
7 minute read
Sura 36. Migogoro Inayokaribia
Tangu mwanzo kabisa wa vita kubwa mbinguni, kusudi daima la Shetani lilikuwa kuvunja sheria ya Mungu. Kwa yeye kufikia kusudi lake ni kukataa sheria yote ama kukataa mojawapo ya amri zake, matokeo yatakuwa namna moja. Mtu anayekosa “katika neno moja tu” anaonyesha zarau kwa sheria yote; mvuto wake na mfano yanakuwa kwa upande wa kosa; anakuwa mwenye kukosa juu ya yote”. Yakobo 2:10.
Shetani amepotesha mafundisho ya Biblia, na kwa hivi makosa yakaingia katika imani ya maelfu. Mapigano makubwa ya mwisho kati ya ukweli na uwongo ni juu ya amri ya Mungu, kati ya Biblia na dini ya uwongo na mambo ya asili. Biblia inafikia wote, lakini wachache tu wanaoikubali kama kiongozi cha uzima. Katika kanisa wengi wanakana nguzo za imani ya Kristo. Uumbaji, kuanguka kwa mtu, upatanisho wa Yesu Kristo kwa kufa kwake, na sheria ya Mungu hutawaliwa yote ao sehemu. Maelfu wanaizania kuwa kama ushuhuda wa uzaifu kuweka tumaini kamili katika Biblia.
Advertisement
Ni rahisi kufanya sanamu na maelezo ya uwongo kama kufanya sanamu ya mti ao jiwe. Kwa kueleza Mungu vibaya, Shetani anaongoza watu kumzania katika tabia ya uwongo. Sanamu ya utilivu imewekwa katika pahali pa Mungu mwenye uhai kama anavyofuniliwa katika Neno lake, katika Kristo, na katika kazi ya uumbaji. Mungu wa watu hodari wengi, watunga mashairi, watu wa siasa, waandishi wa habari kwa magazetu-wa vyuo vikubwa (universités) vingi, hata wavyama vya elimu ya tabia na za Mungu na dini (théologie) ni afazali kidogo kuliko Bali, mungu wa jua wa Foiniki katika siku za Eliya. Hapana kosa linalofika kwa ujasiri zaidi juu ya mamlaka ya Mungu, hapana linalokuwa mbaya zaidi katika matukio yake, kuliko mafundisho ya kwamba sheria ya Mungu haina na masharti tena. Ufikiri ya kama wahuduma wenye kujulikana walikuwa wakifundisha kwa wazi ya kuwa sheria zinazotawala inchi yao hazikuwa za lazima, ya kama zilizuia mambo ya uhuru wa watu na haiwapashwi kutiiwa; muda gani watu kama wale wangevumiliwa katika mimbara?
Ingekuwa muaminifu zaidi kwa mataifa kuvunja sheria zao kuliko kwa mtawala wa viumbe vyote kutangua sheria yake. Jaribio la kufanya nafasi sheria ya Mungu lilijaribiwa katika Ufransa wakati kukana Mungu ulipokuwa na uwezo wa kutawala. Ilionyeshwa ya kwamba kwa kutupa amri ambazo Mungu aliamuru ni kukubali kanuni ya mtawala wa uovu.
Kuweka Kando Sheria ya Mungu
Wale wanaofundisha watu kutunza sheria za Mungu kwa urahisi wanapanda uasi kwa kuvuna uasi. Kuacha amri iliyoamuriwa kwa sheria ya Mungu kuweka yote kando, na sheria za kibinadamu kwa upesi hazitajaliwa. Matokeo ya kutangua amri za Mungu ingekuwa kama hazikutumainiwa. Mali hayangekuwa tena na usalama. Watu wangekamata milki ya jirani zao kwa jeuri, na walio hodari zaidi wangekuwa watajiri kuliko. Maisha yenyewe hayangeheshimiwa Kiapo cha ndoa hakingedumu tena kuwa kama boma kwa kulinda jamaa. Yeye aliyekuwa na uwezo angekamata mke wa jirani yake kwa jeuri. Amri ya tano ingekuwa kando pamoja na ya ine. Watoto hawangekataa kukamata maisha ya wazazi wao kama kwa kufanya vile wangeweza kupata tamaa ya mioyo yao iliyoharibika. Ulimwengu uliostaarabika ungekuwa kundi la wezi na wauaji wa siri, na amani na furaha ingekomeshwa duniani.
Tayari mafundisho haya yamefungua milango ya uovu ulimwenguni. Bila sheria na uovu vinafiagia kama pepo kali ya kipwa. Hata katika nyumba za wale wanaojidai kuwa Wakristo kunakuwa unafiki, mvunjo wa urafiki, usaliti wa matumaini matakatifu, upendeleo wa tamaa mbaya. Kanuni za dini, msingi wa maisha ya ushirika, unaonekana wa kutikisika sana karibu kuanguka. Wavunja sheria waovu mara kwa mara wanafanywa kuwa wenye kupokea mambo ya uangalifu kama kwamba walifikia sifa nzuri. Matangazo makubwa yametolewa kwa makosa yao. Mtambo wa kupiga chapa unatangaza maelezo ya uasi wa uovu, kuingiza wengine katika madanganyo, wizi, na uuaji. Kupumbazuka kwa kosa, kukosa kuwa na kiasi kwa kutisha na uzalimu wa namna yo yote ulipasa kuamsha mambo yote. Ni kitu gani kinaweza kufanyika kuzuia mwendo wa uovu?
Kukosa Kiasi Kumetia Wengi Katika Mashaka
Baraza za hukumu zimeharibika, watawala wamevutwa na tamaa kwa faida na upendo wa anasa za mambo ya uasherati. Kukosa kiasi kumetia wengi katika mashaka hivyo Shetani amekuwa na utawala karibu kamili juu yao. Wana sheria wamapotoshwa, wanavutwa kwa feza (rushwa), wamedanganyika. Ulevi na ulafi, udanganyifu wa kila namna, unaonekana miongoni mwa wale wanaosimamia sheria. Sasa Shetani hawezi tena kulinda ulimwengu chini ya utawala kwa njia ya kuzuia Maandiko, anatumia njia zingine kwa kutimiza kusudi lile lile moja. Kwa kuharibu imani katika Biblia ni kutumia pia kuharibu Biblia yenyewe.
Ni kama katika miaka ya kwanza, alikuwa akitumika katika makanisa kuendelesha mashauri yake. Kwa kupinga mambo ya ukweli yasiyokuwa ya watu wengi katika Maandiko, wanatumia maelezo ambayo yanapenda kueneza mbegu za mashaka. Kushikama na kwa kosa la Papa la maisha ya milele ya asili na ufahamu wa mtu katika mauti, wanakataa ulinzi wa kipekee juu ya madanganyo ya elimu ya kuwa roho za watu waliokufa kurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme). Mafundisho wa maumivu mabaya ya milele yameongoza wengi kuwa kutoamini Biblia. Kwa madai ya amri ya ine yanavyoshurutisha, inaoonekana ya kuwa kushika Sabato ya siku ya saba kunaamriwa; na kwa namna inavyokuwa njia moja tu kwa kujiokoa wenyewe kwa shuguli ambayo hawataki kuifanya, waalimu wa watu wote wakatupilia mbali sheria ya Mungu na Sabato pamoja. Kama matengenezo ya Sabato inavyoenea, kukataa huku kwa sheria ya Mungu kwa kuepuka amri ya ine kutakuwa karibu kuenea pote. Waongozi wa dini wanafungua mlango kwa kumkana Mungu, kwa imani ya kuwa roho za watu waliokufa kurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme), na zarau kwa sheria takatifu ya Mungu-daraka la kutisha kwa uovu unaokuwako katika jamii la Kikristo.
Kwani jamii lilelile linalodai ya kama mkazo wa kushika siku ya kwanza (dimanche) kungesitawisha mafundisho yahali ya kijamii. Ni mojawapo ya mashauri ya Shetani kuchanganya uwongo na ukweli shauri laonekana kuwa njema. Waongozi wa mwendo wa siku ya kwanza (dimanche) wangeshindania matengenezo ambayo watu wanahitaji, kanuni katika umoja pamoja na Biblia; lakini wakati ambao kunakuwa na madai pamoja na hizi kinyume kwa sheria za Mungu, watumishi wake hawawewzi kujiunga pamoja nao. Hakuna kitu kinachoweza kuthibitika kuweka kando amri za Mungu kwa ajili ya amri za watu.
Katika makosa mawili makubwa, kutokufa kwa nafsi na utakatifu wa siku ya kwanza (dimanche), Shetani ataleta watu chini ya madanganyo yake. Wakati kosa la kwanza linapowekwa msingi wa imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisma), kosa la mwisho hufanya kifungo cha huruma pamoja na Roma. Waprotestanti wa Umoja wa Mataifa ya Kiamerika watakuwa wa kwanza kunyoosha mikono yao ngambo ya shimo kubwa kushika mkono wa imani ya kuwa roho za watu walikufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (Spiritualisme); wakifikia kwa shimo kubwa kukumbatia mikono na mamlaka ya Roma. Na chini ya mvuto wa umoja huu wa mara tatu, inchi hii itafuata katika hatua za Roma kwa kukanyanga haki za zamiri.
Kwa namna imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme) , inakuwa na uwezo mkubwa kwa kudanganya. Shetani yeye mwenyewe “hujigeuza”. Ataonekana kama malaika wa nuru. Kwa njia ya imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu, miujiza itafanyika, wangonjwa wataponyeshwa, na maajabu mengi yasiyokukanishwa yatafanyika.
Wafuasi wa kanisa la kiroma wanaojisifu juu ya miujiza kuwa alama ya kanisa la kweli watadanganyika upesi kwa uwezo huu wa kufanya miujiza; na Waprotestanti, wanapokwisha kutupia mbali ngao ya ukweli, watadanganyika vile vile. Wafuasi wa kanisa la Roma, Waprotestanti, na watu wapendao anasa za dunia wataonekana vivyo hivyo katika umoja huu mabadiliko makubwa kwa ajili ya toba ya ulimwengu.
Kwa njia ya imani ya kuwa roho za watu waliokufa hurudi na kujionyesha na kuongea na watu (spiritualisme), Shetani hutokea kama mtenda mema wa kabila, kuponyesha magonjwa na kuonyesha kawaida mpya ya imani ya dini, lakini wakati ule ule anaongoza wengi kwa maangamizi. Kukosa kiasi kunaondoa akili; mapendeleo ya anasa, vita, na kumwanga damu hufuata. Vita huamsha tamaa mbaya sana ya nafsi na kufutia kwa milele mateka wake walioloanishwa katika uovu na damu. Nikusudi la Shetani kuchochea mataifa kwa vita, kwani anaweza kupotosha watu kwa matayarisho ya kusimama kwa siku ile ya Mungu.
Shetani amejifunza siri za maumbile, na anatumia uwezo wake wote kutawala mwanzo kadiri Mungu anavyoruhusu. Ni Mungu anayelinda viumbe vyake kutoka kwa mharibu. Lakini jamii ya Ukristo limeonyesha zarau kwa sheria yake, na Bwana atafanya kile alichotangaza ya kwamba-angeondoa ukingaji wa ulinzi wake kwa wale wanaoasi kwa sheria yake na kukaza wengine kufanya pamoja. Shetani anakuwa na utawala wa wote ambao Mungu asio walinda kwa kipekee. Atasaidia na kusitawisha wengine, ili kuzidisha makusudi yake wenyewe; na ataleta taabu kwa wengine, na kuongoza watu kuamini ya kama ni Mungu ndiye anayewatesa.
Anapotokea kama tabibu mkuu anayeweza kuponya magonjwa yao yote, Shetani ataleta ugonjwa na msiba hata miji ya watu waingie kwa maangamizi. Katika misiba baharini na inchini, katika mateketeo makubwa, katika tufani kali na mvua ya mawe, katika zoruba, garika, kimbunga, mawimbi ya maji kujaa, na tetemeko la inchi, katika namna maelfu, Shetani anatumia uwezo wake. Anaondolea mbali mavuno yenye kukomea yote, na njaa na taabu hufuata. Hugawanya mawaa ya mauti angani, na maelfu huangamia.
Ndipo mdanganyifu mkubwa atashawishi watu kutwika taabu zao zote kwa wale wanaokuwa na utii kwa amri za Mungu ni laumu la daima kwa wakosaji. Itatangazwa ya kama watu wanamkosea Mungu juu ya mvunjo wa siku ya kwanza, ya kwamba zambi hii imeleta misiba ambayo haitakoma hata kushika kwa siku ya kwanza kutakapo kazwa kabisa.
“Wale wanaoharibu heshima kwa ajili ya siku ya kwanza wanazuia kurudishwa kwa majaliwa ya Mungu na kufanyikiwa”. Kwa hivyo mashitaki yaliyofanywa ya zamani juu ya watumushi wa Mungu yatakaririwa. “Wakati Ahaba alipomuona Eliya, Ahaba akamwaambia: Ni wewe mwenye kutaabisha Israeli”? 1 Wafalme 18:17,18. Uwezo wa kufanya miujiza utatumia mvuto wake juu ya wale wanaomtii Mungu kuliko watu. “Pepo” watatangaza ya kama Mungu amewatuma kusadikisha wanaokataa siku ya kwanza kwa kosa lao. Watalilia uovu mkubwa ulimwenguni na kusaidia ushuhuda wa waalimu wa dini ya kama hali iliopoteza cheo cha mafundisho imaletwa na ukufuru wa siku ya kwanza
Chini ya utawala wa Roma, wale walioteseka kwa ajili ya habari njema walishitakiwa kama watenda maovu katika mapatano pamoja na Shetani. Ndivyo hivyo itakavyokuwa sasa. Shetani ataletea wale wanaoheshimu sheria ya Mungu kushitakiwa kuwa watu wanaoleta hukumu duniani. Kwa njia ya kutisha anajaribu kutawala zamiri, anasukuma watawala wa dini na wa dunia kukaza sheria za kibinadamu katika kuasi sheria ya Mungu.
Wale wanaoheshimu Sabato ya Biblia watashitakiwa kuwa adui wa sheria na ukimya, kuvunja amri za maana za kijamii, kuleta machafuko ya mambo ya utawala na makosa, na kuita hukumu za Mungu inchini. Watashitakiwa juu ya chuki kwa serekali. Wajumbe wanaokana kanuni ya sheria ya Mungu wataonyesha kwa mimbara shuguli ya utii kwa utawala wa dunia. Katika vyumba vikubwa vya kufanya sheria na baraza za hukumu, wanaoshika amri watahukumiwa. Rangi ya uwongo itatolewa kwa maneno yao; maana mbaya kuliko itawekwa kwa mashitaki yao.
Wakuu wa kanisa na serekali watajiiunga kwa kushawishi ao kushurutisha wote kuheshimu siku ya kwanza. Hata katika watawala wa Kiamerika wenye uhuru na wenye kufanya sheria watakubali matakwa ya watu wote kwa ajili ya sheria ya kukaza kushika siku ya kwanza. Uhuru wa zamiri ambao umegaramishwa kwa kafara kubwa hauta heshimiwa tena. Katika kuja kwa karibu kwa shindano tutaona kuonyesha kwa mfano maneno ya nabii, “Joka akakasirikia yule mwanamke, akakwenda zake kufanya vita juu ya wazao wake waliobaki, wanaoshika amri za Mungu, na kuwa na ushuhuda wa Yesu Kristo”. Ufunuo 12:17.