Pccb huduma

Page 1

Aidha, huduma hii inatoa fursa kwa TAKUKURU kutoa ufafanuzi wa masuala mbalimbali kwa wananchi kuhusu mapambano dhidi ya rushwa. Vilevile inaiwezesha TAKUKURU kupokea taarifa za vitendo vya rushwa kutoka sehemu mbalimbali ambazo isingekuwa rahisi kuzipokea na kuzishughulikia. JE, MWANANCHI ANA WAJIBU WA KUTOA TAARIFA? Ndiyo. Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Namba 11 ya Mwaka 2007, Kifungu cha 39 kifungu kidogo cha (i), inamtaka kila mtu kutoa taarifa za vitendo rushwa kwa TAKUKURU. Kifungu hicho kinatamka kuwa …kila mtu anayefahamu juu ya kufanyika kwa au mpango wa kufanya kosa la rushwa, anapaswa kutoa taarifa TAKUKURU. JE, KUNA UTARATIBU WOWOTE WA KUMLINDA MTOA TAARIFA? Ndiyo. • Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007, kifungu cha 51 na kifungu cha 52 kinatoa ulinzi wa kisheria kwa mtu yeyote anayetoa taarifa au ushahidi mahakamani kuhusu kufanyika kwa vitendo vya rushwa. Ulinzi huo ni pamoja na kutotoa utambulisho wake kwa kutotajwa jina, makazi au anwani yake; kuzuia kulipiziwa kisasi au kutendewa vibaya; kutounganishwa kwenye mashtaka au kutofunguliwa kesi ya madai au jinai . • Endapo mtoa taarifa atatishiwa, kuumizwa au kulipiziwa kisasi na watu aliowataja au wanaohusiana nao, Serikali inaweza kumpa ulinzi au kumlipa fidia au kumpa msaada wa aina yoyote kulingana na madhara aliyoyapata. Kifungu cha 52 (3) kinatamka adhabu kwa mtu yeyote atakayemhujumu kwa aina yoyote ile mtoa taarifa ambayo ni kulipa faini isiyozidi shilingi laki tano ama kifungo kisichozidi mwaka mmoja au adhabu zote mbili. • Sheria ya kuwalinda Watoa Taarifa za Uhalifu na Mashahidi Na. 20 ya Mwaka 2015, inatoa ulinzi kwa mtu yeyote anayetoa taarifa za uhalifu wa makosa ya aina mbalimbali ikiwemo vitendo vya rushwa vilivyotokea, vinavyotokea au vinavyoweza kutokea. Vilevile Sheria hii inatoa ulinzi kwa mashahidi wanaotakiwa kufika mahakamani. • Ili kumlinda mtoa taarifa, inashauriwa mtoa taarifa atunze siri kuhusu nia yake na hatua ya kuwasilisha taarifa hiyo TAKUKURU.

• Mtumishi yeyote wa TAKUKURU, kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007, analazimika kutunza siri ya taarifa aliyopokea ikiwemo utambulisho wa mtoa taarifa na anaweza kuchukuliwa hatua za kisheria iwapo atavujisha siri hiyo. JE, KUNA NJIA NYINGINE ZA KUIFIKIA TAKUKURU? Ndiyo, zipo njia zifuatazo: • Kufika katika ofisi ya TAKUKURU iliyo karibu na muhusika. • Kuandika barua kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, 16 Mtaa wa Urambo, S.L.P 4865, Dar es Salaam. • Kupiga simu Ofisi ya Makao Makuu nambari: +255 22 2150043 -6 • Kuandika barua au kupiga simu kwa Wakuu wa TAKUKURU wa Mikoa au Wilaya kadiri ya eneo alipo mtoa taarifa. • Kutuma malalamiko kwa kujaza ‘fomu ya malalamiko’ iliyopo katika wavuti ya TAKUKURU - www.pccb.go.tz. • Kuandika baruapepe kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU:dgeneral@pccb.go.tz au kwa Wakuu wa TAKUKURU wa Mikoa au Wilaya. • Kutumia nukushi nambari: +255 22 2150047 HITIMISHO: TAKUKURU imeweka huduma ya simu ya dharura nambari 113 ili kurahisisha mawasiliano na wananchi. Tunamsihi mwananchi kutumia huduma hii kwa mujibu wa sheria za nchi na kadiri ya malengo yaliyokusudiwa ili kwa pamoja tuweze kutokomeza tatizo la rushwa nchini. Taarifa zinazotolewa zinapaswa kuwa za kweli na si zenye chuki binafsi au zenye nia ya kumkomoa mtu. Ikumbukwe ni kosa kisheria kutoa taarifa za uongo TAKUKURU au kwa mamlaka nyingine yoyote inayoshughulika na makosa ya jinai. Tuungane kuitokomeza rushwa kwa maendeleo, amani na usalama wa nchi yetu

MKURUGENZI MKUU TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA (TAKUKURU)

16 Mtaa wa Urambo, S.L.P 4865, 11102 Dar es Salaam, Tanzania. Simu: +255 22 215 0043 - 6, Nukushi: +255 22 215 0047, Barua pepe: dgeneral@pccb.go.tz Wavuti: www.pccb.go.tz, Simu ya Bure 113, *113#, SMS 113

KITUO CHA HUDUMA KWA MTEJA - TAKUKURU


KITUO CHA HUDUMA KWA MTEJA TAKUKURU KINASHUGHULIKA NA NINI? Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) - PCCB CALL CENTER, kipo ofisi ya Makao Makuu na kilianzishwa mwezi Mei mwaka 2016. Kituo hiki kina jukumu la kutoa huduma kwa kupokea taarifa, maoni, malalamiko ya wananchi kuhusu vitendo vya rushwa pamoja na kutoa elimu ya mapambano dhidi ya rushwa kwa njia ya simu ya dharura nambari 113. Kituo hiki kinafanya kazi saa 24. KWA NINI KITUO HIKI KIMEANZISHWA? Kituo hiki kimeanzishwa ili kumuwekea mwananchi mazingira rafiki, rahisi na yasiyo na gharama ya kuifikia TAKUKURU wakati wowote na ndiyo maana kinafanya kazi saa 24. Hili limefanyika ili kutimiza matakwa ya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11 ya Mwaka 2007. Matakwa hayo yanatajwa katika Kifungu cha 39(ii) ambacho kinataka kuwekwa kwa utaratibu wa kutoa taarifa na Kifungu cha 7(b) kinachoitaka TAKUKURU kushirikisha umma katika mapambano dhidi ya rushwa kwa njia ya elimu. NINI CHIMBUKO LA HUDUMA YA NAMBARI 113? Huduma ya simu ya dharura 113 ilikuwepo tangu miaka ya 2000 kupitia Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) ambapo zilitumika simu za mezani kwa lengo la kumwezesha mwananchi kuwasiliana na Taasisi bila ya kutozwa gharama yoyote. Hata hivyo huduma hiyo haikuwafikia wananchi wengi. Mwaka 2015, ili kwenda na wakati ambapo wananchi wengi walitumia simu za kiganjani kwa mawasiliano, TAKUKURU iliunganisha nambari 113 na baadhi ya mitandao ya simu za kiganjani. Hatua hii ilipata msukumo zaidi wa Sheria ya Mawasiliano ya mwaka 2003 inayozitaka kampuni za simu kuwezesha baadhi ya taasisi kuwa na huduma ya dharura ya mawasiliano. Aidha, mwaka 2016 TAKUKURU iliboresha huduma hii kwa kupanua wigo wa matumizi ya nambari 113 ambapo sasa kwa kutumia simu ya kiganjani mwananchi anaweza kuwasiliana na TAKUKURU kwa namna tatu tofauti ambazo zimeelezewa katika andiko hili. HUDUMA HII INAPATIKANA KUPITIA MITANDAO GANI? Mitandao ya simu iliyounganishwa na huduma ya nambari 113 ni TTCL, TIGO, AIRTEL, HALOTEL, VODACOM na ZANTEL.

JE, NAMBARI 113 INATUMIKA VIPI? • Kupiga simu nambari 113 na kutoa malalamiko au taarifa za vitendo vya rushwa. • Kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) kwenda nambari 113 na kutoa malalamiko au taarifa za vitendo vya rushwa. • Kupiga *113# (USSD) na kufuata maelekezo ya kuwasilisha taarifa za vitendo vya rushwa. Inashauriwa mwananchi ajaze maelezo kuhusu taarifa yake kadiri mfumo unavyomuelekeza ili taarifa ijitosheleze kuiwezesha TAKUKURU kuifanyia kazi. MAELEKEZO YAKE NI KAMA IFUATAVYO

NINI MANUFAA YA KUTUMIA HUDUMA HII? Haraka Ni njia ya HARAKA na inayomuwezesha mwananchi kuwasiliana na TAKUKURU wakati wowote na popote na kushughulikia tatizo lake hivyo kupunguza uwezekano wa vitendo vya rushwa kufanyika. Siri • Mwananchi anapowasiliana na TAKUKURU halazimiki kujitambulisha na hata akifanya hivyo, utambulisho huo unakuwa siri kati yake na TAKUKURU. • Mwananchi anaweza kutoa taarifa akiwa eneo la tukio bila watu wengine kusikia au kufahamu kuwa anawasiliana na TAKUKURU. Hili ni rahisi zaidi kwa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS). Haina gharama Mwananchi anapotumia huduma hii hatozwi gharama yoyote na kampuni ya simu na wala hahitaji kusafiri kutoka alipo hadi Ofisi ya TAKUKURU ili kutoa taarifa. Anapata huduma hii pale alipo na BURE hata simu yake isipokuwa na fedha ya kufanya mawasiliano. Wigo mpana - inawafikia wananchi wengi Huduma ya simu nambari 113, pasipo vizingiti vya muda, mahali au hali na kutokana na maendeleo ya teknolojia, imewafikia wananchi wengi kwa sababu wanamiliki na kutumia simu za viganjani kuwasiliana.


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.