Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 187

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 172

katika Uislamu

matukio hayo ziliendelea kufika Madina na mwisho Mtume (s.a.w.w.) akaamua kuwashambulia kabla hawajawadhuru Waislamu. Kwa hiyo katika mwezi wa Muharram, 7 A.H Mtume (s.a.w.w.) alielekea Khaybar na jeshi lake la askari 1,400. Siku hizo Mtume (s.a.w.w.) alikuwa akisumbuliwa kuumwa kichwa mara kadhaa. Siku aliyofika Khaybar ikawa pia anaumwa kichwa. Kwa hiyo ikawa Mtume (s.a.w.w.) anawatuma masahaba mbali mbali kuongoza mashambulizi, hadi zilipotekwa ngome sita zenye askari 20,000. Ngome hizo zilitekwa kirahisi. Lakini ngome ya Qamus ilishindikana kwa sababu ilikuwa ngome imara sana yenye kulindwa na mashujaa wa Kiyahudi. Wakati huo Imam Ali Ibn Abi Talib (a.s.) alikuwa kaachwa Madina anaugua macho. Kwa hiyo Mtume (s.a.w.w.) akawa anachagua sahaba mmoja mmoja kuongoza mashambulizi ya ngome hiyo ya Qamus. Kwanza alichaguliwa bwana Abu Bakr Sidiq na kupewa bendera. Bwana Abu Bakr alihamasisha Waislamu na kupigana kwa nguvu zote lakini hakufanikiwa kuiteka Qamus. Kisha Umar Ibn al-Khattab naye akapewa bendera na akaongoza mapigano makali zaidi lakini bila mafanikio. Kutokana na hali hiyo Mtume (s.a.w.w.) alisema, “Kwa jina la Allah kesho nitampa bendera ya vita mtu yule mwenye kumpenda Allah na Mtume Wake na ambaye Allah na Mtume wake wanampenda, ambaye daima hushambulia na wala hakimbii (vitani) bali husonga mbele, na Mwenyezi Mungu keshapima moyo wake kwa imani.” Tunayakuta haya katika Sahih Muslim chini ya kifungu cha, Matendo ya Imam Ali (a.s.). Masahaba wote walilala na shauku ya kuona ni nani huyo mwenye sifa hizo. Kesho yake Mtume (s.a.w.w.) akauliza, ‘Yuko wapi Ali?’ Masahaba wakajibu kuwa anaumwa macho. Mtume (s.a.w.w.) akaagiza aletwe mbele yake. Mara ikawa Ali Ibn Abi Talib (a.s.) amefika. Mtume (s.a.w.w.) akachukua mate yake akampaka machoni Imam Ali (a.s.) na ikawa macho yamepona! Mtume (s.a.w.w.) alimpa Imam Ali (a.s.) bendera. Imam Ali (a.s.) akaishika na ikawa masahaba wote wametambua aliyekusudiwa kwa 172


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.