Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 197

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 182

katika Uislamu

Aliwajibu kuwa amezigawa kama alivyoamriwa na Allah (swt). Wake zake walizidi kumhoji kuwa, ‘Unafahamu kuwa baada yako hatutaolewa na mtu yeyote?’ Mtume hakuwajibu bali aliwatenga kwa mwezi mmoja ambapo ikashuka Aya hii na ndipo Mtume (s.a.w.w.) aliwaita wake zake wote akawaeleza maneno hayo ya Mwenyezi Mungu juu yao, ili wachague ama kupokea mahari zao na zawadi nono kisha wapewe talaka milele, au waishi kwa amani na Mtume (s.a.w.w.) na waridhike na maisha hayo. Hapo hapo alinyanyuka bibi Salma na kusema, ‘Namchagua Mwenyezi Mungu na Mtume Wake.’ Hapo ndipo ilifuatia kushuka Aya ya pili yake yaani:

“Na kama mnampenda Mwenyezi Mungu na Mtume Wake na maisha ya Akhera, basi Mwenyezi Mungu amewaandalia watendao mema miongoni mwenu, malipo makubwa.” (Qur’ani 33:29). Katika historia tunaona kuwa bibi Aisha na bibi Hafsa walikuwa na kawaida ya kujiona bora zaidi ya wake wenzao, na hivyo wakimdai Mtume (s.a.w.w.) awapendelee, lakini kila mara akiwakatalia. Siku moja bibi Aisha alidai apewe ngawira toka vita mojawapo ya Jihad. Madai hayo ya bibi Aisha yalikuwa ni kukiuka kanuni za haki za kugawa ngawira lakini bibi Aisha alizidi kugan’gania apewe, hata ikawa Mtume (s.a.w.w) alisikitika kwa majivuno ya bibi Aisha na madai yake batili. Imam Ali (a.s.) alikuwepo na akajaribu kumtuliza bibi Aisha bila mafanikio na badala yake bibi Aisha akamkemea Imam Ali (a.s.). Mtume alisononeka sana hapo alipokemewa Imam Ali (a.s.). Rejea (1) Rawazatul Ahbab (2) Habib Siyar (3) Asimi Kufi (4) Manaqib Murtazawi.

182


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.