Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 270

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:23 PM

Page 255

katika Uislamu

Talha na Zubair walitaka kumkamata gavana wa Basra, Uthman Ibn Hunaif kwa kujidai kumkaribisha kambini kwao lakini gavana alitambua njama hizo za kutaka kumwua na hivyo akakataa. Rejea:- (1) Sahih alBukhari, Jz.12, uk. 68 (Kuhusu Mama Aisha) (2) Tarikh Tabari. Usiku mmoja wa giza, waasi hao walichagua kundi la askari na kuvamia nyumba ya gavana na kumkamata baada ya kufanikiwa kuwaua walinzi wake 40. Jitihada za kumwokoa zilishindwa na mama Aisha akapoteza askari 70 kabla ya kuichukua Basra. Mama Aisha aliulizwa ni adhabu gani apewe gavana huyo, akaamuru auawe, lakini mama mmoja mwenyeji maarufu akaomba hukumu hiyo isitishwe. Ikawa hukumu hiyo imetenguliwa lakini gavana huyo aliteswa sana kwa kung’olewa nyusi na ndevu moja moja na mwisho akawatoroka. Vita vya Jamal Ndogo vilipigwa mnamo tarehe 25 Rabi al-Thani, 36 A.H sawa na 656 A.D. Wafuasi 40 wa Imam Ali (a.s.) waliuawa kwa amri ya mama Aisha, katika msikiti wa Basrah, na wengine 70 sehemu nyinginezo. Bwana Hakim Ibn Jablah aliyekuwa chifu wa ukoo wa Abd al-Qays, na mwenye hekima na elimu, akiwa pia ameikariri Qur’ani yote, alijitokeza na watu wake wakisaidiwa na watu wachache wa ukoo wa Rabiah, wakashambulia jeshi la mama Aisha kwa ushujaa lakini walizidiwa na kuuawa wote. Baada ya hapo likafika jeshi la Imam Ali (a.s.) na Vita vya Jamal Kubwa vikaanza. Vita vya Jamal Kubwa: Huko Madina Imam Ali (a.s.) alipata taarifa za uasi huo wa Talha, Zubair na mama Aisha. Aliingia msikitini na kuwahutubia Waislamu akiwataka wabebe silaha lakini watu walionekana wazito, na baadhi yao waliona labda si sahihi kuingia vita dhidi ya mama Aisha, ingawa Hadithi za Mtume (s.a.w.w.) ziko wazi. Hata hivyo mwisho wake watu walijitokeza kujiunga na jeshi hilo la Imam Ali (a.s.). 255


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.