Visa vya Wachamungu

Page 43

Visa vya wachamungu final Lubumba.qxd

5/15/2010

8:54 AM

Page 37

Visa vya wachamungu wakimwonea huruma na kumpa sadaka ambayo alitumia kwa chakula chake kila siku na hivyo basi aliendelea na maisha yake ya huzuni. Siku moja Ali, Kiongozi wa Waumini alipitia kwenye njia hiyo na kumwona muombaji huyo katika hali hiyo, na kutokana na kujali maslahi ya wengine Ali aliuliza kuhusu huyo mzee. Alikuwa anataka kujua sababu ambazo zilimfanya awe katika hali hiyo. Alikuwa hana mtoto wa kumsaidia? Ama hakuna njia nyingine ya yeye kuishi maisha ya kuheshimika katika uzee wake?” Watu ambao walimjua mzee huyo walisogea mbele na kumjulisha Ali (a.s.) kuwa alikuwa mkristo na alifanya kazi kwa bidii kwa muda mrefu alipokuwa na macho yake, na ni kijana mwenye nguvu zake. Lakini sasa alivyopoteza ujana wake na pia akawa kipofu hakuweza kufanya kazi yeyote; pia hana chochote alichojiwekea akiba hivyo basi kumlazimu aombe. Ali akasema: “Ajabu! Alipokuwa na nguvu mlidondoa kazi za nguvu zake, lakini sasa mumemtelekeza peke yake?” Kisa chake hiki kinaonesha kuwa alifanya kazi alipokuwa na nguvu. Kwa hivyo ni wajibu wa Serikali na Umma kumsaidia hadi atakapofariki. Nendeni mumpe malipo ya maisha uzeeni kutoka Hazina ya Taifa.

* * * * 14. KATIKA ARDHI YA MINA Mahujaji walikuwa wamekusanyika Mina. Imam Sadiq (a.s.) na maswahaba wake walikuwa wameketi sehemu fulani wakila zabibu zilizokuwa zimeandaliwa mbele yao. Muombaji alitokea na kuomba sadaka. Imam alichukua zabibu na kumpa lakini alikataa kuchukua na akaomba pesa, Imam alimwambia kuwa amsamehe kwa kuwa hakuwa na pesa za kumpa. Muombaji yule akaenda 37


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.