Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 412

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:25 PM

Page 397

katika Uislamu

(7) Mwanamke akiwa kipofu, kiziwi na bubu amefungiwa ndani ya sanduku la moto na ubongo wake ukitokota kwa joto. Sababu? Alikuwa akimdanganya mumewe kwamba watoto aliowazaa ni wa yule mume wakati ambapo ni watoto haramu watokanao na uzinifu. (8) Mwanamke ambaye Malaika walikuwa wanamkatakata nyama yake ya mbele na mgongoni kwa mkasi, vipande vipande. Sababu?: Alikuwa akipenda kuonyesha sura yake ili wanaume wamtamani. (9) Mwanamke aliyekuwa na kichwa kama nguruwe, mwili kama punda. Sababu? Alikuwa mfitini na mwongo. (10) Mwanamke ambaye mikono yake yote miwili ilikuwa inaungua huku anachomwa moto mwili wake wote na anakula utumbo wake mwenyewe. Sababu? Alikuwa kuwadi akiwapeleka na kuwafanyia mipango wanawake kwa wanaume ili wazini. (11) Mwanamke akichochewa moto kwenye sehemu zake za siri. Sababu? Alikuwa mwimbaji na mwenye kijicho. Mpaka hapo tumeona baadhi tu ya adhabu zinazowasubiri wanawake ambao hapa duniani wanajidai kwenda na wakati, kwa maana kwamba sheria za Mwenyezi Mungu zimepitwa na wakati! Kama ni hivyo basi, tusubiri hicho kifo ndipo tuone kama ahadi ya Mwenyezi Mungu itatimia au hapana. Kila mtu maarufu anapofariki utasikia watu wanasema, ‘Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi’. Hayo ni maneno ya kujifurahisha kwa sababu kuingia peponi ni matendo binafsi ya mtu katika uhai wake, na siyo maombi ya watu kumwombea marehemu! Kama wewe binadamu hutaki kutii amri za Mwenyezi Mungu, ufahamu kuwa wewe ni mtu wa kuteseka huko akhera hata ukiombewa na mji mzima au kijiji kizima au nchi nzima! Ukichunguza Aya za Hijabu nilizozitaja hapo nyuma, utaona kuwa yanayokatazwa humo ndiyo yanayopelekea wanawake wengi kwenda motoni! Kwa hiyo kama akina mama watazingatia makatazo katika Aya 397


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.