Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 239

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:22 PM

Page 224

katika Uislamu

(1) Tamko la Ndoa. (Kwa ndoa zote): Tamko rasmi lazima litamkwe na wahusika kwa kauli zao au kwa kuwakilishwa na mawakili wao.

(2) Idhini ya baba au babu wa mke (Ndoa zote): Msichana bikira aliyefikia umri wa kuolewa lazima apate idhini ya baba yake au babu yake. Mwanamke aliyepoteza bikira kwa uzinifu au ndoa iliyotangulia, hahitaji idhini hiyo kuolewa.

(3) Muda wa ndoa utajwe na kiasi cha mahari: Tamko la Ndoa litataja muda wa ndoa na kiasi cha mahari. Mwenye haki ya kupanga mahari ni mwolewaji (mwanamke) katika aina zote za ndoa. Wazazi hawana haki ya kupanga kiasi cha mahari. Na kile kiwango cha pesa ambacho hupangwa na wazazi mfano kama shilingi laki tatu au moja, siyo mahari kidini, bali hiyo ni mila. Kwa hiyo ndoa haiwezi kuzuiwa isifungwe eti kwa mume kushindwa kulipa hizo pesa. Mwanamke awe huru kupanga mahari atakayo, hata kama ni shilingi elfu tano kutegemea hali ya mume na makubaliano kati yao. Na mahari hiyo ni mali ya huyo mke. Masharti mengineyo ya kimila, hayo yanaweza kutekelezwa baadaye lakini yasiingilie kanuni za ndoa za dini ambazo ni muhimu ili ndoa iswihi. Ndoa ni rahisi bali mila ndizo zinakatisha tamaa wanaume na wanawake. (4) Mashahidi (Kwa ndoa zote): Mashahidi si muhimu, kwa sababu ndoa ni ibada sawa na kufunga Swala. Unapofunga Swala huwaiti mashahidi waone ulivyofunga Swala! Au unapochinja kuku huwaiti watu washuhudie kuwa hujala kibudu! Au unapofunga saumu huweki shahidi wa kushuhudia kuwa umefunga kweli! Mashahidi katika ndoa, umuhimu wao ni sharti la serikali kwa ajili ya vyeti vya ndoa basi. Kwa sababu tuelewe kuwa nia ya wewe kuoa au kuolewa imo moyoni mwako. Mashahidi hawajui nia yako kama kweli una nia ya kuoa au huyo mke utamwacha kesho! Sawa na mtu kushinda anatema mate 224


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.