Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 365

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:24 PM

Page 350

katika Uislamu

hayo hayakutumika? Au baada ya kufariki Muawiyah kwa nini Sunna zake potofu ziliendelea na Waislamu hawakuachana nazo hadi miaka 40 baada ya Muawiyah! Kisha tumeona kuwa baadhi ya Sunna hizo bado zinaendelea mpaka leo kama vile kufunga mikono katika swala! Tumeona pia kwamba Waislamu walitekeleza amri ya Muawiyah ya kumlaani Imam Ali (a.s.) katika Swala za Ijumaa na Idd kwa miaka 60 hata baada ya yeye Muawiyah kufariki! Hizo ndizo hoja muhimu kihistoria kuhusu Ahlul Sunna Wal- Jamaa. Kwa kadri ya historia sahihi ni kwamba, Waislamu waliomtii Muawiyah na wakaitwa Ahlul Sunna Wal-Jamaa (Sunni), waliendelea kujitambulisha hivyo na vizazi vyao, mpaka dini ikadidimia kabisa, na mwisho akazaliwa Abu Hanifa na harakati zake za kutaka kufufua Uislamu, miaka kama 100 baada ya kufariki Mtume (s.a.w.w). Ni kitu gani kilichosababisha Abu Hanifa aanzishe harakati za kuufufua Uislamu baada ya miaka yote hiyo tangu kufariki Bwana Mtume (s.a.w.w.)! Bila shaka ni kwa sababu ya watawala wabovu waliodidimiza Uislamu hadi Waislamu wakapoteza muelekeo! Wafuasi wa Abu Hanifa, Malik, Shafii na Hambal ni Waislamu wale wale waliokuwa wanaitwa Ahlul Sunna wal-Jamaa. Kwa hiyo jina hilo likaendelea chini ya viongozi wapya na kurithishwa kwa vizazi mbalimbali hadi leo hii! Hata kama sasa hivi hatukubaliani na msimamo huo, lakini asili yake ni hiyo. Lakini kwa upande wa Shia Ithna’asheri tumeona jinsi ambavyo Sunna za Mtume (s.a.w.w) zilidumishwa muda wote wa uhai wa Ahlul-Bayt wake (a.s.). Ndiyo maana katika Shia Ithna’asheri matendo na mafunzo yote ya Ahlul-Bayt (a.s.) wa Mtume (s.a.w.w) yanapewa uzito sawa na sunna za Mtume (s.a.w.w), kwa sababu nimeeleza alivyokaririwa Mtume (s.a.w.w) akisema kuwa, “Nawaachieni vizito viwili, (Qur’ani na Ahlul-Bayt wangu) ambavyo havitaachana hadi vinifikie katika kisima cha Kawthar huko Peponi. Jihadharini na mtakavyojihusisha navyo.” Nimeeleza pia jinsi ambavyo Ahlul-Bayt (a.s.) wanaongozwa na Mwenyezi Mungu na ambavyo wamelindwa na dhambi, kwa hiyo mafunzo na matendo yao hayawezi kuwa ya upotofu. (Qur’ani 33:33). 350


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.