Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 266

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:23 PM

Page 251

katika Uislamu

Wanafiki wawili Talha Ibn Ubaidullah na Zubair Ibn al-Awam walibuni njia nyingine ya kuwawezesha kuondoka Madina bila kutiliwa shaka. Walimwendea tena Imam Ali (a.s.) wakiomba waende Makkah kwenye Hijjah ya Umra! Imam Ali (a.s.) alitambua ujanja wao na kuwakumbusha kiapo cha utii kwake walichotoa kwa hiari zao. Aliwakumbusha kuwa aliwataka watoe bay’at kwa hiari zao hadharani hapo mwanzo, kwa sababu alifahamu kuwa si waaminifu. Imam Ali (a.s.) aliwaachia waende. Wakati huo Mama Aisha alikuwa anarejea toka Makkah kwenye Hijja. Akiwa njiani alipata habari za kuuawa Uthman, akawa amefurahi, kama nilivyoelezea huko nyuma, juu ya kauli yake baada ya Uthman kuwanyima urithi. Lakini hapo hapo, akapata habari za kuchaguliwa Imam Ali (a.s.) kuwa khalifa. Kusikia hivyo alikasirika sana na kusema, “Natamani mbingu zingeporomoka kabla Ali (a.s.) hajawa khalifa!” Pale pale aliamuru arejeshwe Makkah. Kutoka Makkah alielekea Basra akiwahamasisha watu njia nzima kujiunga na jeshi la uasi dhidi ya Imam Ali (a.s.)! Aliondoka Makkah na wapanda ngamia 600, wapanda farasi 400, na aliwashawishi watu 3,000 kuwa askari hadi kufikia askari 30,000. Kati ya Makkah na Basra maelfu ya Waislamu wanaomwunga mkono Imam Ali (a.s.) waliuawa kwa amri ya Bibi Aisha! Hadithi ya Mtume (s.a.w.w.) juu ya Imam Ali (a.s.): Anakaririwa Mtume (s.a.w.w.) akisema kuwa, ‘Utawatambua wanafiki kwa chuki yao dhidi ya Ali Ibn Abi Talib’. Rejea: 1. Sahih Muslim, Jz. 1, uk. 61 2. Sahih-Tirmidh, Jz. 5, uk. 306 3. An-Nasai al-Kafiya, Jz. 8, uk. 116 4. Kanzul-Ummal, Jz. 15, uk. 105 Mama Aisha akiuka amri ya kukaandani akiwa mke wa Mtume (s.a.w.w.): Wake za Mtume (s.a.w.w.) waliamriwa na Mwenyezi Mungu kukaa ndani majumbani mwao milele - (Qur’ani 33:33). Lakini tunamwona hapa 251


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.