Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 220

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:22 PM

Page 205

katika Uislamu

“Na (pia mmeharamishiwa) wanawake wenye waume isipokuwa wale wanaomilikiwa na mikono yenu ya kulia. Hii ni sheria ya Mwenyezi Mungu juu yenu, pia mmehalalishiwa wasiokuwa hao, ili muwatafute kwa mali zenu pasi na kuzini nao. Na wale ambao mmestarehe nao katika hao, basi wapeni mahari yao yaliyolazimu. Wala si vibaya kwenu (kuwapa kiasi zaidi) katika yale mliyokubaliana, hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi, Mwenye hekima.” ( Qur’ani 4:24 ). Ukichunguza Aya hii utaona kuwa inawazungumzia wanawake wa aina tatu kama ifuatavyo: Wanaomilikiwa na mikono yenu ya kulia: Katika madhehebu ya Shia Ithna’asheri, tafsiri yake ni wanawake watumwa waliotekwa katika vita halali vya Jihadi au kununuliwa. Lakini vita hivyo viwe vimeamrishwa na Mtume (s.a.w.w.) au na mmojawapo kati ya Maimamu 12 (a.s.) au kwa wakati huu amri itoke kwa Mujitahid anayeongoza Waislamu katika misingi ya Taqlid. Vita vilivyoamrishwa na kiongozi yeyote wa nchi yoyote kwa misingi ya kidunia, haviwezi kuitwa Jihadi labda kama ni vita vya kuwahami Waislamu dhidi ya maadui wa nje bila uchokozi kuanzia kwa Waislamu wanaojihami. Na pia mmehalalishiwa wanawake wengine wasiokuwa hao, ili muwatafute kwa mali zenu: Hapa tafsiri yake ni wanawake katika ndoa za kawaida tulizozoea yaani ndoa za ‘kudumu’. 205


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.