Kuwaongoza vijana wa kisasa 2.qxd
7/2/2011
10:57 AM
Page 58
Kuwaongoza vijana wa kizazi kipya yanawatangazia wengine kwamba wakati wote yanahitaji kitu kipya ndani yake, hivyo wale watu ambao wako karibu na mtoto huyo ni lazima wampatie kile anachoomba. Jambo hilo hilo linaweza kusemwa juu ya jamii. Kama ndani ya jamii, hisia au uelewa mpya ukipatikana, basi hii pia ni dalili ya ustawi na maendeleo ya jamii hiyo. Hii pia ni dalili kwamba zile sehemu ndani ya jamii zina haja mpya ambayo ni lazima itimizwe. Mambo ya namna hii lazima yaonyeshwe kama ni mambo ambayo ni tofauti na tamaa duni na haja ya kuabudu nafsi, na hivyo tusije tukachukulia kamwe kwamba maswali haya ni namna ya uendekezaji wa tamaa duni. Hivyo, wakati mambo haya yanapojitokeza, ni lazima tuzingatie akilini haraka sana aya hii ifuatayo ya Qur’ani:
“Na kama ukiwatii wengi katika (hawa) waliomo duniani watakupoteza mbali na njia ya Mwenyezi Mungu. Wao hawafuati ila dhana tu, hawana ila (ni wenye kusema) uongo tu.” (alAn’aam; 6: 116) Na kwa nyongeza zaidi tunasoma hivi:
“Na kama haki ingelifuata matamanio yao, zingeharibika mbingu na ardhi na vilivyomo. Lakini tumewaletea ukumbusho wao, nao walijitenga mbali na ukumbusho huo.” (al-Muuminun; 23: 71)
58