Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 352

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:24 PM

Page 337

katika Uislamu

maana kuwa Mwenyezi Mungu atatuhukumu kwa kutumia sheria tofauti wakati dini yake ni moja tu! Lakini hata hapa duniani, hakuna nchi huru inayowahukumu raia wake kwa aina tofauti za sheria kwa makosa yanayofanana! Uislamu ni ule ule mmoja mbele ya Mwenyezi Mungu; na kwa hiyo sheria zake pia ni aina moja tu. Migawanyiko hii tuliyonayo ni upotofu na ndiyo maana Mtume akasema kuwa tutagawanyika makundi mengi lakini ni kundi moja tu litakalonusurika. Watawala walidhibiti ijtihadi katika madhehebu ya Sunni: Iwapo Uislamu siyo ‘Dogma’ ina maana kuwa utafiti ufanywe ili kila tendo la ibada lithibitishwe na lipimwe katika mizani ya mantiki kwa kadri ya ushahidi wa Qur’ani na Sunna sahihi. Kinyume na hivyo tutajikuta tunatekeleza sunna potofu za watawala waovu wa ‘Dola ya kiarabu’. Watawala ambao hawakuwa hata na sifa yoyote njema ya kushika uongozi huo. Kwa upande mwingine tunaona kuwa tatizo la sunna potofu linatusababisha kufanya ibada batili zisizo na thawabu yoyote mbele ya Mwenyezi Mungu. Sunna potofu zinatokana na Hadithi potofu kama tulivyoona katika Sura ya 15. Ukizidi kuchunguza utaona kuwa, mara nyingine watu waovu walitumia majina ya watu mashuhuri na kukariri kwao Hadithi za uongo lakini historia inawaumbua! Kwa mfano katika madhehebu ya Sunni, wanaelezea tukio la ‘Miraj’ kwa kukariri maelezo yanayodaiwa kutoka kwa bibi Aisha! Lakini tukirejea historia tunagundua kuwa, wakati huo (kabla ya Hijra) bibi Aisha alikuwa hajaingia kwa Mtume (s.a.w.w)! Ukweli ni kwamba wakati huo bibi Aisha alikuwa na umri wa miaka kati ya 8 na 9. Umri huo unatumiwa na maadui wa Uislamu kumdhalilisha Mtume (s.a.w.w) kwamba alikuwa mpenda wanawake sana kiasi cha kuoa binti mdogo kama huyo!

337


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.