Qurani Tukufu - Al Kashif Juzuu No - 2

Page 185

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Pili

2. Sura Al-Baqarah

YAMINI Aya 224 - 227 Wala msimfanye Mwenyezi Mungu ni pondokeo la viapo vyenu Mwenyezi Mungu amekataza kutangulizwa katika kila jambo kwa kuapa sana, kwa sababu mwenye kukitaja kitu sana huwa amekifanya ni pondokeo lake. Mwenyezi Mungu amekushutumu kuapa sana kwa kauli Yake:

“Wala usimtii kila mwenye kuapa sana, aliye dhalili." (68:10) Mwenye kuapa sana haiba yake hupungua, dhambi zake zikazidi na akatuhumiwa uwongo. (Ili) mfanye mema na mumche (Mwenyezi Mungu) na kusuluhisha kati ya watu Hili ndio sababu ya kukatazwa kuapa; maana yake ni kwamba Mwenyezi Mungu anawakataza kuapa bila ya dharura, ili muwe wema wanaomcha Mungu, wenye kufanya wema duniani, sio ufisadi. Mwenyezi Mungu hatawapatiliza kwa sababu ya kuapa kwenu kwa upuuzi upuuzi Baada ya Mwenyezi Mungu kukataza kuapa bila ya dharura, amebainisha kwamba mengi yanayowapitia watu katika ndimi zao mfano Wallahi vile'au Sio hivyo Wallahi, n.k.; siyo viapo vya uhakika isipokuwa ni mchezo tu unaokuja kwenye ulimi bila ya kukusudia, wala hayana athari yoyote; ndiyo ikawa Mwenyezi Mungu hakuwajibisha kafara katika dunia wala hakuna adhabu Akhera.

175


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.