Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 449

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:26 PM

Page 434

katika Uislamu

zoea kusikia kwa wenzetu kuwa eti ni haramu kumlilia marehemu ambaye inadaiwa huadhibiwa kwa vilio hivyo! Nimetangulia kusahihisha imani hiyo kwamba, bibi Aisha alimsahihisha Umar kwa kusema kuwa, ‘Mwenyezi Mungu amsamehe Umar, Mtume (s.a.w.w.) alisema kuwa kafiri huadhibiwa iwapo atakufa na watu wakamlilia.’ Kwa hiyo mtu anayefaa kuliliwa ni muumini peke yake. Ukweli ni kwamba kuwa Mwislamu siyo kuwa muumini moja kwa moja! Kuna matendo mengi na itikadi nyingi potofu ambazo ukizikumbatia unageuka kafiri bila kujijua! Mwenye kujua siri ya kila Mwislamu ni Mwenyezi Mungu. Kwa tahadhari ni bora tuache kuwalilia marehemu kwa kuwa hatujui matendo yao kama bado ni Waislamu au Waumini au Makafiri? Kwa mfano tunasikia Mashekhe wengi wanasema kuwa Mwislamu akiacha Swala tano huwa ni kafiri, na kwamba tofauti kati ya Mwislamu na Kafiri ni Swala tano. Tujiulize hilo peke yake linabakiza Waislamu wangapi miongoni mwetu? Zaidi ya hayo bado kuna kasoro nyingine nyingi kama kupiga ramli na ushirikina wa aina mbali mbali n.k. Je, tunapomlilia marehemu tuna hakika kuwa kasafika na hayo? (b) Kukusanyika Waislamu kwa wafiwa: Mkusanyiko unaotakiwa ni ule wa kutayarisha mazishi ya marehemu. Mambo ya wajibu kwa Waislamu ni kuosha maiti na kumkafini, kumsalia na kumzika. Gharama za sanda ni wajibu zitokane na mali za marehemu. Iwapo Waislamu watachanga pesa kugharimia sanda, siyo wajibu bali ni sadaka. Inasisitizwa kila Mwislamu anunue sanda akae nayo katika uhai wake; ni thawabu kuiangalia kila siku. Ni wajibu kwa Waislamu kumwosha maiti bure bila ujira. Kwa mafunzo sahihi ya dini, ni kwamba kumwosha maiti kwa ujira ni sawa na kumzika bila kumwosha! Kwa hiyo tabia ya siku hizi iliyoenea kote ya waoshaji kuweka viwango vya ujira, siyo sahihi. Waislamu wote tunapaswa kupata mafunzo ya kuosha na kukafini maiti na ndiyo maana wajibu huo ni juu ya Waislamu wote wa mji au kijiji alikofariki Mwislamu, mpaka apatikane japo Mwislamu mmoja atimize wajibu huo, la sivyo Waislamu wote wa 434


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.