwazi na kumkoromea.

“Ondoka machoni mwangu mara moja.

Huyu ni rafiki yangu. Nitamuua yeyote

atakayethubutu kumgusa siku yoyote,” Sam alionya na kumpiga teke.

Wanaume hao wawili wakakimbia mara moja. Kila mtu alijua kuwa neno la Sam Harrison lilikuwa sheria kwenye baa za eneo hilo. Kumkasirisha ilikuwa ni sawa na kujitakia kifo.

“Pamela, njoo, twende. nitakupeleka nyumbani.” Sam alimsaidia Pamela kuinuka. Pamela alimuegemea huku akiyumbayumba kwani alikuwa

amelewa sana asiweze kutembea kwa usawa. Mdomo wake bado ulikuwa ukipiga kelele, “Siendi nyumbani! Bado nataka kunywa! Siku njema ya kutengana! Ni kwa kuagana na wabaya tu ndipo utakutana na walio sahihi…”

Sam alimsaidia kumkokota hadi kwenye gari, akionekana kuwa na huzuni.

“Mwanamke huyu ameachwa na mpenzi wake, sijui amekunywa kiasi gani?'

"Unakaa nyuma." Alvin alikwenda kwenye kiti cha mbele cha abiria, hivyo

Sam aliweza kukaa tu nyuma na Pamela. Hans akaendesha.

Mara baada ya Sam kuingia kwenye gari, Pamela alimshika kola na kumkaripia.

“Patrick Jackson, wewe b*stard, wewe *sshole! Nilikupenda kwa miaka minane, lakini una Linda tu machoni pako. Wewe ni kipofu?”

Mara Pamela akacheua kwa nguvu

kama anataka kutapika, lakini hakutapika. Akaendelea tu kuongea kilevi. "Nakulaani kuwa utasalitiwa na kila mwanamke katika maisha yako yote."

Sam alipigwa butwaa. "Pamela

Masanja, angalia kwa karibu. Mimi ni Sam Harrison.”

"Nani Sam Harrison?" Pamela aliinamisha kichwa chake. “Sijawahi kusikia habari zako. Unajaribu kuniteka nyara kwa sababu mimi ni mrembo sana?”

Sam alikosa la kusema na akamwelekeza mbele. “Unamfahamu

Alvin Kimaro? Ni mpenzi wa rafiki yako mkubwa, Lisa Jones.”

Pamela alimtazama kwa butwaa, na macho yake yakaangaza ghafla. “Oh, ni mjomba. Habari, Mjomba.”

Alvin akasugua macho yake. Pamela alikuwa akimuita kwa jina hilo la kipuuzi kila alipokuwa amelewa .

Lakini, Sam alicheka. “Umekosea. Yeye si mjomba wako.”

“Sijakosea. Yeye ni Mjomba.” Pamela

alitikisa mkono wake. “Sijakosea

kamwe. Ni yule mpuuzi mjomba wa Ethan Lowe. Mimi na Lisa tulikuona mara ya kwanza tukiwa kwenye baa.”

Alvin alikunja uso na kuuliza kwa sauti ya chini, "Mbona umenikazia macho?"

"Lisa alitaka kuolewa na wewe kulipiza

kisasi bila shaka. Ikiwa Lisa angeweza kuwa shangazi ya Ethan, hakika hilo

lingemkasirisha hadi kufa. Inaweza pia kusababisha ghasia katika familia ya Lowe, haha.” Pamela alikuwa amelewa kabisa akiropoka hovyo. “Oh, ngoja, wewe si mjomba wa Ethan. Sorry!

Nilikosea. Nimekuchanganya tena kama

nilivyochanganya kumwelekeza Lisa.

Yaani nikinywa pombe tu nakuonaga

kama mjomba wake Ethan sijui kwanini, hahahaaa…nisamehe sana mjomba!”

Macho ya Alvin yalizidi kuwa meusi

huku akisikiliza, Sam akameza mate

akihisi amepata siri kubwa.

“Vipi uliishia kunifananisha?” Alvin

alijaribu kulainisha sauti yake.

“Ninafanana na mjomba wako?”

"Sina mjomba." Pamela alionekana

mjinga. Baada ya muda, alijichanganya tena, "Mjomba, unapaswa kuwa mzuri

kwa Lisa. Usiwe na hasira naye. Ni mimi

niliyemtia moyo kukutumia dawa za

kulevya. Kwa kweli haikuwa na uhusiano wowote na Lisa… ” Kisha,

aliegemea mlango kwa butwaa na kulala. Ndani ya gari, iwe Hans aliyekuwa

akiendesha gari au Sam aliyekuwa

amekaa nyuma, wote wawili walihisi joto

la mle ndani lilikuwa limeshuka hadi

kufikia kiwango cha baridi. Baada ya

kuendesha gari kwa dakika tano, Alvin

ghafla alisema, "Simamisha gari."

“Alvin.” Sam alikuwa na wasiwasi kidogo. “Umechelewa sana, twende nyumbani kaka.”

"Ninahitaji kufikiria juu ya kitu pekee

yangu. Nyie mrudisheni kwanza.” Sauti ya Alvin ilikuwa ya nguvu.

Hans aliweza tu kusimamisha gari. Alvin

akatoka nje, akafunga mlango na kutembea peke yake kando ya barabara. Sam akahema. Ingawa kile

Pamela alisema hapo awali hakikuwa

wazi, alikuwa na dhana isiyo wazi juu ya kile kilichotokea.

Aliweza tu kupata picha kwamba

kutokuelewana kati ya Alvin na Lisa

kulisababishwa na mkanyiko huo wa awali. Maskini Alvin!

Sura ya 142

Katika jumba la kifaharila Alvin, Lisa

alitazama tena wakati. Ilikuwa saa sita

na nusu usiku, lakini Alvin alikuwa bado

hajarudi. Je, alienda kunywa nje tena?

Kwa kweli hakutaka kumjali na alitaka

kumpuuza tu, lakin alishindwa kuudhibiti moyo wake. Bila yeye, hakuweza kulala

hata kidogo.

Ghafla, sauti ya mlango kufunguliwa ikasikika kutoka chini. Haraka akajilaza

na kujifanya amesinzia. Dakika chache baadaye, mlango ulifunguliwa, na hatua za miguu zikakaribia kitanda. Aligundua kuwa Alvin alisimama kando yake.

Moyo wake ukasisimka.

Ghafla, taa ikawaka. Kisha, blanketi juu ya mwili wake lilitolewa. Sauti ya mwanaume huyo ilisikika kutoka juu yake. "Simama."

"Alvin, unafanya nini sasa?" Lisa aliketi

kwa uchovu na kumtazama. Macho ya

mwanamume huyo yalikuwa mekundu

kama damu na kumfanya aonekane

mwenye sura ya kutisha.

Alvin alimtazama usoni Lisa

aliyeonekana kutokuwa na hatia. Bado alikumbuka waziwazi mara ya kwanza

alipokutana naye, pamoja na kila neno na kila usemi wa hila aliosema. “Ngoja nikuulize. Kwanini ulinitongoza kule kwenye baa?”

“Mbona unauliza hivyo ghafla?” Lisa

alikwepa macho yake, hakutaka kujibu swali hilo.

Hata hivyo, Alvin hakumruhusu kujificha na kumshika kidevu chake. Macho yake malegevu yalifungwa kabisa na macho makali ya Alvin. "Ilikuwa ni kwa sababu ulinidhania kuwa mimi ni mjomba wa Ethan Lowe?"

Sauti ya Alvin ilionekana kusikika katika

ubongo wa Lisa kana kwamba alikuwa

amepigwa na radi. Akili ya Lisa ilikuwa

imepotea. Alvin alijuaje kuhusu hilo?

Alvin alimtazama na kuona wazi

mabadiliko yote katika sura yake. Uso wake ulibadilika rangi. Kulikuwa na hofu, mshtuko, na wasiwasi mkubwa machoni pake. Moyo wake pia uliongezeka mapigo inchi kwa inchi.

Alvin alijihisi kana kwamba alikuwa mpumbavu tu. Aliamini kwamba Lisa alimpenda mara ya kwanza tu alipomuona. Alifikiri kwamba alikuwa na uwezo mkubwa katika uhusiano huo, lakini alikuwa akichezewa naye tangu mwanzo. Mapenzi yake yote yalikuwa ya uwongo. Utamu wake wote ulikuwa bandia. Kila kitu kizuri kilikuwa bandia.

Hata hivyo, moyo wake uliguswa sana na mwanamke huyo mnafiki.

“Hapana… Hiyo si…” Lisa alishikwa na butwaa na hakujua la kusema.

"Mipango yako inanifanya niwe

mgonjwa sana." Alvin akamtikisa na kuufuta mkono wake kwa kitambaa

kana kwamba amegusa kitu kichafu.

Lisa alichomwa sana na matendo yake. “Sawa, nakubali. Ilikuwa kweli

mwanzoni, lakini baadaye"

"Kisha ulikutana na Kelvin Mushi

kwenye sherehe ya uchumba ya Ethan

Lowe na ukagundua kuwa mtu huyo

ndiye mjomba halisi wa Ethan, kwa

hivyo ndiyo maana mara moja ukaanza

kudai talaka, sivyo?"

Alvin alikuwa tayari ameshafahamu kila

kitu. Hakutambua hapo awali, lakini

sasa aligundua kwamba kulikuwa na kila aina ya mambo ambayo yalikuwa ya

kutiliwa shaka. "Kwa bahati mbaya,

baadaye ulifanyiwa njama na familia ya

Jones Masawe na ulikuwa karibu

kwenda jela. Hakuna mtu ambaye

angeweza kukuokoa, hivyo rafiki yako wa karibu angeweza tu kuja kuniomba na kuendelea kunidanganya, akiniacha nifikiri kwamba ulinipenda kweli.”

Midomo ya Lisa ilikuwa imepauka. Kwa kweli alikuwa na akili sana. Kila kitu kilikuwa kama alivyokisia. “Ndiyo, lakini uliponiokoa kwenye eneo la ujenzi, niliguswa moyo sana nawe.”

"Funga mdomo wako. Hakuna ukweli katika chochote kinachotoka kinywani mwako wala rafiki yako wa karibu."

Alvin alizidi kupandwa na hasira huku akiongea. Alishindwa kujizuia na kumkandamiza kitandani huku akiikaba shingo yake kwa nguvu.

“Hata kama hukuleweshwa na Lina

Jones kwenye hoteli usiku ule, ungetaka

kulala na Kelvin Mushi hata hivyo, kwa hiari yako mwenyewe. Yaani mimi

unanipetipeti tu kisha unaenda kulala na Kelvin, si ndiyo?”

"Kweli mimi ni mtu wa namna hiyo moyoni mwako?" Alipokuwa akibanwa, hakuweza kupumua. Upande huu wa Alvin ulimtisha sana.

“Si wewe? Nilitaka kulala nawe hapo awali, lakini uliendelea kunikatalia.

Baadaye, ulipogundua kuhusu utambulisho wangu wa kweli, mara

moja ulitaka kulala na mimi. Inasikitisha kwamba picha hizo zilinifanya nitambue

kabisa sura yako halisi. Unajua kwamba mtu wa mwisho aliyeniudhi tayari

amekwisha kwenda kuzimu?”

Alvin alikuwa kama mnyama mwenye hasira. Nguvu za mikono yake

ziliongezeka.

Uso wa Lisa ulikuwa mwekundu, machozi yaliendelea kumtoka. Nuru ya macho yake ikawa nyeusi, naye akafikiri

ya kwamba alikuwa karibu kukosa hewa na kufa. Alvin akamsukuma na kuupiga mto uliokuwa kando yake kwa nguvu.

Macho yake yaliyokuwa na damudamu yalimtazama. "Sitakuua kwa sababu sitaki kuchafua mikono yangu." Kisha, akafunga mlango kwa nguvu na kutoka chumbani.

Lisa alikumbatia magoti yake na kuzika

kichwa chake ndani yake. Moyo wake ulijihisi mtupu. Pengine, yote yalikuwa ni bahati mbaya tangu mwanzo. Lisa

alikuwa amemwendea Alvin kwa nia

chafu. Baada ya hapo, alimdanganya tena na tena ili atoke jela. Sasa kwa

kuwa uwongo wake ulikuwa wazi, uhusiano wao ulikuwa kama povu

ambalo lingepasuka kwa kuguswa

kwake. Lisa hakupata usingizi usiku mzima.

Aliamka mapema na kumuandalia Alvin

kifungua kinywa. Pengine kingekuwa kifungua kinywa cha mwisho alichomtengenezea Alvin.

“Mbona umeamka mapema sana? Ni saa kumi na mbili na nusu tu” Aunty Linda aliingia jikoni huku akipiga miayo.

Alipouona uso wa Lisa uliopauka, alipigwa na butwaa. “Jana usiku hukulala? Huonekani vizuri sana.”

"Anti Linda, haya ndio mapishi niliyoandika jana usiku." Lisa hakujali

kile Aunty Linda aliuliza bali alimwambia yake na kumkabidhi kijitabu. "Haya

ndiyo baadhi ya mapishi anayopenda sana Alvin. Yeye ni mbaguzi sana, kwa hivyo ninaweza kuhitaji kukusumbua ili

kumpikia katika siku zijazo.”

"Unamaanisha nini?" Shangazi Linda

alishtuka. Alijua kuwa wote wawili

walikuwa kwenye mzozo mkali muda

huo lakini migogoro ilikuwa ya kawaida

kati ya wanandoa. “Haraka weka mbali

hayo mawazo. Bwana Kimaro anapenda upishi wako. Hata nikipika

vizuri hataki kula chakula changu.”

"Hakuna jinsi… sioni namna nnyingine tena." Lisa alitoa kicheko cha

kujidharau. Kwa mtazamo wa mambo wakati huu, hakuthubutu kutarajia

kwamba angeweza kuendelea kukaa ndani ya nyumba hiyo.

Hata kama yeye mwenyewe alimwambia Alvin kwamba alikuwa

akimpenda, asingeamini pia. Angefikiri tu kwamba anapendezwa naye yote

kwa sababu tu ya utajiri wake alioufahamu. Isitoshe, walikuwa

wamepoteza imani katika kila mmoja

wao. Ikiwa wangebaki pamoja, huenda wasingeweza kuishi kwa furaha.

alikataa kupokea kijitabu hicho. Kwa

hayo, aligeuka na kuondoka. Lisa

“Usiongee ujinga.”
Shangazi Linda

hakuwa na la kufanya zaidi ya kukiweka

kwenye kabati la jikoni huku akiamini

kuwa Aunty Linda angekiona.

Asubuhi hiyo, aliweka juhudi nyingi

katika kuandaa kifungua

kinywa. Kifungua kinywa cha siku hiyo

kilikuwa sawa na kifungua kinywa cha

kwanza walichopata walipoanza kuishi

pamoja.

Saa mbili kamili asubuhi, Alvin alishuka

akiwa amevalia sweta jeusi na suruali

nyeusi. Kwa umbo lake refu, hakuwahi

kushindwa kufanana na mtu mashuhuri

aliyependeza na kung’ara bila kujali

alivaa nini. Lakini, uso wake tu ndiyo

ulitisha zaidi. Macho yake meusi

yalikuwa makali kama ncha ya mkuki, na kumfanya Lisa kutetemeka.

Shangazi Linda alitaka wapatane, hivyo

akatabasamu na kusema, “Bwana

Kimaro, Bi Kimaro aliamka mapema

sana saa kumi na mbili asubuhi ili

kukuandalia kifungua kinywa. Hata hakuniruhusu nimsaidie. Angalia kupikia

kwake"

“Anti Linda, endelea na unachohitaji kufanya kwanza,” Alvin akakatisha sentensi yake.

Aunty Linda akahema. Hakuwa na budi ila kuondoka. Sebule ya nyumba ilibaki na wao wawili tu. Charlie na wanae watatu walikuwa wakicheza kwenye

kochi. Alipowaona wakicheza kwa

furaha, Lisa alijawa na wivu wenye

huzuni. Alitamani bora kuwa paka

mwenye furaha muda wote kuliko

mwanadamu aliyeandamwa na matatizo tu, kwa kuzingatia maisha yasiyo na presha ya paka wale.

"Tia saini hii." Alvin akatupa hati kwenye meza ya chakula. Maneno

yaliyoandikwa ‘Divorce Agreement’

(Makubaliano ya Talaka) yalimtoboa macho Lisa. Alivuta pumzi kwa upole, lakini bado aliweza kuhisi maumivu.

Kwa kweli, bado alikuwa akimpenda. Wakati picha za Kelvin na yeye zilipofichuliwa kabla ya hilo jingine kuzuka, hakuwa ametaja nia yake ya kutengana naye au kumtaliki.

“Isaini. Nitamwomba mtu ashughulikie suala la talaka yetu.” Alvin akatazama pembeni. Kadiri alivyokuwa akiutazama uso wake wa kinafiki, ndivyo ilivyozidi

kumkumbusha jinsi alivyomdanganya kama mjinga.

Jana yake usiku, alikuwa ametumia usiku kucha akifikiria mbinu nyingi, kulingana na uzoefu wake, kulipiza kisasi kwake.

Ghafla, aliona haina maana tena baada ya mbinu hizo za kikatili kumpita

kichwani moja baada ya nyingine.

Hakujisikia tena kuishi maisha ya

namna hiyo. Kwa kuwa lilikuwa ni kosa tu, alitaka kurudisha kila kitu jinsi ilivyokuwa kabla ya hilo. Baada ya yote, alikuwa mpita njia tu ambaye hakuona kuwa wa kuthaminiwa. Lisa aliinyanyua ile hati taratibu na kuipitia. Alvin alipomsikia akiipekua ile hati, alikunja uso kwa kejeli.

“Tulipooana, nilikuahidi kuwa nitakulipa baada ya kuachana, na nilikusudia.

Lakini sasa sijisikii kukulipa hata senti moja. Unapaswa kujisikia bahati

kwamba ninakuacha oundoke na roho yako, vinginevyo... Ni bora nisiende mbali sana.”

“Sijawahi kuwaza pesa zako…” Lisa

alicheka kwa uchungu. Alibaini kuwa

mawazo ya Alvin yalikuwa kwenye pesa

zake, kwamba Lisa alikuwa akiziwinda.

Sura ya 143

Alvin hakujisumbua kumtazama Lisa machoni. Lisa aliinamisha macho yake kimya

kimya. Kwa mtazamo wa mambo, ilionekana kuwa hakuna kitu ambacho

angeweza kuelezea zaidi akaeleweka. Alichukua kalamu na kusaini karatasi.

Moyo wake haujawahi kuwa mzito hivi alipokuwa akisaini 'Lisa Jones'.

"Nimemaliza. Naenda ghorofani kufunga vitu vyangu, nitaondoka mara baada ya hapo.” Aligeuka na kuelekea juu. Alvin

hakuwa na mpango wa kugeuza kichwa chake. Lakini, mwishowe alitazama

nyuma na kujikuta anamtazama licha ya yeye mwenyewe kutaka.

Alikuwa amevaa nguo za kulalia za

waridi, na nywele zake zilianguka juu ya

mabega yake kama maporomoko ya

maji. Harufu kama ya mwerezi ilitanda

mahali alipotoka.

“Unafikiri bado nitaamini maneno yako?”

Alvin alikunja ngumi. Kadri alivyozidi

kukunja ngumi ndivyo alivyokuwa

akikosa hewa kifuani. Hapo awali

alifikiria alikuwa anamtisha tu na

asingesaini karatasi. Bila kutarajia, alisaini bila kusita zaidi. Pengine

hakungoja kukutana na Kelvin tena.

Hah…

Alidhihaki kwa kejeli. Kwa kuwa alikuwa

amepitia vikwazo vingi, hakika

asingekufa kwa sababu tu ya kuondoka

kwake. Nusu saa baadaye, Lisa aliburuta

masanduku yake chini. Kwa wakati huo, hakuna mtu aliyekuwa sebuleni, na

kifungua kinywa kizuri alichotayarisha

hapo awali kilikuwa kimeishia kwenye

pipa la takataka. Alikunja midomo yake

kwa huzuni, akajifuta machozi kwenye

kona za macho yake, akaondoka.

Alipotazama jumba hilo likiwa mbali

zaidi kupitia kioo cha nyuma cha gari, alinung'unika ndani kwa ndani, 'kwaheri, Alvin.' Alikuwa akipaona mahali hapo

kama nyumba yake pekee na Alvin

kama mwanafamilia wake pekee. Lakini

sasa, hatimaye alikuwa peke yake tena.

Kwa kuwa hakuwa na pa kwenda kwa

wakati huo, Lisa alielekea kwenye

nyumba ya Pamela. Baada ya Lisa

kubonyeza kengele ya mlango kwa

muda, Pamela alifungua mlango.

Nywele zake zilikuwa chafu na kulikuwa

na harufu kali ya pombe juu yake.

“Kwa nini umekuja na masanduku yako?” Akiwa amechanganyikiwa na kustaajabu, Pamela alitazama

masanduku mawili yaliyokuwa kando ya miguu ya Lisa.

“Nimepewa talaka, na nimefukuzwa

nyumbani kwa Alvin. Kwa vile sijanunua

nyumba, sina pa kukaa isipokuwa

mahali pako.” Lisa akaburuta

masanduku yake ndani ya nyumba. Alijilaza kwenye kochi kama kikaragosi

asiye na roho.

"Nini?" Pamela alipandwa na hasira. "Ni kwa sababu ya picha? Kama mpenzi

wako, asingewezaje kukuamini? Mimi naenda kumfanya alipe. Ameenda mbali sana…”

“Usiende kwake.” Lisa alimsimamisha

Pamela. “Tayari anafahamu kuwa

mwanzoni nilimwendea kwa sababu

nilimdhania kuwa ni mjomba wa Ethan.

Pia amegundua kuwa ulimdanganya kabla ya hili kwa ajili ya kunitoa jela.”

"Nini? Aliwezaje kujua?” Pamela alipigwa na butwaa.

"Sina uhakika. Ni mimi na wewe tu ndo tulikuwa tunajua kuhusu suala hili." Lisa alimtazama kwa sura ya kinyonge.

“Sikumwambia chochote. Kwa

kuzingatia harufu kali ya pombe juu yako, labda ulikunywa sana jana usiku.

Una tabia ya kuzungumza upuuzi baada ya kulewa.”

“Usinituhumu…” Pamela alishikwa na wazo alipokuwa akizungumza. Alishika nywele zake. “Sasa nakumbuka.

Nadhani Sam ndiye aliyenirudisha

nyumbani jana usiku, na nilikuwa

nimelewa sana wakati huo. Kulikuwa na mwanamume mwingine ndani ya gari, na alidai kuwa mpenzi wako."

Lisa alikosa la kusema. Alikuwa

kishajua tangu aliposikia akinuka

pombe. Bila shaka, Pamela alikuwa ameropoka bila kujijua. Pamela

aligonga kichwa chake kwa nguvu.

Alitamani angepasua kabisa ubongo

wake. “Samahani, Lisa.”

Akiwa amehuzunika,

Pamela alipiga magoti mara moja mbele

ya Lisa. “Nimekuingiza kwenye matatizo tena. Sijui jinsi ninavyoweza kukusaidia

wakati wa maisha yangu. Naona aibu sana kukukabili. Vipi kuhusu kukutolea ndugu yangu kama fidia ya kosa langu?

Ninaahidi kwamba atakupenda kikweli na atabaki mwaminifu kwako.”

"Acha kuongea ujinga." Lisa alipunga mkono wake akimaanisha kuwa alikuwa amechoka sana asiweze kumkaripia.

“Hata hivyo, bado ingekuwa vigumu

kwetu kuendelea na uhusiano wetu hata kama hukusababisha tatizo. Kuna suala

kuhusiana na Kelvin na... mpenzi wake wa zamani ambaye hawezi tu kumshau.

Kila mara hutaja jina lake anapokuwa amelewa.”

"Nini? Kwa nini wanaume huwa na macho ya kupepesuka?” Pamela alisaga meno kwa kufikiria kile

kilichomkuta yeye mwenyewe.

“Vipi, ulimpeleka Patrick pamoja na familia yako kula chakula cha jioni jana usiku, sivyo? Kwa nini uliishia kunywa pombe?” Lisa alianza kushangaa ghafla. “Inaweza kuwa hivyo… Patrick alikutosa tena?”

Pamela alisema kwa uchungu, “Linda alipata ajali, Patrick akaenda kumwangalia. Hakunipigia hata simu.

Nimeachana naye moja kwa moja safari hii.”

“Jamani. Ni balaa gani hili?” Lisa alitukana kwa hasira. Ghafla, akahema.

“Sawa. Ulinifanya niishie kuachwa, na wewe uko single sasa hivi pia. Ngoma droo. Nitakuchukulia tu kama kampani yangu. Hata Patrick akikuomba

urudiane naye wakati huu, usikubali kukutana naye tena.”

“Ndiyo, bila shaka. Mimi ndiye

niliyekuumiza. Maadamu haujaolewa, sitathubutu kuolewa. Ikiwa hutapata hata mwanamume mzuri wa kukuoa, tunaweza kushiriki katika uhusiano wa jinsia moja. Kwani wanawake wangapi wanasagana?”

“Potelea mbali. sina hamu na wewe.” Lisa, ambaye mwanzoni alikuwa

amekasirika, hakujua kulia au kucheka wakati huo.

Chini ya dakika 20 baada ya kuondoka, gari la Sam lilionekana kwenye jumba la Alvin. Alikimbia kwa kasi hadi ghorofani, akamkuta Alvin akiwa amesimama

kwenye kibaraza huku macho yake

yakiwa barabarani. Alikuwa ameshika

sigara, na sinia ya majivu iliyokuwa

kando yake ilikuwa imejaa virungu vya

sigara. "Alvin, kweli utarudi Nairobi?" Sam

•••

alisema kwa hisia, "Nitaku’miss sana, na itakuwa tofauti kutokuwa na wewe karibu."

"Utani’miss kama rafiki au utakosa kuwa

nami kama chanzo cha mapato cha kampuni yako?" Alvin aliacha majivu ya sigara yadondoke bila kujali.

Kwa aibu, Sam alitoa kikohozi chepesi. "Angalia, ingawa umekuwa hapa kwa muda mfupi tu, umeipatia zaidi ya shilingi bilioni moja kampuni yangu ya sheria mwaka huu."

Alvin akaingiza mikono yake mfukoni. Macho yake meusi, mazito yalionyesha hali ya ujeuri.

Sam akahema. “Sawa. Kama ningelijua hili mapema, nisingekualika Dar es

Salaam. Kwa hiyo unaondoka lini?”

“Kesho. Tafuta mtu wa kuuza nyumba

hii." Baada ya kuongea kwa sauti ya kupuuza, Alvin aligeuka na kuingia ndani ya nyumba.

••• Asubuhi iliyofuata. Kitu cha kwanza alichofanya Lisa baada ya kuinuka

kitandani ni kumuandalia Alvin kifungua kinywa. Dakika akitoka chumbani, alipigwa na butwaa baada ya kuiona sebule hiyo asiyoifahamu. Alisahau

kuwa Alvin alikuwa ameachana naye. Hakuhitaji kuamka mapema ili kumpikia tena. Isitoshe, kusingekuwa tena na mlinzi wa kumuangalia. Kwa kweli, alikuwa ameachwa kama jongoo na mti wake.

Kama mwenyekiti wa kampuni yenye

thamani ya zaidi ya dola milioni 500, alipaswa kuishi maisha kwa uhuru

mkubwa zaidi. Alipaswa kufurahishwa na jambo hilo, lakini hakuweza kuhisi

furaha hiyo hata kidogo. Baada ya

kifungua kinywa, Lisa aliendesha gari

hadi hospitali kumtembelea Kelvin.

Hakuwa amemtembelea tangu siku

alipopoteza fahamu.

Sura ya 144

Lisa alikuwa akijisikia hatia kwa jinsi alivyomtendea Kelvin.

Alisimama mbele ya wodi akiwa na maua na matunda. Wakati anakaribia

kugonga mlango, mara akasikia

mwanamke akilia kwa sauti ya chini

ndani ya chumba hicho.

“Usilie mama.” Kelvin alimfariji mama yake. “Siwezi kulia vipi? Wewe ndiye mwana

pekee wa kiume katika familia ya Mushi.

Nilitarajia uendeleze ukoo wa familia ya Mushi, lakini angalia nini kimetokea.

Najiuliza ni nani aliyefichua suala hilo

kuhusu figo yako? Wanawake wote

ambao mwanzoni walitaka kuolewa na

wewe sasa watakukwepa. Hakuna atakayetaka kuolewa wewe.”

Kelvin alijibu, “Haijalishi, Mama. Hata hivyo, sijisikii kuoa bado.”

“Mimi ndiye niliyekuzaa. Unafikiri nitajisikiaje? Huwezi kuacha kumfikiria

Lisa? Hata ulihatarisha maisha yako kwa sababu yake.”

Akiwa ameshikilia kikapu cha matunda kwa nguvu, Lisa alisikiliza kile ambacho

Mama Mushi alisema mwishoni. “Hata hajali kuhusu wewe. Umelazwa hospitalini kwa siku nyingi, lakini hajakutembelea hata kidogo.”

“Inatosha mama. Ni chaguo langu.

Kumpenda mtu haimaanishi kuwa lazima uwe naye. Kumlinda na

kumwangalia akiishi kwa furaha ni zaidi ya kutosha.” Kelvin alieleza.

Lisa alihisi uvimbe kwenye koo lake.

Kuna kitu kilionekana kukwama kwenye

koo lake, jambo ambalo lilimfanya

akose raha. Kamwe hakutarajia

kwamba Kelvin angempenda sana.

“Mbona umesimama hapa?” Mzee

Mushi alikoroma kwa hasira nyuma ya

Lisa nje ya wodi.

Lisa alishtuka, na wale waliokuwa

chumbani wakamtazama.

Kwa hayo, aliingia chumbani kwa

kusitasita. Kelvin aliguswa kuwa huenda

Lisa alikuwa amesikia alichokisema.

Kwa hiyo, uso wake mzuri ulianza

kuona haya usoni. “Lisa, kwa nini

umenitembelea leo, Alvin hatachukia?”

“Nimefika hivi punde. Mimi na yeye

tayari tumeshaachana.” Lisa aliinua

kichwa na kumtazama. Alionekana

kuwa mwembamba sana ndani ya siku

chache tu. Gauni alilovaa lilionekana

kumlegea huku uso wake wa kifahari na mrembo ukionyesha kama mgonjwa anayesumbuliwa na utapiamlo.

"Mbona mmeachana ghafla?" Kelvin

alipigwa na butwaa. "Ilikuwa kwa sababu yangu?"

"Hapana. Kuna matatizo mengi sana kati yetu.” Lisa alibadilisha mada.

“Unaendeleaje sasa?”

"Anaendelea vizuri?" Mama Mushi

aliinuka akiwa na uso mchangamfu.

“Alipoteza figo, sasa figo moja si sehemu ya nyama yake tena. Hawezi

hata kurejesha kimetaboliki chake bado.

Kwa kuwa mikono yake inakabiliwa na uharibifu wa neva, anahitaji kupitia miezi michache zaidi ya matibabu. Mbaya

zaidi, maisha yake ya baadaye

yataathiriwa. Daktari alisema kuwa

hatakiwi kufanya kazi ama mazoezi

magumu, na anapaswa kuwa

mwangalifu katika lishe yake.

Vinginevyo, atapoteza maisha yake. Kwa kuzingatia kwamba kwa kawaida

anahitaji kusimamia kampuni kubwa kama hiyo, nadhani hawezi kuishi maisha marefu.”

Mzee Mushi alimkemea, “Unaongea upuuzi gani? Zingatia maneno yako."

“Nimekosea? Tayari tuko katika miaka ya mwisho ya uzee wetu, kwa sababu tulikuwa na mtoto wetu mmoja tu wa kiume, pengine tunapaswa kumtunza milele.” Mama Mushi alijifuta machozi usoni mwake. “Unafikiri kuna

mwanamke yeyote kutoka katika familia

yenye heshima ambaye yuko tayari

kuolewa naye? Maskini mwanangu, nina wasiwasi na maisha yako ya baadaye.”

Akiwa ameshikwa na hatia, Lisa

alihuzunika sana. Alikuwa mwishoni

kabisa mwa akili zake.

“Acha, Mama.” Kelvin alimsimamisha

katikati ya maumivu ya kichwa chake.

“Nimekosea? Ulijeruhiwa kwa sababu yake. Alikutunza hata siku moja?

Ingekuwa afadhali ungeokoa mtu

usiyemjua kuliko yeye,” Mama Mushi

aliongeza kwa uchungu, “Kwa maoni yangu, yeye ndiye anapaswa kuwa

mwangalizi wako milele ili akusaidie. Hata hivyo, huwezi kupata mke kwa

sasa, basi yeye awe fidia yake.”

“Mama…” Kelvin alishindwa kujizuia, na uso wake mzuri ukageuka kuwa wa kustaajabisha ghafla. Maumivu yalikuwa

makali sana hadi akatoka jasho la

baridi. Wakati huo huo, shinikizo lake la damu lilionekana kupanda juu ya

kiwango.

Kila mtu aliingiwa na hofu na kumpigia

simu daktari haraka.

Daktari alifika haraka na kuwakemea, “Mgonjwa amefanyiwa upasuaji

mkubwa, badala ya kumfariji, mnampandisha presha. Mnataka afe?”

Kila mtu alinyamaza mara moja. Hata

Mama Mushi alifunga mdomo kwa aibu. Kelvin alichoka sana hata akapitiwa na usingizi muda si mrefu.

Tena, Mama Mushi alimtazama Lisa kwa hasira. Lisa aliinamisha macho kwa

hofu. “Acha kulalamika mama. Nitalipa fadhila kwake. Kuanzia leo na

kuendelea, nitamtunza. Hata baada ya kupona, nitashughulikia lishe na maisha yake hadi apate mke.”

"Lakini vipi ikiwa hawezi kupata mke?"

"Hilo halitawezekana." Lisa alimtoa wasiwasi.

Mama Mushi alidhihaki. “Nani yuko

tayari kuolewa na mwanaume aliyekosa kiungo? Ikiwa kuna matatizo na figo

nyingine, labda atakufa kwanza. Isitoshe, sidhani kama kuna mtu

mwingine yeyote ulimwenguni angekuwa tayari kuhatarisha maisha

yake ili kukuokoa.”

Lisa alikaa kimya kwa muda wa nusu

dakika kisha akaongea taratibu kwa

sauti ya ukali, “Sawa. Ninaahidi atanioa.”

•••

Katika mgahawa, Pamela alipopata

habari hizo, karibu amwage kahawa.

“Umerukwa na akili? Unapanga

kurudisha fadhila kwa kutoa maisha

yako, huh?"

"Sina la kufanya tena." Lisa aliinywa

kahawa iliyokuwa na ladha chungu

sana. "Zaidi ya hayo, picha yetu

imesambazwa kila mahali. Kila mtu ana

hisia kwamba tuna uhusiano wa karibu. Hata hivyo ni sawa tu, alitoa figo yake

moja kwa sababu ya kuniokoa…”

Pamela alishtuka baada ya kusikia hivyo. “Kelvin anakupenda sana. Siku

zote amekuwa akikulinda kwa siri, lakini

wewe na

Alvin…”

"Hatutarudiana kamwe." Lisa alionyesha sura ya uchungu. Hakumwambia

Pamela kwamba Alvin alikuwa mtoto wa familia ya Kimaro. Lisa na Alvin

walitenganishwa na bahari, na wote

wawili walikuwa katika ulimwengu

tofauti. Kwa kuongezea, mawazo yao

yalikuwa tofauti kabisa.

“Sawa basi. Kwa kweli, wakati mwingine

ni bora kwa mwanamke kutafuta

mwanaume anayempenda zaidi kuliko

yeye. Kwa njia hii, mwanamke hatahisi

kuchoka.” Akikumbushwa kuhusu

uzoefu wake wa mapenzi, Pamela aliugua. "Kwa upande wangu ninapanga kufanya kazi huko Nairobi mara tu baada ya mwaka mpya."

Lisa aliinua kichwa chake kwa

mshangao. "Kwanini unaenda huko ghafla?"

“Si ghafla. Mwaka jana, kampuni ya Osher kutoka Kenya lilinipa nafasi ya mkemia mkuu wa vipodozi. Sikuweza

kuvumilia kuachana na Patrick, kwa hiyo nilikataa kazi hiyo. Kampuni hiyo

ilinipa kazi hiyo tena mwezi uliopita, na niliikubali jana.”

Pamela alitazama nje ya dirisha kwa

huzuni. "Nimekuwa nikifikiria juu ya

Patrick katika wakati wangu wote nikiwa

hapa Dar. Natamani kuona ulimwengu mpya, na ninaamini nitasahau kuhusu

uhusiano huo polepole baada ya muda."

"Inaonekana kama wazo zuri." Ghafla, hali hiyo iliacha pengo kwa Lisa kwani

rafiki yake wa pekee naye angemuacha.

"Ninaweza kuelekea Nairobi pia na

kukuza biashara ya Mawenzi

Investments huko mwaka ujao. Kuhusu

kifo cha mama yangu… nataka kuja kuchunguza pia.”

“Uko sahihi. Baba yako anatoka Nairobi pia. Nitakusubiri uje.”

Usiku, Lisa alipakua masanduku yake. Alipofungua moja, ghafla akakuta Mkufu

wa Malkia ndani yake. Wakati anahama

kwa Alvin alikuwa amepakia vitu vyake

haraka na kusahau kuviangalia kwa

uangalifu. Kwa kushangaza, alikuwa

amebeba na Mkufu pamoja. Kwa

kuzingatia kwamba kitu hicho kilikuwa

cha gharama kubwa, asingeweza

kubaki nacho.

Siku

iliyofuata, aliendesha gari hadi kwa

Alvin tena. Alitumia muda mwingi

akibonyeza kengele ya mlango, lakini

hakuna aliyefungua mlango.

“Huna haja ya kuibonyeza tena. Mmiliki ameondoka Dar es Salaam.”

Mwanaume aliyevalia suti nyeusi akatokea nyuma yake.

"Wewe ni…" Lisa aliuliza.

“Mimi ni dalali wa nyumba. Nilikuja

kuchukua picha chache za jumba hilo ili kuisambaza kwa wateja na kuiuza,”

mwanamume huyo alitabasamu na kusema, “Mmiliki alisema anataka

kuiuza kwa bei nafuu. Kwa kuzingatia eneo na muundo wake, ninaamini

itauzika hivi karibuni.

Sura ya 145

Mara tu dalali yule alipomaliza

kuzungumza, ghafla aligundua kuwa

uso mzuri wa mwanamke yule

ulionekana kupauka. Alikaribia kukosa

mwelekeo wake. "Uko sawa, mwanamke mzuri?"

“Mimi… nipo sawa.” Lisa akamkabidhi

kadi yake ya biashara. "Ningependa kununua nyumba hii ya kifahari, lakini

natumai hutafichua utambulisho wangu kwa mmiliki wa awali. Nitakulipa

kamisheni pia.”

“Oh, sawa, hakika.” yule dalali alifurahi.

Hakutarajia kwamba angeweza kuuza

jumba lile kwa kutembea tu hadi mlangoni. Ni kazi rahisi iliyoje.

Baada ya kuingia ndani ya gari, Lisa

alitawaliwa na hali ya kuchanganyikiwa.

Ghafla, alihisi kana kwamba moyo wake

ulikuwa umetoweka. Ingawa alikuwa

ametia saini hati za talaka, hakutarajia

Alvin angeondoka Dar es Salaam

mapema namna ile. Hiyo ilimaanisha

kwamba wote wawili wangeweza

wasikutane tena kwa vile walikuwa

katika miji tofauti. Alikuwa amejitoa

katika maisha ya Alvin, lakini kwa nini

moyo wake ulikuwa bado unauma kiasi cha kushindwa kupumua? Aliushika

Mkufu wa Malkia huku akilia kwa jazba.

Dakika 40 baadaye, alijitokeza kwenye ukumbi wa kampuni ya mawakili ya

Jeninnings akiwa na miwani ya jua usoni. Mhudumu wa mapokezi pale

mlangoni akamtambua mara moja.

Baada ya kumuona mhudumu wa mapokezi alihema kwa huzuni kwani

asingeweza tena kuiona sura nzuri ya

Mr. Kimaro kila siku. “Unamtafuta

Bwana Kimaro? Ameondoka.”

"Namtafuta Sam." Lisa alimsahihisha.

Mhudumu wa mapokezi aliwasiliana na msaidizi wa Sam mara moja. Muda si

muda, aliagiza Lisa apande ofisini

kwake. Ofisini, Lisa alipitisha boksi la velvet kwa Sam. “Mkufu wa Malkia uko

kwenye boksi. Tafadhali mpe.”

"Alvin hataitaka" Sam alisema kwa uhakika, "Itunze tu. Nadhani ataitupa mara atakapoiona.”

“Hebu atupe basi. Bidhaa hii ina thamani ya shilingi bilioni tatu, ambayo ni gharama sana. Sitaki anidai.” Kwa hayo, Lisa aliinuka na kuondoka.

Lisa alipokea simu kutoka kituo cha

mahabusu mchana. Ilitajwa kuwa Jones

Masawe alikuwa na hamu ya kumuona

kwa mara ya mwisho. Hukumu za Jones

Masawe na mkewe zilikuwa zimetolewa.

Kwa kuwa mama Masawe ndiye

aliyekuwa muuaji, alihukumiwa kifungo

cha miaka 20. Kwa upande wa Jones

Masawe, alihukumiwa miaka kumi tu kwa kuwa msaidizi. Ukizingatia uzee

wao, maisha yao yalikuwa yamekwisha.

Baada ya kufikiria kidogo, aliamua kuwatembelea.

Alipomwona Jones Masawe tena baada ya siku kadhaa, tayari alikuwa na mvi kana kwamba alikuwa amekua kwa miaka kumi.

“Kwa nini ulinitaka nije?” Lisa aliuliza bila kujali. Tayari hakuwa na hisia naye hata kidogo.

Jones Masawe alijibu kwa huzuni, “Najuta, na nimejisalimisha kwa hatima yangu. Nimehamisha hisa zote za

Mawenzi Investments kwako.

Ninachotumai ni kwamba utamruhusu

Lina atoke kwenye ndoano. Baada ya yote, yeye ni binamu yako, ambaye pia ndiye mwanafamilia wako pekee.”

"Amefanya mambo mengi maovu." Lisa alikunja uso kwa kejeli. "Aliponiumiza,

hata alinifikiria kama mimi ni binamu yake?" Jones Masawe aliuma midomo yake. “Ulimtumia pia mtu kumdhuru? Tangu

mimi na mama yake tufungwe jela, hajatutembelea hata kidogo.”

Lisa akabaki ameduwaa. “Pamoja na mambo mengi yanayoendelea kwa

sasa, sikupata hata muda wa kumfanyia

chochote. Haishangazi kwamba

hajaja kukutembelea. Umemlea kwa

muda gani? Kwa mtu katili kama yeye

ambaye atafanya chochote kufikia

malengo yake, bado unatarajia atakuwa na mawazo na wewe? Nina hakika sasa

atakukwepa kadri awezavyo.”

Jones Masawe aliyatoa macho yake

kwa butwaa. Alichosema Lisa

kilionekana kuwa pigo kubwa kwake.

Jones Masawe na mkewe walipofikiria,

waligundua kuwa Lina ndiye mtu

ambaye alikuwa mbinafsi zaidi yao.

Wangewezaje kuweka matumaini yao

kwa binti huyo? Alikuwa binti yao wa

kuzaa, lakini vipi hakwenda kuwaona?

Jones Masawe alilazimisha tabasamu. Kwa kweli, Lisa alikuwa binti mzuri.

Hata hivyo, Jones Masawe na mkewe

hawakuwahi kumjali kwa sababu tu hakuwa mtoto wao wa kumzaa. “Uko sahihi. Ni kosa langu, Lisa."

"Natumai utajuta gerezani kwa yale

uliyofanya." Lisa alisimama na kuondoka kwenye kituo hicho cha mahabusu.

Baada ya kurudi ofisini, alimwomba

msaidizi wake amtazame Lina.

Msaidizi haraka alimletea habari kuhusu

Lina. "Amepotea kwa siku kadhaa. Hata

hakuchukua vitu vya nyumbani kwake.

Hakujawa na miamala yoyote katika

akaunti yake ya benki pia. Anaonekana

kutoweka kimaajabu sana. Lisa alipigwa na butwaa. Hakutarajia

kwamba Lina angetoweka vile vile baada ya kupigana naye kwa muda

mrefu. Kwa mwonekano wa mambo, hakukimbia kweli. Labda maisha yake

yalikuwa hatarini.

Kwa wakati huo Lisa alifanya kazi huku akimhudumia Kelvin. Kimsingi, mtu

angeweza kusema kwamba walikuwa wakiishi pamoja. Alitumia mkesha wa

Mwaka Mpya katika jumba la kifahari la Kelvin. Usiku, nyumba ya familia ya

Mushi ilikuwa na mwanga mzuri. Lisa alipomsukuma Kelvin aliyekuwa

amekaa kwenye kiti cha magurudumu

kutoka chumbani, akakutana na Ethan,

Tracy na Sonya waliokuja kula chakula

cha jioni. Wote watatu walipigwa na

butwaa kumwona. Uso wa Sonya

ukawa mgumu mara moja.

"Lisa, huna aibu kama nini kuonekana

nyumbani kwetu -

"Nyamaza. Mwite wifi wakati mwingine."

Mama Mushi alimsogelea Sonya na

kumwambia aondoke. “Atachumbiwa na Kelvin baada ya Mwaka Mpya. Acha

kuongea chochote kilichotokea huko nyuma." Alinyamaza kisha akamwambia

Ethan, “Lazima umuite ‘Shangazi’.”

Wakati huo, Sonya na Ethan walivaa

sura ya kustaajabisha.

Lisa alihisi kutokwa na machozi

kutokana na hali hiyo kuwa mbaya.

Hili ndilo tukio aliloliota miezi kadhaa

iliyopita. Ingawa tukio kubwa lilikuwa

limefanyika hatimaye, hakufurahishwa

nalo kwa sababu mambo mengi

yalikuwa yamebadilika.

"Baba, unatania?" Sonya karibu aingie

kichaa. Hapo awali, Lisa alikaribia kuwa

‘binti-mkwe’ wake, lakini Sonya

alilazimika kumwita 'wifi' sasa. Je, Mungu alikuwa akimdanganya?

Mzee Mushi alimkodolea macho Sonya. "Sasa ndiye mtu anayesimamia

Mawenzi Investments. Hadhi yake ni kubwa kuliko yako. Je, ni vigumu kwako

kumwita ‘wifi’?” Sonya alinyamaza mara moja.

Hakuwa mjinga. Ikiwa Kelvin na Lisa

wangefunga ndoa, ingefaidisha familia ya Mushi. Zaidi ya hayo, kwa hali ile ya

Kelvin, mwanamke yeyote kutoka katika

familia mashuhuri bila shaka angekataa

kuolewa naye.

Jikoni, Lisa alivaa apron na kuandaa

vyakula vya kiasili zaidi. Kwa kuzingatia

kwamba mwili wa Kelvin ulikuwa dhaifu,

alikuwa amechukua usimamizi kamili wa lishe yake. Ethan alipoingia ndani alihisi

kubanwa kifuani kwa kuuona mgongo

wa Lisa. Alikuwa anajua upishi wake

mkubwa. Mara nyingi alipika vyakula

mbalimbali kwa ajili yake wakati ule pia. Hata hivyo, asingepata tena upendeleo huo.

"Lisa, upo tayari kuolewa na mjomba wangu?" Ethan alimsogelea na kutazama umbo lake zuri na la kuvutia chini ya taa.

Lisa aliinamisha kichwa chake, akaweka viungo kwenye sufuria na kusema.

"Anahitaji mimi nimtunze."

Ethan alitoa kicheko cha uchungu.

“Natamani ningekuwepo siku hiyo.

Ningekuwa tayari kukuokoa kutokana na kuchomwa kisu pia…”

"Kama nisingekuwa mwenyekiti wa Mawenzi, usingeniokoa." Lisa aliinua kichwa chake na kumtazama kwa kutokubali.

Uso mzuri wa Ethan ukawa mgumu.

“Acha kusema mambo ya namna hii. Mpenzi wako yuko nje anakusubiri.”

Lisa alitoka jikoni huku akiongea.

Sura ya 146

Saa sita kamili usiku, fataki ziliangaza anga la usiku. Lisa alimshika Kelvin mkono na kumpeleka kitandani.

Alipomlaza kitandani, Kelvin alimshika mkono. Huku fataki zikionekana katika macho yake yenye giza, alionekana kuangaza macho yake vizuri. “Lisa upo tayari kuolewa na mimi kweli? Usijute.”

"Ninaogopa kuwa wewe ndiye utajuta badala yake." Lisa alikunja uso na kusema kwa mawazo, “Ninapanga kuhamisha makao makuu ya Mawenzi

Investments hadi Nairobi mwaka ujao.

Nataka kujua sababu ya kifo cha mama yangu. Sijui adui zangu wa baadaye

watakuwa na nguvu kiasi gani—”

“Nitakusindikiza. Nitaenda hadi miisho ya dunia ili kukusaidia wakati wa maisha yangu,” Kelvin alikatiza sentensi yake kwa sauti ya kudhamiria.

Lisa alibaki kimya kwa muda. Kwa kuzingatia tabia ya Kelvin, hakuweza kuvumilia kumkataza na kumuumiza.

"Asante."

Baada ya mwaka mpya, Lisa alielekeza akili yake kwenye kazi.

Mali mpya za Mawenzi Investments ziliuzwa haraka, na kurahisisha mtiririko wa pesa wa kampuni.

Alipokuwa akipakia vitu vyake ili

aondoke jioni hiyo, mhudumu wa mapokezi akampigia simu ghafla.

“Mkurugenzi Maganga yuko hapa.

Alikuja na mtu ambaye anadai kwamba

anataka kukutana nawe."

Lisa alipigwa na butwaa. Chris

Maganga alikuwa amerudi Mwanza

baada ya kumsaidia katika kuimarisha cheo chake kama mwenyekiti, kwa hiyo kwa nini alikuwa amerudi kwa ghafla?

Dakika tano baadaye, mlango wa ofisi ukasukumwa. Chris alitokeza mlangoni na kunyoosha mkono wake kwa heshima. Baadaye, mtu mrefu ambaye

alitoa mwonekano wa utulivu na heshima aliingia.

Mwanamume huyo alikuwa na sifa za kuvutia, lakini aliweza kutambua

kwamba alikuwa na umri wa makamo kutokana na mikunjo ya macho yake.

Wanaume walikuwa watu wazima zaidi katika umri huu.

Chris pia alikuwa na umri wa makamo, lakini mwonekano na sifa zake

hazikuweza kulinganishwa na za

mwanamume huyo. Mwanaume huyo

alipoingia tu ofisini, alimkazia macho

Lisa. Macho yake yalionekana

kuwasilisha kila aina ya hisia ikiwa ni pamoja na furaha, huzuni, na taabu.

“Mjomba Chris, huyu…” Lisa alijawa na mshangao.

Chris akajibu, "Yeye ni baba yako, Joel Ngosha."

Kichwa cha Lisa kikamlipuka. Alikuwa amemfikiria baba yake mzazi hapo

awali. Hata hivyo, kwa kuonekana

kwake ghafla sasa, hakuweza kujizuia

kuhisi amepigwa na butwaa. Zaidi ya hayo, jina la 'Joel Ngosha' liligonga

kengele akilini mwake! Alikuwa mmoja

wa wafanyabiashara watanzania kumi

mashuhuri zaidi waliofanikiwa nje ya nchi kwa mwaka uliopita. Hapo awali

alikuwa amekutana na habari

zinazoelezea kwamba Joel alitoka

kwenye familia ya kisukuma huko

Mwanza na alianza na baishara akiwa

Mwanza hadi akafanikiwa kukuza na

kuvuka mipaka hadi Kenya. Alikuwa

mmoja wa watu wema zaidi huko

Nairobi, na zaidi ya hayo, alikuwa mtu

mashuhuri mwenyewe.

Iliaminika kuwa familia ya Ngosha haikuwa na nguvu sana mwanzoni.

Chini ya uongozi wa Joel katika miaka michache, hata hivyo, waligeuka kuwa

moja ya familia tajiri zaidi katika jiji la Nairobi. Mwanaume huyu kwa kweli

alikuwa baba yake mzazi. Hakuweza kuamini kabisa.

"Wewe ni picha ya mama yako." Joel

aliendelea kumtazama Lisa huku

machozi yakimtoka. “Sikutarajia kuwa

Sherly angenificha. Hakika alijifungua binti yetu.”

"Sherly alikuwa na matumaini kwamba

Lisa angeweza kukua salama," Chris alisema kwa sauti ya chini.

“Uko sahihi. Sikuwa na uwezo wakati

huo.” Joel alikunja ngumi akionekana kukumbushia jambo la uchungu. "Kama nisingesikia kuhusu kuteuliwa hivi majuzi kwa mwanamke mchanga, ambaye alikuwa binti ya Sheryl, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, nisingejua uwepo wako."

Mambo mengi sana yalikuwa yamemtokea Lisa ndani ya kipindi kifupi. Licha ya kukumbwa na wimbi la hisia ndani yake, alijituliza baada ya muda

mfupi. "Kwa hivyo, kwa nini unataka kukutana nami?" Aliuliza bila kujali na bila kujadili.

Joel alipigwa na butwaa lakini punde si punde alionyesha hali ya kusikitisha.

“Tabia yako inafanana na ya Sherry enzi hizo, Lisa. Ningependa

kukurudisha kwa familia ya Ngosha ili

kufidia malezi yote ambayo umekuwa

ukistahili kutoka kwangu kama baba

yako kwa miaka mingi.”

“Sidhani kama hilo ni wazo zuri. Tayari una familia yako mwenyewe na una watoto. Mimi si mtoto tena, sitarudi nyuma.” Akiwa amechoshwa na migogoro ya kifamilia, Lisa alikataa.

“Lisa…” sura ya wasiwasi ilivuka uso wa Joel. “Lazima uende nami. Nahitaji kukutazama ili niweze kukulinda.

Utambulisho wako utafichuliwa hivi karibuni. Wengi wao kutoka kwa ukoo wa Ngosha wamegundua uhusiano wangu na mama yako wakati huo.”

Lisa alipigwa na butwaa.

Chris kisha akaeleza, “Familia ya Ngosha ina mali nyingi ambazo vijana

wengine katika familia wanatazamia.

Kwa kuwa wewe ni binti wa Bwana

Ngosha, utaingia katika urithi wake siku

zijazo. Baadhi ya watu watahatarisha

maisha yao kwa ajili ya madaraka.”

Lisa alikasirika na kukosa kusema, lakini hakupendezwa na utajiri wake

hata kidogo. Kwa kweli, kuonekana kwa

ghafla kwa baba yake kulikuwa

kumeweka mzigo juu yake.

“Usiogope bwana Ngosha. Nitamshawishi. Tumtembelee Sheryl sasa.” Chris alibadilisha mada.

Lisa alikubali kuungana nao. Wakati wa safari, Joel alimsimulia hadithi nyingi

kuhusu jinsi alivyokutana na Sheryl. Hata hivyo, hakuguswa hata kidogo.

Aliuliza, “Kwa nini uliachana na mama yangu wakati huo?”

'Miaka 20 iliyopita, sikuwa na uwezo

kiuchumi. Katika uhangaikaji wangu kwa

bahati mbaya nikakutana na kulala na

mke wangu wa sasa, Nina Mahewa.

Baada ya mama yako kujua, aliamuua

kuondoka akiwa na mimba yako. Muda

si mrefu, nilisikia kwamba amefariki.”

Sura ya uchungu iliosha uso wa Joel.

"Kisha, nilianza kuishi maisha yangu katika hali ya mshangao. Nina alipopata

ujauzito, nilikubali kumuoa ili niwajibike kwa mtoto.”

Lisa alipokuwa akimsikiliza, alijawa na chuki. Ilikuwa hadithi ya kuudhi iliyoje.

Alimuonea huruma mama yake kwa

kuwa mwathiriwa. Baada ya kutembelea makaburi, aliondoka kwa kisingizio cha kuwa na kitu cha kuhudumia.

Joel alipomtazama akiondoka, alishusha pumzi ndefu. “Oh, Chris.

Inaonekana binti yangu hataki

kunitambua.”

"Lisa ameteseka sana katika familia ya Jones mwaka jana," Chris alieleza.

“Ndiyo. Ni kosa langu kwamba nilikuja

kujua kwa kuchelewa sana. Lazima

nimrudishe kwa familia ya Ngosha.

Ninataka kumfanyia kazi na kumtunza vizuri,” Joel alisema kwa hatia.

Asubuhi iliyofuata, Lisa alikuwa na mkutano. Baada ya hapo, alirudi ofisini na tayari Chris alikuwa akimsubiri pale.

"Mjomba Chris, ulishajua mapema kuwa yeye ni baba yangu?" Lisa aliuliza moja kwa moja, "Je, unatarajia kwamba

nitarudi kwa familia ya Ngosha pia?"

Chris alikuwa mkweli naye. "Lisa, unaweza tu kujua ni nani aliyemuua

mama yako wakati huo ikiwa utarudi kwa familia ya Ngosha. Nimekuwa

nikishuku kwamba huenda alikuwa

Nina.”

Lisa kichwa kilimuuma. Ilimbidi

ahusishwe katika mzozo mwingine wa

kifamilia wakati alikuwa amemaliza tu mgogoro mmoja. Uchovu wake ulikuwa

hauelezeki.

“Kwa hiyo, wakati huo alikuwa

akimwonea wivu mama yangu hivyo akaamua kumuua?”

"Nina ni mtu katili sana. Yeye pia ni binti mkubwa wa familia ya Mahewa. Chris alipumua na kusema kwa unyoofu, “Ni sawa ikiwa hujisikii kuchunguza suala hilo. Kwa kweli, ni miaka mingi imepita

tangu mama yako afariki. Zamani zimepita kwa muda mrefu na upepo.

Kwa sasa, Joel na Nina wako kwenye uhusiano mzuri. Hata hivyo haitakuwa rahisi kwako kushughulika naye.”

Lisa alinyamaza kimya.

Chris kisha akasimama na kusema.

“Nimekuja hapa kukujulisha kuhusu

jambo hili. Baada ya kusema hivyo, kumbuka kwamba ikiwa Nina atapata

habari kuhusu kuwepo kwako, hakika

atakuwa mtu wa kwanza kushughulika

nawe. Badala ya kuachwa juu na kuti kavu, afadhali ukae karibu na Joel.”

“Joel ana mke na binti ambaye ameishi nao kwa zaidi ya miaka 20. Mbali na ukweli kwamba nina uhusiano naye wa damu, nitaweza kweli kuwashinda? Lisa alitoa kicheko cha uchungu.

Chris alijibu kwa uzito, “Joel alikuwa

akimpenda sana mama yako wakati huo. Amekuwa akimfikiria kwa miaka hii yote. Atakulinda.” Lisa aliposikia hivyo alikaa kimya kwa muda mrefu.

Sura ya 147

Usiku, katika ua wa jumba la familia ya Mushi, Kelvin alichukua dawa kutoka

kwenye kiganja cha Lisa. Macho yake

meusi yalibeba huzuni ambayo ilikuwa

ngumu kidogo. “Kweli wewe ni binti

Joel. Hiyo ina maana… siko na wewe

kwenye level moja tena na wewe. Wewe ni wa hadhi ya juu zaidi kwa sasa.”

“Hapana. Sijawahi kuwa na nia ya kupata chochote kutoka kwa familia ya Ngosha.” Sauti ya Lisa ilijawa na uchovu. "Hata hivyo, lazima nielekee Nairobi wakati huu. Mimi…”

"Endelea." Kelvin aliweka mkono wake

kwa upole juu ya nyuma ya mkono wake. “Usijali kuhusu mimi. Mlezi atanitunza.”

"Asante." Kwa kweli, Lisa aliguswa sana. Kelvin na Alvin walikuwa tofauti sana. Kelvin daima alikuwa mpole na mvumilivu kwake. Kinyume chake, Alvin alikuwa jabari na mwenye kiburi. Mara

nyingi alilazimika kuvumilia tabia yake.

Kila alipotaka kufanya jambo, ilimbidi

ajidhatiti kumshawishi ili apate kibali

chake. Aliona ni ngumu kuelewana na

Alvin kwa tabia hiyo. Pia hakupendezwa na ukweli kwamba alikuwa amemwekea mlinzi wa kumtazama kwa kila hatua.

Lakini, kwa njia fulani alikuwa na ugumu wa kuzoea maisha baada ya Alvin.

"Unafikiria nini?" Macho ya Kelvin

yaliangaza kwa utusitusi, na akaushika mkono wake kwa nguvu.

Lisa alirejewa na akili muda huo huku

akijiuliza ni kitu gani kilimkumbusha

Alvin tena. "Nilikuwa nikifikiria kuwa

huenda familia ya Ngosha ni kubwa, na labda ni mahali pa hatari kuwapo huko."

Kelvin alitabasamu kwa uchangamvu sana. “Usiogope. Nitakutambulisha kwa marafiki zangu wa Nairobi baadaye.

Hutakuwa peke yako katika kesi hiyo.

Kwa kweli, nimerejea kutoka ng'ambo

mwaka jana na nimekuwa nikipanga

kuendeleza biashara yangu huko

Nairobi pia. Eneo jipya la kiuchumi

lilipoanzishwa huko miaka miwili

iliyopita, nilikuwa tayari nimenunua kipande cha ardhi ili kupanua kiwanda.”

Lisa alipigwa na butwaa na kumshangaa sana. "Sikutarajia kuwa wewe ni mtu anayefikiria mbele."

“Bora zaidi ni kuwa na mtizamo wa mbele wa kukuangukia wewe.” Kelvin alicheka huku akibana ncha ya pua yake.

Lisa aliganda. Alvin alikuwa akimbana kwa njia hiyohiyo, lakini kubanwa na

Kelvin kulimfanya akose raha na hata kustahimili kidogo.

“Tayari ni usiku sana Nitarudi chumbani kwangu kwanza.” Tabasamu kidogo

liliruka usoni mwake. "Pumzika mapema

baada ya kuchukua dawa." Aligeuka, na

kugundua kuwa Kelvin alikuwa bado

hajaachia mkono wake.

Alitazama nyuma na kukutana na macho ya Kelvin yenye upendo na upole. “Lisa, unaweza kukaa hapa usiku huu? Usijali, sitakufanya lolote kwani

bado sijapona majeraha yangu.”

“…Samahani, Kelvin. Nimetoka tu kwenye uhusiano na mtu mwingine, kwa hiyo bado sijazoea. Nipe muda.” Lisa alimkataa bila kujua.

Ilikuwa rahisi sana kuwa kwenye

mahusiano na Kelvin. Hata hivyo, kwa mawazo ya kulala kitanda kimoja na yeye, hakuweza kufanya hivyo. Macho ya Kelvin yalitiwa giza, lakini

alilazimisha tabasamu. “Sawa.”

Siku tatu baadaye. Lisa na Joel

walielekea uwanja wa ndege wa

kimataitaifa wa Julius Nyerere. Kelvin

binafsi aliwapeleka kwenye uwanja wa ndege. “Nisubiri Lisa. Nitakuja kukutana

nawe huko mara nitakapopona.”

“Sawa. Tuendelee kuwasiliana kwa simu.” Baada ya kupunga mkono, Lisa alipanda ndege pamoja na Joel.

Joel alikuwa akimtazama Kelvin alipokuwa akielekea uwanja wa ndege. Alimpata Kelvin akimfahamu sana, lakini hakumvutia sana baada ya kufikiria kwa makini. Kwa macho ya Joel, ilikuwa ni huzuni kwamba binti yake tayari alikuwa na mchumba katika umri mdogo.

Hakika, Kelvin alikuwa wa kushangaza ukizingatia jinsi alivyokuwa kijana na mwenye mafanikio. Ikilinganishwa na familia ya Ngosha, hata hivyo, hadhi yake ilizingatiwa kuwa ya chini kidogo.

"Ni kweli alipoteza figo kwa sababu ya kukuokoa?" Joel aliuliza.

“Ndiyo. Bila yeye, ningeweza kufa. Ikiwa huniamini, nenda ukachunguze jambo

hilo,” Lisa alinong’ona, “Usinipangie siku ya kutoonana naye wakati tunapokuwa Nairobi. Sitafurahia.”

Joel aliposikia maneno yake aliangua

kicheko. Kisha, akapumua.

“Sitaingilia masuala ya mahusiano yako. Wakati huo, wazazi wangu

walinilazimisha kuoana na mtu ambaye sikumtaka. Kwa hilo, nilianza kuishi

miaka ya maisha yenye huzuni. Kilicho muhimu zaidi ni furaha yako. Hali ya wastani ya Kelvin sio suala kwani

ninaweza kumpa mkono kila wakati.

Uwezo wake pamoja na usaidizi wangu

utamfanya kuwa mzuri kama wale

vijana kutoka familia tajiri huko Nairobi.

Lisa alishikwa na butwaa. Alibadili sana

mtazamo wake kuelekea baba yake.

"Haitakuwa

‘Ni jambo dogo tu.” Joeli bila kujali

... shida sana?"

alimgusa nywele zake ndefu. "Hata

kama utapanga talaka siku zijazo, hutahisi kwamba una deni la Kelvin."

“Baba...” Lisa alishtuka kwamba neno

hilo lilimtoka kinywani mwake bila yeye kutambua.

Joel alifurahi sana. "Sema hivyo tena." Badala yake, Lisa aliinamisha kichwa na kukaa kimya.

Joel alitabasamu. "Nimepata msisimko wa kwanza wa upendo pia. Nilipoagana kwa muda mfupi na mama yako wakati

huo, nilichanganyikiwa sana hivi

kwamba sikuweza kuacha kumfikiria, jambo ambalo ni tofauti na jinsi nyinyi

mnavyochukuliana sasa hivi. Ninaona

kuwa anakupenda. Lakini mara tu

ulipoingia kwenye ndege, nadhani ulifarijika badala yake.”

Lisa hakuongea neno lolote.

Akilinganishwa na Jones Masawe, Joel

alikuwa bora zaidi kwa kuwa alikuwa mwangalifu na alimjali sana. Labda

angeweza kuhisi uchangamfu wa kibaba uliopotea kwa muda mrefu

wakati wa safari yake kwenda Nairobi wakati huo.

Baada ya kushuka kwenye ndege, Joel

alimpeleka kwenye jumba la kifahari

lililopo Sherman Mountain. Hiki ni

kitongoji maarufu ambacho kiko nje

kidogo ya jiji la Nairobi, ambako matajiri

wengi wa Kitanzania waliowekeza

nchini Kenya wamejenga na kuishi

huko. Kulikuwa na idadi kubwa ya majengo ya kifahari na majumba

kwenye Mlima wa Sherman, yote

yakiwa ya watu matajiri na wenye nguvu

huko Nairobi bila kujali ukubwa wao.

Lisa aliona majengo mengi ya kifahari

njiani. Moja ya jumba kubwa zaidi

lililokuwa katikati ya mlima lilisimama

kutoka kwa wengine

Joel alipoona kwamba alikuwa akiitazama nyumba hiyo kwa udadisi, alimjulisha. "Hekalu hilo ni la familia ya Kimaro."

Familia ya Kimaro…Moyo wa Lisa ulirukaruka. Hapo awali, alifikiria kwamba asingeweza kuwasiliana na Alvin tena. Hakutarajia kwamba siku moja angeishi karibu sana na nyumba ya familia ya Kimaro. Je, Alvin alikuwa akiishi huko pia? Utambulisho wake ulikuwa ni nani katika familia ya Kimaro? Je, wangekutana tena? Lakini, aliacha kufikiria juu yake kwani yote yalikuwa yamepita.

Joel na Lisa walifika kwenye jumba la kifahari la Joel Ngosha. Mara tu gari

lilipoegeshwa, mwanamke mrembo na mwenye utulivu akatoka.

“Umerudi,

mume. Lazima atakuwa Lisa.

Sikujua kwamba angekuwa mrembo

sana.” “Huyu ni Aunty Nina,” Joel alisema kwa upole. “Habari, Aunty Nina.” Tabia ya Nina

ilimshangaza Lisa. Alikuwa na hisia kwamba Nina angemkaribisha kwa uso

jeuri. Hata hivyo, hakuamini kwamba

mwanamke yule angemtendea kwa

dhati mtoto wa nje wa mumewe.

Mwanamke huyo lazima angekuwa

mgumu kukabiliana naye.

"Ah, una heshima gani." Nina alitabasamu. Aligeuza kichwa chake na kukimbilia ndani ya jumba ghafla. Kisha

akapiga kelele,

Njoo

“Acha kuchati, Melanie.
ukutane na dada yako."
"Mama, hata hukuzaa binti kabla sijazaliwa."

Binti huyo mdogo ambaye alikuwa karibu umri sawa na Lisa alitoka nje ya jumba. Uso wake ulikuwa na umbo la embe dodo huku mashavu yakivimba

kidogo kama mimba ya paka. Ngozi yake ilionekana kuwa nzuri ya kung’aa, ikiwa kati ya weupe na weusi wa kiafrika. Melanie Ngosha alipokutana na Lisa, alionekana kutokuwa na furaha mara tu baada ya kumtazama Lisa

vizuri. Lisa alijua Melanie alikuwa anatoka wapi. Alifanana na Joel, wakati Melanie alikuwa na mfanano mkubwa naye.

Katika kesi hiyo, wote wawili

walionekana sawa kabisa. Hata hivyo, midomo na meno ya Melanie hayakuwa mazuri kama ya Lisa. Meno yake

yalikuwa yameungua kama kashata, sawa na mabinti wengi wa Arusha.

Basi, mwanadada tajiri ambaye

amekuwa na tabia ya kiburi tangu

utotoni angewezaje kumkubali binti

mwingine aliyefanana naye lakini hata

mrembo kuliko yeye? Melanie alisema kwa mzaha, “Hata hafanani na Baba.

Unawezaje kusema ni binti yako?”

“Vipi hatufanani? Ikiwa hujui la kusema, funga tu mdomo wako. Kuanzia sasa, yeye ndiye binti wa kwanza wa familia ya Ngosha. Wewe ni binti wa pili,” Joel

aliamuru kwa sura ya kiume.

"Baba, mimi ndiye binti wa kwanza."

Melanie alikasirika na kukanyaga miguu

yake kwa kutoridhika.

'Ni sawa, baba. Ikiwa mimi ndiye binti wa kwanza au la, haijalishi. Sisi ni binti zako hata hivyo,” Lisa aligeuza kichwa

chake na kumwambia Joel, “Ninaelewa

jinsi Melanie anavyohisi. Kama

ningekuwa katika viatu vyake, nisingejisikia vizuri pia.”

“Huo ni uelewa wako wa kipekee sana.” Hali ya utulivu ilivuka uso wa Joel.

Sura ya 148

Baada ya kuona Melanie amekasirika, Lisa aliona ni bora kutumia njia ya chinichini. Hakutarajia kwamba siku

moja angeweza kutumia mbinu za

kinafiki kama za Lina. Hata hivyo,

unafiki ulikuwa mkakati madhubuti.

“Baba, pamoja na kwamba umenileta nyumbani, huwezi kuwa upande wangu

kila wakati na kunisifu tu kwa sababu

unanionea huruma. Itamkasirisha

Melanie na kuharibu udada wetu

pamoja na amani ya familia. Ingawa

nimeamua kurudi nyumbani, sitaki

kuathiri familia yako.”

Joel aliguswa sana. Ikilinganishwa na

Melanie mcheshi na mwenye majivuno

ambaye alimlea, Lisa alielewa zaidi.

“Njoo nikuonyeshe chumba chako. Usisite kunijulisha ikiwa haujaridhika nacho.” Alipowaona wawili hao wakiingia ndani ya nyumba hiyo, Melanie alipandwa na hasira. "Mama, mwanamke huyu ni mjanja sana!"

Nina alikunja uso kwa hasira. Alidhani

kwamba ingekuwa rahisi kushughulika na Lisa kwa kuwa alikulia katika familia

isiyo na uwezo. Lakini, mambo

hayakuwa rahisi kama alivyofikiria. Lisa

hakuwa mtu wa kuchukuliwa kirahisi, kama mama yake wakati huo.

Baada ya kusema hivyo, Nina aliamini

kwamba angeweza kukabiliana na Lisa

kwa vile aliweza pia kumshinda mama yake wakati huo.

“Sio tatizo. We tulia. Kwa kuwa

nimekutana na kila aina ya watu

maishani mwangu, hatanipa shida.”

Nina alimshika Melanie. "Umejiandaaje kwa karamu iliyoandaliwa na familia ya Kimaro usiku wa leo?"

Wakati wa kutajwa kwa tukio hilo, macho ya Melanie yaling'aa kwa

msisimko. “Nimechukua gauni la waridi pamoja na mkufu. Pia nimemwajiri

Kayya kunipaka vipodozi. Usiku wa leo, hakika nitakuwa msichana mrembo

zaidi kwenye ukumbi na Bwana Kimaro, bila shaka atavutiwa sana na mimi.”

Nina aliitikia kwa kichwa kwa kuridhika.

"Kutokana na nilivyosikia, Bibi Kimaro

alisema kuwa karamu hiyo inafanyika

usiku wa leo kwani hakujawa na

shughuli nyingi katika jumba hilo. Kwa

hakika, anajaribu kumtafutia Bwana

Kimaro mwenzi wa ndoa. Wanawake

wote ambao hawajaolewa ambao

amewaalika wanatoka katika familia

zenye ushawishi hapa jijini. Nilisikia

kwamba Bwana Kimaro alienda likizo

huko Tanzania mapema mwaka jana na hatimaye akarudi mwishoni mwa

mwaka. Huko Tanzania hakupata mke wa kuoa. Bibi Kimaro alisema lazima

aoe mwaka huu.”

“Mama, nampenda Bwana Kimaro,” Melanie alisema kwa haya, “Yeye ndiye

mwanamume mzuri zaidi ambaye

nimewahi kumuona. Hakuna

anayeweza kumzidi.”

“Kazana sasa. Nina imani na wewe.

Ukiingia kwenye familia ya Kimaro, Lisa

atachukuliwa kuwa si chochote.” Sura

ya dharau ilimjia Nina usoni.

Jioni, Lisa aliendelea kuongea na Joel

pale sebuleni. Ghafla Joel alimwona

Melanie akishuka akiwa amevalia gauni

la pinki. Alikunja uso na kuuliza, "Unaenda wapi?"

“Atahudhuria sherehe aliyoalikwa na rafiki,” Nina alijibu kwa upole.

“Usichelewe sana kurudi.” Joel hakutoa maoni zaidi.

Hata hivyo, Lisa aliona sura ya Melanie

yenye furaha usoni mwake na pia

furaha iliyokuwa machoni mwa Nina.

Alihisi kwamba kulikuwa na jambo la kutia moyo lililokuwa likiendelea kwao.

Usiku. Karamu kuu ilikuwa ikifanywa

katika nyumba ya familia ya Kimaro.

Vijana wazuri na mabinti warembo

walikuwa wamevalia nakupendeza

kupita kiasi na kucheza kwenye sakafu ya dansi.

Usiku huo, familia maarufu na tajiri zaidi

huko Nairobi zilikusanyika hapo. Kila

mmoja wa wasichana matajiri alikuwa

akienda kuonyesha kipaji chake usiku

huo. Kila mtu alijua kwamba ilikuwa

hafla ya juu juu, lakini ilikuwa na nia ya

msingi ya kumtafuta mwanamke

ambaye angekuwa mwenzi wa ndoa

wa Bwana Kimaro.

Yeyote aliyemwangukia angeanza njia

rahisi ya mafanikio. Cha kusikitisha ni

kwamba Bwana Kimaro mwenye sura

nzuri kabisa hakuwa amefika hadi

wakati huo.

Katika chumba cha maktaba kilicho

kwenye ghorofa ya tatu. Alvin alishika

sigara kwa mkono wake huku

akiipekua hati fulani kwa mkono

mwingine. Mwanga mkali juu ya dawati

uliangaza uso wake mzuri, ambao

ulifunua uso wa huzuni. Ni kana

kwamba zogo zote zilizoendela huko

chini hazikuwa na uhusiano wowote

naye.

Mlango ulisukumwa kwa kishindo. Bibi

Kimaro aliingia na kusema kwa

uchungu, “Umejificha humu ndani!

Ninakufanyia hafla hii makusudi ili

uweze kumchagua mke wako

mtarajiwa, lakini hapa umejificha kimya kimya. Huna mpango wa kupata mke?"

"Hapana," Alvin alijibu bila kujali.

Bibi Kimaro alizidiwa na hasira. “Lazima

utoke nje sasa hata kama hujisikii kufanya hivyo. Kwa kuwa wewe ni

mjukuu mkubwa katika ukoo wa moja kwa moja wa familia ya Kimaro, lazima

uoe. Sarah tayari amekufa. Utaacha lini kuahirisha hili?"

Alvin aliyekuwa akiipekua ile hati kwa

vidole vyake vyembamba akanyamaza kwa muda.

Bibi Kimaro aliichana ile hati na

kuitupilia mbali. “Unaweza kufanya kazi

wakati wowote lakini si leo. Nenda

ukamchague mwanamke usiku wa leo, la sivyo nitapiga kichwa changu mbele

yako hadi nife.”

“Bibi…” Alvin alipapasa paji la uso wake. Hii ndiyo sababu hasa hakutaka kurudi. Kama mwanamume ambaye

angetimiza miaka 30 hivi karibuni, alikuwa akilazimishwa kwenda

kuchagua wanawake ambao hata hakuwafahamu. Hapo awali, alimuoa

Lisa kwa makusudi ili kukabiliana na hali kama hiyo kwa wakati huo. Hata hivyo

mpango wake ulikwenda kombo.

Kwa mawazo ya bibi huyo, macho ya Alvin yalitiwa giza. Kwa kuwa ilibidi aoe mapema au baadaye, ilionekana kwamba kuoa mapema au baadaye hakungeleta tofauti. Labda amsikilize bibi yake ili ajisikie raha zaidi.

“Sawa.” Aliinuka na kutoka nje na Bibi

Kimaro. Kwa furaha kubwa, Bibi Kimaro

alimpeleka kwenye ghorofa ya pili ili

kuwatazama mabinti waliokuwa chini. Hali ilikuwa sawa na jinsi mfalme

alivyomchagua mke wake zamani za kale. "Angalia mabinti walio hapa chini na uchague anayekuvutia."

Muda huo macho ya Alvin yalipita juu yao, kichwa kilimuuma. mabinti wote

walikuwa wamepambwa sana, na labda walionekana tofauti na nyuso zao zilizo

wazi mara tu mapambo yao yalipoondolewa. Badala yake, uso wa

Lisa ulikuwa safi kila wakati na mzuri

hata na vipodozi nyepesi. Macho yake

ghafla yakahamia kwenye uso wa binti mmoja. Alvin aliganda.

Bibi Kimaro akahamishia macho yake

kwa binti aliyekuwa akimwangalia na kutabasamu. "Yeye ni Melanie Ngosha, binti wa familia ya Ngosha. Baba yake

ni Joel Ngosha na mama yake ni Nina

kutoka familia ya Mahewa. Anatoka

katika malezi tajiri pia. Kuhusu sura

yake, anachukuliwa kuwa mmoja wa mabinti wenye sura nzuri kati ya wengine hapa usiku wa leo.”

Alvin alikaa kimya kwa muda. Uso wa binti huyo ulimkumbusha yule

mwanamke aliyekuwa mbali huko Dar es Salaam. Kwa kweli, alimchukia sana

alipomwacha. Hata hivyo, alipomwona yule binti aliyefanana naye, hakuweza

kujizuia kumfikiria Lisa. Alimroga kwa

mtishamba gani?

“Kwa hiyo… yeye ndiye?” Bibi Kimaro

aliuliza kwa mshangao.

“…Aha, basi sawa.” Alvin alipomaliza kuongea tu akashuka ngazi taratibu.

Sura ya 149

Usiku sana, akiwa amesimama kwenye

kibaraza, Lisa aliweza kuona nyumba ya familia ya Kimaro kutoka mahali alipokuwa. Usiku huo, taa zote zilimulika. Aliweza kuhisi kwamba ndani ya jumba hilo kulikuwa na shughuli nyingi. Alishangaa pale kwa muda, akashusha pumzi taratibu kisha

akarejea kujilaza tena kitandani. Hata hivyo, alikuwa na shida ya kupata usingizi. Asubuhi, Lisa alishuka chini mapema sana baada ya kukosa usingizi usiku.

Mazingira ya pale sebuleni yalikuwa tofauti kabisa.

Joel alitulia tuli kwenye kochi huku

Melanie akikumbatia mkono wake na

kusema kwa furaha, “Baba, hujui jinsi

Bwana Kimaro alinitendea kwa shauku

jana usiku. Miongoni mwa mabinti wote, alivutiwa na mimi kwa mtazamo wa

kwanza na hata akanialika nicheze

naye. Bibi Kimaro pia alikuwa na

mazungumzo ya muda mrefu nami,

akiniomba niwe mpenzi wake.”

Nina alitabasamu kutoka sikio hadi

sikio. "Mungu ndiye mtoaji wa bahati nzuri. Nilijua Melanie angeweza

kumpata mpenzi sahihi kwa uzuri na kipaji chake, lakini sikutarajia angeweza kuolewa na Bwana Kimaro. Familia ya Kimaro ni miongoni mwa familia tajiri

zaidi hapa Nairobi. Mali zote za familia ya Kimaro zitakuwa zako katika siku zijazo.”

"Usisahau kuna Jack Kimaro pia katika familia." Akiwa amekunja uso, Joel

aliwakumbusha Nina na Melanie baada ya kusikia maneno yao ya tamaa.

"Kwa hiyo?” Nina aliuliza kwa nyodo.

“Ingawa kila mtu anajua kwamba Bwana

Kimaro ameondoka KIM International wakati fulani, Jack hana uwezo wa kusimamia kampuni vizuri.”

Melanie alisema kwa kiburi, “Hata kama

Bwana Kimaro hatapata kuchukua uongozi wa KIM International, utambulisho wake kama kaka mkubwa wa familia bado ni bora. Hakuna mtu

mwingine ambaye ningependa kuolewa naye maishani mwangu isipokuwa yeye.”

Nina alijawa na tabasamu. "Wote wawili mlipendana mara ya kwanza na mmeundwa kwa ajili ya kila mmoja."

Joel alifichua chembe ya kero. "Kwa hivyo ulihudhuria hafla ya familia ya

Kimaro kwa ajili hiyo. Kwanini

mlinificha? Mliogopa kwamba

ningemwomba Lisa ajiunge pia, huh?

Kwanini mna mawazo mabaya kama

hayo?" Melanie alipiga kelele. “Kuna maana

gani ya kumtaka ajiunge nayo? Kwa

kuzingatia kwamba hajawahi kuona

tukio kubwa kama hilo, nilikuwa na

wasiwasi kwamba angeiletea aibu familia yetu. Zaidi ya hayo, si tayari ana mchumba? Ikiwa atakutana na watu wengi matajiri hapa Nairobi, anaweza kuamua kumwacha mchumba wake ambaye ni masikini kama yeye mwenyewe.”

“Wewe…” Joel alikasirika sana hadi akapiga meza na kusimama. Hata

hivyo, dakika tu alipomwona Lisa akiwa amesimama kwenye ngazi, aliganda ghafla. “Lisa…”

“Lo, Lisa, usimchukie Melanie.” Nina alivaa tabasamu. “Kwa kweli, Melanie alikuwa na wasiwasi kwamba hujazoea

kuhudhuria karamu kama hizo, ikizingatiwa kwamba wewe bado ni mgeni hapa. Zaidi ya hayo, hafla za

familia ya Kimaro huwa za ajabu kila wakati.”

Lisa aliinua macho yake kwa siri. Mama

yake wa kambo alikuwa mbunifu sana

katika kutamka maneno yake. Mwisho wa siku, walitaka tu kumdhihaki kwa

sababu eti hajatembelea sehemu kubwa ya ulimwengu. Hawakujua kwamba Lisa alikuwa ametembea sana na hata

kusoma Chuo Kikuu Marekani. Na huyo

Alvin Kimaro waliyekuwa

wakimshobokea kwake alikuwa zilipendwa!

“Haijalishi. Kuweza kuwa binti wa familia ya Ngosha ni heshima kwangu. Sina nia ya kujipandisha hadhi kwa kudandia

wanaume matajiri hata kidogo.” Lisa alitoa tabasamu hafifu na la upole.

Nina na Melanie walipigwa na butwaa.

Je, Lisa alikuwa akijaribu kuwakejeli

kwa kuwa na pupa ya kutamani familia

za hadhi ya juu licha ya asili yao yenye

nguvu tayari? Hakika Joel alionekana

kukasirika zaidi huku akiwatazama Nina

na Melanie.

Nina alisema, “Hubby, ninafanya hivi

kwa ajili yako. Ikiwa binti yetu anaweza kuolewa na Bwana Kimaro, hali yako

itakuwa tofauti.”

"Baba, mimi sasa ni rafiki wa kike wa Bwana Kimaro," Melanie akaongeza

kwa kufoka, "Bwana Kimaro alisema atakuja usiku wa leo kula chakula cha jioni."

"Nini? Bwana Kimaro anakuja?" Nina alitetemeka kwa fadhaa. “Hubby, umesikia hivyo? Inaonekana Melanie ataolewa na Bwana Kimaro hivi

karibuni."

Joel pia alishangaa sana. Hata hivyo, ikiwa Bwana Kimaro alikuwa anakuja

kweli, ilimbidi amtendee kwa uangalifu.

"Sawa, nitamwomba mtumishi wa jikoni

aandae chakula kizuri zaidi na divai

nzuri usiku wa leo."

Akiwa na furaha kupita kiasi, Melanie alisema upesi, “Baba, nadhani nina kabati ndogo. Nahitaji kuvaa vizuri

kwani Bwana Kimaro anakuja usiku wa leo!”

"Sawa, nenda kachukue nguo na mama yako." Joel akatupa kadi. “Usiendelee kumnunulia Melanie nguo pekee. Lisa

amekuja na ana nguo chache sana, kwa hivyo mpe seti 20 hadi 30 za nguo pia.

Agiza maduka yakuletee hapa mara moja."

Tabasamu za Nina na binti yake zikawa ngumu. Melanie alipokuwa karibu

kudhihirisha kufadhaika kwake, Nina alimkazia macho. Baada ya hapo, wawili hao walienda kufanya manunuzi.

Joel alihema huku akiwatazama

wakiondoka. “Lisa, natumai huna shida.

Dada yako ni mpenda mali na amedekezwa sana na mama yake.”

“Baba, ni sawa. Usijali.” Lisa akatikisa kichwa kwa tabasamu mwanana.

Macho yake meusi yalikuwa angavu na ya kupendeza. Hakuwa amepaka kitu chochote usoni mwake, na alionekana aking’aa kama theluji.

Joel alipigwa na butwaa kidogo. Moyoni alimuonea huruma. Kwa mrembo kama

Lisa, kwa kweli alikuwa anamfaa kabisa Bwana Kimaro. Kwa bahati mbaya, hatima ilikuwa ya kikatili. Alitamani angemleta nyumbani mapema.

"Twende, nitakupeleka kwenye ofisi za Ngosha Corporation kwa ziara fupi."

Lisa hakupendezwa na Ngosha Corporation. Hata hivyo, alitembelea ofisi hiyo kwa kuwa hakuweza kukataa ombi la fadhili la baba yake. Alirudi tu

kutoka ofisini na baba yake saa moja

jioni. Taa zilizokuwa zimewashwa katika nyumba ya Ngosha zilimulika sana.

Mimea na maua mengi ya bei ghali pia yaliongezwa kwenye ua uliokuwa umesafishwa vizuri.

Walipoingia ndani ya nyumba hiyo, Nina alikuwa akiwaamuru watumishi wafanye

usafi katika eneo jirani. Melanie alikuwa amebadilika na kuvaa vazi la juu la sufu

ambalo lilikuwa la gharama kubwa zaidi msimu huo. Alivaa sketi ambayo ilikuwa

imeunganishwa na jozi ya tight. Pia kulikuwa na kitambaa cha manyoya

kikiwa kimezungushiwa mabegani mwake. Alitengeneza nywele zake

ndefu kimakusudi pia. Sehemu ya mbele ya nywele zake ilikuwa imejikunja na nyuma yake ilikuwa imesukwa.

Alionekana kama binti wa kifalme.

“Hubby, nilisikia umempeleka Lisa ofisini leo, sivyo?” Nina alimsogelea

Joel na kumuuliza huku akijua kila kitu.

“Kuna ubaya wowote kumpeleka binti yangu ofisini?” Joel alikunja uso.

"Bila shaka hapana." Huku akizuia chuki yake ndani kabisa, Nina alisema huku

akitabasamu, “Lisa, nimekununulia nguo nyingi za chapa maarufu leo. Nguo hizi

pengine hazipatikani Dar es Salaam. Nenda ukajaribu nguo sasa. Huwezi

kuvaa vibaya wakati Bwana Kimaro atakapokuja baadaye.”

Lisa alipopanda ghorofani na kufungua

kabati lake, alitabasamu baada ya kuona nguo zile mle ndani. Hakika zote

zilikuwa nguo zenye chapa maarufu, lakini, zote zilikuwa aimepitwa wakati

miaka kadhaa iliyopita na hazikuweza

kuuzika kwa sababu ya rangi zake za

kizamani. Ikiwa angekutana na kina

Janet huko Dar es Salaam akiwa

amevaa mojawapo ya nguo hizo, bila

shaka angechekwa hadi azimie. Lakini, haikuwa muhimu kwake kwani alijiamini juu ya uzuri wake.

Dakika 20 baadaye, alishuka ngazi.

Nina na Melanie, ambao walikuwa wakimtarajia aonekane wa kizamani

katika mavazi yale, walipigwa na butwaa mara moja. Lisa alivaa koti refu

la kijivu ambalo Nina alinunua. Jacket

ilikuwa kubwa sana ilionekana kama

blanketi juu yake. Bila shaka, mtu yeyote wa kawaida aliyevaa koti hilo

angeonekana kuwa kituko, lakini, Lisa hakufunga zipu ya koti hilo, akaliacha

wazi. Aliiunganisha na kitop cheupe cha rangi ya cream na suruali nyeupe ya kawaida. Hakuwa amepaka chochote

usoni mwake, isipokuwa ndomoni

aliweka lipstick nyekundu. Alionekana

kama binti safi na mrembo mwenye

umri wa miaka 17 au 18. Ikilinganishwa

na Lisa kando yake, Melanie alionekana

mwenye urembo mwingi zaidi na uso

uliopambwa sana hadi ukapitiliza.

Lisa kwa makusudi alisema huku

akitabasamu, “Asante kwa nguo, Aunty

Nina. Zinanipa joto sana na hili baridi la Nairobi. Nimezipenda sana.”

"Nimefurahi kwa kuwa umezipenda."

Nina alikuwa akihema kwa hasira.

Wakati huo, aligundua kuwa Joel

alikuwa akimwangalia sana.

Ijapokuwa Joel hakuwa mzoefu wa

nguo, aliona wazi nia ya mkewe. Kwa

bahati nzuri, Lisa alikuwa na mwili wa

kuvutia na mwonekano bora zaidi, kwa

hivyo angeonekana mzuri katika nguo

yoyote.

Wakati huo, mtumishi aliingia na

kusema, “Bwana Kimaro yuko hapa.”

Wale wanne wakatoka mara moja

kwenda kumpokea. Gari aina ya Rolls-

Royce lilisonga taratibu kuelekea

kwenye jumba la kifahari. Baada ya gari

kusimama, dereva alitoka na kufungua

mlango wa nyuma. Mtu mtukufu, mashuhuri alitoka nje. Alivaa koti la kijivu na suti ya kijivu. Kwa kuzingatia mavazi yake, ilikuwa ni lazima kabisa

kuzingatia sura ya mtu huyo. Kwa

kushangaza, mavazi hayo yalimfaa

vizuri. Miguu yake mirefu ilifanana na ya mwanamitindo wa hali ya juu, ilhali uso

wake ulikuwa mzuri sana hivi kwamba

hakuweza kupatikana hata kasoro

ndogo.

Kipindi Lisa alipomtazama vizuri mtu

huyo usoni, kichwa cha Lisa kilianza

kuunguruma bila kukoma. Inawezaje

kuwa yeye?!

Alijua kwamba Willie alikuwa

anamuogopa Alvin, hivyo aliamini

kabisa kwamba Alvin alikuwa na hadhi

ya juu kabisa katika familia ya Kimaro.

Hata hivyo, asingeweza kamwe

kutarajia kwamba alikuwa

akitetemekewa kiasi kile na familia tajiri

za kitongoji kile maarufu, mtu tajiri zaidi

katika eneo lote lile lililokaliwa na matajiri wa Kitanzania waliowekeza

nchini Kenya, na pengine kitongoji tajiri kuliko vyote jijini Nairobi!

Pamela alikuwa amemuelekezea kwa

bahati mbaya wakati huo, na kumfanya ahusishwe na mtu maarufu kama huyo.

Sasa ujio wake pale ulimaanisha kwamba alikuwa mpenzi wa Melanie.

Alikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa shemeji yake katika siku zijazo.

Sura ya 150

Uso wa Lisa ulibadilika polepole. Alipata hisia kali kwenye kifua chake, ambayo

ilimsababishia maumivu. Ikiwezekana, alitamani asingemwona tena maishani mwake.

“Umefika Bwana Kimaro!” Melanie

alimsogelea Alvin kwa unyonge na kumshika mkono wake kana kwamba

walikuwa wanandoa kwenye mvuto wa kwanza wa mapenzi.

“Ndiyo.” Alvin alikunja uso kwa namna

isiyoonekana, akijiuliza ni nini kinamsibu binti huyo. Walikuwa wamecheza

pamoja tu jana yake usiku, lakini

alijifanya kuwa karibu kwake kana

kwamba walikuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu. Wakati tu alipokaribia

kuachana naye, Joel na Nina

walimkaribia.

"Habari, Bwana Kimaro." Joel alimpa

mkono Alvin taratibu.

“Habari, Mr. Joel. Ni mara yangu ya

kwanza kukutembelea. Pole kwa

kukusumbua." Iilipokuja suala la kutangamana na Joel, Alvin alimtendea

kwa adabu na heshima.

"Bila shaka, hakuna tatizo. Ni heshima yetu kuwa na wewe hapa,” Nina alijibu

kwa pupa huku akiwa amejawa na tabasamu.

Joel alimtazama mkewe akiwa hoi.

Kisha, akasema kwa upole, “Ingia ndani ukaketi. Nje kuna baridi.” Joel na Nina walimtengenezea njia.

Kabla Lisa hajasogea, Alvin alifika kwake na macho yao yakagongana.

Mara ya pili alipokutana na macho yake, haraka akatazama pembeni. Alikuwa na

wasiwasi kwamba kadiri alivyomtazama kwa muda mrefu, ndivyo angehisi

maumivu zaidi. Zaidi ya hayo, akili yake

ilikuwa katika hali ya mkanganyiko

muda huo.

Macho meusi ya Alvin yalimkazia mara

baada ya kumwona. Hapo hapo, hisia

kali zilimtawala kutoka chini kabisa,

lakini, alificha vizuri sana hivi kwamba

hakuna mtu aliyetambua. Kila mtu alimuona tu akimtazama Lisa kwa

makini huku akiwa ameganda palepale.

Alipoona hivyo, Melanie aliingiwa na wivu ndani kabisa. Mara moja alishika

mkono wa Alvin na kusema kwa sauti, “Bwana Kimaro, unatazama nini? Huyu ni binti wa nje wa baba yangu ambaye amefika hapa jana tu, lakini hatushiriki mama mmoja.” Maneno yake yalikuwa mazito ya dharau.

Alvin alielewa kila kitu sasa. Kwa muda

mrefu alikuwa akijua kuwa Lisa ni binti wa Sheryl, lakini hakutarajia kuwa Joel

ndiye mwanaume ambaye Sheryl

alikutana naye hapo awali. Alifikiri

kwamba asingemwona Lisa tena. Bila

kutarajia alikuwa ametokea mbele yake

tena wakati huo. Alikuwa hata binti wa

familia mashuhuri ya Ngosha.

Hatimaye Alvin alipata utulivu, lakini

akapata hisia nyingine nyingi. Wakati

huu, alijawa na uchungu.

"Bwana Kimaro, huyu ni binti yangu

mkubwa, Lisa." Joel alimtambulisha Lisa

kwake huku akionekana kutoridhika na

utambulisho ambao Melanie alitoa.

“Oh, binti yako mkubwa? Si binti yako tu wa haramu?” Kauli ya kikatili ilitoka

kwenye midomo mizuri ya Alvin.

Lisa alikodoa macho. Hakutarajia

kwamba Alvin angekubaliana na

maelezo ambayo Melanie alisema. Kauli

hiyo ilionekana kumpeleka kwenye

dimbwi la kukata tamaa. Hakika, hii

ndiyo ilikuwa asili ya kweli ya Alvin.

Alikuwa mkatili na mwenye dharau.

Nina na Melanie walishangilia kwa

furaha. Hawakuwa wametarajia Alvin

kuchukua upande wao.

Joel alikuwa na shida kidogo. Alvin

alimtupia jicho kisha akasema kwa upole, “Kuwa na mtoto wa nje

kumezingatiwa kuwa ni jambo lisilofaa katika familia ya Kimaro. Ulikuwa mzembe sana, Mr. Joel."

Joel aliipokea kauli ya Alvin kwa machungu, lakini hakuwa na ujasiri wa kujibu. Baada ya yote, familia ya Kimaro

ilikuwa na hadhi ya juu sana, hivyo

hakuweza kudiriki kumkosea Alvin

vinginevyo angeharibu biashara zake.

Akishindwa kuvumilia tabia yake, Lisa

alimwendea Alvin na kumwangalia

machoni kwa namna isiyo ya jeuri wala

kujidharau. "Hata kama Baba yangu

alikuwa mzembe au la, haina uhusiano

wowote na wewe. Baada ya yote, yeye

ndiye mwenyeji wako, unatakiwa uwe na heshima kwake."

Macho ya Alvin yaligeuka kuwa

mabaya, na Nina akamwambia Lisa kwa

ukali. “We mwanaharamu, unawezaje kuthubutu kuongea na Bwana Kimaro

kwa njia hii? Omba msamaha haraka.”

“Hasa. Bwana Kimaro alitushauri tu kwa wema. Wewe ni mkorofi sana.” Kwa

hayo, Melanie aliinua kichwa chake na kumwambia Alvin, “Usikasirike, Bwana

Kimaro. Lisa alikulia katika familia isiyo na uwezo na hajaona sehemu kubwa ya ulimwengu.”

Alvin alikunja midomo yake mizuri na kutoa tabasamu dogo. “Inaonekana sijakaribishwa hapa. basi nitaondoka tu…”

Dakika alipogeuka, kila mtu alianza

kuingiwa na hofu. Melanie alishika

mkono wake kwa nguvu na kunguruma.

"Baba, mwambie Lisa aombe msamaha sasa!"

Joel alikunja ngumi. Ikiwa Alvin

angetoka nje ya nyumba ya familia yake

muda mfupi baada ya kuingia, watu

wote wenye nguvu huko Nairobi

wangejua kwamba alikuwa amewaudhi

familia ya Kimaro. Katika hali hiyo, familia ya Ngosha ingetengwa huko

Nairobi. “Lisa, omba msamaha."

Alipomaliza tu sentensi hiyo, alitoa tabasamu la uchungu na kuhema. Lisa akiwa ameduwaa akakunja ngumi.

Hakuwahi kuchukizwa sana na sura nzuri ya Alvin hapo awali. Alishusha pumzi nzito na ndefu na kusema.

“Samahani, Bwana Kimaro. Sijaona

mengi ya ulimwengu na sijui jinsi ya kuishi kwa heshima katika jiji. Ninatoka mashambani, kwa hivyo natumai hautakwazika na mapungufu yangu.”

Kutoka mashambani? Alvin alicheka.

"Ingia, Bwana Kimaro." Joel alibadili

mada huku akitumai Alvin angesahau tukio lile.

Alvin alipoingia ndani ya nyumba hiyo, Melanie bado alikuwa amemshikilia

mkono. Hapo awali alipanga kujinasua

kutoka mikononi mwake, lakini

alipambana na tamaa hiyo baada ya kuona sura ya Lisa iliyochanganyikiwa.

Baada ya kukaa kwenye kochi, Melanie alienda mpaka kumuegemea begani.

Lisa alisikitishwa na tukio hilo. Sehemu hiyo ilikuwa ya kipekee kwake, lakini sasa ilikuwa ya mtu mwingine. Je, mwanamume huyo alikuwa akimpenda

kweli wakati huo? Angewezaje kubadilika hivyo?

“Mungu wangu, mbona umeleta zawadi nyingi za gharama? Uwepo wako

unatosha, Bwana Kimaro. ” Nina alipiga kelele ghafla na kutazama mbele.

Alimwona dereva wa familia ya Kimaro

akibeba zawadi nyingi kuingiza ndani ya nyumba, ambazo zote zilikuwa adimu na za gharama kubwa.

Alvin akageuza kichwa chake karibu na kushangaa ghafla. Alijua uikuwa ni

mpango wa Bibi Kimaro. Alitaka

kumfanya aonekane kana kwamba

alikuwa akitoa zawadi za harusi kwa

familia ya Ngosha. Alikaa kimya kwa

muda kabla ya ghafla kusema kwa

tabasamu, “Ni wajibu wangu. Kwani,

umemlea binti mzuri kama Melanie.”

“Bwana Kimaro…” Melanie aliguswa sana hivi kwamba macho yake yakawa

mekundu. Alihisi kusukumwa, aliukandamiza mwili wake kwa nguvu

kifuani mwa Alvin. Mwili wa Alvin ukawa

mgumu. Hakuwa na la kusema. Je,

mabinti wa familia ya Ngosha walikuwa

wazi na wasio na aibu? Ilikuwa Lisa

zamani na Melanie baadaye. Lisa

alitazama pembeni. Hakutaka kulifikiria

wala kulitazama.

“Baba, mimi ni binti wa nje ya ndoa.

Nitapanda ghorofani kwani uwepo

wangu humfanya Bwana Kimaro kukosa

furaha.” Aligeuka na kumtaarifu Joel.

Joel alielewa kuwa ilikuwa inamkera

kukaa pale. Alipokaribia kuitikia kwa

kichwa, ghafla Alvin alizungumza kwa

sauti ya kejeli, “Nadhani unahisi kutaka

kuondoka kwa sababu huna furaha

kwamba nilikulazimisha kuomba msamaha.”

“Hapana…” Lisa alifadhaika. Sasa kwa kuwa wawili hao walikuwa wameachana, kwanini alilazimika kumsemesha?

Alvin alikoroma. Baada ya hapo, aliashiria sahani ya matunda na karanga kwenye meza kwa kutumia kidevu chake. “Kwa kuwa unatoka

mashambani, nina hakika unajua kazi za hali ya chini. Nenda kanimenyee matunda na karanga uniletee kwenye sahani. Melanie nami tungependa kula.”

Moyo wa Melanie ulijawa na furaha. Hakufikiri kwamba Bwana Kimaro

angemjali sana. Alikuwa akimtesa Lisa

kwa niaba yake, akijua kwamba

anamchukia Lisa. “Lete matunda

haraka. Bwana Kimaro anataka kula.”

*Sawa.” Lisa alilazimisha tabasamu.

Kwa vile alitaka kumtesa, basi angemruhusu tu.

Aliinama na kuchuchumaa kuanza

kumenya zabibu. Baada ya hapo, alianza kumenya karanga. Hakuwa

amezowe na ilisababisha vidole vyake kuuma. Alipomenya za kutosha, aliweka kwenye sahani na kwenda kuwatengea wale wapendanao!

Kwa upande wa Melanie alimuegemea

Alvin na kumlisha matunda na karanga

ambazo Lisa alikuwa ametoka kumenya na kuwatengea. Lisa hakujishughulisha kutazama tukio hilo kwani aliliona kuwa la kuchukiza.

7
" Bila shaka unaendelea kufurahia mfululizo wa hadithi hii ya kusisimua"

Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.