Asili ya
ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd
7/1/2011
12:18 PM
Page D
Š Haki ya kunakili imehifadhiwa Ni lazima ipatikane idhini ya maandishi kwa Taasisi yoyote ya Kiislamu au Mwislamu anayetaka kuchapisha kitabu hiki kwa shughuli ya Tabligh. Idhini ya kufasiri kitabu hiki katika lugha nyingine yaweza kutolewa pia kwa masharti ya kutuma nakala yake kwa mtungaji. Kitabu hiki kimekusudiwa kwa wasomaji wenye kuzama katika kutafakari mambo kwa undani, hali ya kuwa wako tayari kuiona haki na kuikubali, japo haki hiyo inatambuliwa na kukubalika na watu wachache. (Qur’ani: 6:116) Mwenye kupinga kila hoja kwa sababu ya ujinga wake, atabakia kipofu asiyeuona ukweli. - Mtume (s.a.w.w.) Saa moja ya kutafuta elimu ni bora mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko ibada ya miaka sitini. - Mtume (s.a.w.w.) Usingizi wa mtu mmoja mwenye elimu ni bora mbele ya Mwenyezi Mungu kuliko ibada ya usiku mzima ya kundi la wajinga elfu moja. Mtume (s.a.w.w.) Tafuta elimu toka mberekoni hadi kaburini - Mtume (s.a.w.w.) Kusikiliza ukweli, sio kila sikio linafaa, kama vile chakula kwa kila ndege si kimoja na kilekile. - Mshairi wa Kihindi: Rumi
D