Skip to main content

Swahili - God-given Breath

Page 1

Pumzi Iliyotolewa na Mungu Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA. Msifuni BWANA. Zaburi 150:6

Pentateuki BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. Mwanzo 2:7 Nami, tazama, mimi, naam, ninaleta gharika ya maji juu ya nchi, ili kuharibu kila kitu chenye mwili chenye pumzi ya uhai chini ya mbingu; na kila kitu kilicho duniani kitakufa. Mwanzo 6:17 Wakaingia kwa Nuhu ndani ya safina, wawili wawili wa kila chenye mwili, ambamo mna pumzi ya uhai. Mwanzo 7:15 Kila kitu chenye pumzi ya uhai puani mwake, vyote vilivyokuwa katika nchi kavu, vilikufa. Mwanzo 7:22 Lakini katika miji ya watu hawa akupao BWANA, Mungu wako, iwe urithi, usihifadhi hai kitu cho chote kinachopumua; Kumbukumbu la Torati 20:16

Historia Basi Yoshua akapiga nchi yote ya vilima, na ya kusini, na ya bonde, na ya chemchemi, na wafalme wake wote; hakumwacha hata mmoja aliyesalia, bali aliwaangamiza kabisa wote waliokuwa na pumzi, kama BWANA, Mungu wa Israeli, alivyoamuru. Yoshua 10:40 Wakawapiga roho wote waliokuwamo kwa makali ya upanga, wakawaangamiza kabisa; hakusalia mtu wa kupumua; akauteketeza Hazori kwa moto. Na nyara zote za miji hii, na wanyama, wana wa Israeli wakatwaa kuwa mawindo yao wenyewe; lakini kila mtu wakampiga kwa makali ya upanga, hata walipokwisha kuwaangamiza, wala hawakumwacha hata mmoja wa kupumua. Yoshua 11:11,14 Na mifereji ya bahari ikaonekana, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, kwa kukemea kwa BWANA, kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake. 2 Samweli 22:16 Ikawa, alipotawala, akawapiga nyumba yote ya Yeroboamu; hakumwachia Yeroboamu hata mmoja mwenye pumzi, hata alipokuwa amemwangamiza, sawasawa na neno la Bwana, alilolinena kwa mtumishi wake Ahiya, Mshiloni; 1 Wafalme 15:29 Ikawa baada ya hayo, mwana wa mwanamke huyo, bibi wa nyumba hiyo, akaugua; ugonjwa wake ukawa mwingi sana, hata pumzi yake ikawa haipo tena. 1 Wafalme 17:17

Ushairi Kwa pumzi ya Mungu huangamia, Na kwa pumzi ya puani mwake huangamia. Ayubu 4:9


Turn static files into dynamic content formats.

Create a flipbook
Swahili - God-given Breath by Filipino Tracts and Literature Society Inc. - Issuu