Asili ya
ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd
Asili ya Madhehebu
7/1/2011
12:19 PM
Page 55
katika Uislamu
Al-Jamius–Saghir, cha As-Suyuti Jz. 2, Uk. 56 Al-Riyadh al-Nadirah, Jz. 2, Uk. 229 “Huyu ni ndugu yangu Ali, wasii wangu na khalifa baada yangu. Kwa hiyo msikilizeni na muwe watiifu kwake.” Hadithi hii inapatikana katika vitabu vifuatavyo : (a) Tarikh-Tabari - Jz. 2, Uk. 319 (b) Tarikh Ibn al - Athir - Jz. 2, Uk. 62 (c) Al - Sirah al-Halabiyah - Jz. 1, Uk. 311 (d) Kanzul -Ummal - Jz. 15, Uk. 15 Kwa maelezo haya pamoja na ushahidi wake katika vitabu vya kutegemewa, vilivyoandikwa na Maulamaa, Wanahistoria na Wanahadithi wajuzi wa dini, sina shaka tunauona utukufu na nafasi ya Ahlul-Bayt wa Mtume (s.a.w.w.) juu ya umma wa kiislamu. Sasa tujaribu kwa ufupi kuona sifa za Ahlul-Bayt (a.s.) wa Mtume (s.a.w.w.). Sifa ambazo zinawatofautisha na binadamu yeyote yule mbali na Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe. Sitataja sifa na miujiza ya kila mmoja katika wale viongozi (Makhalifa) 12 aliowataja, kwani hiyo ni historia ndefu ya miaka 244 yaani muda ambao waliishi; kabla ya kiongozi wa mwisho yaani wa 12 (a.s.) hajafichwa na Mwenyezi Mungu machoni pa watu, lakini yupo hai hapa duniani akisubiri kazi maalumu aliyoamrishwa na Mwenyezi Mungu kuifanya itakapowadia. Suala hili la kufichwa Imam wa 12 (a.s.) tusimwone ingawa yupo, linahitaji maelezo marefu, kitabu kizima cha peke yake, kwa ushahidi wa mafunzo ya Mtume (s.a.w.w.) na Qur’ani. Lakini nitajitahidi kutoa maelezo muhimu ili kukamilisha picha ya wasia wa Mtume kwamba viongozi (Maimamu 12) aliowataja wataongoza umma wa kiislamu hadi Siku ya Kiyama. Tukumbuke kuwa hata kwenye Biblia utabiri wake ni huo huo yaani ni sawa na maneno ya Mtume (s.a.w.w.).
55