Asili ya
ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd
Asili ya Madhehebu
7/1/2011
12:19 PM
Page 57
katika Uislamu
wa vijana wa Peponi.”
Bibi Fatima (a.s.): Mama yake Bibi Fatima (a.s.) yaani Bibi Khadija anaelezea kisa hiki kuhusu wakati wa kujifungua mimba ya mwanawe Fatima (a.s.): “Wakati wa kumzaa Fatima nilituma watu wakaniitie majirani zangu mabibi wa Kikuraishi ili wanipatie huduma za ukunga. Mabibi hao walikataa katakata wakidai kwamba nimewasaliti kwa kumuunga mkono Muhammad katika dai lake la utume. Kwa kitambo fulani nilipatwa na wasiwasi lakini mara nikapatwa na mshangao mkubwa kuwaona wanawake wanne nisiowafahamu, warefu na wenye duara za mwanga nyusoni mwao wakinitokea. Waliponikuta kwenye hali ya kukata tamaa, mmoja wao aliniambia: ‘Ewe Khadija, Mimi ni Sara mama yake Isihaka, na hawa mabibi watatu wengine ni Mariam mama yake Isa, Asia binti Muzahim (bibi huyu alikuwa muumini na mchamungu sana aliyekuwa mkewe kafiri mkuu Firauni enzi za Nabii Musa (a.s.)), na Ummu Kulthum, dada yake Nabii Musa. Tumeamrishwa na Allah tukupatie huduma kutokana na utaalamu wetu wa ukunga.’ Baada ya kusema hivyo, wote wanne walinizunguka wakanihudumia hadi nilipomzaa Fatima.”
Msaada wa Allah kwa Bibi Fatima (a.s.) katika shida: Hapo Madina waliishi Wayahudi matajiri sana. Binti mmoja toka katika hao Wayahudi alikuwa anatayarishwa kuolewa. Wayahudi hawa walisikia habari za ufukara wa Bibi Fatima (a.s.) na habari za mavazi yake makuukuu yasiyo na thamani aliyokuwa akiyavaa daima. Wayahudi hao waliona kuwa huo ndio wakati wa nafasi nzuri ya kumdhalilisha na kumfanya kichekesho Bibi Fatima (a.s.). Muda ulipowadia, walimtuma mjumbe kwa Mtume (s.a.w.w.) kumwomba amruhusu Bibi Fatima (a.s.) ahudhurie harusi hiyo.
57