Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 96

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:20 PM

Page 81

katika Uislamu

Mtume Mtukufu (s.a.w.w.) alimwuliza huyo myahudi kama anajua habari za Asbat. Myahudi alijibu; “Ndiyo, walikuwa Kumi na Wawili na katika hao Lawa bin Barkhya alighibu na kujitokeza tena na kupigana na mfalme wa Karastya na kumwua’. Mtukufu Mtume naye akaendelea kusema kuwa: “Kwa hakika yale yaliyowakabili Wayahudi, yatatokea pia kwa wafuasi wangu. Mrithi wangu wa Kumi na Mbili ataghibu. Katika siku hizo Uislamu utabakia jina tu. Qur’ani itasomwa kama kawaida ya dini lakini bila kufuatwa kwa vitendo. Wakati dhuluma (kufuru) itakapokuwa imetawala dunia, mrithi wangu wa Kumi na Mbili atajitokeza na kufufua Uislamu, kurejesha haki na insafu. Watakaobahatika ni wafuasi wale ambao watamtii Mahdi, na ghadhabu ya Allah itawasubiri watakaomuasi Mahdi.” Katika kitabu cha Jami-ul-Usul kinatoa ushahidi toka vitabu vya Sahih Bukhari, Sahih Muslim, Sunan Abudawood na Sahih Tirmidh; kwamba anakaririwa Abu Huraira akimkariri Mtume (s.a.w.w.) kuwa alisema: “Miongoni mwa wafuasi wangu, kikundi kimoja kitatangaza jihadi ya kushinda vita zote. Hapo Nabii Isa atateremka kutoka mbiguni, na kiongozi wa hicho kikundi. Imam Mahdi atamkaribisha Nabii Isa kuongoza swala ya jamaa lakini Nabii Isa atajibu, “Wewe ndiye mwenye mamlaka (madaraka) juu ya viumbe wa Mungu na watokana na dhuria ya Mtume Muhammad (s.a.w.w.), Mwenyezi Mungu amekutunukia heshima na ubora kuliko waumini wote wa wakati huu’. Imam Ahmad Ibn Hanbal, mwandishi maarufu wa vitabu vya Kisunni ameridhia katika sehemu ya kwanza ya kitabu chake cha Musnad, ukurasa 99 kwamba imesimuliwa kuwa: Mwenyezi Mungu atamleta Mahdi (a.s.) aliyetokana na dhuria yangu kutoka mafichoni kabla ya Siku ya Kiyama, japokuwa ibakie hata siku moja kabla ya mwisho wa dunia, naye ataeneza haki, usawa na usalama duniani na kutokomeza dhulma na ukandamizaji.

Elimu ya kuzaliwa ya Imam Muhammad At-Taqi (a.s.) Imam wa Tisa: Imam Muhammad At-Taki (a.s.) aliishi kati ya mwaka 195 A.H-220 A.H. 81


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.