Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 58

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:19 PM

Page 43

katika Uislamu

Hadithi za Mtume (s.a.w.w.) kuhusu uongozi nyuma yake: Baada ya maelezo hayo muhimu, sasa turejee nyuma kabisa tulikoishia kuhusu hoja zetu Shia Ithna’asheri kwamba Mtume (s.a.w.w.) aliacha wasia kuhusu uongozi wa Waislamu nyuma yake. Suala hili kimsingi halistahili kuwa na maelezo marefu iwapo Waislamu tungekuwa waaminifu. Nina maana kwamba katika vitabu vya kutegemewa nilivyovitaja nyuma kuna Hadithi za Mtume (s.a.w.w.) ambazo ni ‘mutawatir’ zinazoeleza suala hili. Kwa kawaida Hadithi za Mtume (s.a.w.w.) zimegawanywa katika mafungu mbali mbali kuhusu kama ni za kutegemewa au zinafaa au zisizoaminika au zisizo na ubishi au zisizofaa kabisa. Huu ni utaratibu uliokubalika na wanavyuoni wote wa Shia Ithna’asheri na Sunni (Ahlul Sunna wal-Jamaa). Kwa hiyo iwapo Hadithi ni Mutawatir (isiyo na ubishani) maana yake ni kwamba itekelezwe kama ilivyo bila kusita. Hata hivyo ili kufupisha ubishi, naweza nikatoa Hadithi moja tu ‘Mutawatir’ kwa ushahidi. Lakini uzoefu unaonyesha kuwa binadamu tuna tabia ya kukwepa ukweli kama isemavyo (Qur’ani 75:31-32). Kutokana na ukweli huo nitalazimika kutoa karibu Hadithi zote muhimu pamoja na kwamba hata moja ingetosha! Tungekuwa waaminifu tungepokea maneno ya Mtume (s.a.w.w.) na kuyatekeleza japo iwe Hadithi moja tu mradi ni ya kweli. Je, angekuwa hai tungeacha kumtii? Mtiririko wa historia fupi ya utukufu wa Bani Hashim utaishia kwanza pale ambapo Mtume (s.a.w.w.) alipozaliwa mwaka 570 A.D. Nisingependa kuelezea kipindi kabla Mtume (s.a.w.w) hajaruhusiwa kutangaza Utume wake, kwa sababu kipindi hicho si muhimu sana kuhusiana na somo letu juu ya utukufu wa Bani Hashim.

Hadithi ya Kwanza: Mtume (s.a.w.w.) alipopata umri wa miaka 40 yaani mwaka 610 A.D. alik43


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.