Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 19

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:18 PM

Page 4

katika Uislamu

Isitoshe kama hivi leo Mtume (s.a.w.w.) angekuwa hai tunamwona, vipi angetuamrisha jambo lolote lile kisha tukatae kumtii? Lakini pamoja na kwamba hatuko naye tena, mafunzo yake na amri zake kwetu zipo na zimehifadhiwa katika vitabu vya Hadithi. Inasikitisha kuona Waislamu tunapuuzia amri muhimu za Mtume (s.a.w.w.) zilizo katika vitabu tunavyodai kuwa vinatuongoza! Kwa hiyo yale nitakayobainisha hapa siyo mageni kwa wale wenye ujuzi wa dini. Ningependa tutambue ukweli kwamba Uislamu ulianza karne kumi na nne zilizopita. Katika muda huo mrefu, ni matukio mengi yametokea. Mtu yeyote asiye na ujuzi wa matukio hayo, hana haki yoyote ya kupinga au kuunga mkono hoja zilizomo humu. Kama ambavyo mimi siwezi kuingia kwenye ndege kwa nia ya kujifanya rubani wakati sina ujuzi wa kazi hiyo. Kwa maana hiyo, nakaribisha mjadala kwa wasomaji wa kitabu hiki, ambao wana mawazo tofauti, mradi mawazo hayo yawe yametoka katika vitabu vinavyotegemewa. Kama zipo hoja za msingi zaidi ya hizi, nitakuwa tayari kuzijadili. Vinginevyo siko tayari kupoteza muda katika kujibu au kujadili hoja kinyume na msimamo huu; kwani itakuwa ni kukiuka misingi ya utafiti. Nina maana kwamba anayetaka tujadili hoja hizi au kunipinga, itabidi kwanza athibitishe elimu yake ya Historia sahihi ya Uislamu kama inamtosha kujadili hoja hizi. Sababu yake ni kwamba, imenichukua miaka 16 kufanya utafiti huu, kwa kusoma vitabu vingi sana, kuliko hivyo nilivyovitaja mwishoni mwa kitabu hiki. Isingekuwa busara katika ulimwengu wa wasomi, kutoa hoja au kupinga hoja bila ujuzi wowote wa kutosha. Kwa kuwa nimetaja vitabu ambamo zinapatikana habari hizi, ni bora anayetaka kutoa hoja atafute vitabu hivyo au awaulize wanaovifahamu, ili athibitishe hoja nilizotoa na ndipo naye atoe hoja zake. Elimu niliyotoa humu ni ya ngazi ya juu sana ukizingatia elimu ya chini sana tuliyonayo Waislamu tulio wengi. Nimejitahidi kuelezea hoja mbali mbali kwa lugha nyepesi, na kwa mtiririko bayana kuhusu matukio kadhaa yalivyofuatana, kuanzia miaka zaidi ya 500 kabla ya Uislamu wa Nabii Muhammad (s.a.w.w.) hadi mwan4


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.