Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 219

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:22 PM

Page 204

katika Uislamu

uchaguzi katika mambo yao wakati Mwenyezi Mungu na Mtume wake wameshakata shauri.” (Qur’ani 33:36). Hatuoni mahali popote katika Qur’ani au Sunna ambapo bwana Umar, Abu Bakr, Uthman au sahaba yeyote yule aliyeruhusiwa kupinga amri ya Mtume (s.a.w.w.) au Qur’ani. Kama angekuwepo sahaba anayestahiki kumkosoa Mtume (s.a.w.w.) ni Imam Ali Ibn Abu Talib (a.s.) kwa sababu Mtume (s.a.w.w.) alisema kuwa, “Mimi ni Jiji la elimu na Ali ni lango lake.” Vile vile Mtume (s.a.w.w.) alisema, “Hakuna amjuaye Allah ila mimi na Ali, na hakuna anijuaye mimi isipokuwa Allah na Ali, na hakuna amjuaye Ali isipokuwa Allah na mimi.” Lakini pamoja na uzito wa maneno hayo ya Mtume (s.a.w.w.) juu ya Ali (a.s.), hatuoni popote katika historia ambapo Imam Ali (a.s.) alikwenda kinyume na mwenendo wa Mtume (s.a.w.w.) au Qur’ani! Rejea: (Kuhusu Umar na Talaka) (1) Al-Ghadir, cha al-Amini, Jz. 6, uk. 83-325 (2) An-Nass wa’l-ij’tihad, cha Sharafu’dDin uk. 155-276. Ndoa ya Muda Maalumu (Mut’ah): Ndoa hii ilitumika wakati wa uhai wote wa Mtume (s.a.w.w.) na pia muda wote wa utawala wa Abu Bakr Sidiq. Umar ibn Al-Khattab alipochukua Ukhalifa, ndoa hii ilitumika muda mfupi wa utawala wake kisha akaipiga marufuku kwa pamoja na ‘Mutatul Hajj.’ Aina hii ya ndoa ilitumika kumwoza binti yake Abu Bakr Sidiq yaani Asma, kwa bwana Zubair-al-Sahab, na kwa ndoa hiyo wakazaliwa watoto halali: Abdallah Ibn Zubair na Urwah Ibn Zubair. Na hiyo Mutatul Hajj au Umra kwa bahati hakufanikiwa kabisa kuifuta ingawa aliitamka kuifuta, kwani bado inatumika hadi leo! Hata hivyo aliamuru kuwa atakayefunga ndoa ya Mut’ah auawe na ikawa baadhi ya watu wameacha. Ingawa hivi leo baadhi ya Sunni wachache hutumia ndoa hii, na walio wengi wanaipinga na kuiita haramu, Shia Ithna’asheri bado wanaendelea kuitumia. Nitatoa maelezo zaidi hapa kama ushahidi wa uhalali wa ndoa hii kutoka katika Sunna na Qur’ani. Tuanze na (Qur’ani 4:24): 204


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.