Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 193

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 178

katika Uislamu

fanyika bila kufikiri na isirudiwe tena. Rejea: Sahih al-Bukhari, Jz. 8, uk. 21 Tarikh Tabari, Jz. 1, uk. 1822 As-Sirah an-Nabawiyyah, Ibn Hisham Jz. 4, uk. 308/309 Tarikh al-Kamil, Ibn al-Athir Jz. 2, uk. 327 Tarikh Ibn Kathir, Jz. 5, uk. 245/246 Al-Ansab al-Baladhuri, Jz. 5, uk. 15 Sharh Ibn Abi al-Hadiid, Jz. 2, uk. 23 Kwa hiyo sisi Shia tunaposisitiza kuwa hatukubaliani na mfumo huo wa ukhalifa tunaungwa mkono na Umar Ibn al-Khattab kwa ushahidi wa vitabu hivyo vya ndugu zetu Sunni! Kabla sijaendelea kuelezea jinsi Umar na Uthman walivyopata ukhalifa na walivyokiri kubatilisha baadhi ya hukumu za Qur’ani na Sunna, ni muhimu kwanza tufahamu historia sahihi ya Bibi Aisha, kwa sababu karibu Hadithi zote za kumsifu bwana Abu Bakr zinakaririwa toka kwa Mama Aisha peke yake, kama tulivyoona madai ya kuwa Abu Bakr aliamrishwa aswalishe watu usiku wa kuamkia kufariki Mtume (s.a.w.w.)!

BIBI AISHA Wengi wetu tunasikia Bibi Aisha akisifiwa kwa sifa nyingi za kupindukia kuliko hata wake wengineo wa Mtume (s.a.w.w.) waliokuwa wacha Mungu kama Bibi Khadija na Mama Salma. Kwa kuwa madhumuni ya utafiti huu ni kuchunguza matukio muhimu katika Uislamu, hatuna budi kuwataja wahusika wakuu kwa nia ya kuweka wazi ukweli wa mambo. Jambo la maana ni kuthibitisha maelezo hayo kutoka katika vitabu vya kutegemewa. Isitoshe katika ulimwengu wa leo, historia siyo siri ya Waislamu bali ni elimu iliyotapakaa katika vitabu vingi duniani! Iwapo sisi Waislamu tutashindwa kujifunza historia yetu, watatokea watu wasio Waislamu wenye ujuzi wa dini yetu kuliko sisi, na hiyo itakuwa ni aibu kwetu.

178


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.