Mikanda ya Ufuatilizi ya GPS na Uzio wa Kijiografia

Page 1

Mikanda ya Ufuatilizi ya GPS na Uzio wa Kijiografia Mikanda ya ufuatiliaji ya GPS (mfumo wa mawasiliano wa kijiografia) ni mfumo sahihi wa urambazaji unaotegemea satelaiti na mfumo wa eneo ambao umewekwa kwenye ndovu ili kufuatilia mienendo yao katika muda halisi katika maeneo mbalimbali.

Save the Elephants (STE) inatumia vifaa vya ufuatilizi vya GPS ili kuelewa maisha ya ndovu, maamuzi na mahitaji yao. Mwanzilishi wa STE Dkt. Iain DouglasHamilton alikuwa mtu wa kwanza kufuatilia ndovu kwa kutumia mikanda ya redio (1969) na STE inaendelea kuwa mstari wa mbele katika teknolojia ya ufuatilizi. Mikanda huwa na vifaa vya teknolojia ya hali ya juu ya GPS ya Satelaiti au vifaa vya kufuatilia vya GSM ambavyo huruhusu wanasayansi na maafisa wanyama pori kufuatilia, kwa muda halisi, wakati na wapi wanyama hufanya harakati katika mazingira.

Kama spishi zinazohama hama, ndovu wengi barani Afrika hutumia muda wao mwingi nje ya maeneo yaliyohifadhiwa, hii inamaanisha kwamba wengi wao wanaweza kuvuka na kuingia kwenye vijiji na mashamba ya karibu. Kuongezeka kwa idadi ya watu kumechochea ujenzi wa makazi ya watu na barabara zinazozuia kabisa kupita au kukinga njia muhimu za uhamaji kwa wanyama pori.

Kuwafunga mikanda ndovu kunajaribu kupunguza migogoro na kuhakikisha usalama wa binadamu na ndovu.

Ndovu dume aitwaye Wide Satao akiwa amevishwa mkanda © Naiya Raja/Save the Elephants Soma zaidi kuhusu: Kufuatilia — Ufuatiliaji wa Muda Halisi (Machi 11, 2022) Save the Elephants.

1.

Tazama: Vita ya Nafasi | Mgogoro baina ya Binadamu/Ndovu Maasai Mara. (Mei 16, 2022).

Kenya inatumia mikanda ya GPS iliyounganishwa na satelaiti kuwalinda ndovu, watu (Septemba 9, 2016). Save the Elephants.


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.