Huduma za kisheria zinazohusiana na vvu mwongozo kwa kliniki za msaada wa kisheria za vyuo vikuu vya

Page 1

HUDUMA ZA KISHERIA ZINAZOHUSIANA NA VVU Mwongozo kwa Kliniki za Msaada wa Kisheria za Vyuo Vikuu vya Tanzania


SHUKRANI 2 Mwongozo huu wa kisheria umetolewa chini ya mradi wa IDLO-UNAIDS wa “Kujenga mbinu za kudumu za kupunguza ubaguzi na upatikanaji wa haki kwa watu wanaoishi na VVU na wale wote walioathirika nchini”. IDLO na UNAIDS wanatambua Mfuko wa Dharura wa Rais wa Nafuu ya Ukimwi (PEPFAR) wa Marekani kwa msaada wa kifedha wa uandikaji wa chapisho hili. Mwongozo huu wa kisheria ulifanyiwa utafiti na kuandikwa na Belice Odamna. David Patterson, Romualdo Mavedzenge, Quinten Lataire na Marie Engel walitoa maoni muhimu juu ya rasimu. Mwongozo huu ulipitiwa kwa ufasaha na Miraji Mambo (Afisa wa Kisheria) Tume ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS); Fredrick Macha (National Programme Officer-UNAIDS); Daniel Naftal Lema, Mwanasheria wa Mahakama Kuu, Tanzania; Asina Omari, Mwenyekiti, Kamati ya Misaada ya Kisheria na Mhadhiri, Shule ya Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Maurice Oduor, Mwanasheria wa Mahakama Kuu ya Kenya na Mhadhiri, Shule ya Sheria Chuo Kikuu cha Moi. Uhariri wa kiufundi ulifanywa na Hilary Cadman, Huduma za Uhariri wa Cadman, Australia.

Kimeandaliwa Na; Tarehe ya chapisho: April 2018. Hati miliki © 2018, Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Sheria (IDLO). Haki zote zimehifadhiwa. Maoni yaliyotolewa katika chapisho hili ni maoni ya waandishi na hayakulazimika kufuata maoni au sera za IDLO au Wanachama wake. Kitabu hiki kina haki miliki lakini kinaweza kuzalishwa kwa njia yoyote bila malipo kwa madhumuni ya elimu, ikiwa ni chanzo cha habari na kimetambulika. Ruhusa rasmi inahitajika kwa matumizi yote hayo. Kwa kuiga kwa namna yoyote ile au kuzalisha machapisho mengine, ni lazima kupata kwanza ruhusa kutoka kwa mmiliki wa haki miliki na gharama inaweza kuombwa. Maombi ya uzalishaji wa kibiashara yanapaswa kuelekezwa kwa IDLO.


CONTENTS 3 Usuli . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 4 Maelezo ya Utangulizi . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 5 Tafsiri ya Maneno . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 6 SEHEMU YA 1: UELEWA WA TATIZO . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 7 1 .2 Epidemiolojia ya VVU nchini Tanzania . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 8 SEHEMU YA PILI: VVU, HAKI ZA BINADAMU NA SHERIA . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.1 Kujua/kuelewa sheria kama inahusiana na VVU katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.1.1 Sheria za kimataifa na za kikanda . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.2 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.3 Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti VVU na UKIMWI, 2008 . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.3.1 kibali cha habari . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.3.2 faragha na siri . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.4 Sheria ya makosa ya jinai inavyohusika na VVU katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.4.1 Kanuni ya adhabu sura ya 16, 2002 . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.4.2 Sheria ya kupambana na kuzuia uingizaji usafirishaji na utumiaji wa madawa ya kulevya sura ya. 95. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.5 Sheria ya ajira na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.6 Ardhi, mali na urithi katika mazingira ya VVU. . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.7 Watu wenye hatari, VVU na sheria . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.7.1 Wahamiaji haramu na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.7.2 Wafungwa na watu wengine walio katika vituo vya marekebisho na VVU 2.7.3 Wasichana vijana na wanawake na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 2.7.4 Watu wenye ulemavu na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . .

10

SEHEMU YA TATU: MAADILI NA UTOAJI WA MSAADA WA SHERIA . . . . . . . . . . . . . . . . . . 3.1 Mfano wa masuala ya Kisheria yanayohusiana na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 3.2 Huduma za kisheria zinazohusiana na VVU . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 3.2.1 Huduma Nyingine za Kimkakati Zinazoweza tolewa na Kliniki ya Sheria 3.3 Wajibu wa kisheria na Kimaadili katika utoaji wa huduma za kisheria . . . . . . . . . . . . 3.3.1 Kanuni za utoaji wa huduma za kisheria zinazohusiana na VVU . . . . . . .

26 27 27 28 28 28

12 12 15 17 18 18 20 21 22 22 23 23 24 24 24 25

KIAMBATANISHO . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 30 Sampuli ya Mkataba wa usiri . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 31 Fomu ya maelezo ya mteja . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 32 MAREJEO . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . . 35


USULI 4 Watu wanaoishi na VVU na watu wengine walio katika mazingira hatarishi ya kupata VVU wanakabiliwa na changamoto nyingi za kijamii na kisheria. Hivyo, ni muhimu kwa wanasheria na wasomi wa sheria kushiriki kikamilifu katika shughuli za mwitikio wa kitaifa wa kupambana na maambukizi ya VVU. Lengo la kitabu hiki ni kuwasaidia wahadhiri wa fani ya sheria, mameneja wa kliniki za msaada wa kisheria na wanafunzi wa sheria nchini Tanzania kushiriki kikamilifu katika programu za mwitikio wa kitaifa juu ya UKIMWI. Mwitikio wa kitaifa unajumuisha kutoa ushauri wa kisheria unaohusiana na VVU, kuendesha mashauri yanayohusiana na uvunjifu wa haki za watu wenye VVU katika vyombo vya utoaji haki; kufanya tafiti zinazohusiana na masuala ya sheria, haki za bianadamu na VVU; na kuishauri serikali kuhusiana na uundwaji wa sheria zinazosimamia VVU pamoja na utekelezaji wa sheria zenyewe. Kitabu hiki kinaainisha changamoto zilizopo katika kutoa huduma za msaada wa kisheria kwa watu waishio na VVU na makundi ya watu walio katika hatari ya maambukizi ya VVU. Kinasisitiza masuala ya kisheria na sera ambayo wanasheria, wakufunzi wa sheria, mameneja wa kliniki za msaada wa kisheria na wanafunzi wanaweza kukabiliana nazo wakati wa kuchangia utaalamu wao wa kisheria katika jitihada za kutoa huduma kwenye muitikio wa kiataifa wa kupambana na VVU. Kitabu hiki, pia ni nyenzo muhimu ambayo wanajamii wanaweza kuitumia ili kuwa viongozi mahiri katika masuala ya utoaji wa huduma za msaada wa kisheria katika kuendesha mashauri ya kisheria, pamoja na marekebisho ya kisheria na sera ili kuendeleza matokeo bora ya mwitikio wa kitaifa wa kupambana na VVU nchini Tanzania.


MAELEZO YA UTANGULIZI 5 Vyuo vikuu vinapaswa kuongoza washirika wengine katika suala la muitikio wa kitaifa kupamabana na maambukizi ya VVU na UKIMWI. Katika vyuo vikuu, hasa, shule ama vitivo vya sheria – wakufunzi, jumuiya za kitaaluma na za wanafunzi, lazima waelimishwe masuala yahusuyo VVU na UKIMWI na washiriki kikamilifu katika juhudi hizi. Jumuiya za manafunzi mara nyingi hujumuisha idadi kubwa ya vijana wenye umri mdogo ambao mara wapo kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa VVU. Kutokana na kuenea kwa VVU katika nchi yetu, kuna uwezekano mkubwa kuwa wapo wakufunzi wanaoishi na VVU ama wenye jamaa au wanafamilia ambao wanaishi au kuathiriwa na VVU. Hivyo basi, vyuo vikuu vinawajibika kujengea wanafunzi uwezo kama wahitimu wa taaluma ya sheria, ili kukabiliana na VVU na pia kutambua na kuunga mkono juhudi za jamii yetu hasa za watu wanaoishi na VVU na athari zake. Kama Mwongozo huu unavyoonyesha, sheria ina nafasi kubwa katika suala la mwitikio wa kitaifa juu ya VVU. Vyuo vikuu, na hasa shule ama vitivo vya sheria, wana wajibu wa kuhakikisha kuwa wakufunzi na wahitimu wana ujuzi wa kutafiti, kufundisha na hata kushauri jamii juu ya masuala ya kisheria yanayohusiana na VVU. Mwongozo huu sio tu unabainisha mambo muhimu kisheria kitaifa, bali pia umeyabainisha mambo hayo katika muktadha wa sheria na sera za kimataifa. Hata hivyo, mwongozo mmoja, hata kama ungekua na mapana kiasi gani hauwezi kushughulikia masuala yote yenye changamoto kwenye eneo la sheria na sera za VVU. Hivyo basi, tunatarajia kuwa mwongozo huu utakua ni chachu ya tafiti nyingine katika sheria za jinai, sheria za familia, sheria ya kikatiba na utawala, sheria ya kimataifa na haki za binadamu, afya na maeneo mengine ya kisheria yanayohusiana moja kwa moja na janga la VVU na UKIMWI. Utafiti huu utaonyesha tena umuhimu wa sheria katika kukabiliana na changamoto kubwa za kijamii kama za usawa, ukosefu wa haki na ubaguzi. Zaidi sana mwongozo huu utakua chachu ya utoaji wa huduma bora za msaada wa kisheria katika kliniki za misaada ya kisheria. Muongozo huu utajenga utajenga utamaduni makundi yote katika jamii zetu ni muhimu na sehemu ya ulinzi na uendelezaji wa haki za binadamu. Kwa hiyo tunapendekeza muongozo huu kwa wafanyakazi wetu wa kitaaluma, wanafunzi wa sheria na kwa jumuiya nzima ya Chuo Kikuu. Kwa hakika muongoz huu ni chombo cha ziada na rasilimali muhimu katika jitihada za kupambana na VVU na UKIMWI nchini Tanzania.

Prof. Hamudi Majamba Dean - School of Law University of Dar es Salaam, Tanzania

Mr. Victorino Kuluchumila Dean - School of Law University of Dodoma, Tanzania


TAFSIRI YA MANENO 6 ACHPR

Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu

UKIMWI

Upungufu wa Kinga Mwilini

ARV

Vidonge vya Kuongeza Kinga

HAART

Tiba ya kupambana na virusi vya ukimwi

HAPCA

Sheria ya Kuzuia na Kupambana na VVU na UKIMWI

VVU

Virusi Vya Ukimwi

IDLO

Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Sheria

ILO

Shirika la Kazi la Kimataifa

KVP

Kundi la Watu Maalum

MSM

Wanaume wanaojamiiana na Wanaume

PWID

Watu wanaojidunga Sindano za Madawa ya Kulevya

PLHIV

Watu wanaoishi na VVU

PMTCT

Kuzuia maambukizi toka kwa mama kwenda kwa mtoto

SDG

Mpango wa Maendeleo Endelevu

STI

Magonjwa ya Zinaa

TACAIDS

Tume ya UKIMWI Tanzania

UN

Umoja wa Mataifa

UNAIDS

Mpango wa Umoja wa Mataifa wa UKIMWI


7

SEHEMU YA 1

UELEWA WA TATIZO


1.1 JE, VVU NA UKIMWI NI NINI? 8 VVU ni virusi ambavyo hushambulia mfumo wa kinga ya mwili wa binadamu. Kama havikupatiwa tiba, mtu aliyeambukizwa VVU anaweza kupata UKIMWI, ambao ni kundi la maambukizi na magonjwa yanayotishia maisha. Mgonjwa wa kwanza wa UKIMWI alitambuliwa nchini Marekani mwaka 1981, na kirusi kijulikanacho kama VVU kilijulikana mwaka 1985. Kwa sasa VVU vimeenea duniani kote, na huathiri watu wa matabaka yote, jinsia, mwelekeo wa kijinsia na kabila. 1 VVU huambukizwa kwa njia kuu zifuatazo: • Kujamiana bila kutumia kinga (yaani bila kutumia kondomu). • Matumizi ya damu kupitia uchangiaji damu, isiyo salama, matumizi ya sindano za madawa ya kulevya au kwa kutumia mabomba ya sindano yaliyotumiwa na waathirika, uwekewaji damu au uzembe katika huduma za afya. • Maambukizi ya wima (yaani kutoka kwa mama kwenda kwa kiumbe kilicho tumboni mwa mama (mtoto), kabla au wakati wa kuzaliwa, na kunyonyesha kwa mama aliye na maambukizi). VVU inaweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi mwingine kwa njia mbalimbali ya vimiminika mwilini: damu, shahawa (ikiwa ni pamoja na majimaji yatokayo kabla ya kufika kileleni), majimaji ya uke, majimaji ya haja kubwa na kunyonyesha maziwa. Mtu hawezi kuambukizwa VVU kwa njia za kawaida za kugusana au mawasiliano ya kawaida ya kijamii (k.m. kushikana mikono, au kuchangia vyakula au vinywaji); kwa hiyo, hakuna uwezekano au hatari ya kuambukizwa VVU kwa wanafunzi wa chuo kikuu au wafanyakazi katika kutoa ushauri na huduma za kisheria kwa watu wanaoishi na VVU. Tiba dhidi ya virusi vya ukimwi (ARV/HART) ambayo inahusisha mchanganyiko wa madawa matatu tofauti ya ARV huzuia VVU kuzalishwa, na huruhusu mfumo wa kinga kuzuia au kurejesha nguvu na kumfanya mtu awe na afya. Ingawa HAART haiui au kukomesha VVU, sasa inakubalika kuwa watu waishio na virusi vya ukimwi wanaotumia Miongozo ya usimamizi wa kliniki ya VVU, ikiwa ni pamoja na mapendekezo kuhusu matibabu ya ARV. Miongozo hiyo pia inatoa mapendekezo kwa makundi maalum (k.m. watoto wachanga na watoto, wanawake wajawazito, au wanaume wanaojamiiana na wanaume) na mazingira maalum (k.m. mipangilio mindogo ya rasilimali); kwa mfano, WHO imetoa miongozo juu ya lini wataaanza tiba ya kupambana na VVU na kuzuia maambukizi ya VVU kabla ya kujifungua (2) 1

ARV na ambao VVU vimefubazwa kutokana na matumizi ya dawa za ARV, hawana virusi vya VVU katika damu yao na hawawezi kuambukiza VVU kwa kiwango kikubwa cha mpaka asilimia 94% kwa njia ya kujamiiana.

1.2 EPIDEMIOLOJIA YA VVU NCHINI TANZANIA Kwa mujibu wa ripoti ya UNAIDS, mwaka 2016 watu milioni 1.4 waliishi na VVU nchini Tanzania (Bara) ambao ni karibu ya asilimia 4.7 ya idadi ya watu. Kwa hiyo, mwaka 2016 pekee,watu 55,000 waliambukizwa VVU na watu 33,000 walikufa kutokana na magonjwa yanayohusiana na UKIMWI nchini. Mkakati wa Taifa wa VVU na UKIMWI (Tanzania Third National Multi-Sectorial Strategic Framework for HIV and AIDS (2013/14–2017/18)) ulitoa picha kamili ya VVU katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Viashiria kadhaa vya kitabia, kijamii, kiutamaduni na kitabibu huchangia katika kusababisha janga hili (6: p 14):

• Sababu za kitabia - Mahusiano mbalimbali ya kingono bila kutumia kinga - Uhusiano wa kijinsia/ngono wa kizazi kimoja au tofauti. - Ngono katika umri mdogo. - Biashara ya ngono. - Unywaji pombe. - Viwango vya chini vya matumizi ya kondom na utumiaji mbovu wa kondom. - Ngono kinyume na maumbile na zisizo na kinga.

• Sababu za kijamii, kitamaduni - Unyanyapaa na ubaguzi. - Athari zitokanazo na Uhamiaji. - kutokuwa na usawa wa kijinsia. - Ukosefu wa usawa na umaskini.


9 • Sababu za Kitabibu: - Viwango vya chini vya tohara kwa wanaume. - kutokuwa na huduma bora, sahihi na salama katika uchangiaji wa damu - matumizi ya sindano zisizo salama katika huduma za afya. - Kuenea kwa magonjwa ya zinaa . - Maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto. - Viwango vya juu vya kutokuwa wawazi (yaani mpenzi mmoja ana VVU na mwingine hana VVU). - Kiwango cha chini cha uelewa juu ya serostatus ya VVU


10

SEHEMU YA PILI

VVU, HAKI ZA BINADAMU NA SHERIA


11 Umoja wa mataifa (UN) una malengo makuu endelevu ya maendeleo (SDGs) 17 yenye malengo 169, na nchi wanachama 191 wa umoja wa mataifa (UN), wamekubaliana kufikia malengo hayo mwaka 2030. Lengo la 3, juu ya masuala ya afya, na linalenga maisha yenye afya na kukuza ustawi kwa wote, katika kipindi chote. Lengo dogo la 3 katika lengo kuu la 3 linalenga kumaliza maambukizi ya UKIMWI, kifua kikuu (TB), malaria na magonjwa ya kitropiki, na kupambana na ugonjwa wa ini, magonjwa yatokanayo na maji na magonjwa mengine ya kuambukiza. Kumaliza UKIMWI mwaka 2030 kutafanikiwa tu kama malengo madogo yatafikiwa kufikia mwaka 2020. Katika hali hii, mpango wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI (UNAIDS) uliunda mkakati wa mwaka 2016-2021 wa kuharakisha ufuatiliaji na kukomesha mlipuko/maambukizi ya UKIMWI. Mkakati huu unaainisha maeneo nane kwa ajili ya kuhakikisha kuwa ugonjwa wa UKIMWI hauwi tishio kwa afya ya jamii kufikia mwaka 2030: • Watoto, vijana na watu wazima waishio na VVU wanapata huduma ya upimaji, wanajua hali zao na kwa haraka kupata huduma stahiki za afya na kubaki katika huduma hizo. • Kuondolewa kwa maambukizi mapya ya VVU kwa watoto na kuimarika kwa afya na ustawi wa mama. • Vijana wadogo, hususani wanawake wadogo na wasichana vijana, kupata huduma za pamoja za kuzuia maambukizi na kuwezeshwa kujikinga na VVU wao wenyewe. • Kusaidia upatikanaji wa huduma ya pamoja ya kuzuia VVU kwa jamii lengo likiwa ni pamoja na wanaofanya biashara ya ngono, wanaume wanaoshirikiana na wanaume wenzao kingono, watu wanaojidunga madawa ya kulevya, watu waliobadili jinsia, wafungwa na wahamiaji. • Wanawake na wanaume kupata mafunzo na kukuza kanuni nzuri za kijinsia, kufanya kazi pamoja ili kukomesha unyanyasaji wa kijinsia na vurugu baina ya wapenzi. • Kuondolewa kwa sheria za adhabu, sera, tamaduni, unyanyapaa na ubaguzi ambazo si rafiki katika kupambana na VVU (k.m. adhabu kwa ujumla katika kusambaza VVU, vikwazo vya usafiri, upimaji wa lazima na kuzuia walengwa kupata huduma)

• Huduma za VVU na afya zinazozingatia hali za watu na kuunganishwa katika mazingira ya mifumo yenye nguvu ya afya (k.m. mipango ya utoaji wa afya duniani kote inayozingatia VVU).

Katika mkakati wake, UNAIDS imesisitiza zaidi kwa kusema kwamba sheria za adhabu, sera na taratibu zetu vimeendelea kukiuka haki za binadamu na kudumisha mtazamo ambao huacha idadi ya watu bila kupata huduma za VVU. Ubaguzi unaohusiana na VVU mara kwa mara huingiliana na aina nyingine za ubaguzi kutokana na jinsia; mwelekeo na utambulisho wa jinsia; utaifa; ulemavu; matumizi ya madawa ya kulevya; hadhi ya uhamiaji; biashara ya ngono au kuwa mfungwa. Ukiukwaji wa haki za wanawake, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa wanawake, umeendelea kuwaweka wanawake na wasichana katika mazingira magumu na hatarishi zaidi ya kupata maambukizi ya VVU na hata kuwazuia kupata huduma na tiba. Hali hii imeimarishwa zaidi na sheria pamoja na taratibu za kibaguzi zinazomzuia mwanamke kupata haki ya usawa katika kufanya maamuzi, kupata elimu, ajira, kumiliki mali na uhuru.

Ulinzi dhidi ya ubaguzi Moja ya hatua za kisheria za ufanisi zaidi ambazo zinaweza kuzuia kuenea kwa VVU ni ulinzi dhidi ya ubaguzi wa watu wanaoishi na/au walioathirika na VVU, na wale walio katika hatari zaidi ya maambukizi. Ulinzi huo unaweza kupatikana kwa kuheshimu haki za binadamu, utu na fursa sawa kwa wote, ikiwa ni pamoja na kuzuia na kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu, na kuhakikisha upatikanaji wa huduma za kisheria. VVU haienei kirahisi; hinyo, ubaguzi katika kupata ajira, makazi, elimu na huduma zingine haziwezi kuharamishwa kwa misingi ya kulinda afya ya umma.


12

2.1 KUJUA/KUELEWA SHERIA KAMA INAHUSIANA NA VVU KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 2.1.1 Sheria za Kimataifa na za Kikanda

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi mwanachama wa Umoja wa Mataifa, Umoja wa Afrika, Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika na Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa hivyo, inafungwa na inapaswa kuwa na mwongozo unaofuata wajibu na utaratibu unaokubalika kimataifa katika kukuza, kulinda na kutekeleza haki za watu waishio na VVU na za makundi maalum. 1

Mwongozo wa kitaifa ya VVU kwa ajili ya huduma kamili ya VVU kwa watu muhimu na walio na mazingira magumu (9) hutoa ufafanuzi wa watu muhimu na watu walio na mazingira magumu katika, Mkakati wa sekta ya afya wa WHO juu ya VVU / UKIMWI 2011- 2015. Angalia pia miongozo ya WHO ya Kuzuia VVU, utambuzi, matibabu na huduma kwa watu muhimu (10). Watu muhimu humaanisha vikundi ambavyo, vipo katika hatari kubwa ya kupata VVU kutokana na tabia na mienendo yao, bila kujali aina ya ugonjwa au mazingira ya ndani. Pia, watu hawa muhimu mara nyingi hukabiliwa na masuala ya kisheria na kijamii kuhusiana na tabia zao zinazoongeza hatari ya VVU. Miongozo ya WHO inazingatia watu watano muhimu: MSM, PWID, watu katika magereza na mazingira mengine ya kufungwa, wafanyakazi wa ngono na watu wa transgender. Watu hawa ni muhimu katika mabadiliko ya VVU. Pia, ni washirika muhimu katika kupambana na janga hili. Watu muhimu ni makundi ya watu ambao kwa hali fulani au mazingira huathirika zaidi na maambukizi ya VVU; wanajumuisha vijana (hasa wasichana vijana katika nchi za Afrika za Kusini mwa Jangwa la Sahara), yatima, watoto wa mitaani, watu wenye ulemavu, wahamiaji na wafanyakazi wa mitandao ya simu.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haizipokei na kuzitumia sheria za kimataifa moja kwa moja ndani ya mipaka yake; kwa hiyo, mikataba yote na sheria nyingine za kimataifa zinapaswa kuhalalishwa na kuingizwa rasmi ndani ya mfumo wa kisheria wa Tanzania kabla hazijatumika rasmi katika mfumo wetu wa kisheria. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 63 (3) (e) 2 inalipa Bunge uwezo wa kupitia na kuthibitisha mikataba na makubaliano yote ya kimataifa ambayo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni mwanachama. Mahakama katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina uhuru mkubwa wa sio tu kutumia sheria za kimataifa kama nyenzo za tafsiri katika maamuzi ya mashauri mahakamani lakini pia kutumia kanuni zilizotajwa katika mikataba na kesi nyingine za kigeni. Jedwali 2.1 linaainisha wajibu wa kimataifa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika mazingira ya VVU na UKIMWI. 3

1

2

3

Ibara ya 63 (3) ya Katiba ya Jamhuri ya Tanzania. Angalia; machapisho kutoka UNAIDS (12), na Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Haki za Binadamu (13)


13 Jedwali 2.1.

Majukumu ya Tanzania kimataifa na kikanda katika mazingira ya VVU na UKIMWI


14

Nyaraka nyingine za kimataifa na kikanda zinazohusiana na VVU/ UKIMWI, zisizokuwa na nguvu kisheria kwa nchi wanachama ni pamoja na; 1. Taarifa ya Kisiasa ya Umoja wa Mataifa kuhusu VVU / UKIMWI, 2016, ambayo inaziataka nchi wanachama kujizatiti katika mikakati ya VVU na UKIMWI inayokuza na kulinda haki za binadamu, kuwa na usawa wa kijinsia, kurekebisha sheria zisizofaa na kushughulikia mahitaji maalum ya watu walioathirika. 2. Maafikiano ya Halmashauri za Haki za Binadamu juu ya VVU na UKIMWI, ikiwa ni pamoja na kuhamasisha ufutaji wa sheria za adhabu ambazo ni kikwazo katika kupambana na VVU. 1 3. Mwongozo wa Kimataifa kuhusu VVU / UKIMWI na haki za binadamu, hutoa mwongozo na kuainisha wajibu wa kimataifa wa kisheria unaosaidia katika kutengeneza sheria za nchi na taratibu za kuthibiti VVU na UKIMWI. Miongozo hii inatoa mwelekeo maalum juu ya (a) kuundwa kwa vyombo yenye ufanisi vitakavyosimamia hatua za Taifa katika VVU na UKIMWI; (b) kutungwa kwa sheria zinazolinda haki za msingi za binadamu, kupunguza hatari ya VVU na kupunguza athari za VVU katika maisha ya watu; na (c) kukuza upatikanaji 1 Azimio A / HRC / 16/28 (2011). http://www2.ohchr.org/english bodies/hrcouncil/docs/16session/A.HRC.RES.16.28_en.pdf

wa haki kwa njia ya kampeni ya kuelimisha kisheria, huduma za kisheria, ufuatiliaji na utekelezaji wa haki za binadamu. 4. Agenda ya Maendeleo Endelevu ya 2030, na Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs). Malengo muhimu kwa VVU na UKIMWI ni Lengo 1 – Kumaliza umasikini; Lengo la 2 kumaliza njaa; Lengo la 3 afya bora na ustawi; Lengo la 5 - Usawa wa kijinsia; Lengo la 6 - maji safi na usafi wa mazingira; Lengo la 8 – kazi za heshima na ukuaji wa uchumi; Lengo la 10 – kupunguza matabaka; Lengo la 16 Amani, haki na taasisi imara; na Lengo la 17 – uhusiano katika malengo. 5. Azimio la Abuja la mwaka 2001 na mpango wa utekelezaji wa VVU / UKIMWI, Kifua Kikuu na Magonjwa mengine yanayohusiana na Ugonjwa wa UKIMWI, hutaka nchi wanachama kutoa kipaumbele katika mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI, na kutambua athari za kutokuwa na usawa wa kijamii na kiuchumi kwa wanawake na wasichana, vile vile madhara na vikwazo vinavyotokana na unyanyapaa, ukimya, kukataliwa na ubaguzi. Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pia imejitolea kugawa angalau 15% ya bajeti ya Taifa (0.7% ya pato la taifa) ili kuboresha sekta ya afya.


15 6. Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu juu ya VVU / UKIMWI mwaka 2001, hutambua VVU kama suala la haki za binadamu, na inazitaka nchi wanachama wa jumuiya kuhakikisha ulinzi wa haki za binadamu katika mapambano dhidi ya VVU. 7. Mkutano wa Bunge la Maendeleo la nchi za Afrika ya Kusini mwaka 2008 SADC PF (SADC PF) kuhusu VVU na UKIMWI. Nchi za Afrika ya Kusini zilitoa sheria ya mfano juu ya VVU na UKIMWI kwa ajli nchi za Africa ya Kusini SADC. 8. Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR) mwaka 2001, Azimio la ACHPR / Res. 53 (XXIX) 01 juu ya janga la VVU / UKIMWI - Tishio dhidi ya Haki za Binadamu na Ubinadamu (Azimio 53). Azimio hili linatambua VVU kama suala la haki za binadamu, na kuzitaka serikali za Kiafrika na nchi wanachama wa mkataba huu kutenga rasilimali za kitaifa zinazoonesha uamuzi wa kupambana dhidi ya kuenea kwa VVU, kuhakikisha ulinzi wa haki za binadamu dhidi ya ubaguzi wa watu waishio na VVU, kutoa misaada kwa familia kwa huduma ya wale wanaokufa kutokana na magonjwa yanayohusiana na UKIMWI, kuandaa mipango ya elimu ya afya ya umma na kuelimisha umma, hasa katika upimaji wa VVU wa bila malipo na hiari na njia sahihi za matibabu. ACHPR pia ilipitisha nyaraka zifuatazo: a. ACHPR / Res. 141 juu ya upatikanaji wa Afya na Madawa yanayohitajika Afrika. b. ACHPR / Res. 260 juu ya ufungaji vizazi usio hiari na Ulinzi wa Haki za Binadamu katika Upatikanaji wa Huduma za VVU.

c. ACHPR / Res. 163 juu ya Uanzishwaji wa Kamati ya Ulinzi wa Haki za Watu Wanaoishi na VVU na wale walio katika hatari na walioathirika na VVU, kwa mamlaka ya kukuza na kulinda haki. d. Kipindi cha kawaida cha 61 cha ACHPR cha Novemba 2017 huko Banjul, Gambia, ACHPR ilizingatia na kuchukua tafiti juu ya VVU, sheria na haki za binadamu katika mfumo wa haki za binadamu wa Afrika, tangu kuchapishwa na UNAIDS.

2.2 KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, 1977 Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1997 ina haki za binadamu kwa wote katika Sehemu ya III, ambayo hutoa haki na wajibu wa msingi. Katiba inalenga kujenga taifa la watu sawa na huru wanaofurahia uhuru, haki, undugu na ushirikiano kwa misingi ya sera ya ujamaa na kujitegemea, wakati inahakikisha heshima na utu wa binadamu na kuzingatia haki za binadamu. Inakataza aina zote za ubaguzi, ama kwa kutunga sheria za moja kwa moja, au vitendo na mienendo ya kibaguzi. Hata hivyo, Ibara ya 7 (2) inasema kuwa- ni wajibu na majukumu ya serikali na viungo vyake vyote na watu wake wote au mamlaka zake kutekeleza majukumu ya kiutendaji, sheria au mahakama katika kuchunguza masharti yaliyotajwa hapo juu. 1

1 Ibara ya 7(2) ya katiba ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania; mashariti ya sehemu hii ya sura hii hayatatiliwa nguvuya kisheria na mamlaka yoyote. Mahakama yoyote nchini haitakuwa na uwezo wa kuamua juu ya suala kama kutendaau kukosa kutenda jambo kwa mtu au Mahakama yoyoteau kama sheria, au hukumu yoyote, inaambatana na masharti au sehemu hii ya surahii.


16 Katiba kwa ujumla inalinda watu waishio na VVU na Makundi Maalum pamoja na haki zao. Jedwali 2.2 linaonesha baadhi ya ibara za Katiba ya Jamhuri

Jedwali 2.2.

ya Muungano ya Tanzania ambazo ni muhimu sana katika utekelezaji wa haki zinazohusiana na VVU.

Muhtasari wa ibara husika za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zinazohusika katika kutambua haki zinazohusiana na VVU


17

Ibara ya 29 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inasema kwamba haki zote hapo juu ni kwa ajili ya watu wote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ibara ya 30 inaelezea mazingira ambayo haki zinaweza kuwa na ukomo. Haki haziwezi kutumika katika namna ambayo itasababisha muingiliano na kupunguza haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya umma.

2.3 SHERIA YA KUZUIA NA KUDHIBITI VVU NA UKIMWI, 2008 Mnamo Februari 2008, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lilipitisha Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti VVU na UKIMWI (HAPCA), No. 28 ya 2008 (26). Sheria hii inatoa mwelekeo wa kitaifa wa kuzuia maambukizi, kutoa matibabu, huduma,


18 msaada na udhibiti wa VVU na UKIMWI, na namna ya kukuza afya ya umma inyohusiana na VVU na UKIMWI. Pia imezungumzia matibabu, huduma na msaada sahihi kwa kutumia rasilimali zilizopo kwa watu wanaoishi na VVU au walio katika hatari ya kupata VVU na UKIMWI. Baadhi ya masharti (vifungu) muhimu katika sheria hii ni: • Wajibu wa kukuza na kulinda haki zinazohusiana na VVU; kwa mfano, haki ya kupima, matibabu, faragha na usiri, kutokuwa na ubaguzi / upendeleo na upatikanaji wa huduma za msingi za afya. • Wajibu wa watu binafsi; kuhamasisha na kupunguza uenezi wa VVU na UKIMWI. • Kuzuia upimaji wa lazima wa VVU, na utoaji taarifa wa matokeo ya kupima VVU, unyanyapaa na ubaguzi. • Uwepo wa makosa ya uvunjaji wa siri, kueneza VVU na vitendo vinayosababisha kuenea kwa VVU. Sheria imetengeneza vifungu ya kisheria na kimaadili kuongoza suala la VVU katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Masharti haya yanahusu kibali cha kutoa na kupata habari juu ya matibabu sahihi ya VVU, faragha na siri, kama ilivyojadiliwa hapa chini.

2.3.1 Kibali cha Habari Upimaji wa VVU ni tofauti na vipimo vingine vya damu kwa sababu husababisha madhara makubwa ya kisaikolojia, kama kukataliwa na familia, ubaguzi katika ajira, kuzuiwa au kutokupata huduma za afya, na vizuizi na kunyimwa bima. Kwa kutambua mazingira hapo juu, na kuhamasisha upimaji na matibabu, watoa huduma wanahitajika kupata kibali kwa ajili ya kupima VVU. Sehemu ya 15 ya HAPCA inakataza upimaji VVU wa lazima. Ili kupima watoto idhini ya maandishi

inatoka kwa wazazi au mlezi anayejulikana. Hata hivyo, idhini haitatakiwa ikiwa upimaji wa VVU unatokana na : (a) amri ya mahakama, (b) uchangiaji viungo vya binadamu na tishu, na (c) wahalifu wa kijinsia. Sehemu hii inaelezea zaidi kwamba wanawake wote wajawazito, na wanaume wanaohusika na mimba, na wapenzi na watu wote wanaohudhuria kituo cha huduma za afya watapewa ushauri nasaha na kushauriwa kupima kwa hiari. 1

2.3.2 Faragha na Usiri Ibara ya 16 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathibitisha haki ya faragha na usalama binafsi. Katika mazingira ya kimatibabu na ya kisheria, taarifa nyingi za kimatibabu hupaswa kuwa siri. Hata hivyo, kwa sababu ya uelewa wa taarifa zinazohusiana na VVU, ni muhimu kwa wale wanaotoa huduma zinazohusiana na VVU kuhifadhi kumbukumbu za matibabu zinazohusiana na VVU. Sehemu ya 16 ya HAPCA inathibitisha usiri wa matokeo ya kupima VVU na matokeo hayo hutolewa tu kwa mtu husika aliyepimwa. Hata hivyo, imetoa mazingira nyeti ambapo matokeo ya kupima VVU yanaweza kutolewa kwa mtu mwingine, mazingira hayo ni kama yafuatayo: (a) katika mazingira ya mtoto, taarifa hupewa mzazi wake au mlezi anayetambuliwa, (b) kwa mtu asiye na uwezo wa kuelewa matokeo, taarifa atapewa mwenzi wake au mlezi anayetambulika, (c) mke au mwenzi au mshiriki wa kingono wa mtu aliyepimwa VVU, au (d) mahakama, kama itahitajika. Kifungu cha 17 2 kinaelezea pia siri ya matibabu, hasa utambulisho na hali ya watu wanaoishi na VVU na UKIMWI. Kinyume chake, kifungu cha 18 3 cha HAPCA hutoa matukio ambapo usiri unaweza kuvunjwa, ikiwa ni pamoja na kutoa ripoti za kitabibu serikalini, wanaotoa huduma za matibabu, na mahakamani katikakesi za kisheria.

1

2

3

Kwa rejea zaidi, angalia miongozo mbalimbali ya taifa na taratibu za kuendeshaji (27-29) Kifungu cha 17 cha sheria ya kupambana na kuthibiti VVU na UKIMWI ya mwaka 2008 Kifungu cha 18 cha sheria ya kupambana na kuthibiti VVU na UKIMWI ya mwaka 2008


19 Taratibu za kiuendeshaji za kupima VVU na huduma za ushauri huelezea kuwa: • Utoaji wa majibu yatokanayo na kupima VVU kwa mtu mwingine utafanyika ikiwa kuna idhini ya kimaandishi kutoka kwa mtu aliyepima VVU. • Ushauri utatolewa kwa faragha ambapo mazungumzo kati ya mteja na mshauri hayawezi kusikika. • Hali ya mgonjwa haitakiwi kuwekwa wazi baina ya washauri na wafanyakazi wenzake. Vilevile taratibu hizo zimeelezewa katika miongozo ya kitaifa juu ya VVU na UKIMWI, na kuzuia maambukizi ya VVU kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (27, 28). Vifuatavyo ni baadhi ya vifungu vya Sheria vinavyochukuliwa na watu waishio na VVU na wanaharakati kama ni vya kibaguzi.

Taarifa ya lazima kwa wenza juu ya hali ya VVU: Kifungu cha 21 Kifungu cha 21 1 kinatoa ulazima kwa mtu yeyote anayefahamu kuwa ni mwathirika wa VVU kumpa taarifa mwenza wake au mshirika mwenzake wa kingono juu ya hali yake ya maambukizi ya VVU, na kuchukua hatua stahiki ili kuzuia maambukizi. Kuna wasiwasi kuwa kifungu hiki kinaweza kuwa kisababishi cha watu kuepuka kupima VVU kwa kuhofia kutoa taarifa zao haraka za hali ya VVU mara baada ya kugundua kuwa ni waathirika wa VVU. (30: p 67). UNAIDS huhimiza utoaji wa taarifa wa hiari, huheshimu uhuru na utu wa waathirika, huzingatia usiri, na hutegemea manufaa stahiki kwa waathirika na wapenzi.. Utoaji huo wa taarifa unapaswa kuzingatia maadili ili kuwanufaisha wote waathirika na wasio waathirika.

1

Kifungu cha 21 cha sheria ya kupambana na kuzuia VVU na UKIMWI ya mwaka 2008

Mwaka 2010, Taratibu za VVU na UKIMWI (Ushauri na Upimaji, Matumizi ya ARV na Utoaji taarifa) ilianza kutumika. Nyaraka hii huelezea kanuni za kutoa ushauri na upimaji wa VVU, ulinzi dhidi ya upimaji wa kulazimishwa, usiri na ulinzi dhidi ya utoaji taarifa wa lazima.

Kusambaza / kuambukiza VVU kwa makusudi: kifungu cha 47 Kifungu cha 47 cha HAPCA kimeweka kosa la maambukizi ya VVU kwa makusudi. 2 Kisheria, kosa la maambukizi VVU kwa makusudi linahitaji kuthibitisha maambukizi ya VVU na dhamira ya kuambukiza VVU, ambapo inatakiwa kuthibitishwa kuwa mtuhumiwa alifahamu kuwa ni mwathirika wa VVU, anauelewa wa jinsi alivyoambukiza VVU na kwamba lazima kuwe na maambukizi kwa kufanya ngono na mtu asiyefahamu kama mtuhumiwa ni mwathirika wa VVU na hakutumia hatua yoyote za kinga (kwa mfano matumizi ya kondomu), na kwamba mtuhumiwa ndiye mtu pekee aliyeweza kuambukiza VVU kwa mlalamikaji. Kifungu hiki kama kilivyo ni cha kiadhabu na kuendelea kuwepo kwake kunaweza kusabisha watu kutopima na kujua hali zao za kiafya, kwa sababu mtu kufahamu hali yake kunaweza muweka katika mashitaka. Tume ya Kimataifa ya VVU na Sheria, katika Ripoti yake ya 2012 kuhusu VVU na sheria (33) 3, ilibainisha kuwa sheria kama zilivyoelezewa hapo juu si za haki, si rafiki kimaadili na haziwezi kutekelezwa katika hali yoyote ile ya kiusawa. Sheria haizingatii mafanikio ya tiba katika kupunguza ukubwa wa hatari za maambukizi. Mwaka 2013, UNAIDS ilitoa mwongozo wake wa Kuondoa makosa yanayohusiana na VVU, taarifa na maambukuzi: masuala muhimu ya kisayansi, kimatibabu na kisheria.

2

3

Kifungu cha 47 cha sheria ya kupambana na kuzuia VVU na UKIMWI ya mwaka 2008 Tume ya Kimataifa ya VVU na Sheria, ilizinduliwa mwezi Juni 2010 ili kuendeleza mapendekezo yanayoweza kutekelezwa, ushahidi na haki za binadamu ili kuwa na jitihada chanya katika kupambana na VVU zanazolenga kulinda na kukuza haki za binadamu za watu wanaishio na VVU na walio katuka hatari zaidi ya kupata VVU.


20 Mwongozo huu unashauri nchi: • Kuzingatia juhudi za UNAIDS za kupanua matumizi ya ushahidi uliothibitishwa na kufanikiwa na haki zinazozingatia utaratibu wa haki za umma wa kuzuia VVU, matibabu na huduma. • Kupunguza matumizi yoyote ya sheria ya makosa ya jinai kwa kesi zenye malalamiko ya ukweli ikiwa kuna uhitaji wa kufikia haki.

Upimaji wa wanawake wajawazito: Sehemu ya 15 (5) Katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kama ilivyo katika nchi nyingi za Kiafrika za Kusini mwa Jangwa la Sahara, wanawake wajawazito wanatarajiwa na kuhimizwa kupima VVU ili kuhakikisha hali yao ya VVU kwa ulinzi wa kiumbe na kukikinga na maambukizi. Wanawake wajawazito na wenzi wao wa ndoa hupata huduma za ushauri na baada ya hapo hupimwa VVU kwa hiari kama ilivyo katika kifungu cha 15 (5) cha HAPCA.1 Wizara ya Afya imeanzisha miongozo ya kutoa huduma na matibabu ya wanawake wajawazito waishio na VVU, ikiwa na lengo la kupunguza maambukizi ya VVU kutoka kwa mama hadi kwa mtoto.2 Hata hivyo, kama ilivyoelezwa katika Ripoti ya tathmini ya mazingira ya kisheria ya kukabiliana na VVU na UKIMWI katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (30), ingawa sheria inaelezea upimaji wa hiari kwa wanawake wajawazito na wenzi wao, mazingira halisi yanaonesha kuwa kupima huku kumechukuliwa kuwa ni lazima. Hii husababisha kunyanyapaliwa kwa wanawake wanaokataa kupima VVU na wahudumu wa afya na kupuuzwa wakati wa kujifungua. Tabia hizi ni za kibaguzi. “Upimaji VVU wa hiari “ una maana ya upimaji huru usio wa kulazimishwa kwa nguvu na ulio na taarifa inayojitoshereza. Kitendo cha kupima wanawake wajawazito VVU bila ridhaa yao na taarifa ni cha kiadhabu na hakipendezi wala si rafiki kwa wanawake, hasa katika kujiandaa kwao kuishi na VVU na utumiaji

1

2

Kifungu cha 15 (5) cha sheria ya kuzuia na kupambana na VVU na UKIMWI ya mwaka 2008 Kifungu cha 25 cha sheria ya kuzuia na kupambana na VVU na UKIMWI ya mwaka 2008

wa dawa za VVU. Pia hukiweka kiumbe katika hatari, ikiwa mama hakujiandaa kisaikolojia dhidi ya matokeo ya kupimwa VVU, ili kuhakikisha kwamba kiumbe kinakingwa na maambukiza wima ya VVU.

2.4 SHERIA YA MAKOSA YA JINAI INAVYOHUSIKA NA VVU KATIKA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Sheria ya makosa ya jinai ni sheria zinazokataza matendo yanayoonekana kuwa kinyume na hatari kwa usalama na ustawi wa umma. Pia zimeanzisha adhabu kwa kila kosa. Baadhi ya makosa hayo yalitengenezwa hata kabla ya uhuru, kabla ya VVU na UKIMWI kugunduliwa, na hayajapitiwa au kurekebishwa kwa kuzingatia mageuzi ya kisayansi na kimatibabu ya ugonjwa wa UKIMWI. Kwa matumizi ya sheria ya jinai kuhusiana na VVU, UNAIDS ilipendekeza kuwa yafuatayo ni lazima kuzingatiwa: (a) inapaswa kuongozwa na ushahidi bora wa kisayansi na wa kimatibabu unaohusiana na VVU; (b) inapaswa kuzingatia kanuni za uhalali wa kisheria na wa kimahakama (ikiwa ni pamoja na kanuni muhimu za uhalali, usahihi, nia, sababu, uwiano na ushahidi); na (c) inapaswa kulinda haki za kibinadamu za wanaohusika katika kesi za jinai (3). Katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, watu wanaoishi na VVU na makundi maalum wapo katika hatari ya kuwa kinyume na sheria kwa sababu ya kuwepo kwa makosa ya jinai yanayoadhibu tabia zao za mathalan kingono na matumizi ya madawa ya kulevya. Kwa mujibu wa (NMSF III) (6: p. 18) , ubaguzi dhidi ya makundi maalum husababisha changamoto kubwa katika upatikanaji wa huduma ya afya.


21 NMSF III pia imekubali kuwa unyanyapaa na ubaguzi ni mkubwa sana dhidi ya watu waishio na VVU ambao ni wafanya biashara ya ngono, wafungwa, watu wa mitaani na wasiokuwa na makazi, watu waliobadili jinsia au watumiaji wa madawa ya kulevya. Hii huleta changamoto kubwa sana kwao ya kutoka na kupokea huduma rafiki ya afya, na hatimaye kupunguza uwajibikaji dhidi ya VVU nchini. Sheria mbalimbali za jinai zina athari mbaya sana kwa watu waishio na VVU na makundi muhimu kama inavyojadiliwa hapa chini.

2.4.1. Kanuni ya Adhabu Sura ya 16, 2002 Kwa Wafanyabiasha wa ngono Kiushi kwa kipato kitokanacho na umalaya na biashara ya ngono si kosa la jinai kwa mujibu wa sheria ya kanuni ya adhabu.Hata hivyo, kwa mujibu wa kifungu cha 139,1146 2 na 148 3 ni kosa la jinai kumchukua au kumtumia mtu kwa madhumuni ya kufanya umalaya/ukahaba. Mwaka 2013, Tume ya Taifa ya Ukimwi Tanzania (TACAIDS) ilibainisha kuwa, ingawa watoa huduma za afya wana mipango ya kuwafikia wafanya biasha ya ngono kwa ajili ya kuwapatia huduma muhimu za afya, polisi wameripotiwa kuingilia programu hizi na kuwakamata wafanyabishara wa ngono. Mtazamo wa watoa huduma ya afya juu ya wafanya biashara wa ngono umezuia utoaji wa huduma za afya na huduma za VVU kwa kundi hili. Kutokuwepo kwa huduma za afya, elimu ya kuzuia VVU na kondomu, inaweza kuwa sababu ya kueneza VVU na magonjwa ya zinaa kwa wafanya biashara wa ngono. Kwa mujibu wa sensa ya watu na Afya ya mwaka 2010, kwa kipindi cha miezi 12 iliyopita zaidi

1 2 3

Kifungu cha 139 cha Kanuni ya adhabu sura ya 16, 2002 Kifungu cha 146 cha Kanuni ya adhabu sura ya 16, 2002 Kifungu cha 148 cha Kanuni ya adhabu sura ya 16, 2002

ya nusu (51.7%) ya wafanya biashara wa ngono wa kike waliripotiwa kunyanyaswa kimwili. Kati yao, 33.3% waliripotiwa kupigwa na wateja wao. Zaidi ya theluthi moja ya wafanya biashara ya ngono wa kike walilazimishwa kufanya ngono. UNAIDS, katika mwongozo wake wa 2014 juu ya Huduma kwa wafanyabiashara wa ngono (37), inashauri serikali kuhakikisha uwepo mkubwa / kamili wa kuzuia VVU, kupata matibabu, huduma na msaada; kutengeneza mazingira ya kuunga mkono na kuimarisha ushirikiano na uwezeshaji wa kiuchumi kwa wafanyabiasha wa ngono; kupunguza hatari na kushughulikia masuala ya kimfumo, ikiwa ni pamoja na kuwezesha mazingira ya kisheria na kisera. Kwa watu wanaofanya ngono kinyume na maumbile (Ikiwa ni pamoja na wanaume wanaojamiana na wanaume) kwa mujibu wa kifungu cha 154 4 cha Kanuni ya Adhabu kufanya ngono kinyume na maumbile ni kosa la jinai kwa wanaume na wanawake. TACAIDS inaeleza kuwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao huofia kukamatwa wanapoudhuria katika vituo vya afya ili kupata huduma za afya na huduma zinazohusiana na VVU (30: p 65). Wanaume hawa pia wanaripoti kwamba utoaji wa taarifa za tabia zao za ngono huwapelekea kunyanyapaliwa na kupata huduma mbaya za matibabu kutoka kwa wahudumu wa afya (30: p 65). Hii hupelekea mazingira magumu kwa wanaume wanaofanya ngono na wanaume wenzao na wanawake wanaofanya ngono na wanaume kinyume na maumbile kupata huduma za afya na huduma za kuzuia VVU, huongeza hatari ya maambukizi ya VVU na kuchochea janga la VVU.

4

Kifungu cha 154 cha Kanuni ya adhabu sura ya 16, 2002


22

2.4.2 Sheria ya Kupambana na Kuzuia Uingizaji Usafirishaji na Utumiaji wa Madawa ya Kulevya Sura ya. 95 Kwa watumiaji wa madawa ya kulevya Kifungu cha 12 (d)1 cha sheria ya madawa ya kulevya, hueleza kuwa ni kosa la jinai kwa mtu yeyote kutumia madawa yoyote yale ya kulevya yaliyotajwa katika sheria ya madawa ya kulevya. TACAIDS inasema kuwa watu wanotumia sindano za madawa ya kulevya wanaweza kuchangia sindao wakati wa kujidunga sindano za madawa ya kulevya, ambapo inahatari kubwa ya maambukizi ya VVU ikiwa mmoja wa watumiaji ni mwathirika wa VVU. UNAIDS, katika mwongozo wake juu ya Huduma kwa watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya (39), hubainisha kuwa – imetoa uelewa mpana wa matumizi ya sindano za madawa ya kulevya na hathari zisizohusiana na VVU kwa watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevyakuzuia VVU na madhara mengine kwa watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya, na kuwapa matibabu fanisi, huduma na msaada ni vipengele muhimu na fanisi vya kitaifa. TACAIDS inasema kuwa upatikanaji wa huduma za afya na VVU kwa watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya ni mdogo, ingawa wafanyakazi wa huduma za afya waliripoti kwa TACAIDS kwamba huduma za kupunguza madhara 2 (ikiwa ni pamoja na kusafisha mabomba na sindano) zilikuwa zikipatikana lakini si kwa kiwango cha kutosha. Polisi wameripotiwa kuwakamata watu wanaojidunga madawa ya kulevya wakipata huduma za afya (30: p 65). Vikwazo katika huduma

1

2

Kifungu cha 12 (d) cha sheria ya kuzuia na kupambana na madawa ya kulevya sura ya 95. Neno “kupunguza madhara” linamaanisha mfuko wa sera, mipango na njia ambazo zinajaribu kupunguza madhara ya afya hatarifu, na madhara ya kijamii na kiuchumi yanayotokana na matatizo ya kifikira. Mfuko unalenga: mipango ya sindano na vifaa vyake; tiba mbadala ya opioid; upimaji VVU na ushauri; Huduma ya VVU na tiba ya kupambana na VVU kwa watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya; kuzuia maambukizi ya ngono; kutembelea jamii ili kupata (taarifa, kutoa elimu na kuzungumza na watu waojidunga sindano za madawa ya kulevya na washirika wao wa ngono); matibabu na chanjo (pale inapowezekana); na kuzuia kifua kikuu, utambuzi na matibabu (40).

za afya na huduma za kuzuia VVU vimewaweka watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU na kuwaambukiza wengine, ikiwa ni pamoja na washirika wao wa ngono. Mwongozo wa mwaka 2014 juu ya Huduma kwa watu wanaojidunga madawa ya kulevya, katika mtizamo wa haki za binadamu, UNAIDS inabainisha mifano hai ya ukiukaji wa haki za binadamu kwa watu wanaojidunga a madawa ya kulevya kama upimaji wa madawa ya kulevya kwa lazima, matibabu ya kulazimishwa na uwekwaji vizuizini. Kwa kuongezea, mara nyingi watu wanaojidunga madawa ya kulevya hawapati huduma za msingi za afya, ama kutokana na kutengwa na watoa huduma wa afya au kwa sababu za kijilinda kutokana na kuwa njia wanazotegemea kwa kujikinga ni kinyume cha sheria. UNAIDS inasisitiza kuwa ni muhimu kuhakikisha kuwa mamlaka za kusimamia sheria na mamlaka ya haki za jinai zinajumuishwa katika majadiliano ya sera na kufahamu haja ya huduma bora za afya kwa watu wanaojidunga madawa ya kulevya (39: p 13) .

2.5 SHERIA YA AJIRA NA VVU Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa haki ya kufanya kazi (Ibara ya 22). Ubaguzi kwa misingi ya VVU mahali pa kazi ni kinyume na kifungu cha 7 (4) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi Namba 8 Mwaka 2006. 3 Kifungu cha 30 (1) cha Sheria ya UKIMWI kinakataza mtu yeyote kubaguliwa katika fursa ya ajira kwa misingi ya hali halisi ya mtu huyo, kuonekana au kuhisiwa na VVU na UKIMWI. Hata hivyo, TACAIDS inasema kuwa waajiri wengine huhitaji upimaji wa VVU kama

3

Kifungu cha 7 (4) cha Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi Namba 8 Mwaka 2006.


23 sharti katika ajira (30, 42). Waajiri wanahimizwa kuzingatia utaratibu bora wa kimataifa ambao unaheshimu haki za binadamu katika kukabiliana na VVU mahali pa kazi. Shirika la Kazi la Kimataifa (ILO), mwaka 2015, liliandaa kitabu cha kusaidia majaji na wataalamu wa kisheria juu ya masuala yanayohusiana na VVU na UKIMWI , kwa kulenga suala la ajira na kazi.1 ILO ilibainisha kuwa unyanyapaa na ubaguzi unaohusiana na VVU hutendeka katika maeneo mengi ya kazi, na kuenea kwa ukiukwaji wa haki za msingi. Vikundi muhimu ambavyo tayari vina hali hiyo vinaweza kukumbana na kiwango cha juu cha unyanyapaa na ubaguzi. Aidha, Pendekezo la ILO No. 200 linatoa wito kwa mamlaka za kitaifa za kimahakama kushiriki katika maendeleo, kupitisha na kutekeleza kwa ufanisi sera na programu za kitaifa na kazi juu ya VVU na UKIMWI, ikiwa ni pamoja na maendeleo na matumizi ya sheria za nchi . ILO pia inasisitiza waajiri kuzingatia taratibu bora za kimataifa ambazo zinaheshimu haki za binadamu katika kukabiliana na VVU mahala pa kazi.

2.6 ARDHI, MALI NA URITHI KATIKA MAZINGIRA YA VVU Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ibara ya 24 imetoa haki ya umiliki wa mali na matumizi, ambayo inahakikisha haki ya umiliki binafsi wa mali na ulinzi wa mali. Katiba imeweka katazo kwa mali ya mtu yeyote kuchukuliwa kwa lazima na serikali bila fidia. Sheria ya Ardhi Sura ya 113 katika kifungu cha 19 imetoa haki ya kila mtu kupata na kumiliki ardhi. Mwaka 2013, TACAIDS, katika ripoti yake juu ya tathmini ya mazingira ya kisheria ya kukabiliana na VVU na UKIMWI, iliona kwamba, katika maeneo

1

Hoffman v South African Airways 2000 (11) BCLR 1211 (CC); 2001 (1) SA (CC); N v. Minister of Defence (2000) ILJ 999 (Labour court of Namibia); I. B V Greece (European Court of Human Rights, Application N0. 552/10); AIDS Law Project v Attorney General and Others, Petition 97/2010.

mengine ya nchi, wajane wananyimwa haki ya kurithi mali za waume zao waliokufa kwa sababu ya hali yao halisi au ya kuhisiwa kuwa na VVU, ambayo pia hupunguza uwezo wao wa kiuchumi na kuongeza hatari ya VVU kwao. Kwa watoto yatima ambao wazazi wao wamekufa kutokana na vifo vinavyohusiana na UKIMWI, haki zao za kurithi mali zimekuwa zikivunjwa na ndugu au walezi wao. Ripoti ya 2017 kuhusu uhusiano kati ya mali za wanawake, haki ya urithi na VVU katika maeneo ya vijijini inaonesha kwamba ukiukwaji wa haki za wanawake na haki ya urithi huhusishwa sana na maambukizi ya VVU (17, 46). Katika ripoti ya Tume ya Kimataifa ya VVU na Sheria juu ya hatari, haki na afya (33), Tume ilibainisha kuwa nchi ni lazima zirekebishe sheria za umiliki mali na urithi ili kuwepo kwa usawa baina ya wanawake na wanaume katika upatikanaji wa mali na rasilimali nyingine za kiuchumi, ikiwa ni pamoja na mikopo. Ripoti hiyo inahimiza serikali kuhakikisha kwamba, katika mazingira halisi, mali zinagawanywa bila ubaguzi wa kijinsia baada ya kutengana, talaka au kifo, na kuanzisha dhana ya umiliki wa mali ya familia kwa mwanamke. Zaidi ya hayo, ikiwa umiliki na urithi wa mali unatatuliwa na mfumo wa kisheria wa kidini au wa kimila, viongozi wa mifumo hii wanapaswa kufanya marekebisho yanayolinda wanawake, ikiwa ni pamoja na wajane na yatima.

2.7 WATU WENYE HATARI, VVU NA SHERIA 2.7.1 Wahamiaji haramu na VVU Watu waishio katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kinyume cha sheria huchukuliwa kama wahamiaji haramu na hivyo hawatambuliki kisheria, hali hii huwaweka katika migogoro ya mara kwa mara na sheria. 2 Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na TACAIDS juu ya mazingira ya kisheria katika kukabiliana na VVU na UKIMWI,

2

Kifungu cha 10, Sheria ya Uhamiaji, Sheria Namba. 7 ya mwaka 1995 (47)


24 wahamiaji haramu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamejichanganya na jamii zetu za ndani, na bado hawapati huduma ya kutosha ya VVU na afya (30). Kwa hivyo, kutokupata huduma ya afya na VVU ni hatari kubwa ya maambukizi ya VVU na kuchochea maambukizi. Pia, kwa sababu ya hali yao, wahamiaji wanafanya shughuli za kujipatia kipato cha chini, ambazo wakati mwingine huchukuliwa kuwa shughuli haramu, na kuwaweka katika hatari zaidi ya kupata VVU na magonjwa ya zinaa, na kuwaweka katika migogoro ya kisheria. Kwa upande wa wahamiaji, ripoti juu ya hatari, haki na afya ilipendekeza kuwa - kuhakikisha jitihada za kifanisi na endelevu za VVU ambazo zinaendana na wajibu wa haki za binadamu-nchi zinapaswa kutoa kiwango sawa cha ulinzi kwa wahamiaji, wageni na wakazi ambao sio raia kama wanavyofanya kwa wananchi wao (33) . Ripoti hiyo pia inahimiza nchi kutekeleza mageuzi ya kitaratibu ili kuruhusu usajili wa kisheria wa wahamiaji na kutoa huduma za afya, ili kuhakikisha kwamba wahamiaji wanapata huduma bora na sawa za kuzuia VVU, matibabu na huduma kama zinazopatikana kwa wananchi wengine. Upimaji wa VVU na Magonjwa ya zinaa kwa wahamiaji unapaswa kuwa wa hiari na tarifa na matibabu yote kwa wahamiaji lazima yawe ya kimaadili na kitabibu.

2.7.2 Wafungwa na watu wengine walio katika vituo vya marekebisho na VVU Watu walioko magerezani wapo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU kwa kujichora picha milini kwa kutumia vifaa visivyo salama, matumizi ya madawa ya kulevya na kuchangia sindano, ngono zenye madhara makubwa na ubakaji. Aidha, idadimsongamano na kubwa ya watu huongeza maambukizi. TACAIDS imeona kwamba wafungwa wanapata huduma ndogo za VVU. Vikwazo hivi ni pamoja na ukosefu wa huduma za msingi-hasa katika magereza yaliyo katika maeneo yasiyofikika kwa haraka na kupelekea wafungwa kukosa huduma za afya zinazohusiana na VVU. Wafungwa hupata ukosefu wa virutubisho vya lishe na malazi. Hakuna sera juu ya utoaji wa huduma za afya kwa

mahabusu wanaosubiri kusikilizwa kwa kesi zao, wala hakuna kifungu cha sheria kinachohakikisha utoaji wa huduma za afya na VVU kwa watu hawa. TACAIDS pia imebaini kwamba wafungwa wengi wanafanya ngono kinyume na maumbile pasipo na hali yoyote ile ya kujikinga na hivyo kuwa katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya VVU na kusambaza VVU. Katika kukabiliana na VVU magerezani, Ripoti juu ya hatari, haki na afya inapendekeza kwamba nchi lazima zihakikishe kwamba huduma muhimu za afya zinapatikana magerezani (ikiwa ni pamoja na huduma za kuzuia VVU na matibabu), bila kujali sheria za jinai dhidi ya ngono kinyume na maumbile au kupunguza madhara (33 ). Huduma hizo hujumuisha utoaji wa kondomu, huduma za kupunguza madhara, na huduma ya kujitolea na ya ushahidi kwa watumiaji wa madawa ya kulevya na tiba ya kupambana na virusi vya UKIMWI. Zaidi ya hayo, matibabu yanayotolewa yanapaswa kukidhi viwango vya kimataifa vya ubora wa huduma magerezani. Huduma za afya,zinapaswa huhusisha zile zinazohusiana na matumizi ya madawa ya kulevya na VVU na lazima ziwe za kishahidi, hiari na kutolewa pale inapohitajika.

2.7.3 Wasichana vijana na wanawake na VVU Nchini Tanzania VVU na UKIMWI huathiri zaidi wanawake kuliko wanaume. Hii husababishwa na utofauti wa kijamii na kibaiolojia, na uwezekano mkubwa wa maambukizi ya VVU kwa wanawake. Kutengwa kijamii na ukosefu wa usawa wa kijinsia kwa wasichana na wanawake nchini ni matokeo ya kanuni na taratibu za kitamaduni na kijadi, ambazo huwaweka wanawake katika hali ya chini (30). Wasichana vijana na wanawake wadogo wanaathirika sana kutokana na mtazamo wa kijinsia ulioenea katika jamii, kanuni za jamii, na vikwazo katika kupata elimu na rasilimali, vyote hivi huwazuia kufanya maamuzi juu ya afya na maisha yao. Sheria na taratibu mbovu zinazohusiana na ndoa za utotoni, mimba za utotoni na ukosefu wa huduma za afya ya ngono na uzazi wa siri zinawazuia wasichana vijana na wanawake wadogo kupata taarifa na huduma muhimu za kuzuia VVU (48).


25 Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 imeelezea haki za mtoto (ikiwa ni pamoja na wasichana vijana), na inahitaji kukuza, kulinda na kudumisha ustawi wa mtoto. Inaelezea mtoto kama mtu yeyote chini ya umri wa miaka 18. Sheria ya UKIMWI katika kifungu cha 34 imeelezea ulinzi kwa watoto (ikijumuisha wasichana vijana), ili kuhakikisha kuwa wanapata elimu, huduma za msingi za afya na kimaisha. Ripoti juu ya hatari, haki na afya ilipendekeza kuwa nchi lazima zimalize aina zote za kibaguzi na unyanyasaji dhidi ya wanawake na wasichana, kuondoa vikwazo vya kisheria vinavyozuia wanawake kupata huduma za afya ya ngono na afya ya uzazi, kurekebisha sheria za kumiliki mali na urithi, na kuhakikisha kwamba hatua za ulinzi za kijamii zinatambua na kuitikia mahitaji ya wanawake wenye VVU na wanawake ambao waume zao wamekufa kwa UKIMWI (33). Sheria za kazi, ulinzi wa jamii na huduma za afya lazima zizingatie mahitaji ya wanawake wenye majukumu ya kutoa huduma ya afya kwa kaya zilizoathirika na VVU. Sheria zinazozuia ndoa za utotoni zinapaswa kutungwa na kupewa nguvu. Wahusika wa sheria za kidini na kimila wanatakiwa kuzuia mila na taratibu zinazoongeza hatari ya maambukizi ya VVU, kama urithi wa mjane, “Utakasaji wa wajane� na ukeketaji wa wanawake. Katika Mwongozo wa UNAIDS juu ya kuzuia VVU kwa wanawake wadogo na wasichana vijana, UNAIDS inahimiza nchi na wadau kutekeleza mipango inayolenga kupunguza maambukizi ya VVU kwa wasichana vijana na wanawake wadogo (48). Mpango huo unapaswa kupunguza maambukizi ya VVU, na kuondoa vikwazo vya kisheria vinavyozuia upatikanaji wa huduma ya afya kwa wasichana vijana na wanawake wadogo, kuwawezesha kutafuta huduma za VVU na huduma za afya, na huduma za kisheria pindi haki zao zinapovunjwa.

2.7.4 Watu wenye ulemavu na VVU Watu wenye ulemavu ni pamoja na wale walio na madhara ya mda mrefu ya kimwili, akili, fikira au hisia, wakikumbana na vikwazo vingi, inaweza kuzuia ushirika wao wa moja kwa moja au ufanisi katika kushiriki shughuli za kijamii kutokana na

kukosa usawa baina yao na wanajamii wengine (49). Mnamo Julai 2004, Wizara ya Kazi, Maendeleo ya Vijana na Michezo ya Tanzania ilianzisha Sera ya Taifa ya ulemavu (50), na mwaka 2010 Tanzania ilipitisha na kutekeleza Sheria ya Watu wenye ulemavu, 2010 (Sura namba 9 mwaka 2010) (51). Sheria hii imeweka masharti ya huduma za afya, msaada wa kijamii, upatikanaji , urekebishaji na uendelezaji wa haki za msingi kwa watu wengine wa watu wenye ulemavu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Mfumo wa Mkakati wa Taifa wa VVU na UKIMWI (2013 / 14-2017 / 18) unaonesha kwamba katika hali yoyote ile walemavu wanapaswa kuwa miongoni mwa wale ambao wanastahili huduma maalum katika programu za VVU (6). Huduma za kuzuia VVU, huduma za afya, matibabu na msaada, na huduma za afya ya ngono na afya ya uzazi ni muhimu kwa watu wenye ulemavu ikilinganishwa na watu wasio na ulemavu. Hii ni kwa sababu ya unyanyapaa na ubaguzi, kutengwa, kutokupata huduma za afya na elimu, kutohusishwa katika elimu ya ngono na athari za kiuchumi. UNAIDS inataka uhusishwaji wa walemavu katika kupambana na VVU na kujitolea katika kukabiliana na ukosefu wa kiusawa na ubaguzi, na huduma za VVU kwa ulemavu.


26

SEHEMU YA TATU

MAADILI NA UTOAJI WA MSAADA WA SHERIA


27

3.1 MFANO WA MASUALA YA KISHERIA YANAYOHUSIANA NA VVU. Katika utoaji wa ushauri wa kisheria na msaada wa kisheria kwa kesi za madai kwa watu waishio na VVU na makundi muhimu, mteja hawezi kutambua au kufichua hali yake ya VVU mara moja, au hawezi kutambua kuwa swala lake la kisheria linahusiana na VVU. Masuala halisi ya kisheria yanaweza kuwa na uhusiano wa moja kwa moja kwa watu wanaoishi na VVU (k.m. ubaguzi mahali pa kazi) au yanaweza kuwa na uhusiano mdogo (kwa mfano, unyanyasaji wa kijinsia unaoonyesha mteja kuwa na VVU).

3.1.1 Mifano ya Masuala ya Kisheria ambayo Inaweza kuwa na Uhusiano wa VVU Ifuatayo ni mifano ya masuala ya kisheria ambayo inaweza kuwa na uhusiano wa VVU, kwa mujibu wa kitengo cha kuandaa na kutoa huduma za kisheria zinazohusiana na VVU (53): • Ubaguzi kwa sababu ya hali ya VVU, mwelekeo wa kijinsia, jinsia-ikiwa ni pamoja na hali ya kubadili jinsia, ulemavu unaohusiana na VVU, matumizi ya madawa ya kulevya au biashara ya ngono. • Matatizo katika kupata huduma, matibabu na huduma ya kwanza • Matatizo yanayohusiana na uvunjaji wa faragha na usiri. • Vurugu dhidi ya wanawake, watu waishio na VVU, wanaume wanaofanya ngono na wanaume, watu wa waliobadilisha jinsia, wafanyakazi wa ngono, watu wanaojidunga madawa ya kulevya na watu wengine muhimu. • Migogoro ya ndani ikiwa mwenzi mmoja anainaishi na VVU au ni mwathirika wa VVU (k.m. ulinzi wa watoto, matunzo na mgawanyiko wa mali). • Uangalizi na utambuzi wa watunzaji wa watoto yatima. • Kulazimishwa kufunga uzazi au utoaji mimba. • Sheria za adhabu kuhusu maambukizi ya makusudi ya VVU.

• Sheria za makosa ya jinai zinazoathiri wafanyakazi wa ngono, wanaume wanaofanya ngono na wanaume, watu waliobadili jinsia na watu wanaotumia madawa ya kulevya. • Vitendo haramu vya polisi, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji, ubakaji, vurugu, ukamataji wa kutumia nguvu na dhuluma. • Kifungo na haki za wafungwa (ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa kondomu, elimu ya kuzuia na matibabu ya VVU). • Taarifa za wapenzi na ufuatiliaji mawasiliano. • Masuala ya ajira, ikiwa ni pamoja na ubaguzi na haki ya likizo ya ugonjwa. • Haki za umiliki wa ardhi, upangaji na makazi. • Mali na urithi. • Haki ya elimu na udhibiti wa masomo ya elimu. • Sheria za afya ya umma na haki ya ridhaa ya kupima na taarifa. • Ufutaji wa habari na udhibiti wa viwango vya vyombo vya habari. • Vitambulisho, usajili wa kuzaliwa na kifo, na usajili wa watumiaji wa madawa ya kulevya. • Dawa na haki ya kupata madawa ya gharama nafuu. • Haki za watoto; kwa mfano, ridhaa, siri, huduma na matibabu. • Waomba hifadhi, hali za wakimbizi, sheria za uhamiaji na uhuru wa kusafiri. • Kulazimishwa “matibabu” katika viwango vya chini. • Haki za mada za utafiti.

3.2 HUDUMA ZA KISHERIA ZINAZOHUSIANA NA VVU Maelezo ya Kisheria

Wateja wanaweza kutafuta habari kuhusu masuala yaliyotolewa katika Sehemu ya 3.1 au masuala mengine yanayohusiana na VVU. Habari za kisheria zinaweza kutolewa kwa maneno, au kupitia vifaa vilivyochapishwa na vinginevyo. Taarifa zinaweza kutolewa na wanafunzi, au kusambazwa na vituo vya afya au mashirika yasiyo ya kiserikali.

Ushauri wa Kisheria

Ushauri wa kisheria huendana na hali halisi na mahitaji ya mteja, na hutolewa na mtaalamu wa sheria, au wanafunzi chini ya usimamizi wa mtaalamu wa sheria.


28

Uwakilishi wa Kisheria na Msaada wa Madai

Inaweza kuwa mifumo isiyo rasimi au mifumo rasmi ya kisheria ikiwa ni pamoja na mahakama, vyombo vilivyo na nguvu ya kimahakama, mabaraza, halmashauri za kijadi, tume ya usuluhishi na upatanishi. Uwakilishi wa kisheria anaweza kuwa wa kutokea mahakamani au kwa njia ya maandishi au memoranda. Matumizi ya njia mbadala za utatuzi wa migogoro katika kutatua masuala ya kisheria yanayohusiana na VVU yanahimizwa, hasa ambapo wanafamilia wanahusika na kesi sio ya jinai. Hii ni kwa sababu mifumo hiyo ni ya haraka na ya bei nafuu, na huhimiza upatanishi, ikiwa mfumo wa kimahakama unawataka wahusika kuthibitisha kesi na hakimu au jaji yeye anakuwa kama refarii tu. Uwakilishi na usaidizi wa madai unaweza pia kuwa katika maslahi ya umma na kesi za madai za kimkakati. Hii hufanyika kutokana na matokeo ya sera za uma, na matokeo chanya ya kesi hizo hayamfaidishi mteja tu lakini jamuii pia kwa ujumla na yanaweza pelekea mabadiliko ya sheria na sera.

3.2.1 Huduma Nyingine za Kimkakati Zinazoweza tolewa na Kliniki ya Sheria Ushiriki wa Wadau na Elimu

Kuhakikisha mafanikio ya mbinu mbalimbali za kupambana na VVU, ushiriki wa wadau wote muhimu unahitajika. Katika sekta ya Sheria wadau hawa ni pamoja na wanasheria, mahakama na maafisa wa utekelezaji wa sheria. Washirika wengine husika ni pamoja na jamii za watu wanaoishi na VVU na makundi muhimu yaliyo katika hatari ya kupata maambukizi, wahudumu wa afya, maafisa wa utekelezaji wa sheria na wabunge. Elimu ambayo inaweza kutolewa inajumuisha kujenga uwezo juu ya njia za haki katika kupambana na VVU, majukumu yao na kile wanachoweza kufanya ili kuhamasisha na kutekeleza sheria ambazo zinaweza kutengeneza mazingira mazuri ya kisheria kwa watu waishio na VVU.

Utafiti wa Kisheria

Kliniki za kisheria na shule za kisheria zinaweza kufanya utafiti wa kisheria juu ya utekelezaji na mapungufu katika sheria zinazohusika kupambana na VVU. Wanaweza pia kufanya utafiti wa kisheria kwa kuandaa nyaraka za kimahakama ili kusaidia katika kesi zilizowasilishwa na watu waishio na VVU au katika kuwasaidia kuwasilisha. Kushiriki katika Majadiliano ya Kitaifa juu ya VVU na Kushauri Bunge juu ya Sheria ya VVU na UKIMWI, Vyuo vya Kisheria vinavyosaidiwa na Kliniki za Kisheria vinaweza kushiriki katika mijadala ya kitaifa na kijamii juu ya Sheria na sera zinazohusiana na VVU. Wahadhiri wa sheria wanaweza kushauri bunge na Serikali juu ya maswala muhimu ya kisheria yanayohusiana na VVU.

3.3 WAJIBU WA KISHERIA NA KIMAADILI KATIKA UTOAJI WA HUDUMA ZA KISHERIA Katika kutoa huduma za kisheria kwa watu waishio na VVU na watu muhimu , wafanyakazi katika Kliniki za Kisheria na wanafunzi wanapaswa kuendeleza haki za binadamu na utawala wa sheria, kulinda haki za wateja wao na kukuza utawala wa haki. Ili kutekeleza kazi hizi, wanafunzi walio katika kliniki za kisheria na wasimamizi wao ni lazima wazingatie sheria, viwango na maadili yanayotambulika katika taaluma ya sheria ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Maadili ya kisheria na wajibu wa kitaaluma huweka viwango, ambavyo vinajumuisha kanuni na maadili ambayo wataalamu wa kisheria wanapaswa kuzingatia kwa wateja wao.

3.3.1 Kanuni za Utoaji wa Huduma za Kisheria Zinazohusiana na VVU Kutokuwa na Ubaguzi

Wanafunzi na Waangalizi walio katika Kliniki ya Sheria wanapaswa kuhakikisha kuwa hakuna ubaguzi dhidi ya wateja katika utoaji wa huduma kwa misingi ya hali yao ya kweli au ya kudhaniwa


29 kuwa na VVU, au kuwa katika kundi la watu walio katika hatari ya kupata maambukizi. Mtazamo usio wa kuhukumu ni muhimu na wateja wanapaswa kujisikia wanakaribishwa na kuheshimiwa wakati wote. Wahudumu wa huduma za kisheria wanabanwa kimaaadili na kanuni ya “cab rank� ambayo huwataka watoa huduma kutoa huduma za kisheria bila ubaguzi.

Uhuru

Kliniki za kisheria (wanafunzi na mameneja wa kliniki) lazima wawe huru wanapowakilisha maslahi ya mteja. Kliniki lazima iwe huru mbali na hali na maslahi mengine yenye nguvu , ili kuwajengea imani ywateja wao na ya upande mwingine katika kesi husika pamoja na mahakama. Wanapaswa pia kuwa huru kwa mteja, hasa kihisia, ili kuwakilisha vizuri kesi ya mteja mahakamani.

Uaminifu, Uhalisia na Usawa

Watoa huduma za kisheria katika Kliniki za kisheria wanapaswa kuwa waaminifu kwa mteja, keshima uongozi wa haki na kumtendea haki mteja.

Uadilifu katika maslahi ya mteja

Uwezo wa kufanya kazi kwa maslahi mapana zaidi ya mteja ni muhimu. Hii huonekana katika majukumu mengine ya kimaadili; kwa mfano, wajibu wa kuepuka migogoro ya kimaslahi, kudumisha usiri na kudumisha uhuru dhidi ushawishi wa nje.

Usiri

Meneja wa kliniki ya kisheria na wasimamizi wanatakiwa kuhakikisha kwamba habari zote juu ya mteja wakati wa kutoa huduma za kisheria zinalindwa na hazitamkwi kwa mtu yeyote wa tatu bila ridhaa ya mteja. Taarifa yoyote ya mteja inapaswa kuwa kwa manufaa ya mteja na kuendeleza kesi iliyopo tu.

Mambo mengine

Mambo mengine muhimu ya kuzingatia katika msaada wa kisheria na madai ni pamoja na utambuzi wa masuala ya kisheria na uchaguzi wa vyombo vya maamuzi (yaani matumizi ya mahakama na vyombo vingine vinavyofanya kazi kama mahakama).

Ukusanyaji, uhifadhi na uwasilishaji wa ushahidi ni muhimu katika utoaji wa msaada wa madai juu ya masuala ya kisheria yanayohusiana na VVU, ikiwa ni pamoja na matumizi ya ushahidi wa matibabu na kisayansi.


30

VIAMBATANISHO


31

Sampuli ya Mkataba wa Usiri Mkataba huu unafanywa kati ya __________________________ (“Mpokea taarifa”) na ___________________ wafuasi wake (“Mtoa taarifa”). Mwanafunzi au meneja wa kliniki ya kisheria anaelewa kwamba mteja (Mtoa taarifa) ametoa au anaweza kitoa taarifa ambayo kwa asili ni ya faragha na ya siri. Taarifa hii inaweza kujumuisha taarifa ya afya “pamoja na taarifa za siri za mteja” ambazo hulindwa ili zisisambae kwa mujibu wa mahusianao ya mwanasheria na mteja. Maelezo ya afya yanaweza kujumuisha, kwa mfano, hali ya VVU, na hali ya VVU ya mpenzi au mwenzi wake wa kijinsia; historia ya matibabu; Taarifa za ndani za washirika wa ngono; na mazungumzo ya kimaandishi. Kwa kuzingatia majadiliano ya pande zote za mkataba na nafasi yoyote ile ambayo Mpokea taarifa atapata juu ya taarifa za afya au taarifa za siri kutoka kwa Mtoa taarifa (au zote), Mpokea taarifa hapa anakubali yafuatayo: 1. Mpokea taarifa anakubali: (a) kushikilia taarifa za afya au taarifa za siri za Mtoa taarifa kwa ujasiri thabiti, na kuchukua tahadhari zote za busara kulinda taarifa hizo; (b) kutotoa taarifa yoyote ya afya au siri kwa mtu wa tatu; (c) kutokutumia taarifa hizo za afya au usiri wakati wowote ule, isipokuwa kwa lengo pekee la kutoa ushauri wa kisheria na msaada wa madai. Mtu yeyote anayepata taarifa hiyo lazima awe na uhalali “wa kutaka kufahamu” na pia atabanwa kimaandishi. 2. Isipokuwa kwa kiwango kinachohitajika na sheria au kama imekubaliwa kimaandishi na Mtoa taarifa, Mpokea taarifa hatotoa taarifa zinazohusiana na suala la kisheria au uhusiano ulioelezewa na Mtoa taarifa. 3. Mkataba huu unaongozwa na Sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Unasimamia majadiliano na maandiko yote ya awali, na hufanya makubaliano yote baina ya pande zote za mkataba huu kwa swala husika. 4. Kuvunja au marekebisho ya mkataba huu yatakayofanywa na upande wowote ule wa mkataba huu isipokuwa kama kuna ridhaa ya kimaandishi na kusainiwa na mwakilishi aliyeidhinishwa. Kushindwa au kuchelewa katika kutekeleza haki yoyote katika mkataba huu haimaanishi Kuvunjika kwa makataba, na majukumu yaliyomo katika maktaba huu yataendelea kwa kudumu. IMESAINIWA na MTOA TAARIFA ) ) ) …………………..…………………………. ) ) IMESAINIWA na MPOKEA TAARIFA ) Mbele ya: ) ) …..………….………………………………


32

Fomu ya maelezo ya mteja


33


34


35

MAREJEO Marejeo muhimu

(kumbuka: nyaraka zimeorodheshwa kwa mpangilio wa uwiano)

Kifafanuzi cha kesi za jinai zinazohusiana na VVU: imeandaliwa kwa ajili ya “Wanasheria wa haki ya VVU na TB: madai ya kimkakati, utetezi wa kisheria na mafunzo ya uraghabishi’ 20-23 Februari 2018 (54)

Kifafanuzi cha Utetezi wa makosa ya jinai yanayohusiana na VVU kina lenga kuwasaidia wanasheria wanaowatetea wale wote wanoshutumiwa kuambukiza VVU kwa wengine. Hujumuisha kesi kutoka pande zote za dunia ambazo hoja kali za utetezi zilipelekea kuachiwa au kupungua kwa adhabu kwa watu wanaoishi na VVU ambao walishitakiwa kwa makosa yanayohusiana na kueneza VVU, kutokutoa taarifa ya VVU na kuambukiza VVU.

Haki ya afya (UNAIDS, 2017) (55)

Novemba 2017, Programu ya Pamoja ya Umoja wa Mataifa kuhusu VVU / UKIMWI (UNAIDS) ilizindua ripoti mpya inayoonyesha maendeleo katika upatikanaji wa tiba. Ripoti hiyo, ya Haki ya afya, inaonyesha kwamba watu wengi waliooneshwa katika jamii na wengi walioathirika na VVU bado wanakabiliwa na changamoto kubwa katika upatikanaji wa huduma za afya na kijamii wanazohitaji. Ripoti hiyo inaeleza wazi kwamba Nchi zina majukumu ya msingi ya kuheshimu haki za binadamu, kulinda na kutimiza haki ya afya.

VVU na UKIMWI na haki za kazi: Kitabu kwa Majaji na wataaluma wa kisheria (Shirika la Kazi la Kimataifa, 2015) (43)

Kitabu hiki kinalenga kuwasaidia Majaji na wataaluma wa kisheria katika kushughulikia masuala yanayohusiana na VVU na UKIMWI, kwa kuzingatia kazi na ajira. Kinatoa habari juu ya sheria husika za kitaifa na kimataifa na matumizi yake katika mahakama za ndani zinazofanya kazi katika mifumo ya kimila kisheria. Kitabu hiki pamoja na vifaa vyake vya mafunzo na majadiliano ya kesi vitasaidia wasomi wa kisheria, wanasheria na wanafunzi katika kuhakikisha ufanisi na uwazi katika kufikia haki ya kijamii na kuzingatia haki ya msingi ya kazi ya wale wote wanaoishi na VVU au walioathirika na janga hili.

Kuhukumu janga: kitabu cha mahakama juu ya VVU, haki za binadamu na sheria (UNAIDS, 2013) (1)

Kitabu hiki kinaelezea mambo muhimu ya kisheria na uzingatiwaji wa haki za binadamu na matumizi bora. Kila sura inatoa maelezo ya jumla ya sheria za kimataifa, kikanda na kitaifa na kanuni za haki za binadamu zinazotumika; Huonesha masuala muhimu ambayo yanafaa kuhukumiwa katika kesi zinazohusiana na VVU; na kuelezea kesi muhimu kutoka mamlaka mbalimbali za nchi.

Ufafanuzi wa hukumu: Nyaraka za msingi - majadiliano ya mahakama juu ya VVU, haki za binadamu na sheria Afrika Mashariki na Kusini, Nairobi, Kenya 28-31 Oktoba (UNDP, 2013) (56) Mwongozo huu ni mkusanyiko wa filosophia ya sheria zinazoendelea juu ya masuala yanayohusiana na VVU unaoonesha utumikaji wa sheria katika kulinda haki za za watu. Unawasilisha ushirikiano rafiki wa hukumu kutoka kwa mamlaka mbalimbali za kitaifa na kikanda.

Tume ya Kimataifa ya VVU na Sheria: hatari, haki na afya (UNDP, 2012) (33)

Programu ya Maendeleo ya Umoja wa Mataifa (UNDP) iliitisha Tume ya Kimataifa ya VVU na Sheria kuchunguza athari za sheria katika kupambana na VVU. Baadhi ya mada muhimu zilizochunguzwa ni pamoja na:


36 • Ujinai wa maambukizi ya VVU, kueneza na kutokutoa taarifa ya VVU. • Madhara ya ubaguzi kwa watu wanaoishi na VVU. • Ujinai wa tabia na vitendo kama vile matumizi ya madawa ya kulevya, kazi ya ngono na mahusiano ya ngono ya jinsia moja; na masuala ya wafungwa na wahamiaji. • Madhara ya sheria na taratibu za kibaguzi yahusuyo wanawake na wasichana pamoja na watoto na vijana katika mazingira ya VVU. • Ujuzi wa kiakili katika mazingira ya upatikanaji wa tiba. Ripoti inachambua jukumu muhimu la sheria na mazingira ya kisheria ya haki za binadamu katika ustawi wa watu waishio na VVU na wale walio na hatari ya VVU.

Kitabu cha Kitengo: Kuongeza huduma za kisheria zinazohusiana na VVU (IDLO, UNAIDS, UNDP, 2009) (53)

Kitabu hiki kinatoa rasilimali ya kusaidia kuboresha ubora na athari za huduma za kisheria zinazohusiana na VVU, na kupanua upatikanaji wa huduma hizo. Hunatoa mwongozo juu ya mambo ya kuzingatia wakati wa kubuni na kuongeza programu za huduma za kisheria zinazohusiana na VVU. Pia hutoa mwongozo juu ya njia na mbinu tofauti za kutoa huduma, kufuatilia na kutathmini huduma za kisheria zinazohusiana na VVU, na hutoa taarifa kuhusu uhamasishaji wa rasilimali.

Ufafanuzi wa Mabaraza ya kesi za VVU na UKIMWI, toleo la kwanza (UNDP, Kenya Kisheria na Masuala ya Kimaadili (KELIN) na Mabaraza ya VVU na UKIMWI, inaendana na wakati) (57)

Hati hii inalenga kusaidia wanasheria, majaji, watafiti wa kisheria, wanafunzi na umma kwa ujumla kuelewa na kutambua jinsi sheria ilivyotumika na kutafsiriwa katika kulinda na kukuza haki za watu waishio na VVU.

Nyaraka zingine za kimataifa na kikanda 1. Taarifa ya mwisho ya Mkutano wa kawaida wa Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (2017 (23) 2. UNAIDS (2017) Ulemavu na VVU (52) 3. UNAIDS (2016) kuzuia VVU miongoni mwa wasichana vijana na wanawake wadogo: Uingizwaji wa kuzuia VVU miongoni mwa wasichana vijana na wanawake wadogo kwenye Orodha ya haraka wakiwemo wanaume na wavulana. Mwongozo (48) 4. WHO (2016) Miongozo iliyounganishwa juu ya kuzuia VVU, utambuzi, matibabu na huduma kwa watu muhimu (10) (7) 5. Mpango wa 2030 wa Maendeleo Endelevu, Malengo ya Maendeleo Endelevu (7) 6. VVU na UKIMWI na haki za kazi: Kitabu cha waamuzi na wataaluma wa kisheria (2015) (43) 7. Miongozo ya Misamiati ya UNAIDS (2015) (40) 8. UNAIDS (2013) Kukomesha ujinai mpana wa VVU, kutokutoa taarifa, kueneza na kuambukiza: ufanisi wa kisayansi, kuzingatia matibabu na sheria. Mwongozo (3) 9. UNAIDS, 2016-2021 Mkakati: Lengo Mahusisi, malengo, Maono. Katika Mpango wa haraka ili kukomesha UKIMWI (8) 10. Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa (2016) Azimio la Kisiasa kuhusu VVU / UKIMWI (14) 11. UNAIDS (2014) Huduma kwa wafanyakazi wa ngono. Mwongozo (37) 12. UNAIDS (2014) Huduma kwa wanaume mashoga na wanaume wengine wanaojamiana na wanaume. Mwongozo (38) 13. UNAIDS (2014) Huduma kwa watu wanaojidunga madawa ya kulevya. Mwongozo (39) 14. ILO (2010) Mapendekezo kuhusu VVU na UKIMWI na ulimwengu wa kazi (44) 15. Sheria ya mfano kuhusu VVU katika Afrika ya Kusini (2008) (18) 16. UNAIDS, OHCHR (2006) Miongozo ya Kimataifa kuhusu VVU / UKIMWI na haki za binadamu (15)


37 17. Azimio la Abuja na mpango wa utekelezaji juu ya VVU / UKIMWI, kifua kikuu na magonjwa mengine ya kuambukizwa (2001) (16) 18. Tume ya Afrika ya Uamuzi wa Haki za Binadamu na Watu juu ya VVU / UKIMWI (2001) 19. UNAIDS (2000) Ufunguzi wa janga la VVU na UKIMWI: mwongozo juu ya kuhamasisha uwazi kuhusu wanufaika, ushauri wa kimaadili wa washirika / wenzi na matumizi sahihi ya taarifa za kesi za VVU (31) 20. UNAIDS (1997) Mwongozo wa UNAIDS kwa Vyombo vya haki za binadamu za Umoja wa Mataifa (12) 21. OHCHR (2006) Machapisho naNyaraka juu ya VVU na UKIMWI (13)

Sheria • • • • • •

Sheria ajira na Mahusiano ya Kazi, 2006 (41) Sheria ya Watu wenye ulemavu, 2010 (26, 51) Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti VVU na UKIMWI , 2008 (26) Kanuni ya Adhabu, Sura ya. 16, 2002 (35) Sheria ya Ardhi, Sura ya 113 (1999) (45) Sheria ya Kuzuia na Kudhibiti Uingizaji na Usafirishaji wa Madawa ya Kulevya. Sura ya 95, 1996 (58) • Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 (25, 51) • Sheria ya Uhamiaji, Namba 7 ya 1995 (47)

Sera na Miongozo ya Kitaifa 1. 2. 3. 4. 5. 6. 7. 8.

Miongozo ya kitaifa ya usimamizi wa VVU na UKIMWI (2017) (28). Mfumo wa Tanzania wa Mipango ya VVU na UKIMWI (2013 / 14-2017 / 18) (6) Miongozo ya kitaifa ya Mfuko kamili wa maambukizi ya VVU kwa watu muhimu (2014) (9). Ripoti juu ya tathmini ya mazingira ya kisheria katika kukabiliana na VVU na UKIMWI ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 2013 (30). Mwongozo wa kitaifa kwa huduma za kina za kuzuia maambukizi ya VVU kwa mama na mtoto na kuhakikisha uhaiwa mama, 2013 (27). Taratibu za kiuendeshaji kwa ajili ya kupima VVU na huduma za ushauri (2009) (29). Ofisi ya Taifa ya Takwimu ya Tanzania (2011), Uchunguzi wa Idadi ya Watu na Afya (36). Sera ya Taifa ya ulemavu, 2004 (50)

Orodha Nzima ya Marejeo

1. UNAIDS. Judging the epidemic: a judicial handbook on HIV, human rights and the law. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2013 (http://www.unaids.org/sites/default/files/media_ asset/201305_Judging-epidemic_en_0.pdf, accessed February 2018). 2. WHO. Guideline on when to start antiretroviral therapy and pre-exposure prophylaxis for HIV. Geneva: World Health Organization (WHO); 2015 (http://apps.who.int/iris/bitstream/10665/186275/1/9789241509565_ eng.pdf, accessed February 2018). 3. UNAIDS. Ending overly broad criminalisation of HIV non-disclosure, exposure and transmission: critical scientific, medical and legal considerations. Guidance note. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2013 (http://www.unaids.org/sites/default/files/media_asset/20130530_ Guidance_Ending_Criminalisation_0.pdf, accessed February 2018). 4. UNAIDS. AIDSinfo. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2017 (http://aidsinfo. unaids.org/, accessed February 2018). 5. UNAIDS. UNAIDS data. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2017 (http://www. unaids.org/sites/default/files/media_asset/20170720_Data_book_2017_en.pdf, accessed February 2018).


38 6. Tanzania Third National Multi-Sectoral Strategic Framework for HIV and AIDS (2013/14–2017/18). Tanzania: 2013 (http://www.nationalplanningcycles.org/sites/default/files/country_docs/Tanzania/ nmsf-iii_eng_final_report_2013mail.pdf, accessed February 2018). 7. UN. The 2030 Agenda for Sustainable Development. Sustainable Development Goals. United Nations (UN); 2015 (http://www.un.org/sustainabledevelopment/sustainable-development-goals/, accessed February 2018). 8. UNAIDS. 2016–2021 Strategy: targets, goals, vision. On the Fast-Track to end AIDS. Geneva: Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS) (http://www.unaids.org/sites/default/files/ media_asset/20151027_UNAIDS_PCB37_15_18_EN_rev1.pdf, accessed February 2018). 9. Ministry of Health and Social Welfare, National AIDS Control Programme (NACP). National guideline for comprehensive package of HIV interventions for key populations. 2014 (http://www.hivsharespace. net/resource/tanzania-national-guideline-comprehensive-package-hiv-interventions-key-populations, accessed February 2018). 10. WHO. Consolidated guidelines on HIV prevention, diagnosis, treatment and care for key populations, 2016 update. Geneva: World Health Organization (WHO); 2016 (http://www.who.int/hiv/pub/guidelines/ keypopulations-2016/en/, accessed February 2018). 11. Shyllon O. Monism/dualism or self executory: the application of human rights treaties by domestic courts in Africa. Abo Akademi University: Institute for Human Rights; 2009 (http://web.abo.fi/instut/imr/ secret/kurser/Advanced09/Essays/Working-group4/Shyllon_Monism%20Dualism%20or%20Self%20 Executory.pdf, accessed February 2018). 12. UNAIDS. The UNAIDS guide to the United Nations human rights machinery. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 1997 (http://data.unaids.org/publications/irc-pub01/jc128hrmachinery_en.pdf, accessed February 2018). 13. OHCHR. Publications and documents on HIV and AIDS. Geneva: Office of the United Nations High Commissioner for Human Rights (OHCHR); 2006 (http://www.ohchr.org/EN/Issues/HIV/Pages/ Documents.aspx, accessed February 2018). 14. UN General Assembly. Political declaration on HIV/AIDS: on the Fast-Track to accelerating the fight against HIV and to ending the AIDS epidemic by 2030. United Nations (UN); 2016 (http://www.unaids. org/en/resources/documents/2016/2016-political-declaration-HIV-AIDS, accessed February 2018). 15. UNAIDS, OHCHR. International guidelines on HIV/AIDS and human rights. Geneva: Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS) and Office of the United Nations High Commissioner for Human Rights (OHCHR); 2006 (http://www.ohchr.org/Documents/Publications/HIVAIDSGuidelinesen. pdf, accessed February 2018). 16. Abuja Declaration on HIV/AIDS, Tuberculosis and Other Related Infectious Diseases. 2001 (http:// www.un.org/ga/aids/pdf/abuja_declaration.pdf, accessed February 2018). 17. SADC Parliamentary Forum. Model law on HIV in Southern Africa. 2008 (http://www.justice.gov.za/ vg/hiv/docs/2008_Model-Law-on-HIV-in-Southern-Africa.pdf, accessed February 2018). 18. ACHPR. ACHPR/Res. 53 (XXIX) 01 on the HIV/AIDS pandemic – Threat Against Human Rights and Humanity. African Commission on Human and Peoples’ Rights (ACHPR); 2001 (http://www.achpr. org/sessions/29th/resolutions/53/, accessed February 2018). 19. ACHPR. ACHPR/Res. 141 (XLIV) 08 on Access to Health and Needed Medicines in Africa. African Commission on Human and Peoples’ Rights (ACHPR); 2008 (http://www.globalhealthrights.org/ wp-content/uploads/2013/10/Resolution-on-Access-to-Health-and-Needed-Medicines-in-Africa.pdf, accessed February 2018). 20. ACHPR. Res. 260 on Involuntary Sterilization and the Protection of Human Rights in Access to HIV Services. African Commission on Human and Peoples’ Rights (ACHPR); 2013 (http://www.achpr. org/sessions/54th/resolutions/260/, accessed February 2018). 21. ACHPR. ACHPR/Res. 163 on the Establishment of a Committee on the Protection of the Rights of People Living With HIV (PLHIV) and Those at Risk, Vulnerable to and Affected by HIV. African


39 Commission on Human and Peoples’ Rights (ACHPR); 2010 (http://www.achpr.org/sessions/47th/ resolutions/163/, accessed February 2018). 22. Gumedze S. HIV/AIDS and human rights: the role of the African Commission on Human and Peoples’ Rights. African Human Rights Law Journal. 2004;4(2):181–200 (http://www.corteidh.or.cr/tablas/ R21549.pdf, accessed February 2018). 23. ACHPR. Final communique of the 61st ordinary session of the African Commission on Human and Peoples’ Rights. African Commission on Human and Peoples’ Rights (ACHPR); 2017 (http://www. achpr.org/files/sessions/61st/info/communique61/61st_os_final_communique_eng.pdf, accessed February 2018). 24. UNAIDS. HIV, the law and human rights in the African human rights system: key challenges and opportunities for rights-based responses – report on the study of the African Commission on Human and Peoples’ Rights. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2018 (http://www. unaids.org/en/resources/documents/2018/HIV_Law_AfricanHumanRightsSystem, accessed February 2018). 25. The Constitution of the United Republic of Tanzania (Cap. 2). Tanzania: 1977 (http://www.judiciary. go.tz/wp-content/uploads/2015/09/constitution.pdf, accessed February 2018). 26. The HIV and AIDS (Prevention and Control) Act. Tanzania: Parliament of the United Republic of Tanzania; 2008 (http://www.ilo.org/wcmsp5/groups/public/---ed_protect/---protrav/---ilo_aids/ documents/legaldocument/wcms_125594.pdf, accessed February 2018). 27. The United Republic of Tanzania Ministry of Health and Social Welfare. National guidelines for comprehensive care services for prevention of mother-to-child transmission of HIV and keeping their mothers alive. Dar es Salaam: 2013. 28. The United Republic of Tanzania Ministry of Health and Social Welfare, National aids Control Programme (NACP). National guidelines for the management of HIV and AIDS. 2012 (https://aidsfree. usaid.gov/sites/default/files/hts_policy_tanzania.pdf, accessed February 2018). 29. The United Republic of Tanzania Ministry of Health and Social Welfare. Standard operating procedures for HIV testing and counselling (HTC) services. 2009 (https://www.jica.go.jp/project/tanzania/001/ materials/pdf/vct_10.pdf, accessed February 2018). 30. TACAIDS. The report on the legal environment assessment in response to HIV and AIDS within the United Republic of Tanzania. Tanzania: Tanzania Commission for AIDS (TACAIDS); 2013 (http://tacaidslibrary.go.tz/bitstream/handle/123456789/88/THE%20REPORT%20ON%20THE%20 LEGAL%20ENVIRONMENT%20ASSESSMENT%20IN%20RESPONSE_TO_HIV_AND_AIDS_ WITHIN_THE_UNITED_REPUBLIC_OF_TANZANIA.pdf?sequence=1&isAllowed=y, accessed February 2018). 31. UNAIDS. Opening up the HIV/AIDS epidemic: guidance on encouraging beneficial disclosure, ethical partner counselling and appropriate use of HIV case-reporting. Geneva: Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2000 (http://www.who.int/ethics/topics/opening_up_ethics_and_ disclosure_en_2000.pdf, accessed February 2018). 32. The HIV and AIDS (Counselling and Testing, Use of ARVs and Disclosure) Regulations – The HIV and AIDS (Prevention and Control) Act. Tanzania: Parliament of the United Republic of Tanzania; 2010 (http://www.ilo.org/wcmsp5/groups/public/---ed_protect/---protrav/---ilo_aids/documents/ legaldocument/wcms_241592.pdf, accessed February 2018). 33. UNDP. Global Commission on HIV and the Law: risks, rights and health. New York, NY: United Nations Development Programme (UNDP); 2012 (https://hivlawcommission.org/wp-content/uploads/2017/06/ FinalReport-RisksRightsHealth-EN.pdf, accessed February 2018). 34. UNAIDS. Counselling and voluntary HIV testing for pregnant women in high HIV prevalence countries. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2001 (http://data.unaids.org/publications/ irc-pub01/jc245-couns_test_en.pdf, accessed February 2018). 35. The Penal Code, Cap 16. Parliament of the United Republic of Tanzania; 2002 (http://www.un.org/


40 Depts/los/LEGISLATIONANDTREATIES/PDFFILES/TZA_penal_code.pdf, accessed February 2018). 36. Tanzania National Bureau of Statistics. Demographic and Health Survey 2010. 2011 (https:// dhsprogram.com/pubs/pdf/FR243/FR243%5B24June2011%5D.pdf, accessed February 2018). 37. UNAIDS. Services for sex workers. Guidance note. UNAIDS; 2014 (http://www.unaids.org/sites/ default/files/media_asset/SexWorkerGuidanceNote_en.pdf, accessed February 2018). 38. UNAIDS. Services for gay men and other men who have sex with men. Guidance note. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2014 (http://www.unaids.org/sites/default/files/media_ asset/2014unaidsguidancenote_servicesforMSM_en.pdf, accessed February 2018). 39. UNAIDS. Services for people who inject drugs. Guidance note. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2014 (https://www.unodc.org/documents/hiv-aids/publications/2014_guidance_ servicesforpeoplewhoinjectdrugs_en.pdf, accessed February 2018). 40. UNAIDS. UNAIDS terminology guidelines. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2015 (http://www.unaids.org/sites/default/files/media_asset/2015_terminology_guidelines_en.pdf, accessed February 2018). 41. The Employment and Labour Relations Act. Parliament of the United Republic of Tanzania; 2006 (http://tanzania.go.tz/egov_uploads/documents/Employment%20and%20LAbour%20Relation%20 Act.pdf, accessed February 2018). 42. Kassile T, Anicetus H, Kukula R, Mmbando BP. Health and social support services to HIV/AIDS infected individuals in Tanzania: employees and employers perceptions. BMC Public Health. 2014;14:630–630 (http://www.ncbi.nlm.nih.gov/pmc/articles/PMC4074831/, accessed February 2018). 43. ILO. HIV and AIDS and labour rights: a handbook for judges and legal professionals. Geneva: International Labour Organization (ILO); 2015 (http://www.ilo.org/wcmsp5/groups/public/---ed_protect/--protrav/---ilo_aids/documents/publication/wcms_228498.pdf, accessed February 2018). 44. ILO. Recommendation concerning HIV and AIDS and the world of work. Geneva: International Labour Organization (ILO); 2010 (http://www.ilo.org/global/topics/hiv-aids/WCMS_194088/lang--en/index. htm, accessed February 2018). 45. The Land Act: Chapter 113 Laws of Tanzania. Parliament of the United Republic of Tanzania; 1999 (http://tanzania.eregulations.org/media/The%20Land%20Act%201999.%20Cap%20113.pdf, accessed February 2018). 46. Shoki P, Nyenga C, Kasongi D. Women’s property and inheritance rights and HIV in farming communities around Lake Victoria, northwestern Tanzania – a quantitative analysis. Measure Evaluation, 2017 (https://www.measureevaluation.org/resources/publications/wp-17-179, accessed February 2018). 47. The Immigration Act, Act No. 7 Parliament of the United Republic of Tanzania; 1995 (http://tanzania. go.tz/egov_uploads/documents/The_Immigration_Act,_7-1995_en.pdf, accessed February 2018). 48. UNAIDS. HIV prevention among adolescent girls and young women: putting HIV prevention among adolescent girls and young women on the Fast-Track and engaging men and boys. Guidance note. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2016 (http://www.unaids.org/sites/default/ files/media_asset/UNAIDS_HIV_prevention_among_adolescent_girls_and_young_women.pdf, accessed February 2018). 49. UN. Convention on the Rights of Persons with Disabilities. United Nations (UN); 2008 (https://www. un.org/development/desa/disabilities/convention-on-the-rights-of-persons-with-disabilities.html, accessed February 2018). 50. National policy on disability. Tanzania: Parliament of the United Republic of Tanzania; 2004 (http:// www.ilo.org/dyn/natlex/natlex4.detail?p_lang=en&p_isn=94120&p_country=TZA&p_count=283, accessed February 2018). 51. Persons with Disabilities Act. Tanzania: Parliament of the United Republic of Tanzania; 2010 (http:// www.ilo.org/dyn/natlex/docs/ELECTRONIC/86525/97738/F727574943/TZA86525.pdf, accessed February 2018). 52. UNAIDS. Disability and HIV. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2017 (http://


41 www.unaids.org/sites/default/files/media_asset/JC2905_disability-and-HIV_en.pdf, accessed February 2018). 53. IDLO/UNAIDS/UNDP. Toolkit: scaling up HIV-related legal services. Rome: International Development Law Organization (IDLO), Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS) and United Nations Development Programme (UNDP); 2009 (http://data.unaids.org/pub/ manual/2010/20100308revisedhivrelatedlegalservicetoolkitwebversion_en.pdf, accessed February 2018). 54. SALC. HIV criminalisation case compendium. Johannesburg, South Africa: South African Litigation Centre (SALC); 2018 (http://www.southernafricalitigationcentre.org/2018/02/13/hiv-criminalisationdefence-case-compendium/, accessed March 2018). 55. UNAIDS. Right to health. Joint United Nations Programme on HIV/AIDS (UNAIDS); 2017 (http://www. unaids.org/en/20171120_right_to_health_report, accessed February 2018). 56. UNDP. Compendium of judgements: background material – judicial dialogue on HIV, human rights and the law in Eastern and Southern Africa, Nairobi, Kenya 28–31 October. United Nations Development Programme (UNDP); 2013 (https://hivlawcommission.org/wp-content/uploads/2017/06/Compendiumof-Judgments-for-Judicial-Dialogue-on-HIV-Human-Rights-and-the-Law-in-East-and-Southern-Africa. pdf, accessed February 2018). 57. UNDP, KELIN, The HIV and AIDS Tribunal. The HIV and AIDS Tribunal compendium of cases, 1st edition. United Nations Development Programme (UNDP), Kenya Legal and Ethical Issues Network (KELIN) and The HIV and AIDS Tribunal;( , accessed February 2018). 58. The Drugs and Prevention of the Illicit Traffic in Drugs Act Cap. 95. Parliament of the United Republic of Tanzania; 1996.


42


43



Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.