Asili ya Madhehebu katika Uislamu

Page 181

Asili ya

ya madhehebu katika Uislamu final Lubumba.qxd

Asili ya Madhehebu

7/1/2011

12:21 PM

Page 166

katika Uislamu

Amr Ibn Abd-Wudi alifaulu kujipenyeza kupita njia nyembamba na kujitupa mbele ya Waislamu na kuwataka ajitokeze wa kupigana naye. Waislamu kwa kujua umaarufu na nguvu za Amr na ujuzi wake mkubwa wa vita; pamoja na tukio mojawapo ambapo Amr akiwa katika vita, aliwahi kumshika ngamia mdogo kama ngao yake kwa mkono mmoja na kupigana na kundi la maharamia 1000 ambao aliwashinda vibaya, wakaogopa kujitokeza! Mtume (s.a.w.w.) aliwageukia masahaba na kuwauliza, “Ni nani kati yenu ambaye kwa niaba ya Mwenyezi Mungu na Uislamu atajitokeza kupambana na kafiri huyo tishio?” Wote waligeuka mabubu na wakainama kuangalia chini ili pengine, wasichaguliwe kupambana na Amr! Lakini Imam Ali (a.s.) alijitokeza haraka na kusema kuwa yuko tayari kwa kazi hiyo. Mtume (s.a.w.w.) alirudia wito wake huo mara tatu lakini aliyekuwa akijitokeza kila mara ni Imam Ali (a.s.) peke yake! Katika tukio hilo walikuwepo masahaba wote maarufu kama Abu Bakr, Umar na Uthman na wengineo lakini hakuna aliyethubutu kuitikia mwito huo. Sahaba mmoja alimweleza Mtume (s.a.w.w.) kuwa “Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, unatutaka kukabiliana na yule ambaye ukimkabili matokeo yake ni kifo tu; kwani tumemwona akikabiliana peke yake na kundi la maharamia elfu moja na kuwashinda, huku akishikilia ngamia mdogo kama ngao yake!’ Maneno hayo yalikuwa sawa na kumtukuza adui na hivyo kumpa kichwa cha kujigamba kwa Waislamu. Mwisho ikawa Mtume (s.a.w.w.) amemwita Imam Ali (a.s.) akamvalisha kilemba chake na kumkabidhi upanga wake kisha kumwombea ushindi juu ya adui. Imam Ali (a.s.) alijitokeza kumkabili adui na ndipo Mtume (s.a.w.w.) aliposema: “Uislamu (imani) wote unakabiliana na ukafiri wote.” Mtume (s.a.w.w.) aliomba kwa Mwenyezi Mungu: “Ewe, Mola, huyu ni ndugu yangu na binamu yangu. Usiniache peke yangu. Wewe ni mbora wa kurithisha.” Wakati huo Imam Ali (a.s.) alikuwa kijana mdogo, urefu wa wastani na umbo la kati. Adui yake alikuwa na umbo kubwa la kutisha na ni mzoefu wa vita. Amr alikuwa kapanda farasi wakati ambapo Imam Ali (a.s.) alikuwa chini bila kipando. 166


Issuu converts static files into: digital portfolios, online yearbooks, online catalogs, digital photo albums and more. Sign up and create your flipbook.