Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 71

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:19 PM

Page 56

katika Uislamu

Sifa za Ahlul-Bayt wa Mtume (s.a.w.w.): Hapa nitaeleza kwa ufupi sana badhi ya mambo yaliyotokea katika maisha ya Ahlul-Bayt. Mambo hayo ni pamoja na miujiza mbalimbali inayodhihirisha kuwa wao hawakuwa binadamu wa kawaida kama sisi.

Imam Hasan na Imam Husein (a.s.): Kwa kadri ya Hadithi ya Mtume (s.a.w.w), Imam Hasan (a.s.) ni kiongozi wa pili, wakati ambapo Imam Husein (a.s.) ni kiongozi wa tatu katika mpangilio wa uhai wa hao viongozi 12 (a.s.). Siku moja katika uhai wao karibu na Sikukuu ya Idd, Hasan na Husein (a.s.) walimwendea mama yao, Bibi Fatima (a.s.) na kumwuliza: ‘Mpendwa mama, kesho ni Sikukuu, wapi nguo zetu mpya za Sikukuu?’ Mama yao alijua kuwa wakati huo hapakuwepo nguo wala uwezo wa kuzipata, kwani hata chakula kilikuwa cha taabu na nguo yake mwenyewe ilijaa viraka vya majani ya mtende. Zaidi ya hayo urithi wake alioachiwa na Mtume (s.a.w.w) yaani ‘Fadak’ ulikuwa umetaifishwa na watawala wa wakati huo (yaani khalifa Abubakr Sidiq). Kwa hiyo Bibi Fatima (a.s.) akawajibu wanawe kuwa wasubiri kesho yake fundi ushonaji atazileta nguo zao. Usiku huo walipokuwa wamelala watoto Hasan na Husein (a.s.), Bibi Fatima aliamka na kukaa kwenye mswala akaswali na kuomba: “Ee Allah, Fatima mtumishi wako anayetegemea neema zako ameahidi nguo mpya kwa watoto wake Hasan na Husein (a.s.). Bwana wangu, wakipata nguo hizo watafurahi na wewe utaridhika na kufurahi kwao. Ee Allah usiache ahadi ya Fatima iache kutimia na usiache watoto hawa wasikitike.” Mapema kesho yake asubuhi Siku ya Idd, watoto hao wakaamka na kitu cha kwanza wakauliza nguo mpya. Pale pale ikasikika sauti mlangoni mtu akitoa salamu na kusema, ‘Enyi Ahlul-Bayt wa Mtume, chukueni nguo hizo za Hasan na Husein.’ Nguo hizo zililetwa na Malaika toka Peponi. Walipovaa nguo hizo na kutoka mitaani. Watu walishangaa kuona mavazi hayo ya ajabu yasiyopatikana popote wakati huo! Hadithi ya Mtume (s.a.w.w.) anakaririwa akisema kuwa: “Hasan na Husein (a.s.) ni viongozi 56


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.