Asili ya
ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd
Asili ya Madhehebu
7/1/2011
12:24 PM
Page 336
katika Uislamu
DINI SIYO NADHARIA POTOFU ‘DOGMA’ BALI NI TAALUMA Bila shaka uchambuzi huu umeonyesha kuwa yapo mambo mengi ambayo Waislamu wengi hatuyafahamu. Lakini kutofahamu jambo fulani hakulifanyi jambo hilo kuwa halipo. Mfano mzuri ni kwamba kila nchi inayo katiba lakini katika nchi zetu zinazoendelea, ni raia wachache wanaofahamu haki zao zilizomo kwenye katiba! Kwa hiyo akitokea mwananchi akadai haki yake fulani iliyomo kwenye katiba ya taifa lake, hata kama raia wenzake hawadai haki hiyo kwa kutoijua, sidhani kama haki hiyo itabatilika! Katiba ndiyo itahukumu. Katika mtazamo huo, niliyoyaandika hapa yasipuuzwe kwa kuwa walio wengi hawayajui! Mimi naamini kuwa Dini siyo ‘Dogma’ (nadharia potofu). Dini ya kiislamu ni sayansi ambayo hoja zake zote lazima zithibitishwe na zisiwe zenye kupingana na mantiki. Katika Qur’ani tunakuta hoja nyingi za kisayansi kuonyesha kuwa Uislamu siyo ‘Dogma’. Hivyo basi katika Uislamu wa kila siku hatuwezi kuingiza ‘Dogma’ yaani hatuwezi kutenda matendo ambayo hayana ushahidi wowote kuhusu ukweli na uhalali wake. Yawezekana hatuna elimu ya kutosha kutambua tufanye nini, lakini tusijenge hoja za kupingana na ukweli. Tusipoweka bidii kupata ukweli, tutatoa mwanya wa mtu yeyote kupenyeza ‘dogma’ katika dini, kwa kuzusha ibada au tendo lolote lisilo na uhusiano wowote na dini, kama nilivyotoa mifano mingi nyuma, kwa matendo kadhaa tuliyorithi bila uchunguzi wowote wa kielimu. Kama tunaamini kuwa tutahukumiwa Siku ya Kiyama, kwa nini wajibu wetu kiroho usiwe na kanuni maalumu hapa duniani? Vipi Mwenyezi Mungu atuhukumu kwa kukiuka sheria au kanuni ambazo hazikuwekwa wazi kwetu sote! Hiyo siyo sifa ya Mwenyezi Mungu kwa viumbe wake! Kama tunatetea madhehebu ambayo yanatawaliwa na kanuni tofauti, ina 336