Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 325

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:24 PM

Page 310

katika Uislamu

Imam Husein (a.s.) akiwa Makkah alipata taarifa kuwa Yazid kawatuma wauaji 30 ili wamwue hata kama yuko katika ibada ya Hijjah. Wauaji hao waliamriwa wavae kama mahujaji na kuchanganyika humo ili wapate fursa ya kumuua Imam Husein (a.s.). Wakati huo huo Imam Husein (a.s.) alipokea barua ya mjumbe wake huko Iraq kumtaka aende huko. Imam Husein (a.s.) alibadili mavazi ya Hijjah. Mnamo tarehe 8 Dhul Hajj 60 A.H Imam Husein (a.s.) aliondoka Makkah na kukatisha Hijjah yake akaelekea Kufa - Iraq. Akiwa njiani pamoja na watu wake, Imam Husein (a.s.) alizingirwa na jeshi la Yazid la askari 1000 waliokuwa jangwani karibu na mji wa Kufa. Kwa ushauri wa kiongozi wa jeshi hilo Hurr Ibn Yaziid, Imam Husein (a.s.) aliacha njia ya Kufa na kuelekea porini kwa sababu njia zote za kuelekea Kufa zilifungwa. Akiwa njiani alifika sehemu moja tambarare ambapo farasi wake alikataa kabisa kwenda mbele! Imam Husein (a.s.) alibadili farasi sita lakini wote wakakataa kuondoka hapo! Imam Husein (a.s.) ilimbidi awaendee wenyeji kuwauliza mahali hapo ni wapi. Baada ya kutajwa majina kadhaa, mzee mmoja alisema kuwa alisikia kwa babu zake kuwa hapo ni Karbala. Kusikia hivyo Imam Husein (a.s.) aliamuru watu wake wasimame na kupiga kambi hapo, kwa sababu tukio hilo lilishatabiriwa mara nyingi na Mtume (s.a.w.w) pamoja na matokeo yake. Uzito wa tukio la Karbala katika Uislamu ni kwamba Mtume (s.a.w.w) alielezwa na Malaika Jibril kuwa siku hizo Uislamu utakuwa katika migogoro mikubwa sana karibu kufutika, lakini kunusurika Uislamu kutatokana na kafara kuu ya damu ya Imam Husein (a.s.) huko Karbala. Vilevile anakaririwa Mtume (s.a.w.w) akisema kuwa adhabu ya muuaji wa Imam Husein (a.s.) itakuwa sawa na nusu ya adhabu zote za watenda madhambi wa dunia nzima! Tukio hilo la kikatili lilitokea jangwani Karbala ambapo Imam Husein (a.s.) na wafuasi wake waaminifu 72, waliuawa kikatili tarehe 10 mwezi wa Muharram mwaka 61 A.H, na kukatwa vichwa vyao, vikatundikwa 310


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.