waandishi ebook 1686264694.7096112

Page 1

Sura ya 101

Lisa hakuwa na wasiwasi juu ya shopping baada ya kufika kwenye maduka. Alichagua nguo chache bila mpangilio na kuzitazama kwa haraka kabla ya kuzirudisha kwenye rafu.

Alvin akamgeukia muuzaji na kumwambia, “Nitanunua nguo yoyote atakayogusa."

Hilo lilimshangaza Lisa. “Unamaanisha nini?”

"Tutanunua chochote kinachokuvutia."

Alvin hakumpa nafasi ya majadiliano.

"Mwanamke wangu anaweza kununua chochote anachotaka. Nina zaidi ya pesa za kutosha."

Muuzaji alisema kwa wivu, “Lo, mpenzi wako anakujali vizuri sana! Sijawahi

kuona mwanamume yeyote mkarimu

STORY............. LISA KURASA......101-125

namna hii akiwa na mpenzi wake.”

Lisa alishtuka sana na kumwangalia

Alvin aliyesimama mbele yake. Ghafla, aliweza kusikia moyo wake ukipiga kwa nguvu. Hata alihisi hatia kwa

kumkasirikia muda mfupi uliopita.

Alvin hakuwa mtu wa kujali zaidi kuhusu

pesa, lakini kwenye mapenzi alikuwa haeleweki. Lisa hakumwelewa kabisa

msimamo wake, alimpenda kweli au alikuwa anamzingua tu? Kwa mtu wa nje angeweza kudhani kuwa upendo wake ulikuwa wa kujilazimisha na mapenzi yao yalikuwa ya upande mmoja. Lakini, wao tu ndio waliojua ukweli juu ya uhusiano wao. Haikuhitaji mtu mwingine yeyote kuthibitisha jinsi walivyotendeana.

“Ni sawa, basi nitachagua chache tu.”

Lisa alitikisa kichwa. Hatimaye, aliendelea kujaribu mavazi kadhaa. Kila

nguo ilionekana nzuri kwenye mwili

wake kwa ujumla. Mwishowe, Alvin

alilipa kila kitu ambacho alijaribu. Lisa

aligundua tu baada ya malipo kupita.

Lisa alimshika mkono Alvin kwa furaha, wakatoka huku akijisikia vibaya kidogo

kwa sababu nguo za hapo zilikuwa za bei ghali. "Sikuhitaji nguo nyingi kiasi

hiki, Alvilisa."

'Ni sawa. Ilimradi unazipenda,” Alijibu

Alvin. “Mi sijali kuhusu gharama.”

"Asante." Lisa alihisi kuguswa, alisimama kwa vidole vyake ili kumfikia

Alvin sikioni na kumpa busu la shukrani.

Sura ya aibu ilimwangazia usoni mwake.

Macho ya Alvin yaliingiwa giza na ubongo wake kuhisi kama umepigwa shoti kwa sekunde kadhaa baada ya busu la Lisa kupenya sikioni mwake.

Kwa kweli, Chester alikuwa sahihi.

Kumpeleka shopping mwanamke

aliyekununia bila sababu

kunasawazisha kila kitu.

••• Siku iliyofuata. Lisa alivaa nguo zake

mpya kabla ya kwenda kuangalia

maendeleo ya ukarabati wa jumba la Kelvin Mushi huko Mbezi

Beach. Mafundi walikuwa wakiendelea na kazi ya ujenzi. Alizunguka eneo hilo na kujadili maendeleo na fundi mkuu.

Kelvin aliingia kutoka nje na kuelekeza macho yake kwenye nguo zake mpya.

"Nguo ni nzuri sana mrembo. Ni shopping ya hivi karibuni?" Kelvin alimuuliza kwa mshangao.

"Ndio." Lisa alitabasamu kwa furaha

baada ya kufikiria kuwa ni zawadi

kutoka kwa Alvin. Furaha iliyofurika moyoni mwake na kuonekana machoni mwake ilimshangaza Kelvin ambaye alijikuta akiingiwa na kiroho cha wivu.

Maongezi yao yalikatishwa ghafla

baada ya Lisa kupokea simu kutoka

kwa nambari isiyojulikana.

“Halo, wewe ni Lisa Jones?” Sauti

kutoka kwenye simu iliuliza na kuendelea kueleza. “Mwanamke

anayeitwa Manka amezimia katika

nyumba yake ya kupanga. Nimejaribu

kutafuta majina ya ndugu zake kwenye simu yake lakini nimekuta namba

iliyoseviwa ni yako tu…”

“Manka… Shangazi Manka?” Lisa

alimkatisha mara moja, “Tafadhali piga simu ambulance ili kumpeleka hospitali ya karibu. Usijali kuhusu nauli nitakuja sasa hivi.”

Baada ya kukata simu, alitoka kuelekea mlangoni na Kelvin alimfuata. “Nitakusindikiza.”

Lisa aligawanya midomo yake ili

kuzungumza lakini alikatishwa na Kelvin, “Usitake kunizuia. Kuna kila aina

ya usumbufu hospitalini na kuwa na mtu wa kukusaidia ni bora kuliko kuwa peke

yako. Kama mtu ninayekuthamini sana

siwezi kusimama kando na kukuacha

uhangaike peke yako. Isitoshe, huu si wakati wa kubishana, twende tuwahi

kwa mgonjwa.” Lisa akiwa amezidiwa na wasiwasi, hakuweza kuwa mgumu zaidi.

Baada ya kufika hospitalini, muuguzi mmoja alikuwa akipiga kelele karibu na mlango wa chumba cha dharura.

"Ndugu yoyote wa Bi Manka? Jitokezeni tadhadhari na mwende kwenye mapokezi ili kulipa bili haraka iwezekanavyo."

"Niko hapa." Lisa alijitokeza na kukimbia kwa daktari. “Dokta anaendeleaje?”

"Ana hitilafu kubwa katika ubongo. Upasuaji lazima ufanyike mara moja.

Nenda ukafanye malipo sasa hivi na muandae mtu wa kutia saini fomu za upasuaji." Daktari alisukuma ankara ya malipo mikononi mwake.

Lisa alikimbia chini kushughulikia malipo. Upasuaji ulikuwa tayari

umeanza wakati aliporudi kwenye ghorofa ya juu.

"Ninafahamiana na madaktari kadhaa

katika hospitali hii, kwa hivyo

nilimeshashughulikia kila kitu na wanaendelea na upasuaji," Kelvin alieleza.

“Asante, Kelvin.” Lisa aliguswa.

Upasuaji huo hatimaye ulikamilika saa tatu baadaye. Aunty Manka alitolewa

nje ya chumba cha dharura. Lisa karibu

hakuweza kumtambua mwanamke huyo dhaifu. Aunty Manka alikuwa akionekana mwenye afya njema na mwenye nguvu wakati bado akiwa mlezi wa bibi yake Lisa, lakini alionekana kuwa mtu tofauti kabisa muda huo.

Mbali na kichwa chake kilichojaa mvi,

mashavu yake yaliyozama pia

yalimfanya aonekane mzee sana. ‘Ni nini kilikuwa kimetokea kwake?’ Lisa alijiuliza.

Ilikuwa ni saa kumi na moja jioni wakati

Aunty Manka alipofumbua macho na kumuona Lisa. Machozi yalitiririka mashavuni mwake mara tu alipomuona.

"Bi Jones, sikufikiria kama ningekuona tena."

"Huna haja ya kuniita hivyo tena." Lisa alilazimisha tabasamu la uchungu.

“Mimi si mtoto wa Jones.”

"Hapana, utakuwa Bi Jones

daima."Aunty Manka aliongea kwa sauti dhaifu.

“Aunty Manka, ni sawa, tayari ninajua ukweli kwamba nilichukuliwa na familia ya akina Jones. Nina hakika unajua hilo pia baada ya kuwa mlezi wa bibi yangu kwa miaka mingi iliyopita.”

“Nani kasema hivyo?” Aunty Manka

alijibu huku akiwa amekasirika. "Bila shaka wewe ni sehemu ya familia ya Jones!"

Jambo hilo lilimshangaza Lisa. “Nilisikia

kutoka kwa Lina. Mbali na hilo, sidhani kama wanandoa wa Jones wangefanya

mambo hayo kwa binti yao wa kuzaa wenyewe.”

“Haya yote lazima yamekuwa magumu sana kwako. Familia ya Jones imekosa utu kabisa." Aunty Manka alikohoa mara

kadhaa kwa hasira. "Sio tu kwamba

walinifukuza nyumbani kwao, lakini hata

walikuambia kwamba wewe si mtoto

wao. Ina maana wamesahau ahadi

walizotoa kwa babu yako na bibi yako??" "Anti Manka, ulifukuzwa nyumbani?" Lisa alishtushwa na habari hii. "Lakini

nilichosikia kutoka kwao ni kwamba uliondoka kwa sababu haukuwa tayari kumtunza Bibi baada ya kupooza."

“Bibi Masawe amenisaidia sana na alinitunza maisha yangu yote. Nisingeweza kumtupa alipokuwa akinihitaji sana.” Aunty Manka alijibu. Macho yake yaling'aa kwa machozi.

“Bibi mdogo Lisa, kwa kweli wewe si binti wa Jones Masawe. Mama yako

mzazi ni Sheryl Masawe, yule

mwanamke unayeamini kuwa ni shangazi yako. Alikuwa na mimba yako

kabla ya ndoa. Babu na Bibi yako

waliogopa kupoteza heshima yao, bila

kusahau kwamba hii ingeweza kufanya

iwe vigumu kwa mama yako kuolewa

tena. Ndiyo maana walikukabidhi kwa

Jones Masawe ambaye ni mjomba

wako.”

Lisa alihisi ulimwengu wake ukipinduka chini-juu. Kamwe asingetarajia kuwa

Sheryl alikuwa mama yake. Ilikuwa na maana sasa kwamba babu na bibi yake

walimchukua kutembelea kaburi la Sheryl kila tarehe ya kumbukumbu ya kifo chake. Haishangazi pia alifanana

naye sana! Hata Alvin alishawahi

kumwambia hivyo siku walipokwenda kumtolea sadaka bibi yake kaburini.

"Baada ya kukuzaa, mama yako

alifunga safari ya kikazi kwenda Kigoma

na kwa bahati mbaya akatoweka

kwenye ajali ya kimbunga," Aunty

Manka alisema katikati ya kwikwi.

“Kilikuwa kimbunga cha ajabu na cha

kutisha na zaidi ya watu kumi walikufa.

Kufikia wakati walipoupata mwili wake, ulikuwa umeharibika sana, hata

hawakuweza kumtambua.”

Lisa alihisi kukosa hewa kana kwamba

hewa yote ilikuwa ikitolewa kwenye

mapafu yake. Kelvin, ambaye alikuwa

akisikiliza kando, alimpigapiga begani kwa upole.

Aunty Manka aliendelea, “Mama yako

alikuwa mwanamke aliyefanikiwa ingawa alikuwa mdogo. Mawenzi

Investiments, ambayo ni kati ya biashara 100 zilizofanikiwa zaidi

Tanzania, ilianzishwa na yeye peke yake.

"Mama yangu ndiye mwanzilishi wa Mawenzi Investiments?" Sura ya mshangao iliwaka usoni mwa Lisa. Mwanga wa upeo ulipita akilini mwake."

Sasa aliweza kutambua ni kwanini

Jones alifanikiwa kuwa mwenyehisa

mkuu wa Mawenzi Investiments."

"Nini? Jones ndiye mmiliki mkuu wa hisa?" Aunty Manka alicheka.

“Inawezekana bibi yako ana…”

"Bibi alifariki siku chache zilizopita." Lisa

alimkatisha ghafla. Aunty Manka alitoa

macho kwa mshtuko. Dakika chache

baadaye, hatimaye machozi mengi

yalimtoka kwenye kona za macho yake.

Aunty Manka alijikaza na kusema kwa

unyonge, “Bibi yako asingekufa ghafla.

Hakika kuna mengi nyuma ya kifo

chake! Lisa, kuna kitu unahitaji kujua. Baada ya mama yako kufariki, babu na bibi yako walikuwa wakisimamia

Mawenzi Investiments kwa siri. Ili

kuhakikisha Jones atakutunza, aliweka wosia. Wewe na Jones kila mmoja

angepewa 30% ya hisa za kampuni hiyo mara tu utakapokuwa mkubwa na baada ya bibi kufa.”

Lisa alianguka kwenye kiti alipopokea

habari hiyo ya kutisha kama bomu.

“Baada ya Kibo Group kushuka, kuna

uwezekano kwamba Jones Masawe alipanga njama ya kumuua bibi yangu ili

kurithi hisa zote za Mawenzi

Investiments? Hapana, hilo

haliwezekani. Yeye ni mama yake, baada ya yote.” Lisa alishindwa kuamini.

Kelvin alishusha pumzi na kusema.

“Jones amezoea kuwa katika nafasi ya

madaraka maisha yake yote. Huenda

hujui hili lakini watu wanaweza kufanya

lolote ili kudumisha maisha yaliyojaa

utajiri na ushawishi. Tangu mwanzo wa wakati, kumekuwa na rekodi za ndugu

wa damu kushambuliana, kurogana na kuuana wakipigania kuwa warithi wa

familia tajiri. Isitoshe, bibi yako alikuwa amepooza kabla ya hii. Pengine

alimwona kuwa mzigo.

Sura ya 102

Aunty Manka aliitikia kwa kichwa. “Pia, sikuwahi hata siku moja kuamini kuwa

kupooza kwa bibi yako ilikuwa ajali. Siku

moja Lina alikuja nyumbani na mara bibi

yako akaanguka kutoka ghorofa ya pili

muda mfupi baada ya kupanda. Tangu

siku hiyo nikafukuzwa na baadaye

nikasikia kuwa bibi yako amepooza."

Lisa aliinua macho yake kutoka chini

huku mshtuko ukipita ndani yake. Mtu

kama Lina angewezaje kuwa mshenzi

kiasi hicho kumdhuru bibi yake

mwenyewe?

"Nina hakika kwamba lazima

amegundua kuhusu uhusiano wako na Mawenzi Investiments na kwamba

wewe si binti wa kuzaliwa wa Jones"

Aunty Manka alikisia.

"Shangazi Manka, ulipaswa kuniambia kuhusu hili mapema." Lisa alijisikia hatia

sana.

“Nilitaka sana lakini nilishindwa kwa

sababu familia ya Jones ilikuwa

ikinitafuta ili kunidhuru. Sikutaka

kukuingiza katika matatizo makubwa.

Nadhani Jones hakuridhika bila kujua

asilimia 30 ya hisa zimeenda wapi, au labda alitaka kuniua ili nipeleke siri hii

kaburini. Ndiyo maana nimekuwa

nikiishi kwa kujitenga na kujificha, bila

kuthubutu kuonyesha uso wangu

hadharani. Na hata namba za simu

nilibadilisha.” Aunty Manka alimshika

Lisa mikononi na kumwambia, "mtafute

mmoja wa wanahisa huko Mawenzi

Investiments anayeitwa Chris Maganga.

Mama yako aliokoa maisha yake hapo awali. Anazo nyaraka zinazohitajika za kampuni ya Mawenzi."

“Sawa.” Lisa alikubali kwa huzuni, hatimaye akauliza kwa msisitizo, “Shangazi Manka, unajua baba yangu halisi ni nani?”

Mwanamke yule mzee akatikisa kichwa, akihema. "Sina hakika, lakini nadhani anaishi huko Nairobi."

Mwanga wa matumaini ukaangaza machoni mwa Lisa. Ilionekana kuwa

angeweza kupata nafasi ya kukutana na baba yake mzazi siku moja. Hata hivyo, kwa nini alimtelekeza yeye na mama yake? Labda alikuwa ameanzisha familia nyingine kwa muda mrefu.

Wanawake wote wawili katika wadi ya hospitali walinyamaza kimya. Bila kujali, Kelvin alipendekeza, “Kwa ajili ya

usalama wa Aunty Manka, ni bora

tukimhamishia hospitali nyingine ili

akina Jones wasimpate. Namfahamu

mkurugenzi mkuu wa hospitali binafsi

ambaye anaweza kutusaidia.”

“Uko sahihi. Aunty Manka hawezi

kubaki hapa,” Lisa alikubali.

Baada ya hapo, walitumia saa iliyofuata

kuwasilisha makaratasi yaliyohitajika kwa ajili ya uhamisho huo. Hata hivyo,

alipokuwa akiandaa taratibu pale

mapokezi, Lisa alishindwa kumuona

Angela Harrison, yule dada mdogo wa Sam Harrison aliyekuwa anampenda

sana Alvin, ambaye kwa bahati mbaya

alikuwepo kwa ajili ya kumfanyia

uchunguzi wa kawaida mama yake.

Alichukua picha ya Lisa akiingia kwenye lifti na Kelvin.

Angela alimtumia Alvin picha hiyo bila

kusita. [ Alvin, huyu si mpenzi wako?

Ina maana mmeachana? Nilimwona

akiwa na mwanaume mwingine.] Angela

alifurahi baada ya kutuma ujumbe huo.

Kwa muda mrefu alikuwa

amekasirishwa na Lisa na alikuwa

akitafuta nafasi ya kumgombanisha na

Alvin. Sasa, hatimaye alipata nafasi ya kumchongea.

Alvin ambaye alikuwa anatoka kazini

ghafla alisikia simu yake ikitetemeka. Uso wake ulianguka mara ya pili

alipobonyeza ujumbe huo. Picha hiyo ilidhihirisha wazi Lisa na Kelvin wakiwa pamoja hospitalini. Akampigia simu mara moja. “Uko wapi?”

“Um… Hospitalini,” alikiri baada ya kusitasita kwa muda mfupi.

Uso wa Alvin ulilegea kidogo. Angalau hakusema uwongo juu ya hili. “Upo pamoja na nani?”

Lisa alimtupia jicho la haraka Kelvin ambaye alikuwa akiongea na daktari aliyehusika kabla ya kwenda pembeni.

"Nipo na daktari. Mlezi ambaye alikuwa akimtunza bibi yangu ametoka tu kufanyiwa upasuaji. Yeye hana ndugu au jamaa wa karibu wa kumwangalia.

Labda nitachelewa kufika nyumbani

baadaye kidogo leo."

Alvin alijua Lisa alikuwa anadanganya.

Alijua alikuwa na Kelvin. Nia ya hatari

ikaangaza machoni pake. Alvin alijisikia vibaya kwa kuona Lisa akiwa na shida

angependelea kutafuta msaada kutoka kwa Kelvin badala yake. Uhusiano wake na mwanaume huyo ulikuwa wa karibu kiasi gani, kweli?

"Umekasirika?" Lisa aliuliza kwa tahadhari baada ya ukimya wa muda

mrefu kutoka kwa Alvin. "Muuguzi wa zamu anaweza kuja saa tatu usiku, kwa hivyo itabidi nisubiri hadi wakati huo."

"Sawa!" Alvin alijibu kinyonge kabla ya kukata simu ghafla. Kisha, alijaribu

kutuliza hasira yake iliyokuwa ikimpanda kwa kukisugua kichwa chake taratibu.

Alvin alijikumbusha kuwa asiwe na huzuni sana. Alihisi huenda labda Lisa hakuwa na mpango naye ndiyo maana

mara nyingi alikuwa akitaka kuwa karibu na Kelvin.

Simu ilikatika ghafla. Lisa alibaki

akiitazama simu ile kwa sekunde

kadhaa mpaka Kelvin alipomshtua. "Alikuwa Mheshimiwa

Kimaro? Anakuja kumuona Aunty

Manka? Basi labda niende ili kuzuia

ugomvi usio wa lazima.”

"Hapana, hakusema kama anakuja au la." Ghafla, hisia ya ajabu ikatokea moyoni mwake. Hiyo ilikuwa ni hisia

yake tu. Alvin alikuwa hajasema lolote kuhusu kwenda ama kutokwenda

kumuona Aunty Manka.

Kelvin alionekana kushtuka lakini punde

akaonyesha tabasamu. “Naam, ni kawaida. Yeye si familia hata hivyo.”

Alichana na mada hiyo na kumwambia, “nilizungumza na daktari mapema kwa

hiyo usiwe na wasiwasi sana.”

“Asante.” Lisa alikuwa na shukrani za

dhati kwa Kelvin. Asingefanikiwa sana

siku hiyo bila msaada wake. Kwa kweli, alifikiria kumwomba Alvin msaada hapo

awali lakini alipokumbuka tabia yake ya

dharau na kutojali, alikuwa na hakika

kwamba wasingeishia pazuri. Pia

alikumbuka kwenye makubaliano ya ndoa yao alishawahi kumwambia

kwamba hataonana na ndugu zake.

"Ni sawa. Naam, naweza kuondoka

sasa. Nina miadi ya chakula cha jioni kazini jioni hii." Kelvin alielewa umuhimu wa kutovuka mipaka.

“Sawa.” Lisa akamsogeza mpaka

mlangoni.

Alvin hakumpigia simu usiku mzima.

Hatimaye Lisa aliendesha gari hadi nyumbani baada ya muuguzi kujitokeza.

Ukiachana na Charlie na watoto wake

watatu waliokuwa wakicheza huku na kule, alikuwepo Aunty Linda pekee

aliyekuwa akitazama TV sebuleni.

"Mheshimiwa Kimaro yuko wapi?" Swali

hilo lilimshangaza sana Aunty Linda.

“Si alikuaga? Bw. Kimaro alinipigia simu

mapema jioni hii akisema anaenda kwa

safari ya kikazi hadi Nairobi. Hatarudi

kwa siku chache.”

Lisa alipigwa na butwaa na kukaa

kimya. Kwa kweli hakuwa na habari

kuhusu hilo. Lisa aliingiwa na simanzi

sana. Akiwa mpenzi wake, Alvin

hakuuliza kuhusu hali ya Aunty Manka

wala hakumjulisha kuhusu kwenda

safari zake za kikazi. Nini kilikuwa kikiendelea naye?

Baada ya kuelekea ghorofani, alimpigia simu Alvin. Kelele ya mandhari

iliyosikika nyuma ilikuwa kubwa kwenye simu. Aliweza kujua mara moja kwamba

alikuwa mahali fulani pa starehe kama

baa au klabu.

“Uko wapi? Si umeenda kwa safari ya kikazi?” Lisa alimuuliza kwa mshangao.

"Ndio." Sauti yake ilionyesha kutojali.

Lisa hakufurahishwa na jibu hilo.

“Mbona hukuniambia?”

“Kwani ni lazima nikuage kila ninaposafiri?” Sauti yake kujeuri na ya dharau ilimkatisha tamaa.

"Sawa, sitauliza tena siku nyingine."

Lisa alikata simu, akajilaza kitandani na kuanza kulia.

Hata hivyo, Lisa alifurahishwa sana na taarifa alizopata kutoka kwa Aunty

Manka siku hiyo, kwamba mtu alyeamini

kuwa ni shangazi yake kumbe ndiye alikuwa mama yake, na yeye ndiye

mrithi wa Mawenzi Investments. Alitamani kumwambia habari hizo Alvin lakini hakumpa hata nafasi hiyo.

Sura ya 103

Siku mbili zilizofuata, Lisa alitumia juhudi nyingi kupata anwani ya nyumbani ya Chris Maganga. Lakini, mtu huyo aliishi Mwanza muda mwingi.

Hakuwa na chaguo ila kuchukua ndege ya mapema kuelekea huko.

Baada ya kufika kwenye jumba lake, mlinzi alifungua mlango na kuuliza, “Shida?”

Lisa akajitambulisha moja kwa

moja.“Tafadhali mwambie Bw. Maganga

kwamba mimi ni binti ya rafiki yake wa zamani, Sheryl Masawe.”

Mlinzi alimpandisha juu na chini kwa

mashaka kabla ya kupiga simu.

Alipopata jibu, mlinzi huyo alimkaribisha

Lisa ndani kwa upole, “Bw. Maganga anakungoja ndani.” Akaingia mara moja.

Alitarajia kuona kuwa Chris Maganga angekuwa mzee katika miaka yake ya mapema ya 70, kwa hivyo alishangaa kumwona mwanamume wa makamo

ameketi kwenye kochi. Mtu huyu

alionekana mdogo kuliko miaka 40.

Ingawa kulikuwa na mikunjo kwenye

pembe za macho yake, alionekana kuwa bado kijana kabisa. Lazima alikuwa mzuri sana alipokuwa mdogo.

“Wewe ni… Mjomba Chris?” Lisa aliuliza kwa wasiwasi.

Alama ya mshangao ilimtoka Maganga machoni mwake alipokuwa

akimchunguza binti huyo. “Miaka 20

imepita kwa kufumba na kufumbua.

Mtoto mdogo wa kike kutoka wakati huo

umekua sana. Unafanana na mama yako kweli.”

Lisa alikuwa na hamu ya kutaka kujua.

"Nilisikia mama yangu aliokoa maisha yako hapo awali, kivipi?"

"Hiyo ni sawa. Usidanganywe na unachokiona sasa. Wakati fulani

nilikuwa kijana mdogo mwenye madeni makubwa. Kwa bahati nzuri, nilikutana na mama yako, akaniajiri na kuanza kumfanyia kazi. Ndivyo nilivyofika hapa

nilipo leo.” Chris Maganga aliachia tabasamu hafifu huku akikumbuka yaliyopita.

Lisa alipepesa macho taratibu. Machale yake yalimwambia kwamba huenda mwanamume huyo aliwahi kupendezwa na mama yake kimapenzi kwa namna alivyoongea kwa hisia kila alipomtaja mama yake.

"Kwa bahati mbaya ... alikufa angali bado mwanamke mdogo sana,"

Maganga alisema kwa majuto. “Ndiyo.

Sielewi kwanini mama yako aliamua

ghafla kuelekea Kigoma. Wengine walisema ni bahati mbaya lakini

sikuweza kamwe kuondoa hisia

kwamba kuna mtu alikuwa nyuma ya hili. Asingesombwa na kimbunga kama si kwa hili…” Huzuni ilikuwa imeandikwa usoni mwa Chris.

Lisa aliona habari hiyo kuwa ngumu kumeza. "Unamaanisha kuwa mama yangu aliuawa?"

"Ndio, babu na bibi yako hawakujua

lakini nilikuwa nikimfanyia kazi wakati huo." Maganga alifumba macho ghafla.

“Nilichunguza baadaye. Mtu

aliyesababisha kifo chake anaweza

kuwa yuko Nairobi.” Chris alisema na kunyanyuka mara moja kuelekea

chumbani. Lisa alitikisa kichwa kwa unyonge.

"Hizi ndizo hati ambazo babu yako

alinikabidhi ili nizihifadhi." Chris

alishusha pumzi huku akimkabidhi

Lisa faili alilorejea nalo kutoka

chumbani. “Kwa bahati nzuri, babu yako

alikuwa na mpango mbadala dhidi ya

Jones ingawa nina uhakika hakutaka

siku hii itokee. Lakini Jones hakuwa na uhusiano wowote na mafanikio ya Mawenzi Investiments leo. Alitengewa asilimia 30 tu ya hisa kwa sababu ya kukulea, na bado hajashukuru.”

'Hiyo ni sawa. Kama wasingenifukuza mimi, angeweza kupata hisa zote baada ya Bibi kufa, lakini hakutaka kusubiri. Badala yake alimuua bila huruma.” Alizungusha vidole vyake kwenye faili. "Kwa hati hizi, anaweza

kusahau kuhusu kuwa mwenyekiti wa Mawenzi Investiments mwezi ujao."

"Usijali, nitakusaidia kupata nafasi hiyo." Chris akatabasamu.

“Asante Mjomba Chris.” Lisa alihisi kuguswa. “Umekuwa ukifanya kazi kwa ajili ya mama yangu kwa muda mrefu.

Ulishawahi kumuona baba yangu?"

Aliuliza kwa kusitasita.

Uso wa Maganga ulianguka kabla ya

kujibu baada ya muda mrefu, “Nimewahi. Lakini usifadhaike sana.

Hajui uwepo wako."

Ghafla, Lisa alihisi faraja. “Sawa. Ili

mradi tu nimefahamu ukweli kuhusu wazazi wangu.”

“Kwa kweli mchango wake ndiyo uliofanya Mawenzi Investiments kufanikiwa leo. Lakini ... tayari ana familia." Chris alimtazama kwa huzuni.

Lisa alielewa. "Nilitarajia tu. Miaka 20 ni mingi sana. Hakuna mtu ambaye

angengojea milele."

Chris akamuonya. "Kuwa makini na Jones, amekuwa akijaribu kupata upendeleo kwa wanahisa na

wafanyikazi wa ngazi za juu wa kampuni. Lazima uchukue hatua kwa tahadhari."

"Ndio. Hakika nitarudisha kilicho changu.” Lisa alimhakikishia.

Alasiri hiyo, Lisa alikataa mwaliko wa

Maganga wa kukaa muda mrefu na

akapanda ndege ya kurudi Dar.

Aliwasha simu yake baada ya kushuka

kwenye ndege lakini bado hakukuwa na

habari yoyote kutoka kwa Alvin. Hisia ya uchungu ilionekana moyoni mwake.

Alijiuliza nini kilikuwa kimeharibika tena

kati yao.

Baada ya kuwaza mara mbili, aliamua kumtumia ujumbe. [Uko wapi?] Bado

hakusikia majibu kutoka kwake baada ya muda mrefu. Aliamua kuachana na

Alvin na kumtafuta shoga yake Pamela

ili kumpasha habari.

"Hongera, bosi wa baadaye wa

Mawenzi Investiments! Ah, utakuwa na thamani ya mamia ya mabilioni ya

shilingi hivi karibuni. Ninapaswa kukaa karibu nawe na kamwe usinisahau.”

Pamela alicheka vibaya. “Unafikiri Cindy atajisikiaje mara tu atakapojua?”

"Hakuna maana kufikiria juu ya watu wanaoyumbishwa na upepo." Lisa

akatikisa kichwa. “Angekuwa pamoja

nami ningemdhamini hata kwenda

kufanya shooting Afrika Kusini au Ulaya.”

"Lakini nilisikia kwamba ... amepata

bwana tajiri," Pamela alinong'ona, "mtu mashuhuri huko Nairobi. Umaarufu wake umekuwa ukiongezeka hivi karibuni."

Wakati huo huo, Sam alimtumia Lisa ujumbe kwenye WhatsApp. [Lisa, umepata chakula cha jioni? Kama bado

unaweza kuja Millionaires' Pub kwa muziki? Alvin yuko hapa pia. Unaweza

kuja na rafiki yako.]

Moyo wa Lisa uliruka kwa kumfikiria

Alvin. Alimuonyesha Pamela ujumbe huo. "Vipi, twende?"

“Twende.” Pamela alikonyeza macho.

“Ulikuwa unaniambia tu kwamba Alvin

hajazungumza na wewe kwa siku kadhaa. Nini tatizo?”

Lisa akakunja uso kabla ya kusema

tena kwa kufadhaika, “Lazima kuna

jambo linamsumbua. Alikuwa vizuri tu siku chache zilizopita lakini

sasa…Ananiona kama toy! Hajafika

nyumbani kwa siku chache sasa, sijui….”

"Ah, nasikia harufu ya wivu kutoka

kwako!" Pamela alitania.

“Mimi sina wivu. Sipendi tu anavyonichukulia, yaani anapenda niwe nambembeleza na kumyenyekea kila

dakika.” Lisa alikataa kukubali. “Haya, ni bora kwa kuwa mali zangu zitarudi, hatimaye nitapata uhuru wangu tena.”

Kabla hawajaondoka, Lisa

alimkumbusha kitu Pamela. "Sawa, uliendesha gari kuja hapa lakini nina

uhakika kuwa utakunywa pombe

baadaye huko Club, nakushauri

ungemwambia Patrick akuijie baadaye.”

‘Wazo zuri, ngoja nimpigie simu.”

Pamela aliafiki.

Patrick ambaye ni mpenzi wa Pamela

alipopigiwa simu alijibu kinyonge sana, “bado kuna vimeo vichache ninayohitaji

kuvikamilisha ofisini jioni hii, nitakutumia pesa ya usafiri utachukua taxi.”

Katika dakika chache, Pamela alipokea

shilingi laki mbili kwenye akaunti yake

ya m-pesa. Hakuweza kumlaumu au

kumkasirikia tena mpenzi wake, kwani

alionyesha kumjali hata hivyo.

Sura ya 104

Millionaires' Pub ni Club ya starehe

iliyopo Masaki ambayo hutoa huduma

kwa matajiri wenye hadhi ya umilionea pekee. Huwezi kuingia kama humo

kama weye ni hohehahe ama hadhi yako ni chini. Si ajabu kukuta bia

ambayo inauzwa elfu na mia tano

mitaani pale ikauzwa elfu hamsini au zaidi. Usishangae kuuziwa sahani ya chipsi kwa elfu hamsini, na vitu kama

hivyo.

Saa mbili usiku, Lisa na Pamela ndo

kwanza walikuwa wanaingia pale

Millionaires' Pub walipoona

mwanamume na mwanamke

wakitembea kuelekea kwao kutoka

upande wa pili. Mwanamke aliyevalia

vizuri alionekana mrembo wa kuvutia

sana. Mwanaume naye alikuwa

ametokelezea kiroho safi. Kwa kweli

walikuwa wamevunja kabati siku hiyo. Papo hapo, Pamela alihisi

kufadhaika kabisa. Mwanamume

aliyekuwa ametoka kumwambia muda si mrefu kwamba alikuwa amebanwa sana na kazi ofisini alikuwa

amesimama mbele yake akiwa na mwanamke mwingine.

Lisa alikunja uso. Alimvuta rafiki yake hadi kwa wawili hao na kusema kwa

tabasamu la kubandika, “Bw. Patrick, ni sadfa iliyoje! Nilidhani ulimwambia

Pamela unafanya kazi za ziada ofisini?

Ulisema ulikuwa na shughuli nyingi na usingeweza kuja kumchukua baadaye, mbona sasa upo hapa tena na mtu

mwingine?" Kauli yake ya moja kwa moja ilimfanya Patrick aone haya.

"Ilibidi nifanye kazi ya ziada lakini Linda

alniipiga simu kusema kuna mtu

alikuwa akimsumbua, kwa hivyo nilifika hapa mara moja kumsaidia."

Linda akaongeza haraka, “Hiyo ni kweli.

Pamela, nina hakika umewahi kusikia

kuhusu Master Cook. Yeye ni mkorofi kama nini."

Pamela alitingisha tu kichwa chake. Lisa alisema, akitabasamu. “We binti, nakuonea wivu sana kwa kuwa na kaka anayekujali. Sio tu kwamba

anahudhuria kila sherehe na wewe

kama mwenza wako wa kiume bali pia

anakimbia haraka mara moja kukuokoa unapokuwa na matatizo. Lakini huenda

usiweze kupata mchumba ikiwa utaendelea na tabia hii. Wanaume

wengine wanaweza wakafikri kuwa nyinyi wawili ni wapenzi.”

Bila kutarajia, sura iliyochanganyikiwa ilitanda kwenye uso wa Linda. “Lisa, unajaribu kusema nini? Kwa nini

huamini kwamba sisi hatuna uhusiano mbaya? Umefikiria jinsi maneno yako

yanavyoweza kumuathiri Pamela?"

Patrick pia alikunja uso baada ya

maneno hayo ya Lisa. Linda akageuka

kumtazama kwa hatia. “Patrick,

samahani. Unapaswa kwenda kwa

Pamela. Nitatoka mahali hapo haraka nikihisi hatari yoyote.”

Kwa hasira, Patrick akamtupia jicho

Lisa. "Bi Jones, kama kuna mambo

ambayo huelewi, nakushauri usiwe unachonga mdomo wako."

Lisa akafuatia na kusema. "Nilikuwa tu nampa ushauri wa kirafiki ..."

“Tunajua tunachofanya bila kuhitaji ushauri wako,” alikatishwa kwa maneno yaliyonyooka.

“Kweli? Nadhani hujui unachofanya.”

Pamela alihisi hasira ikizidi kumpitia rafiki yake alipotukanwa. "Unakimbia mara moja kila wakati Linda anapokuhitaji. Lakini vipi kuhusu mimi?

Nilienda hospitalini peke yangu

nilipougua na nilichukua teksi

kunipeleka nyumbani baada ya kurudi

kwa safari ya ndege usiku wa manane.

Siku hizi hata hutoki kula chakula

pamoja nami tena…”

“Tafadhali usimsikilize rafiki yako. Moyo

wa Patrick upo kwako tu.” Linda alisema

kwa haraka.

"Funga mdomo wako." Pamela

alimfokea mwanamke huyo, “Kama mnapendana kwanini msiweke wazi tu nikawaachia uhuru wenu?”

“Pamela, sikuwa…” Machozi yalitiririka mashavuni mwa Linda.

Patrick hakuweza kuvumilia zaidi na

mara moja akapiga hatua mbele ya Linda. “Pamela Masanja, una tatizo gani? Linda hajafanya lolote la kukukera. Kwanini ukubali

kushawishiwa kwa urahisi na rafiki yako? Jifunze kufikiri kwa kujitegemea,” alifoka.

"Uko sawa, mimi ni mjinga, na ndiyo sababu nilikukubali." Kisha kusema

hayo, Pamela akamshika Lisa kwa

mkono na kuondoka hadi ghorofa ya pili.

Nyuma yake, Linda alimhimiza

mwanaume huyo. “Patrick, mfuate

haraka ukambembeleze. Amekasirika.”

"Aah! Achana naye bana. Kwa nini

unamjali? Hukusikia alichosema sasa hivi?”

“Nilisikia kila kitu. Lakini….”

"Achana naye..."

Pamela alisikia sauti zao zikitokomea kwa mbali nyuma yake. Machozi ya hasira yalianza kuteremka kwenye mashavu ya Pamela alipokuwa

akipanda ngazi. Kwa bahati nzuri, Lisa alikuwepo kumshikilia.

"Samahani, sikupaswa kusema hivyo."

Lisa alimfariji.

“Siku zote nilitaka kusema hivyo, sema wewe umenisaidia tu." Pamela alifuta machozi kwa nyuma ya mikono yake.

"Uligundua kuwa kuna kitu kibaya

baada ya kuona mwingiliano wao mara

mbili. Lakini mara ambazo nimemwona

Linda akiwa na Patrick zinakaribia

kulingana na zile nilizotoka na Patrick.”

Jambo hilo lilimshtua Lisa. Alikuwa

akisoma nje ya nchi kwa miaka

michache iliyopita, kwa hivyo

hakufahamu sana juu ya maisha ya mapenzi ya rafiki yake. Tabasamu la uchungu lilienea kwenye uso wa Pamela.

“Mara saba kati ya mara kumi tulizotoka na Patrick, alikuwa na Linda, hata

kwenye ukumbi wa sinema. Mara nyingine tatu tulipokaa peke yetu, angeondoka baada ya muda mfupi kwa sababu alipigiwa simu na Linda.”

“Mbona hukuniambia?” Lisa alijisikia vibaya lakini pia alikasirika kwa wakati

mmoja. “Basi, sikupaswa kuwa mpole. Ningewapaka zaidi ya hapo.”

“Sikutaka kukuona wewe na Patrick mkipigana,” Pamela alisema kwa

huzuni, “Ninampenda sana na nilijaribu kwa muda mrefu kumfanya awe pamoja

nami. Pia niliiambia hadi familia yangu

kwamba nitampeleka nyumbani

Krismasi hii. Ndiye mtu ninayetaka kuolewa naye.”

Lisa alisema kwa hasira, “Ikiwa siku

zote anachukua upande wa Linda, inawezekana kwamba mtatalikiana hata mkifunga ndoa.” Hii ilimshangaza

Pamela. Alionekana kuchanganyikiwa kabla ya kutikisa kichwa polepole.

“Usifikirie sana kwa sasa. Zimisha hisia zako na pombe. Nitakupeleka nyumbani baadaye.” Lisa alimshika mikono na wakatembea kuelekea ukumbi binafsi

aliokodisha Sam kwa ajili ya ‘bata’ hilo usiku ule.

Mlango ulisukumwa na mbele yao

wakaonekana watu kumi au

zaidi waliokuwa wameketi ndani ya ukumbi huo wa kupendeza. Kati ya

umati mkubwa, alimjua tu Sam

Harrison, Clark Zongo, na mtu aliyeketi

kwenye kona ya mbali… Alvi Kimaro.

Kiyoyozi kilikuwa kimewashwa. Alvin

alikuwa amevaa shati jeupe na

ameshika glasi ya mvinyo katika mkono

wake wa kushoto. Ilikuwa ngumu

kutomtambua mtu huyo aliyeonekana

kama mfalme miongoni mwao.

Pia alikuwa katikati ya tahadhari, alikuwa makini zaidi hata katika chumba kilichojaa watu. Hata hivyo, Alvin

hakumtazama Lisa tangu alipotokea. Macho yake hayakutilia maanani kabisa

ujio wake. Jambo hili lilimtia aibu Lisa. Ghafla, alijutia uamuzi wake wa kwenda pale.

"Halo, warembo Lisa na Pamela!" Sam

aliwasalimia kwa shauku. "Nendeni mkakae na Alvin." Baada ya kusitasita

kidogo, alimnong’oneza Lisa sikioni, “Alvin hayupo hapa kimawazo. Nenda ukaongee naye.”

Lisa pia aliingiwa na kiburi, kwanini yeye awe wa kwanza kumfuata

Alvin? Kwa kweli alishindwa kutembea

kumfuata wakati Alvin alikuwa akijifanya

hamjui kabisa. Kwa hivyo, Lisa alibaki

kama kaota mizizi kwenye miguu.

Kwa bahati mbaya au nzuri, Clark

Zongo alimpa ishara na kusema, “Lisa, njoo uketi hapa.”

Watu wengi walimgeukia waliposikia

hivyo. Pamoja na hayo, bado Alvin

alikuwa busy tu akiongea na mtu aliyekaa karibu yake. Uso wake

uligeukia upande mwingine na kumpuuza kabisa Lisa kana kwamba

hakuwa na uhusiano wowote naye. Kwa hasira, Lisa alimkokota Pamela

kuelekea kwa Clark. "Bwana Zongo..."

"Lisa, njoo tafadhari nina deni kwako.

Nimekuwa nikikusudia kukuomba

msamaha siku nyingi lakini sikupata

nafasi ya kuonana na wewe,” Clark

Zongo alisema kwa dhati. "Sikuelewa

mara ya mwisho na karibu nikutupe gerezani. Ingawa ulishinda katika kesi

ya mahakama, angalau nilipata kujua ni nani hasa aliyekuwa akijaribu

kunichezea.”

"Bwana Clark, bila samahani, bila shaka

mahakama iliwawajibisha wale wote

waliohusika kwa kile kilichotokea."

"Sawa, acha yaliyopita yawe yamepita basi." Wawili hao walipeana toast kabla

ya kuanza kujadili mradi wa hoteli ya

Lublin.

Kwa pembeni kabisa, Alvin, ambaye

aliwaona wakipiga soga na kucheka

kwa furaha, alihisi hasira ikipanda ndani yake. Joto la hewa karibu naye

lilionekana kuwa limeshuka sana.

Sura ya 105

Wakili aliyekuwa akizungumza na Alvin

alihisi tofauti ya ghafla katika

mazungumzo ya Alvin na akanyamaza

haraka. Alichukua glasi yake ya mvinyo

na kwenda kujiunga na mchezo wa pool pembeni.

Sam alimfuata Alvin. Aliketi karibu na rafiki yake na kumwambia taratibu.

“Kaka nimeshamkaribisha Lisa hapa

kwa wema. Utaacha lini tabia yako ya kumkaushia?"

“Una uhakika hukumwalika hapa kwa

ajili ya Clark Zongo?” Alvin alidhihaki

kwa kejeli.

“Noo.” Sam hakuwa na uhakika wa

kusema. "Kweli, wewe ndiye ambaye

hukuonyesha kupendezwa alipojitokeza."

Tabasamu la kujilazimisha likaangaza usoni mwa Alvin. "Hah, achana naye.

We endelea na mishe zako tu.”

Wakati huo huo, watu wengine

wachache waliingia ukumbini. Alikuwa ni Stephen Kileo pamoja na dada yake, Janet Kileo wakiwa wameambatana na Lina Jones. Sam alishindwa cha

kusema. Hakuwa amewaalika watu

wale na hakujua walijuaje kwamba

ameandaa ‘bata’ kwa ajili ya marafiki

zake. Ilionekana kama vile alipanga

kualika maadui wakubwa katika chumba

kimoja. Alikuwa na utabiri kwamba kitu

kibaya kingetokea.

Stephen Kileo alikagua chumba kwa

macho makali kabla ya kuelekea kwa

Sam. “Bw. Harrison, nilikuwa tu

nikitembea na marafiki zangu kwenye

ukumbi mwingine. Master Cook

akaniambia kwamba wewe pia uko

hapa, kwa hiyo nilikuja kukusalimu. Na huyu… lazima awe wakili anayeheshimika, Bw. Kimaro. Nimesikia mengi juu yako na nimefurahi hatimaye kukuona ana kwa ana.”

Alvin hakutetereka, aliendelea kubaki na sura ya dharau na kutojali usoni mwake.

Lakini, Sam hakuweza kufanya vivyo hivyo. Ilibidi amjali Janet na kaka yake.

Stephen ndiye aliyekuwa kaka mkubwa na mrithi mpya wa biashara za familia ya Kileo, kwa hiyo ilimbidi aonyeshe heshima. Mbali na hilo, familia ya Kileo ilikuwa ikipata nguvu na ushawishi mkubwa wakati huo.

"Hongera, Bw. Kileo, kwa kuchukua biashara ya familia." Sam alimtupia jicho la haraka Lina huku akiweka tabasamu usoni mwake. "Lakini kwa nini uko na mwanamke wa familia ya kutisha ya

Jones? Kwani hakuna samaki tena

baharini mpaka unaamua kwenda kuvua kwenye vidimbwi?"

Stephen alicheka kwa sauti kubwa

kabla ya kumshika Lina karibu na

kumbatio lake na kupiga kelele, “Sikilizeni kila mtu, wacha

nimtambulishe mpenzi wangu, anayejulikana pia kama binti Jones

Masawe—mwenye hisa mkuu wa Mawenzi Investiments.”

Kila mtu aliingia kwenye mjadala mkali. Wote Sam na Alvin walishtushwa na

habari hiyo."Hapana, tangu lini Jones

Masawe akawa mwenye hisa mkuu wa

Mawenzi Investiments?"

“Unadiriki kutudanganya?” Alvin aliuliza.

“Stephen, tuachane nayo,” Lina alisema kwa haya.

“Kwanini? Sio uongo kusema wewe

ndiye mwanamke kijana tajiri kwa sasa, kutokana na hadhi yako mpya.” Stephen akambusu Lina shavuni. "Hata sijui

niliwezaje kupata hazina kubwa kama wewe!"

"Acha bwana." Lina alishusha macho

yake chini huku akionekana kuwa na aibu.

Janet alimtupia jicho Lisa aliyekuwa

kando kabla ya kusema kwa sauti, “Ndugu yangu hapa hapakufai. Ukijilinganisha na wengine wewe humu una nini? Humu tunaingia watoto wa matajiri tu kama vile warithi wa Mawenzi Investiments, pesa ni za kusaini tu muda wowote. Na wewe mpaka usubiri kuajiriwa au kupewa vijihela na bwana wako utaweza wapi mambo haya?”

Chumba kikawa na fujo. "Wow, kwa hiyo Lina ndiye atakuwa mrithi wa Mawenzi siku zijazo?"

"Halo, Bi Jones, nilikuwa na mpango wa kukutana na watendaji wa Mawenzi Investiments hapo awali. Tunaweza kupata nafasi ya kuonana na kuongea jambo?” Jamaa mmoja akaona fursa papo hapo.

Lina aligeuza uso wake wenye tabasamu na kusema. “Bila shaka.

Msipojali, nyote mnakaribishwa

kujumuika nasi katika ukumbi niliokodi upande wa pili.”

“Twendeni.” Stephen alisema kwa

bashasha. “Sam Harrison, mnakaribishwa pia.”

Baada ya dakika chache, ni Lisa, Pamela, Alvin, Clark, na Sam pekee

ndio walioachwa kwenye ukumbi wa faragha uliokuwa umechangamka sana

hapo awali.

“Nakufahamu wewe Stephen Kileo.

Unafanya hivi kwa malengo yako, siyo bure, sawa?” Sam alimuuliza Stephen

kwa sauti ya chini kabla hajaondoka.

"Nadhani unanijua vizuri. Watu wenye fedha hufuata pesa zilipo." Stephen

alimjibu kwa kejeli. "Labda hivi karibuni pia mtalazimika kuniabudu kama kijana

tajiri zaidi Masaki nzima, tehtehteheee…”

"Utakuwa unaota kama bado unafikiria

kupata mafanikio kwa njia za kijima

kama hizo." Sam alimnyooshea kidole

Lina na kucheka kwa kejeli. “Mwanamke

gani huyu unayejivunia? Alikuwa

mchumba wa mtu mwingine mwezi

uliopita tu, leo unatutambia kwa

mbwembwe utadhani umepata bikira?"

Hasira kali ilujaza uso wa Lina ndani ya sekunde chache. “Sam, chunga kauli

zako. La sivyo, mara baba yangu atakapokuwa mwenyekiti wa Mawenzi

mwezi ujao, ninaweza kuiangusha familia ya Harrison mapema kabisa.”

Lisa aliyekuwa akisikiliza pembeni alicheka kejeli. “Usijiaibishe sana.

Itakuwa aibu kubwa kama hilo halitatokea.”

"Hiyo ni sawa." Pamela alicheka kwa furaha. "Familia ya Jones ina sifa

mbaya. Ni bora kutolichafua jina zuri la Mawenzi Investiments pia.”

"Nimekubali," Sam aliingia pia, akicheka.

"Chekeni mnavyotaka, ongeeni yote

mnayotaka, ila nitawaona nyote

mkifyata mikia yenu baada ya mwezi

mmoja tu." Kwa uso ulionyooka, Lina

alimshika Stephen kwa kifundo cha

mkono na kuondoka kwenye ukumbi ule

wa matajiri.

Janet aliyeachwa nyuma, alijisogeza

karibu na Alvin huku akitabasamu kwa

upole. "Bwana Kimaro, kwanini usiende na sisi? nina machache ya kukuambia.”

Alvin alimtazama tu kwa kejeli. Janet

hakujali kuonekana mtovu wa akili.

Tangu alipomwona Alvin kwa mara ya

kwanza kule kwenye mgahawa wa Grapefruit, kwa kweli alivutiwa naye

sana. Hakuwahi kumwona mwanaume mwingine wa kifahari zaidi yake.

Pamoja na uzuri wake, Janet aliona

Alvin haendani naye kwa hadhi ya utajiri

wa familia yake. Hata hivyo, baada ya

kujua kwamba alikuwa wakili bora zaidi

wa kimataifa, alifikiri kwamba

wangeweza kulingana kikamilifu.

"Bwana Kimaro, labda hujui mengi

kuhusu familia ya Kileo.” Janet

aliendelea kujinadi huku akitabasamu.

"Familia ya Kileo ina utajiri wa zaidi ya

shilingi bilioni 50 za mali na kwa sasa

tunawekeza katika biashara ya mavazi, usafiri, fedha, teknolojia na sekta

nyinginezo. Hivi karibuni, tutashirikiana na Mawenzi Investiments, ambayo ni mojawapo ya makampuni 100

yaliyofanikiwa zaidi Tanzania. Siku

zijazo kwa kweli naamini tutazipita

familia zote tajiri hapa jijini.”

"Pfft." Kicheko kilimponyoka Sam

mdomoni bila kupenda. Alitamani sana

kumfokea yule binti asiye na haya

ambaye alikuwa akijitongozesha kwa

mtu tajiri zaidi kuliko familia yake.

Uso wa Alvin ulimsisimka huku

akitamani sana kumsukuma yule binti.

Harufu kali ya pombe iliyokuwa ikimtoka

mdomoni ilikuwa inashambulia pua

zake. Hata hivyo, baada ya kumwona

Lisa akiwatazama pembeni, aliizuia ile

jazba yake na kuibana midomo yake

kimya kimya.

Akifikiri alikuwa amepata nafasi, Janet

kwa ujasiri alilaza kichwa chake kwenye

bega la Alvin na kumwambia kwa

mahaba. "Ikiwa uko tayari kuwa mtu

wangu, utakuwa na pesa nyingi kuliko utakayopata maisha yako yote kwa

kufanya kazi kama wakili."

Macho ya Alvin yaliganda. Janet akajua hiyo ilikuwa ni ishara ya kueleweka, akazidi kumnong'oneza sikioni, "Lisa hakufai, yeye sio maskini tu bali pia mjinga. Mimi ni bora kuliko yeye.”

Mkono wake ukasogea taratibu kwenye kifua cha Alvin. Lisa hakuweza

kutazama tena kwani hisia kali za hasira

zilimpanda. Alichukua glasi ya mvinyo na kumkimbilia Janet kabla ya kumtupia usoni. Vipande kadhaa vya barafu hata vilitua kwenye kichwa chake.

"Ah, Lisa Jones! Umerukwa na akili!”

Janet alipiga kelele kwa hasira na akasimama kwa nguvu. Mara moja

akatoa leso ili kujifuta uso na mwili wake.

“Nadhani wewe ndiye uliyerukwa na akili. Ni dhahiri kwamba uko kwenye

joto, kwa hivyo ninakusaidia

kukupunguzia joto." Lisa akakaa

mapajani mwa Alvin kabla ya kusema kwa ujeuri, “Ninakuonya kuwa kaa naye

mbali, huyu ni mtu wangu. Nitakukata mkono ikiwa nitakuona ukimgusa tena.”

“Mtu wako?” Janet alicheka kana kwamba ameambiwa utani. “Ulikuwa

umekaa mbali naye sana hapo awali, una uhakika kuhusu hili? Mapenzi ya upande mmoja huishia katika fedheha wakati mwingi.”

Lisa alikosa kujiamini kwa sababu muda

wote Alvin alikuwa kimya. Hata hivyo, kejeli za Janet zilimfanya asiwe na chaguo zaidi ya kumlinda mtu wake.

Wakati huohuo, sauti kali ya Alvin

ilisikika nyuma yake. “Hebu tokeni nje.”

Sura ya 106 Rangi zote zilitoka kwenye uso wa Lisa

ndani ya sekunde chache, akidhani

kwamba kauli hiyo ilimlenga yeye pia.

“Ninamaanisha wewe.” Alvin aliinuka

taratibu, akaupanua mguu wake mrefu

na kumpiga teke Janeth kwenye kochi. Kila mtu alishtuka. Binti huyo alipiga

kelele, "Alvin Kimaro, unafikiri wewe ni nani?! Unathubutuje kunipiga teke!

Sitakucha kwa hili.”

“Oh, kweli? Ngoja nione basi.” Akiwa na sura ya kuchukizwa usoni mwake, alinyakua kitambaa kutoka mezani na

kujifuta bega kwa uangalifu ambapo

Janeth alikuwa ameegemeza kichwa

chake muda mfupi kabla.

Hasira ndani ya moyo wa Lisa ilitoweka

ghafla baada ya kuona vile. Angalau

Alvin alifanya jambo sahihi. Vinginevyo, angeweza tu kumchukia milele.

“Alvin, utajuta kwa hili. Ngoja uone. Siku

moja, utakuja kuniomba mwenyewe

nilale na wewe.” Janet aliuma meno na kuondoka baada ya kudhalilishwa.

Sam alimkaripia yule binti, “pumbavu!

Unadhani unastahili kulala na Alvin

wewe? Takataka! Rundo la kinyesi wewe!”

Pamela na Clark walishindwa kuzuia

vicheko vyao. Lisa na Alvin pekee ndio walibaki na nyuso zilizonyooka.

“Una hata jeuri ya kusema hivyo?

Tazama umati mchafu ulioalika leo.”

Alvin alimshushua rafikiye Sam kwa tabasamu la kejeli.

Sura ya aibu iliufunika uso wa Sam.

"Sijawaalika mimi wehu hawa

wamevamia tu. Bora wameenda, njooni tunywe na tuendelee na furaha. Ni wale

wa kweli tu ndio waliobaki humu.”

Aliongoza na kuchagua wimbo. Pamela alimfuata pia na kuchangua nyimbo

kadhaa na kuziweka kwenye playlist.

Ukumbi mkubwa ukawa mtupu ghafla.

Kwa bahati mbaya, Lisa alikuwa

ameketi kati ya Alvin na Clark. Uso

wake ulitiririka kwa aibu. Kweli, alikuwa

amedai hadharani tena kwa kiburi

kwamba Alvin alikuwa mtu wake muda si mrefu. Oh hapana…

iliyokuwa karibu naye huku akimtaka

Lisa asogee. Hakuwa na la kufanya

zaidi ya kujisogeza karibu zaidi na Alvin hata wakagusana kabisa.

Akamkumbatia mkono mmoja na kumshika kidevu kwa mwingine.

"Ulitangaza mapema kwamba mimi ni mtu wako?" Alisema, akiinua macho

yake kumtazama.

Lisa alihisi mashavu yake yakiwaka

moto. Alipotazama moja kwa moja ndani ya kina cha macho yake yenye

giza, hakuweza kujua ni nini kilikuwa akilini mwa Alvin, lakini alimtazama na kusema, “Hiyo ni kweli, wewe ni mtu wangu. Nirekebishe wakati wowote

ikiwa unaona kuwa hii si sawa. Naahidi

sitakusumbua tena.” Hisia ngumu

ikaangaza machoni pake. Hakujua

kama ahisi hasira au furaha.

Alvin alionyesha kuguswa na kufurahi

ghafla. “Sawa, nimefurahi bado

unakumbuka msimamo wako. Lakini

"Sogea karibu." Alvin akapapasa nafasi

kwa nini huwa unasahau niliyosema?

Kwanini unafurahia kuzungumza na wanaume wengine?"

Lisa alishtuka, akakumbuka alikuwa anazungumza tu na Clark mara baada ya kuingia ukumbini mle. “Clark alikuwa akinishukuru mara baada ya kuniona.

Nilitaka kuja kuketi karibu nawe lakini

wewe… Kwanza hujafika nyumbani kwa

siku chache zilizopita na bado uliendelea kunipuuza hata uliponiona nikiingia. Ulijifanya hunijui kabisa.” Sauti yake ilishuka kuelekea mwisho.

Ilionekana kuwa alikuwa na aibu na alihisi kama alikuwa amekosewa.

“Una jeuri ya kusema hivyo? Nachukia

sana wanawake wanaponidanganya,”

Alvin alisema huku akikoroma. “ Mimi

simaanishi Clark Zongo. Nilikuambia

usikae karibu na Kelvin lakini

hukunisikiliza. Unafikiri ninaweza

kukuvumilia na kukusamehe kila mara?”

Hatimaye ikawa wazi kwake.

"Unamaanisha tukio la hospitali siku

chache zilizopita, ulijuaje?" Aliendelea kuwa na uso ulionyooka ingawa macho

yake yalionyesha wazi kutofurahishwa.

"Nilikuwa Mbezi Beach wakati huo

nilipokea simu kuhusu Aunty Manka. kelvin alikuwepo kwa bahati kwenye

saiti kuangalia maendeleo ya kazi.

Alinisikia kwenye simu na kuniambia

kuwa anamfahamu mtu kutoka

hospitalini hivyo alitaka kunisaidia ndo

nikaongozana naye. Ni hayo

tu,”Lisa alieleza.

Alvin hakujisikia faraja aliposikia hivyo

lakini alikata tamaa zaidi. “Hukuja

kwangu mara moja ulipohitaji msaada.

Badala yake, ulimgeukia mtu ambaye

anavutiwa nawe. Lisa Jones, mimi ni nani kwako na Kelvin ni nani kwako?"

“Hapana, nilizungumza na Kelvin na anaelewa pia—”

“Usithubutu kuniambia kwamba

anakuona tu kuwa rafiki sasa hivi.”

Alitabasamu kwa kejeli. "Kwa hivyo

utakuwa sawa na mimi kuwa na urafiki na wanawake ambao walijaribu

kunishawishi hapo awali?"

Hilo lilimshangaza. Baada ya kujiweka

katika viatu vyake, hatimaye aligundua kosa alilofanya.

"Samahani." Muda mrefu baadaye, aliinamisha kichwa chake. “Nitakupigia simu mara moja nikihitaji usaidizi siku nyingine na sitakubali msaada kutoka

kwake tena. Hakika nakujali wewe tu.”

Alvin akamuachia na kuwasha sigara.

Alipovuta pumzi na kuzitoa, moshi ukafuka kimya kimya.

Kwa bahati mbaya, aligundua wimbo wa mapenzi ambao Pamela alikuwa

ameweka ulikuwa ukiisha. Wazo

likamjia akilini. Alikimbilia kwenye

mashine ya kucheza muziki na kuuweka

wimbo huo kwenye playlist. Baada ya

dakika chache, wimbo wa mapenzi

uliokuwa ukitamba ulijaza chumba. Kila

mtu alijua ni wimbo gani huu na mara

akageuka na kumtazama Lisa kwa

mshangao. Mashavu yake yalimtoka kwani ilikuwa ni mara yake ya kwanza kujaribu kitu kama hiki hadharani. Hata hivyo, alipoona mwonekano mzuri wa Alvin, alivuta pumzi ndefu kabla ya kuogea hadharani kwa aibu. "Ningependa nitoe dedication ya wimbo 'Tupendane' kutoka kwa Wananjenje, kwa mtu ninayempenda."

Alimtazama Alvin haraka baada ya kusema hivyo. Alvin aliinua macho yake

kumtazama. Mwangaza mkali

ulioning'inia kutoka kwenye dari

ulimwangazia usoni mwake. Aliona mashavu hayo mekundu na macho yaliyokuwa yakimeta kama nyota

zinazometa angani usiku. Alihisi kuna

kitu kilikuwa kinaonekana moyoni

mwake. Sam alipiga mluzi na kuanza kupiga

makofi. “Oh, jamani Lisa! Alvin, umesikia hivyo? Anakiri kukupenda.”

Alvin aligeuza uso wake bila kutoa

maoni. Alisimama na kumtazama moja kwa moja Lisa.

Lisa alinyanyua kipaza sauti na kukisogeza kwenye midomo yake

taratibu.

"Mpenzi wangu, ninaombaa…nikueleze pendo, langu lililo moyoni, moyoni mwanguuu…,

"Mpenzi wangu, Mwenyezi Mungu, muumba ardhi na mbingu, ndiye shahidi wa pendo, mhh…moyoni mwanguuu…

"Mapenzi niiii…kuvumilianaaa…Nami mpenzi, nimekuvumiliaaaa…,

"Mapenzi niii ...Kuaminianaaa….Nami mpenzi nimekuaminiiii…."

Hakuwa amemsikia akiimba hapo awali.

Sauti yake tamu na nyororo ilituliza

moyo wake na kutoa burudani masikioni

mwake. Kusikiliza muziki haikuwa tabia

ya Alvin, sembuse muziki wa kiutu

uzima kama huu, lakini, alihisi wimbo

huo kuwa mzuri sana wakati huo.

Nyimbo iliisha. Ilikuwa huzuni sana

kwamba iliisha haraka. Watu wote

walianza kupiga makofi. Wote wawili

Sam na Pamela walianza kupiga kelele.

" Busu, busu, busu ..."

Akiwa na aibui, Lisa alimkodolea macho

rafiki yake wa karibu akitamani kwenda kujiunga naye.

"Njoo hapa." Alvin akampungia mkono.

Lisa alitembea kuelekea kwake kwa

aibu. Alvin alimweka kwenye mapaja yake, akamshika uso wake mdogo, na

kufunga midomo yake kwa midomo yake.

Lisa, akiwa na aibu kufanya hivyo

hadharani, alitamani apotee hewani

papo hapo. Hata hivyo, alipofikiri

kwamba hakuwa na hasira naye tena, alimbusu kwa upendo.

Bila kutarajia, Alvin alipoteza fahamu

zake kabisa katika busu hilo. Moyowake

uliachilia kabisa chuki za mvutano wote

uliokuwa ukijengeka ndani yake katika

siku chache zilizopita. Hata hivyo, wengine bado walikuwa wakiwatazama.

Lisa alijisikia kulia kwa aibu. Haraka

alitazama huku na huko baada ya busu kuisha, akagundua kwamba wengine

tayari walikuwa wameenda upande mmoja kucheza pool.

Sam alicheka na kumwambia. “Njoo ujiunge nasi kwa kuwa umemaliza kumbusu. Tayari tumemaliza mechi chache tangu wakati huo.” Alihisi

mashavu yake yakimtoka kwa mara nyingine.

“Hapana,” Alvin alijibu kwa uvivu na kuuzika uso wake kwenye nywele zake ndefu. “Tunaelekea nyumbani.”

"Bado." Lisa alimzuia. "Pamela amekuwa akinywa pombe. Nahitaji kumsindikiza kwenda nyumbani.”

"Atachukua teksi."

Lisa alisita kwa muda mfupi kabla ya kukataa. "Hapana, aligombana na mpenzi wake na niliahidi kumrudisha nyumbani. Siwezi kumpuuza kwa

sababu nimekuona wewe.”

Sura ya kukasirika ikaangaza tena usoni

mwake. "Unamaanisha nini, mimi si muhimu kuliko rafiki yako?”

"Bila shaka wewe ni muhimu sana, lakini marafiki ni muhimu pia." Lisa

aliweka wazo hilo moyoni na kujibu kwa sauti ya kupendeza, “Hey, acha kuwa

na haraka kupita kiasi. Hatujawahi

kutoka na kufurahi kama hivi, kaa

kwanza. Kuna mengi zaidi nataka kukuambia.”

Alvin alilegea na kukaa. Bila kujizuia, Lisa alimweleza yote aliyoyasikia kutoka

kwa Aunty Manka katika siku chache zilizopita.

Alvin alitabasamu kwa furaha huku

akielewa picha kubwa sasa.

"Inaonekana kujeruhiwa kwangu

kwenye saiti ya ujenzi mara ya mwisho

haikuwa ajali pia lakini mpango kutoka

kwa familia ya Jones. Kweli, vizuri, wanathubutuje kunidanganya?"

Mtu wa mwisho aliyemsababishia

madhara hakuwa tena katika ulimwengu

huu. Wawili hao, baba na binti Jones

walikuwa na hamu ya kuishia gerezani. Alvin akatoa simu yake kuitafuta namba ya Hans.

"Unafanya nini?" Lisa aliuliza.

"Nataka kumwambia Hans aandae hati ya mashtaka kwa ajili ya bwana na bibi

Jones, nawashtaki kwa mauaji." Kiburi kilionekana katika sauti yake.

“Usifanye kwa kukurupuka. Familia ya Jones Masawe imeanza kupata

ushawishi mkubwa kwa sasa na huwezi kumudu kuwashtaki, wanaweza

wakakusumbua sana. Mbali na hilo, wanapanga kuunganisha nguvu na familia ya Kileo kupitia ndoa. Wataipiku hata familia yenye nguvu zaidi hapa

Masaki kwa sasa, familia ya Harrison.”

Alvin akanyamaza. Eti hawezi kumudu

kuwashtaki? Alvin alihisi kucheka.

"Usijali,

Lisa alimfariji

kwa dhati. “Ninapanga kujiunga na

Mawenzi Investiments kupigania nafasi

ya Mwenyekiti wa bodi iliyo wazi.

nitalipiza kisasi."

Nitahakikisha kwamba familia ya Jones

inaangamizwa mwishowe na mimi

binafsi nimtupe gerezani muuaji wa bibi yangu.”

Alvin alimwangalia Lisa na

kumlinganisha na uzito wa maneno aliyotamka. Hakuweza kujua kama Lisa

aliongea kwa dhati ama kwa kujiridhisha tu. Hakuongea lolote bali uso wake

haukuonyesha imani kwa maneno ya Lisa.

Lisa alikohoa kidogo na kuendelea.

"Niamini kwamba nina ushahidi wa 100%. Mawenzi Investiments

ilianzishwa na mama yangu na lazima

niirudishe. Hilo likitokea… ninaweza

kukusaidia kifedha pia ikiwa unataka

kustaafu kutoka kwenye kazi ya uanasheria.”

“Umh, sawa. Nitasubiri siku hiyo.”

Tabasamu la fumbo lilimwangazia usoni mwake.

Hakika, ikiwa ndivyo alitaka, basi Alvin

asingeingilia kati. Hakuweza kusubiri

kuona ni kiasi gani alikuwa amekomaa

katika miezi michache iliyopita. Baada ya yote, ilibidi akabiliane na familia yake

siku moja kwa kuwa walikuwa wamefunga ndoa.

Lisa na Alvin walibarizi pamoja hadi saa tano usiku. Pamela hakuweza kuacha

kuangalia simu yake kila baada ya dakika tano. Alikata tamaa kabisa

kwamba Patrick alikuwa hajampigia simu tangu wakati huo. Alikunywa

pombe nyingi zaidi kuliko kawaida kwa

sababu ya hali yake mbaya kimawazo.

Lisa hakunywa sana pia kutokana na kelele za kina Lina waliovamia ghafla.

Alvin akawapa lifti ya kwenda nyumbani

wale wanawake wawili. Wakiwa njiani,

Pamela ghafla alilia kwa sauti kubwa na

kuanza kupiga kelele kuhusu mpenzi

wake mchafu. Lisa aliingilia kati

kumfariji.

Alvin alikuwa akipata maumivu ya

kichwa kutokana na kelele za hao

wanawake. Kwa hiyo, alikanyaga

mwendo na kuongeza kasi ili

kuharakisha safari ya kuelekea nyumbani kwa Pamela.

"Asante, ah, asante, mjomba." Pamela alifungua mlango na akatoka nje ya gari

kwa uangalifu na miguu yake iliyokuwa imelegea kama mlenda. Hakusahau

kumsujudia mwanaume huyo.

"Tafadhali mtunze vizuri mpenzi wangu

Lisa kila siku, usiwe kama huyu mbwa wa kiume Patrick..."

Sura ya 107

Wakati huo, Lisa alishtuka sana hadi

akakosa hata amani. Haraka akasema, “Hiyo ni… Unaweza hata kutembea

kweli? nitakupandisha juu.”

“Hapana, mimi si mlevi. Sitawahi

kulewa.” Pamela alipunga mkono bila

utulivu na kujikongoja hadi jirani.

“Mjomba?” Pamela alizidi kumuita Alvin, ambaye aliinua tu macho yake kwa kushangaa.

Lisa alimwambia kumtoa shaka, "ni kwa

sababu unafanana kidogo na mjomba wake, kwa hivyo anakuita 'Mjomba'

kujifariji."

“Mwambie asiniite hivyo. Sina uhusiano naye.” Alvin akawasha gari, na Lisa akapumua. Kwa bahati nzuri, hakushuku chochote. Pamela alikuwa

kimwita Alvin mjomba kwa maana ya mjomba wa Ethan.

Wakati wa kurudi nyumbani, pombe na usingizi vilimkamata Lisa kwa pamoja.

Akalala kama pono. Baada ya muda

usiojulikana, alihisi kuna mtu akimbeba kwa upole. Alifumbua macho kwa

kuduwaa na kuona wazi uso mzuri.

Akifikiri alikuwa anaota, aliinua midomo

yake minono na kuizungusha mikono

yake shingoni.

“Alvilisa, usikasirike, sawa?

Nimekukumbuka sana siku hizi chache.

Nimechoka. Mambo mengi yametokea

hivi karibuni na ninataka mtu wa

kuzungumza naye. Nina wewe tu sasa.

Utakuwa karibu nami kila wakati, sawa?"

Kisha, alilia ghafla huku akimkumbatia.

Machozi yake yalishuka shavuni mwake na kutiririka shingoni mwake. Alvin

alipigwa na butwaa. Pengine alichanganyikiwa baada ya kuzinduka na kudhani bado hajarudi. Moyo wake ulijawa na dalili za maumivu. Lazima

siku hizo chache alikuwa na msongo wa mawazo sana. Baada ya yote, bado

alikuwa mwanamke. Mambo mengi

sana yalimtokea lakini hakuwa karibu

naye. "Ndio, nitakaa karibu nawe kila wakati," alinong'ona sikioni mwake.

Sauti ya upole ya Alvin ilimtuliza taratibu

Lisa. Alifumba macho na kulala begani mwake. Alvin alimbeba juu juu na kumuweka kitandani taratibu. Kuangalia

mashavu yake laini, akahema. Alikuwa

amechoka kabisa wakati huo. Siku

chache alizokuwa hayupo hakulala

hata kidogo.

Wakati anakaribia kwenda kuoga, kuna

mtu aligonga mlango polepole nje.

Alifungua mlango na kumuona Hans akiwa amesimama nje, akamwambia kwa sauti ya chini, "Kuna kitu kimetokea."

Alvin alitoka nje ya mlango, na Hans akamkabidhi picha ya mtu fulani.

"Nilipata habari kwamba Zigi Kabwe amefika Dar es Salaam kukutafuta.

Naamini yuko hapa kulipiza kisasi cha dada yake tena.”

"Alijuaje kuwa niko Dar?" Mwanga wa tahadhari ulimulika machoni mwa Alvin.

"Ulikuja Dar na kushughulikia kesi

kadhaa kubwa, haswa kesi ya Kibo

Group ambayo ilivuma sana. Ingawa

nimejaribu kuficha sana jina lako,8 lakini

mitandao sasa imeenea mno…” Hans

alikunja uso na kutafakari kabla ya

kusema, “Mtu huyu amekuwa

akikusumbua tangu miaka mitano

iliyopita. Kwani huwezi ku…”

“Hakuna haja.” Alvin alikunja uso na kumkatisha.

Hans alikuwa na wasiwasi. "Ninajua

unaweza kufikiria moyoni mwako jinsi

anavykuchukia kwa sababu ya kesi ya

dada yake, lakini yeye ni- ... Yeye ni hatari sana na ameapa kulipiza kisasi

kwa mtu unayempenda. Lisa atakuwa hatarini.”

"Mletee mtu wa kumlinda." Alvin aliamuru.

Siku iliyofuata, Lisa aliamkaalibadilisha nguo zake za kulalia na kushuka chini.

Aliona kwamba kulikuwa na mwanamke

kijana mwenye nywele fupi na umbo

thabiti.

“Habari, Bi Jones. Mimi ni mlinzi wako, Shani. Nitawajibika kwa usalama wako kuanzia sasa.” Lisa alipepesa macho na kumtazama Alvin aliyekuwa amekaa

pembeni. “Umenitafutia mlinzi?”

“Mmh, familia ya akina Jones inapanda

tena. Huna bahati, kwa hivyo nitakuwa

na amani zaidi ikiwa kuna mtu kando yako." Alvin hakumwambia ukweli, asije

akakasirika siku nzima. kuna jambo

alikuwa akimficha Lisa.

"Alvlisa, wewe ni mzuri sana kwangu."

Lisa alikumbuka mara ya mwisho

alipoangukia kwenye mtego wa Lina. Baada ya kufikiria kidogo, hakukataa.

“Ni vizuri kwamba unajua. Macho ya Alvin yalikuwa ya upole, lakini yakawa

makali tena alipomgeukia Shani.

“Mlinde vyema. Ikiwa mtu yeyote

ataweka mkono juu yake, utawajibika kabisa. Pia, nijulishe ikiwa mtu wa jinsia

tofauti atamkaribia.”

Shani akaitikia kwa kichwa.

“Imeeleweka.”

Kwa pembeni, Lisa alikosa la kusema.

"Unanipeleleza tu kwa kisingizio cha ulinzi, sivyo?"

Alvin alibana mashavu yake. “Sitaki

upate shida, bado nasubiri kwa hamu

kustaafu kazi yangu baada ya wewe

kuipata Mawenzi Investiments.” Sauti ya

sumaku ilimfanya Lisa ashindwe kabisa

kusema lolote.

Baada ya Alvin kwenda kazini, alimuuliza Shani huku akitabasamu, “Unamfahamu Alvilisa?”

Aliposikia jina la 'Alvilisa', Shani alitabasamu na kujibu kwa heshima, "Ndiyo."

Lisa alitazama huku na huku na kuuliza, “Basi lazima ujue kama amewahi kuwa na mpenzi zamani. Amekuwa nao wangapi na…"

“Bi. Jones, unaweza kumuuliza Bw.

Kimaro kuhusu hili wewe mwenyewe.”

Shani aliifuta mada hiyo kwa maneno

machache. Lisa alikata tamaa ghafla.

Mlinzi huyu alionekana kuwa na msimamo sana.

Baadaye siku hiyo, Lisa alijiuzulu kazi

yake huko kwenye kampuni ya zamani

na kufanya maandalizi yake kwa ajili ya

kujiunga rasmi na Mawenzi

Investiments.

Nako katika makazi ya Jones, Jones

Masawe alikuwa katika hali nzuri baada

ya kupokea simu kutoka kwa

mwenyekiti wa bodi ya Mawezi Investments. "Mwenyekiti Amiri hatimaye alikubali kuniunga mkono.

Nafasi ya mwenyekiti itakuwa yangu kesho.” Jones alimwambia mkewe.

"Mpenzi, pongezi." Mama Masawe alitabasamu kwa kiburi. Habari za hadhi ya Jones kuwa mwenye hisa mkuu wa Mawenzi Investiments zilikuwa

zimeenea kila mahali, hivyo wanawake wale matajiri waliokuwa wakimdharau walikuwa wanakimbilia na kumtamani tena. "Unapochukua nafasi ya mwenyekiti na Lina na Stephen watakapooana, familia yetu ya Masawe itasimama kileleni mwa matajiri wa jiji hili."

"Hiyo ni sawa. Muda mrefu tulikuwa

tukiongozwa na familia za Harrison na Zongo, lakini hivi karibuni, tutazipita na

kuwa familia yenye nguvu zaidi hapa

Masaki.” Jones alizidi kuibuka mshindi

kadiri alivyozidi kuwaza juu yake na

hakuweza kujizuia kuangua kicheko.

Lina naye akacheka. “Baba

umeshampata Aunty Manka? Yeye ni bomu linalosubiri kulipuka. Atatuharibia

usipoangalia"

“Ndiyo, yule mwanamke mzee anajua

mambo mengi sana,” Mama Masawe alisema kwa haraka.

"Kwa hivyo hata kama anajua mambo?

Mimi ndiye niliye madarakani sasa. Lisa

ni msichana mdogo tu. Anaweza

kunifanya nini?” Jones alidhihaki bila

kuweka umuhimu wowote kwa watu hao hata kidogo. "Hata kama ana Alvin

Kimaro nyuma yake, ninashuku kuwa

Alvin hatabaki hai kwa muda mrefu."

"Baba, huyu Alvin hata asikutishe, habari zimeenea kuwa anatafutwa na

mtu hatari anayeitwa Zigi Kabwe." Lina

aliachia tabasamu la ajabu. “Tangu kifo

cha dadake, anamchukia sana Alvin

kiasi kwamba hatamuacha hadi amuue.

Kusudi lake lote la kuishi ni kumuua

Alvin Kimaro.”

"Hiyo ni habari nzuri sana." Jones

alimpa tano za kumsifu. "Endelea kupeleleza habari zake, kama atamuua atakuwa ametusaidia sana." Lina

hakuweza kuficha furaha yake. Baada ya kumiliki Mawenzi investiments, angekuwa sosholaiti nambari moja jijini Dar es Salaam. Hakutaka kuvumilia tena wengine kumdharau.

Sura ya 108

Siku iliyofuata saa tatu asubuhi, mkutano wa mwaka wa wanahisa wakuu ulifanyika. Jones Masawe alifuatana na Lina wakaingia ukimbini

kwa hatua kubwa. Alipokelewa na watu wote waliosalimiana naye kwa kupeana naye mikono.

“Mwenyekiti Jones, hongera! Ninaamini nafasi ya mwenyekiti itakuwa yako

mara mwenyekiti Amiri atakapoondoka madarakani.” Mwanahisa mmoja

alimpokea Mzee Jones Masawe kwa

bashasha.

"Unasema nini? Ndo kwanza nimejiunga na Mawenzi Investiments na bado sijaelewa kabisa mambo ya ndani

yanavyofanyika,” Jones alijibaraguza kwa unyenyekevu huku akizuia nia yake isijulikane.

“Una nini cha kukuzuia? Hivyo ndivyo

watendaji tunaowaajiri kwa mishahara mikubwa wanavyokufikiria” mtu

mwingine alisema kwa kujipendekeza, “Maendeleo ya baadaye ya kampuni yanakutegemea Mwenyekiti Jones sasa.”

“Ndiyo, ndiyo, Mwenyekiti Jones. Hata mimi na familia ya Levy tutakuwa tunakutegemea wewe na Mawenzi Investiments,” Bwana Levy pia aliunga mkono.

"Hakuna shida, kama ndivyo

mlivyoamua." Jones hakuweza tena

kuzuia sura ya furaha usoni mwake na kucheka.

Mwenyekiti aliyekuwa anaachia ngazi, Amiri Gumbo, alikunywa chai ili

kulainisha koo lake na kuuliza, "Kila mtu amefika?"

"Kila mtu amewasili, isipokuwa hakuna

mwakilishi wa KIM International inayomiliki asilimia 2`5[ ya hisa, labda na BwanaChris Maganga. " Bwana Issa Kawe, katibu wa bodi, alisema, "Lakini

kila mtu anajua kwamba KIM International kamwe haishiriki katika

masuala ya kampuni na inasubiriaga tu gawio la faida, na Chris Maganga huwa

hahudhurii mkutano wa wanahisa kwa

sababu anaishia mbali. Kwa hiyo hatuna

haja ya kusubiri"

"Kwa hali hiyo, acha kikao cha bodi

kianze." Mwenyekiti Amiri aliidhinisha. Mwenyekiti wa bodi na kiongozi wa mkutano, Mzee Amiri alisema, “Sasa

nina umri wa miaka 70 na afya yangu si nzuri kama ilivyokuwa zamani. Nataka

kuachia nafasi yangu nijali afya yangu, hivyo nafasi ya mwenyekiti lazima

ijazwe na mtu mwenye uwezo. Kwa

bahati ni kwamba mwaka huu, Bibi

Mkubwa Masawe alifariki na 60% ya

hisa zake zilipitishwa kwa mtoto wake, Jones Masawe. Katika siku zijazo,

atakuwa mwenye hisa mkuu wa

kampuni na atakuwa na mamlaka kamili

ndani ya bodi. Kwa hiyo tunaweza kufikira kumwachia kiti hiki cha

mwenyekiti kama hamtajali.”

Chumba cha wanahisa mara moja

kilimtazama Jones Masawe kwa wivu.

Uso wa Jones ukanyanyuka juu kwa sifa.

Bwana Levy, mmoja wa wanahisa,

akatabasamu na kusema. "Mwenyekiti Jones yuko katika umri wake wa

dhahabu na ni mkomavu na thabiti.

Naamini ni bora achukue nafasi ya mwenyekiti.”

"Ndio, tunakubali." Ukumbi mzima

ukaripuka kwa makofi.

“Acha awe Mwenyekiti Jones. Anafaa kwa nafasi hii." Maneno ya watu fulani

yakasikika. Chumba kikubwa cha

mikutano kilijaa kila aina za sauti za

kuunga mkono.

Mwenyekiti Amiri Gumbo aliitikia kwa kichwa na kusema, “Kwa kuwa huu ni uchaguzi, bado tunapaswa kufuata utaratibu wa kawaida. Kila mtu

anayemkubali Jones Masawe anyanyue mkono wake juu."

Wanahisa wa bodi waliinua mikono yao, na Mwenyekiti wa mkutano akahesabu.

“Kura kumi kati ya wanahisa 15.

Inaonekana kama nafasi yangu ni ya

Bwana Jones sasa. Hapana, nikuite

Mwenyekiti Masawe sasa hivi.”

Jones Masawe aliinuka na chemchemi ya majivuno katika hatua yake.

"Asanteni kwa ushirikiano wenu. Kwa

kuwa mmeniamini na kuniwezesha

kuchukua wadhifa wa mwenyekiti, bila

shaka nitaifikisha Mawenzi Investiments hadi kwenye orodha ya makampuni 10 bora Tanzania, au hata 100 bora Afrika.

Nitamwezesha kila mtu kupata faida

nzuri zaidi kila mwaka.”

"Tunaimani na wewe." Kila mtu aliinua

mikono yake na kupiga makofi.

Mwenyekiti Masawe hakuweza kuacha kutabasamu. Mwili wake wote

ulionekana kuelea kwenye ombwe la furaha. Alikuwa mwenyekiti wa Kibo

Group kwa nusu ya maisha yake, lakini

Kibo Group haikuwa chochote

ikilinganishwa na hadhi ya Mawenzi Investiments. Katika siku za usoni, Dar

yote ingekuwa chini ya miguu yake.

Na wale ambao hawakumpigia kura siku

hiyo …! Akamgeukia Lina na kusema, “Niandikieni majina ya wale ambao

hawakuniipiga kura.”

“Usijali, Baba. Nimeandika majina yote.”

Lina alijibu kwa jeuri kama ya baba yake. “Baba naweza kuwa na nafasi ya meneja mkuu wa kampuni? Sihitaji tena

kuwa meneja wa mradi wa ukuzaji mali, ni nafasi ndogo sana kwangu hiyo.”

“Kuwa na subira. Nitalizungumza

kwenye kikao baadaye.” Baba yake

hakumvunja moyo.

Lina alitetemeka kwa furaha. Katika siku

zijazo angekuwa binti mdogo mwenye utajiri wa thamani ya makumi ya mabilioni ya shilingi. Mtandao mzima wa watu mashuhuri nchini ungekuwa kituo chake, achilia mbali Dar es Salaam. Kwa Lisa, angekuwa mchwa tu.

“Mwenyekiti Jones, kaa kiti changu. Mahali hapa ni mali yako sasa."

Mwenyekiti mstaafu, mzee Amiri akainuka. "Mkutano unaofuata wa wanahisa utakuwa mikononi mwako."

"Mwenyekiti Amiri, wewe ni mwema sana." Mwenyekiti Jones alisema kwa furaha, na miguu yake mara moja

ikasogea kuketi.

Ghafla, mlango wa chumba cha

mkutano ulifunguliwa kwa kishindo, na mzee wa makamo aliyevalia suti nyeusi

akaingia ndani akionekana mwenye

nguvu na mamlaka. Nyuma yake, mwanamke kijana alimfuata. Suti yake ya kifalme ya bluu ilifunika ngozi yake

nzuri, na nywele zake ndefu ziliwekwa

juu ya mabega yake. Haiba yake

ilisisitiza sifa zake za kupendeza. Uso wake mdogo haukuwa na hisia, lakini

ulibeba tu hali ya tahadhari

kwa mwonekano wake. Wakati huo, nyuso za Jones na Lina zilibadilika papo hapo.

Lina akapiga kelele kwa nguvu, “Lisa, unafanya nini hapa? Toka nje! Hii ni mali ya Mawenzi Investiments. Nani alikuruhusu kuingia humu? Ondoka sasa hivi!”

Sauti yake ilikuwa ya kiburi, lakini Lisa

naye alikuwa ameshiba dharau huku

Chris Maganga akiuliza, "Kwani

nimepoteza haki yangu ya kuleta mtu

kwenye mkutano wa wanahisa kwa

sababu tu sijaja kwenye kampuni kwa

miaka michache?"

Jones Masawe alihisi tu kwamba mtu

huyo hakuwa mgeni machoni pake, lakini hakumtambua. Mwenyekiti

aliyetoka madarakani Amiri alisimama na kusema, “Bwana Maganga, si

unaishi Mwanza kwa sasa? Kwanini

umekuja ghafla kwenye mkutano wa kampuni leo?”

Uso wa Lina ukapoa. mara moja akawa

ametambua kwamba huyo ndiye

mwenyehisa ambaye alionekana mara chache sana kwenye kampuni, Chris

Maganga. Hata hivyo alikuwa na 10% tu ya hisa ukilinganisha na baba yake

aliyekuwa na 60%. zaidi ya hayo, Jones

Masawe alikuwa tayari ni mwenyekiti wa

Mawenzi Investiments, hivyo Lina

hakuwa hata na tone la wasiwasi

moyoni mwake. Hakuonyesha heshima

yoyote kwa Chris na alimdhihaki bila

kujali, akisema, "Ni kweli, unaweza

kuingia kwenye mkutano kama

mwanahisa, lakini huwezi kutumia

nafasi yako kuleta takataka."

Alimtazama Lisa baada ya kuongea.

Lisa aliinua ndita zake na kucheka.

“Unajizungumzia wewe mwenyeweee, au kuna takataka nyingine?”

"Lisa, bado unaota?" Lina alidhihaki,

“Baba yangu sasa ni mwenyekiti wa

Mawenzi Investiments. Ninaweza kuja hapa wakati wowote ninapotaka. Unafikiri wewe ni nani?”

“Hata sijapiga kura. Ilikuwaje akawa mwenyekiti mpya?" Chris akaburuta kiti na kuketi.

Sura ya 109

Mwenyekiti Jones alimdharau Chris.

“Inaonekana kwamba Bwana Maganga hajaridhika nami, lakini tayari kuna watu

kumi katika kampuni ambao walinipigia kura. Hata ukipiga kura haina maana.”

“Ndiyo.” Mwenyekiti mstaafu Amiri alijisikia vibaya. “Bwana Jones ndiye mwenyekiti mpya. Hakuna anayeweza kubadilisha hilo. Kura moja

haitabadilisha matokeo.”

“Pia ndiye mwanahisa mkubwa ambaye

anamiliki asilimia 60 ya hisa. Unawezaje kujilinganisha naye?” Baadhi ya watu

walianza kudhihaki.

Mwonekano wa Mwenyekiti Masawe ulikuwa wa kiburi. "Bwana Maganga, ikiwa uko hapa kuleta shida, usinilaumu

kwa kuagiza walinzi wakutoe nje."

"Nani alisema wewe ndiye mwenyehisa mkubwa?" Chris akatabasamu. "Una 30% ya tu ya hisa."

Jones alikunja uso. "Mama yangu alipofariki, nilipewa 60% ya hisa."

"Si zako." Chris akazitupa zile nyaraka zilizokuwa mkononi mwake mezani.

“Bibi Mkubwa Masawe alitoa wosia

kabla hajafa. Baada ya kufa, Lisa Jones

atakuwa na 30% kati ya 60% ya hisa.

Vipi, unapanga kuchukua kila kitu bila

kusema chochote?"

Wakati kauli hii inatolewa, chumba

kizima kilikuwa na ghasia. Nyuso za

Jones na Lina zilibadilika sana.

Mwenyekiti mstaafu Amiri alichukua

nyaraka na uso wake ukageuka ghafla.

'Ni kweli. Muhuri na saini ya Bibi

Masawe viko juu yake."

“Hilo haliwezekani…” Jones alipiga

meza na kusimama.

"Ni nini kisichowezekana juu yake?"

Lisa alienda kutazama umati wa watu.

"Ninaamini kuwa wanahisa wote

wanajua kuwa Mawenzi Investiments

ilianzishwa na Sheryl Masawe zaidi ya miaka 20 iliyopita. Mimi ni binti wa

Sheryl, na hii ni kampuni ya mama yangu. Babu na bibi yangu walimpa tu

30% ya hisa kwa sababu Jones

Masawe alinilea, lakini hajatosheka na anataka kumiliki yote.”

“Funga mdomo wako!” Jones alijaribu

kumpiga kofi, lakini kuna mtu alikuwa mwepesi kuliko yeye, Shani alimshika

mkono na kumminya kwa nguvu, na kumfanya apige kelele kwa maumivu

mara moja.

"Wewe ni nani? Niache mara moja, la sivyo!” Jones Masawe alijitetea

kinyonge.

"Ukithubutu kumpiga mwajiri wangu tena, nitakuvunja mkono." Shani alionya

kwa upole kabla ya kuachilia mkono

wake. Jones alipiga hatua chache

nyuma. Mkono wake ulikuwa umekufa ganzi kwa maumivu.

Lina alimuunga mkono baba yake na kusema kwa kutokuamini, “Lisa, unazungumzia nini? Kwa ajili ya utukufu na mali, ungeweza hata kumkana baba yako mzazi? Kila mtu anajua kwamba

Sheryl Jones hajawahi kuolewa.

Angewezaje kupata binti? Umekuwa wazimu?"

“Sivyo ulivyosema hapo awali?” Lisa alimuumbua “Uliniambia mwenyewe kuwa mimi si binti wa Jones Masawe bali ni mtoto wa kuokota kwenye vituo vya watoto yatima.”

Macho ya Lina yaliangaza kwa dhihaka.

“Nilikuwa naongea upuuzi tu wakati ule.

Wosia wa babu na Bibi unasema waziwazi.”

Mwenyekiti Amiri alitikisa kichwa tena

kinyonge. "Ndio, imeandikwa kweli

kwamba Lisa Jones ni binti wa Sheryl Masawe."

Jones Masawe alikunja ngumi kwa

nguvu na kusema. “Hata kama ni kweli, hisa zote zimehamishiwa kwenye jina langu. Ni upuuzi kuendelea kuongea. Kikao hiki cha bodi hakiwezi kubadilisha ukweli kwamba mimi ni mwanahisa mkuu.”

“Nani alisema kwamba hisa zote

zimehamishiwa kwa jina lako?” Lisa

alitabasamu kijeuri. “Hujatazama? 30% ya hisa zimehamishwa kwa jina langu

kwenye Idara ya Viwanda na Biashara.”

Uso wa Jones ukabadilika. Hakuweza

kuvumilia tena na akachukua simu na kupiga moja kwa moja kwenye idara ya viwanda na biashara. Chini ya dakika

moja tu baadaye alimgeukia Lisa kwa

macho makali, hakutaka kingine zaidi ya kumchuna ngozi akiwa hai.

Lisa akaugeukia umati. “Imekuwa bahati

sana. Bibi yangu alifariki ghafla baada ya kupooza ghafla pia. Taarifa za kifo

chake niliambiwa na mtu baki, na ni kitambo kifupi tu baadaye nikagundua

kuwa nina uhusiano na Mawenzi

Investiments. Vinginevyo hisa zangu zote zingekuwa mali ya mjomba.”

Umati wote ukalipuka kwa minong’ono.

“Mungu wangu, inaonekana kwamba

kuna kitu cha ajabu juu ya kifo cha Bibi Masawe.”

"Hiyo ni kweli. Yule bibi alikuwa mwenye afya nzuri tu nilipomuona siku si nyingi...”

“Tsk, kweli hafai. Alikuwa ni mama yake mzazi!”

“Lazima tumwepuke mtu huyu. Anatisha!”

Mtazamo wa kila mtu kwa Jones ukabadilika.

Jones aligonga meza kwa hasira. “Lisa

Jones, jaribu kuongea upuuzi tena uone!”

“Mjomba, sijakutusi. Kwanini unajihami

sana? Kweli hauna hatia kwenye hili?”

Lisa alipaza sauti kwa macho makali.

“Lakini sikuamini kabisa kama

ungemuua mama yako mzazi. Kama

ulimuua, bibi yangu hata kuacha uishi kwa amani.”

Jones alikurupuka na kutokwa na jasho baridi. Haraka alibadilisha mada katika

hali mbaya. “Unapanga kufanya nini hapa?”

"Bila shaka, ni kugombea dhidi yako kwa nafasi ya mwenyekiti." Lisa

alimtazama kila mtu. "Sasa nina 30% ya hisa, sawa na Jones Masawe, kwa

hivyo ninastahili kushiriki."

"Lazima una wazimu." Jones alionekana

kama amesikia utani mkubwa. "Una miaka mingapi? Wewe ni msichana

mdogo tu mjinga. Huna uzoefu na huna uwezo. Nani atakuwa na imani na wewe

kukukabidhi kwa hiari kampuni kubwa kama hii?”

"Hiyo ni sawa." Bwana Levy akaitikia

kwa kichwa. "Hatutaki kuingilia ugomvi

wako na familia ya Jones, lakini

kusimamia kampuni sio mzaha."

“Ndiyo, Mawenzi Investiments haikosi

watu. Hata iweje, huyu binti mdogo

hawezi kuwa mwenyekiti.” Baadhi ya wanahisa walikunja uso na kupinga.

Jones Masawe aliridhika sana na akaketi tena na kunywa chai yake.

Baada ya yote yaliyosemwa na kufanyika, ilionekana kuwa nafasi ya mwenyekiti bado ilikuwa ni yake.

"Kwanini siwezi kuwa mwenyekiti?" Lisa

aliuliza bila kuhangaika, “Kama sote

tunavyojua, Jones Masawe aliwahi

kuwa mwenyekiti wa Kibo Group

aliyorithi kutoka kwa babu, lakini chini ya uongozi wake, Kibo Group ilisusiwa na mtandao mzima wa wafanyabiashara na hata ikamlazimu kuiuza kwa hasara.

Mtandao bado unazungumza juu yake

sasa. Sifa yake imeharibika kabisa na hakuna anayemwamini. Aliongoza

kampuni hiyo kupokea hongo, huku

ufisadi na visasi vingine vikiwa

vimeshamiri. Ikiwa ataiongoza Mawenzi

Investiments, ulimwengu wa nje utatilia

shaka ubora wa bidhaa na mali za

Mawenzi Investiments.” Taarifa hii

iliposemwa, wanahisa kadhaa walikubali kwa kutikisa kichwa. Uso wa Jones

ulizidi kuwa mgumu huku akimkazia macho Lisa, hakutaka kitu zaidi ya kumla akiwa hai.

Lina alisema kwa hasira, “Bado una ujasiri wa kusema hivyo! Kwani sifa ya Kibo Group ingeharibika ikiwa si wewe?

Yote ni makosa yako."

Sura ya 110

Lisa alicheka kwa madaha. “Ndiyo, mimi ndiye niliyeibua ufisadi wa mpwa wa mtu fulani. Aliingiwa na pupa ya tamaa ya pesa kuanza kuharibu miradi ya

ujenzi kwa kutumia vifaa feki

akishirikiana na wewe Lina. Huwezi

hata kujenga nyumba lakini sasa

unataka kuwa mbunifu. Nani atathubutu

kukubali mradi uliobuniwa na wewe?"

"Ndio, hiyo haitafaa." Bwana Haruna, mmoja wa wanahisa alikuwa wa kwanza

kupinga hadharani dhidi yake.

“Nataka kutafakari upya pia. Hatuwezi

kuharibu sifa ya Mawenzi Investiments.”

Mwanahisa mwingine akadakia.

Wanahisa walipoanza kurudi nyuma, Lisa alisema kwa sauti ya upole kwa kila mtu, “Ni kweli kwamba mimi ni mdogo, lakini nina mawazo wazi na makini.

Ikiwa sijui chochote, naweza kuwauliza

wazee wangu waliopo hapa kwa

ushauri. Haikuwa rahisi kwa Mawenzi

Investiments kufikia kiwango ilichopo.

Haijalishi ni faida ngapi ambazo Jones

ameahidi kwa kila mtu, lengo letu kuu ni kukuza faida ya kampuni ili tupate gawio bora zaidi.

“Ndiyo hivyo,” hatimaye Chris

alizungumza. Sauti yake ilikuwa na mamlaka sana. "Wasifuwa bosi wa

kampuni kubwa kama hii ni muhimu

sana. Nitamuunga mkono kikamilifu Lisa

ikiwa atakuwa mwenyekiti. Kila mtu

anapaswa kujua kwamba niliwahi pia

kumsaidia Sheryl. Ni shukrani kwa

Sheryl kwamba Mawenzi Investiments

ndivyo ilivyo leo.”

"Bado tunaamini katika uwezo wa Bwana Maganga." Bwana Haruna alikubali kwa kutikisa kichwa.

“Kwa hali hiyo, tupige kura tena. Una maoni gani, Mwenyekiti Amiri?" Chris Maganga alimtazama Mkwenyekiti Amiri na kumkumbusha, “Mwenyekiti Amiri, kama ningetaka kushindana na wewe katika nafasi ya mwenyekiti hapo awali, usingekaa kwa furaha hapa leo.”

"Nakubali." Mwenyekiti Amiri alikwepa kumtazama Chris Maganga na kutikisa kichwa. "Wacha tuanze kupiga kura upya."

Kila mtu aliinua mkono wake mmoja

baada ya mwingine, na matokeo ya mwisho yalikuwa tisa kwa saba. Lisa ni tisa dhidi ya saba za Jones.

"Wacha tumpongeze Lisa Jones kama mwenyekiti mpya." Chris aliongoza kupiga makofi.

Jones Masawe alipiga meza, uso wake

ukiwa na hasira. “Uchaguzi huu si mchezo. Unawezaje kurudia mchakato wa kupiga kura? Ni mimi niliyechaguliwa hapo awali. Unafikiri wewe ni nani?”

"Bwana Jones anaonekana kutoshawishika." Kulikuwa na kitu kingine kilichojificha chini ya tabasamu la Lisa. "Lazima uelewe kwamba kama si ukarimu wa mama yangu, usingekuwa na uhusiano wowote na kampuni hii. Unapaswa kuridhika na ulichonacho.”

“Wewe…!” Jones alimkazia macho.

Hakuamini yule binti ambaye aliwahi kuwa adabu sana mbele yake sasa alithubutu kuwa mkaidi mbele yake.

“Ikiwa utaendelea kufanya fujo, ninaweza kuwaita walinzi wakutoe nje,”

Lisa alionya bila huruma.

Jones alipandwa na hasira. Kulikuwa na wanahisa wengi hapo, lakini hakuna

hata mmoja aliyemtetea.

"Bw. Jones, kaa chini." Mwenyekiti Amiri

alihema kwa nguvu. "Tayari

tumechelewesha hii kwa muda wa kutosha. Bado kuna mambo mengi tunapaswa kuyashughulikia katika mkutano huu."

"Ni sawa, lakini kabla ya hapo, ni wakati wa watu wa nje ambao hawana uhusiano wowote na mkutano kutoka

nje." Lisa alimtazama Lina.

Lina alikuwa akifedheheshwa

hadharani, na macho yake yakiwa mekundu, aliongea kana kwamba

amedhulumiwa, “Lisa, najua hunipendi, lakini—”

“Nimesema kitu kibaya? Kwani wewe una sifa za kukaa hapa?” Lisa alidhihaki. “Bi. Jones hajui hata sheria za nidhamu za kampuni."

"Inatosha, nenda nje," Mwenyekiti Amiri alisema bila subira.

Lina alijawa kiburi, akatuna kama puto

lililopulizwa, lakini hakuwa na ujanja

zaidi ya kutoka nje. Mlango wa chumba

cha mikutano ukafungwa tena, naye

alikasirika sana hivi kwamba machozi

yakamtoka.

Muda si muda, Stephen Kileo alimpigia

simu. "Lina, hongera! Baba yako lazima awe mwenyekiti mpya wa

Mawenzi sasa.” Sikio la Lina lilihisi uchungu kana kwamba alipigwa kofi

kali. Stephen hakujua na akaendelea kusema, “Baba yako anapochukua ofisi, mradi wa Nairobi ambao tulijadili mara ya mwisho unaweza kuanzishwa mara

moja. Kisha, familia za Kileo na Masawe zitashirikiana kuunda hotel ya nyota

tano huko Nairobi. Hivi karibuni, iwe ni Nairobi au Dar es Salaam, itakuwa ulimwengu wetu. Hahahaa, nataka sana kuona nyuso zilizoshindwa za familia za Harrison na Clark sasa…! Hee..Lina, mbona huongei chochote?” Stephen, ambaye alikuwa akizungumza kwa

muda, hatimaye alishtuka kwa kuona

kimya chake.

"Ni Lisa ndiye ameshinda nafasi ya uenyekiti." Hatimaye Lina akaongea

ukweli mchungu.

"Nini?" Stephen akapiga kelele. “Si ulisema una uhakika 90% baba yako

atakuwa mwenyekiti? Wewe na baba yako mnafanya nini? Hamwezi hata

kumshughulikia Lisa Jones?”

Uso wa Lina ulihisi joto aliposema bila

raha, “tungejuaje kwamba angeungana na Chris Maganga? Sisi pia tulishikwa na bumbuwazi.”

“Kweli mambo ndiyo yamegeuka kuwa hivi? Hata nilijitapa nikisema kuwa

mpenzi wangu ni binti wa mwenyekiti wa Mawenzi. Ni fedheha iliyoje sasa eeh....! sitaki kusikia hii tena." Stephen alilaani sana.

Sauti ya Lina ilikata. “Stephen, unamaanisha nini kusema hivyo? Sasa

unanichukia kwa sababu baba yangu

hakupata nafasi ya mwenyekiti?”

Stephen alirudi kwenye fahamu zake

ghafla. Hata kama baba yake Lina

hakuwa mwenyekiti wa Mawenzi

Investiments, mwaka wa gawio ulikuwa

unatosha kuwafanya wawe na pesa

nyingi mno. Alicheka kwa haraka na kusema, “Bila shaka, usinifikirie vibaya.

Nimekasirishwa tu na dhuluma uliyotendewa. Nakupenda wewe, sio utambulisho wako."

“Usijali. Hii ni ya muda tu. Lisa hatakaa katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda mrefu,” Lina alisema kwa ukali.

“Uko sahihi. Si rahisi kufanikisha mambo makubwa ikiwa Lisa atakuwa mwenyekiti.” Stephen pia alitabasamu kwa huzuni. "Sitaacha juhudi yoyote kukusaidia."

"Asante." Lina akajibu na simu ikakatwa.

Mkutano uliisha saa sita mchana.

Mmoja baada ya mwingine, wanahisa

walipeana na mwenyekiti mpya mikono na kuondoka kwa heshima.

"Mwenyekiti Jones, nitakupeleka ofisini kwako." Msaidizi wa mwenyekiti, Tunu

Omari, alimjia Lisa kwa hatua kubwa.

Alikuwa na tabia njema na mwenye

bidii.

“Sawa, nipeleke huko.”

Alikuwa ameanza kuondoka tu wakati

Jones alipomzuia njia. Maneno yake yalikuwa ya huzuni na ya kutisha. "We

paka malaya, lazima utajuta mwenyewe. Umeweza kuketi kwenye

kiti hicho, lakini hiyo haimaanishi kuwa utaendelea kukaa muda mrefu—”

“Paah!” Lisa aliinua mkono wake na kumpiga kofi Jones Masawe bila

huruma wala aibu.

Jones hakuwahi kutarajia kitu kama

hicho. Alishikwa na machozi na hasira

sawasawa. Hatimaye alipojibu, alitoa

meno yake kwa hasira na kumkimbilia ili kumfundisha somo. Lakini, Shani

alisimama mbele ya Lisa na kumpiga

teke Jones, na kumfanya aruke mita

kadhaa chini. Hakuweza kuinuka kwa

muda mrefu kwa sababu ya maumivu.

“Wewe… Wewe msichana usiye na

shukrani! Unathubutu vipi kumpiga

mzee? Utapata laana ya Mungu.!"

Jones alinguruma kwa hasira.

"Uliniita malaya, kwa hivyo kama mkuu wako, ni kawaida tu kukufundisha somo." Lisa akapuliza kiganja chake kilichokuwa kikiwaka kwa maumivu.

“Zaidi ya hayo, kwani wewe na mkeo mmenipiga makofi mara ngapi? Sijafikia hata chembe ya makofi mliyokuwa mkinipiga bila hata kosa.”

“Kwa hiyo tulikuwa tunakuonea?

Tulikuwa tunakulea. Tunakudai deni

kubwa la shukrani kwa kukulea,” Jones

Masawe alisema kwa huzuni.

Sura ya 111

Macho maangavu ya Lisa yaligeuka na kuwa makali kidogo. “Umenileaje?

Ulinisaidia nilipokuwa nasoma?

Niliposhikwa na homa, babu na bibi ndio

waliniuguza. Kuhusu gharama za

maisha ulizolipa, babu na bibi yangu

walitumia hisa za mamia ya mamilioni

kukufidia, lakini hujaridhika!” Hasira ya

Jones ilisababisha koo lake kukwama.

Lisa akasogea mbele na kumtazama kwa juu. “Ni sawa, lakini hata mama

yako mzazi ulimuua, unaweza kujihesabu kuwa wewe ni binadamu?”

Jones Masawe aliruka juu kama paka ambaye mkia wake umekanyagwa. "Bibi

yako alikufa kwa ugonjwa."

“Ndiyo, inasikitisha kwamba Bibi alikufa

nikiwa sina msaada. La sivyo, kuchunguza maiti yake kungetosha

kwetu kugundua sababu ya kifo chake,”

Lisa alidhihaki, akisema, “Lakini

sitakuacha. Hakika nitakulipa pole pole

maumivu yote niliyopata, ikiwa ni pamoja na kumlipizia Bibi.” Kisha, alitoka kwenye chumba cha mikutano

bila kuangalia nyuma. Alipotoka nje, mwili wake ulikuwa ukitetemeka kwa

msisimko.

Muda wote huo, alikuwa

amenyanyaswa na kuonewa na familia ya akina Jones. Alikaribia kupoteza

maisha mara kadhaa. Kuanzia siku

hiyo, angekuwa na nguvu ya kujilinda

yeye na watu wanaomzunguka.

Baada ya kurudi ofisini kama

mwenyekiti, mara moja alimwomba

Tunu aende kuleta taarifa muhimu

kuhusu uongozi wa juu wa kampuni.

“Mwenyekiti Lisa, huhitaji kuwa na haraka hivyo. Kula chochote kwanza.

Nitakuagizia …”

"Agiza mtu alete kitu rahisi."

Baada ya Tunu kuondoka, Lisa

alimgeukia Shani na kusema, “Asante.

Kama usingekuwepo leo, Jones

angenipiga bila shaka.”

"Karibu. Ni wajibu wangu kukulinda.”

Shani aliachia tabasamu hafifu. "Ikiwa unashukuru, basi mshukuru Bw.

Kimaro."

Lisa naye alitaka kumweleza Alvin

habari hiyo njema na kumpigia simu.

"Alvlisa, unafanya nini?"

“Kula.” Jibu la mtu huyo lilikuwa fupi

sana.

Lisa alikosa furaha na akapiga kelele.

“Mbona hauulizi kama nimefaulu leo?

Hunijali hata kidogo, hmph.”

"Shani tayari amenitumia ujumbe saa moja iliyopita." Sauti ya chini ya Alvin

ilichanganyika na tabasamu.

"Mwenyekiti Lisa alijitokeza katika

mkutano wa wanahisa leo, akionekana kama mwanamke wa chuma.

Inaonekana kama ninaweza tu kuwa mwanamume anayesimama nyuma ya mwenyekiti katika siku zijazo.”

“Hadhi yangu si ya kawaida kwa sasa

na wanaume wengi wanataka kuwa wao wanaosimama nyuma yangu. Jihadhari, afadhali uwe mtiifu na unisikilize, ama sivyo watachukua nafasi yako.” Lisa

alifoka kwa utani huku akitabasamu.

Sikuzote Alvin ndiye aliyekuwa na mamlaka juu yake na kumsimamia, lakini hatimaye alihisi kwamba alikuwa

huru kutoka katika hadhi yake ya chini.

“Ndiyo, nitakuwa mtiifu. Nikirudi usiku

huu, nitakuhudumia hadi

utakaporidhika,” Alvin alisema kwa utata.

Simu iliyokuwa sikioni mwa Lisa ilifanya

ionekane kama alikuwa akipumulia sikioni, na ghafla aliona haya huku

akikemea, “Wewe mpuuzi, nitakata simu sasa hivi.”

"Nazungumza juu ya kukupa massage."

Alvin alicheka. “Au unawaza nini?

Inaweza kuwa…”

"Sahau…" Lisa akakata simu huku

akicheka. Alipogeuka pembeni, alimuona Shani akiwa na tabasamu

usoni mwake na kuhisi aibu zaidi.

Baada ya kula, Tunu alimletea orodha ya watendaji wakuu wa kampuni na kuiangalia. Lisa aliitazama na kuikazia macho post ya Lina. Meneja mkuu wa mradi wa maendeleo ya mali. Alidhihaki

papo hapo, akitambua ukweli wa jinsi

alivyokaribia kufa alipoenda kwenye

eneo la ujenzi mara ya mwisho.

"Ina maana hakuna mtu mwingine

katika kampuni yangu? Kwa nini huyu

kanjanja asiye na elimu wala uzoefu

anachukua nafasi hiyo muhimu?" Lisa alisema kwa kusikitisha, "Watendaji wa kampuni wanakuja lini? Nataka kuwa na mazungumzo mazuri nao.”

Tunu aliona mawazo yake na akasitasita kabla ya kusema, "Walitoka kwa chakula cha mchana na Jones Masawe."

Uso mzuri wa Lisa uliingia giza mara moja. Alikuwa ametoka tu kuchukua

nafasi ya mwenyekiti, lakini sio tu kwamba watendaji wakuu

hawakumtembelea, lakini hata walitoka kwa chakula cha mchana na Jones.

Ilikuwa wazi kwamba hawakumchukulia kwa uzito hata kidogo.

Tunu aliitikia kwa kichwa. "Meneja Mkuu

Changala ameshikilia wadhifa muhimu

katika kampuni kwa miaka kumi. Wakati

wa umiliki wake, aliongeza faida ya

kampuni kwa 10%, na wanahisa

wameridhika naye sana. Ikiwa… Ikiwa

Mwenyekiti unataka kumfukuza kazi, ninahofia itasababisha kutoridhika sana miongoni mwa wanahisa.”

“Sawa, nimeelewa. Unaweza kwenda nje kwanza.” Lisa akanyamaza kimya, kisha, alienda kukagua idara kuu za kampuni. Hata hadi jioni, hakuna hata

mmoja wa wasimamizi wakuu aliyefika kumuona.

Kulipoingia giza, Lisa alimwambia Shani, “Nifanyie msaada na uajiri mpelelezi binafsi. Nataka kujua kuhusu jambo fulani.”

Saa moja jioni, Lisa alirudi nyumbani akiwa na rundo la hati mikononi mwake.

Alvin alikaa sebuleni akiwa amevaa

nguo za kawaida huku mikono yake

ikiwa inatetemeka kidogo. Alionekana

mwenye hofu kwa mbali, akimsikiliza

Hans alipokuwa akiripoti kitu kwake kwa

heshima. Lisa alibadilisha viatu na

kuingia ndani. Alvin akageuka, na

midomo yake maridadi iliinama chini.

"Mwenyekiti Lisa, hatimaye yuko tayari

kurejea."

"Nimekuwa nikifanya kazi kwa muda wa ziada katika kampuni yangu. Vipi, umekula?" Lisa aliona kuhudhunishwa kwake na akaelezea kinyonge. Alvin alishika midomo yake lakini

hakuzungumza. Aunty Linda alijitokeza kueleza, “Bw. Kimaro hapendi chakula

ninachotengeneza. Anataka chakula unachopika wewe mwenyewe.”

Lisa alishusha pumzi. Alikaa kando yake kwa uchovu na kumuegemea

begani. “Nimechoka baada ya kufanya kazi siku nzima na siwezi kufanya

chochote. Upikaji wa Aunty Linda unafanana na wangu, kwa hiyo jaribu tu kula.”

"Kwanini, mambo hayakwenda sawa

kwenye kampuni?" Alvin akageuka

kumwangalia. Nywele zake zilisonga

kwenye sehemu ya juu ya pua yake, na

kumfanya anuse harufu hafifu.

“Mmh, hao watendaji wa ngazi za juu

hawanitilii maanani hata kidogo. Bado kuna vita ngumu kupigana." Kadri Lisa

alivyozidi kuongea ndivyo alivyozidi kuzama kwenye hisia za kumuegemea

Alvin. Alijihisi amani bila kufikiria chochote.

Alvin alikunja uso kabla ya kumwambia

Hans, “Nenda kwenye kampuni yake

kesho ukamsaidie kupanga mambo yake. Hakikisha wanakuwa watiifu ndani ya siku moja.”

"Nimeelewa," Hans alijibu mara moja.

Alikuwa msaidizi wa milionea mkubwa nchini. Kiasi hiki kilikuwa kipande cha keki.

Lakini, Lisa alisema haraka, "Hapana.

Ingawa Hans kwa kawaida ana uwezo

mkubwa, yeye ni msaidizi wako tu na

hajui chochote kuhusu kampuni ya

Mawenzi. Ataliwa na hilo genge la watu

mpaka hata mifupa yake haitabaki.

"Hans huyu, ambaye yeye ndiye

amezowea kula watu, leo hii aje aliwe

yeye?" Alvin akacheka. "Hiki kitakuwa

kichekesho cha mwaka."

'Ninathamini nia yako nzuri, lakini hili

nitapambana nalo mwenyewe" Lisa

alisema kwa unyoofu, "pia nilipata

sababu iliyonifanya ulijeruhiwa kwenye eneo la ujenzi mara ya mwisho. Hakika

nitalipiza kisasi kwa ajili yako.”

“Sawa. Mwanamke wangu wa nguvu

sasa ana uwezo kweli kweli." Alvin alisugua nywele zake na kumwambia

kwa mapenzi, "una njaa, kwa hivyo nenda ukale."

"Na wewe je?"

“Kama utanipikia nitakula.”

Sura ya 112

Lisa alimtazama kwa makini kwa muda.

Hakukuwa na cha kufanya kwa jinsi

alivyomuona mumewe, zaidi ya kwenda

jikoni na kupika chakula ili ale.

Hans alitazama umbo la Lisa likipotea

kabla ya kuendelea kuongea, “Baada ya

siku chache, Willie Kimaro ataingia Dar.

Watu hapa tayari yanajua kuhusu hilo. Nahofia itasababisha zogo.”

“Yeye ni kipande cha takataka tu. Mahali kama hapa tu ndio patamchukulia kama mtu mwenye nguvu,” Alvin alidhihaki.

"Unataka kupanga kukutana naye?" Hans aliuliza.

"Hapana. Bado hastahili.” Alvin akasimama. “Usiku umeenda sana.

Rudi nyuma." Hans na Shani wote waliondoka.

Lisa alikuwa amevaa vazi la jikoni akiwa amezama kwenye mapishi akimpikia mumewe. Taa ya jikoni yenye joto iliangaza juu ya kichwa chake, na kumpa mumewe hamu ya kumshika.

Akamsogelea na kumkumbatia kwa

upole kwa nyuma, akaegemeza kidevu chake kichwani. “Ongeza zaidi. Chapati

hizi hazitatosha kuniridhisha.”

"Ushukuru tu kwa kuwa ninakupikia."

Lisa alisema kwa kujigamba. "Ikiwa

unataka kula, basi katakata hiyo nyama ya nguruwe wewe mwenywe."

Alvin alionekana kusikia kitu kisichoaminika. “Unathubutu kuniagiza?”

Lisa alifikiria kabla ya kuchukua kadi kutoka mfukoni mwake na kumkabidhi.

"Hii ni nini?" Alvin aliuliza kwa mshangao.

"Kuna milioni 500 ndani yake. Ni ada ya kesi uliyonitetea hapo awali…” Lisa

alikuwa bado hajamaliza kuongea akahisi hali ya hewa iliyomzunguka

imebadilika ghafla. Macho ya Alvin yalionekana kufunikwa na unyonge, na kusababisha akose raha.

“Unamaanisha nini kwa hili?” Alvin

aliishika kadi kwa vidole viwili na

kudharau kwa macho yake. "Umekuwa mwenyekiti leoleo tayari umechota pesa

zote hizi kwenye kampuni, si utafilisi

kampuni wewe?"

"Wala," Lisa alijibu akitabasamu kwa

kuridhika, "sema tu ni deni lililokuwa likininyima amani."

"Una pesa sasa, kwa hivyo unataka kufuta uhusiano wetu, si ndiyo?" Alvin

aliuliza na kukaribia kuichana kadi hiyo vipande viwili. "Endelea kuota. Ulitia

saini wewe mwenyewe karatasi.

Haijalishi una nafasi gani, itabidi uendelee kukaa nami kwa utiifu.”

“Huwezi kunisubiri nimalizie…?” Lisa

aliitazama ile kadi na kuikandamiza miguu yake kwa hasira. "Nataka

kukulipa deni lako ili niishi na na wewe kwa usawa. Sitaki kuwa mtumishi wako.

Nataka kuwa mpenzi wako kwa kila maana ya neno hilo.”

“Hiyo ina maana gani?” Alvin alikunja uso, alikuwa haelewi.

Lisa akashusha pumzi ndefu. “Siku zote

nimekuwa nikijisikia kuwa duni kwa

sababu tulisaini mkataba na ulinisaidia

katika kesi hiyo. Mimi ni kama mpenzi

wako na mtumishi wako, na daima ni

lazima niwe mnyenyekevu mbele yako.

Siwezi kukukosoa pia. Hali hii inanifanya nijihisi kama mtumishi wako tu. Nachukia hilo. Ikiwa tutaondoa hayo mashariti, ninatumaini kwamba

tunaweza kuwa kama wanandoa wa kawaida.”

“Tangu lini nikakuchukulia kama mtumishi? Si ni wewe nduye umekuwa ukiniudhi mara nyingi zaidi?” Alvin alimkazia macho. Hakuweza kuelewa mawazo ya mwanamke huyo. “Unataka kunipa pesa ili usinipikie tena, sivyo?”

Lisa alikosa la kusema kabisa. “Hebu ngoja nuikueleweshe tena. Natumia hii milioni 500 kuvunja makubaliano ya awali ya mkataba wa ndoa. Nataka

kuwa mpenzi wako rasmi. Nikitaka

kupika, nitapika, na ikiwa sitaki kupika, sipiki. Nitakasirika ikiwa ninataka

kukasirika, na nitapigana na wewe ikiwa

ninataka kupigana. Nitafanya kila kitu kwa uhuru.”

Kifua cha Alvin kilitanuka kwa hasira.

Alitaka kuitupa ile kadi moja kwa moja kwenye moto ili iwake. Lisa aliruka

ghafla na kumbusu kwenye midomo. Akikumbatia shingo yake na kusema kwa umakini, “Alvilisa, sijui kama umewahi kuwa na mpenzi hapo awali, lakini hivi ndivyo wapenzi wa kawaida wanavyokuwa. Utakuwa pipa langu la takataka na sufuria yangu ya asali. Ninakupenda, kwa hiyo nataka kukupenda kwa usawa.”

Mdomo wa mwanamke ghafla ulikuwa

mtamu kama asali. Hasira za Alvin zilikatika ghafla. Akimtazama usoni, alisita kabla ya kusema, “Makubaliano yanaweza kusambaratika, lakini usinipe pesa. Wewe ni mwanamke wangu.

Ikiwa nitakushtaki kwa kesi hiyo, nawezaje kujiita mwanaume?"

“Lakini…”

"Nyamaza. Sema neno moja zaidi nami nitakufundisha somo.” Alvin akaendelea

kumnyonya mdomo. Uso wa Lisa ukawa

mwekundu mara moja huku akikanyakanyaga miguu yake.

“Mhhhhh…Wewe mpuudhiii.”

“Vipi mimi ni mpuuzi? Wewe ndiye

unayetaka tuwe kama wanandoa wa kawaida. Wanandoa wa kawaida wako hivi." Alvin alitabasamu vibaya. Lisa alipigwa na butwaa na kumkodolea macho ghafla. “Unaonekana una ujuzi sana. Lazima uwe mzoefu sana. Nina

hakika ulishawahi kuwa na wapenzi wengi sana kabla yangu.”

Uso mzuri wa Alvin ukakakamaa, na macho yake yakageukia pembeni.

"Usifikirie ujinga. Nimekuwa na mpenzi mmoja tu." Alvin hakutarajia angekuwa na wivu kiasi hicho na alikuwa hana la kusema.

“Bado una hisia naye? Uso wako unapomtaja unachangamka.” Lisa alizungumza. Hali yake ya furaha ilipotea mara moja.

“Amekufa.” Alvin alikunja uso kwa huzuni.

Lisa aliganda, ghafla asijue la kusema.

"Samahani."

“Acha kufukua makaburi. Hukuwa pia na Ethan Lowe hapo awali?” Alvin alikumbusha kwa huzuni.

Lisa hakuweza kusema chochote na akawasha jiko tena kwa utiifu. Alvin

akairudisha kadi mfukoni mwake na kutoka nje. Ni baada ya kutoweka tu ndipo Lisa alikumbuka kuwa alimwomba akate nyama lakini hakufanya. Mjinga!

Mlegevu!

Baada ya chakula cha jioni, Lisa

alimsumbua sana Alvin kuhusu kuvunja mkataba wao. Alvin hakuweza

kumshinda Lisa kwa king’ang’anizi ikabidi tu kuuondoa.

"Unaweza kuvunja mkataba, lakini bado

huwezi kuwasiliana na mtu yeyote

kutoka jinsia tofauti kama Kelvin Mushi

au Ethan Lowe. Lazima uje nyumbani

kwa wakati pia. Huruhusiwi kuchelewa

kutoka nje,” Alvin alikumbusha kwa

utulivu, “Pia, huruhusiwi kuniacha.”

"Ndio, ndio, ninajua tayari. Wewe ni mzuri sana, naanzaje kukuacha? Kuna msingi imara wa upendo kati yetu sasa.”

Maneno ya Lisa yalijaa mahaba. Lisa alichukua hatua ya kuketi kwenye

mapaja yake na kumbusu. Hali ya Alvin ilikuwa taabani, na akatoa mkataba bila shuruti.

Lisa alichoma makubaliano hayo, na lile

jiwe kubwa lililokuwa likimwelemea

moyoni likaonekana kumshuka. Usiku

mzima, alilala akiwa mwepesi sana.

Alvin pia alihisi kuwa sasa yuko

mchangamfu zaidi. Alipomwona hivyo, ghafla alihisi furaha hata yeye bila kujali

kuwa makubaliano yao yalikuwa yamechomwa.

Sura ya 113

Siku mbili zilizofuata ambazo Lisa

alienda ofisini kwake, hakuna kiongozi

yeyote aliyekuja kumuona. Hakuna

aliyeripoti chochote kuhusu kampuni hiyo kwake pia. Mambo mengi

aliyojifunza yalitoka kinywani mwa

Tunu. Hakuna mtu katika kampuni

aliyeonekana kumchukulia kwa uzito kama mwenyekiti.

Saa sita mchana, alienda kwenye

mgahawa kwa chakula cha mchana, lakini hata baada ya kungoja kwa dakika

20 kwenye chumba cha chakula, hakuna mtu aliyetoa chakula hicho.

Tunu alienda kuongea na mhudumu wa

mgahawa na kurudi akiwa mtupu baada ya dakika tano hivi huku akihema kwa hasira. “Wako pia hapa. Chakula

ulichoagiza kimeishia kwenye chumba

cha Jones na Meneja Mkuu Changala.

“Wapo chumba jirani?” Lisa alikodoa macho.

“Ndiyo,” Tunu alisema kwa hasira, “watu

katika mgahawa wote wanawahudumia wao tu.”

Hali ya Lisa ilikuwa ngumu. Hakutarajia

kwamba Jones alikuwa ameshinda hata

wafanyakazi wa mgahawa. “Achana

nao, sitakula hapa tena. Rudi ofisini na uagize usafiri.”

Lisa alisimama na kutoka nje. Kisha

akamuona Lina akiwa amesimama

kando ya mlango huku akionyesha

dhihaka. "Mwenyekiti Lisa, inaonekana

kwamba kuwa mwenyekiti sio jambo la kufurahisha. Ulikuja kwenye mgahawa

kula lakini hakuna hata mtu mmoja hapa

wa kukuhudumia, kwa hivyo lazima

uagize take-out. Maskini wewe."

Lisa alimwangalia Shani. Bila kusema

neno, Shani alinyanyuka na kumpiga

Lina usoni, na kusababisha shavu lake

kuvimba mara moja. Shani kisha

akampiga kofi lingine upande wa pili wa

uso wake, na kumfanya Lina ashindwe

kusema lolote kutokana na maumivu

hayo. Alimkazia macho Lisa lakini

hakuthubutu kupiga hatua tena.

Lisa alitabasamu. "Naweza hata

kumpiga baba yako Jones, sembuse wewe? Usipotazama maneno yako

wakati ujao, nitakupiga hadi ujifunze somo lako.” Kisha, akamsukuma Lina

pembeni na kuondoka huku akitabasamu. Lina alishika mashavu yake, chuki ikimchoma machoni. 'Lisa, ngoja tu uone. Nitakuua wewe mimi binafsi siku moja.' Lina aliishia kujiapiza mwenyewe kimoyomoyo.

Saa tisa alasiri Kwenye ghorofa ya 17 ya jengo hilo, mkutano ulikuwa ukiendelea bila uwepo wa Lisa. Meneja mkuu, Lazaro Changala, alikaa kwenye kichwa cha meza, akifuatiwa na wasimamizi wakuu wa Mawenzi Investiments.

Naibu Meneja Ngololo alisema, "Meneja

Mkuu Changala, Mwenyekiti Lisa

alichukua nafasi hiyo. Ni sawa kama

tusipomwita kwa ajili ya mkutano wa kwanza wa mwanzo wa juma?”

"Unafikiri yeye ni nani?" Lazaro

Changala alisema kwa dharau, “Yeye ni msichana mdogo tu asiyejua lolote.

Sawa, tuanze mkutano. Meneja Lina Jones, je, kampuni ya mapambo ya mradi wa ukuzaji mali imekamilika?”

Lina alivaa barakoa kufunika uso wake

huku akivumilia maumivu usoni mwake. "Bado. Bei zinazotolewa na kampuni za ujenzi ni kubwa mno. Ninafikiri kwamba tunaweza kuiomba timu yetu ya ujenzi ili

kushughulikia sisi wenyewe. Hivi majuzi niliandaa muundo na kila mtu aanaweza kuona sasa."

Kisha alitoa rundo nene la makaratasi yenye michoro ya miundo juu.

Watendaji wote walimjaza sifa. "Miundo hii ni ya kibunifu sana. Ni ya hali ya juu na imechorwa kisomi, lakini sio ya anasa kupita kiasi. Ina mchanganyiko wa ladha nzuri sana."

“Umezibuni wewe mwenyewe, Meneja Jones? Unashangaza.” Lazaro

Changala hakuamini. "Ni bora zaidi

kuliko jumba lililojengwa katika mradi wa maendeleo uliopita."

Lina alijifanya kuwa mwenye kujua na kusema, “Karatasi ya makadiro ya gharama pia iko ndani. Nilifanya makadirio na ni gharama nafuu zaidi kuliko tukiajiri kampuni ya ujenzi kutoka nje.”

Lazaro alijawa na sifa. “Meneja Jones, umefanya kazi nzuri. Miundo hii lazima iwe imechukua muda wako na juhudi nyingi."

"Sijalala kwa siku kadhaa, lakini nina furaha sana kuchangia kampuni." Lina alijisifia.

Kabla Lina hajamaliza, mlango wa chumba cha mkutano ulisukumwa. Lisa aliingia kutoka nje akiwa na watu wengine. "Kila mtu yuko kwenye mkutano? Mbona hakuna hata aliyenipa habari kuhusu tukio kubwa kama hili?”

Lisa alifoka mbele ya meneja mkuu

Lazaro Changala..

Lazaro hakubabaika. Uso wake ulikuwa

unatabasamu kama kawaida, lakini macho yake yalikuwa ya dharau.

“Mwenyekiti Jones, wewe ni mdogo sana kuliko mimi. Hata nikikwambia kuna vitu unaweza usivielewi kwa hiyo sikukupigia simu.” Baada ya kuongea, chumba cha mkutano kilikuwa kimya sana.

Kila mtu alingoja kutazama mchezo wa kuigiza ukiendelea wakati Lisa angekasirika, lakini uso wake mzuri ulionyesha tabasamu tulivu. “Meneja

Mkuu Changala, nimesimama hapa kwa muda mrefu sasa. Kwa hiyo utaendelea na tabia hii hadi lini? Umeshindwa kujua ni nani anayesimamia kampuni baada ya kukaa kwa muda mrefu sana?”

Alikuwa akicheka waziwazi, lakini hasira

machoni mwake iling'aa sana. Mara

moja Lazaro aliona aibu.

Lisa aliwageukia Shani na Tunu.

"Inaonekana kama Meneja Mkuu

Changala amejisahau kidogo. Tafadhali

mkumbusheni maana ya heshima ni nini.” Kabla Lazaro hajajibu, aliburutwa chini na Shani kwa mkono mmoja.

Alikasirika wakati akiburutwa akatoka akifoka kwa hasira.

“Hebu tuendelee na mkutano. Mlikuwa mnazungumza nini?” Lisa alimkatisha na kutazama umati wa wafanyakazi.

"Tulikuwa tunazungumza juu ya muundo wa mradi wa maendeleo. Meneja Jones alikuja na miundo fulani. Meneja Mkuu Changala na sisi wengine tunahisi kuwa muundo uko vizuri sana.”

Naibu Meneja Ngololo alikabidhi miundo kwa shida.

Moyo wa Lina ulidunda. Hakuwahi

kufikiria kuwa Lisa angetokea. Lisa bila shaka angetambua miundo hiyo. Hata

hivyo, haikujalisha. Hata kama Lisa

angelisema kwamba Lina aliiba michoro yake, hakuna mtu angemwamini.

Badala yake, ingechochea tu wafanyakazi kumdhihaki. Lisa alichukua

miundo na kisha akamnong'oneza

Shani maneno machache. Baada ya Shani kutikisa kichwa na kutoka nje, Lisa aliendelea, "Miundo ni nzuri. Inaonekana ilichapishwa saa moja asubuhi ya leo. Meneja Jones, lazima umekesha hadi usiku sana

ukitengeneza miundo hii.”

"Ndio, Meneja Jones alisema hakuwa amelala kwa siku kadhaa." Mtu mmoja alidakia.

"Meneja Jones anafanya kazi kwa bidii sana." Mwingine akaongezea sifa juu yake.

Chumba cha mkutano kilisikika kwa

pongezi. Lina alijivunia sana. Alikuwa amechelewa kuzichapisha kwa makusudi.

"Mwenyekiti Jones, una maoni gani kuhusu miundo yangu?" Lina alijibaraguza kuuliza.

"Miundo ni mizuri sana. Lakini unafahamu kwamba nilipoteza rasimu ya muundo sawa na hii nusu mwezi

uliopita.” Lisa aligeuza maneno yake ghafla.

Kila mtu alipigwa na butwaa, lakini Lina

hakuwa na wasiwasi. Badala yake, alijifanya kupepesuka na kuziba mdomo wake. “Hauna maana ya kumaanisha kwamba nilikunakili, sivyo?”

"Mwenyekiti Jones, una wivu na talanta ya Meneja Jones?" Lazaro Changala

alicheka kwa uchungu. “Kila mtu anajua kwamba nyinyi ndugu wawili

hamwelewani, lakini hakuna haja ya kuhusisha kampuni katika marumbano yenu.”

Kwa muda, kila mtu alimtazama Lisa

kwa dharau. Alikuwa mdogo sana kuwa mwenyekiti.

“Nilijua nyinyi hamtaniamini.” Lisa

akashusha pumzi. “Kwa bahati nzuri, tayari nilitoa taarifa polisi siku kumi

zilizopita. Data yangu ya asili ya

muundo wakati huo imekabidhiwa kwa

polisi pia. Wana rekodi ya kesi hiyo, kwa

hivyo itakuwa wazi tutakapoiangalia."

Lina aliingiwa na hofu na haraka

akajifanya analia. "Mimi ni meneja tu Mwenyekiti Jones, kwanini unifanyie hivi? Nilimaliza miundo muda mrefu

uliopita na niliichapisha kwa

kuchelewa.” Mwonekano wake mpole uliwafanya watendaji wengi wafikirie kuwa Lisa alikuwa akimlenga kimakusudi.

Lisa akatoa michoro na kuuliza, “Unasema kwamba ninakusingizia? Sawa. Kwa kuwa michoro hii iliundwa na wewe, unapaswa kujua aina na mwelekeo wa nyumba. Je, ina sakafu ngapi? Vitalu vingapi? Ni kubwa kiasi gani?" Lina alipigwa na butwaa na akajibu tu baada ya muda mrefu, "Kuna

vitalu sita, na vinakaa kusini huku

vinatazama kaskazini ..."

Sura ya 114

Mara tu baada ya kumaliza

kuzungumza, watendaji wachache

waliokuwa wakijadili muundo huo

walikunja uso.

Lisa kisha akauliza, “Kwa nini unahitaji

kabati kubwa katikati hapa?”

"Kwa ajili ya nafasi kubwa ya kuhifadhia." Lina alijibu bila kujiamini.

Lisa alifoka. “Ni kwa sababu kuna nguzo

kubwa katikati ambayo haiwezi kung’olewa, nikachagua kuweka kabati

kubwa hapo.” Lina akabaki ameduwaa, hana cha kumkosoa Lisa. “Na kwa

kuongezea, ni jumba lenye ghorofa mbili na ukubwa wa mita za mraba 128.7.

Iinakaa mashariki, likitazama magharibi.” Uso wa Lina ulipauka mara

moja kwa aibu.

Lisa alikodoa macho. "Unadai kuwa

ulitengeneza hizi, lakini hujui chochote

kuhusu maelezo yake ya kitaalamu, ungewezaje kuwashauri mafundi?

Wewe ndiwe msimamizi wa mradi, ilhali

hujui lolote kuhusu aina ya nyumba na ni majengo mangapi yanajengwa katika

mradi huo, unafaa kweli wewe?”

Lina hakuweza kukanusha neno lolote

kwa sababu hakuwa anaelewa chochote kuhusu michoro hiyo. Kundi la wafanyakazi waliokuwa kwenye

mkutano huo lilitingisha vichwa vyao

mmoja baada ya mwingine, wote wakiwa wamekata tamaa sana.

Wakati huo huo, Shani aliingia na maafisa wachache wa polisi. Mmoja

wao alimfunga pingu mikononi Lina. “Bi. Jones, tulipokea ripoti kwamba umeiba

kazi ya mtu mwingine. Tafadhali fuatana nasi hadi kituoni kwa ajili ya uchunguzi.”

“Hapana, sitaki! Sikufanya hivyo!” Lina alipiga kelele kwa hofu.

“Acha kupiga kerere weye, hiri ni jeshi ra porisi, tii sheria bira shuruti.” Polisi

mmoja mwenye sura mbaya zaidi

alimuadabisha Lina. Polisi hao wawili

walimnyanyua na kumtoa nje bila subira.

“Ninafanyiwa njama tu! Mimi sikuiba. sikufanya hivyo!” Lina alilalamika bila msaada.

Mayowe yake yalipofifia, Lisa alitazama

kwenye chumba cha mikutano kabla ya kumgeukia Lazaro Changala. “Meneja

Mkuu Changala, nilisikia kuwa wewe

ndiye uliyemteua Lina Jones kuwa

meneja wa mradi huu. Nina shaka na maono yako na uwezo wako wa kuongoza kampuni."

Lazaro Changala akaingiwa na hamaki

na kujibu kijeuri. “Kama Mwenyekiti

Jones unatilia shaka uwezo wangu basi niondoe kama unaweza.”

Alimwangalia moja kwa moja Lisa

alipomaliza kuongea. Hakuamini kama

Lisa alikuwa na ujasiri wa kumwondoa

kwenye nafasi yake. Bodi ya wakurugenzi wa Kampuni

wasingemwacha salama.

“Inawezaje kuwa hivyo? Meneja Mkuu

Changala ameongoza utendaji wa kampuni kwa mafanikio mengi. Kwa

kawaida, nakuamini.” Lisa alitabasamu

ghafla na kubadilisha mawazo yake.

"Mkutano huu nitakuachia ili uendelee

nao." Kisha akamaliza kuongea na kuondoka zake. Lazaro Changala alimtazama nyuma kwa dharau.

Alifamini kwamba asingemfanya lolote kwa sababu alikuwa na uzoefu zaidi

kuliko yeye.

Hata hivyo, baada tu ya Lisa kuondoka tu, kuna kituko kilitokea ghafla. Mke wa

Lazaro Changala aliingia ndani ghafla

na kumpiga kofi usoni. "Lazaro Changala, wewe mwanaharamu!

Unathubutuje kuwa na mchepuko nje?

“Kama nisingekuoa enzi hizo, leo hii

ungeweza kuingia Mawenzi Investiments ukiwa na jeuri hivi?”

Changala alichukia kupitiliza.

“Kwa hiyo unanifanyia makusudi siyo?

Umenitumia miaka yoote hiyo hadi

umenizeesha ndiyo unaamua kurudi

kwa mabinti? Nitapambana nawe.”

Mama yule wa makamo aliwaka kwa hasira.

Habari za ghasia kwenye chumba cha

mkutano zilienea haraka katika kampuni

nzima. Tunu alicheka wakati wa kuripoti

habari hiyo kwa Lisa. “Hukuona jinsi uso wa Meneja Mkuu Changala ulivyokuwa

karibu kupasuka alipopigwa kofi. Alifedheheka kabisa. Hata aliamua

kumpiga vibaya mke wake hadharani.”

'Huu ni mwanzo tu." Lisa alitabasamu

na kumpigia simu Sam. “Sam, huna namba yoyote ya mwandishi wa habari?

Kuna mambo ya kuruhashisha hapa nataka yaripotiwe kwa jamii.”

“Haha, hakuna shida, nitakutafutia.”

Sam alijibu kwa furaha. “Ni mara

chache sana shemeji yangu huwa anaomba msaada wangu…lakini ni jambo gani hilo?”

Lisa akaeleza kituko kilichomtokea

Meneja Lazaro Changala.

Kabla Sam hajaendelea kusema, ghafla

alihisi kushtuka. Akatazama upande

wake alipokuwa amekaa Alvin huku uso

wake ukiwa unapunguza furaha

taratibu. Alijiuliza kimykimya. “Lisa, kwa

nini haombi msaada wa Alvin? Kwani

Alvin hawezi kushughulikia mambo

kama haya? Au kwa sababu Meneja

Changala ni mkorofi na mtu hatari

anahofia atamsababishia Alvin matatizo?”

Lakini Alvin asingeshindwa

kushughulikia hilo. Familia ya Kimaro

ilimiliki kampuni yenye nguvu zaidi ya

vyombo vya habari nchini, lakini Lisa

hakuwa amepata nafasi ya kufahamu

hilo kwa hiyo ikabaki kuwa ni siri ya

Alvin hadi muda huo.

Sam alikosa la kusema. “Lisa, unaenda mbali sana. Huogopi kwamba Meneja

Mkuu Changala ataniletea shida?”

"Atakuletea shida gani? Wewe ni kijana wa familia tajiri ya Harrison, atathubutuje kukugusa?” Lisa alicheka.

“Ukinisaidia, Mawenzi Investiments

itashirikiana nawe katika siku zijazo.

Ninahakikisha kwamba familia ya

Harrison inashirikiana na Mawenzi

katika miradi ambayo familia yenu

inashughulikanayo. Familia ya Jones

haitakuwa na nafasi.”

“Oh jamani, shemeji hakika unajua

kunipanga.” Sam akakosa ujanja.

“Usiseme hivyo. Wewe ni rafiki wa Alvin, kwa hiyo sisi sote ni familia.”

Sam karibu aanguke kwa kicheko.

“Sawa, uko sawa.”

Baada ya kukata simu, Sam alifurahi sana. "Lisa ni mcheshi sana. Kila kitu anachosema ni sehemu ya mkakati.

Nilikuwa na wasiwasi asingeiweza nafasi yake kama mwenyekiti.

Inaonekana kwamba yuko thabiti kuliko nilivyokuwa namfikiria.”

“Unajua unazungumzia mwanamke wa nani?” Alvin alitabasamu kwa kiburi, lakini ghafla alifikiria kitu na kumtazama

Sam kwa uso kuchukia.

Sam alijibu akiwa na uso uliotulia. “Una

wivu kwa sababu Lisa amenipigia simu

kuniomba msaada? Lisa ni mjanja sana, anataka kukulinda. Ana wasiwasi

kwamba utaumizwa na Lazaro

Changala. Nakuonea wivu sana kwa

kuwa na mwanamke kama huyu."

Alvin akatabasamu. Alichokisema Sam kilionekana kumwingia akilini. Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa mwanamke

kujaribu kumlinda. Moyo wake ulijawa na hisia za furaha sana. “Uko sahihi.

Alisema atanitunza.”

Tabasamu tata lilichanua kwenye uso wake mzuri, na kusababisha uso wa Sam kuwa na matuta kila mahali. “Alvin, huna aibu sana. Tayari wewe ni tajiri

sana lakini una ujasiri wa kuruhusu

mwanamke akutunze?”

Macho ya Alvin yalimtoka kwa furaha.

Aliukumbuka usumbufu wote ambao

Lisa alimsababishia hapo awali, sasa

ulikuwa umefika muda wa kula

matunda.

Sura ya 115 Siku iliyofuata, habari za mambo ya

meneja mkuu wa Mawenzi Investiments

kupigwa na mkewe ofisini zilienea

mtandao mzima. Lazaro Changala alikasirika. Sifa yake iliharibiwa kabisa.

Picha zake akipigwa na mke wake

hadharani zilienea kila mahali, na hata

video yake iliyomwonyesha akiwa na mchepuko wake ilisambaa.

Katika ofisi ya mwenyekiti, Meneja

Mkuu Changala aliingia kwa hasira na kumwelekeza Lisa kidole cha usoni.

“Umefanya nini? Kwanini umesambaza picha zangu mtandaoni, zinakuhusu nini?”

“Sijui unazungumza nini Bwana Changala.” Lisa alikaa tuli kwenye kiti

chake huku akionyesha uso wa kujiamini. "Meneja Mkuu Changala, sikuwahi kutarajia ungekuwa mtu kama

huyo. Umetukatisha tamaa sana.

Umeharibu hata sifa ya kampuni.”

“Unawezaje kuthubutu kusema hivyo, wewe b*tch?! Usifikirie kuwa sijui

kwamba wewe ndiye upo nyuma ya hili.

Unafikiri unaweza kunichezea mimi?"

Lazaro Changala alimwendea Lisa na

alikuwa karibu kuinua mguu wake ili kumpiga teke, lakini Shani alimkimbilia na kumsukuma kwenye ukuta.

"Wewe b*tch, niachie!" Lazaro

Changala alipiga kelele bila kujizuia.

Lisa alipiga intercom kuita usalama.

“Fanya haraka umtoe. Nadhani hali ya

Meneja Mkuu Changala si nzuri kwa

sasa, kwa hivyo nitamkabidhi Naibu

Meneja Ngololo masuala ya kampuni.”

"Lisa Jones, we subiri tu! Unathubutuje

kunifanyia mambo kama haya?

Endelea, siku yako yaja!" Baada ya

Lazaro Changala kuvutwa nje, Naibu

Meneja Ngololo aliingia kwa haraka.

Akiwa amekabiliana na sura nzuri ya

Lisa tena, ghafla alihisi hofu moyoni

mwake. Watendaji wa kampuni hiyo

hawakumchukulia Lisa kwa uzito hapo

awali, lakini ilikuwa ni siku moja tu na

sifa ya Meneja Mkuu Changala

iliharibiwa kabisa. Kila mtu sasa alitia

adabu kwa Lisa. Hakuna aliyekuwa na

ushahidi wowote, lakini wote walikuwa

na uhakika kwamba Lisa alikuwa na mchango mkubwa katika hilo.

"Naibu Meneja Ngololo, wewe ni mtu mwenye uwezo na uzoefu, lakini daima

ulikuwa unakandamizwa na Meneja

Mkuu Changala kwa makusudi. Lazima

ulijisikia vibaya, sivyo?" Lisa mwenyewe aliinuka na kummiminia kikombe cha kahawa.

Naibu Meneja Ngololo alishtuka na

akapokea kahawa haraka, kisha akasema, “lakini Meneja Mkuu

Changala amekuwa madarakani kwa zaidi ya miaka kumi. Watu wengi katika

kampuni wanatii maagizo yake, na wakurugenzi wengi wanampenda pia.”

Lisa akaenda moja kwa moja kwenye

maamuzi yake kwa uhakika. “Nitakupa muda wa wiki moja. Amua ikiwa

unataka kupaa angani au ubaki chini ya

Lazaro Changala kama nyumbu wake

maisha yako yote." Moyo wa Naibu

Meneja Ngololo ulitetemeka sana.

Wakati huo huo, Tunu alikimbia kutoka

nje. “Mwenyekiti, Meneja Mkuu

Changala alipigwa na kundi la wanawake wakati alipotoka nje ya geti la kampuni. Ni wanawake kutoka umoja wa wanawake wanoteswa na waume zao majumbani, wanaochukia watu

wote wanaosaliti wake zao. Walimpiga nusura kumvunja mguu na kichwa

kilikuwa kikivuja damu. Anapelekwa hospitali sasa hivi.”

Naibu Meneja Ngololo ghafla alitazama

juu na kuona uso wa Lisa usio na hisia.

Miguu yake ilitetemeka kwa hofu.

“Nitafanya hivyo. Namfahamu Lazaro

Changala vizuri sana. Ninaweza

kuchukua udhibiti wa kampuni katika

wiki moja. Nitakufanyia kazi Bibi

Mwenyekiti,” alisema kwa sauti.

“Vizuri sana, nakuamini. Fanya hivyo ili

Changala asiwe tena na nafasi katika

kampuni hii.” Lisa aliongea kwa umakini na mamlaka. Pembeni, Shani

alimtazama na kugundua kuwa tabia ya

Lisa ilizidi kufanana na Alvin wakati

anafanya kazi. Baada ya Naibu Meneja Ngololo

kuondoka, Lisa alijilaza kwenye sofa kwa uchovu na kusema kwa sauti yenye

hatia, “Mimi ndiye niliyemtengenezea njama hizi Lazaro Changala. Shani, unafikiri mimi ni mbaya?"

"Hapana," Shani alijibu kwa urahisi, "Kama hutakuwa mkatili, utawaongozaje mbwa-mwitu hao chini?"

"Ndio, nahitaji kuwa na udhibiti kamili

juu ya Mawenzi Investiments. Lazima

nilipize kisasi kwa bibi yangu." Lisa alikunja ngumi. Ilibidi alipize kisasi cha mama yake pia. Mzigo uliokuwa juu

yake ulikuwa mzito sana kwa yeye kuwa na huruma tena.

Katika wiki moja tu, Naibu Meneja

Ngololo alipanga upya kila kitu katika

kampuni ya Mawenzi Investiments

haraka. Aliwafukuza wafanyakazi wote

ambao walikuwa kinyume na Lisa

kutoka kwenye uongozi wa juu.

Kuhusu Lina naye alifukuzwa kazi bila

huruma. Lina hakujua juu ya suala

kubwa lililokuwa linaloendelea huko nje.

Alipokuwa kizuizini, wafungwa

walimpiga na kumwagilia maji baridi kila

siku. Kwa sababu ya hii, ngozi yake

iliharibiwa kabisa. Baada ya Lina

kuteseka kwa siku saba hadi nane, Jones alijitahidi kumwokoa kutoka

katika kituo hicho baada ya kutumia

kiasi kikubwa cha pesa. Alitoka akiwa

amebebwa.

Alipoona uso wake umevimba, Mama

Masawe alimkumbatia na kulia kwa uchungu.

“Mpenzi wangu, umepatwa na nini?

Nani alikupiga? Sitamwacha mtu huyo

abaki salama.”

“Baba, mama, lazima mlipize kisasi kwa

niaba yangu. Inauma sana… Ooohoohooo!” Lina alilia sana. Uso wa Lina

ulimuuma sana hata akashindwa kuinua macho.

Uso wa Lina uliokuwa umevimba

ulimjaa Stephen kwa karaha.

Mwanamke huyu alizidi kuwa mbali na mawazo yake. “Usijali, msichana mzuri.

Baba yako hakika atawarudia watu hao

kwa kukuumiza.” Stephen Kileo alisema

mdomoni lakini moyoni alikuwa

amekerekea sana.

Jones alipandwa na hasira. Alipogeuka, aliona kwamba Stephen alikuwa ametulia tuli. Alimwamia kwa hasira,

“Stephen, fanya haraka umchukue Lina. Anahitaji kupelekwa hospitali sasa hivi.”

“Sawa, sawa.” Stephen alitenda kulingana na maagizo ya Jones bila

kupenda. Tangu Lina aingizwe kwenye

kituo cha polisi, hakuwahi kuoga. Harufu

mbaya iliyotoka kwake ilikaribia

kumfanya ashindwe kuvumilia. Wakati

huo, alijuta sana. Ikiwa angejua

mapema kwamba hii ingetokea, wala

asingejihusisha na Lina kabisa.

Katika hospitali, akiwa na macho

mekundu, Lina alimwamuru daktari, “Nipe dawa bora zaidi. Nahitaji kupona

ndani ya siku tatu zijazo nirudi ofisini.”

"Samahani, hatuna dawa kama hiyo."

Daktari alimshangaa.

“Mnafanya nini hapa kama hamna

dawa? Kundi la watu wasio na maana.

Mama, nataka kuhamishwa hospitali

nyingine. Nataka kupona haraka iwezekanavyo na nirudi ofisini

kushughulika na Lisa.” Akiwa na uso uliovimba, Lina alionekana kuwa mbaya

zaidi alipokasirika.

Akivumilia chuki yake kwa Lina, Stephen alisema kwa unyonge, “Huwezi kurudi ofisini tena. Umefukuzwa kazi.”

"Nini?" Lina alitoa macho akiwa haamini

kabisa. “Lisa amerukwa na akili?

Anathubutuje kunifukuza kazi?! Meneja

Mkuu Changala alitoa idhini yake kwa hili?"

Jones Masawe alikunja uso na kujibu

kwa kuudhika, “Lazaro Changala ni

majeruhi na sasa yuko katika wodi

maalumu ndani ya hospitali hiihii.

Hawezi kuruhusiwa katika siku kumi

zijazo au hata nusu ya mwezi. Hivi sasa, Freddie Ngololo ndiye

anayesimamia kampuni nzima. Lisa alimpandisha cheo na kuwa meneja mkuu.”

Lina alipigwa na butwaa kujua jinsi

mambo yalikuwa yamebadilika sana

alipokuwa kizuizini kwa siku chache tu.

“Hili haliwezekani, ni yeye ndiye

aliyepanga njama za kumpiga Meneja

Mkuu Changala? Umepiga simu polisi?"

"Hapana." Akiwa amechoka kabisa

kimawazo, Jones aliongeza, “Iilikuwa ni kundi la wanawake wanaoteswa na

waume zao ndio ambao walimpiga

Lazaro Changala. Nilisikia kwamba ni

kwa sababu walikasirika kujua kwamba

Lazaro Changala alimsaliti mkewe.

Lazaro Changala sasa yuko kwenye

kina kirefu, na wafanyakazi wengine

walio kwenye usimamizi mkuu wa

kampuni tuliowahonga wote wanaogopa

sasa kumuudhi Lisa. ”

Lina alipatwa na wazimu. "Hujafanya lolote?"

"Lisa amebadilika kabisa. Tulitumia

miaka mingi kumlea na haya ndiyo anayotulipa sasa.” Mama Masawe

alisema kwa chuki, “Jones, lazima ulipize kisasi kwa niaba ya Lina na upate mamlaka tena kwenye kampuni ya Mawenzi Investiments.”

Katika siku chache ambapo Jones

Masawe alikuwa kama mwenyehisa

mkuu wa Mawenzi, Mama Masawe alifurahia kupendelewa na wanawake wengi matajiri. Hakutaka fahari hiyo ipotee na kurudi katika siku zile za dhiki baada ya kufirisika.

Sura ya 116

“Ni rahisi sana kupata tena mamlaka," Stephen Kileo alisema ghafla.

Wakishangazwa na maoni hayo, Jones

na familia yake walimtazama kwa makini. “Stephen, tuambie haraka wazo

lako. Sisi ni familia,” Lina akasema mara moja, “Mara tu Lisa atakapoanguka madarakani, tutaoana mara moja.”

Stephen alikodoa macho na kusema; "Willie Kimaro kutoka familia ya Kimaro

anakuja Dar kwa ukaguzi wa miradi

waliyowekeza hapa jijini. Kma tutaweza kumfurahisha, tunaweza kumtumia kuwamngusha Lisa.”

Macho yao yote yakang'aa. Willie

Kimaro alitoka familia tajiri ya Kimaro. Yeye na Alvin Kimaro walikuwa watoto wa kaka na dada, yaani mtu na binamu yake. KIM International, ni kampuni ya familia ya Kimaro na ilikuwa ikimiliki

asilimia 25 za hisa za Mawenzi

Investments. Kwa maana hiyo ilikuwa na nguvu kubwa kwenye bodi ya wakurugenzi. Kama kweli KIM

International ingeungana na Jones

Masawe kumwangusha Lisa, basi

angeondolewa kwenye nafasi yake ya

Mwenyekiti na mtendaji mkuu wa Kampuni ya Mawenzi.

Mgawanyo wa hisa katika Kampuni ya Mawenzi ulikuwa ni 30% kwa Lisa, 30% kwa Jones Masawe na 25% kwa KIM

International, 10% Chris Maganga na 5% zilizobaki zilimikiwa na wanahisa wengine wadogowadogo. Kwa hiyo

wanahisa wakubwa walikuwa wanne, Lisa, Jones Masawe, KIM Internatonal na Chris Maganga. kama wawili kati yao

wangeungana basi ilikuwa rahisi

kumwangusha mwingine, ndiyo njia

aliyotaka kutumia Jones Masawe, kutafuta njia ya kuungana na KIM

International kumwangusha Lisa. Jones alitetemeka kwa fadhaa. "Familia

ya Kimaro ndiyo inamiliki KIM

International. Ingawa Willie si mzao wa moja kwa moja wa familia ya Kimaro, tutaweza kumtumia kuunganisha nguvu

yetu mradi tu tufahamiane na familia ya

Kimaro. Ikitokea hivyo, hatutasumbuliwa na Lisa tena.”

"Ni wazo zuri sana." Stephen aliitikia

kwa kichwa. “Sifahamiani na Willie lakini najuana na msaidizi wake. Kwa kuwa

msaidizi wa Willie nipo naye vizuri, nitajitahidi anisaidie kuwa karibu naye

na kuwatambulisha nyinyi kwake. Ili kumteka kwa urahisi mnatakiwa

kuandaa zawadi ya kumfurahisha. Willie anavutiwa na vito vya thamani, na pia wanawake warembo!"

“Asante Stephen. Ninajuta kutokutana na wewe mapema. Wewe ndiye ninayeweza kukutegemea kwa sasa.”

Lina alimtazama kwa hisia za kuguswa.

"Ni jukumu langu kukusaidia. "Stephen alijaribu kuficha chukizo lake kwake.

••••

Ndani ya Mawenzi Investiments, saa

kumi na mbili za jioni, Lisa alipozima taa

na kutoka nje ya ofisi, mjukuu wa

mmoja wa kwakurugenzi wa bodi ya

Mawenzi, Amiri Gumbo alikuwa nje

akimsubiria na alipomuona alimsalimia

kwa shauku.

“Lisa, unatoka kazini. Ningependa

kukukaribisha kwa chakula cha jioni

kwenye hoteli maarufu ambayo hutoa

chakula kizuri…”

Lisa alikuwa mwisho wa akili yake.

Tangu alipoanza kupata tena mamlaka

katika kampuni, wakurugenzi wa bodi

wote walijaribu kujipendekeza kwake

kwa kuwatambulisha watoto wao na

wajukuu zao kama washirika wake watarajiwa.

"Nashukuru, lakini nilipanga kula

chakula cha jioni nyumbani ... " Lisa

alimtosa kwa upole.

“Ngoja basi nikupeleke nyumbani.”

Kijana yule aliongea kwa shauku.

“Mkoba wako unaonekana kuwa mzito.

Acha nikusaidie kuubeba.”

Kabla hajaugusa, Shani alishika mkono

wake. Macho ya mwanamke huyo

yalimtoka kwa ukali, jambo lililomfanya

kijana yule ashtuke. Alikuwa amesikia

kwamba mlinzi wa Lisa alikuwa mkatili

na hasa stadi wa kupiga watu makofi.

“Ikiwa utafanya hivyo kwa mara

nyingine, sitasita kukuvunja mkono,” Shani alimwonya kwa ukali.

Kijana yule alirudi nyuma kwa aibu.

"Unajua mimi ni nani? Sawa, hata hivyo

wewe ni mlinzi tu. Ulinzi ni kazi gani?

Hata mbwa anaweza kulinda, kwa hiyo

mimi siongei na mbwa, naongea na mwenye mbwa.” Kijana yule aliropoka tu kwa aibu ya kuadhibiwa na mwanamke.

Wakati huo lifti ilikuwa tayari imefika.

Kiijana huyo alipoona Lisa anaondoka akamfuata akiwa na maneno ya kuvutia.

“Lisa, umesikia kuhusu mkufu wa Malkia? Kuna stori kuwa miaka mingi

iliyopita, mfalme alimpa malkia wake

mpendwa mkufu. Mtu yeyote ambaye

atavaa mkufu huo atafikia furaha katika

uhusiano wake. Mkufu huo utauzwa

kwa mnada hivi karibuni kule Mlimani

City. Nitakununulia, sawa?"

kifupi. Kijana yule alionekana kumganda kama jojo iliyong’ang’ania kwenye nguo

ambayo ilikuwa vigumu kuiondoa. Mara tu Lisa alipotoka nje ya jengo hilo, aliona mtu aliyemfahamu vizuri akiwa amesimama kwenye mraba. Alijawa na mchanganyiko wa mshangao na furaha. Taa za rangi mbalimbali ziliwaka

polepole usiku. Alvin, ambaye alisimama kando ya geti kuu, alikuwa

amevalia suti nyeusi na koti la rangi ya parachichi kana kwamba alikuwa

ametoka kushiriki katika Wiki ya Mitindo ya Paris. Alionekana mtanashati sana, na sura yake ilikuwa ya kuvutia kweli.

Hata hivyo, macho yake meusi

yaliangaza kwa huzuni dakika moja

alipomwona mtu aliyemfuata Lisa kwa nyuma.

hakugundua mawazo ya Alvin.

Alimkimbilia na kuzungusha mikono

yake kwenye kiuno chake kwa furaha.

"Hapana Asante. Sihitaji.” Lisa alijibu
"Alvlisa, kwa nini uko hapa?" Lisa

Unyogovu ndani ya macho yake

ulipungua polepole. Alimwangalia yule kijana kwa macho mabaya. "Inaonekana nilikuja kwa wakati mbaya, ona sasa nimevuruga miadi yako."

"Yeye ni nani, Lisa?" Yule kijana naye alikasirishwa na Alvin. Huku wote wawili

wakiwa wamevalia kifahari, jinsi Alvin

alivyokuwa na umbo bora na maridadi

ilimfanya yule kijana aonekane mtu wa chini sana.

Alvin alikaa kimya. Aliinua uso wake

huku akimwangalia Lisa, akiwaza ni namna gani atamtambulisha kwa mwanaume huyo.

“Ni mpenzi wangu,” Lisa alijibu moja kwa moja. "Ninajua nia ya babu yako,

Mzee Amiri Gumbo, lakini tayari

ninampenda mtu mwingine. Tafadhali

pia mwambie babu yako kuwa nina

shughuli nyingi hivyo asitume tena

vijana wake kuja kunisumbua. Sina

wakati wa kukaa kuongea na vijana

wadogo kama nyinyi."

Hakutaka kukata tamaa, yule kijana

mjukuu wa Mzee Amiri alisema, “Wewe ni mjanja. Afadhali ufikirie kwa busara.

Ukiolewa na familia ya mkurugenzi katika kampuni, itatusaidia sote wawili.

Kwa maoni yangu, mpenzi wako hana kitu kingine isipokuwa sura ya mauzo tu.

Yeye si mpenzi mzuri kwako.”

Uso wa Alvin ukaingia giza huku mikono

ya Shani ikianza kumuwasha na kuchezacheza kwa nguvu, akisubiri tu

ruhusa ya bosi wake ili agawe kichapo.

Shani alimtazama kijana yule kana

kwamba ni mtu wa ajabu sana.

“Asante kwa ushauri wako, lakini ndiye

ninayempenda. Nimeanguka katika

kumpenda bila matumaini, na ndiye

anayestahili upendo wangu. Tafadhali ondoka sasa hivi.” Lisa alimfukuza kwa

namna ya kudharirisha sana.

"Kwa kweli hujui ni nini kinachokufaa."

Kijana yule alimkodolea macho Lisa

kabla hajaondoka kwa kukata tamaa.

Lisa akashusha pumzi. Aligeuza kichwa

chake na kukutana na macho ya Alvin yaliyochangamka. Alishtuka kwa

kufikiria maneno ambayo alikuwa ametoka kusema yangekuwa yamemuudhi. “Nilitaka tu asiendelee kunisumbua. Usielewe vibaya…”

“Kwani umekosea nini?” Alvin aligeuka ghafla. Akayakazia macho yake huku

akitoa tabasamu la busara. “Ina maana unanipenda bila matumaini?”

“Tatizo lenu wanasheria kila kitu lazima mtafsiri.” Lisa akacheka.

“Hili lipo wazi wala halihitaji tafsiri, kwamba unanipenda tu lakini huna matumaini yoyote na mimi, sivyo?” Alvin alidadavua na kumchosha kabisa Lisa.

Lisa akakosa la kusema.

Ukimya wake ukamfanya Alvin

atabasamu. "Ingia kwenye gari."

Lisa alimwambia Shani aondoke na gari

lake kisha yeye akaingia kwenye gari la

Alvin. Gari ilisafiri hadi barabara kuu na

ili kuondoa upweke, Lisa alijaribu

kuanzisha mazungumzo mengine. "Umekula?"

Tumbo la Alvin lilinguruma hata kabla

hajajibu. Baada ya kimya cha sekunde mbili, Lisa alicheka. "Ni saa kumi na mbili tu sasa hivi. Mbona tayari una njaa? Hukula chakula cha mchana?”

“Chakula cha ofisini hakikuwa na ladha nzuri,” Alvin alisema kwa hasira, “Ni muda mrefu umepita tangu unipikie. Unafikiri kwamba kuvunjika kwa

mkataba ndiyo mwisho wa makubaliano? Kumbuka bado sisi ni wanandoa.”

"Nina mengi kwenye kichwa changu sasa hivi." Lisa alihisi kuchoka kabisa.

“Nitatayarisha kifungua kinywa ili uende nacho ofisini kila asubuhi, sawa?”

"Unanichukulia kama mwanafunzi?"

Alvin alimkazia macho. Sekunde chache

baadaye, aliongeza, "Sawa basi, utakavyopenda mwenyewe." Lisa alikosa la kusema.

Ni mabadiliko ya haraka kama nini

katika maisha ya Lisa ndiyo yaliyomnyima raha Alvin. Tangu aanze

kufanya kazi huko Mawenzi

Investiments, hakuwahi kumwandalia

chakula kitamu kama zamani, Alvin ali’miss sana mapishi yake.

“Nisikilize. Tukifika nyumbani usiku huu, ninataka kula nyama ya choma ya

nguruwe, saladi ya…”

Lisa alimshika mkono na kupiga kelele

za furaha kabla hajamaliza sentensi yake. “Tulia…Acha! Wacha nikupeleke

tukale vyakula vya uswahilini usiku wa leo. Ghafla natamani miguu ya kuku, shingo, vichwa, firigisi na vipapatio vya kuku vilivyokaangwa, mihogo ya

kuangwa na kachumbari...”

“Una kichaa? Unawezaje kunilazimisha kula takataka za aina hii?" Alvin

alishtuka na kukasirika sana hata ndita

zake zilikuwa zimejikunja.

“Umekosea kusema hivyo. Watu wengi

wanaishi kwa kula aina hii ya chakula,

sawa? Weka vizuri kauli zako. Hata

kama hupendi lakini mimi nina hamu ya firigisi za kuku zilizokaangwa. Kama

mume wangu ni wajibu wako

kunisikiliza, haya ndiyo makubaliano yetu mapya!”

Lisa aliendelea kukuna mikono yake.

Wakati mkataba ulipovunjika na makubaliano mapya yalipoanza

kutumika, msimamo wao katika

uhusiano haukuwa kama zamani na

ilimbidi Alvin amsikilize. Sasa, angeweza kufanya chochote alichotaka

na kula chochote alichotamani na roho yake.

Alvin hakuwa na la kufanya zaidi ya kuendesha gari hadi Coco Beach na kuegesha kando ya barabara. Wawili

hao waliingia kwenye vibanda vya

wakaanga nyama za kuku pamoja.

Sura ya 117

Msongamano wa wateja wengi

waliokuwa wakiingia na kuondoka pale

Coco Beach pamoja na harufu ya

nyama vilimyima kabisa amani Alvin.

Alikosa raha hadi akakunja uso.

“Nenda ukachukue kiti. Chukua kiti hicho kiko wazi..." Lisa alimwambia

Alvin aliyekuwa amesimama tu akishangaashangaa. Lisa alionekana

kutokuwa mgeni sana kwenye mazingira kama hayo.

Lisa alinyoosha kidole kuwelekeza Alvin kwenye meza tupu ambayo ndo kwanza

mteja alikuwa ametoka. Takataka za mabaki zilizokuwa mezani hazikuwa

hata zimesafishwa.

"Sitakaa hapo mimi." Alvin alimpiga Lisa

jicho kali. Lisa akamfuata na kumsisitiza. Maneno ya Lisa ya

kubembeleza yalimfanya Alvin akose la kusema. Kwa hayo, akasogea pale na

kuketi kwa kusitasita.

Dakika kumi baadaye, Lisa aliandaa mlo

kamili wa familia, ambao ulijumuisha

firigisi na kila sehemu ya kiungo cha

kuku vikiwa vimekaangwa, mihogo ya kukaangwa, kachumbari na aiskrimu.

“Kula hii firigisi ya kuku, ni tamu.” Lisa alinyakua kipande na kumlisha kwa shauku. Alvin akakwepesha na kusukuma mkono wake pembeni.

"Ngoja nikuonyeshe kitu." Alvin akatoa simu yake na kusogeza hadi kwenye ukurasa unaoonyesha habari mbaya kuhusu nyama za kukaangwa hovyo mitaani. Kisha, akampitishia Lisa.

Baada ya kuangaza macho kwenye

picha mbaya ya sahani ambayo ilikuwa na vipande vichache vya vipapatio na zaidi ya miguu kumi ya kuku, Lisa alijawa na karaha. "Alvin, huwezi kupata

madhara kwa kula chakula hiki mara moja tu."

"Vitu vya aina hii vina kiasi kikubwa cha

viambato vya sumu. Baada ya leo,

huruhusiwi kula aina hii ya chakula tena. Wewe hata si mtoto.” Alvin alidhamiria.

Lisa hakuweza kuwa na wasiwasi juu

yake. Aliinamisha kichwa chini na kupiga msosi kisawasawa. Baada ya kula vipande kadhaa, aligundua kuwa vingine vilikuwa na ladha mbaya, na badala yake akaviingiza kinywani mwa Alvin.

Huku mdomo wake ukiwa umejaa chakula ghafla, Alvin alimtupia jicho la hasira. Lisa alijifanya kuwa mwadilifu.

“Si wapenzi wa kiume hutakiwa kula

chochote ambacho wasichana wao huwalisha? Angalia wanandoa kando yetu. Ndivyo wanavyofanya pia.”

Wapenzi vijana walioketi kando yao

walikuwa wanafunzi wa chuo kikuu.

Baada ya msichana kukerwa kidogo na kipande cha nyama alichokuwa

anatafuna mdomoni, alimpa mpenzi

wake. “Haina ladha nzuri. Unaweza kula?”

Mpenzi wake naye akajibu, "Unafikiri

naweza kusema hapana?"

Lisa naye alikoroma kwa wivu. “Kwanini

hutaki kula firigisi niliyoiuma, unanionea kinyaa, huh? Kumbe hunipendi?” Alvin

alishindwa cha kusema.

Lisa aliyekaa mkabala naye alikunja uso

huku akimwangalia. “Jinsi ninavyowatamani. Ninapenda kuwa

kwenye uhusiano kama huo."

"Nyamaza." Huku akifungua mdomo, Alvin alichukua kipande cha kuku

kilichobaki mkononi mwake na kukiuma.

Kwa wakati huo, Alvin bado hakuweza

kumwelewa Lisa hata kidogo. Alikuwa

akimtii, lakini kwa nini kulikuwa na

badiliko kubwa hivyo ndani yake sasa?

Baada ya hapo, walimaliza kula firigisi

zote za kukaanga, na hata ice cream

iliyobaki. Hawakutambua kuwa kuna

mtu alikuwa amewapiga picha kwa siri

na kuiweka kwenye group whatsapp la

kikundi cha wanasheria wenzake na

Alvin.

Sam alikuwa akipata nyama choma

katika mgahawa mmoja wa kisasa alipoona picha hiyo. Karibu apaliwe na minofu ya nyama. Haraka alisevu picha hiyo na kuisambaza kwenye makundi mengine aliyokuwa na marafiki zake.

Chester: [ Macho yangu yananidanganya? Alvin angewezaje kuingia Coco Beach?]

Rodney: [Damn! Sijawahi kuona

Alvin akila firigisi za kukaangwa uswazi.

Huyu ni Alvin kweli? ]

Sam: [Nooooo. Hii ni kweli.

Mwanasheria mwenzetu kutoka

kampuni yetu alimpeleka binti yake

huko Coco beach na kumwona Alvin

akila vipande vya nyama ya kuku wa kukaangwa kwa furaha pamoja na Lisa.]

Chester: [ Hiyo ni mbaya

sana, si hadhi ya Alvin. Utakaporudi,

nitakupokea kwa mlo wa hali ya juu wa Kijapani.]

Rodney: [Nakubali. Rudi haraka, Alvin.

Nitamwomba mmoja wa wapishi wakuu Kenya akuhudumie.]

Sam: [ Nathubutu kuweka dau la milioni tano kwamba Alvin hawezi

kuhangaika kuhusu nyinyi. Nina hakika hatajali kula hata Losholi la kimasai ama

kichuri cha kikurya mradi tu Lisa yuko karibu naye.]

Ni pale tu Alvin alipotoka kwenye eneo la ufukwe huo ndipo alipogundua fujo

zilizokuwa zikiendelea kwenye group

hilo la whatsapp. Alifadhaika sana na kujawa na hasira.

Baada ya kuingia kwenye gari, Lisa

alimsogelea na kumbusu mdomoni.

Macho yake meusi angavu yaliwasilisha

hisia za furaha na mahaba. “Asante, Alvilisa. Nimefurahia sana chakula cha

jioni ya leo."

Alvin hakuonekana kufurahia kabisa.

"Kwa hiyo unajaribu kunifanya nisahau

kuhusu jambo hili kwa njia hii, huh?

Unajua kuwa hii ni mara yangu ya kwanza kuingia Coco Beach usiku wa leo na kula chakula cha ajabu?”

Lisa alihisi kuwa Alvin alikuwa

anajifanya tu kuchukia. Wakati

mwingine, wanawake hutawala kwa

urahisi tu. Mara baada ya kugundua

kuwa Alvin alifurahia kitu alichomfanyia, alimwongezea dozi ili kumlainisha

kabisa. Aliuma mdomo wake wa waridi, kisha, akaweka mikono yake shingoni mwake na ulimi uliojaa mate na akambusu tena.

Safari hii, Alvin alimshika kichwa na kumpiga busu refu. Alipoanza kuvuta

pumzi za uchovu ndipo alipomwacha

apumue.

Sura ya 118

Katika hoteli moja ya kifahari, Stephen

Kileo na dada yake Janet walikuwa wakimfanyia mapokezi ya heshima mtu

mmoja maarufu aliyeketi katikati ya kochi. Mtu huyo alikuwa ni Willie Kimaro

ambaye alikuwa ametoka Nairobi. Willie na Alvin walikuwa mtu na binamu yake.

Familia ya Kimaro ilikuwa familia ya kifahari sana na utajiri wa kutupwa.

Ilimiliki makampuni mengi hapa

Tanzania na Kenya, yakiwemo ya mawasiliano, Vyombo vya habari, usafirishaji na hata vituo vya mafuta ya

magari. Pia walimiliki hisa kwenye

makampuni mengine makubwa nchini

ikiwemo Mawenzi Investiments. Ni vile tu Alvin hakuwa tayari kujionyesha kwa

watu kama alitokea kwenye familia hiyo

ndiyo maana watu wengi hawakumjua

kiundani. Hata hivyo Kimaro ni jina la

ukoo kwa familia nyingi za kichaga

hivyo ilikuwa rahisi sana kwa Alvin

kuficha uhusiano wake na familia yake.

“Bwana Kimaro, ngoja nikutambulishe kwa mpenzi wangu, Lina.” Stephen Kileo alikuwa ameambatana na Lina.

"Baba yake, ambaye ni mwanahisa mkubwa katika kampuni ya Mawenzi Investiments, amekuletea zawadi usiku wa leo."

Usiku huo, Lina alivaa nguo ndefu ya rangi isiyokolea iliyokazia mikunjo ya mwili wake maridadi. Ingawa hakuwa mrembo kama Lisa, alikuwa

amependeza sana. Familia ya Jones ilichukuliwa kuwa mojawapo ya familia

za juu zilizo na ‘mbegu’ nzuri. Alikuwa amejipodoa ipasavyo usiku huo.

Alipotabasamu kwa upole, hakika alionekana kama malaika aliyeshuka

duniani kwa bahati mbaya.

Macho ya Willie Kimaro yaliangaza kwa

hisia. Lina alikuwa na mawenge sana

na wanaume matajiri. Ikiwa angeweza

kumvutia kimapenzi mwanamume yule

kutoka familia maarufu ya Kimaro,

asingekuwa na muda na watu kama

Stephen Kileo tena. Lina alimfuata kwa tabasamu la kichokozi. “Willie, familia yangu ingependa kukupa zawadi hili. Mkufu wa dhahabu wenye kidani cha jiwe la thamani la Tanzanite kutoka Mererani, umenakshiwa na sonara maarufu hapa jijini, Enjipai Jewellery."

Alipomaliza tu kuongea, alifungua boksi. Macho ya Willie yakaangaza. “Woooh!

Kidani hiki kina thamani ya mamilioni ya pesa, sivyo?”

“Sio muhimu sana, ilimradi tu unaipenda," Lina alijibu huku akijaribu kumfurahisha.

“Hahaah! Kwa kweli sikutegemea.

Nakupenda sana wewe!” Willie alisugua

kidani kwenye sehemu ya juu ya pua yake. Haikujulikana kama alimaanisha kuwa anampenda Lina au kidani.

Ghafla, kimya kikatanda kwenye

chumba kile cha kifahari cha Hoteli maarufu. Macho ya kila mtu yalikuwa

kwa Willie. Stephen alitabasamu kwa

utulivu, na mara akanyanyuka yeye na Janet wakatoka nje. Kisha Lina alikaa na Willie kwa muda wote wa usiku.

Aliimba na kuzungumza naye. Kwa vile

alikuwa mzuri katika kukonga nyoyo za wanaume, mara alimfanya Willie acheke kimoyomoyo.

Baadaye Lina alielekea mapokezi mara moja. Dakika alipotoka nje ya kaunta, alimuona Stephen akisubiri nje.

“Asante kwa usiku wa leo, Stephen.

Natumai Willie anaweza kuisaidia

familia yangu kurejesha nafasi ya mwenyekiti wa Mawenzi Investiments.”

Lina alitabasamu huku akizungusha mkono wake kiunoni kwa Stephen.

"Natumai atasaidia." Stephen

alitabasamu bila huruma. “Kwa hiyo

Willie na wewe—”

Lina akamkatisha mara moja, “Usinielewe vibaya. Unajua kuwa wewe bado ndiye ninayekupenda. Sasa hivi, Kimaro bado nina maongezi naye—”

“Ninaelewa. Sina wazo lolote baya

kuhusu hilo.” Stephen alimpiga piga nyuma ya mkono wake. "Ni wakati tu familia yako itakaporejesha kiti chake cha uenyekiti wa kampuni ya Mawenzi ndipo familia zetu zote mbili zinaweza kufanya maendeleo zaidi na kufikia mambo bora zaidi."

"Ni vizuri umeelewa." Lina hakuwa

akimfikiria kabisa Stephen moyoni mwake tena baada ya kuona Willie amekaa mkao wa kueleweka.

"Kilicho muhimu zaidi kwa sasa ni kumfurahisha Willie Kimaro." Stephen alipitisha vidole vyake kwenye nywele zake. “Nitakusubiri.”

“Asante.” Lina alijibu kisha akarudi na keti kando ya Willie tena. Wakati huo, Willie aliweka mkono wake kiunoni mwake na kuanza kumpapasa kama alivyotaka.

Saa tano usiku, Willie alikuwa amelewa.

Stephen alimuomba Lina ampeleke

chumbani akapumzike.

Sura ya 119

Baada ya Lina na Willie kuondoka, Janet alimwambia Stephen kwa

mshtuko, “Umerukwa na akili, Lina si mpenzi wako? Kwa nini

hukunitambulisha mimi kwa Willie? Bila

shaka ningeifaidisha familia yetu ikiwa

ningekuwa binti-mkwe wa familia ya Kimaro.”

“Willie hakuvutiwa nawe,” Stephen alijibu kwa dharau huku akiwasha sigara.

Janet alipandwa na hasira.

"Unamaanisha nini? Machoni pako, mimi si mrembo kama Lina, huh?

Kwanza mimi sikukulia kijijini kama yeye—”

“Ninafanya hivi kwa faida yako.”

Stephen akamkatisha. “Willie ana tabia

chafu ya kulala na wanawake hovyo, hajali hata kama ni mpenzi au mke wa mtu.”

Janet alipigwa na butwaa. Stephen

aliongeza, “Wewe ni dada yangu wa damu. Ikiwa kuna njia rahisi ya

mafanikio makubwa, bila shaka

ningekupendelea wewe kwanza. Hata hivyo, Willie ni mhuni na malaya sana. Amewahi hata kuua mwanamke.”

"Una uhakika?" Janet akatetemeka.

“Ni kweli kabisa. Isingekuwa jamaa yetu

ambaye anafanya kazi kama msaidizi wake, nisingelijua hilo.” Stephen

alisimama taratibu na kusimama.

“Vinginevyo, kwa nini unadhani nilimpa

Lina nafasi kubwa namna hii? Yeye hana heshima pia.”

Stepehen alitulia kidogo kisha

akaongeza tena, “Lakini usijali. Willie

atashukuru kwamba nilimpa nafasi ya kuwa karibu na Lina. Katika hali hiyo, nitapata fursa ya kuwa rafiki wake wa karibu. Nitatumia nafasi hiyo kuinufaisha

familia yetu kibiashara.” Mara Janet akaridhika.

Asubuhi iliyofuata Lina aliporejewa na fahamu, alishtuka baada ya kumuona

mwanaume aliyekuwa pembeni yake

ambaye alikuwa akimtumbulia macho. Huku kila kitu kilichotokea jana yake

usiku kikimulika akilini mwake, alihisi kana kwamba alikuwa ameenda kuzimu

kwa mara nyingine tena. Mtu huyo

alikuwa anatisha, kwa kweli. Kifupi

alikuwa mnyanyasaji. Wakati huo, Lina

alikuwa ameumizwa vibaya sana

kutokana na kuingiliwa kinyama

kinyume na maumbile.

“Umeamka?” Willie alipogeuza kichwa chake na kumwangalia Lina, mtetemeko ulimtawala mwili mzima.

“Umenifanyaje hivi?” Lina aliuliza

kinyonge huku akishika sehemu zake

zilizokuwa zinawaka kwa maumivu.

“Kwanini? Hujaridhika na mimi?" Willie

aliwasha sigara, macho yake yakimeta

kwa chuki.

"Hapana." Lina alilazimisha tabasamu.

Kwa kuwa alikuwa ameyataka

mwenyewe kulala naye, alifikiri kwamba

haikuwa na maana tena kujutia yaliyomkuta. Aliuma meno na kujifanya

kuwa na haya. Aliongeza, "Ni furaha yangu kuweza kulala na wewe, Mpenzi

Kimaro."

'Ni vizuri kwamba umefurahia. Kwa

kweli wewe mtoto ni mtamu sana.”

Willie alivuta sigara, akimwangalia Lina

kwa udadisi. "Ilikuwa mara yako ya kwanza kufanya jana usiku?"

Lina alipigwa na butwaa. Alikumbuka

kwamba alikuwa amefanyiwa upasuaji

wa plastiki kurudisha bikra yake

kimakusudi ili kumfurahisha Stephen

endapo kama wangekutana kabla ya hapo. Hakutarajia kwamba angelala

ghafla na Willie jana yake usiku.

Inavyonekana, Willie hakuelewa jambo hilo.

“Ndiyo-Ndiyo.”

"Sikutarajia." Willie akamgusa kidevu

chake. "Huogopi kwamba Stephen atachukia?"

"Kama nilivyosema, ni heshima yangu kuweza kulala na wewe kwa usiku kucha nikizingatia hadhi yako nzuri,"

Lina alijibu kwa kujiamini. Aliposikia hivyo, Willie aliangua kicheko.

“Inavutia. Nakupenda sana. Nitakuwa Dar kwa muda, na utanisindikiza katika muda wangu wote hapa.”

“Sawa.” Lina alilazimisha tabasamu.

"Nashangaa ni mradi gani uliokuleta hapa Dar, bila shaka ni mkubwa sana!"

“Oh. Kando na kuhudhuria hafla ya Mawenzi, Kampuni ya teknolojia chini ya familia ya Kimaro ingependa kuwekeza katika sekta ya viwanda.

Nimekuja kutazama fursa.”

Lina aliuliza kwa tahadhari, “Utawekeza kiasi gani?”

"Pengine mamia ya mabilioni ya shilingi.

Hakuna kikomo kwa kiasi, ukomo

utategemeana na fursa

itakayopatikana.” Willie alijibu kwa kawaida.

Roho ya Lina ilimruka. Ikiwa Mawenzi

Investments ingeweza kufanya kazi

kwenye mradi huu, Jones na hadhi yake

ingeinuliwa.

"Mpenzi Kimaro, nadhani ungetaka

kufanya kazi na kampuni ya ndani kwenye mradi mkubwa kama huu..."

"Mawenzi Investments ana nia ya kushiriki katika hilo, huh?" Willie alitoa

tabasamu la nguvu.

“Mpenzi, ningependa kushirikiana nawe kwa ajili ya mradi huu, lakini

nimefukuzwa kutoka kwenye kazi yangu

huko Mawenzi Investments. Baba

yangu pia amenyang’anywa cheo cha uenyekiti wa Kampuni” Akiwa amekata

tamaa, Lina alitoa tabasamu la uchungu. "Baba yangu na mimi wote

tupo hatarini ..."

"Naweza kukutatulia chochote mradi tu ufanye wajibu wako vizuri katika

kuniweka sawa." Tabasamu likaangaza

usoni mwa Willie. "Wanawake wote

wanaonizunguka hawajawahi

kushindwa kupokea thawabu nzuri kutoka kwangu."

"Kwa hali hiyo, hakika nitakutendea vizuri." Kwa dhamira mbaya, alimbusu

kwa hiari yake mwenyewe.

Muda mfupi baadaye, kilio cha Lina

kilisikika kutoka chumbani kwa mara nyingine tena. Willie alimgeuza tena na kuanza kumshughulikia kinyama. Akiwa analia kwa uchungu, alijiwazia, 'Lisa, ninateseka sana sasa kwa ajili yako.

Hakika nitakulipa na riba katika siku zijazo!”

Mwaka ulikuwa unaelekea ukingoni.

Maadhimisho ya kumbukumbu ya

Mawenzi Investments yaliadhimishwa

katika hoteli ya nyota saba.

Sio tu kwamba

Mawenzi Investments

alialika watu mashuhuri wachache kwa

usiku huo, lakini idadi kubwa ya

wafanyabiashara wenye nguvu pia

walikuwa wamejitokeza.

•••

Ilikuwa ni saa moja kamili jioni ambapo

Lisa akiwa ni mwenyekiti aliyeteuliwa hivi karibuni, aliwasili katika hoteli hiyo.

Lisa aliendesha polepole hadi hotelini kwa gari aina ya Range Rover.

Mlango wa gari ulipofunguliwa, alionekana akiwa amevalia gauni refu

jeusi la mtindo wa zamani na akiwa

ameshikilia mkoba wa zamani

uliopambwa. Kwa kawaida si rahisi

kuwa kivutio cha watu kwa mtu aliyevaa

nguo nyeusi. Hata hivyo, Lisa alibaki

mrembo na mzuri akiwa na uso wake

mwanana na wa kuvutia na mdomo

uliokolea lipstick nyekundu iliyofanana na waridi linalochanua.

Waandishi wa habari walianza

kuchukua kamera zao ili kupiga picha

zake. Kwa wadhifa wake na

utambulisho wake, angeweza

kuchukuliwa kuwa C.E.O mwanamke

mwenye umri mdogo na mrembo zaidi

jijini Dar es Salaam. Lisa akapiga pozi

kwa ajili ya picha, lakini muda mfupi

baadaye, kelele za ghafla zikasikika

kando yake kutoka kwa waandishi wa habari.

“Fanya haraka utazame! Je, hili si toleo la pekee la Bugatti Veyron L'Or Blanc?"

“Nilisikia limetengenezwa kwa chuma cha titanium. Linagharimu zaidi ya Shilingi milioni mia saba!"

“Angalia namba ya usajili, ni private number. KIMARO! Inashangaza.”

“Kweli inashangaza. Ni nani huyo? Yuko

hapa kuhudhuria sherehe ya ukumbusho wa Mawenzi Investments?”

“Tazama! Mlango unafunguliwa.”

Akiwa amezungukwa na sauti za watazamaji, mwanaume mmoja aliyevalia suti ya bluu iliyokolea alitoka

kwenye kiti cha dereva. Sifa zake

zilitamkwa, na tabasamu la kishetani lilionekana usoni mwake.

Kulikuwa na vifijo kutoka kwa waandishi wa habari katika umati huo.

"Yeye ni mzuri sana!"

“Namfahamu yeye ni nani. Yeye ni Willie kutoka familia ya Kimaro."

"Familia ya Kimaro? Familia yenye

utajiri zaidi hapa Tanzania?”

“Ndiyo. Ni hiyo familia ya Kimaro!

Wanakaaga Nairobi.”

"Mungu wangu. Mawenzi Investments

wana uhusiano na familia ya Kimaro?”

Katikati ya majadiliano ya umma, mlango wa abiria ulifunguliwa. Akiwa amevalia gauni jekundu, Lina alitoka nje

ya gari kwa kuvutia huku akiushika mkono wa Willie. Sauti ikazidi kuvuma

tena kutoka kwa umati.

“Huyu ni nani?”

"Lina, binti ya Jones Masawe ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa bodi ya Mawenzi Investments."

“Kwa hiyo yuko kwenye uhusiano na Willie. Anajaribu kugeuka kutoka kuwa

mkulima hadi kuwa binti wa kifalme, huh?

"Kwa kuwa sasa ana uhusiano na

familia ya Kimaro, familia ya Harrison na

familia ya Zongo sasa watamheshimu Jones."

Maneno hayo yalimfanya Lina azidi

kuridhika. Ilifaa kujipendekeza na Willie kama mtumwa kwa siku chache ili apate

taji la utukufu na heshima siku za baadaye. Alipogeuza macho yake, alitokea kumwona Lisa aliyekuwa mbele yake akiwa anamshangaa bila ukomo.

Akiwa amekunja midomo ya waridi, Lina alimshika Willie mara moja na kuelekea kwa Lisa. "Halo, Lisa. Willie, huyu ni dada yangu, ambaye pia ni Mwenyekiti na CEO wa Mawenzi Investments.”

Sura ya 120

Baada ya kumwona Lisa mapema, Willie alimtazama kwa shauku. Hakujua

kamwe kuwa Lisa aliyekuwa amemsikia

mapema alikuwa mwanamke mwenye

sura nzuri kama hiyo. Uzuri wake

ulionekana kuwa wa aina yake miongoni

mwa mamia ya wanawake aliokuwa

amekutana nao.

"Halo, Bi Jones." Willie alinyoosha

mkono wake kwa kumpa salamu. Lisa

pia alishangaa kwamba Lina aliwezaje

kupata ushirikiano na mtu kutoka kwa

familia ya Kimaro. Lisa hakuwa na la

kufanya zaidi ya kunyoosha mkono

wake bila kupenda, akijua kuwa hawezi

kukataa salamu yake bila sababu.

Nani alijua baada ya Willie kumshika

mkono, alichora miduara kwenye

kiganja chake kwa utani kwa kutumia

kidole chake kidogo na kumchoma

kichokozi Lisa. Mabadiliko kidogo

yalionekana katika uso wa Lisa. Alijaribu

kujinasua kutoka kwa mguso wake,

lakini kwa makusudi Willie alimshika

kwa nguvu na kumzuia.

"Bi Jones, unataka kunishika mkono

wangu hadi lini?" Willie alitabasamu kwa

ujanja.

Lina mara moja akainua mdomo wake

na kusema, "Unafanya nini, Lisa?" Hapo

hapo Lina akamvaa Lisa na

kumwanzishia varangati, akidhani kwamba Lisa alijaribu kumchombeza Willie.

Waandishi wa habari waliosimama

kwenye ukingo wa zulia jekundu walichukua picha za watatu hao mara moja. Pamoja na dada wawili kutoka kwa familia ya Jones wakipigana juu ya mtu maarufu wa familia ya Kimaro, lilikuwa tukio ambao lingetengeneza kipande cha habari nzuri.

“Kwanini hukumuuliza alichonifanyia pia?" Akiwa na tabia ya utulivu, Lisa hakuwa na jeuri wala kujidharau. “Hivi nyie mnafikiri kwamba mimi kama mtu anayesimamia Mawenzi ningemtongoza mpenzi wa binamu yangu bila aibu?

Samahani, hata hivyo si mpenzi wako.

Ninavyokumbuka, Stephen ndiye mpenzi wako, sivyo?”

Waandishi wa habari walianza

kushangaa. “Kweli? Stephen ni mpenzi

wa Lina kweli, lakini kwa nini alikuja na Willie leo?”

“Sasa kwa kuwa alikutana na Willie, inawezekana kwamba anajaribu kumtosa Stephen?”

“Hilo linawezekana. Hapo awali alikuwa mchumba wa Ethan, lakini Ethan alipokabiliwa na wakati mgumu, mara moja alimbwaga kwa kushutuma za usaliti.”

“Ni fedheha iliyoje! Willie anavutiwaje na mwanamke wa aina hii?"

Uso wa Lina ulikuwa mweupe kama

karatasi wakati huo. Willie hakutambua

kwamba Lina alihusishwa na habari

nyingi mbaya. Aliishia kujiingiza kwenye matatizo.

Bila bughudha, Lisa alijiondoa kwa

nguvu kutoka kwa Willie na kugeuza

mkono wake kwa maumivu. "Ulinibana

mkono wangu kwa nguvu sana hadi

unauma, Bwana Kimaro."

Mkono wake, ambao hapo awali ulikuwa

wa kawaida, ulikuwa mwekundu wakati

huo. Waandishi wa habari waliposogea karibu, waliweza kuiona ngozi yake nyekundu vizuri. Macho ya Willie yakaangaza kwa dharau mara moja.

Hawakutarajia mtu kutoka kwa familia ya Kimaro angekosa haya. Siku zote Willie alikuwa mtu wa kupenda kunyenyekewa na wengine.

Ilikuwa ni mara yake ya kwanza

kudhalilishwa na mwanamke hadharani.

Macho yake yalionyesha uhasama, lakini alitabasamu kwa unyonge.

"Samahani kwa kukuumiza bahati mbaya." Akamsogelea Lisa hadi karibu na kumnong’oneza, “Utanijua mimi ni nani, Lisa.”

Alipomaliza tu kuongea, aliingia moja kwa moja ndani ya hoteli hiyo. Na Lina

alimfuata haraka. Lisa alipoutazama mgongo wa Willie, alihisi kana kwamba

alikuwa amelengwa na nyoka mwenye sumu kali. Alikuwa na hasira ya kuzama.

Willie alipanda lifti uso wake ulikuwa na hali ya huzuni. Akiwa ameingiwa na mawazo ya wasiwasi, Lina alisema kwa

utulivu, “mpenzi, natumai hautajali kuhusu hilo. Lisa anajidai na anajigamba kwa kuwa yeye ndiye mwenyekiti wa kampuni na kufanya mambo yasiyo ya kiungwana.”

“Yeye ni nani wa kufanya hivyo? Yeye ni mwenyekiti tu wa kampuni, kufumba na kufumbua anaweza kukuta kiti hicho

kina mtu mwingine.” Willie alikuwa akifuka kwa hasira.

"Kwa kweli, yeye si kitu ikilinganishwa na wewe. Labda ni kwa sababu ana

mpenzi mwenye nguvu, na yeye ni mwaminifu sana kwake.” Baada ya

kukaa siku chache na Willie, Lina alijua

kuwa Willie alipenda sana kusifiwa.

Kwa hakika, macho ya Willie

yalionyesha kupendezwa kwake dakika tu aliposikia hivyo. Alipenda sana

wanawake ambao muda wote walikuwa

wakimsifia, kumbembeleza na kumpetipeti. Zaidi ya hayo, ukizingatia jinsi Lisa alivyokuwa mkali muda si mrefu, alifanana na waridi lenye miiba na alionekana mrembo zaidi kuliko Lina.

Alipoona hali ya kuvutia machoni pake, Lina alitabasamu na kusema, “Ninaweza kumfanya alale nawe kama utapenda.” Lina alisema bila aibu. Kwa

kuwa amekuwa akidhalilishwa na Willie kama mbwa kwa muda waliokuwa

pamoja, alitaka Lisa pia aonje adha hiyo.

"Wewe ni mwanamke mbaya sana."

Willie alimpiga jicho la mshangao.

"Furaha yako ndiyo muhimu kwangu.

Hutaki kumfundisha somo?” Lina aliuliza

kwa kupendeza.

Willie aliinua macho yake. Aliwasha

sigara kisha akasema kwa uovu, “Wale

walionidhalilisha wote waliishia katika

hali mbaya sana. Lisa pia anastahili kujuta!”

•••

Sherehe kuu ya kumbukumbu ya

kampuni ya Mawenzi ilianza rasmi. Lisa

alipaswa kuwa kivutio cha tukio hilo,

hata hivyo, wageni wote walimzunguka

Willie, Jones, na Lina badala yake.

Kwa macho ya wengi, familia ya Kimaro

ilionekana kuwa ya hadhi ya kipekee.

Ingawa Willie hakuwa mzao wa moja

kwa moja wa Kimaro, uwepo wake jijini

Dar es Salaam ulikuwa na nguvu ya

kutosha kupata heshima kutoka familia

kubwa za kitajiri.

Chris Maganga akajongea kuelekea

kwa Lisa na kumuuliza. "Jones Masawe

aliwezaje kujenga uhusiano na Willie

Kimaro?"

"Nadhani Lina alilala naye." Lisa

alifanya dhana ya kuridhisha. Tayari

aliweza kuona tabia mbaya ya Willie

kupitia tukio fupi alilokutana nalo

mlangoni wakati wanaingia.

Sura ya dharau iliosha usoni mwa Chris.

“Babu na bibi zako walikuwa na sifa ya

uungwana na uadilifu, hii tabia chafu

yenye aibu ameitoa wapi dada yako?”

“Ni kwaida yake kujua ndani ya kila

suruali ya mwaname aliyefanikiwa kuna mdudu gani.” Lisa kichwa kilimuuma.

Hapo awali, alikuwa na uwezekano mkubwa wa kumvutia kila mtu, lakini

mwonekano wa Willie ulimfunika kabisa. Willie alikuwa amevutia umakini wa

wasanii, waalikwa, wakurugenzi wa kampuni na wasimamizi wakuu.

Kwa wakati huo, wakurugenzi wawili wa bodi ya kampuni ya Mawenzi, Amiri

Gumbo na Mzee Levy walimwendea na kumwambia. "Lisa, ulipaswa kuwa wa

kwanza kutoa hotuba kwenye jukwaa

usiku wa leo. Lakini baada ya

kujadiliana na wakurugenzi wengine, tuliamua kumwacha Bwana Kimaro

aanze kwanza, akifuatiwa na Jones

kisha—”

“Nyie watu ni wazima kweli?” Chris

alipandwa na hasira. “Bwana Kimaro

hata hajui kinachoendelea katika

kampuni yetu, wao huja kuchukua faida

tu. Unahitaji kujua kuwa usiku wa leo ni sherehe ya kumbukumbu ya Mawenzi

Investments. Pia, kwa nini Jones

anapanda jukwaani kabla ya mwenyekiti? Hii haina maana.”

Mkurugenzi Amiri alijibu kwa aibu,

“Angalia Bwana Kimaro ni nani. Ukweli

kwamba amejitokeza kwenye sherehe

ya ukumbusho wa Mawenzi

Investments unaonyesha kwamba

anatufikiria sana. Zaidi ya hayo, yuko

tayari kupanda jukwaani kutoa hotuba,

ambayo ni heshima yetu kubwa. Bei ya hisa za kampuni yetu itaongezeka

kesho. Kuhusu Jones, ni Bwana Kimaro

ambaye alimwomba azungumze. Ana

uhusiano wa karibu naye. Huwezi

kunilaumu kwa hili.”

Uso wa Lisa ulibadilika kidogo.

“Itakuwaje kama sikubaliani?”

"Hapana," Mkurugenzi Levy alijibu kwa

njia ya moja kwa moja, "Sote tulifikia

uamuzi huu kwa ajili ya kampuni.

Lazima ukubaliane nao.”

Lisa alicheka. "Ikiwa Willie ataamua

kumpendekeza Jones kuwa mwenyekiti, nyinyi pia mtakubaliana naye? Je! ni

Sheryl au Kimaro ambaye alianzisha

Mawenzi Investments?"

"Tunafanya hivi kwa ajili ya matarajio ya kampuni," Mkurugenzi Levy alisema

kwa kukerwa, "Kwa kuzingatia hali ya familia ya Kimaro, utajiri wa familia yao

una thamani ya mamia ya mabilioni ya shilingi.” Mkurugenzi Amiri alikubali kwa

kichwa pia.

Saa mbili na nusu usiku, Willie alipanda

jukwaani na kutoa hotuba, akifuatiwa na Jones Masawe…

Sura ya 121

Saa tatu usiku, Lisa alikuwa kwenye

chumba chake cha mapumziko baada ya kumaliza kutoa hotuba yake.

Alisimama kwenye kioo akipaka lipstick

yenye rangi ya hudhurungi kwenye

midomo yake maridadi, huku akitafakari hotuba aliyotoka kuitoa punde.

Lina akaingia ghafla. Akiwa na tabasamu la ufidhuli, alisema, “Pengine hukutarajia kwamba hivi karibuni ungeweza kupoteza nafasi yako ya uenyekiti ambayo ndiyo umeipata hivi punde, sivyo?”

"Wewe bado hujabadilika kabisa Lina."

Lisa aligeuza kichwa chake na kukutana na macho ya Lina. “Kwanza, ilikuwa

Ethan, ikifuatiwa na Stephen na sasa

Willie. Umelala na wanaume wangapi zaidi kabla ya hawa? Wewe ni zoazoa, cha wote, au chakula cha wageni?”

Kauli fupi kama hiyo iligusa ujasiri wa Lina ghafla na kusababisha damu yake

kuchemka. “unanionea wivu, huh? Sasa

ninakupa nafasi hii pia. Ni heshima

kubwa sana kuweza kulala na Willie

Kimaro sivyo? Nadhani utafurahia pia, yupo vizuri kwa bedi.”

Mara tu alipomaliza kuzungumza, Willie

aliingia ndani ya chumba akiwa

amevimba kama mbogo.

"Bwana Kimaro, nitakusaidia kulinda

nje." Lina alifunga mlango wa chumba mara baada ya kusema hayo.

“Unataka kufanya nini?” Lisa alijaribu kukimbia, lakini Willie alimshika mkono.

Kukiwa na mlango kati yao, alisikia sauti ya mlango ukiwa unafungwa.

Wimbi la wasiwasi lilimkumba Lisa.

Shani hakuwemo chumbani wakati huo.

Alimwambia abaki tu nje kwenye

gari kwani hakutarajia tukio kama hilo

kutokea wakati wa hafla ya ndani ya kampuni.

“Niache niende, Kimaro.” Lisa alimuuma

Willie kwa nguvu.

Willie aliachia mkono wake kwa

maumivu kisha akacheka. “Hakika

wewe ni mjanja. Hiyo inavutia. Napenda

wanawake wachangamfu kama wewe.”

“Una kichaa?” Lisa alishangaa, “familia ya Kimaro ni moja ya familia zenye

heshima kubwa. Sikutegemea kama

kuna mtu mwenye kuchukiza na mchafu

kama wewe katika familia yenu, au wewe si mtoto halisi wa familia ya Kimaro?” Lisa alikosoa.

“Endelea kunikosoa. Kadiri

unavyonikosoa, ndivyo nitakavyokuletea taabu zaidi.” Willie alidhihaki.

“Wakurugenzi wa kampuni yako wote wananichukulia kama mheshimiwa.

Jones Masawe ameniomba nimsaidie kupata nafasi ya mwenyekiti kesho.

Ninaweza kusema kitu kwa urahisi na kukufanya upoteze nafasi yako mara

moja. Unajua nina nguvu ya 25% ya hisa za kampuni. Kwa hivyo, nitafikiria upya ikiwa utanihudumia vizuri usiku wa leo.”

Akiwa na mawazo, Lisa alijifanya kuwa na hofu na kusema, “Hii ni kweli?”

“Bila shaka.” Willie alifoka, akijua kuwa

Lisa tayari alikuwa anaingia kwenye

anga zake.

"Lazima unisaidie, Bwana Kimaro," Lisa

alidakia na kusema kwa huruma,

“Vizuri sana kwa kuwa umeelewa. Unajua kilicho bora kwako. Njoo hapa

basi.” Willie alifungua mikono yake. Lisa akajitupa mikononi mwake. Harufu

ya kuburudisha ya mwili wake ilijaza pua yake. Kwake, umbo lake lilikuwa

bora zaidi kuliko la Lina. Moyo wa Willie

ulikuwa unawaka. Alipotaka

kumkumbatia kwa nguvu, alipigwa na nguvu kubwa.

Willie akainama kwa uchungu. Lisa

alikuwa amechukua kalamu ya

chuma kutoka kwenye mkoba wake na

kumchoma nayo Willie kwa nguvu

kwenye mbavu. Kalamu hiyo ilikuwa na

kichwa chembamba kilichopenya

kwenye nyama kama risasi. Willie

aliganda kwa maumivu na hakuweza

kusogea hata kidogo.

Lisa alivua viatu vyake virefu na

kumpiga usoni na mwilini kwa visigino

vikali vya viatu vyake. Alimpiga hadi

chini, na akaishia kuwa kama samaki

"naweza kukufanyia chochote."

aliyetolewa baharini na kuwekwa nchi

kavu, asiweze kusogea hata kidogo.

Baada ya kuona amefanikiwa kumdhibiti

Willie yeye mwenyewe, Lisa hakuwa na haja hata ya kumpigia Shani.

Baada ya kumpiga Willie, Lisa alishtuka

kuona uso wake umevimba. Alifikiria

kwa muda na kugundua kuwa alihitaji

kumfanyia zaidi ya hivyo, na akamvua

nguo zake pia.

“Unataka kufanya nini?” Willie alilalama

kwa uchungu. Siku zote ndiye aliyekuwa

akiwavua nguo wanawake. Yeye

kamwe hakuwahi kufikiri kuwa kuna siku

nguo zake zingekuja kuvuliwa na

mwanamke. Macho wake yalidhihirisha

ukali. Alitamani kumpasuapasua Lisa

lakini hata hivyo hakuwa na nguvu hata

kidogo ya kupinga kwani alipigwa

vibaya viatu vya mbavuni na usoni.

Baada ya kumvua nguo, Lisa alichukua

simu yake na kumpiga picha zaidi ya

kumi kutoka pembe tofauti. Alimtisha

kwa njia ya dharau, “Ikiwa utathubutu

kuniletea matatizo kuhusu kilichotokea leo, nitatupia picha zako hizi chafu

mtandaoni. Hebu tuone kama familia ya Kimaro inajali utu wao.”

“Wewe…” Willie alikasirika. Katika kipindi cha miaka 25 ya maisha yake, hakuna hata mwanamke mmoja aliyekuwa na ujasiri wa kumfanyia hivyo. “Nakuonya! Nitakushughulikia, Lisa."

“Na mimi nitakushughulikia pia.” Lisa alimjibu kwa dharau. “Ni mara yangu ya kwanza kuona mwili mbaya kama huu. Unakera na kuchukiza kama nini!"

Lisa akampa kidole cha kati na kuziitupa nguo na simu ya Willie dirishani. Baada ya hapo, alimburuta hadi chooni na kumfungia humo. Kisha Lisa alitoroka

kupitia dirishani ili kumfanya Lina asielewe chochote.

Willie alilala kwenye sakafu baridi ya choo kile akiwa uchi. Hata baada ya

kutumia muda mrefu kuomba msaada

kwa sauti dhaifu, hakuna mtu aliyekuja kumsaidia. Ni baada ya nusu saa kupita ndipo

alianza kupata nguvu. Alitetemeka huku akinyanyuka na kuufungua mlango kwa nguvu. Baada ya kusikia kelele, Lina alikimbia kwa uangalifu kuelekea kwenye chumba hicho na kufungua mlango.

Pindi alipouona tu uso wa Willie uliojeruhiwa, alipiga kelele kwa mshtuko. “Imekuwaje tena mpenzi…”

“Nyamaza, mpuuzi wewe!” Willie

alimpiga Lina kibao cha usoni na kumpiga mateke machache dhaifu kwa hasira. “Nilikuwa nakuita sasa hivi.

Ulikuwa kiziwi?”

“Usinipige, mimi sikusikia. Niliogopa kukusumbua, na nilikuwa nimesimama mbali sana… Ohoo-hoo!” Lina alipiga magoti na kumsihi. Mwanaume huyo

alitisha sana alipokuwa na Lina, utadhani si yeye aliyekuwa kama panzi

mbele ya Lisa muda mchache uliopita.

Willie alianza kutetemeka tena. Kwa hasira alifoka na kuapa, “Lisa, nikishindwa kukuua, nitakula mavi yangu!”

Sura ya 122

Alvin, ambaye alikuwa na mkutano wa video katika chumba chake cha maktaba, alisikia sauti ya gari kutoka chini. Wakati huo alikuwa anasikiliza mipango mbalimbali ya maendeleo ya miradi yake. "Mpango huu hauwezekani. Njoo na mwingine."

Alipomaliza tu kuongea, alikatisha mkutano na kuelekea chini.

Akiwa katika hali ya kuchanganyikiwa, Lisa akaingia mlangoni. Alisahau hata

kubadili viatu vyake. Alvin alikodoa

macho na kutazama gauni lake refu

jeusi. Alionekana kuvurugwa tofauti na alivyoondoka.

"Potea, wewe huna maana kabisa!"

Akiwa amekunja uso, Alvin alimtupia macho ya mshangao na udadisi Lisa.

Alipoyaelekeza macho yake chini, ghafla aliona ufa kwenye pindo za gauni

lake. “Mbona nguo yako imetatuka?” Macho yake meusi yalikuwa yakimtazama kama mshale.

Alipojitazama tu chini ndipo alipogundua. Labda nguo hiyo ilikuwa

imeshikana na kitu chenye ncha kali

alipotambaa nje ya dirisha kutoka

kwenye chumba kile cha hoteli.

“Nilinasa sehemu kwa bahati mbaya.”

Lisa aligeuza macho yake, hakutaka

ajue kwamba alikuwa amemchokoza

Willie Kimaro. Hata hivyo hakujua

kabisa kama wana uhusiano wa aina

yoyote. Kwa mawazo yake, Alvin

alikuwa wakili tu, na asingekuwa na

uwezo wa kuwa na uhusiano wowote na

familia tajiri ya Kimaro. Alijua ni majina ya ukoo tu ndiyo yamefanana.

"Una tabia mbaya ya kunitazama kila wakati unaposema uwongo." Alvin

alishika kiuno chake chembamba kwa nguvu, macho yake meusi yakionyesha hisia kali ya ukali. “Ulihudhuria sherehe ya ukumbusho usiku wa leo, sivyo?

Nani alikuletea shida?”

“Hakuna aliyenifanya chochote. Haya, nani anaweza kunigusa wakati mimi ni mwenyekiti?” Lisa alimsukuma na kwenda juu. “Naenda kuoga."

"Usinifiche Lisa." Alvin akamvuta

kuelekea kwake tena. “Angalia jinsi ulivyokosa amani kwa sasa. Afadhali

unieleze ukweli kama unanichukulia

kama mume wako.”

Lisa alipiga kelele, na macho yake

yakawa mekundu licha ya yeye

mwenyewe kupenda. “Nimemkosea mtu

ambaye sikupaswa kumkosea katika

ulimwengu mzima wa kibiashara.

Alvlisa, kama… Ikiwa… mtu huyo ananilenga, usithubutu kufikiria

kunisaidia. Afadhali unikane kabisa

kuliko kunisaidia vinginevyo utapoteza

kila kitu. Yeye si sawa na Clark

Zongo…”

Alvin aliinua macho yake na kuuliza.

“Unaamaanisha nani huyo anaweza kunitisha mimi?”

"Willie Kimaro, kutoka familia ya

Kimaro." Lisa alisema huku akihema.

“Biashara zao kubwakubwa

zimetapakaa kwenye ukanda wa Afrika

Mashariki yote, pia wanamiliki asilimia

25 za hisa za Mawenzi.”

Alvin alishindwa cha kusema. Hilo

lilimshangaza sana. Tangu lini Willie, yule bwana mdogo mpuuzi tu, akawa

mtu ambaye kwa hakika anaogopwa

kiasi kile na matajiri wa Dar es Salaam? Ina maana Lisa hakumchukulia

yeye kama mtu mwenye nguvu?

Anyway, halikuwa kosa lake kwa

sababu alimficha utambulisho wake halisi.

“Umeshtuka sana?” Lisa alituliza baada ya kumuona Alvin akiwa kimya sana, hivyo mara moja akamfariji. “Lakini usijali. Kwa bahati nzuri, nilikuwa na kalamu ya chuma kwenye mkoba, alipojaribu kunivamia chumbani

nilimchoma na kalamu kwenye mbavu akaanguka, nikampiga sana na visigino vya viatu. Kisha, nilimvua nguo zake na kumpiga picha…”

“Ulimvua nguo?”

Macho ya Alvin

yalionyesha hasira na huzuni, na

kusababisha hali ya mazingira kuwa tata ghafla.

"Ah ... nilikuwa najaribu kumtisha tu akae mbali na mimi, nimemwambia akijaribu kunifuatilia wakati mwingine nitamdharirisha mtandaoni." Kwa kupoteza, Lisa alieleza, “Sikuwa na la kufanya. Unafikiri nitakuwa nimekosea sana?”

“Una akili?” Alvin alishusha pumzi ndefu huku akihofia kuwa angepatwa na wazimu. “Kwa hiyo umeona na nanihii yake?”

Akiwa chini ya macho ya hatari ya mwanaume huyo, Lisa alikuna kichwa na kukohoa kidogo. "

Eeh..Aah..Hapana. Inachukiza. Yeye ni ngozi na mifupa tu, na umbile lake si zuri kama lako pia. Kinyume chake, wewe ni mrefu na umejengwa vizuri.

Ninapokutazama, ninavutiwa na wewe.

Kukutazama kwa mara ya pili

kunanipaga wazimu kwe—”

“Nakupandisha

ya Alvin yalimtoka huku akivaa tabasamu la sifa.

Lisa alijisikia mkanganyiko wa kimawazo. Akijihisi hana cha kusema, alimwambia, “Sasa si wakati wa kuzungumzia jambo hili…”

“Nipe simu yako.” Alvin alinyoosha mkono wake kuelekea kwake.

Mara moja akampitishia simu yake.

Alvin alipozitazama zile picha alizidi kusononeka. Muda mfupi baadaye, alihamishia picha hizo kwake na kuziondoa zote kwenye simu ya Lisa.

“Haya, kwanini umezifuta…” Lisa alikosa raha.

"Kama mwanamke wangu, huoni aibu

kuweka picha za mwanamume

mwingine kwenye simu yako?" Akiwa

anamwangalia kwa ukali, alionya, "tena

wazimu?” Macho meusi

umepiga picha ukiwa umezingatia

kabisa sehemu zake za siri!" Lisa alikosa la kusema. Aliinamisha kichwa

chini bila kutamka neno lolote.

“Nenda ghorofani ukalale. Usifikirie mambo kupita kiasi kwani tayari

umempiga picha kama hizo. Familia ya Kimaro inajali sana hadhi yao,

hawawezi kukuacha salama pindi utakapozisambaza picha hizi.” Alvin

alisema kile ambacho hakumaanisha kumfariji.

“Kweli?” Lisa alikuwa na shaka juu

yake. "Lakini sidhani kama Willie ni mtu anayejali hadhi ya familia yake.

Anastahili kutendewa vibaya kama hivyo. Nilimpiga vibaya sana.”

“Hujui ni kiasi gani wanaume wanajali

utu wao ikilinganishwa na wanawake.

Wewe si mwanaume, kwa hivyo

hutaelewa. Naamini hatakuwa na ujasiri

wa kukutafuta. Umelishughulikia jambo

hili vizuri sana,” Alvin aling’oa risasi na kuendelea kueleza kimafumbo.

Ni mara chache alimpongeza Lisa. Kwa hivyo Lisa alishtuka kidogo aliposikia pongezi zake. Labda Alvin alikuwa sahihi. Huenda alikuwa haelewi kabisa wanaume.

"Baada ya kusema hivyo, usivue nguo za mwanaume tena." Baada ya kutulia, Alvin alimuonya kwa huzuni, "Bila shaka, isipokuwa mimi tu." Lisa

alishindwa cha kusema na kubaki anacheka tu.

“Nenda ukaoge. nitakusaidia kwa hilo.”

Alvin hakujali macho yake ya kusema, akauweka mkono wake kiunoni na kumbeba juu juu moja kwa moja.

“Sitaki." Lisa alipiga kelele kwa aibu.

Alikuwa ameweka wasiwasi na hofu

nyuma yake.

Usiku, ilimchukua Alvin muda kutafuta usingizi wake bila mafanikio. Mwishowe aliamua kushuka chini, akaingia kwenye gari na kuondoka kwenye nyumba yake ya kifahari.

•••

Usiku wa manane, Willie alirudi hotelini baada ya kufungwa majeraha yake hospitalini. Kwa hasira kali, akatoa simu yake ili apige.

"Kwa ndoano au kwa hila, nyinyi watu lazima mumtie Lisa kuzimu. Sitaki kusikia anaendelea kuishi mbwa yule.”

Alipomaliza tu kuongea, mlango ukasikika ukigonwa kwa nguvu. “Ni nani huyo mwenye kelele anayebisha saa za usiku hivi? Una hamu ya kifo, huh?"

Willie alikimbia kuelekea mlangoni ili

kuufungua, lakini akafunikwa na gunia.

Ghafla, mtu fulani alianza kumpiga.

Mtu huyo alikuwa mkatili na mkali.

Aliendelea kuupiga teke mwili wa Willie kwa nguvu. Wakati gunia liliipofunuliwa.

Mtu mrefu na mpana aliingia ndani. Mwanaume huyo alikuwa amevalia

sweta nyeusi. Vipengele vyake vya kuvutia vilipoainishwa chini ya taa zenye

giza kwenye chumba, Willie alihisi hofu na hali ya hatari iliyouzunguka mwili

wake.

“Alvin… Hapana, ninamaanisha kaka

Alvin. Kwa nini… Kwa nini uko hapa?”

Willie angeweza kumtambua mara ya kwanza. Kwake, mtu huyo

alifananishwa na shetani. Alikuwa

mwanaume pekee katika familia nzima ya Kimaro ambaye Willie alikuwa anamuogopa.

"Umekuwa ukifanya kazi na Jack

Kimaro hivi karibuni lakini hukujua

nilipo?" Huku mikono yake ikiwa

mfukoni, Alvin aliingia ndani kwa

majivuno na kumkanyaga Willie kifuani.

Willie alitetemeka kwa hofu. “Kaka

Alvin, sijui unasemaje. Ndiyo, ni Jack ambaye amekuwa akisimamia KIM

International hivi karibuni, lakini… Lakini sote tunafahamu kuwa uwepo wako

katika kampuni ni wa umuhimu mkubwa. Kwa kweli, wewe ndiye bosi wa KIM International.”

"Ujuzi wako wa kuongea maneno ya kuhadaa umeongezeka. Hivi ndivyo unavyofanya mbele ya Jack pia?" Alvin

alimpiga teke Willie kidevu kwa madaha kwa kutumia ncha ya kiatu chake. “Bado ninakumbuka mambo yote ambayo baba yako alifanya. Alimsaidia Jack kushusha cheo changu.”

“Hapana, kaka Alvin. Sote tunakungoja.”

Willie aliogopa sana kufanya kelele yoyote.

"Mnaningojea wapi wakati umekuja Dar es Salaama kimyakimya kukagua

biashara na kufanya mipango ya

kupanua uwekezaji?" Sura ya dharau

iliosha usoni mwa Alvin. "Mnajaribu

kubadilisha teknolojia za kimsingi za

kampuni wakati mimi sipo karibu, huh?"

Sura ya 123

Huku akiendelea kumkaripia kwa hasira, Alvin alikanyaga kifua cha Willie. "Leo, umeonekana kuwa wa kushangaza

sana huko kwenye sherehe za

Mawenzi, huh? Kwa tabia zako chafu, unawezaje kuthubutu kuanzisha fujo

huko hotelini? Huenda usijali kupoteza

sifa yako, lakini familia ya Kimaro inajali

sana hadhi yake. Unajichukulia kama

bosi wa KIM international na kisha

unatumia nafasi hiyo kufanya mambo ya hovyo ya kushusha hadhi ya kampuni?"

“Kaka Alvin, najua ni kosa langu.

Sitafanya tena,” Willie aliendelea

kumsihi kwa woga.

"Hapana. Nadhani wewe ni jasiri sana.

Unathubutu hata kujaribu kupata kipande cha mapenzi ya mwanamke wangu.” Alvin alicheka kwa huzuni.

Willie alipigwa na butwaa. "Lina ni mwanamke wako?"

"Sitavutiwa na mwanamke mchafu wa aina hiyo." Alvin akainama taratibu na kuchuchumaa. Macho yake ghafla

yakageuka kuwa makali sana.

Akiwa amepigwa na mawazo, Willie akauliza kwa mshangao, “Unamaanisha… Lisa…?”

“Ni vizuri kwamba unamkumbuka.

Sipendi kudhani kwamba nilimuonea mtu asiye na hatia baada ya kumalizana na wewe.” Alvin akajiweka sawa.

Willie alifahamu mbinu ambayo Alvin

angetumia. Akiwa amechoka, mara

akatambaa kwa shida. Alipiga magoti

sakafuni na kumsujudia Alvin. “Pole, kaka Alvin! Kwa kweli sikujua. Ni kosa langu. Nilikuwa kipofu. Tafadhali niruhusu niachane na…”

Alvin alimpiga teke kali hadi akajibamiza ukutani. Willie alitema damu iliyojaa mdomoni. "Kwa kuwa huwezi kudhibiti hiyo sehemu yako ndogo ya mwili, wacha tuiondoe kabisa..." Alvin akapiga hatua kuelekea kwake.

"Hapana." Willie alitetemeka kwenye buti zake. “Kaka Alvin, sitarudia tena. Ukiharibu, bibi yangu ataumia moyoni kwani ananipenda. Pia Babu atakasirika.”

"Sawa, niambie ninachoweza kufanya ili nifikirie kukusamehe." Alvin alimkanyaga kwa nguvu kwenye

‘jongoo’ lake.

Machozi yalitiririka usoni mwa Willie

kutokana na maumivu. Akiwa ameshikilia sehemu ya chini ya suruali ya Alvin, aliomba na kusihi, “Hapana, hapana. Naweza kufanya vile

unavyotaka. Nitapiga magoti na kuomba msamaha kwa Lisa kesho.”

“Sawa. Kumbuka ulichosema.” Alvin

aligeuza kichwa chake na kumwambia mtumishi wake wa chini, “Kwa vile

anafurahia kufanya wanawake vibaya, vua nguo zake na umpeleke kwenye

kibaraza. Wacha apigwe na upepo baridi wa baharini usiku kucha, labda

ataikumbuka siku ya leo kila atakapokuwa anafikiria kufanya ujinga.”

Mtetemeko ulishuka kwenye uti wa

mgongo wa Willie. Kabla ya hapo, Lisa

alikuwa amemvua nguo na kumwacha

amelala kwenye sakafu ya choo kwa

muda wa nusu saa, na kumfanya

ashikwe na baridi. Mbaya zaidi alikuwa

anaenda kupigwa na upepo wa baharini

kwa usiku mzima. Ilikuwa ni saa sita usiku na dakika kadhaa. Wawili hao

walikuwa wakatili kwelikweli.

“Kaka Alvin, nitaganda hadi kufa.” Willie alijitetea.

“Usijali. Kwa kuzingatia kuwa wewe ni binamu yangu, sitakuacha ufe.

Ambulance ya hoteli hii iko kwenye

standby hapo chini. Utaokolewa mara moja ukibaki na pumzi yako ya mwisho."

Alvin akampiga bega huku

akimkumbusha kwa sauti ya upole. Kwa

hayo, aligeuka na kuondoka.

Willie alikuwa kwenye hatihati ya kuanguka. Aliapa kwamba

hatamchokoza Lisa tena.

•••

Saa mbili kamili asubuhi, Lisa alipokuwa

akiandaa kifungua kinywa jikoni, alipokea simu kutoka kwa Chris

Maganga. "Lisa, wakurugenzi wanataka kufanya mkutano mkuu wa dharura leo asubuhi." Chris alieleza. “Wanadai kwamba ulimpiga Bwana Kimaro jana usiku, kwa hivyo wanaomba ufukuzwe kwenye nafasi yako ya mwenyekiti. Pia, ikiwa hautapiga magoti na kuomba msamaha kwa Bwana Kimaro, watakuondoa kwenye bodi ya wakurugenzi pia."

Lisa aliondoa apron yake mara moja. “Nakuja sasa hivi.” Alipokata simu, alielekea mlangoni kama upepo.

“Kifungua kinywa changu kiko wapi?”

Akiwa amevalia nguo za kulalia nyeusi, Alvin alitokea akishuka chini kivivu huku

akipiga miayo. Haijalishi alivaa nini, alikuwa akivutia tu kwa macho kutokana na umbile lake lenye nguvu.

"Kuna jambo la dharura limetokea ofisini. Shangazi Linda atakuja

kukuandalia.” Lisa alibadilisha viatu

vyake haraka na kukimbilia nje ya jumba hilo. Ndita za Alvin zilijikunja

sana. Ilikuwa ni muda mrefu sana tangu apate kifungua kinywa kilichoandaliwa naye.

Saa mbili na nusu asubuhi Katika

chumba cha mkutano, wakurugenzi

wote walikuwa na nyuso za huzuni na zenye hasira. Kwa kutajwa kwa Lisa, walitamani kumla.

"Chris ndiye wa kulaumiwa kwa jambo hili. Kama asingemtetea Lisa na kuwa

mwenyekiti, Mawenzi Investments isingeiudhi familia ya Kimaro."

“Amerukwa na akili? Alithubutu vipi

kumpiga Willie? Kimaro ni familia

mashuhuri, na kwa wazi hatuwezi

kumudu kuwachokoza.”

"Nilisikia mtu ambaye alimuudhi Willie

kabla ya huyu alikuwa bilionea kutoka

Kenya. Familia yake ilifilisika kwa

usikummoja tu.”

“Ndiyo. Willie anatisha."

Katikati ya majadiliano ya wakurugenzi, Jones Masawe alishusha pumzi ndefu.

“Yote ni makosa yangu. Sikupaswa kumruhusu Lina kumleta Willie jana.

Lakini nilisikia Willie alikuja hapa kwa

ajili ya ukaguzi, na nilikuwa na

matumaini kwamba Mawenzi

Investments ingeweza kufanya kazi na KIM International.”

“Kweli. Ikiwa tungeweza kushirikiana na KIM International, ingeinufaisha sana

Mawenzi Investments.

“Tulikosea. Tungemfanya Jones kuwa mwenyekiti.”

“Najutia uamuzi wangu pia. Sikupaswa

kumpigia kura Lisa wakati huo.”

Akihisi mnyonge, Mkurugenzi Amiri alisema, “Sasa kwa vile mambo

yamekuwa hivi, hatuna chaguo ila

kumwondoa katika nafasi yake ya

mwenyekiti kwa ajili ya matarajio ya Mawenzi Investments. Labda Jones

ndiye pekee anayeweza kutusaidia kukabiliana na dhoruba wakati huu.

Baada ya yote, binti yake ana uhusiano wa karibu na Willie.

Jones alipunga mkono kwa

unyenyekevu. “Sina hakika kama

naweza kusuluhisha hili. Baada ya

kusema hivyo, Bwana Kimaro

anampenda sana Lina. Ataenda naye

popote aendako. Una maoni gani, Lina?"

Akivumilia maumivu kutoka kwenye

majeraha yake ya sehemu za siri

yaliyosababishwa na Willie jana yake, Lina alilazimisha tabasamu tamu.

"Bwana

Hata aliniambia mambo mengi kuhusu mradi huo.”

Kila mtu alishangilia kwa furaha.

Mkurugenzi Amiri alisema, "Ni mpango wetu sasa. Jones atakuwa mwenyekiti wetu mpya.”

Lisa aliusukuma mlango na kujipenyeza ndani. Macho ya wazi na makali yaliwakumba wakurugenzi wote.

“Kwangu, ninyi nyote ni wakurugenzi wa

Mawenzi Investments, ambao pia mnachukuliwa kuwa wazee wangu.

Nilimpiga Willie jana usiku, ndiyo! Lakini kuna yeyote kati yenu aliyeniuliza kwa nini nilifanya hivyo?” Kila mtu alipigwa na butwaa.

Lisa aliongeza kwa hasira, “Jana usiku,

Willie alinifungia kwenye chumba changu cha hoteli na karibu kunibaka.

Lina alisimama nje ili kumsaidia

Kimaro ananipenda sana.

kufuatilia hali ya nje. Kwa sababu ya

njama yao chafu, mimi, kama

mwenyekiti wa Mawenzi Investments, nilikuwa karibu kuharibiwa. Kwa nini?

Kwa sababu Willie ni mjanja na hajali

kabisa. Hakuwa tu anajaribu

kunidhalilisha mimi bali pia Mawenzi

Investments nzima.”

'Hilo ni jambo lisilo na akili kwa Willie," mkurugenzi alinong'ona.

“Vipi Lina anathubutu vipi kufanya vile?!

Hiyo inatisha.”

“Sikufanya hivyo. Lina alisimama mara

moja. “Wewe ndiye uliyetaka

kumtongoza Bwana Kimaro, lakini

hakuwa na hamu na wewe. Anaweza

kupata mwanamke yeyote anayemtaka

kwa urahisi. Kwa nini atake

kujilazimisha kwako?”

Jones alisema kwa mzaha, “Hata

waandishi walikupiga picha ukiwa

umemshika Bwana Kimaro kwa mkono wake kwenye lango la hoteli jana usiku.

Hata hivyo, Bwana Kimaro alidai kuwa ulimvua nguo.

"Ni aibu kama nini!"

"Ni aibu kubwa kuwa na mkurugenzi kama huyu Mawenzi Investments." Kila mtu alimtazama Lisa kwa dharau.

Mkurugenzi Amiri alikunja uso na kusema. “Acha kujitetea. Umeingia kwenye matatizo makubwa wakati huu.

Tunataka tu kuilinda Mawenzi Investments. Kwa kuwa lilikuwa ni kosa

lako, unapaswa kubeba jukumu.

Kusema kweli, huwezi tena kukaa katika kampuni tena.”

Mdomo wa Lisa ulitetemeka kwa kejeli

huku macho yake yakionyesha sura ya jeuri. "Kwa hivyo mnapanga kunifukuza

kutoka kwenye bodi ya wakurugenzi?"

Jones alitabasamu kwa dharau. “Hilo

ndilo jambo pekee tunaloweza kufanya.

Afadhali ufungashe na kuondoka sasa

hivi.”

Lisa alidondosha macho yake. Alikuwa amechanganyikiwa kabisa na kampuni

hiyo. Wakati huo, mfanyakazi mmoja

alikimbia ndani na kupiga kelele, "Willie

yuko hapa! Sasa yuko chini, na anataka kukutana na Mwenyekiti Jones.”

Sura ya 124

"Nilijua Bwana Kimaro angefanya jambo

kuhusu hilo." Jones Masawe

alimwonyesha kidoleLisa na kumwambia, "Tazama, Bwana Kimaro

yuko hapa sasa. Afadhali umalizane

naye peke yako.”

"Usiende kinyume naye kamwe." Lina

alijaribu kumpiga teke alipokuwa chini.

"Ikiwa utamkosea tena Bwana Kimaro, hata mimi sitaweza kumtuliza kwa niaba yako."

"Hebu tumshike tu na kumpeleka chini."

Pendekezo la Jones lilikubaliwa mara moja na wengi.

Maofisa usalama wanne hadi watano

mara moja wakatembea kuelekea kwa

Lisa. Akiwa amekunja uso, Shani

akawazuia mbele ya Lisa. "Ikiwa nyinyi watu mtathubutu kumgusa, msinilaumu kwa kukosa adabu."

“Nyie mnangoja nini? Washikeni wawili hao sasa hivi." Jones Masawe bado

alimchukia Shani kwa kumpiga teke siku

nyingine. Sasa ikaja nafasi ya kulipiza

kisasi kwake.

Lisa alipogundua kwamba

wangepigana, alimzuia Shani. “Ni sawa.

Hakuna haja ya kunishika. Nitaenda

huko peke yangu." Mara tu alipomaliza

kusema, alikuwa wa kwanza kutoka

kwenye chumba cha mikutano.

Lina alipendekeza, “Twendeni

tukaangalie pia. Ni afadhali kujionea kuliko kusimuliwa.”

“Kweli. Hata hivyo, inabidi tumzuie asimkasirishe Bwana Kimaro zaidi.”

Kila mtu alishuka pia. Wakaelekea

kwenye chumba cha mapokezi pale chini. Akiwa amefungwa bandeji nene

chini, Bwana Kimaro alikuwa

amejikunyata huku akiwa ameshikilia

kikombe cha kahawa ya moto. Kutoka kwa sura ya uso wake mzuri, ilionekana

wazi kuwa alikuwa ameshikwa na homa na kuugua. Lisa alipofikiria juu ya tukio la Willie

akiwa amelala kwenye sakafu ya choo

akiwa amevua nguo zake jana yake

usiku, hakuwa na uhakika ni muda gani

alikuwa amepatwa na homa hiyo.

Pengine alishikwa na homa kwa sababu ya tukio hilo, ambalo lilimfanya akose

raha kabisa. Kwa kweli alihisi kwamba mtu asiye na haya kama Willie huenda

asisumbuliwe kuhusu picha hizo.

Lisa hakuwa na wasiwasi juu yake mwenyewe kwa vile hakuwa na ndugu

pia. Hakukuwa na kitu kingine chochote alichokuwa na wasiwasi nacho, isipokuwa kwamba Alvin angeweza kuvutwa kwenye matatizo tena.

"Samahani sana, Bwana Kimaro."

Jones Masawe alimsogelea na kisha

akainamisha kichwa kwa kumwomba

msamaha kwanza. “Natumai utakuwa

mkarimu wa kutusamehe. Usitazame

kiwango cha makosa yetu.”

“Hasa.” Mkurugenzi Amiri aliongeza

mara moja, "Tumemfukuza Lisa kutoka

kwenye nafasi ya mwenyekiti na

kumfukuza kutoka bodi ya wakurugenzi."

Willie Kimaro alikuwa ameganda tu, na moyo wake ulikuwa ukitetemeka kwa

nguvu. Aliinua kichwa chake huku macho yakiwa yametapakaa damu.

"Kwa hiyo yeye si mwenyekiti tena?"

“Ndiyo.” Jones alisema kwa uungwana, “Ni kwa sababu alikudhalilisha.

Hatukufikiri Lisa angekuwa na ujasiri wa kukufungia kwenye chumba na kukutongoza. Hiyo haikuwa aibu kwake.” Bila shaka, Jones alijua ukweli

vizuri. Hata hivyo, ili kumpa Willie njia ya kutoka, alimshtaki Lisa huku akiamini

kwamba Willie angemshukuru.

Alipokuwa akiwaza kabla hajaongea, Willie alimuangaza kwa hasira. Kabla

Jones hajapata fahamu zake, Willie aliinua mguu wake na kumpiga teke

kali. “Nani aliwaambia nyie kumfukuza

Lisa kwenye nafasi hiyo? Nani alisema

kuwa alinitongoza? Nyinyi mnajaribu

kuniletea matatizo!” Willie alimpiga teke

Jones Masawe kwenye mwili wake kwa

nguvu. Alikuja kuchelewa sana kuokoa

hali hiyo. Ikiwa Alvin angejua kuhusu

hilo, labda angepoteza maisha yake

kabisa.

Kila mtu alishtuka sana, na hata Lisa pia. Lina akapiga kelele. Alimkimbilia

Willie kwa haraka na kumshika mkono.

“Acha kumpiga teke, Bwana Kimaro.

Huyu ni baba yangu—”

“Nyamaza, btch!” Willie alimpiga kofi usoni, na baadaye akaanguka chini.

"Yote ni kazi yako. F*ck! Ninachojutia

zaidi ni kukufahamu wewe malaya mkubwa!”

Kama si Lina, Willie asingemkasirisha

Lisa, akifuatiwa na Alvin. Licha ya

kupigwa na kjeruhiwa, alikabiliwa na

upepo wa baridi wa usiku kucha kwenye

kibaraza cha hoteli kwa muda wote wa jana yake usiku. Akiwa ameganda kwa

baridi, karibu apate hamu ya kuruka

kutoka kwenye jengo ili kumaliza mateso yake. "Unafanya nini, Bwana Kimaro?" Lina alihisi kizunguzungu baada ya kupigwa kofi hadharani. Alipokuwa na Willie kwa

siku chache zile, Willie alijifurahisha

naye kila siku. Alimfanya na kumgeuza kwa jinsi alivyotaka. Akitaka kwa bibi, twende! Akitaka kwa mpalange twende!

Akitaka mdomoni, haya! Alifanya hayo

yote kwa nia moja tu ya kujisaidia yeye na Jones kubadilisha mambo katika kampuni.

Hata hivyo, kabla ya kumfanya Lisa

ajifunze somo lake, badala yake yeye

ndiye aliyepigwa.

Akiwa na huzuni, Lina alilia. “Bwana

Kimaro, alikuwa Lisa. Yeye ndiye

aliyekuumiza.”

“Najua. Sihitaji uniambie.” Macho ya Willie yakatulia kwa Lisa.

Moyo wa Lisa ulimshtua. Haraka akatoa simu yake na kuizungusha kama

ukumbusho kwake. “Bwana Kimaro, wewe—”

“Bi Jones, kuhusu tukio la jana usiku, lilikuwa kosa langu.” Willie alimsogelea na kumuomba msamaha wa dhati.

Umati ukakosa la kusema. Lisa naye alishindwa cha kusema. Alipigwa na butwaa kabisa. Kumbe kutumia picha

zake zisizo na heshima kumtishia

ilifanya kazi? Kweli Alvin alikuwa sahihi, familia ya Kimaro walikuwa wanajali

zaidi kuhusu utu wao. Hawakuweza

kumudu kuipoteza heshima yao.

Lina na Jones walipapasa macho yao

kwa nguvu. Walitilia shaka sana ikiwa

macho yao yalikuwa yanawadanganya.

"Bwana Kimaro, nadhani umekosea."

Lina akaongeza ujasiri wake tena na

kuvuta upindo wa shati la Willie.

"Umesahau jana usiku"

“Funga mdomo wako!” Akihisi kukosa subira, Willie alimpiga Lina teke.

“Nilikukera kwa bahati mbaya baada ya

kulewa jana usiku, Bi Jones. Samahani kwa tabia ya ghafla na ya kimbelembele. Mimi ni fisadi ambaye sistahili kuwa binadamu. Bahati nzuri

uliniamsha kwa kunipiga, au ningeharibu sifa ya familia ya Kimaro na kuwadhalilisha wazee wangu.”

Umati ulishangaa na kuhisi kuwa

ulimwengu umegeuka kuwa ndoto. Lisa

alipepesa macho na kumtazama Willie

kwa makini. Je, ilikuwa ni kalamu ya

chuma aliyomchoma mbavuni jana yake

usiku ambayo ilikuwa imeharibu ubongo

wake, au? Alikumbuka vizuri kwamba

hakuwa amelewa jana yake usiku.

Ingawa alikuwa na picha za kumtishia, hakuhitaji kuwa na tabia ya unyenyekevu hivyo.

Mkurugenzi Amiri alikuwa mwishoni mwa akili yake. “Lakini sisi…”

“Lakini nini? Nyinyi watu mnawezaje

kuthubutu kumfukuza Lisa kwenye

nafasi ya mwenyekiti na kumfukuza nje ya bodi ya wakurugenzi?!” Macho ya Willie yakawa magumu huku

akiwatazama wakurugenzi. “hivi nyinyi

wazee mnafikiri kwamba bado mna

nguvu sana na hamwezi kufikiria

kustaafu? Au mnafikiri kwamba bila

nyinyi Mawenzi Investments itafilisika?"

Wakurugenzi walitetemeka na

hawakuhisi kwamba walikuwa na umri

wa kutosha kustaafu bado. Bado

walipanga kufanya kazi kwa miaka kumi

hadi 20 kwenye kampuni.

"Bwana Kimaro, tulikuwa bado hatujalipisha hilo," Mkurugenzi Amiri

alisema mara moja kwa sauti ya kutetemeka, "Hakufukuzwa kazi yake.

Yeye bado ni mwenyekiti, na hii haitabadilika kamwe.”

Mwili wa Jones ulitetemeka. Akiwa

amezidiwa na hali ya kutokuamini, alinguruma kwa fadhaa. "Unasema nini, Amiri Gumbo? Nyinyi mlinichagua kama mwenyekiti asubuhi ya leo!”

Mkurugenzi Levy alimtazama kwa

hasira. "Wewe na binti yako ndio mlidai

kuwa Bibi Jones alimkosea Bwana

Kimaro. Kumbe haikuwa hivyo.

Hatuwezi kufanya lolote kwa sasa.”

“Hasa.” Wakurugenzi wakaanza

kumgeuka. "Kila mtu anajua kwamba una tamaa ya

kuwa mwenyekiti, lakini haukupaswa

kupeleka mambo mbali sana huku ukipuuza utu wako." mwingine

akamshushua.

"Hata hivyo, Lisa ni sehemu ya familia ya Jones. Hukupaswa kumtendea ukatili

hivyo.” Wanahisa walianza kumwambia Jones. Jones na Lina walionekana

wameanguka kutoka mbinguni hadi kuzimu. Kwa hasira, Jones alimfokea

Lina, "Ni nini kinaendelea duniani?!"

"Sijui." Lina alikuwa ameduwaa, akishangaa kwa nini kila kitu kilikuwa

kimebadilika kabisa usiku mmoja.

Lina ndiye aliyesema kwamba alikuwa

amemweka Willie kwenye kiganja cha

mkono wake. Yeye ndiye aliyesema

kwamba Willie angewasaidia. Yeye

ndiye aliyesema kwamba Willie

alimchukia sana Lisa hivi kwamba

asingeweza kungoja kumuua.

Kwa sura ya kusihi, macho yake yakatua kwa Willie. “Bwana Kimaro, Lisa alikuroga au? Si ulisema hivyo... unanipenda sana?”

Sura ya 125

"Ninakupenda?" Mwitikio wa Willie ulikuwa kana kwamba alisikia mzaha.

“Uliingia kitandani kwangu licha ya kuwa una mpenzi. Unafikiri ningekuacha bure? Huna tofauti na makahaba

wanaojiuza huko nje.” Kofi lilitua kwenye

shavu lake, lakini safari hii, lilionekana

kuwa limetua moyoni mwake pia. Lina

karibu aanguke chini kabisa.

Kulikuwa na idadi kubwa ya watu karibu

naye, ikiwa ni pamoja na wafanyakazi

na wanahisa wa Mawenzi Investments.

Hali hiyo ilikuwa imezua tafrani

miongoni mwao, wakamtazama kwa

dharau. “Sikutarajia angekuwa mtu wa aina hii.

Kabla ya hili, alinipa hisia ya kuwa safi na mtukufu.” Mnong’ono ulisikika.

“Ndiyo. Wanaume wengi katika kampuni

walimwona kama mungu wa kike.”

Mwinginea naye akatoa yake.

“Bahati nzuri sikumtambulisha kwa

mwanangu. Hakika hana aibu.”

Katikati ya fedheha ya mara kwa mara, uso wa Lina ulibadilika rangi. Alikuwa

ameweka juhudi nyingi katika kujenga

sifa ya kuvutia kabla ya hii, lakini yote

iliharibiwa wakati huo.

Kama mwanaye, Jones Masawe

alitetemeka kwa aibu. “Umeenda mbali

sana, Bwana Kimaro. Lina anakupenda

kweli. Alianguka kwa ajili yako mara ya kwanza.”

Bila kutarajia, Willie aliangua kicheko kana kwamba maneno ya Jones

yalikuwa ya mzaha. “Anapenda nini kuhusu mimi? Kusema ukweli, baada ya

kuwa na wanawake wengi, ninatambua kwamba yeye ndiye mwanamke

mlegevu zaidi. Bwana Jones, ninafurahia jinsi unavyomchukulia binti

yako kama kitu kwa ajili ya mali na mamlaka.”

Matamshi hayo yalibadilisha mtazamo wa umma kuhusu Lina na Jones kwa

mara nyingine tena. Lisa, ambaye

alikuwa akitazama tu tukio hilo, naye alishangaa. Hakushangaa kwamba

Willie alikuwa mpotovu, kilichomshtua zaidi ni kwamba Lina aliweza kukubali.

Lisa alitoa kikohozi chepesi kisha

akatabasamu na kumtazama Lina.

“Dada siwezi kujizuia kukuona kwa

mtazamo tofauti sasa. Je, wakati huo

ulinipokonya Ethan kwa kutumia mbinu

kama hiyo?” Swali hilo liliukumbusha mara moja umma wa watu kuhusu

uhusiano wa awali wa Lina na Ethan.

Kila mtu alimtazama Lina kwa unyonge sana. Hata walijiweka mbali naye, wakiogopa kwamba angewachafua.

Kutetemeka kulitawala mwili mzima wa

Lina. Alitoa macho yake moja kwa moja, akijifanya kuzimia kwa hasira kali.

“Linal” Jones alimbeba upesi na kutoka

ukumbini kwa aibu.

Willie alikunja uso. Kisha akageuza

kichwa chake na kumtazama Lisa.

"Alikuwa na mpenzi hapo awali?"

“Ndiyo. Hata wakachumbiana kwa

sherehe kubwa. Hata hivyo, mara moja

alimlenga mtu mwingine kwa sababu

mpenzi wake wa zamani aliondolewa

kwenye madaraka ya kampuni.” Lisa

alimtupia jicho la ajabu. "Ulidhani kuwa

wewe ndiye mwanaume wa kwanza kulala naye?" Willie alishindwa cha kusema. Hakika hilo ndilo alilolidhania lakini hakuweza kujihakikishia.

Akifikiria kwamba alimsaidia

kushughulika na Jones na Lina, Lisa alimkumbusha hivi kwa fadhili, “Mambo fulani yanaweza kutengenezwa tu katika ulimwengu huu.”

Kwa kujieleza kwa aibu, Willie alitabasamu bila kupenda. "Sasa naweza kustahili mshamaha wako, Bi Jones?"

Kwa kweli, Lisa hakuelewa ni nini

kilikuwa kikiendelea kichwani mwake.

Kabla hajamjibu alimuuliza, “Naweza

kuwa na maneno machache nawe, Bwana Kimaro?”

“,..Bila shaka, najua hili, hehee! Asante kwa kunikumbusha.”

“Hakika. Hakuna shida." Lisa alitoka ofisini huku Willie akimfuata. Miguu

yake ilitetemeka baada ya kumtazama Shani aliyekuwa pembeni yake.

Shani alimtazama kwa tabasamu. “Uko sawa, Bwana Kimaro?”

“Mimi…Niko sawa. Kweli, wewe ni mtaalamu sana." Willie alihisi bomu la atomiki likilipuka kichwani mwake. Lisa alilindwa na Shani mahiri, ambaye alitoka ONA.

ONA lilikuwa kundi la siri zaidi la chini kwa chini chini ya familia ya Kimaro.

Ilijumuisha maveterani kutoka jeshini na washiriki kutoka kwenye tasnia za

sanaa ya mapigano ya kimwili. Kwa

muda huo, ilisimamiwa na Alvin pekee.

Lisa alimroga vipi Alvin hadi akawa

naye? Shani alikuwa anashangaa kila

siku, alimfahamu vizuri Alvin.

Jinsi Willie alivyomtazama Lisa sasa ilikuwa tofauti kabisa.

Lisa alisimama baada ya kufika umbali fulani. Shani kwa makusudi alienda mbali zaidi ili kuwapa nafasi wawili hao. Lisa alikaa kimya akimsubiri Willie amuulize kuhusu zile picha. Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda mrefu, hakusema neno. Alimtazama hata kwa mchanganyiko wa kupendeza, woga, na hofu. Lisa alikosa la kusema kabisa. “Vema…

Bwana Kimaro, unakumbana na madhara yoyote kutokana na kupigwa jana usiku?”

“Hapana kabisa. Badala yake nimekuwa mwenye busara.” Willie alitabasamu. “Bi

Jones, ni heshima yangu kubwa kuweza

kukutana nawe hapa Dar es Salaam.

Tunaweza kuwa marafiki?"

Willie alipunga mkono wake. "Unaweza kuhifadhi picha ukipenda."

Lisa alijikuta midomo yake ikitetemeka. Kwa nini ahifadhi picha zake zisizo na heshima? “Usinilaumu kwa kukuvua nguo na hata kukufedhehesha jana usiku…”

Willie aliganda na kusema kwa kusitasita, “Ulikuwa unasema ukweli tu.

Ningewezaje kukulaumu… Ah-choo!”

Alijifuta pua kwa aibu huku komeo lake likishuka. "Bi Jones, nijulishe ikiwa unahitaji msaada wowote. Nitajitahidi kukusaidia.”

Baada ya kuwa kimya kwa muda, Lisa aliuliza, "Labda ulipiga picha za Lina

akiwa amelala nawe, sivyo?"

Willie alipigwa na butwaa. Kwa jinsi

“Lakini picha…”

alivyokuwa akimtazama Lisa ni kana

kwamba ni rafiki yake wa karibu. "Sikutarajia ungenijua vizuri."

Lisa alijisikia vibaya. Kwa hakika

alikutana na baadhi ya vitabu vya

saikolojia na akajifunza kwamba

wapotovu kama yeye kwa kawaida wangepiga picha za aina hiyo. “Hapana, mimi—”

"Naelewa. Nina idadi kubwa ya video zake. Unapanga kushughulika na Lina, sivyo? Ninaweza kukutumia video hizo

sasa, lakini… Usiwahi kuzionyesha kwa mtu yeyote, hasa mpenzi wako.”

Ikiwa Alvin angegundua kuwa Lisa

alitazama video hizo, bila shaka

angemtoa utumbo Willie akiwa hai. Lisa

alipigwa na butwaa. Wazo la ajabu

likaangaza akilini mwake. “Sawa.”

Aliitikia kwa kichwa.

Willie alimtumia video hizo mara moja.

Alipopokea video hizo, Lisa alionekana

kutojali kwa nje, lakini msukosuko wa

mhemko ulikuwa tayari umeanza ndani yake. Kwa kweli, alikuwa ameomba tu video hizo kwa njia ya kawaida. Alidhani kwamba Willie asingeweza kuzituma

kwake kwa kuzingatia tabia yake ya kishenzi jana yake usiku. Hata hivyo, alionekana kuwa tofauti kabisa leo.

Alikuwa na hakika kwamba haikuwa tu

kwa sababu ya picha zisizofaa

alizotumia kumtishia, kulikuwa na sababu nyingine.

"Alvin, kwa nini uko hapa?" Ghafla, alitazama mahali fulani nyuma ya Willie wakati akiuliza.

Willie alitetemeka sana kwa hofu. Alivaa

tabasamu la kubembeleza na kugeuka

nyuma, na kugundua kwamba

hakukuwa na mtu nyuma yake. Alipigwa

na butwaa kwa muda. Hapo hapo

akahamishia macho yake kwa Lisa

ambaye alikuwa na sura ya ajabu machoni mwake.

“Bwana Kimaro, unamfahamu Alvin?

Kwa nini ulionekana kuwa na wasiwasi na hofu nilipoita jina lake?” Wazo

lisiloaminika likamwingia taratibu kichwani Lisa. "Majina yenu nyote wawili ni Kimaro. Je! inaweza kuwa hivyo…”

“Sijui unasema nini. Hata simfahamu Alvin.” Akiwa amechoshwa, Willie alitikisa mkono wake kwa haraka.

Lisa alicheka. "Kwa kuzingatia utu wako, wewe ndiye mtu ambaye

utafanya chochote ili kufikia malengo yako. Wewe ni mkatili na unapenda

kulipiza kisasi, kwa hivyo haishangazi

kwamba hata picha zako nilizonazo

hazikubabaishi. Kama huna mpango wa kuniambia, nitarudi na kumuuliza Alvin

kisha…”

TUKUTANE KATIKA KITABU CHA 6

Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.