Kila mwanadamu amepewa zawadi ya maisha, lakini siyo watu wote wanaofikia umri mkubwa au kujiandaa kwa safari ya kuzeeka. Biblia inatufundisha, “Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku zilizo mbaya” (Mhu 12:1). Maneno haya yanatufundisha kuwa maa-ndalizi ya uzee huanza mapema, katika ujana, kwa imani thabiti na nidhamu ya maisha.
Katika toleo hili la RIZIKI, tunatafakari maana ya kuzeeka kwa heshima. Kuzeeka siyo kupoteza thamani, bali ni hatua ya kuonesha hekima, urithi wa kiroho na heshima inayojengwa kwa muda mrefu. Tunajifunza kutoka kwa mifano ya watu wa Biblia kama Yakobo, ambaye uzee wake ulikuwa ushuhuda wa baraka na urithi wa imani.