Visa vya Wachamungu

Page 57

Visa vya wachamungu final Lubumba.qxd

5/15/2010

8:54 AM

Page 51

Visa vya wachamungu sokoni pamoja. Walipokuwa njiani Mtume (s.a.w.w) alimuona msichana mjakazi, ambaye alikuwa akilia. Alimuendea na kumuuliza: “Kwa nini unalia?” “Tajiri yangu amenipa dirham nne niende kununua vitu kutoka sokoni. Sijui pesa hizo zilipotea vipi. Sasa nahofia kwenda nyumbani.” Katika zile dirham kumi na mbili, Mtume Muhammad (s.a.w.w) alimpa dirham nne yule msichana na akamuambia; “Nunua ulichokuwa unataka ununue na urudi nyumbani.” Mtume (s.a.w.w) mwenyewe alikwenda sokoni na baada ya kununua kanzu kwa dirham nne, akaivaa. Alipokuwa akirundi nyumbani alimuona bwana mmoja ambaye alikuwa hajavaa nguo. Kwa haraka alivua ile kanzu na akampa. Kisha alimrudia muuzaji na akununua kanzu nyingine ya dirham nne akavaa. Njiani alimuona tena yule msichana mjakazi akiwa ameketi huku akiogopa na kuwa na wasiwasi. Alimuuliza: “Kwa nini haujakwenda nyumbani?” “Ewe Mtume wa Allah nimechelewa sana na naogopa huenda watanipiga na kuniuliza kwa nini nimechelewa hivi.” “Nieleze unapoishi na unifuate ili nikawaombe kwamba wasikuulize kitu chochote.” Mtume Muhammad (s.a.w.w) alimchukua yule msichana na walipofika karibu na nyumba hiyo, msichana alisema ; “Nyumba ndio hii.” Kwa sauti ya juu Mtume wa Allah (s.a.w.w) alisema: “Amani iwe juu yenu enyi watu wa nyumba hii.” Hakupata jibu lolote; aliwaamkia kwa mara ya pili hakupata majibu pia. Aliamkia kwa mara ya tatu na hapo ndipo kila mtu alijibu akisema:

51


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.