VITUO VYA MAJI VYA PAMOJA/MBADALA Vituo vya maji mbadala vinatoa usalama kwa jamii za vijijini na mifugo yao ambayo inatumia vyanzo vimoja na ndovu. Hii inawawezesha ndovu na mifugo kunywa maji bila kufarakana.
Katika miaka yote iiyopita kumekuwa na ukame wa muda mrefu na uhaba wa maji.
1.
Ndovu wanavutiwa na harufu ya maji yaliyohifadhiwa kwenye vijijini na kuvunja mabomba, matangi ya maji na vifaa vya kupata maji.
Hii inasababisha hasara kubwa na inaweza kuwaacha watu na mifugo bila maji kwa siku kadhaa, hivyo kuongeza migongano na chuki dhidi ya ndovu. Wanawake na watoto wanaweza kuathiriwa vibaya kwani mara nyingi wao hukusanya maji kwa ajili ya familia.