Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 18

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:18 PM

Page 3

katika Uislamu

UTANGULIZI Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu. Namwomba Mwenyezi Mungu amteremshie baraka njema za milele Bwana wetu Muhammad na watu wa Familia yake ambao walitoharishwa kikamilifu kwa kadri ya “Hakika si mengineyo Mwenyezi Mungu anataka kuwaondolea uchafu, enyi watu wa nyumba ya Mtume, na kuwatakasa kabisa kabisa.” (Qur’ani 33:33); pamoja na maswahaba waaminifu walioshikamana na mwendo wa Mtume (s.a.w.w) - Amin. Ndugu zangu, namshukuru Mwenyezi Mungu (s.w.t.) kuniwezesha kukamilisha kazi hii ambayo ni wajibu kwa kila Mwislamu. Kama tulivyotangulia kusoma kuwa ni muhimu kila mmoja wetu achunguze upya imani na itikadi yake ya kidini, ili afikie dini moja ya kweli mbele ya Mwenyezi Mungu, kuliko kubakia kujivunia madhehebu mbali mbali. Kwa msingi huo nilijaaliwa kufanya utafiti kwa miaka 16 kwa kusoma vitabu mbalimbali hasa vile vya Historia sahihi ya Uislamu. Niliyoyakuta katika vitabu hivyo, yalinitia simanzi moyoni kwa muda mrefu, kwa kuona jinsi ambavyo Waislamu kwa miaka mingi tumekuwa tunaendeleza utamaduni wa kiislamu lakini Uislamu wenyewe upo mbali na sisi. Nasema hivi kwa sababu tumetangulia kuona kuwa sisi binadamu tunapaswa kuishi hapa duniani chini ya amri za Muumba wetu wakati wote. Pale tunapoachana na amri hizo au tunapoacha amri hizi na kuanza kuchagua tunayotaka, na kuacha tusiyoyataka, hiyo si dini tena. Hali hiyo ndiyo tuliyonayo wakati huu katika Uislamu wetu. Kwa sababu tutambue kuwa maana ya neno ‘Islam’ ni kujitoa nafsi yako yote kumtii Mwenyezi Mungu. Utiifu wa nusu nusu sio Uislamu unaotakiwa.

3


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.