Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 263

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:23 PM

Page 248

katika Uislamu

Hiyo ilikuwa mara ya kwanza tangu kufariki Mtume (s.a.w.w.), Waislamu kumchagua khalifa kwa ridhaa ya walio wengi! Quraishi wa Bani Umayyah na wafuasi wa Uthman hawakufika hapo kutoa bay’at. Mabwana Sa’d Ibn Waqqas, Maslama Ibn Khalid, Mughira Ibn Shu’ba, Abdallah Ibn Salam, Husein Ibn Thabit na Ka’ab Ibn Malik hawakutoa bay’at kwa Imam Ali (a.s.). Kazi ya kwanza ya Imam Ali (a.s.): Kwanza kabisa aliwang’oa madarakani viongozi waovu wote. Magavana waovu waliondolewa isipokuwa Muawiyah Ibn Abu Sufyan aliyekuwa gavana wa Syria tangu enzi za utawala wa Abu Bakr Sidiq. Kwa jinsi Muawiyah alivyojijenga kijeshi kwa miaka mingi kwa kutumia vibaya ‘Baitul Maal’, iwapo Imam Ali (a.s.) angejaribu kumwondoa madarakani, kungetokea vita kubwa na watu wengi kupoteza maisha yao. Baadhi ya Magavana walioondolewa madarakani ni kama Yala aliyekuwa gavana wa Yemen na Ibn Amir aliyekuwa gavana wa Basra. Mara baada ya kuvuliwa madaraka, magavana hawa walitoroka na mali nyingi kutoka ‘Baitul Maal’ na kumpelekea Bibi Aisha. Kwa mfano bwana Yala alimpelekea bibi Aisha pesa, Dinari 60,000 na ngamia 600. Miongoni mwa ngamia hao alikuwepo ngamia mmoja mwenye sifa za pekee ambaye thamani yake ilikuwa sawa na vipande 200 vya dhahabu. Ngamia huyo ndiye aliyetumiwa na bibi Aisha katika vita vya Jamal (vita vya ngamia) na ndiyo sababu ya vita hivyo kuitwa vita vya Jamal. Vita hivyo vilipigwa mahali paitwapo Khoreiba - Iraq. Magavana wapya wafuatao walichaguliwa kushika nafasi za uongozi kama ifuatavyo :Ubaidullah Ibn Abbas - Yemen Qais Ibn Saad Bin Ubada - Misri Qutham Ibn Abbas - Makkah Samaha Ibn Abbas - Tihama Uthman Ibn Hunaif - Basra Ammara Ibn Shahab - Kufa - Iraq Saidi Ibn Abbas - Bahrain 248


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.