Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 441

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:25 PM

Page 426

katika Uislamu

zetu tano. Sasa hivi tofauti hizo zimeongezeka miongoni mwetu, baada ya itikadi mpya za Kiwahabi kuingia katika Uislamu. Yote haya ni changamoto kwetu Waislamu. Inatubidi tujiulize: Kwa nini Qur’ani haijabadilika hata nukta, lakini kanuni nyingine (hukumu) za dini zinahitilafiana, wakati ambapo Mtume (s.a.w.w.) ni yule yule aliyetuletea Qur’ani na mafunzo mengineyo? Qur’ani ilishuka kwa miaka 23. Katika muda huo Mtume (s.a.w.w.) alionyesha kwa vitendo hukumu zote za dini. Kwa nini Qur’ani isalimike lakini mafunzo mengineyo yapotee? Kipi kigumu kati ya kukariri msahafu wote wa Qur’ani, na kukumbuka mafunzo ya ibada za kila siku za Mtume (s.a.w.w.) kama Swala tano? Hapa tunaona wazi kuwa, zilikuwepo njama za makusudi kupotosha dini baada ya kufariki Mtume (s.a.w.w.). Na huo ndio ukweli wa kihistoria kama nilivyoeleza kwa kirefu katika sura za nyuma, hasa katika historia juu ya ukusanyaji wa Hadithi mbali mbali za Mtume (s.a.w.w.) Kwa hiyo ni wajibu wetu kama Waislamu waaminifu, kuhakikisa kuwa, tunachunguza na kutekeleza mafunzo sahihi ya kiongozi wetu mpendwa Nabii Muhammad (s.a.w.w.). Waislamu tusiridhike na kurithi dini bila kuchunguza ukweli wake. Kwa mfano suala la kutoa Zaka ya mali na Zaka ya Khums - (Qur’ani 8:41), ni wajibu kwetu lakini hatujali kutoa. Hukumu za madhehebu yetu matano zinatambua Zaka hizi japo kwa viwango na kanuni tofauti. Baadhi ya Sunni wanaojali kutoa Zaka, hawatambui Zaka ya Khums! Kanuni sahihi za kutoa Zaka ya mali hazizingatiwi! Tukumbuke maneno ya Mtume (s.a.w.w.) aliposema kuwa, ‘Umma wangu baada yangu utagawanyika makundi 73 hadi siku ya Kiyama, na makundi yote yataangamia motoni (kwa upotofu) isipokuwa kundi moja tu litakalonusurika (kwa uongofu) Rejea: Sahihi Muslim, Jz.8 uk.7. Maana yake ni kwamba Uislamu ni mmoja tu mbele ya Mwenyezi Mungu. Je, ni Uislamu upi huo? Kuhusu hukumu tofauti miongoni mwa madhehebu, Rejea: Manhajul-Fiqhil-Islam - cha S.H. Al Musawi, Islamic Republic of Iran.

426


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.