Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 149

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 134

katika Uislamu

Tukio hilo liliwafanya masahaba wanafiki kumwudhi Mtume (s.a.w.w.) kwa kueneza uvumi wa uongo kumsingizia tendo la uzinifu mama Aisha! Kiongozi wa unafiki huo alikuwa Abdulla bin Ubay - kiongozi wa wanafiki wa Madina. Miongoni mwa waenezaji wa uvumi huo alikuwemo Mistah ambaye alikuwa mtoto wa mjomba wake Abu Bakr. Mtume (s.a.w.w.) alimwita Imam Ali Ibn Abu Talib (a.s.) na Ibn Zayd na kuwaeleza uvumi huo potofu ulioenezwa na wanafiki. Zayd alisema kuwa maneno ya wanafiki yapuuzwe. Imam Ali (a.s.) alishauri kuwa Burairah mtumishi wa mama Aisha aitwe na kutoa ushahidi kuhusu tabia ya mama Aisha. Yule mtumishi aliitwa na akasema kuwa hajaona dalili zozote za yeye kuamini uvumi huo. Uvumi huo ulipuuzwa na ndipo ikashuka Aya, (Qur’ani : 24:11). Katika Aya hiyo maneno ya mwisho ya: “......... Yule aliyebeba sehemu kubwa ya kueneza uvumi huo atapata adhabu kali.” Maneno hayo yanamhusu Abdullah bin Ubay kwa kuongoza kueneza uvumi huo. Na huo ndio umuhimu wa kutafuta sababu za kushuka Aya, na siyo kufasiri maneno tu kwa kanuni za lugha peke yake. Lengo la kueleza kisa hiki ni kuonyesha kuwa kundi la hao masahaba waliueneza uvumi huo kinyume na mafunzo au amri ya Qur’ani inayoamuru kuwa tuhuma ya uzinifu ithibitishwe kwa ushahidi wa watu wanne. Je, masahaba hao, nao ni waadilifu? Hao wanaodai kuwa masahaba wote ni waadilifu, ni kwa ushahidi gani? (g) Katika historia ya vita vya Uhud tunaelezwa kuwa Mtume (s.a.w.w.) aliondoka Madina na Jeshi la watu (sahaba) elfu moja. Lakini huko njiani Abdullah bin Ubay Salul alimkimbia Mtume (s.a.w.w.) akarejea Madina na wenzake 300! Sitawataja majina yao lakini jambo la msingi ni kwamba walikuwa masahaba! Je, Qur’ani inasemaje juu ya watu kama hao:

134


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.