Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 127

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:20 PM

Page 112

katika Uislamu

hani hayo kuwa ni madogo lakini ni makubwa kwa Mwenyezi Mungu. “Na pia waliponiudhi si mara moja, hadi ikafikia kuniita Sikio, wakidai niko hivyo. Kwa ajili ya kutangamana naye na kumwelekea sana, hadi Mwenyezi Mungu akateremsha Aya kwenye Qur’ani:

“Na miongoni mwao wako (wanafiki) wanaomuudhi Mtume na kusema: Yeye ni sikio tu. Sema; Sikio la heri kwenu” (Qur’ani 9:61). “Lau ningalitaka kuwaita (kwa majina ya kukebehi) ningelifanya hivyo au kuwaonyesha wajionee wenyewe; au kuwajulisha kwa watu, basi ningefanya lakini Wallah, kwa mambo yao hayo nimefanya staha, na yote hayo Mwenyezi Mungu hapendi niyafanye ila tu nifikishe lile aliloniamrisha. Kisha baada ya hapo (Jibril) akanisomea Aya:

“Ewe Mtume, fikisha uliyoteremshiwa toka kwa Mola wako, na kama hutafanya basi hukufikisha ujumbe Wake. Na Allah atakulinda na watu .” (Qur’ani 5:67). “Jueni enyi watu! Mwenyezi Mungu amemhusisha (Ali) kwenu awe kiongozi na Imam; akalazimisha atiiwe na Muhajirina na Ansari pamoja na wale wote, waliowafuatia wao kwa wema, na pia (akalazimisha) kwa walio mbali na waliopo hapa, Waarabu na wasio Waarabu, waungwana na watwana, wadogo na wakubwa, weupe na weusi. “Na ni juu ya kila mcha Mungu kutekeleza hukumu yake na kupitisha usemi wake. Basi amelaanika yule atakayempinga, atarehemewa kila atakayemfuata, na atakuwa Muumin yule atakayemsadikisha, Mwenyezi Mungu amsamehe huyo na kila mwenye kumsikia na kumtii. “Enyi watu! Hakika hii ni fursa ya mwisho kuipata mahali hapa, hivyo sik112


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.