Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 269

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:23 PM

Page 254

katika Uislamu

Jeshi la mama Aisha likiwa njiani lilipata habari kuwa Imam Ali (a.s.) katuma jeshi lake linawafuata kuwazuia wasifike Basra. Hivyo mama Aisha aliamuru waache njia kuu watumie njia ya pembeni ili wafike Basra bila upinzani. Mtu mmoja mjuzi wa njia, alipitisha usiku akiimba na kutangaza majina ya vijiji wanavyopitia. Wakiwa njiani usiku mmoja, kiongozi huyo wa njia alitangaza, ‘Hili ni bonde la Haw’ab’ Rejea:Successors of Muhammad - cha Bwana W. Irving, Uk. 172. Mama Aisha kusikia neno ‘Haw’ab’ alisisimka mwili na hapo hapo mbwa wa pale kijijini wakafika na kumzunguka ngamia wa Mama Aisha na kuanza kubweka! Mama Aisha aliuliza tena, “Hapa ni wapi?” Yule kiongozi akajibu, “Hili ni bonde la Haw’ab.” Mama Aisha alisikika akipiga ukulele, kwani utabiri wa Mtume (s.a.w.w.) ulitimia kama nilivyoeleza hapo nyuma! Lakini Talha na Zubair walikula kiapo cha uongo na wakawanunua (wakawahonga) wenyeji 50 kula kiapo cha uongo na kudai kuwa mahali pale siyo Haw’ab na kwamba kiongozi kakosea! Hapo ndipo mama Aisha aliamuru wapige kambi hapo kwa kutoridhika na uongo huo. Lakini Talha na Zubair wakabuni ujanja na kupiga kelele ghafla kuwa jeshi la Imam Ali (a.s.) tayari linawafukuzia! Ndipo mama Aisha akanyanyuka upesi na kupanda ngamia wakaondoka haraka na mwisho kufika pembezoni mwa mji wa Basra mahali paitwapo Khoreiba wakapiga kambi hapo. Mama Aisha alituma ujumbe kwa gavana wa Basra Uthman Ibn Hunaif akimtaka kujiunga naye. Gavana aliondoka na wafuasi wake wengi kumsikiliza mama Aisha na akakuta jeshi la waasi limetapakaa. Talha na Zubair wakahutubia kisha mama Aisha naye akahutubia akiwa juu ya ngamia wake. Ikawa kumezuka kutoelewana. Mtu mmoja mkazi wa Basra akasema, “Ewe mama wa waumini! Kumuua khalifa ni kosa lingine, lakini wewe kusahau heshima yako na amri juu yako ya kukaa ndani (Qur’ani 33:33) na badala yake kuja hapa bila hijabu tena ukiwa juu ya ngamia ni vipi uzito wake?” Mtu mwingine akawageukia Talha na Zubair akasema, “Nyie mmemleta mama yetu Aisha mbona wake zenu hamkuwaleta pia?”

254


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.