Barefoot Guide 1 Kiswahili

Page 40

Kupooza kwa dhamira Kwa nini hatufanyii kazi mawazo na hisia zetu?

Yatubidi kuendelea kusikiliza hisia zilizo nyuma ya fikra, pamoja na kusikiliza dhamira kama inavyoelezwa na msemaji. Huu ndio usikilizaji wa kina zaidi.

NAMNA YA KUFIKIRI Hii yote inaonyesha kwamba watu wana jinsi yao ya kufikiri, na maana yao ya maneno na wanaleta uzoefu tofauti na wetu ili kupata maana. Kama hatuwezi kuruhusu utofauti wa kimtazamo baina yetu na mtu mwingine kuna uwezekano wa kutoeleweka tunapoongea nao. Mbaya zaidi, huwa tunajifanya kujua kile wanachoongelea wakati hatukijui. Sote tumewahi kusikia mtu akisema “ninafahamu kabisaa unachomaanisha”. Nasi tumeona wale wanaojifanya wanajua wakishindwa kujua hata chembe ya kile tunachomaanisha. Tunatakiwa kuwa makini tusifanye kosa kama hilo.

Mara nyingi tunajisikia hatuna uwezo kwa kuwa tunajua tunahitaji kubadilika lakini hatuwezi. Kuna kitu kinatuzuia. Tunakuwa na dhamira iliyopooza.

Kudhani kuwa watu wote hufikiri sawa ni chanzo kikubwa kwa utata.

3

CHANGAMOTO: JIFAHAMU • JIELEZE • CHUKUA HATUA

Mara nyingi hii inatokana na:

Shaka au kujitilia mashaka Tunahofia kama watu au hali fulani yaweza kweli kubadilika na kuwa bora. Tunaonea shaka uwezo wetu wa kubabiliana na changamoto za siku za usoni.

Chuki au kujichukia: Tunaudhika au hata kuchukia wengine kwasababu ya machungu yaliyowahi kutupata. Tunajichukia sababu ya yale tuliyofanya..

Hofu: Tuna woga wa kuachana na yale tunayofahamu hata kama hayatusaidii. Tuna woga wa mambo yajayo ambayo hatuyafahamu. Mabadiliko yanaweza kutuhitaji sisi kupambana na hizi hofu, chuki na woga, ili tuweze kukabiliana nayo. 32

“ 1

Martin Buber

Kuna kanuni tatu katika nafsi ya mwanadamu na maisha, kanuni ya mawazo, kanuni ya maneno na kanuni ya matendo. Chanzo cha migogoro yote baina yangu na binadamu wenzangu ni kwamba sisemi kile ninachomaanisha na sitendi kile ninachosema.

JIFAHAMU

Fikiria zaidi kuhusu mawazo yako mwenyewe! Uliza zaidi maswali yako mwenyewe! Kuwa karibu na hisia zako mwenyewe! Jua zaidi yale unayohitaji!

2

JIELEZE

Kujua kile unachofikiria, unachohisi, na unachohitaji inakusaidia kujieleza na kujitetea mwenyewe!

3

CHUKUA HATUA

Kutenda kutokana na mawazo yako mwenyewe, hisia zako na utashi wako! Kuwa mwenyewe! Fanya kile ambacho lazima ufanye! Uwe na ujasiri! WWW.BAREFOOTGUIDE.ORG


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.