Asili ya
ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd
Asili ya Madhehebu
7/1/2011
12:23 PM
Page 259
katika Uislamu
“Mwenyezi Mungu amepiga mfano wa wale waliokufuru, kwa mke wa Nuhu na mke wa Lut, wawili hawa walikuwa chini ya waja wetu wema wawili kati ya waja wetu, basi (wanawake hao) wakawafanyia khiana, (lakini waume zao) hawakuwasaidia chochote mbele ya Mwenyezi Mungu; na ikasemwa: Ingieni motoni pamoja na waingiao.” (Qur’ani 66:10) Kwa hiyo hapa tunaona kuwa mke wa Nabii Nuhu (a.s.) na mke wa Nabii Luti (a.s.) walikufa makafiri kwa vitendo vyao, na kwamba walitupwa motoni! Hivyo basi sisi tunamheshimu bibi Aisha kama mke wa Mtume (s.a.w.w.) lakini hatuna sababu za kufumbia macho matendo yake. Imani yetu ni kwamba hukumu yake ipo kwa Mwenyezi Mungu. Siyo juu yetu kuamua. Vita vya Siffin: Baada ya vita vya Jamal, bwana Muawiyah aliunda jeshi imara la askari 120,000 kwa nia ya kumwondoa madarakani Imam Ali (a.s.). Imam Ali (a.s.) aliunda jeshi la askari 90,000. Baada ya Muawiyah kukataa suluhu, Imam Ali (a.s.) alilazimika kupigana vita hivyo vya Siffin kwa siku 10 tangu tarehe 11 Safar, 37 A.H. Nimetangulia kueleza kuwa Muawiyah alikuwa gavana wa Sham (Syria) tangu enzi za utawala wa bwana Abu Bakr Siddiq. Syria ilikuwa na raslimali nyingi, na Bani Umayyah wengi walihamia huko na hivyo kumfanya Muawiyah kuwa imara kijeshi. Muawiyah alishuhudia kwa masikitiko jeshi lake likiangamizwa na askari hodari wa Imam Ali (a.s.), huku Imam Ali (a.s.) mwenyewe akionyesha 259