Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 128

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:20 PM

Page 113

katika Uislamu

ilizeni, tiini na mzingatie amri ya Mola wenu, kwani Yeye ndiye Mlezi wenu, Kiongozi wenu, (wa haki), kisha baada ya yeye ni Mtume wake Muhammad, kiongozi wenu mliye naye sasa akiwahutubia, kisha baada yangu mtakuwa naye Ali, Kiongozi na Imam wenu kwa amri ya Mola wenu, kisha baada yake watakuwepo Maimamu (viongozi) kutokana na kizazi (Ahlul-Bayt) changu katika uzao wake (Ali) hadi siku ya Kiyama, hapo mtamkabili Mwenyezi Mungu na Mtume Wake. “Hakuna halali isipokuwa ile aliyoihalalisha Mwenyezi Mungu, na hakuna haramu isipokuwa ile aliyoharamisha; kwani ameshanifahamisha ya halali na ya haramu, nami natangaza hayo na yale aliyonifundisha Mola wangu kwenye Kitabu Chake, na kutokana na ya halali na ya haramu Kwake. “Enyi watu! Kila elimu Mwenyezi Mungu ameidhibiti kwangu, na kila elimu niliyopewa, basi nimemnukulia Ali, kiongozi wa wacha Mungu na hakuna elimu ila nimekwisha mfundisha, naye ni kiongozi anayepambanua kati ya haki na batili. “Enyi watu! Msijitenge naye wala msimtoroke, na wala msiwe wapinzani kwa uongozi wake; kwani ndiye aongozaye kuielekea haki na huku akiitekeleza, anayeondoa batili na kuikataza, kwani kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, haimuathiri lawama ya mwenye kumlaumu, kisha yeye ni wa mwanzo kumwamini Mwenyezi Mungu na Mtume Wake kwa sababu hakuna yeyote miongoni mwa wanaume aliyemwabudu Mwenyezi Mungu akiwa pamoja na Mtume Wake isipokuwa yeye Ali. Enyi watu! Mtukuzeni na kumkubali; kwani Mwenyezi Mungu amemchagua. “Enyi watu! Hakika yeye ni kiongozi aliyeteuliwa na Mwenyezi Mungu na kamwe Mwenyezi Mungu hatakubalia toba ya yeyote anayekanusha uongozi wake; na wala hatasamehewa!

113


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.