Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 36

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:19 PM

Page 21

katika Uislamu

Sababu kubwa ya kueleza ujuzi wangu wa lugha ya kiingereza siyo kujisifu bali nataka ieleweke wazi kuwa ujuzi wa lugha yoyote peke yake, hautoshi kumwezesha mtu kuandika kitabu. Mwandishi wa kitabu chochote kile ni muhimu awe na ujuzi wa uandishi au kipaji cha uandishi. Lazima kitabu kiwavutie waliokusudiwa kukisoma, na maelezo yake yawe na mtiririko unaofaa. Matukio yaelezwe kama yalivyofuatana n.k. Mara nyingi tunasikia wanafunzi wakilalamika kuwa mwalimu fulani ana elimu kubwa lakini hajui kufundisha. Njia za kueneza mafunzo ya Mtume (s.a.w.w.) zipo nyingi. Yawezekana mtu akawa na kipaji cha kutoa hotuba za kuwavuta wasikilizaji. Kwa hiyo ni vizuri anayetaka kufanya ‘tabligh’ kwanza aelewe kipaji chake na aendeleze kipaji hicho. Kwa kweli ujuzi wa lugha ni njia tu ya kupata elimu iliyokusudiwa. Kufikisha elimu hiyo kwa watu wengine, ni suala linalohitaji kipaji au ujuzi mwingine tofauti. ‘Tabligh’ ina misingi yake. Kwa upande mwingine kama sisi wazazi tunataka vijana wetu wawe na moyo wa kuipenda dini, ni muhimu sana sisi wenyewe tuonyeshe mfano wa kujali dini. Mimi baba yangu alifariki nikiwa na miaka miwili tu. Lakini marehemu mama ambaye hakujua kusoma wala kuandika, alikuwa tayari keshafundishwa kuswali Swala tano na marehemu baba! Sikuwahi kumuona mama akipitwa na kipindi cha Swala maisha yake yote! Leo hii sisi elimu tuliyonayo pamoja na urahisi wa kuipata elimu zaidi, bado hatusali! Je! hao watoto wetu vipi wataipenda dini?

21


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.