Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 192

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 177

katika Uislamu

pale yule Kasisi aliingia Uislamu mbele ya Imam Ali (a.s.) na akasema kuwa yapo maandishi katika vitabu vya zamani kwamba kuna kisima kilichofichika maeneo hayo, na ni Mtume wa Mwenyezi Mungu au mrithi wake aliyechaguliwa na Mwenyezi Mungu, ndio pekee wawezao kukigundua kilipo. Kasisi huyo aliongozana na Imam Ali (a.s.) katika vita vya Siffin na akauawa huko kishahidi. Tutaona kuwa yule Kasisi alipotambua wadhifa wa Imam Ali (a.s.) alisilimu hapo hapo. Lakini leo hii tunapotoa ushahidi mzito wa cheo na utukufu wa Ahlul-Bayt wa Mtume (s.a.w.w.) juu ya umma wa Kiislamu, bado utaona Waislamu walio wengi hawaoni bado umuhimu mkubwa wa kuwa wafuasi wa hao warithi halali wa Mtume (s.a.w.w.) Baada ya kuteka maji katika kisima hicho na kutosheleza mahitaji ya jeshi lake, Imam Ali (a.s.) alifunika tena kisima hicho na kurejea kambini kwake. Baada ya muda Imam Ali (a.s.) aliwataka wale alioongozana nao kisimani hapo, warejee tena waone kama watagundua sehemu hiyo tena. Watu hao walijibu kuwa isingekuwa vigumu kwao kugundua sehemu hiyo kwa kuwa ilikuwa karibu na Parokia. Kwa hiyo waliondoka na kuelekea huko lakini hawakuweza kamwe kugundua sehemu hiyo! Imam Ali (a.s.) aliwaelezea kuwa hadi Kiyama kisima hicho kitabakia kimefichika. Rejea: Early History of Islam – cha S.S. Husein, toleo la mwaka 1933. Kwa hiyo tumeona kuwa katika historia za vita vya Jihadi, ushujaa wa Imam Ali (a.s.) pamoja na elimu yake iliyotajwa na Mtume (s.a.w.w.) kuwa Ali ni lango la elimu ya Mtume (s.a.w.w.) mwenyewe, bila shaka hata kusingekuwepo na wasia wa Mtume (s.a.w.w.), Imam Ali (a.s.) alistahiki kuwa kiongozi hata kwa sifa za kawaida za kidunia. Madai yote ya Umar kumzuia Imam Ali (a.s.) asipate uongozi huo muhimu hayana msingi wowote kwa Waislamu waaminifu. Zaidi ya hayo ushahidi niliotoa mapema juu ya Abu Bakr alivyopata ukhalifa pale Saqifah, ni wazi kwamba njia zilizotumika si za kidini wala si za kisiasa. Ndiyo maana Umar anakaririwa akisema kuwa njia iliyotumika kumchagua Abu Bakr ni makosa na ili177


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.