Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 429

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:25 PM

Page 414

katika Uislamu

duniani ambayo Katiba yake ni ya kiislamu na sheria zake vile vile. Nchi hiyo ni Jamhuri ya Kiislam ya Watu wa Iran. Pamoja na nia nzuri ya marehemu Imam Khomeini (R.A.) kuongoza harakati ndefu za kufufua Uislamu nchini humo, bado kuna makundi ya upinzani yanayopinga utawala huo! Je, nchi zetu ambazo tunaishi watu wa dini tofauti kwa miaka mingi, vipi itawezekana zitawaliwe na sheria za kiislamu? Faida gani kukazania malengo yasiyowezekana? Mwezi wa pili mwaka 2000, dunia nzima ilielekeza masikio nchini Iran ili kujua matokeo ya uchaguzi wa wabunge wapya. Vyombo vya habari vilitangaza kwa furaha kwamba matokeo yanaonyesha kuwa, wamechaguliwa wabunge wengi wapenda mageuzi, na kwamba wabunge wasiopenda mageuzi ni wachache, na kwa hiyo bunge litakuwa na uwezo mkubwa wa kupitisha maamuzi ya kuwapa raia uhuru zaidi wa mambo yao. Matokeo hayo yana maana kwamba raia wa Iran walio wengi hawapendi kubanwa na sheria za Mwenyezi Mungu bali wanataka kujitungia sheria kwa manufa yao ya kidunia. Lakini nimeeleza huko nyuma kuwa Taifa la Serikali ya kiislamu ni lile ambalo mambo yake yote yanaongozwa na Sharia sahihi ya kiislamu kwa ushahidi wa Qur’ani:

“Haiwi kwa muumin mwanamume au muumin mwanamke kuwa na uchaguzi katika mambo yao wakati Mwenyezi Mungu na Mtume Wake wameshakata shauri.” (Qur’ani 33:36)

“Sikuwaumba majini na binadamu ila waniabudu” (Qur’ani 51:56).

414


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.