Qurani Tukufu - Al Kashif Juzuu No - 2

Page 154

Tafsir Al-Kashif: Juzuu ya Pili

2. Sura Al-Baqarah

Na pamoja nao akawateremshia Kitabu kilichoshikamana na haki ili kihukumu baina ya watu katika yale waliyohitilafiana.” Hapa inatubainikia kwamba katika maneno kuna jumla iliyokadiriwa ambayo ni : "Watu wote walikuwa mila moja kisha wakahitilafiana” Linalofahamisha hilo ni kauli inayosema: "Ili kihukumu baina ya watu katika yale waliyohitilafiana." Na hilo linatiliwa nguvu na kauli hii:

"Na watu hawakuwa isipokuwa mila moja; kisha wakahitilafiana..."(10:19). Na hawakuhitilafiana katika hayo ila waliopewa Kitabu, baada ya kuwafikia ubainifu, kwa sababu ya uhasidi baina yao Yaani: Watu ambao walikuwa ni mila moja, kisha wakahitilafiana na Mwenyezi Mungu akawapelekea Mitume, watu hao pia walihitilafiana Mitume hao; wengine waliamini na kusadiki, na wengine wakakufuru na kukadhibisha baada ya kuthubutu hoja na dalili wazi za mkato. Hakuna sababu yoyote ya kukadhibisha huku isipokuwa uhasidi na kuhofia manufaa yao ya kibinafsi na uadui. Ndipo Mwenyezi Mungu akawaongoza alioamini waliyohitilafiana kwa idhini Yake.

katika haki

Yaani Mwenyezi Mungu (s.w.t.) amewafikisha wenye nia njema kwenye imani ya haki aliyokuja nayo Mtume; na imani hiyo ni kwa amri Yake Mwenyezi Mungu (s.w.t.) Kwa hivyo makusudio ya idhini ni ‘amri.’ Na Mwenyezi Mungu humwongoza amtakaye kwenye njia iliyonyooka

144


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.